Thursday, March 08, 2007

Ni Ubaguzi, Uonevu au Upendeleo?

UPDATE: ANTONELLA KATOLEWA ALHAMISI. Alilia kweli. Lakini amepata offers za kupiga picha uchi Playboy magazine na ku-host Girls Gone Wild. Frenchie ata sue American Idol kwa uonevu!
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@



Kwa wapenzi wa American Idol, naomba maoni yenu. Mnakumbuka mwaka 2003, (msimu wa pili aliyoshinda Ruben Studdard) kulikuwa na dada fulani, Frenchie Davis. Huyo dada ni mweusi, mnene na ana zinga la sauti. Yaani anaimba huyo si mchezo, Jennifer Hudson alie kwake.

Kwa bahati mbaya, Frenchie aliwaambia Producers kuwa akiwa mwanafunzi, alipiga picha nusu uchi (topless) kwa ajili ya kupata pesa za kumsaidia kulipia masomo yake Howard University. Producers waliamua kumfukuza kwenye show. Mungu ni mwema na Frenchie sasa ni mwimbaji maarufu kwenye mchezo wa kuigiza, Rent, huko Broadway, New York.

Msimu huu wa American Idol kuna dada fulani, Antonella Barba, ambaye naye ali picha za uchi kwenye internet. Hajafukuzwa na bado yumo. Amepiga picha za uchi kabisa. Kwenye picha zingine anamfurahisha mwanaume kwa kumnyonya ume wake! Zingine kapanua miguu. Loh! Ajabu hajafukuzwa kwenye American Idol.

Sasa imekuwa issue, mpaka Rosie O’Donell anaongelea kwenye show yake The View, yeye anasema kuwa eti ni ubaguzi. Pia wiki hii kulikuwa na maandamano mbele ya Kodak Theater Hollywood kupinga Antonella kuendelea kuwa kwenye show wakati Frenchie alitolewa.
Na Frenchie mwenyewe sasa anataka maelezo kutoka kwa Producers wa American Idol. Anasema kuwa anamtakia huyo Antonella mema lakini ni lazima wamweleze kwa nini alitolewa na kudhalalishwa wakati ule na picha zake siyo mbaya kama za Antonella.

FYI- Producers wanajitetea kwa kusema eti Frenchie alilipwa hela kwa ajili ya zile picha wakati za Antonella zilibandikwa na boyfriend wake.

Mimi navyoona ni ubaguzi. Frenchie ni mweusi na ni mnene. Huyo Antonella ni mwembamba na wanasifia uzuri wake. Lakini jamani uwongo mbaya, Antonella hawezi kuimba.

Mnasemaje wasomaji?

Kwa habari zaidi soma hapa:

http://www.showbuzz.cbsnews.com/stories/2007/03/06/tv_realty_tv/main2540578.shtml?source=RSSattr=Entertainment_2540578

2 comments:

Anonymous said...

Nadhani nimechelewa hapa. Ubishi sina kwamba Antonella kuimba hawezi wala hakustahili kuwa wenye top 24. lakini kwa upande wa pili utagundua Frenchie alikubali kuwa picha za topless ni zake lakini Antonella amekana kwamba picha siyo zake na ukiangalia vema zile picha utagundua inawezekana ni za mdada mwingine tena mwenye miguu mirefu kuliko Antonella. Nadhani maproducer wangemfukuza halafu wagundue hizo picha ni feki wangekuwa wamefanya makosa. Kwa wiki hii ilikuwa vema ametolewa kwa kura, nadhani ni haki kwa sababu hawezi kuimba kama wenzake na jaji Simon Cowell alimweleza wazi kwamba shida ni kuwa hawezi kuimba zaidi ya hapo, nukta.

Chemi Che-Mponda said...

Niliona picha kadhaa za huyo Antonella akiwa nusu uchi au uchi kabisa, na moja ananyonya nanahii ya mwanaume. Hiyo ya kunyonya ndo anasema siyo yeye. Kuna nyingine kajipanga na wasichana wengine, wote wako topless matiti nje nje. Hajakataa kabisa. Walimhoji kwenye TV na anasema anafikiria kama atapose kwenye Playboy na ku-host Girls Gone Wild. Lakini ni nora katolewa maana sauti ya kuimba hana ukilinganisha na waliobaki hasa kama Melinda na Lakisha.