Showing posts with label Mpakanjia. Show all posts
Showing posts with label Mpakanjia. Show all posts

Monday, August 27, 2007

Mume wa Marehemu Amina Chifupa Anaumwa


Kuna habari kuwa mume wa marehemu Amina Chifupa, Bwana Mohamedi Mpakanjia yuko hoi hospitalini na ugonjwa wake unafanana na ugonjwa uliyokuwa unamsumbua marehemu mke wake. Pia wikiendi kulilkuwa na uzushi kuwa Bwana Mpakanjia amefariki dunia lakini si kweli.

Huko Bongo gazeti la Sani umeandika kuwa Mpakanjia na Kepiteni John Komba, walienda nyumbani kwa mke wa Mpakanjia wa kwanza kuomba msamaha kwa mabaya aliyomtendea.

Kwa kweli kitu ambacho sikufurahi ni ile tendo la bwana Mpakanjia kwenda kwa Spika wa Bunge kutangaza talaka aliyompa mke wake, marehemu Amina Chifupa. Lakini uwongo mbaya hao walikuwa ni chakula kikuu cha mapapparazzi. Bado mapaparazzi watasaka habari zao hata kama jamaa kaugua malaria au mafua.

Tumwombee Bwana Mpakanjia apone na aweze kuendelea na shughuli zake, na kulea watoto wake.

Kwa habari zaidi someni:




**************************************************************************

Kutoka Ippmedia.com

Hali ya afya ya Mpakanjia si shwari

2007-08-25 19:21:22 Na Mwandishi wetu, Jijini

Kuna taarifa kuwa mfanyabiashara maarufu wa Jijini Dar es Salaam, Mohamed Mpakanjia amekumbwa na kile kile kilichomuua mkewe, marehemu Amina Chifupa. Baadhi ya watu walio karibu na familia hiyo wamelidokeza gazeti hili kwamba dalili alizokuwa nazo marehemu Amina siku za mwanzo za ugonjwa wake, tayari zimeanza kuonekana kwa mumewe.

Baadhi ya watu wamedai kuwa kutokana na hali yake kutoridhisha, sasa Mpakanjia kalazwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi iliyopo Lugalo Jijini.

Amesema namna ya ugonjwa unaomsumbua Mpakanjia ulivyo ni fumbo linalowashangaza hata wao, hasa kutokana na ukweli kuwa dalili za ugonjwa wenyewe ni kama zile alizowahi kuwa nazo mkewe, marehemu Amina Chifupa.

``Hali yake si nzuri. Hivi sasa, hata anachokizungumza hakieleweki? amedhoofu mno na hata kusimama mwenyewe hawezi. Kwakweli anasikitisha sana,`` akasema ndugu huyo.

Dalili kama hizo pia zililipotiwa kujitokeza kwa aliyekuwa mkewe, marehemu Amina Chifupa, ambaye alifariki dunia Juni 26 mwaka huu katika hospitali hiyo hiyo ya Lugalo. Kabla ya kifo chake, marehemu Amina aliripotiwa kuzungumza mambo yasiyoeleweka na mwili wake kudhoofu kiasi cha kushindwa kuinuka.

Baadhi ya ndugu wa mfanyabiashara huyo wamedai Bw. Mpakanjia alilazwa hospitalini hapo mwanzoni mwa wiki hii. Akizungumzia kile kinachomsibu Mpakanjia, ndugu mmoja wa mfanyabiashara huyo amesema mgonjwa wao hivi sasa ana hali mbaya na kwamba hata kula kwa mikono yake hawezi. Amesema amewekewa mirija kwa ajili ya kumsaidia huku madakitari wakijitahidi kumhudumia.

Wednesday, June 27, 2007

Mipango ya Mazishi ya Marehemu Mheshimiwa Amina Chifupa

The late Amina Chifupa's ex-husband Mohamed Mpakanjia talks to ITV.



Jeneza lenye mwili wa Marehemu Amina Chifupa



From ippmedia.com

Bunge laahirishwa...mwili kuagwa leo

2007-06-27

Na Usu-Emma Sindila, Dodoma

Kifo cha Mbunge wa Viti Maalum-CCM, Mheshimiwa Amina Chifupa kimelifanya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuahirisha shughuli zake ili kujipa muda wa kumlilia mwenzao, Mheshimiwa Amina Chifupa aliyefariki usiku wa kuamkia leo.

Spika wa Bunge, Mhe. Samweli Sitta amesema shughuli za Bunge zitaendelea tena kesho asubuhi saa tatu. Hata hivyo amesema wabunge kadhaa wameteuliwa kuja Jijini Dar es Salaam kuungana na ndugu wa marehemu kuomboleza na kushiriki shughuli nyingine za msiba huo mzito.

Awali ilikuwa imetangazwa kwamba mwili wa marehemu ungepelekwa Dodoma kuagwa na kisha kusafirishwa kwenda Njombe kwa maziko.

Spika amewataja watakaoongoza msafara huo wa wabunge kwa ajili ya kuuaga mwili na kisha kesho kushiriki maziko kule kijijini Lupembe wilayani Njombe kuwa ni pamoja na yeye mwenyewe, kiongozi wa upinzani bungeni, Mhe. Hamad Rashid Mohamed, wabunge wote wa Dar es Salaam, wabunge wote wa Iringa na Mbunge Anne Kilango aliyekuwa mlezi wa marehemu.

Amesema watakaowakilisha Serikali katika msiba huo ni Waziri wa Usalama wa Raia, Bw. Bakari Mwapachu. Amesema marehemu atazikwa kesho katika kijiji cha Lupembe wilayani Njombe kule Iringa, alasiri. Kwa mujibu wa Spika Sitta taarifa marehemu alifariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo Jijini Dar.