Friday, July 14, 2006

Sinema ya Gone baby Gone





Mcheza sinema maarufu, Ben Affleck (aliyetaka kumwoa J Lo) yupo hapa Boston anatengeneza sinema inaitwa Gone Baby Gone. Mimi nilibahatika kuwa extra kwenye hiyo sinema. Kama watatumia footage waliyopiga nitakuwa kwenye scene wahusika wakuu wakila chakula kwenye restaurant ya Ghetto. Ilipigwa kwenye restaurant ya Silver Slipper. Insemekana wenye hiyo retaurant walipewa donge nono kwa matumizi ya hapo, eti $100,000! Sijui kama ni kweli. Najua ilibidi wafunge siku nzima, na restaurant enyewe ni ndogo.

Nilibahatika kupiga picha na mcheza sinema maarufu, Ed Harris, alikuwa kwenye sinema kama Radio, Nixon, The Firm, Apollo 13, A Beautiful Mind, na zingine nyingi tu! Ed alikuwa mungwana kweli, alipita kasalimiana na kila extra na kutuuliza majina na kwenye seti akawa anatuita kwa jina. Ben Affleck hajatusemesha hata neno moja. Wengine walisema eti kwa vile tulikuwa weusi, maana huwa anasamlimiana na extras wazungu. Lakini hatukujali tulifanys kazi na tumelipwa!

Pia tulikuwa na John Ashton. Kama mmeona sinema ya Beverly Hills Cop ni yule polisi aliyekuwa na roho mbaya kwa Eddie Murphy.

Cheki walivyogeuza Roxbury kuwa Hollywood set. Hapo ni corner ya Washington St. karibu na Dudley station karibu na kituo cha polisi.

No comments: