Showing posts with label Church. Show all posts
Showing posts with label Church. Show all posts

Friday, September 16, 2016

Usabato na Historia ya Aibu

HISTORIA HALISI YA WASABATO: AIBU TUPU

Imeandikwa na Padri Titus Amigu

Ndugu zanguni nitaendelea na mada yetu ya “viboko hamsa wa ishirini” lakini naomba nikatishe kidogo nipate kujibu swali moja linalojirudia rudia sana. Swali lenyewe naulizwa kwa namna nyingi mno. Mtu wa mwisho ameniuliza akisema hivi: “ Asante sana baba gombera mstaafu, hivi huyu Bi Ellen G. White ni nani katika Kanisa Katoliki? Mbona amekuwa akishambulia sana Kanisa Katoliki au kuna makanisa mengine huanzishwa na misingi yao ni lazima kushambulia Kanisa Katoliki?
Jibu fupi: Bi Ellen G. White ni mmojawapo wa waanzilishi wa kanisa la Wasabato lakini fundi sana wa kulitukana Kanisa Katoliki. Yeye hakuwamo ndani ya Kanisa Katoliki na wala hakujihusisha nalo kwa nia njema isipokuwa aliondokea kuongoza kulitukana.

Wala si siri yapo makanisa ambayo huanzishwa na misingi yao ni lazima kulishambulia Kanisa Katoliki kwa sababu zao mbalimbali. Kanisa mojawapo kati ya hayo ndilo kanisa aliloshiriki Bi. Ellen White kulianzisha yaani kanisa la Sabato. Inasikitisha sana na kukera sana, lakini tutafanyaje. Ndiyo hivyo tena, kisera, kanisa la Sabato limepania kulibomoa Kanisa Katoliki. Sisi hatuwezi kuwachukulia hatua ya kiuhalifu isipokuwa kufahamishana kama ninavyokusudia kufanya ili tukae chonjo nalo tu. Kumbe kwa busara ya maisha, anayekuwinda walau mjue tu kusudi ujue namna ya kumkwepa. Wala si lazima upigane naye.

Sasa kusudi vijana mmwelewe vizuri mtu huyo aheri nikupeni historia nzima ya kuanzishwa kwa kanisa la Wasabato. Katika historia hiyo mtaona aibu ya kushindwa utabiri wa mwisho wa dunia. Cha kushangaza waliposhindwa kutabiri mwisho wa dunia kama walivyojinasibu kuweza, wakageukia kulitukana Kanisa Katoliki ambalo halina kosa lolote na halikuwafanya chochote.

Hivi acheni niitumie fursa ya kujibu swali hili kwa kuwaleteen historia halisi ya Kanisa la Wasabato. Nawaanikieni hadharani aibu yao, aibu inayowatia hasira na hasira yenyewe kuilekeza kwa Kanisa Katoliki ambalo halijawakosea.

Jibu hili nimewahi kuliandika kwenye Gazeti la Kiongozi na vile vile kulirusha hewani kwa njia ya radio. Lakini kwa kuwa bado naendelea kuulizwa, kwa mitindo mbalimbali, kila uchao napenda nilijibu tena sasa kwa kupitia ukurasa wangu wa Facebook. Sina nia ya kuleta uchochezi. Najibu swali kwa kadiri inavyostahili tu.

Jibu refu: Wakatoliki tunatukanwa kwa sababu Wasabato wanajaribu kufunika aibu yao ya kihistoria na wanadhani matusi ndiyo njia ya kuliua Kanisa Katoliki. Hawajui kwamba matusi hayawezi kumharibu mtu isipokuwa kumfedhesha mtukanaji tu. Waungwana hawatukani. Kumbe, aheri tuielewe historia ya dhehebu la Wasabato au S.D.A tupate kuwapuuza wanaotutukana huku wakijiabisha wenyewe. Basi, historia hiyo ya aibu inayofichwa ndiyo hii ifuatayo:
Ni hivi ndugu zanguni, kwa kuiweka bayana historia ya Wasabato, tuambatane katika kuwaelewa watu wanne ambao hutajwa kama watangulizi au waasisi wa dhehebu la Wasabato. Mwishoni nitayapembua waliyofundisha kibiblia na kisaikolojia.

Mtu wa kwanza ni William Miller, wa pili ni Hiram Edson, wa tatu ni Joseph Bates na wa nne na wa mwisho awe Bi Ellen G. White.
Tukianza na Bw. William Miller, yeye alizaliwa mwaka wa 1782 katika mji wa Pittsfield, Massachusetts, huko Marekani.  Ingawa alizaliwa katika familia ya Kikristo, aliuacha Ukristo alipokuwa kijana mbichi.  Kwa kweli hakuiamini Biblia kuwa neno la Mungu.  Basi, akajiunga na jeshi. Baada ya kutumika kama mwanajeshi kwa muda mfupi, akaishi kama mkulima.  Kumbe, mwaka wa 1816, akaongoka na kuurudia Ukristo wake kwa kasi mpya.  Kwa kweli, tangu mwaka huo wa kuongoka kwake, Bw. William Miller alisoma unabii kwa kina na hasa unabii uliohusu kurudi kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. 

Kumbe, kutokana na kujifunza huko, Bw. William Miller akashawishiwa kwamba mwisho wa dunia ungetimia mwaka 1843.  Kifupi, Bw. William Miller alishawishiwa kufundisha jinsi hiyo na unabii wa kitabu cha Danieli 9:24-27, unabii unaohusu majuma sabini yaliyowekwa kwa ajili ya watu wa Mungu, taifa la Israeli.

Zaidi ya hayo, katika Danieli 8:13-14, kuna unabii wa watakatifu wawili wanaoulizana lini patakatifu patatakaswa.  Mintarafu unabii huo, Bw. William Miller alitafsiri kwamba patakatifu patakapotakaswa, ni dunia hii iliyochafuliwa na dhambi za kila sampuli.  Kwa maoni yake, mwaka wa 1843 B.K., ndio mwaka ambao Yesu Kristo angerudi katika dunia iliyonajisiwa kupita kiasi na dhambi na hivyo kuitakasa kabisa kwa kuwapo kwake.
 
Msimamo huu ulimfanya awe maarufu sana katika sehemu nyingi za Marekani, na hatimaye akawa mhubiri mkubwa wa dhehebu la Kibaptisti.  Kwa kuwa mwisho wa dunia ulikuwa unaambatana na kurudi kwa Yesu Kristo, ambako kwa Kiingereza huitwa “Christ’s Advent”, wafuasi wake walianza kujulikana kama “Adventists” au kwa Kiswahili “Waadventisti”, yaani “Watu watarajiao kurudi kwa Kristo”. Ijapokuwa mwanzoni hakutaja tarehe bayana ya kurudi kwa Yesu, punde si punde alisema kurudi kwa Yesu kungekuwa kati ya tarehe 21 Machi, 1843 na 21 Machi, 1844. 

Baada ya mambo kufikia hapo, mfuasi mmoja wa Bw. William Miller aliyeitwa Samwel Snow, akawa jasiri zaidi na kutaja kwamba Kristo angerudi tarehe 22 Oktoba, 1844 saa 6.00 usiku; yaani ndipo parapanda litakapopulizwa, mbingu kukunjwa kama kurasa, na Yesu Kristo kufika  kwa utukufu mwingi.  Lakini mambo hayakutukia hivyo walivyohubiri. Basi, kwa vile Kristo hakurudi kama walivyotarajia, Bw. Miller akakiri kukosea kwake, lakini akawaonya wafuasi wake wasisahau kwamba Kristo atarudi upesi. 

Kwa bahati mbaya, Bw. William Miller alifariki mnamo mwaka 1849 ndoto yake ya kumwona Yesu akirudi upesi ikiwa bado haijatimia.  Hadi hapo, ieleweke kwamba Bw. William Miller, hakuwahi kuwa Msabato.  Hivyo kama Mbaptisti, alikuwa anasali siku ya Bwana, yaani Jumapili au Dominika. Kutokana na kutokutumia kwa utabiri wa Bw. William Miller wafuasi wake wengi wakarejea nyuma.
Basi, tumwachie Bw. William Miller hapo, nasi tusonge mbele tukamwangalie mtu wa pili, yanii Bw. Hiram Edson.  Kwa bahati, bwana huyu alikuwa kati ya Waadventisti wachache waliobaki baada ya kuvunjika moyo kwa wafuasi wengine wa William Miller kutokana na kutorudi kwa Kristo kama ilivyotazamiwa.  Kwa upande wake  kwa kusudi la kuwafariji wenzake kwenye huzuni yao, yeye alidai kwamba Mungu alikuwa ametoa jibu kwa aibu yao kwani alipata mafunuo juu ya kile kilichofanyika siku hiyo ya tarehe 22 Oktoba, 1844. 

Kwa jinsi gani? Sikiliza. Alifundisha kwamba alioneshwa kulikuwa na hekalu mbinguni mfano wa hekalu la duniani. Akadai hekalu hilo lilikuwa na sehemu mbili: patakatifu na patakatifu pa patakatifu, yaani sawa na lilivyokuwa hekalu la Kiyahudi zamani zile.  Kumbe, kilichofanyika siku hiyo ya tarehe 22 Oktoba,  ni kwamba Kristo alitoka patakatifu na kuingia patakatifu pa patakatifu.  Akasema kwisha Yesu kuingia patakatifu pa patakatifu atabaki humo mpaka siku atakapokuja duniani mara ya pili. 
Mintarafu swali, Yesu anafanya nini siku zote hizo? Akasema Yesu anafanya ‘hukumu ya upelelezi’ kwa Kiingereza “investigative judgement”.  Kwa maelezo hayo mapya akadai kwamba kitu alichokuwa amekosea Bw. William Miller kilikuwa tafsiri tu, kwa maana kwamba utakaso uliofanywa tangu siku ile ya tarehe 22 Oktoba haukuwa wa dunia hii, bali wa patakatifu pa patakatifu katika hekalu hilo la mbinguni.

Kwa namna hii, Bw. Hiram Edson akawa Mwadventista wa kwanza, hata kabla hajawa Msabato, kuleta duniani maelezo ya kuwafariji wenzake kwa kutorudi kwa Kristo siku ya tarehe 22 Oktoba 1844.  Hivi basi, mchango wake mkubwa kwa teolojia ya Wakristo ambao baadaye walijiita Wasabato ni suala  hilo la ‘hukumu ya upelelezi’.  Kifupi, kwa maelezo hayo, Wasabato wanafundisha kwamba Yesu Kristo, tangu 22, Oktoba 1844 yuko huko mbinguni, katika patakatifu pa patakatifu akichunguza kwa kina maisha ya Wakristo wote ambao majina yao yapo katika kitabu cha uzima wa milele na kuamua nani anastahili kufutiwa dhambi zake zilizosamehewa wakati alipoamini.  Hivyo, kila mtu anayeonekana kurudi nyuma, naye hakutubu dhambi zake zote, anafutwa jina lake kutoka katika kitabu cha uzima na hivyo huko, mwishoni mwa historia, atakosa nafasi katika ufufuo wa kwanza.  Kinyume chake, kwa upande wao, wote ambao walitubu dhambi zao, majina yao yanabaki kitabuni pasipo kufutwa, nao watafufuliwa katika ufufuo wa kwanza.
Ndugu zangu, hadi hapa umeshagundua mafundisho ya uongo. Mbinguni hakuna hekalu. Huo ndio ukweli wa kibiblia maana mwandishi wa kitabu cha Ufunuo anatuandikia habari za maono yake matakatifu mintarafu Yerusalemu ya mbinguni akisema “Nami sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Bwana  Mungu Mwenyezi na Mwanakondoo, ndio hekalu lake” (Ufu 21:22). Sasa iweje Bw. Hiram Edson amzungumzie Yesu anayetoka patakatifu kuingia patakatifu pa patakatifu? Zaidi ya hayo, mafundisho ya hukumu ya upelelezi ni uzushi kwa sababu ni matokeo dhahiri ya tafsiri potofu ya neno la Mungu. 

Haya tuachane naye, nasi twende tukamwangalie mtu wa tatu, ambaye ni Bw. Joseph Bates.  Kikazi, Bw. Joseph Bates alikuwa baharia.  Bada ya kustaafu kwake alihamia Fair Haven, katika jimboni Massachusetts, huko huko Marekani.  Kwa kweli, Bw. Joseph Bates ni mmoja wa viongozi maarufu  wa Waadventisti.  Yeye aliposoma maandishi ya Thomas Prebble kuhusu Sabato, alishawishiwa kuamini kwamba Sabato ya Wayahudi ilikuwa siku halali kwa watu wote wa Mungu kuabudu.  Basi, akaandika kijitabu chake kilichoitwa, “The Seventh Day Sabbath, a Perpetual Sign””. 
Baada ya kitabu hicho Bw. Joseph Bates aliendelea kuandika vijitabu kuhusu Sabato.  Hivi bwana huyu anakumbukwa sana na Wasabato kwa mchango mkubwa katika kuirudisha Sabato ya Agano la Kale. Kwa kweli, ni yeye aliyekuwa wa kwanza kutafsiri siku ya Jumapili kama siku ya alama ya mnyama; na kwamba siku ya Sabato ndiyo muhuri wa Mungu kwa watu wake walio waaminifu, yaani Waadventisti Wasabato 144,000 (rej. Ufu 7:4). 

Kutokana na ushawishi wake huu, kuabudu siku ya Jumamosi, kukaanza kupata nguvu nyingi, zilizoambatana na vitisho vya hukumu kali kwa wanadamu wote wasioishika Sabato  ya Agano la Kale. Kifupi, miongoni mwa Waadventisti waliomfuata Bw. Joseph Bates kwa karibu, walikuwa ni James na mkewe Ellen White.  Kumbe, Bi Ellen White ndiye aliyeuendeleza usabato, kwa motomoto zaidi kuliko watu wengine wote naye anaheshimiwa na Wasabato kama nabii wao.  Kwa hali hii ya mambo, yafaa tumalizie historia hii fupi kwa kumwangalia mwanamama huyo hata kama ikiwa kwa kifupi sana.

Ndugu zanguni, Bi Ellen G. White, anafahamika pia kwa jina la Bi Ellen Gould Harmon. Ni kwamba kabla hajaolewa alikuwa anaitwa Ellen Gould Harmon na baada ya kuolewa kwake na mpenziwe James White, aliyekuwa mhubiri wa kibaptisti aliyekuwa muadventisti hapo tarehe 30 Agosti, 1846 akajulikana kama Bi Ellen Gould White.

Kwa kufupisha mambo, Bi Ellen Gould Harmon alizaliwa mwaka 1827 huko Goharm, jimboni Maine, maili kumi hivi toka Portland.  Akiwa mtoto mdogo bado, wazazi wake walihamia Portland kwenyewe.  Hapo mwanzoni, yeye pamoja na familia yake walikuwa wafuasi wa dhehebu la Methodisti.  Kumbe, familia ya akina Ellen ilijiunga na uadventisti baada ya Bw. William Miller kuhubiri mjini Portland katika mwaka wa 1840 na 1842.  Lakini kwa kuwa familia hiyo ilisadiki maneno  ya Bw. William Miller, kanisa lao la Methodisti liliitenga familia hiyo. Familia nzima ilitengwa kwa sababu ya kuyapokea mafundisho ya Kiadventisti.  Kwa ujumla, mchango wa Bi Ellen White ulianza kama alivyodai mwenyewe kwamba alipokea maono mengi nyakati mbalimbali, maono ambayo baadaye yalimfanya ajulikane kama nabii wa Waadventisti.  Inasemekana maono yake ya kwanza yalimjia mwezi Desemba, 1844, yaani si muda mrefu sana baada ya watu kukatishwa tamaa na kutokurudi kwa Yesu Kristo. 

Bi Ellen White aliingia ulingoni akidai kuliona kundi la Waadventisti wakisafiri katika njia yenye mwanga wa utukufu, huku wakiongozwa ya Yesu hadi walipoufikia mji wa Mungu.  Bi Ellen akadai kwamba baada ya kuonywa katika maono ya pili asikae kimya juu ya yale aliyooneshwa, alilazimika kutangaza na kuyahubiri maono yake wazi mahali pengi.  Kuanzia hapo, Waadventisti wa Portland na Maine wakaanza kumtambua Bi Ellen White kama nabii wao na kusisitiza kwamba Roho Mtakatifu alikuwa juu yake na kwamba ilikuwa ni lazima unabii wake ufuatwe na Waadventisti wote popote pale walipokuwa. 

Kama jambo hilo halitoshi, mwezi Februari 1845, Bi Ellen White alidai kupata maono yaliyothibitisha maono ya Bw. Hiram Edson mintarafu kitu kilichotokea hapo tarehe 22 Oktoba 1844, yaani kwamba Yesu alikuwa ameingia patakatifu pa patakatifu katika hekalu la mbinguni.  Zaidi ya hapo alidai kwamba miaka miwili baadaye, alipata maono mengine ambapo alidai kwamba alichukuliwa na kupelekwa katika hekalu la mbinguni.  Alisema kwisha kufikishwa mbinguni, kwanza kabisa aliingizwa patakatifu na baadaye patakatifu pa patakatifu ambapo aliona amri kumi zikiwa ndani ya sanduku la agano.

