Thursday, April 06, 2006

Kwa Heri Mandisa!

Dada Mandisa kawa VOTED OFF on April 5, 2006. Mbele ya umati wa wapenzi wa American Idol, Mandisa mwenye sauti nzuri kuliko wanawake wote katika mashindano ya Season 5 katolewa kwa vile hakupata kura za kutosha. Mimi nimekasirika kweli, sijui kama nitakuwa na moyo wa kuangalia tena!

WaMarekani walisema kuwa ana sauti nyororo lakini hawezi kuwa American Idol kwa sababu ni mnene mwenye mizinga ya hips na matako!

Wengine wansema eti alivaa nguo mbaya na ana mikono minene! Jamani Kama hufanani na Paris Hilton watu hawaridhiki!

Naamini kuwa Mandisa atakuwa SUPERSTAR, na American Idol ndo ilikuwa mwanzo tu!

3 comments:

boniphace said...

Sirudi kamwe sirudi, safari nilifungani
Siwezi ikana jadi, kwani imenikuzani
Nitabakia shahidi, ukweli kuuusemani
Haya matapishi yao, wayale siyatamani!

Nipende kipi kikundi, cha wano nihujumuni?
Nipate upi ushindi, huu unaopangwani
Bora nitwike kilindi, ngoma acha tazamani
Ngano twaila kwa lele, si ngoma mbwa kachoka.

ARUPA said...

usikasirike haikuwa bahati yake kushinda.

John Mwaipopo said...

Pole Chemi kwa sononeko hilo. Yataisha haya.