Saturday, December 17, 2016

Kongamano la Kumuenzi Fidel Castro


Nilibahatika kuhudhuria japo kwa muda mfupi Kongamano ya Kumuenzi Marahemu Rais Fidel Castor wa Cuba, iliyofanyika mjini Dar es Salaam, Tanzania, jumapili iliyopita December 11, 2016 kwenye hall ya Taasisi ya Watu Wazima. (Symposium to Honor the Legacy of Fidel Castro).  Waliongolea jinsi Castor alivyotoka kwenye familia ya matajiri lakini alipenda kusaidia na kunyanua maskini.  Pia jinsi Cuba ilivyosaidia Tanzania.


Jenerali Ulimwengu Akiongea
Audience Participants
The Symposium Leaders

Mfuko wa PPF Wadhamiria Kuwafikia WaTanzania Wote Wakiwemo Wasnatasnia wa Filamu

Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Meshack Bandawe, akizungumza kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara. 

Mafunzo hayo yalanza Disemba 14 na yanafikia tamati leo Disemba 16, 2016 katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Musoma. Yameandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kuwajengea uwezo wadau wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora.
#BMGHabari
Wadau wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, wakati akiwaeleza umuhimu wa kujiunga na mfuko huo
Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, akiwasilisha mada kwa wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara
Wadau wa filamu mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Afisa Masoko PPF, Evance Baguma
Wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara wamefurahishwa na mada kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kutoka PPF na kuonesha mwitiko mkubwa wa kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PPF.

Mfuko wa Pesheni wa PPF umesema umedhamiria kuhakikisha kwamba wananchi wengi walio kwenye sekta zisizo rasmi ikiwemo wajasiriamali wananufaika na mafao ya hifadhi za jamii kupitia huduma ya Wote Scheme.

Meneja wa mfuko huo Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, ameyasema hayo Musoma mkoani Mara, wakati akieleza umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo mbele ya wadau wa filamu mkoani humo.

Amesema wananchi wasio kwenye sekta rasmi wakiwemo wajasiriamali wanayo fursa ya kujiunga na mfuko wa PPF na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, mikopo ya elimu, maendeleo pamoja na mafao ya uzeeni kwa kila mwanachama kuchangia shilingi elfu 20 kwa mwezi ambazo mwanachama hulipa kadri awezavyo.

Naye Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, amesema lengo la mfuko huo kuanzisha huduma ya Wote Scheme kwa wajasiriamali ni kuondoa dhama potofu kwa baadhi ya wananchi kwamba anayeweza kunufaika na huduma za mifuko ya hifadhi za jamii ni lazima awe mtumishi wa taasisi binafsi ama serikali.

Wadau wengi wa filamu mkoani Mara wamefurahishwa na ufafanuzi wa mfuko huo ambapo wamebainisha kwamba awali walikosa fursa mbalimbali za mifuko ya hifadhi za jamii ikiwemo PPF kutokana ufahamu duni waliokuwa nao.
Tazama picha zaidi HAPA

Katibu Tawala Moani Mara Ahitimisha Mafunzo kwa Wadau wa Filamu Mkoani Humo

Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (katikati) akizungumza hii leo kwenye kilele cha mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu mkoani humo. Mafunzo hayo yalianza juzi Disemba 14,2016 kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Msoma.

Yaliandaliwa na Bodi ya Filamu nchini kwa lengo la kuwajengea welezi wanatasinia wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora na hivyo kukidhi ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi ambapo zaidi ya washiri 200 walionufaika na mafunzo hayo wamepatiwa vyeti. Tayari mafunzo ya aina hiyo yamefanyika mikoa ya Morogoro na Mwanza na yataendelea katika mikoa mingine.
#BMGHabari
Wanatasnia wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Katibu Tawala mkoani humo, Adoh Mapunda, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia hao. Ameahidi kutoa fulana (Tshirt) 250 kwa ajili ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara waliohudhuria mafunzo hayo ambapo zitawasaidia hususani kuwa na sare ya aina moja wakikutana kwa pamoja
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, amesema sekta ya filamu ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wanatasnia wake na taifa kwa ujumla hivyo Bodi za filamu mikoani zihakikishe zinasimamia maendeleo ya tasnia hiyo.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso, amebainisha kwamba wadau wa filamu wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji wamefundishwa vyema mafunzo hayo ili kuzalisha kazi bora.
Mgeni rasmi, Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda (wa pili kulia), akipokea cheti cha utambuzi kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, akipokea cheti cha utambuzi
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso
Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Bi.Deograsia Ndunguru, kutoka Chuo Kikuu Dodoma, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Genoveva kutoka Idara ya Habari Serikalini, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani Mara, Johnson Ibambai, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwakilishi wa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mara, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba yake kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Amicus Butunga, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya TBC kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari George Binagi akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya 102.5 Lake Fm kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki zaidi ya 200 wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mwigizaji Dan Msimamo kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuinua ubora wa filamu mkoani Mara na hivyo kukuza soko lake
Mwigizaji Justar Lucas kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yamewaongezea weledi na kutambua kwamba filamu ni ajira na ikitumika vyema husaidia kukuza kipato cha wanatasnia wa filamu na taifa kwa ujumla.
Mwigizaji Innocent Mbalwa kutoka Bunda ameishukuru Serikali kupitia Bodi ya Filamu kwa kutoa mafunzo hayo ambapo amesema yatafungua milango mipya kwenye tasnia ya filamu mkoani Mara.
Mwigizaji Jackline James kutoka Musoma amesema mafunzo hayo yamemsaidia kutambua kwamba filamu ni ajira tofauti na alivyokuwa akidhani awali kwamba tasnia hiyo ni sehemu ya burudani.
******************
Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda, amewahimiza wanatasnia wa filamu mkoani humo kuwa wabunifu katika uzalishaji wa kazi zao ili kupanua soko la filamu ndani na nje ya nchi.

Mapunda ametoa rai hiyo hii leo, wakati akihitimisha mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu mkoani Mara, yaliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kukuza welezi katika uzalishaji wa kazi bora na zenye maudhui yanaykubalika katika jamii.

"Ubunifu ndio unahitajika hivi sasa, watu wengi wanahitaji ubunifu binafsi na siyo "kucopy" na "kupaste" kazi za wengine". Amesisitiza Mapunda na kuongeza kwamba serikali itatoa ushirikiano wa dhati katika kuboresha tasnia hiyo ya filamu kwani hivi sasa hutoa ajira na kukuza uchumi kwa taifa.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nuru Millao, ameziagiza Bodi za Filamu za mikoa kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuboresha zaidi sekta hiyo.

Naye Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisso, amewahimiza wadau wa filamu mkoani Mara wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji walionufaika na mafunzo hayo, kuyatumia vyema ili kukuza soko lao la filamu.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, amewasisitizia hao kutumia mafunzo hayo ili kuzalisha filamu na vipindi vya luninga vyenye ubora ili kunufaika na uhitaji uliopo.

Akisoma maazimio ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara, Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani humo, Johnson Ibambai, ametaja baadhi ya maazimio hayo kuwa ni pamoja na kuiomba serikali kuweka mitaala ya filamu kuanzia shule za msingi na vyuo vya ufundi VETA ili kusadia utoaji wa elimu hiyo ya filamu.
Tazama picha zaidi HAPA

