Showing posts with label TAMWA. Show all posts
Showing posts with label TAMWA. Show all posts

Saturday, October 14, 2017

Support the new TAMWA History Book


I am a Founding Member of  the Tanzania Media Women's Association (TAMWA). TAMWA is celebrating 30 years and a friend has set up this self explanatory link. Wd like your support.

Saturday, June 20, 2015

Tanzia - Florence Dyauli, Mtangazaji wa TBC

 Nimesikitika sana kusika habari ya kifo cha Dada Florence Dyauli.  Nilifanya kazi naye nilipokuwa Practical Training RTD nikiwa mwanafunzi Tanzania School of Journalism. Pia tulikuwa pamoja kwenye shughuli za TAMWA.  Rest in peace Dada Florence.

*************************************************

KUTOKA LUKWANGULE BLOG:


The Late Florence Dyauli (1961-2015)

MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa upande wa Televisheni Florence Dyauli amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Rabininsia memorial iliyopo jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa kutokana kusumbuliwa na maradhi ya Nimonia

Taarifa iliyotolewa jana na ofisi za TBC ilisema kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Nimonia na alilazwa kwa ajili ya matibabu hadi jana usiku mauti ilipomfika.

Taratibu za mazishi zilikuwa bado hazijafanyika na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo ya Rabininsia ukisubiria taratibu za mazishi kutoka kwa ndugu wa familia.

Florence alizaliwa Julai 27, 1961 ambapo alipata elimu yake ya msingi kuanzia 1968 hadi mwaka 1975 katika shule ya Msingi Chang’ombe iliyopo jijini Dar es salaam.

Alifanikiwa kujiunga na elimu ya Sekondari katika shule ya Kisutu girls kati ya mwaka 1976 hadi 1979. Baadae alijiunga na chuo cha Tabora secretarial College kuanzia mwaka 1980 hadi 1981 na kujipatia mafunzo ya cheti cha ukarani.

Mnamo mwaka 1986 hadi 1988 alijiunga na chuo cha uandishi wa habari kwa ngazi ya stashahada ya uandishi wa habari.

Aliniajiriwa kama mwandishi wa habari msaidizi katika kituo cha Radio Tanzania Dar es salaam kuanzia 1982 hadi Novemba 1999.

Kisha mwaka 1994 hadi Novemba 1999 alikuwa Shift Editor .

Hadi mauti inamkuta, marehemu alikuwa mwandishi wa habari daraja la kwanza kwa upande wa Televisheni ya Taifa TBC.

Thursday, January 01, 2015

Kwa Nini Levina Alijiua ? The Case of Levina Mukasa - UDSM

Wadau niliandika habari hii nikiwa mwandishi wa habari Daily News mwaka 1991.  Kesi hii ilikuwa chanzo cha ile Movement ya Kumpambana na Unyanyasaji wa Kijinsia wa Akina Mama Tanzania (Sexual Harassment).  TAMWA iliongoza movement hiyo. Nasikia mmoja waliyomnyanyasa Levina, Omari Saloti ni marehemu. Sijui huyo Mark Victgor yuko wapi, lakini ana damu mikononi mwake.

******************************************************************************
The Late Levina Mukasa
Na Chemi Che-Mponda

 Tarehe kama ya leo mwaka 1990 wakati mwanafunzi wa kike wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alipojiua, watu wengi walifikiri kuwa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa na matatizo kwao na kuwa masomo yalikuwa yanamshinda. Hata hivyo, waliposikia kwamba alifanya hivyo kutokana na unyanyawaji wa kijinsia uliofanywa na wanafunzi wawili wa Kitivo cha Uhandisi pamoja na kikundi kilichojukana kama “Punch”, baadhi walikasirika wakati wengine walicheka tu.

Marehemu Levina Mukasa, alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliyekuwa akisomea shahada ya ualimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kulingana na maelezo ya waliokuwa wakimfahamu wanasema alikuwa mkimya mwenye msaada na ambaye wakati wote alikuwa tayari kutumia vitu vyake na wenzake. Kila aliposoma wakati wote alishika nafasi ya juu darasani.

Mnamo tarehe 7 Februari 1990, Levina alikatisha maisha yake kwa kumeza vidonge vingi vya klorokwini (vinavyotumika kutibu Malaria). Swali linabaki, “kwa nini alifanya hivyo?” Karibu kila mwanafunzi wa kike aliyesoma katika kampasi kuu ya Chuo Kikuu (inayojulikana sana kama Mlimani) atakuwa amenyanyaswa kijinsia katika kipindi cha Miongo miwili iliyopita. Wamekuwa wakidhihakiwa, kutishiwa kijinsia au kuvamiwa papo kwa hapo na kubakwa.

PUNCH

Pamoja na hayo lipo kundi la kisirisiri hapo mlimani linajukana sana kama PUNCH, linafikia hata kiwango cha kuchapisha maandishi na michoro michafu kuhusu habari za kimapenzi za sasa au za zamani za Mhasirika wao. Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwaweka wanawake chini ya wanaume, kuwafanya wanafunzi bora wa kike washindwe masomo yao na hata kulazimika kukatisha masomo. Inatumiwa pia kuwatishia wasichana wakubali kufanya mapenzi na watu wanaowataka ambao wako katika kundi la PUNCH. Kumkataa mtu aliyeko kwenye kundi la PUNCH kunamfanya mhusika“apanchiwe”.

Bahati mbaya, wanawake walio katika kampasi wanaiogopa PUNCH. Wanafungwa na sheria zake kama vile kutokunywa chai ya saa 10.00 katika mgahawa, kutokukaa kwenye high table, kutokuvaa khanga Mgahawani n.k. Wengine wanafurahia hata kumwona mwanamke mwenzao akipanchiwa. Kutokana na maelezo ya shangazi wa marehemu, Dkt. V.K. Masanja, ambaye ni mhadhiri wa hapo Mlimani, matatizo ya Levina yalianza wakati wa dansi ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza iliyofanyika kwenye hoteli ya Silversands ambapo alikataa kwenda na mwanafunzi wa mwaka wa nne wa Kitivo cha Uhandisi aitwaye Mark Victor.

FUJO

Levina alienda dansi hiyo na rafiki zake. Victor alipomuona alimtaka warejee pamoja na akalalamika kwa nini alidhubutu kwenda kwenye dansi na watu wengine wakati alikataa kwenda naye. Levina alikataa kuondoka naye na Victor akamvuta gauni, rafiki zake walijaribu kumtetea na papo hapo ugomvi ukaanza. Baadhi ya marafiki wa Victor wanaojita “Engineers” [Wahandisi] [kundi linalofahamika sana kati ya wanafunzi] walimsaidia Victor. Kundi jingine lijulikanalokama “insiders” walimsaidia Levina. Hatimae, baada ya kushindwa Wahandisi waliondoka kwenye dansi, lakini huo haukuwa mwisho wa matatizo ya Levina.

Waliporejea kwenye dansi mgogoro mwingine ulizuka kati ya Victor na kundi lake na Levina na rafiki zake. Walipofika kwenye mabweni yao, Victor alikuwa akimsubiri ndipo ikawa usiku mzima kutupiana matusi. Asubuhi na mapema Levina alipeleka malalamiko MUWATA [Serikali ya wanafunzi] uongozi ambao ulisulihisha tatizo hilo. Victor aliomba radhi na akadai kuwa alikuwa amelewa.

Siku iliyofuatia, tukio la Silversands lilipanchiwa. Michoro ya Punch haikumwonyesha jina lake lakini kwa kutoa namba yake yakusajiliwa ilidhihirisha kuwa michoro inayofuatia angekuwemo. Baadhi ya wanafunzi wa kiume walimwendea Levina na kumwambia kuwa walikuwa kwenye kundi la PUNCH. Walimtishia kumpanchi iwapo angekataa kufanya nao mapenzi. Aliwakatalia na akakosa raha sana. Mmojawapo wa wanafunzi hawa alikuwa Omari Saloti, mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Uhandisi.

Dkt. Masanja alisema kuwa yeye (Levina) ndiye alimweleza yaliyotokea. Dkt. Masanja alisema kuwa alimweleza Levina kuhusu uzoefu wake na mambo ya PUNCH alipokuwa mwanafunzi na jinsi alivyoweza kuyapuuza. Alisema kuwa Levina alionyesha kupata ujasiri na akafikiria kuwa mambo yamekwisha. Marafiki wa Levina waliambiwa kuwa wangepanchiwa iwapo wangeonekana wakiandamana naye. Alitengwa. Maelezo machafu yalitolewa na maandishi yaliandikwa dhidi ya jina lake katika kila orodha ya majina ambamo majina yake yalikuwemo.

Usiku wa tarehe 3 Februari mwaka huu kiasi cha saa 7.30 wakati Levina alipokuwa kitandani akijisomea alisikia mlango ukigongwa. Kabla hajajibu, mlango ulifunguliwa na Omari Saloti aliingia kwa nguvu chumbani. Walipigana. Levina alimng’ata mkono naye alimpiga ngumi za mashavuni na kwenye matiti. Levina alikimbia akiwa amevaa gauni ya kulalia tu na akajificha kwenye kichaka kilichoko nje ya bweni wakati Saloti akiwa bado anamnyemelea. Aligonga nyumbani kwa mlinzi, ambaye alimsindikiza hadi chumbani kwake na akasubiri kwa muda nje.

Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwadhalilisha wanawake

Inasemekana kuwa Saloti alitaka kumbaka, wakati wengine wanasema alimbaka. Wanasema Levina alikataa tu kusema. Hata hivyo Saloti alikuwa amemtishia Levina kuwa angembaka na kumwibia vitu vyake. Asubuhi iliyofuatia, mlinzi alisema kuwa alizungumza na saloti na akasema alikuwa “Amelewa” wakati huo. Levina pia aliwona meneja wa bweni, ambaye alizungumza na Saloti. Alisema kuwa Saloti alimwambia kuwa alifunguliwa mlango na Modesta mwenzake Levina ambaye walikuwa wakiishi naye chumba kimoja. Modesta, alikanusha madai hayo kwani yeye ameoloewa na kila mwisho wa juma huwa nyumbani na familia yake.

Dkt. Masanja alisema alimpa barua Levina na kumwelekeza kwa Mshauri wa wanafunzi, Dkt. Biswalo ambaye alikuwa akienda kwenye Mkutano wa Baraza hivyo naye alimelekeza kwa Mama Rajabu. Waliitisha jalada la Meneja wa bweni/Mlinzi lakini halikuwa na chochote. Levina alifariki jioni ya tarehe 7, Februari 1990. Inaonekana kuwa kundi la Punch ni mabingwa wa vita vya kisaikolojia na wamefanikiwa lengo lao kinyume cha matarajio yao kwa kumkatisha tamaa Levina mpaka akaona kuwa maisha yake hayana maana tena. Zaidi ya hayo utu wake ulikuwa umedhalilishwa na jitihada za Saloti za kutaka kumbaka [Maana katika jamii ya Kitanzania inaaminika kuwa mwanamke akibakwa amependa mwenyewe].

Kutokana na Punch kuwalazimisha marafiki wa Levina wamtenge, kumdhihaki mbele ya kadamnasi, kumdhalilisha na kumuonea, kutokana na malalamiko yake kutoshughulikiwa na MUWATA kwa kumwambia kuwa hakuna awezaye kushindana na Punch, wakati wengine walikuwa wakimcheka tuu anavyolalamika na rafiki zake wakimuepuka, yote haya yamemfanya alazimike kukata maisha yake kwani aliamini jamii nzima ilikuwa dhidi yake.

Punch ilifanikiwa kuondoa umoja kati ya wanawake. Saloti alifanikiwa kumkosanisha Levina na Modesta, mtu pekee ambaye ndiye alikuwa akimwamini, kwa kudai kuwa yeye ndiye alimpa ufunguo. Ukweli ni kwamba funguo zote za Hall 7 [alimokuwa akiishi Levina] ziliweza kufungua angalau milango mitano, wakati katika Hall 3 bweni lingine la wanawake ufunguo mmoja unafungua milango yote ya gorofa hiyo. Walimfuatafuata na kumgongea mlango usiku wa manane, walimtupia maneno machafu na kumtishia mlangoni pake, walifanya aonekane kama ‘mwenda wazimu’ na asiyefaa.

Mkutano wa dharura wa wanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu, wahadhiri, wafanyakazi na wakazi wengine kwenye kampasi uliotishwa tarehe 9 Februari ulikubaliana kuwa wanawake walilaumu uongozi kwa kukataa kuchukua hatua za kinidhamu wakati mambo kama hayo yalipotokea. Wanasema iliendelea hivyo hadi kufikia hatua ya kuwakatisha tamaa wahasirika wasichukue hatua za kisherina kushindwa kutoa ushauri unaofaa kwa wanafunzi.

Levina Shujaa

Walisema kuwa Serikali ya wanafunzi [MUWATA] imekuwa kimya ikiangalia tu na mara nyingine ilishirikiana na waovu hao. Walisema kuwa wanafunzi wa kike ambao walijaribu kupata msaada kutoka MUWATA walijikuta katika matatizo makubwa zaidi, maana walihubiriwa kuhusu ukubwa na uwezo wa Punch.

Zaidi ya hayo wakina mama walisema kuwa jumuiya ya wanafunzi wanaichukulia Michoro ya matusi ya Punch kama burudani muhimu na wanafunzi wanaonewa wametumbukia kutokana na mgawanyo na mbinu za utawala za Punch, wakati wasomi na uongozi wamekaa kimya wakihofia visasi kutoka kwa Punch ambayo ilikuwa, inatikisa jamii nzima. Wakina mama walikubiana kuwa, Levina “asipotee hivi hivi, sisi tumtangaze shujaa ambaye hatimae ameikomesha Punch”.

Hata hivyo wanaume wanaposikia haya wanacheka. Wanauliza, “kwa nini mmuite Levina shujaa? Alikuwa malaya! Alikula pesa za watu! Mlitaka ale tu halafu asilipe? Kwani yeye ni wa kwanza kujiua! Ni m.p.u.m.b.a.v.u. Alikuwa mdhaifu. Alikuwa mjamzito! Unyanyaswaji wa kijinsia ni jambo la kawaida, wanawake pia wanayanyasa kijinsia. Mwanafunzi mmoja alirukwa na akili kwa sababu alikataliwa na msichana.” hayo ni baadhi ya maelezo yanayotolewa na wanaume wetu ndani na je ya kampasi.

Hati zenye kuonyesha uso wa levina zilikuwa zimebandikwa fuvu la Punch. Aliyekuwa Waziri wa nchi asiye na Wizara Maalum, Mheshimiwa Getrude Mongella, alipozungumza kwenye mgahawa baada ya kunywa chai katika ‘high table’ alilaani unyanywasaji wa kijinsia huko Mlimani na kusema ni sawa na kitu kilichokuwa kinachemka na sasa kimepasuka baada yua kufikia kikomo. Mapambano ndiyo kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi zote za elimu ya juu na sehemu za kazi. Lazima kuwepo na mapambano ya kitaifa dhidi ya uovu huu!

Makala hii iliandikwa na Chemi Che-Mponda.

Saturday, October 18, 2014

Chemi Katika Sinema, HIstoria ya Khanga 1994



Mwaka 1994, TAMWA, walitengeneza sinema kuhusu Historia ya Khanga. Mimi nilikuwa mmoja wa waigizaji pamoja na Issa Michuzi.  Mnaweza kuona Clip yote YOU TUBE:

CHEMI & MICHUZI IN HISTORY OF KHANGA

Saturday, July 12, 2014

Chidi Benz Ampiga Ray C

Jamani, jamani, jamani! Mambo gani tena haya! Dume anampiga dada wa watu namna hii! Halafu bado huyo dume anaitwa Staa! Huyo ni mhalifu na anstahili kuwa jela kwa kitendo alichokifanya kwa Ray C.  Mmeona hatua zilizichukuliwa dhidi ya Chris Brown alivyomtwanga Rihanna? Nilipokuwa TAMWA, nilishughulikia sana maswala ya uoneveu dhidi ya akina mama. Loh! Huyo jamaa siyo Chid Benz ni Chizi Benz!

*********************************************

Kwa habari kamili ya Tukio Tembelea GLOBAL PUBLISHERS:


http://api.ning.com/files/Jlj7Yacjzg3*Iyvt90DSt5oT20Lf6U4hQjUZP8Q9QGKLl7Ba9HNopUt0VXWvUSXeDCKIuek51EB2qvq0z85a*SGDrfCArDwR/chdi.jpg
Huyo ni Mwanaisha ambaye alipigwa kabla na Chid Benz

Bongo Flava Star - Rehema Chalamila aka. Ray C
 
Ray C Hospitalini Baada ya Kipigo


Na Musa Mateja
Uonevu! Rapa mwenye ‘swagger’ za Ja-Rule Bongo, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, anadaiwa kukwaa kisanga kingine kibaya baada ya kukurupuka kutoka nyumbani kwake na kwenda kumvamia staa mwenzake, Rehema Chalamila ‘Ray C’ nyumbani kwake anapoishi na kumtwanga makonde ikiwa ni siku chache tangu jamaa huyo apate msala mwigine wa aina hiyo.

 TUJIUNGE NYUMBANI KWA RAY C
Ilidaiwa kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita nyumbani kwa Ray C, Changanyikeni jijini Dar es Salaam ambapo ilisemekana kwamba Chid Benz alimvamia mishale ya saa 4:00 usiku kwa gia ya kumsaka mzazi mwenzake aliyemtaja kwa jina moja la Mariam.


CHID BENZ ATAKA KUMUONA MWANAYE
Ilidaiwa kwamba Chid Benz alisema kuwa alizungumza na mpenziye huyo kwamba alitaka kwenda kumuona mwanaye ambapo Mariam alimjibu kwamba kwa muda huo alikuwa nyumbani kwa Ray C  Changanyikeni.

UNGA WATAJWA
Sosi wetu alidai kwamba baada ya kujibiwa hivyo, Chid Benz alianza kulalama na kumwambia anamfuata palepale kwa nini usiku ule alale kwa Ray C, wakati ana uwezo wa kwenda nyumbani au amekwenda kwa staa huyo ili kunywa dawa zao za kuondoa sumu ya madawa ya kulevya ‘unga’,
 jambo ambalo jamaa huyo siku zote huwa hataki hata kulisikia masikioni mwake.


CHID BENZ AWAVAMIA
“Huwezi kuamini baada ya muda kama wa saa moja, Ray C na Mariam wakiwa ndani wakitazama TV, ghafla mlango ulisukumwa kwa nguvu kisha akaingia Chid Benz na kumdaka Mariam na kuanza kumshushia kipigo.“Yaani huo mshtuko walioupata walidhani wamevamiwa na Al-Shabaab.
KIBAO CHAMGEUKIA RAY C
“Mungu mkubwa kwa sababu Mariam alifanikiwa kuchoropoka na kukimbilia chumbani ndipo kibao kikamgeukia Ray C.
“Ray C akiwa anashangaa ghafla naye alipokea kipigo kikali kutoka kwa Chid na kumsababishia majeraha mbalimbali mwilini.
RAY C AKIMBILIA KWA MAJIRANI
“Baada ya kuona maji yanazidi unga, Ray C alitafuta upenyo na kukimbilia kwa majirani huku akipiga kelele za kuvamiwa, mara moja majirani waliambatana naye mpaka nyumbani kwake.
“Walipofika Chid Benz alikuwa ametumia staili za kininja kwa kuruka geti na kutokomea kusikojulikana huku akiwaacha Ray C na Mariam wakiangua vilio kwa kipigo kikali walichopokea.
RAY C AVUJA DAMU
“Ray C aliumia mkono na mguu ambao ulionekana ukivuja damu. Mariam alikuwa akililia mbavu zake kuchakazwa kwa makonde mazito na upande mwingine baadhi ya vyombo vya ndani vikionekana kuvunjwa na vingine kusambaratishwa kufuatia tafrani iliyozuka muda mfupi baada ya Chid Benz kutia maguu nyumbani hapo,” chanzo kilishusha madai hayo mazito.

RAY C ATIRIRIKA SAKATA LILIVYOKUWA

Akizungumzia na gazeti hili Alhamisi iliyopita juu ya sakata hilo, Ray C alisimulia mkasa mzima: “Kweli Chid Benz alikuja nyumbani kwangu na kunivamia.
“Alinipiga vibaya sana na kuvunja baadhi ya vitu vya ndani kwangu, jambo ambalo lilinishangaza zaidi ni namna alivyopafahamu nyumbani kwangu hadi kuja kunifanyia fujo nikiwa na mzazi mwenzake, Mariam ambaye nilitoka naye ofisini kwangu.
“Ujue jana (Jumatano) tulikuwa na kazi sana ofisini kwangu mimi na Mariam, sasa kutokana na kubanwa na kazi kweli muda ulienda sana hivyo nikamwambia Mariam akalale kwangu.
“Kwa kuwa muda ule ilikuwa ngumu kwenda kwao Mbezi Beach, Mariam alikubali na tulikwenda wote nyumbani kwangu.

“Huko nyuma Mariam alikuwa mwathirika wa madawa ya kulevya lakini baada ya kusikia mimi nimeacha, naye aliachana nayo na kuanza kutumia dawa za kuondoa sumu.
“Tumeendelea kutumia naye dawa na sasa ameshapona kabisa hivyo kuna baadhi ya kazi nimekuwa nikimshirikisha kunisaidia kwenye ofisi yangu. Pia alishawahi kumshawishi Chid Benz ili aje kutumia dawa lakini jamaa alikataa na kumfanyia vurugu sana huku akimkataza kuwa na mimi kwa madai mimi ndiyo namfanya amwambie kuachana na utumiaji dawa za kulevya.
“Sasa jana alipojua hivyo nadhani Chid Benz alikuja kutimiza dhamira yake ambayo siku nyingi alikuwa akiahidi kunipiga.”

SOO LIPO POLISI

Ray C alisema baada ya tukio hilo alikwenda kuripoti kwenye Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Kinondoni na kufunguliwa jalada la kesi ambapo Chid Benz anasakwa na polisi.
Juhudi za kumpata Chid Benz hazikuzaa matunda kwani simu yake haikuwa hewani hivyo jitihada zinaendelea na kama ana ufafanuzi au utetezi anaweza kutupigia.

CHID BENZ NI TATIZO?

Chid Benz anadaiwa kuwa ni tatizo kwani tukio hilo la Ray C amelifanya wakati akiwa na tukio la pili kwa wanawake kwani kwenye Mahakama ya Mwanzo, Ilala ana kesi mbichi aliyoshitakiwa kwa kosa la kumpiga mrembo aitwaye Mwanaisha.
Mbali matukio hayo pia Chid Benz ana rekodi ya kukorofishana na wasanii wenzake kama Kalapina na marehemu Ngwea.

KWA HABARI ZAIDI TEMBELEA EDWIN MOSHI BLOG

Saturday, June 28, 2014

TAMWA kutoa Elimu Kupambana na Ulevi Kupindukia

TAMWA kutoa elimu kupambana na ulevi Kupindukia
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka akisisitiza jambo katika mkutano na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo.
KITUO cha Usuluhishi (CRC) kinachofanya kazi chini ya Chama cha Wanahabari Wanawakecha (TAMWA) kimejipanga kutoa elimu kwa jamii kuhakikisha kinapambana na matumizi ya pombe kupindukia kwa jamii suala ambalo limezidisha vitendo vya ukatili wa jinsia unaofanywa na watumiaji pombe kupindukia.

Akizungumza na wahariri wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka alisema utafiti uliofanywa na Shirika la IOGT International unaonesha kuwa kiwango cha unywaji pombe jijini Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake huku ikibainika kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya vitendo vya ukatili na matumizi ya pombe kupita kiasi. 

Bi. Soka alisema takwimu zinaonesha kuwa wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha vipigo, kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77, huku kiwango cha ukatili kwa wanawake ambao waume ama wenzi wao hawanywi pombe ni asilimia 33.

"...Utafiti uliofanywa na shirika la IOGT International unaonyesha kwamba kiwango cha unywaji pombe katika jiji la Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake...lakini takwimu kutokana na utafiti wa Demographia na Afya Tanzania (TDHS) 2010...unaonesha wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha kipigo/kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77," alisema.

Aidha aliviomba vyombo vya habari kushirikiana na TAMWA kutoa elimu kwa jamii kupunguza matumizi ya pombe kupindukia kwani licha ya ukatili huo familia pia zimekuwa zikiathirika kiuchumi juu ya matumizi ya pombe huku baadhi ya watoto wakikosa huduma za msingi kutoka kwa baadhi ya wazazi ambao ni walevi kupindukia.

Alisema TAMWA inatekeleza mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana unaosababishwa na pombe huku lengo kuu ikiwa ni kuhakikisha maisha ya wanawake na watoto yanaboreshwa kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupindukia.

Hata hivyo alisema tayari chama hicho kimeanza kufanya utafiti mwingine katika Wilaya ya Kinondoni kuangalia madhara yanayotokana na unywaji wa pombe kupindukia ili kuangalia hali halisi ya matumizi ya pombe eneo hilo na madhara ambayo yamekuwa yakitokana na matumizi hayo.

Alisema malengo mengine ya mradi ni pamoja na kuboresha maisha ya wanawake na watoto kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe katika wilaya ya Kinondoni na pia kujenga uelewa miongoni mwa jamii juu ya madhara yatokanayo na unywaji wa pombe kupindukia. 

Mkurugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA aliongeza kuwa mapambano hayo pia yatasaidia, kukabiliana na matumizi ya pombe na kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu ukatili dhidi ya wanawake unaotokana na matumizi ya pombe, ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo wa jamii kukabiliana na ukatili unaosababishwa na unywaji wa pombe dhidi ya wanawake na watoto.

Tuesday, September 18, 2012

Mh. Shy-Rose Bhanji Atoa Shs. 2 Milioni Kwa TAMWA


Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Ndugu Ananilea Nky, akikmkaribisha Mbunge wa Afrika Mashariki, Mh. Shy-Rose Bhanji kwenye ofisi za TAMWA, Sinza

Mbunge wa Afrika Mashariki, Mh. Shy-Rose Bhanji akikabidhi shs. milioni mbili (2,000,000/-)  kwa TAMWA ikiwa ni mchango wake kwa TAMWA kuendeleza harakati zake nchini.

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Monday, October 03, 2011

Sinema 'Historia ya Khanga" Cheki Mimi na Kaka Michuzi!

MaStaa wa Bongowood 1991 Michuzi & Chemi


Kabla ya Kanumba na Ray kulikuwa na Chemi na Michuzi!

Wadau, kwenye mwaka 1992 nilishiriki katika sinema ya TAMWA, "The History of Khanga".  Hebu itizame, Utaniona mimi na Kaka Michuzi, "Tunajiandaa kulala"

Mwongozaji alikuwa Dada Fatma Alloo. Pia kuna mahojiano na marehemu Bibi Titi Mohamed.

Sinema sasa iko YOU TUBE kwa hisana ya Dada Fatma na Kaka Michuzi:

http://www.youtube.com/watch?v=jAuhAB0HeeA&feature=player_embedded

Thursday, July 08, 2010

Sauti ya Siti - Gazeti la TAMWA

Mwezi Machi, 1988 TAMWA ilizindua gazeti 'Sauti ya Siti'. Mimi ni mmoja wa waanzilishi wa TAMWA. Nakumbuka siku tulipotaarifiwa kuwa serikali imekubali kusajiliwa kwa TAMWA, na siku tuliporuhusiwa kuchapisha Sauti ya Siti. Ilikuwa jambo kubwa mno maana wanaume walitupinga kweli hata baadhi ya wanawake. Walisema TAMWA ni chama cha mashoga. Cha ajabu hao hao waliokuwa wanatusema walikuja kujiunga na TAMWA baada ya kuona mafanikio yetu.

Gazeti ya Sauti ya Siti ilikuwa na nia ya kuelezea habari za akina mama ambazo zilikuwa haziingii katika magazeti ya kawaida. Kumbuka wakati ule magazeti yalikuwa machache, Daily News, Uhuru, Mfanyakazi, Kiongozi. Redio ilikuwa Radio Tanzania tu!

Mzee Ali Hassan Mwinyi (Mzee Ruksa) ndiye alikuwa Rais. Mke wake alikuwa anaitwa Siti. Basi watu walisema eti sisi wanaTAMWA tuliamua kuita gazeti Sauti ya Siti ili kumpendeza Rais. Jamani!

Watu walikuwa wamesahau kuwa kulikuwa na Siti Binti Saad. Nia ya TAMWA ilikuwa kukumbusha watu juu ya mchango wa Bibi Siti katika muziki na pia hasa kuwa Siti ndiye alikuwa mwanamke wa kwanza wenye uwezo wa kufikisha ujumbe kwa Umati. Taarab aliyokuwa anaimba ilikuwa na ujumbe za kisiasa pamoja na mapenzi. Wangapi wanajua kuwaa Bibi Siti ndiye alihamisha watu kufanya mgomo huko Zanzibar miaka ya 1930's? Wanasema Siti alitunga zaidi ya nyimbo 600! Bahati mbaya nyingi zimepotea maana hazikuwa Recorded.

Nitafanya jitihada hivi karibuni za kufufua ile website niliyokuwa nayo iliyokuwa inaelezea mengi kuhusu maisha ya Siti Binti Saad.

Leo tunakukumbuka Bibi Siti Binti Saad.

Saturday, March 06, 2010

Mkurugenzi wa TAMWA apata Tuzo Muhimu!

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya akipiga posi na tuzo nje ya ofisi za TAMWA huko Sinza mara baada ya kuwasili kitoka ubalozi wa Marekani

HOTUBA YA MKURUGENZI MTENDAJI WA CHAMA CHA WANAHABARI WANAWAKE NCHINI (TAMWA), ANANILEA NKYA KATIKA MKUTANO WA WANAHABARI, UBALOZI WA MAREKANI KWA AJILI YA KUKABIDHIWA TUZO YA MWANAMKE JASIRI WA TANZANIA KWA MWAKA 2010


Mheshimiwa Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt,
Wafanyakazi wa Ubalozi wa Marekani,
Wanahabari na wanaharakati wenzangu,
Wageni waalikwa,
Mabibi na Mabwana.


Ninashukuru kwa kupata heshima hii kubwa ya kusimama mbele yenu kama mteule wa tuzo ya Mwanamke Jasiri wa Tanzania kwa mwaka 2010.

Kwa heshima na taadhima nianze kwa kushukuru Ubalozi wa Marekani hapa nchini na wananchi wa Marekani kwa ujumla kwa kunichagua mimi kama MWANAMKE JASIRI WA TANZANIA KWA MWAKA 2010 kutokana na juhudi na ubunifu wa kutumia vyombo vya habari katika kuimarisha usawa, fursa na haki za wanawake na watoto wa kike wa Tanzania.

