Showing posts with label Kupigwa Risasi. Show all posts
Showing posts with label Kupigwa Risasi. Show all posts

Sunday, August 11, 2013

Sheikh Ponda Yuko Muhimbili Kwa Matibabu

Video Kwa Hisani ya Imma Mbuguni




Sheikh Ponda Akitibwa Jereha la Kupigwa Risasi Begani Muhimbili



Kutoka: MICHARAZO MITUPU BLOG

Sheikh Ponda Issa Ponda ameletwa Dar na kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu na tayari kuna habari kwamba Polisi wakiwa kwenye madifenda yao wameshatimba hospitalini hapo.

MICHARAZO inafuatilia taarifa hizo zilizopenyezwa hivi punde kujua ukweli na ikiwezekana kuwatupia na picha kama ni kweli Sheikh huyo machachari na kiongozi wa umma wa waislam walio wengi amepelekwa hospitalini hapo.
Pia taarifa rasmi kuhusu hali ya Sheikh Ponda inatarajiwa kutolewa Alasiri hii katika Msikiti wa Mtambani na Amir wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha baada ya kuwepo kwa mkanganyiko juu ya hali ya kiongozi huyo wa umma wa waislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda juu ya tukio la kujeruhiwa kwa risasi begani na Polisi wakati alipotaka kukamatwa, japo Polisi wanaendelea kukomaa kwamba hawajui lolote.

Picha Kutoka Daily Mirror

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Tamko la Jeshi la Polisi Kuhusu Sakata la Sheikh Ponda

TAMKO LA JESHI LA POLISI TANZANIA KUHUSU 
SAKATA LA SHEKHE PONDA
1. MNAMO TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO. DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA ALIFIKA SHEKHE PONDA ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.

2. KONGAMANO HILO LILIFUNGWA MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA ENEO HILO, ASKARI WA JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA UVUNJIVU WA AMANI.

3. BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO KWA KUWARUSHIA MAWE ASKARI. KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.

4. KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA. HIVI SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.

5. KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI CP ISSAYA MNGULU IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.

6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA WITO KWA WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHE
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Saturday, August 10, 2013

Muda Mfupi Kabla ya Sheikh Ponda Kupigwa Risasi


 Kutoka Jukwaa Huru.com

Huku taarifa ambazo zinaendelea kusambaa zikiwa zinadai kuwa Sheikh Ponda amepigwa risasi na Polisi, na huku Jeshi la Polisi likikanusha kuhusika na tukio hili, likieleza kuwa halikuhusika na wala halijui aliko mwanaharakati huyo wa Uislamu, hapa ni picha za kinachoelezwa kuwa kilitokea kabla ya tukio la Ponda kupigwa risasi (kama ni kweli amepigwa risasi) 

Picha hizi ni kutoka blog ya Google Habari, na zimeambatana na maelezo yaliyo chini yake: 




Leo kwenye kongamano la kuita umoja wa waislam katika yanayo wakabili waislam mkoani Morogoro.
Kongamano lillienda vizuri likiwa limepambwa na mashekh wakubwa wakubwa kama vile Riko, Mwaipopo, Kondo pamoja na shekh Ponda.
Shekh ponda alikuwa wa mwisho kutoa mawaidha na aliaga waislam ili aweze kuelekea Msikiti wa Mungu mmoja hivyo waislam walitaka kumsindikiza Shekh Ponda mpaka Mskiti wa mungu mmoja.
Maaskari waliovalia nguo za Field Force wakiwa kwenye defender waliingia na kuanza kuifuata gari kwa nyuma. 
Waislam waliendelea kuizunguka gari ya Shekh Ponda ila maaskari walianza kupiga mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi kisha kuifukuza gari ya sheikh Ponda.
Sikubahatika kushuhudia nini kiliendelea kutokana na mabomu ya machozi yaliyopigwa na maaskari hao lakini dakika chache baadae nilipata taarifa ya kwamba amepigwa risasi ya bega na amepelekwa hospitalini…..endelea kutembelea blog ili ujue nini kinaendelea kwa Shekh Issa Ponda amabae inasemekana yupo Hospitali tayari kupata tiba.

Sheikh Ponda ApIgwa Risasi Na Polisi Morogoro!

Sheikh Ponda Issa Ponda


Mda kama dakika 20 zilizopita  mjini Morogoro shehe Ponda amepigwa risasi na polisi .
Inasemekana pengine umauti umemkuta .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo
akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano
kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye
alikuwa hayupo .

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi za kutosha.

 UPDATE:

Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.


Chanzo: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/502527-sheikh-ponda-ajeruhiwa-vibaya-baada-ya-kupigwa-risasi-kwenye-mhadhara.html#post7045479

*************************************************

 From All Africa.Com

Tanzania: DPP Directs Arrest of Sheikh Ponda for Disobeying Order


Sheikh Ponda was in May, convicted of forcible entry into a plot by the Kisutu Resident Magistrate's Court in Dar es Salaam. He was given a oneyear suspended jail term and directed to refrain from taking part in incitement activities likely to lead to breach of the peace in the country.
Dr Feleshi noted that recent reports have it that the cleric is engaged in organising religious gatherings in Zanzibar, which threatened peace in the Isles. "Such a behaviour is intolerable," the DPP said in an interview with the 'Daily News' on Wednesday.
He added: "We hope the police will exercise their powers wisely to arrest Sheikh Ponda and take him to court for penal actions." Dr Feleshi said what Sheikh Ponda was currently doing was contrary to his sentence. "He was convicted of a similar offence, but was still conducting acts that threaten the public order and concord.
This is not acceptable. We cannot let one disobey court orders and go on unpunished," he said. Counsel for Sheikh Ponda Juma Nassoro was not reached for comment on the matter.
Reports from Zanzibar have it that police are tracing Sheikh Ponda's whereabouts. He is alleged to have called on the citizens to initiate strikes against the government. Zanzibar Commissioner of Police, Mussa Ali Mussa was reported to have said that Ponda's statements breached police directives to religious leaders to avoid giving messages which threaten the country's peace.
The police in the Isles arrested five persons who reportedly gave shelter to the controversial Muslim Sheikh. They were interrogated for hosting Ponda.
Sheikh Ponda, according to the police, had requested the believers to be ready to fight for their rights and stressed that they should soldier on.
Adjourning the Zanzibar House of Reps budget session for 2013/2014, the Second Vice-President, Amb. Seif Ali Iddi announced a ban for Sheikh Ponda to set his foot in the Isles for the purpose of inciting the people. Amb. Iddi warned that the government should not be blamed for serious measures that would take against leaders of such calibre