Naibu Katibu Mkuu Mpya wa CCM Akagua Mali za Chama Dodoma

MPOGOLO AKAGUA MALI ZA CHAMA LEO MJINI DODOMA, LUHWAVI AMKABIDHI KILA KITU HADI MSAIDIZI
 Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimpa maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo, kuhusu jengo la mikutano la CCM, lililopo Kilimani mjini Dodoma wakati Naibu Katibu Mkuu huyo mpya alipotembelea jengo hilo akiwa katika ziara ya kukagua mali za CCM, leo. Kushoto ni Mkuu wa Utawala Makao Makuu ya CCM, Innocent Msena na kulia ni Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Utumishi na Uendeshaji Makao Makuu ya CCM Filbert Mdaki.
 Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimpa maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo, kuhusu jengo la mikutano la CCM, lililopo Kilimani mjini Dodoma wakati Naibu Katibu Mkuu huyo mpya alipotembelea jengo hilo akiwa katika ziara ya kukagua mali za CCM, leo. kulia ni Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Utumishi na Uendeshaji Makao Makuu ya CCM Filbert Mdaki.
 Mafara wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo ukiwa mbele ya jengo hilo la mikutano la CCM
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo, akimoji jambo, Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara Rajabu Luhwavi baada ya kukagua jengo hilo, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama, leo mjini Dodoma.
KIWANJA
🔻
 Meneja wa Miliki wa Makao Makuu ya CCM, Abdallah (kulia) Msangi akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo (wapili kushoto), alipoenda kukagua kiwanja cha CCM kilichopo eneo la Kilimani mjini Dodoma, akiwa katikaziara ya kukagua mali za Chama, leo mjini Dodoma. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi.
 Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Utumishi na Uendeshaji Makao Makuu ya CCM Filbert Mdaki akiongeza maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo alipoenda kukagua kiwanja cha CCM kilichopo eneo la Kilimani mjini Dodoma, akiwa katikaziara ya kukagua mali za Chama, leo mjini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi, akimuonyesha mwisho wa shamba la CCM, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo (wapili kulia), Naibu Katibu Mkuu huyo alipoenda kukagua kiwanja hicho kilichopo eneo la Kilimani mjini Dodoma, akiwa katikaziara ya kukagua mali za Chama, leo mjini Dodoma, leo.

NYUMBA YA CCM YA NAIBU KATIBU MKUU-BARA
🔻
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akiwasili kukagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama, mkoani Dodoma, leo
 Mkuu wa Utawala Makao Makuu ya CCM, Innocent Msena akimpa maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo, aliyefika kukagua nyumba ya Chama atakayoishi, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo
 Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Utumishi na Uenedeshaji Filbert Mdaki akionyesha sehemu ya jikoni, wakati Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo alipokagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama leo mjini Dodoma. Kushoto ni Luhwavi
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akikagua meza kwenye jiko, alipokuwa akikagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma leo. Kulia ni Msaidizi Msaidizi wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mbwana Kambangwa.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akikagua kabati la jikoni, alipokuwa akikagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma leo
 Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimpa maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo wakati wakiizunguka kuikagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mpogolo alipokuwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo.
 Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimpa maelezo Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo baada ya kuikagua nyumba ya CCM ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mpogolo alipokuwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo.

KUKAGUA MAGARI WHITE HOUSE
🔻
 Msafara wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo na Rajabu Luhwavi, ukiwa umepumzika kwa mda katika jengo la White House la Makao Makuu ya CCM kabla ya kuanza kazi ya kukagua magari, Mpogolo alipokuwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rodrick Mpogolo (wapili kushoto), akipatiwa maelezo na Fundi wa magari, Ramadhani Mbelwa (kushoto), kuhusu hali ya magari yaliyoharibika, Mpogolo alipokuwa akikagua magari hayo akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo amhoji jambo Fundi wa magari ya Chama, Ramadhani Mbelwa (kushoto), alipokuwa akikagua magari mabovu ya Chama, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama mjini Dodoma, leo. Kulia ni Luhwavi.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akionyeshwa gari lililofunguliwa boneti, kupata uthibisho wa gari tatizo la gari, alipokuwa akikagua magari mabovu ya Chama, akiwa katika ziara ya kukagua mali za Chama, leo mjini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akimshukuru Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi baada ya kumalizika kazi ya kukagua baadhi ya mali za Chama, mjini Dodoma leo.
KUNZIA SASA HUYU NDIYO BOSS WAKO, SIYO MIMI TENA: Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akimtambulisha aliyekuwa Msaidizi wake, Mbwana Kambangwa(kulia), kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo kabla ya kuagana, mwishoni mwa ziara ya Mpogolo kukagua mali za Chama, mjini Dodoma, leo. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog