Friday, February 10, 2006

Wanaume Mkienda ‘Abroad’ Mzoee Kufanya Mambo ya Kike Kike

Leo ngoja niongee kuhusu tatizo wanaume wa kiBongo wanaopata wakija hapa Marekani au Ulaya Hasa wakienda sehemu enye baridi sana.

Ni kweli huko Tanzania tumezoea kukaa kwenye joto na kutoka jasho kila wakati. Lakini ukienda sehemu wakati wa winter mbona utakoma ha huo ubaridi.

Na kama ulikwishafika Ulaya/Marekani wakati wa winter unajua kuna tatizo kubwa sana na ni ngozi kukauka. Utaona mtu mweusi mikono meupe kama vile kaziingiza kwenye poda vile. Kumbe ngozi umekauka shauri ya hali ya hewa. Ukiwa ndani ukiwa nje ngozi utakauka tu! Tena bila kupaka mafuta kwenye ngozi mtu anajikuta anajikuna kila saa. Wakati mwingine sehemu anajikuna hata sehemu nyeti kama matakoni, mwasho unazidi. Halafu ukicheki mdomo, umekuwa mweupe kama vile katoka kubusu kopo la poda. Ubaya zaidi ukikuna ngozi hiyo utaona kama unatoka unga kwa vila ngozi umekauka.

WaMarekani weusi wanaita hiyo tatizo ‘ashy’. Ukiambiwa ngozi yako ni ‘ashy’ basi ni kama vile umetukanwa. Wataalum wanasema kuwa ngozi nyeusi haupendi baridi. Of course, haupendi baridi asili yetu ni Afrika.

Kumbe watu wangejiepusha na huo balaa kwa kupaka mafuta au lotion mwilini. Lakini wanaume ambao ndo kwanza wameshuka kwenye ndege kutoka Bongo wanasema, “Ah siwezi kupaka mafuta mwilini kama mwanamke!’ Heh! Mteseke eti kwa vile hutaki kufanya mambo ya kike kike. Basi utaendelea kuchekwa kwa vile unaonekana kama umedumbukia kwenye poda.

Lakini nimeona kuwa baada ya kukaa siku kadhaa na udume wake, mwenyewe anaenda kununua hiyo lotion, mafuta, na kuanza kujisikia vizuri. Kwani hakuna haja ya kujikuna kila saa na ngozi unapendeza. Na hata wanawake wanaanza kumsalimia.

Hakuna ubaya kukaa na kopo au stiki ya Lip Moisturizer au tube ya lotion na kujipaka. Kila mtu anafanya hivyo wakati wa baridi, kwa hiyo watu hawakuona kinyago. Watashangaa zaidi kuona unapenda kutoka hadharani ukiwa 'ashy'.

Kumbe kuna mambo ya kike mazuri yanayofaa hata kwa wanaume.

No comments: