Showing posts with label Lucas Lukumbo. Show all posts
Showing posts with label Lucas Lukumbo. Show all posts

Thursday, August 09, 2007

Viongozi wa TAMWA

Hapa niko na Dada yangu mpendwa, Bi Evodia Ndonde, ambaye aliwahi kufanya kazi Tanzania Film Company. Sasa ana kampuni yake ya video production. Naye ni mwanachama wa TAMWA miaka mingi.
Mwandishi wa Habari wa The Guardian, Lucas Lukumbo alipita kusalimia wana TAMWA. Kulia ni mwenyekiti wa TAMWA, Bi Ananilea Nkya.

Hapa niko na Dada Edda Sanga ambaye amestaafu kutoka Radio Tanzania hivi karibuni. Dada Edda aliwahi kuwa Mwenyekiti wa TAMWA.

TAMWA wanapokea interna kutoka nchi mbalimbali kila mwaka. Huyo dada yuko TAMWA kwa kipindi cha mwaka moja, anatoka Norway. Pia kulikuwa na akina dada kutoka Zambia, Ethiopia na Canada.
Hapa nipo na Dada Fatma Alloo, aliyekuwa Mwenyekiti wa TAMWA miaka mingi. Alitufundisha mengi kuhusu uongozi katika zile siku za mwanzo wa TAMWA.
Mwenyekiti wa TAMWA kwa sasa, Bi Ananilea Nkya, Mimi, Dada Evodia Ndonde na Edda Sanga. Dada Ndonde ana kampuni ya video production, na mimi niliwahi kuwa Publicity Secratary wa TAMWA na kwenye Executive Board.

Tuesday, April 03, 2007

TAMWA

Bila shaka mmesikia majina kama Fatma Alloo, Leila Sheikh, Edda Sanga, Maria Shaba, Pili Mtambalike, Wema Kalokola (marehemu), na Ananilea Nkya. Hao ni kati ya waanzalishi wa chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Tanzania, TAMWA. Na mimi ni mmoja wa waanzalishi wa TAMWA (Tanzania Media Women's Association).

Tulitoka mbali maana mwanzoni tulipata pingamizi nyingi kutoka kwa wanawake na wanaume. Tulitukanwa na kuitwa majina ya ajabu kama, 'frustrated women, na malesbo'. Hivi sasa wanaume wakisikia jina la TAMWA wanatetemeka. TAMWA imefanya mengi kutetea haki za akina mama nchini Tanzania na inaendelea kwa nguvu! Tulianzisha kwa ajili ya kusaidia akina mama waliokuwa waandishi wa habari lakini ilikuwa mpaka kutetetea haki za akina mama Tanzania.

TAMWA Oyee!

Hii picha ilipigwa mwaka 1992. Tulikuwa kwenye safari Zanzibar na wageni wetu kutoka vyama vya akina mama mbalimbali barani Afrika. Mimi niko kushoto kabisa na miwani! Pia wamo Edda Sanga (3rd from left, Maria Shaba 5th from left, Halima Shariff 2nd from right). Wengine ni wageni kutoka nje.
Ndo baada ya hii safari iliyofana ilitokea kasheshe kubwa kutokana na picha fulani aliyopiga Muhidini Michuzi, na kuwekwa kwenye front page ya gazeti ya Daily News mpaka ilibidi viongozi wa TAMWA warudi Zanzibar kuomba radhi. Picha eneyewe ilipigwa kwenye shughuli ya mpendwa somo na kungwi mkuu wa Tanzania, Bi Kidude.
Kwa habari zaidi kuhusu TAMWA someni: