Thursday, July 20, 2006

Rais Bush Apata Ashki Mkutanoni!





Jamani, watu Marekani wamekuwa wakisema kuwa Rais Bush ana utaira fulani wa akili. Kama watu walikuwa hawaamini, nadhani sasa wanaamini.

Wiki hii Rais Bush yuko Urusi kwenye mkutano wa G-8 Summit, na marais na viongozi wa nchi kadhaa. Kiongozi pekee wa kike hapo ni waziri mkuu wa Ujerumani, Bi Angela Merkel. Basi Bush ailiingia kwenye ukumbi wa mkutano, sijui kaingiliwa na kitu gani, huyo anaanza kumpapasa mabega. Na yule mama kamfukuza haraka haraka! Kwa kweli hapa Marekani hiyo initwa unyanyasaji wa kijinsia (sexual harassment), na mtu anaweza kufukuzwa kazi kwa ajili hiyo. Je, Rais Clinton angefanya hivuo watu wangesema awe impeached (avuliwe urais)! Maana kaibisha taifa la Marekani.

Na kabla ya hiyo tukio ya kumpapasa alitukana alivyokuwa anaongea na Waziri Mkuu wa Uingereza, bwana Tony Blair. Alitamka neno 'shyt' akiongea kuhusu waarabu! Jamani kumsikia rais wa Marakeni akitukana ni maajabu na sijui kama imekwishawahi kutokea. Labda tuseme asante teknolojia dunia nzima inaweza kujua vituko vya Rais wa Marekani.

Watu wanasema ndo matokeo ya Bush kutokuwa na 'handlers' wake, akina Cheney, baba yake na Bi Condoleeza Rice. Na ndo matekeo ya kuongea bila scripts!

Ione clip hapa:
http://www.youtube.com/watch?v=q0tEQhaK4VM&search=bush%20back%20rub

Monday, July 17, 2006

Hongera Miss F.A.T. 2006! Ana Boxi huyo!



Tanisha Malone & Mo'nique

Natoa pongezi kwa Bi Tanisha Malone wa Newark, New Jersey. Yeye alifanikiwa kutwaa taji la Miss F.A.T 2006, (Fabulous and Thick)! Ukimwona utadhania kazaliwa Afrika. Ni mweusi halafu ana matako makubwa sana! Yaani kabarikiwa hasa hata Miss Bantu wa Bongo ataona wivu! Na najua angekata mitaa Bongo eksidenti zingetokea maana midume ingebakia kumtamzama kwa mshangao. Nilikuwa nacheki comments kwenye neti, nyingi zinazungumzia matako yake yalivyo makubwa, ( big azs)! Juu mdogo lakini chini... midume mtabaki mnahema ovyo!

Kazi anayofanya huwezi kuamini, ni mortuary attendant! Lakini anaongea vizuri na kwa kweli alivyokuwa anatembea anavutia. Kwenye mashindano ya Lingerie (Nguo za ndani) alivaa two piece (Kama bikini)! Nyie mapaja hayo! Shepu kama kibuyu. alisimulia kuhusu jinisi alivyokuwa mdogo alivyoungua na maji ya moto na ikabidi akae hospitali mwaka mzima. Ona makovu kwenye bega na mikono. Lakini kwenye pageant hakuona haya, aliyaonyesha makovu yake bila wasiwasi.

Natafuta full picha yake nibandike. Lakini unaweza kusoma habari za ushindi wake hapo:

http://oxygen.com/specials/monique/tanisha_malone.aspx

WEBSITE YAKE NI: http://www.tanishamalone.com

Friday, July 14, 2006

Sinema ya Gone baby Gone





Mcheza sinema maarufu, Ben Affleck (aliyetaka kumwoa J Lo) yupo hapa Boston anatengeneza sinema inaitwa Gone Baby Gone. Mimi nilibahatika kuwa extra kwenye hiyo sinema. Kama watatumia footage waliyopiga nitakuwa kwenye scene wahusika wakuu wakila chakula kwenye restaurant ya Ghetto. Ilipigwa kwenye restaurant ya Silver Slipper. Insemekana wenye hiyo retaurant walipewa donge nono kwa matumizi ya hapo, eti $100,000! Sijui kama ni kweli. Najua ilibidi wafunge siku nzima, na restaurant enyewe ni ndogo.

Nilibahatika kupiga picha na mcheza sinema maarufu, Ed Harris, alikuwa kwenye sinema kama Radio, Nixon, The Firm, Apollo 13, A Beautiful Mind, na zingine nyingi tu! Ed alikuwa mungwana kweli, alipita kasalimiana na kila extra na kutuuliza majina na kwenye seti akawa anatuita kwa jina. Ben Affleck hajatusemesha hata neno moja. Wengine walisema eti kwa vile tulikuwa weusi, maana huwa anasamlimiana na extras wazungu. Lakini hatukujali tulifanys kazi na tumelipwa!

Pia tulikuwa na John Ashton. Kama mmeona sinema ya Beverly Hills Cop ni yule polisi aliyekuwa na roho mbaya kwa Eddie Murphy.

Cheki walivyogeuza Roxbury kuwa Hollywood set. Hapo ni corner ya Washington St. karibu na Dudley station karibu na kituo cha polisi.

Tuesday, July 11, 2006

Minjemba walikoma Boston!

Ninacheka! Na bado nacheka! Loh! Nimeanguka kwenye kiti, niko kwenye sakafu! Bado nacheka! Mbavu zinauma Jamani, nisaidie! Uwwwwiiiii!

Ni hivi, juzi nilienda kwenye klabu fulani Downtown Boston na rafiki yangu (dada Mmarekani mweusi). Ni msanii mwenzangu na tuliamua kufanya ‘Girls Night Out!” Tulikaa mezani na vinywaji vyetu na sahani ya buffalo wings (mabawa ya kuku enye pilipili). Karibu na sisi kulikuwa na wanaume wawili kutoka Tanzania tena ndo siku yao ya tatu hapa Marekani. Mimi siwajui na wao hawakunijua. Walikuwa wanaongea Kiswahili. Mimi nilijikausha tu, sikutaka wajue naelewa wanasema nini. Nikamwambia rafiki yangu kuwa hao wanaume ni wageni kutoka Tanzania. Aliniomba nimwintroduce kwao na mimi nakakubali ila baadaye kidogo.

Basi, hao minjemba, walikuwa wanasuka mipango ya kuopoa mademu wa kizungu hapo klabuni. Na kutokana na walivyokuwa wanaongea lazima walisuka mpango wa kuonja wazungu kutokea Bongo. Walikuwa wanamcheki kila dada hapo klabuni, mara huyo mbaya, yule mbaya, yule mwembamba, yule hana matako, matiti madogo, yule mzuri kidogo, huyo vile. Wakawa wanajadili watupe offa au la (hatukupata), lakini mmoja kasema nia yao ni kutoka hapo na wazungu. Wakawa wanacheki nani yuko na nani, na wakajadili jinsi ya kuwatongoza. Nikamwambia rafiki yangu walikuwa wanasema nini, tukawa tunacheka.

Basi, kwenye meza karibu na mimi kulikuwa na akina dada wawili wa kizungu, wazuri kweli kweli. Si kawaida yangu kusifia wazungu, lakini hao walikuwa ni wazuri, walijremba vizuri, walivaa vizuri, nywele ndefu zimechanwa vizuri mno, yaani ukiwaona unasema ni ‘perfect’. Tukasema lazima ni models. Walikuwa wamekaa wenyewe wanatazama mambo hapo klabuni. Naona hao minjemba ikawaona. Basi, walikunywa vinywaji vyao kusudi wapate moyo ya kuwa-approach.

Wimbo ukapigwa, na hakuna mzungu aliyewaomba densi, basi wale wakamka na kuwaomba densi. Wale akina dada, bila kusita walikubali. Ungeona nyuso za hao minjemba walivyokuwa na furaha. Wakacheza densi ya kwanza, wakacheza ya pili, mwisho wale akina dada walihamia kwenye meza ya hao minjemba.

Wakati huo watu klabuni wanawatazama, wengine walikuwa wanacheka. Na mimi nikawacheki vizuri. Nikasikiliza maongezi ya hao akina dada. Halafu nikacheki mikono yako, duh, mikubwa! Ikaniingia! DAH! Kumbe si akina dada hao ni midume! Ni ma transvestite! Sasa nikabakia nawatazama wa waBongo kwa mashangao! Nikasema hao akina kaka hawajui wameopoa akina nani, maana usoni walionekana kuwa na furaha kama vile wameshinda bahati nasibu! Na huyo rafiki yangu kaniambia tujiandae kwa ajili ya sinema ya bure.

Nilitaka kuondoka kuelekea kwenda nyumbani, lakini nikamua kukaa maana nilitaka kujua itaishia vipi. Wale akina kaka wakaanza kuwaambia, wako Boston kwenye business, na wako Hoteli fulani. Wakawa wanawaambia habari za Tanzania na kuwa ingekuwa vizuri siku moja wawatembelee huko. Wana majumba ya fahari, na watawapeleka mbuga za wanyama. Mwisho wakawakaribisha hotelini kwao kusudi wapate vinywaji zaidi. Pia walikuwa na zawadi kutoka Tanzania ambazo walitaka kuwapa. Nilishangaa, wale wawili wakasema, “Okaaay!” Basi wakaamka wakasema wanaenda restroom, kujipodoa halafu watarudi.

Walivyoinuka kwenda huko na mimi nikaona ni chensi ya kuwaonya. Rafiki yangu kaniambia nisiwaonye. Lakini nikasema bora niwaonye maana wakifika hoteli na wakikuta si wanawake inaweza kuwa balaa. Nikaamka na kwenda kwenye meza ya hao minjemba, nikawasalimia kwanza kizungu. “Hey guys, how are you?”

Wakajibu, “We are good” Nikasema kwa kiswahili, “Nafurahi kusikia hivyo!” Wakanitazama kwa mshangao, “Heh, Dada Mbongo wewe?”

Asante Pina Colada ulimi ukawa unateleza...nikajibu, “Mimi Mbongo ndiyo. Na nyie kama kaka zangu, nimeona niwaulize, mtawafanya, au mtafanywa?” Wale akina kaka wakajibu, “Heh, nini tena!’ Nikajua kuwa bado hawajajua wako na akina nani.

Nikawambia, “Hamjui kuwa hao akina dada wakizungu mliyonao ni akina kaka! Shauri zenu!” Ungeona nyuso zao, yaani ilikuwa “Kodak Moment!” Bahati mbaya camera niliacha nyumbani. Mmoja kaanza kuongea kwa kigugumizi, Yaa yaa nii, ni wa se se senge!” Nikajibu, “Naam!”

Ungeona ile minjemba ilivyoshikwa na wasiwasi. Mmoja kumwambia mwenzako, “We Bwana si nilikuambia wazuri mno hao na kwa nini wazungu wenzao hawakuwataka!” Waliinuka haraka, na mimi nilitia ndogo ndogo na kurudi mezani kwangu kwa rafiki yangu. Nikamweleza ilivyokuwa naye akawa anacheka kwa sauti mpaka watu klabuni wanatutazama. Rafiki yangu kasema wakome kutaka wazungu. Wale akina kaka wakatoka haraka, haraka klabuni kabla wale trans wamerudi kutoka restroom.

Wale trans wakarudi na kukuta minjemba wamekimbia! Walirudi kwenye ile meza yao ya awali. Wakaonekana na huzuni kidogo. Nikaona watu wengine wanacheka cheka nadhani walijua ilitokea nini. Na sisi tulitoka klabuni na ile minjemba sijui ilipotelea wapi! Naona walikodi teksi kwenda hotelini kwao.

Siku tatu zimepita, na mimi kila nikikumbuka nacheka. Jamani, hapa Marekani wakati mwingine huwezi kujua nani mwanaume, nani mwanamke. Wanawake wengine wanavaa kidume, wanatembea kidume, utadhani wanaume, na pia kuna wanaume kama hao wanapenda kuwa kama wanawake, tena ni wazuri kuliko wanawake.

Kwa hiyo, muangalie mnataka kuopoa nani. Najiuliza, je, wangefika huko hotelini sijui nani angekunjwa, maana na wale minjemba walikuwa wamekunywa hasa. Wangeenda huko hotelini na kukuta wako sawa nao, ingekuaje?!!

Mbavu sina jamani.