Tukiwa tayari kusonga mbele, tunaweza kujiuliza swali dogo la kuchangamsha bongo zetu. Hebu tujiulize, hivi, humo patakatifu pa patakatifu Bi Ellen White alikumta Yesu akifanya hukumu ya kipelelezi? Tukikijibu  wenyewe,  ndugu yangu, jibu ni kwamba suala hilo haligusiwi ilivyotarajiwa. Basi, acha tuzidi kumfuatilia katika madai ya maono yake. Bi Ellen White anasema alipong’aza macho yake kwenye sanduku la agano la humo hekaluni, aliona amri ya sabato ikiwa imezungukwa na utukufu na hapo eti akang’amua kwamba amri ya kushika Sabato ilikuwa kubwa zaidi.
Ndugu yangu, hadi hapo, tukimpima Bi Ellen White kibiblia, anaongeza uongo mwingine mbaya. Uongo wa kwanza ni ule wa kuliona hekalu mbinguni wakati mbinguni, Maandiko Matakatifu yanasema hakuna hekalu (rejea tena Ufu 21:22). Uongo wa pili ni huu wa kuhesabu amri ya kushika Sabato kama amri kuu kwani amri ya kwanza na kubwa kupita zote, kadiri ya Yesu Kristo mwenyewe, ni ile ya kumpenda Mungu huku ikifuatiwa na ya pili yake, yaani ile ya kumpenda jirani kama tunavyojipenda sisi wenyewe (rej. Mt 22:34-40).
Lakini basi, ndugu zanguni, maono aliyopata Bi Ellen White yakawa, kwake na hatimaye kwa Wasabato wote, kurunzi la kutafsiria  Maandiko Matakatifu yote.  Ndipo, kwa njia ya vitabu vingi alivyoandika, mafundisho ya Kiadventisti yakasambazwa. Hivyo, tangu wakati huo, Waadventisti Wasabato, huitafrisi Biblia kwa vipimo vya maono ya White, na siyo kuyatafsiri maono ya Bi White kwa vipimo vya Biblia.  Je, si ajabu ya mwaka hiyo? Basi, ndugu yangu, fumbuka macho ya roho yako, uyaone na kuyapima mambo haya sawa sawa pasipo kiwi cha macho! Usitoe hoja ya uongo!
Basi, kwa kukata maneno, Bi Ellen White ndiye aliyewapandikiza chuki Wasabato dhidi ya Kanisa Katoliki. Amelifanya hilo kwa kupitia vitabu vyake vingi vyenye chuki ambavyo vinasomwa na kutumiwa na Wasabato karibu kama misahafu.  Kwa taarifa yako, baadhi ya vitabu hivyo ni, kama vile, Vita Kuu, Afya na Raha na Siri ya Ushindaji. Ndani ya vitabu hivi Kanisa Katoliki linatukanwa na kushtakiwa kuhusika na maovu mengi. Kwa mfano, wanashtakiwa kuondoa amri ya kuabudu Sabato. Wanashtakiwa kuabudu sanamu. Wanashtakiwa kumwabudu Bikira Maria. Wanashtakiwa kumwabudu Baba Mtakatifu (Papa) ambaye eti ndiye mnyama anayetajwa katika kitabu cha Ufu 13:1-18. Wanashtakiwa kufundisha mambo ya kidunia badala ya ufalme wa Mungu. Wanashtakiwa kuongeza vitabu kwenye Biblia na mengine mengi ya namna hiyo yanayosikika mitaani na katika mahubiri yao. Mungu utuhurumie!
Ndugu zanguni, kwa ujumla, kanisa la Wasabato likawa muungano wa vikundi vitatu vya Waadventisti: mosi, kikundi cha Bw. Hiram Edson, kilichosisitiza zaidi mafundisho ya huduma ya Yesu patakatifu pa patakatifu mbinguni; pili, kikundi cha Bw. Joseph Bates, kilichosisitiza zaidi kufuata Sabato ya Agano la Kale; na tatu kikundi cha Bi Ellen G. White, kilichomwona Bi Ellen kama nabii ambaye unabii wake ni lazima ufuatwe na Waadventisti wote duniani.
Vikundi hivi vilipoungana Waadventisti Wasabato wakapata kujichipusha duniani. Mwaka 1860, jina la Seventh Day Adventist lilichaguliwa nalo likawa jina rasmi la Waadventisti hao.  Kishapo, mwezi Mei, 1863, katika mkutano mkuu wa kwanza, uliokuwa na wawakilishi kutoka majimbo yote Marekani, isipokuwa jimbo la Vermont, kanisa la Wasabato likazaliwa rasmi duniani.
Basi, tukipiga muhtasari wa historia ya Wasabato, tuseme tu kwamba mwasisi wa Waadventisti Bw. William Miller alikuwa ni Mbaptisti lakini mwanzilishi wa Wasabato yaani Bi Ellen G. White alikuwa ni Mmethodisti. Hata hivyo, kwa kuhitimisha sehemu hii, yafaa sote tukumbuke kwamba makanisa hayo mawili, yaani Wabaptisti na Wamethodisti si chochote isipokuwa matawi ya kanisa la Anglikana, kanisa lililoanzishwa na Mfalme Henry VIII wa Uingereza hapo mwaka 1534 baada ya kukasirika kukataliwa na Kanisa Katoliki kumwacha mkewe aliyeshindwa kumzalia  mtoto wa kiume.

WASABATO MITUME WA MATUSI DHIDI YA KANISA LA KWELI

Msomaji wangu bila shaka umeiona historia ya aibu na ya zigzaga ya Wasabato. Wasabato wenyewe huificha sana historia hiyo, hasa kwa wafuasi wao wanaoingia katika kanisa lao putaputa. Hufichwa ukweli kama paka wanaosafirishwa katika gunia. Kwa nini? Wanafichwa ili wasiujue ukweli walikotokea wasije wakajua kwamba wamekosea njia kiimani.
Kifupi, madai yao kwamba Baba Mtakatifu, Kanisa Katoliki au Mfalme Constantino ndio waliobadili Sabato kwenda Jumapili ni mojawapo ya matusi ya Wasabato. Wenyewe wanahubiri hayo kwa jasho jingi kabisa wakati ni kusepetuka kwa uelewa na fichio la aibu yao katika kushindwa kwao katika utabiri wa tarehe ya mwisho wa dunia, tarehe ambayo Yesu  Kristo, Bwana wetu na Maandiko yanatuambia kwamba haitabiri kabisa.  Kwa maneno mengine, ndiyo matawi ya chuki iliyokosewa mwelekeo na uongo wa binadamu dhidi ya wanadamu wenzake.
Tusisahau, kutokana kushindwa hoja na aibu kubwa waliyoipata mbele ya ukweli unaoshikiliwa na kufundishwa na Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki, Wasabato na makanisa mengine wameamua kutumia mbinu ya kujikosha kwa matusi makali.  Wameamua kujitwika utume wa matusi wakati mwingine hata matusi ya nguoni. Kwa vyovyote, Wakatoliki hawana namna rahisi ya kukabiliana na madai hayo ya kimatusi. Usistaajabu haya kufanyika hivi. Kwa mtindo wa vijijini, ukishindwa hoja kwa mtu fulani unaanza kumtukania wazazi wake, nyumba yao na kadhalika.

KUITUNZA SABATO NI KUSHEREKEA MKESHA WA SIKU YA UHURU
Kuitunza Sabato mbele ya Dominika ingelingana na kusherekea mkesha wa siku ya uhuru badala ya siku ya uhuru yenyewe. Taifa litakalofanya hivyo litachekesha na labda litakuwa la watu punguani. Aidha mtu kupita huko na huko kuwahimiza watu washerehekee mkesha wa uhuru badala ya siku ya uhuru wenyewe ingelikuwa sawa na kucheza Ze Comedy.
Nani amegeuka mkondo wa mambo hata kugeukia tena Sabato wakati Wakristo wa kwanza kwa kumwelewa vyema Yesu Kristo walishaitupilia mbali?  Jibu ni wazi. Ni mmoja wa waanzilishi wa dhehebu la Wasabato, yule mama anayejulikana kama nabii. Kwa taarifa yako waanzilishi wa dhehebu la Wasabato ni akina Hiram Edson, Joseph Bates, E.G. Harmon na Hellen White. Katika hawa aliyekuja na moto wa kurudisha Sabato ni huyo mama ambaye alikuwa mke wa E.G. Harmon. Mwanamke huyo anaheshimiwa na Wasabato kama nabii na vitabu vyake , kama vile Vita Kuu, Afya na Raha na Ushindaji, vinasomwa na Wasabato karibu kama misahafu.

WASABATO WASIMNYANYASE YEYOTE

Maono ya uwongo ya Bi Hellen yasiwe sababu ya kuwanyanyasia Wakristo wasio Wasabato. Wala si siri, makanisa yanayofuata mabadiliko yaliyoletwa na Mungu mwenyewe kutoka Sabato kwenda Dominika yananyanyaswa kweli kweli na kauli za Wasabato wanaomfuasa Bi Hellen White. Lakini, hivi unabii wa mama huyo ni wa kweli hata tutishik
e nao? Hapana, wala si wa kweli. Unabii wa mama huyu lazima tuukatae. Kwa nini tuukatae?

TUHIMIZANE TUMKATAE BI HELLEN NA MAONO YAKE

Ni kwa sababu kuna sababu tatu zinazotuhalalisha tumkatae Bi Hellen White kama nabii. Mosi, kitabu cha Ufunuo kinaonesha kufungwa kwa unabii, yaani kwamba baada ya mambo yaliyoandikwa humo kusingekuwa na ufunuo wowote wa pekee. Ukamilifu wa ufunuo ulitokea katika ujio wa Yesu Kristo. Alichosema yeye ndicho kitu cha kilele. Sasa Bi Hellen anakujaje na mapya kumpikua Yesu Kristo? Tunasoma, “Mungu ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi, amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akavichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu, amefanyika bora kupita malaika kwa kadiri jina alilorithi liliyo tukufu kuliko lao” (Ebr 4:1-4).

Si hivyo tu hata mintarafu ufunuo wa zamani mihuri yake imevunjwa na Yesu Kristo mwenyewe, sasa unabii wa Hellen White unaanzia wapi? Tunasoma, “Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba. Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, Ni nani astahiliye kukifungua kitabu na kuzivunja muhuri zake. Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kikifungua hicho kitabu, wala kukitazama. Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba.

Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwanakondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote. Akaja , akakitwaa kile kitabu katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi. Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya Mwanakondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya wakatakatifu, nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaaa hicho kitabu na kizifungua muhuri zake, kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme wa makuhani, kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi” (Ufu 5:1-10).

Mintarafu kusasambua ovyo ufunuo wa Mungu, mwandishi wa kitabu cha Ufunuo alishakatazwa, sasa Bi Hellen White anapata wapi nguvu ya kuja na ufunuo mpya? Kuhusu marufuku hiyo tunasoma, “Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike” (Ufu 10:4). Hatimaye, maneno ya ufunuo yaliachwa wazi bila muhuri kwa vile yalivyokuwa njiani kutimia. Juu ya jambo hili, tunasoma hivi: “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki kwa maana wakati huo umekaribia” (Ufu 22:10). Sasa Bi Hellen White anaongezaje maneno ya ufunuo mpya?

Pili, tuukatae unabii wake kwa vile zile anazoziita njozi, kama elfu mbili hivi, ni batili kwani zinaonesha jinsi alivyojaa chuki kwa Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki nasi tunajua kwamba si kazi ya Mungu Roho Mtakatifu kumjaza mtu chuki kali hivyo dhidi ya mwanadamu mwingine. Kazi hiyo hufanywa na Shetani nayo huonesha kwamba moyo wa mtu umejaa uovu kwani kilichomjaa mtu moyoni ndicho kimtokacho. Tunasoma, “Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. Mtu mwema  katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake”  (rej. Lk 6:43-45). Hakika chuki dhidi ya Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki inatoka katika moyo uliofurika uovu. Na kwa jinsi hii maono yake hayawezi kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Tatu, tuukatae unabii wake kwa sababu mafundisho yake yanaonesha kwamba haijui Biblia. Hoja hii ya tatu nimeshaishuhudia tayari. Nimesema ameota ndoto akaona huko mbinguni kuna hekalu wakati Maandiko yanatakaa jambo kama hilo (rej. tena Ufu 22:22-24). Kisha nimeshashuhudia kwamba kule kusisitiza kwamba Sabato ndiyo amri kuu kunapingana na kile alichotuambia Bwana wetu Yesu Kristo aliyesisitiza kwamba amri kuu ni upendo (rej. tena Mt 22: 34-40).  Naomba itoshe nilivyokuambia nawe uyapuuze maono ya Mrs. Harmon tunayemchambua hapa.

MAJIBU KWA MASHTAKA YA ZIADA

Nikiendelea kidogo, naomba ruksa nijibu mashtaka mawili sambamba wanayotoa Wasabato dhidi ya Wakatoliki: mosi kwamba ndio mnyama yule Shetani aliyejipa jukumu la kubadili majira na pili kwamba Kanisa lenyewe linakiri kufanya hivyo katika Katekisimu zake na katika vitabu vya waandishi fulani fulani wa Kanisa Katoliki.
Mintarafu hoja ya kwanza ni hivi mnyama ni Bi Hellen White aliyethubutu kumpinga Mungu. Mungu aliibadili siku ya Sabato yeye akijipa jukumu la kuirudisha kwa maelezo ya maono yake batili kabisa. Tumeshaonesha jinsi yalivyo batili kwa kadiri ya mizani na darubini ya Maandiko Matakatifu.

Halafu mintarafu hoja ya pili ni hivi Kanisa linajihusisha na mabadiliko hayo si kama ‘mtendaji’ kwani hakuna mkutano mkuu (mtaguso) wowote wa Kanisa Katoliki uliojadili hoja ya Sabato na kuamua kuibadili kwenda Dominika ila kwamba Mungu aliibadilisha Sabato pale alipoanzisha enzi ya Israeli mpya yaani Kanisa.  Natumaini wasomaji wangu hoja hii si ya kitaalamu mno kiasi cha kutonielewa ninachosema. Ninasema hivi Kanisa linajisikia kuhusika na ubadilishaji wa Sabato kwenda Dominika kwa vile Mungu aliufanya kuanzia pale lilipoanza kuwako nalo kwa mamlaka uliyopata kutoka kwa Mungu ikayasimamia na kuyaendeleza mabadiliko hayo.

MALUMBANO SASA YAKOME

Naomba hadi hapa shtaka la kwamba Kanisa Katoliki limebadili majira, yaani kutoka Sabato kwenda Dominika (Jumapili), lififie kabisa. Si unajua kwamba hoja yenyewe hukokotolewa kutoka Dan 7:25 mahali palipoandikwa, “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye Juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye Juu, naye ataazimu kubadili majira na sheria”. 
Kama unavyoisoma sasa, hoja hii haitaji Kanisa Katoliki bali kwa kinyume chake inawataja Wasabato wenyewe. Ndugu zangu Wasabato haliwafahamu jambo hili kwa sababu ndivyo ilivyo, “Jambo usilolifahamu ni sawa na usiku wa giza.” Kwa vipi? Ni hivi, kama Yesu kwa maneno na matendo yake alisema Sabato si lolote na wala si chochote “maana mtu hakuuumbwa kwa ajili ya Sabato”, mtu anayesema Sabato ndiyo yote katika yote ndiye anayeazimu kubadili majira na sheria. Na moja kwa moja mtu huyo anakuwa ndiye mpinga Kristo kwa sababu anapingana na kauli ya Kristo mwenyewe. Hilo ndilo alilofanya nabii Hellen na kuwasadikisha maelfu ya watu kauli yake kengeufu.

Aidha, kama Yesu alisema kwamba amri kuu ni upendo (rej. Mt 22:37) na akataka iwatambulishe wafuasi wake popote watakapokuwa (rej. Yn 13:35), anapokuja nabii Hellen na kusema eti amri kuu ni Sabato ni upinga Kristo wa wazi wazi na kumfuasa mpinga Kristo kama huyo ni kuwa wapinga Kristo wadogo wadogo nyuma ya huyo mkubwa. Ona ushuhuda wa Maandiko Matakatifu. Bila shaka, hata wewe unakumbuka Yesu aliulizwa swali juu ya amri ya kwanza na kuu naye akatoa jibu mwafaka hata wasomi na walimu wa enzi zake wakamvulia kofia.

Tunasoma, “Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. Mmoja wao, mwanasheria, akamwuliza, akimjaribu: Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” na wakati akiwaaga wanafunzi wake jioni iliyotangulia kifo chake alisema na kuagiza, “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi” (Yn 13:35). Sasa Nabii Hellen anathubutuje kusema kinyume cha maneno hayo ya Kristo ambaye tumepewa tumsikilize? Kama huo si upinga Kristo wenyewe ni nini tena? Hukumu mwenyewe; wewe ni mtu mzima. Hivi wewe na mimi na sisi sote hatukumbuki maneno ya Maandiko Matakatifu, “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye” (Mk 9:7)? Na kwa upande wetu, kwa nini, tunamsikiliza binadamu tena? “Tumechanganyikiwa” au “tumerogwa”?

UCHAMBUZI WA KISAIKOLOJIA WA WALIOHUSIKA NA HISTORIA HII YA AIBU

Jina Ugonjwa Tunaoweza Kumtuhumu Upinga Kristo Wake Ulipo
William Miller Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kujaribu kuitaja tarehe ya mwisho wa dunia Kukokotoa tarehe ya mwisho wa dunia kinyume na Mk 13:32.
Samwel Snow Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kujaribu kuitaja tarehe ya mwisho wa dunia Kukokotoa tarehe ya mwisho wa dunia kinyume na Mk 13:32.
Hiram Edson Schizophrenia – kuona hekalu ambalo halipo mbinguni na kudai mwisho wa ulimwengu umeshatokea.  Kuota ndoto ya kuliona hekalu mbinguni ni kinyume cha Ufu 21:22-23.
Joseph Bates Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kuunga mkono uongo kwamba mwisho wa ulimwengu umeshatokea. Kuidharau Jumapili, siku aliyoitumia Bwana kufanya mambo yote makubwa.
Hellen White Schizophrenia – kuona hekalu ambalo halipo  Kuota ndoto ya kuliona hekalu mbinguni ni kinyume cha Ufu 21:22-23 na kudai Sabato ndiyo amri kuu kinyume na Mt 22:34-40.

MASWALI NA MASHTAKA 12 MAARUFU YA WASABATO KWA WAKATOLIKI

i. Sabato ndiyo siku ya kuabudu iliyoamriwa. Wakatoliki ndio walioifuta Sabato na kuweka Jumapili.
ii. Wakatoliki wanafuata mapokeo ya binadamu, hawajui na wala hawafuati Maandiko Matakatifu.
iii. Baba Mtakatifu ndiye mnyama yule anayewakilishwa na namba 666. Namba hiyo imeandikwa kwenye kofia na mavazi yake.
iv. Wakatoliki wameifuta amri ya pili ya Mungu. Wamefanya hivyo ili waabudu sanamu.
v. Wakatoliki wanaabudu sanamu. Tazama sanamu makanisani mwao!
vi. Kwa nini Wakatoliki wanakunywa pombe wakati imekatazwa kwenye Biblia?
vii. Wakatoliki wanamwabudu Bikira Maria. Kwa nini wanamfanyia heshima kubwa isivyostahili?
viii. Je, Bikira Maria alikuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu Kristo?
ix. Kanisa Katoliki linafanya makosa kuwatangaza wanadamu kuwa watakatifu. Mwanadamu ana uwezo gani wa kumtangaza mtu mwingine kuwa mtakatifu?
x. Wakatoliki wana sakramenti saba. Wana makosa kwa sababu hazijaandikwa kwenye Biblia.
xi. Kuungama ni kwa Mungu moja kwa moja. Kuna uhalali gani kwenda kuungama kwa mapadri wakati wenyewe wana dhambi?
xii. Wakatoliki wana hatia kubwa kwa sababu hawataki kuokoka. Kwa nini Wakatoliki ni wabishi hivyo?
Ndugu yangu Mkatoliki jaribu kuwa na majibu ya maswali haya, hutahangaishwa na Wasabato wowote katika imani yako na maisha yako yote. Kumbe, usipokuwa nayo siku zote utayumbishwa kama wimbi la baharini wakati ulipaswa kutulia tuli kama maji kwenye mtungi.

HATIMA: TUSIHANGAISHANE TENA JUU YA SABATO KWANI  ILIKUWA KIVULI TU

Kwa sasa Wakatoliki wote tuhitimisha fikra zetu kwa nukuu hii: “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni KIVULI cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo” (Kol 2:16-17).
Ndugu zanguni, kama inavyosomeka katika aya hizi, Sabato ilikuwa kivuli na kivuli hakishonewi suti. Sisi ni watu wazima tuachane na Sabato. Nina hakika tutaadhibiwa na Mungu kwa hatia ya kukipa hadhi kitu kisicho na uzito wa kimani.

Imeandikwa na
Pd. Titus Amigu (2016)

Saturday, August 27, 2016

Kanisa la EAGT Lumala Mpya jijini Mwanza Kufanya Harambee ya Kanisa Jipya la Kisasa

Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji kiongozi, Dkt.Daniel Moses Kulola, linapenda kuwakaribisha watu wote kwenye Harambee ya Ujenzi wa Kanisa jipya na la kisasa linalotarajiwa kujengwa katika viwanja vya kanisa hilo.

Harambee hiyo inatarajiwa kufanyika kesho jumapili Agosti 28,2016 kanisani hapo ambapo watu wote wakiwemo waumini na viongozi wa Madhehebu mbalimbali, Viongozi wa Serikali na Taasisi binafsi, wanakaribishwa ili kuungana na viongozi na waumini wa Kanisa hilo katika kushiriki kwenye harambee hiyo.

Kumbuka "Bwana Hufurahi  Anapojengewa Hekalu Lenye Kufana" hivyo utabarikiwa ikiwa utashiriki katika harambee hiyo. Kwa mawasiliano zaidi, tumia nambari za simu; 076774 90 40 AU 0787 74 90 40.

Saturday, November 21, 2015

Kanisa za WaKenya Boston Zimeguezwa Miradi ya Kutafuta Pesa

 
Pastor Elizabeth Wanyoike of the newly launched International Restoration Reformed Church (IRRC) in Tewksbury, near Lowell during dedication ceremoney on Sunday November 15, 2015. AJABU MEDIA PIC/H.MAINA
 
Kenyan Churches in Boston turned into financially motivated Social Clubs, says new Pastor
 
LOWELL, Mass.,( Ajabu African News) Nov 19__Most Kenyan community churches in Boston have abdicated their primary role of spreading the true gospel of Jesus Christ and instead have been turned around into "help those who help you" social clubs emphasizing too much on financially motivated manipulations. 
The charge was made by pastor Elizabeth Wanyoike last Sunday during the dedication ceremony of the newly launched International Restoration Reformed Church (IRRC) in Tewksbury, near Lowell.

She said that many Kenyans attending Kenyan community churches today have no clue of where they are headed yet they are being lead down the drain by church leaders many of whom are only concerned with parishioner contributions to cater for their weekly paychecks and social problems among members. 

"There is a lot of ungodliness in the church today.The church has been turned around to help those who help you. It is the spirit of Jezebel and somebody must wake up to breaks the yokes of this spirit," she said during the sermon top about a dozen Kenyans present"

It is time to destroy the ungodliness in our church just like Elijah destroyed the idols that citizens were worshipping during King Ahab's rule," she added while quoting from the book of1st Kings Chapter 16 &17.

.Wanyoike said that there is a spirit of fear, oppression and intimidation going around the body of Christ today in the Kenyan community similar to what took place during King Ahab's reign.

"You can be in the church but the people in authority are taking you nowhere. People are covered in the spirit of oppression and intimidation."
She called on Kenyans of faith to take a proactive effort to change things so that the church "can operate on what God wants us to do."

"Things have to change and the church return to order. We don't have to gather for the sake of gathering. Even Obadiah was so afraid to tell the King that Prophet Elijah had arrived with a message to the people but Elijah forced him to bring up King Ahab to listen to the message and destroy the alters of worshiping idols instead of the read God," she added.

