Showing posts with label Bloggers. Show all posts
Showing posts with label Bloggers. Show all posts

Saturday, April 07, 2018

Serikali ya Marekani Kufuatilia blogu zote DunianI!

Kama una blogu, serikali ya Marekani itakuchunguza!  Watafuatlia zipi zina nguvu ya kushawishi wasomaji....pia watafuatilia waandishi wa habari, magazeti na wahariri.

******************************************

Homeland Security to Compile Database of Journalists, Bloggers

The U.S. Department of Homeland Security wants to monitor hundreds of thousands of news sources around the world and compile a database of journalists, editors, foreign correspondents, and bloggers to identify top “media influencers.”

It’s seeking a contractor that can help it monitor traditional news sources as well as social media and identify “any and all” coverage related to the agency or a particular event, according to a request for information released April 3.

The data to be collected includes a publication’s “sentiment” as well as geographical spread, top posters, languages, momentum, and circulation. No value for the contract was disclosed.

“Services shall provide media comparison tools, design and rebranding tools, communication tools, and the ability to identify top media influencers,” according to the statement. DHS agencies have “a critical need to incorporate these functions into their programs in order to better reach federal, state, local, tribal, and private partners,” it said.

The DHS wants to track more than 290,000 global news sources, including online, print, broadcast, cable, and radio, as well as trade and industry publications, local, national and international outlets, and social media, according to the documents. It also wants the ability to track media coverage in more than 100 languages including Arabic, Chinese, and Russian, with instant translation of articles into English.

The request comes amid heightened concern about accuracy in media and the potential for foreigners to influence U.S. elections and policy through “fake news.” Nineteen lawmakers including Reps. Josh Gottheimer (D-N.J.), Lee Zeldin (R-N.Y.), Ron DeSantis (R-Fla.), and Sen. Ted Cruz (R-Texas), sent a letter to Attorney General Jeff Sessions last month, asking whether Qatar-based Al Jazeera should register as a foreign agent because it “often directly undermines” U.S. interests with favorable coverage of Hamas, Hezbollah and al-Qaeda’s branch in Syria.

The DHS request says the selected vendor will set up an online “media influence database” giving users the ability to browse based on location, beat, and type of influence. For each influencer found, “present contact details and any other information that could be relevant, including publications this influencer writes for, and an overview of the previous coverage published by the media influencer.”

A department spokesman didn’t immediately return a phone call and email seeking comment.

Responses are due April 13. Seven companies, mainly minority- or women-owned small businesses, have already expressed interest in becoming a vendor for the contract, according to the FedBizOpps web site.

Monday, September 07, 2015

Sheria Mpya ya Mtandao Mwisho Chumbe?

Logo ya Zanzibar Diaspora Association (ZADIA)
Na Muandishi wetu swahilivilla Blog
Wanadiaspora wameelezea wasiwasi wao kuwa sheria mpya ya Makosa Ya Mtandao iliyoanza kufanya kazi tarehe mosi mwezi huu nchini Tanzania, huenda ikaishia Chumbe, imefahamika.
Hayo yamekuja kwenye kongamano maalum lililoandaliwa na Jumuiya Ya Wazanzibari Waishio nchini Marekani (ZADIA) kujadili Sheria Mpya ya Makosa Ya Mtandao na Athari zake Kisiasa.
Wageni rasmi katika kongamano hilo lililofanyika kwa njia ya simu walikua ni Mwandishi khabari Bi Salma Said, na Mwanadiplomasia mstaafu Bw. Muhammed Yussuf Mshamba.
Utata wa Kisheria:
Akizungumza kwenye kongamano hilo, Bi Salma Said alisema kuwa sheria hii itakuwa na utata kutokana na jinsi ya mchakato mzima wa kuipitisha ulivyokwenda. "Sheria imepitishwa kimabavu, kwani wadau wote hawakushirikiswa, pia ilipitishwa wakati Wabunge wa upinzani wakiwa wametoka Bungeni" alifafanua Bi Salma na kuongeza kuwa Baraza la Wahariri Tanzania liliikataa sheria hiyo na kupitisha azimio la kumshauri rais Kikwete asiitie saini, lakini Mheshimiwa rais aliitia saini.
Kwa upande wake, Bwana Muhammed Yussuf Mshamba ambaye pia ni Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alielezea wasiwasi wake juu ya uwezekano wa sheria hiyo kutekelezeka kwa vile mfumo uliotumika kuiptisha haukukidhi haja.
Akizungumza katika kongamano hilo, Bwana Mshamba ambaye aliwahi kuwa mtia nia wa kuwania urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM alisema "Sharia ile ilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini Zanzibar hawakupata nafasi ya kuiangalia".
"Kwa mujibu wa kifungu cha 234 cha Katiba ya Zanzibar, sharia zote zinazopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambazo zinatakiwa kutumika Zanzibar na Bara, kwa mujibu wa kipengele kile ni lazima Baraza la Wawakilishi la Zanzibar lipewe nafasi ya kuziangalia". 
Alisema Bwana Mshamba na kuongeza kuwa, sheria ile ilipitishwa wakati Baraza la Wawakilishi limeshavunjwa na hakukuwa na njia ya kuliitisha angalau kwa kikao cha dharura ili kuweza kuijadili.

Sunday, March 01, 2015

Team Michuzi Production Yarekodi Kwa Weledi wa Hali ya Juu Mnuso wa Tanzania Bloggers Party Serena Hotel Jijini Dar es Salaam

Ankal akiwa na MD wa Michuzi Media Group (kulia kwake) pamoja na kikosi kazi cha Team Michuzi Production chini ya Production Manager Barbra Kilugira (wa tatu kushoto) ambayo ilipata heshima ya kurekodi mnuso wa kihistoria wa Tanzania Bloggers Network (TBN) Meet and greet Party katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia March 1, 2015. Mnuso huu ulifanikiwa sana kwa udhamini mkubwa wa VODACOM TANZANIA (wadhaini wakuu), NMB, COCACOLA, RAHA.COM na SERENA HOTEL. 

Saturday, November 23, 2013

Teteeni nchi badala ya kuiponda kwenye mablogu - Rais Kikwete awaambia Watanzania

Teteeni nchi badala ya kuiponda kwenye mablogu, Rais Kikwete awaambia Watanzania

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

  • Teteeni nchi badala ya kuiponda kwenye mablogu, Rais Kikwete awaambia Watanzania 

Watanzania waishio nje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema wajibu mkuu wa Watanzania wanaoishi nje ya nchi ni kuisemea vizuri, kuihangaikia na kuitetea nchi badala ya kushinda kwenye mablogu wakiiponda, kuibeza na kulalamika.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa kuishi kwa Watanzania nje ya nchi kutaonekana jambo la maana zaidi ikiwa watatumia rasilimali na fursa wanazozipata ugenini kusaidia kubadilisha hali na maisha ya ndugu zao waliobakia Tanzania.

Rais Kikwete pia amewaonya Watanzania hao wasije kuchanganyikiwa na kujichanganya wenyewe kwa kuiga tamaduni za kigeni kupita kiasi. 


Rais Kikwete alikuwa anazungumza na Watanzania waishio nchini Poland usiku wa jana, Alhamisi, Novemba 21, 2013, kwenye Hoteli ya Bristol mjini Warsaw ambako alifikia wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku nne katika Poland.

Aliwaambia Watanzania hao na familia zao: “Matumaini na matarajio yetu sisi tuliobakia nyumbani ni kwamba mtaisemea vizuri nchi yetu, mtaitetea nchi yenu, mtaihangaikia nchi na kuleta faida nyumbani. Ni jambo haliingii akilini kuwa baadhi yenu mnaweza kuishi hapa na kazi yenu ikawa ni kushinda kwenye mablogu mkilaumu nchi yenu wenyewe. Nchi mbaya,
viongozi hawafai..mnapata faida gani. Mnazo nchi ngapi?”

Aliongeza Rais Kikwete: “Kuhangaikia nchi yetu ni wajibu wenu ambao hamwezi kuukwepa. Matumaini yetu ni kwamba asukuma mbele maslahi ya nchi yenu, mtatetea ustawi wa nchi yenu na ndugu zenu. Fursa zilizoko hapa mnazijua wenyewe, sisi hatuzijui. Nyie ndio mnaishi hapa, sisi tuko mbali na hatuwezi sisi kutegemewa na kutarajiwa tufanye
mambo ya hapa ambayo hatuyajui.”

Alisisitiza Rais Kikwete: “Mbona kazi za ma-Ngo’s mnazifanya vizuri bila kusukumwa ama kushawishiwa lakini kazi za kusaidia ndugu zenu hamfanyi? Kama hata hamwezi kusaidia ndugu zenu mnachangia nini nchi yenu?”
Rais amesema kuwa kwa Watanzania waishio nje kuonekana wanajali na kutetea nchi yao kutasaidia kujenga hoja ya msingi kuhusu umuhimu wa kuanzishwa kwa uraia pacha (dual citizenship) ambao Watanzania waishio nje wanaulilia. “Mnaweza kuhalalisha hoja ya uraia pacha kwa kuwa watu wenye faida kwa nchi.”

Kuhusu ombi lao la uraia pacha, Rais Kikwete amesema kuwa ni wajibu wa Watanzania waishio nje kuongeza kasi ya kuchangia mjadala kuhusu suala hilo ili likubaliwe kuingizwa kwenye Katiba Mpya.

“Rasimu ya kwanza ya Katiba ililikataa jambo hilo kwa sababu hili ni jambo lisilokuwa na ushabiki na upenzi mwingi nyumbani. Ujumbe wangu kwenu ni jipangeni vizuri kutetea hoja yenu hii. Saidieni mjadala wa jambo hilo badala ya
kushinda kwenye mablogu mkijadili siasa na hivyo kusahau yenye maslahi kwenu.”

Kuhusu kuiga tamaduni za nchi nyingine na kusahau za nyumbani, Rais Kikwete aliwaambia kuwa inaelekea kuwa baadhi wachache wanaoishi nje ya nchi, wamejichanganya na kuchanganyikiwa kiasi cha kusahau mambo ya kwao.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo baada ya mmoja wa Watanzania kudai kuwa suala zima la mahari limepitwa na wakati na kuwa kutoa mahari ni sawa ni kuwauza watoto wa kike.

Rais ambaye alionyesha kushangazwa na kauli hiyo, alijibu: “Msiige mambo ya kigeni kiasi cha kuanza kuchanganyikiwa.”

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

22 Novemba, 2013

Sunday, February 10, 2013

WITO KWA MABLOGA WETU KUWA WABUNIFU BADALA YA KUIBA AU KUNUKUU TU KAZI NA PICHA ZA WENZAO BILA IDHINI

WITO KWA MABLOGA WETU KUWA WABUNIFU BADALA YA KUIBA AU KUNUKUU TU KAZI NA PICHA ZA WENZAO BILA IDHINI

by Kitoto
Ukingoni mwa Ziwa Nyasa- Revo Meza
Wimbi la “blogging” liliikumba dunia kati ya 1995 hadi 1998 na kuanza kumea kwetu Tanzania kupitia mwanahabari Ndesanjo Macha miaka kumi iliyopita. Wakati Ndesanjo anaanza kublogu si wengi tuliomwelewa. Nakumbuka alivyokua akiniongelea juu ya fani hii kwa hamasa kwenye 2002. Baadaye kidogo aliendesha Jikomboe, blogu lililokua na taswira ya majani mabichi ya ukoka. Enzi hizo hakukua na hata senti moja aliyoichuma.
Ndesanjo Macha
Ndesanjo Macha- mwasisi wa blogu Tanzania
Ndesanjo alikua akisema blogu ni dunia ya kesho ya mawasiliano.
Wakati huo vyombo vikubwa vya habari nchi zilizoendelea vilianza kuona umuhimu wa blogu vikaanza kuunda idara pembezoni mwa tovuti zake mama. Kwetu wenye magazeti wengi hawakupenda wanablogu;waliwaona washindani.
Mwaka ambapo wanablogu wetu walianza kuchomoza ilikua 2006 baada ya kifo cha wapenzi wawili wa Kitanzania waliouliwa kinyama Marekani. Blogu la Michuzi (ambalo halikua maarufu kama leo) na Radio Butiama (inayojulikana kwa jina Podcast) zilisimama dede kutangaza habari hizo. Hapo ndipo miye binafsi nilipoanza kuona namna blogaz walivyokuwa na mwendo mkali - zaidi ya vyombo vya habari vya kijadi.
Nilianza rasmi kublogu mwaka 2007- nikisaidiwa na Ndesanjo na wanabloga wengine walionitangulia; akina Simon Kitururu, Jeff Msangi (Bongo Celebrity) mathalan. Nilichogundua siku za mwanzo ni kwamba Blogaz husaidiana sana. “Ukiwa mbinafsi huendelei kama Bloga” alisisitiza Ndesanjo.
Goats feeding on rubbish
Mbuzi wetu Bongo wakila kila aina ya takataka mitaani. Nyama yake tamu. Lakini je, ina nini kinachotudhuru tusichokijua? Nilipiga picha hii, Zanzibar, mwaka 2011.
Leo Jikomboe na ule ukoka havipo tena.
Ndesanjo, mwasisi wa blog za Kiswahili duniani, anafanya kazi shirika la habari- Global Voices. Kati ya mamia ya waandishi wa shirika hilo la kimataifa, Mtanzania huyu anaongoza kwa habari asilia za uchambuzi zaidi ya 4,200 . Tofauti ya mtu kama Ndesanjo na baadhi ya blogaz ni kwamba yeye kiasilia ni mwanahabari hivyo anachanganya ujuzi na mitindo hii miwili ya kusanifu matukio. Si ajabu mwaka jana Ndesanjo alishinda tuzo la Mwanablog bora wa Afrika.

KWA HABARI ZAIDI BOFYYA HAPA: