Showing posts with label Women. Show all posts
Showing posts with label Women. Show all posts

Saturday, March 28, 2015

Asiimilia 40 ya Wanwake Zanzibar Wanaishi Maisha Duni

DSC_0081
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (aliyefunikwa mwamvuli) akiwasili kwenye sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika ndani ya ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel mwishoni mwa wiki.
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
UTAFITI uliofanywa na taasisi ya wanawake nchini Zanzibar ya Zanzibalicious Women umeonyesha kuwa asilimia 40 ya wanawake Zanzibar, wanaishi katika mazingira duni ya umasikini kwa kutojitambua na kukosa elimu ya uelewa jinsi ya kukabiliana na mazingira waliyomo.
Akisoma risala siku ya wanawake mbele ya mgeni rasmi mke wa rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mama Mwanamwema Shein , katika siku ya wanawake hafla iliyofanyika hoteli ya Bwawani, Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal alisema hali hiyo ni changamoto kubwa na sasa kunatafutwa namna ya kumfikia mwanamke huyu ambaye ameshagota katika jamii yetu.
“Mama Shein asilimia hii ni kubwa saana, na sisi kama wanawake ambao tayari tumejaaliwa elimu na tunajitambua, ikiwa ni pamoja na tayari tumepiga hatua kimaendeleo katika nyanja mbalimbali, tumeguswa sana sana na suala hili.” Alisema Shekha.
Zanzibalicious ni umoja wa wanawake wanaoishi Zanzibar,ulioanzishwa mwaka 2011,na kusajiliwa rasmi mwaka 2013, ikiambatana na uzinduzi uliofanyika tarehe 28 Machi 2014.
DSC_0227
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akiwasili kwenye sherehe ya siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel.
Mweka hazina huyo alisema kwamba wanajiuliza maswali mengi kama mwanamke huyo elimu ya kujikwamua imemfikia au kama kuna jitihada zozote za kumfikishia elimu hiyo.
“Je hili ni jukumu la serikali peke yake? Au sisi tunatakiwa tujumuike na serikali? mheshimiwa mgeni rasmi tumeona ya kwamba tuungane pamoja na serikali katika kutekeleza suala hili.” Alisema Shekha akielezea nia ya taasisi hiyo ya kuondoa umaskini miongoni mwa wanawake nchini Zanzibar.
Alisema taasisi yao inajipanga kutoa elimu za aina mbili ili awali kumuwezesha kujikimu kupitia ujasiriamali, kwa kumpatia elimu kwa vitendo,kwa mfano:-ushonaji,ufugaji na utengenezaji wa bidhaa mbali mbali na pili kumtoa katika hali ya upweke ili elimu atakayopata imfikishe kwenye mifuko mbali mbali pamoja na mfuko wa Rais Dk. Ali Mohammed Shein .
Alisema katika program hiyo wanatarajia baada ya miaka 2 wanawake 100 watakuwa wanajitegemea wenyewe na kuwa mabalozi katika kuelimisha wanawake wengine zaidi.
DSC_0471
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akisoma hotuba wakati wa sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group na kufanyika ndani ukumbi wa Salama, Bwawani hoteli mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akifuatiwa na Mwenyekiti mstaafu wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Ummukulthum Ansel.
“Na kama kila mwanamke akiweza kuelimisha wanawake katika kaya yake ,baada ya miaka kadhaa, Zanzibar itakuwa na wanawake walioweza kujikomboa katika dimbwi hili la kuishi maisha duni.” Alisema.
Akizungumzia mafanikio ya asasi hiyo alisema kwamba imefanikiwa kutoa elimu na kuwawezesha kina mama kuunda vikundi vidogo vidogo vya maendeleo kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kwa mfano kina mama wa Chaani na Matemwe.
Aidha imetoa misaada ya hali na mali kwa waathirika wa madawa ya kulevya ikiwa ni moja ya kumkwamua mwanamke na kutoa misaada mbali mbali kwa wanawake wasiojiweza ikiwemo hospital kuu ya Mnazi mmoja na kina mama wajane.
Alisema pamoja na mafanikio hayo bado wanawake wanakabiliwa na changamoto za ndoa za utotoni, uzazi salama, ukatili wa kijinsia,mfumo dume, ubaguzi na mimba za utotoni.