Thursday, September 24, 2015

Ibada ya Kiswahili Katoliki - Dayosisi ya Cleveland East

IBADA YA KISWAHILI KANISA KATOLIKI DAYOSIS YA CLEVELAND EAST
 
KARIBUNI
 
Wapendwa wakristo mnkaribishwa kushiriki sherehe ya kutimiza mwaka
mmoja wa ibada ya Kiswahili kanisa letu Katoliki Dayosis ya Cleveland.
Ibada itaanza saa kumi jioni, na baada ya ibada kutakuwa na chakula na
vinywaji, pia kubadilishana mawazo.
Ibada hii itafanyika;
 
St Adelbert Church
East 83 Street,
Cleveland Ohio 44103
 
Kwa taarifa zaidi wasiliana kwa simu zifuatazo;
Father. F. January 216 650 2734
Father Rogerio. 267 206 2613
Tumaini. 216 645 5171

Sunday, May 05, 2013

Mlipuko wa Bomu Katika Kanisa Katoliki Arusha


 HABARI KWA KIFUPI:Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.
Anasema ni tukio la kighaidi.

Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu.

Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi.

Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana.

Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano



Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi.
Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.
Tanzania Field Force Unit (FFU) on site of Catholic church bombing
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ibrahim Kilongo.


JESHI la Polisi Mkoani Arusha linamshikilia mtu mmoja ambaye anahusishwa na kutokea kwa mlipuko uliotokea katika kanisa la Katoliki la St Joseph Olasiti Arusha leo asubuhi.

Tukio hilo lilitokea wakati Balozi wa Papa kutoka Vatican akizindua Parokia hiyo mpya ya St Joseph Olasiti ya Jijini Arusha.
Kanisa lililolipuliwa likiwa linaonekana kwa mbali huku wananch wakilitazama kwa mbali kutokana na tishio la kutokea kwa milipuko mingine ...Mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na tukio hilio wakati wengine wanasadikika kukimbia.
Majeruhi wa tukio hilo wakiwa katika hali mbaya..
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMRQWe-3DwwaUndhYh1ip8NOsy0SUDnS9ZaDT4mkleioWUxd9pwcn58XwJEoIty_6JpgECCFiBJrCcsQ3dQoNHKMVOYKG_Ov_IeEUNXNFszp3wwIvmBnDmaMwcziTz4a6MJJKIWA/s1600/IMG_20130505_130432_0.jpg
Waumini pamoja na baadhi ya wanacchi wakiwa katika hali ya taharuki wasiamini nini kilichotokea kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea asubuhi ya leo.






Kanisa Katoliki Lalipuliwa na Bomu Arusha Wakati wa Ibada!

 Hivi Tanzania kuna nini siku hizi? Mapadri wanauawa, kanisa zinachomwa moto na sasa kulipuliwa na mabomu!  Tunalilia nchi yetu!  Shaidi anasema kuwa wakati wa Misa maalum ya kubariki kanisa jipya mwanaume fulani alitokea na kurusha bomu ya petroli.  Baada ya kuirusha alikimbia nje ya kanisa na kuingia ndani ya gari na kuondoka. Misa ilikuwa inafanyika mbele ya kanisa.

KWA KIFUPI:

Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.

Anasema ni tukio la kighaidi.

Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu.

Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi.

Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana.

Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano

Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DAR ES SALAAM (Reuters) - A suspected bomb blast struck a Catholic church in the northern Tanzanian town of Arusha on Sunday, police said, wounding a number of people.
Sectarian tensions have been simmering in east Africa's second biggest economy after two Christian leaders were killed in the predominantly Muslim islands of Zanzibar earlier this year and there have been attacks on Muslim leaders and mosques.
"Some kind of explosion went off at the church. It is believed to have been a bomb but we don't know what type of bomb it was," Tanzania police spokesperson Advera Senso said.
Senso could not confirm if anyone had been killed in the attack or how many had been wounded.
Tanzania's foreign affairs minister Bernard Membe said in a message on Twitter he was "deeply shocked" by the explosion.
President Jakaya Kikwete has warned about rising religious tensions in several televised addresses.
(Reporting by Fumbuka Ng'wanakilala; Editing by Richard Lough and Mike Collett-White)

********************************************

ARUSHA, Tanzania, May 5 (Xinhua) -- A bomb blast hit a Catholic church on Sunday in Arusha in northern Tanzania, killing one child and injuring more than 30 people, witnesses reported.
The dead was among the church followers who were gathering for Sunday prayers.
The church located in Arusha's Olasiti suburb was bombed just before a mass in the presence of Bishop Josaphat Louis Lebulu of Arusha Diocese, who was accompanied by a representative of Pope of Vatican.
Police in Arusha said one man was arrested in connection with the incident, which caused a lot of panic in the tourist capital of the East African country.
Casualties are yet to be updated. "We are still working on the matter. We'll give more detail after investigating the matter," said Arusha Regional Police Commander Liberatus Sabas.
He said the man was arrested following a tip-off from people at the scene when the explosion occurred.
"We are still interrogating the suspect," he said.
Regional Commissioner Magesa Mulongo described the blast as horrific and unique in Tanzanian history, calling on the public to remain calm.
"So, people should continue with their daily activities, as police and other security organs have normalized the situation," Mulongo said.
A witness said, "I saw more than 30 people, taken by a police vehicle, which took them to the Mount Meru Regional Hospital."
Another witness said the bomb hit the church at around 10:00 a. m. local time when church followers were gathering for the historic Sunday prayer at the new church.
"We were trying to organize ourselves for the mass, when we heard loud sound, the situation that made more people to start rushing out of the church," a witness told Xinhua.
This is the first bomb explosion at the church in the northern safari capital of Arusha. 



One of those injured in Bombing receiving First Aid

Sunday, February 17, 2013

Priest Shot Dead in Zanzibar Another Beheaded on Mainland

 Kutoka : http://atlasshrugs2000.typepad.com/atlas_shrugs/2013/02/priest-shot-dead-in-zanzibar-pastor-beheaded-on-mainland.html

 Sunday, February 17, 2013