Mhe.Mgeni rasmi, Umoja huu umekuwa ukiendesha shughuli zote tokea mwaka 2011 kwa kutegemea michango yetu sisi binafsi.
DSC_0314
Baadhi ya wakinama waliohudhuria sherehe hiyo wakionekana kufurahishwa na hotuba ya Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani).
Changamoto hii imesababisha kutokutimiza kwa malengo yetu kwa muda tulioupanga kutokana na kukosa fedha za kutosheleza utekelezaji wa malengo hayo.
Akijibu risala hiyo Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein, ameikumbusha jamii kuunganisha nguvu zao kuwakomboa wanawake kujiendeleza kimaisha na kujiongezea kipato.
Alisema hatua hiyo itaongeza kasi ya kuimarisha ustawi wa familia na jamii hususan wanawake wanaoishi vijijini ambao wanakabiliwa na changamoto zaidi.
Alisema sherehe ya siku ya wanawake duniani inakuwa na maana zaidi kama juhudi zitafanyika kuangalia changamoto na kujipanga kuzifanyia kazi.
“Rai yangu ni kuwa tuwazingatie zaidi akina mama wanaoishi vijijini na wenye mahitaji maalum kutokana na kukosa fursa kama hizo za kuwaendeleza kimaisha”, alisisitiza.
DSC_0344
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Shekha Hilal akisoma risala kwa mgeni rasmi Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani) Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicous Women Group, Bi. Evelyne Wilson.
Aidha, aliongeza kuwa wanawake ni jeshi kubwa ambalo likiandaliwa vyema linaweza kushinda katika mapambano yanayokusudiwa huku akisisitza mshikamano ili kufikia malengo yanayowekwa.
Akizungumzia ujumbe wa sherehe hizo ambao ni kuhamasisha hatua mathubuti kumwendeleza na kumtambua mwanamke, alitoa rai kwa wanawake kushirikiana na serikali katika kampeni za kupambana na madhila wanayokabiliana nayo ikiwa ni pamoja na ukatili wa watoto na wanawake.
Kuhusu uzoefu wake katika maisha na malezi ya watoto, alisema amebahatika kupata watoto 11 ambao amewalea katika mazingira mbalimbali ikiwa ni kwenda na kurudi kazini na kuwa pekee huku mumewe akiwa safarini kikazi.
Aidha, aliwataka wanawake kuwa wastahamilivu katika malezi ya watoto hasa watoto Njiti ambao huzaliwa kabla ya kufikisha muda.
Hata hivyo aliwaonya wanawake wanaojali kujiremba na kuwa sahau watoto na kukumbusha kwa ‘watoto ni wageni’ kwamba wanahitaji matunzo na ukarimu mkubwa kutoka kwa wazazi wao.
IMG_6571
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akizindua Mfuko wa Zanzibalicious Women Group kwa kuchangia shilingi milioni tano, wakati wa maadhimisho ya sherehe ya wanawake duniani visiwani Zanzibar yaliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika katika ukumbi wa Salama uliopo Bwawani Hotel Zanzibar. Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicious Women Group, Bi Evelyne Wilson Baruti.
DSC_0082
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal akinakili majina ya watu waliokuwa wakichangia kwenye harambe ya mfuko wa Zanzibalicous Women Group uliozinduliwa rasmi na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (hayupo pichani).
DSC_0074
Mbunifu nguli wa mavazi Mama wa mitindo, Asia Idarous akinadi moja ya nguo alizotengeneza kwa ajili ya kuchangia mfuko wa Zanzibalicious Women Group.
DSC_0075
Mke wa Naibu Waziri wa Afya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Zakhia Kombo akitangaza dau la kununua nguo hiyo iliyokuwa ikinadiwa kwenye harambe ya mfuko wa ZWG iliyozinduliwa na Mama Mwanamwema Shein.
DSC_0091
Meza kuu kwenye picha ya pamoja na Zanzibalicous Women Group.
Unaweza kutembelea mtandao wao na kuona shughuli mbalimbali walizozifanya hapa http://www.zanzibalicious.org/
DSC_0388
Mmoja wa wadhamini ZANLINK wanaotoa udhamini kwa Zanzibalicious Women Group wakisikiliza kwa makini yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo. Kwa picha zaidi bofya link hii

Saturday, June 21, 2014

Dr. Francis Manda's Male Chauvinist Views

PRESS RELEASE
For Immediate Release
20th June 2014
NGOCC CONDEMNS DR. MANDA’S PATRIARCHAL REASONING

Dr. Francis Manda

THE Non Governmental Organisations’ Coordinating Council (NGOCC) condemns in the strongest terms the sweeping statement by Dr Francis Manda that Zambian women had lost their cultural values.
Dr Manda’s statement epitomizes the entrenched gender prejudices against women and the patriarchal nature of our society. It is totally unacceptable for Dr. Manda to say Zambian women had lost their cultural values because of the misconduct of a few. Just like some men, there are women who misbehave in public. For example, should all men be condemned just because of the few grandfathers and fathers who defile babies?
It will be unfair for anyone to suggest that men had lost their values just because of the many men we see every day in bars and on the streets drinking alcohol. Society’s moral decay should not only be made dependent upon the conduct of women. Issues of moral decay need to address both men and women.
While NGOCC does not support immoral conduct by either women or men, it is wrong to suggest that there is too much careless drinking among women in Zambia, especially in the absence of any credible baseline. We would like to remind Dr Manda that both men and women are equal and enjoy equal rights.
It is strange that Dr. Manda wants to ascribe the responsibility of parenting to women only to the exclusion of men. It is the responsibility of both men and women to take care of their children. The Zambian women demand an apology from Dr Manda over his imprudent statement.
Zambia has well respected women who are role models and it is unacceptable to denigrate all Zambian women in such a manner.
for/NGOCC
BEATRICE GRILLO
CHAIRPERSON

Saturday, December 07, 2013

Mh. Angela Kairuki Yuko Kwenye Listi ya Forbes

Mhe. Kairuki
Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Angela Jasmine Kairuki (37) ametajwa katika  jarida la kimataifa la Forbes kuwa ni mmoja wanawake vijana 20 wenye nguvu barani Afrika mwaka huu. 

 Katika toleo lake la hivi karibuni chini ya kichwa cha habari ‘The 20 Young Power Women in Africa 2013’, jarida la Forbes linamuorodhesha Mhe Kairuki sambamba na wanawake wengine 19 kama vijana wa kike wenye nguvu kwa nafasi zao kikazi na kibiashara. 

Kutajwa kwa Mhe Kairuki katika orodha hiyo kumezua msisimko katika mawasiliano ya mtandao wa 'twitter' ambapo Watanzania wengi wamekuwa wakielezea furaha na fahari zao kwa kuona Mtanzania mwenzao, tena mwanamke kijana, anatambulika kimataifa kwa utendaji wake.

Mhe. Angela Kairuki akitembelea Jeshi la Magereza
 katika mojawapo ya shughuli zake za kikazi
 Wanawake wengine waliotajwa na jarida hilo ni Mimi Alemayehou (Ethiopia) Makamu wa RAis Mtendaji wa Overseas Private Investment Corporation (OPIC),   Vera Songwe(Cameroon) Mkurugenzi Mkazi World Bank Senegal, na Tara Fela-Durotoye (Nigeria) Mwanzilishi wa House Of Tara.
Wengine ni  Rapelang Rabana (Afrika Kusini) Mjasiriamali,   Claire Akamanzi (Rwanda) Afisa Mtendaji Mkuu wa Rwanda Development Board,   Valentina da Luz Guebuza (Msumbiji) Mwekezaji,  Hadeel Ibrahim (Sudan) wa Mo Ibrahim Foundation,  Alengot Oromait (Uganda) Mbunge, na   Monica Musonda, (Zambia) Afisa Mtendaji Mkuu na MWanzilishi wa kampuni ya Java Foods.


Wengine ni NoViolet Bulawayo (Zimbabwe) Mtunzi wa vitabu, Minoush Abdel-Meguid (Misri) Mwekezaji, mjasiriamali na mwendesha benki,  Ola Orekunrin (Nigeria) Daktari na Mwanzilishi wa The Flying Doctors,  Sibongile Sambo (Afrika Kusini) Afisa Mtendaji Mkuu na Mwanzilishi wa SRS Aviation,  Lupita Nyong’o (Kenya) Mwigizaji na mtengeneza filamu,    Amini Kajunju (Congo DRC) Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Africa-America Institute na  Folake Folarin-Coker (Nigeria) Mbunifu wa mitindo.

Wengine katika orodha hiyoni  Lindiwe Mazibuko (Afrika Kusini) Mwanasia na Kiongozi wa chama cha Democratic Alliance (DA) bungeni,   Minoush Abdel-Meguid (Misri) Mwekezaji, Mjasiriamali na mwendesha benki,  Sibongile Sambo (Afrika Kusini),  Wangechi Mutu, (Kenya) Msanii na mchongaji.