Sina shaka kwamba Ubalozi wa Marekani ulifanya utafiti kikamilifu na tena kwa mapana na kupata majina mengi tu, maana kuwa jasiri maana yake ni kuzungumza kwa sauti kile unachokiamini kuhusu uonevu na uvunjifu wa haki hasa za wanyonge ili hatua ziweze kuchukuliwa kurekebisha hali hiyo. Katika mapambano ya kutetea haki za watu wa hali ya chini hasa wanawake, wasichana na watoto hapa nchini, wako watu wengi wanaofanya harakati hizi kwa juhudi kubwa mijini na vijijini. Hivyo mimi kuchaguliwa miongoni mwao, ni ishara kwamba Marekani imetambua mapambano yetu, ambapo mimi ni mwakilishi wa wapambanaji wengi.

Kwa hiyo, nachukua fursa hii kushukuru na kuipongeza serikali ya Marekani kwa kubuni TUZO YA MWANAMKE JASIRI. Kwa kubuni tuzo hii serikali ya Marekani imedhihirisha kuwa inaunga mkono mapambano mbali mbali ya wanawake katika kupigania haki zao.

Wanawake wanapambana kuweza kushiriki katika masuala ya maendeleo; wanapambana ili waweze kunufaika na rasilimali mbali mbali za taifa, wanapambana kupata haki yao kwenye huduma ya afya, elimu, mirathi, uchumi na uongozi wa nchi yao.

Natambua kuwa tuzo hii ilishatolewa kwa wanawake wawili hapa nchini; Helen-Kijo Bisimba (2008) kwa ujasiri wake mkubwa wa kutetea haki za binadamu akiwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela (Mbunge wa Same Mashariki) kutokana na ujasiri wake katika kupambana na ufisadi.

Nina hakika, baada ya muda, tuzo hii itazaa matunda ya neema hasa kwa wanawake wengi wanaotaabika kwa madhila mbali mbali mijini na vijijini. Wanawake ambao wanapambana ili wapate haki ya kuthaminiwa utu wao. Wanawake wengi hapa nchini hawana amani wala furaha kwa sababu mifumo gandamizi imewapora haki na fursa ya kutoa maamuzi kuhusu mambo yanayohusu maisha yao na familia zao na wameporwa pia fursa ya kushiriki katika vyombo vya kutoa maamuzi kuhusu namna wanavyotaka nchi yao iendeshewe.

Ninaamini kuwa kama taifa letu lingejenga mazingira sahihi ya kuwawezesha wanawake kuwa sehemu ya rasilimali uongozi katika ngazi mbali mbali, hakika wangedhihirishia taifa kuwa wana uwezo mkubwa wa kuongoza, na bila shaka nchi yetu ingenufaika kiuchumi, kisiasa na kijamii kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa. Kwa hali hiyo tungepiga hatua kubwa katika nyanja ya demokrasia na maendeleo na kuweza kufikia ndoto ya ukombozi siyo Tanzania pekee bali pia ukombozi wa Bara la Afrika.

Wanawake na wasichana na hata wanaume na vijana wengi hapa nchini nao wameonyesha uwezo mkubwa wa kuhimili changamoto zinazotokana na sera mbaya za uchumi. Wengi wao wamekuwa wakitegemea kilimo cha jembe la mkono na biashara ndogo ndogo kuweza kujikimu huku wakiwa na jukumu kubwa la kulea yatima ambao wanaongezeka kila siku na kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI ambao hulazimika kurudishwa majumbani kutokana na mfumo duni wa afya.

Wanaume, Wanawake na vijana hawa wa kike na wa kiume wa taifa hili siyo tu wamedhihirisha kuwa ni ni watu jasiri, bali pia ni watu wenye uwezo wa kuibadilisha Tanzania kuwa ni mahali pazuri pa kuishi watu wa wakundi yote wanaume, wanawake, wazee na vijana, wenye ulemavu na wasio na ulemavu. Ndiyo sababu Tanzania inahitaji kuwa na mipango ya maendeleo yenye malengo mahususi na mikakati madhubuti ya utekelezaji wa mipango hiyo. Mipango hiyo ni muhimu itengenezwe kwa kuzingatia sauti, mitizamo, uwezo na mahitaji ya watu wa ngazi za chini na wanaharakati na wanahabari wana wajibu wa kushinikiza bila woga hatua zichukuliwe kutekeleza mipango hiyo kwa ufanisi.

Ukatili wa kijinsia una athari mbaya kwa wanawake na wasichama kwa kuwa unawaathiri kisaikolojia na hivyo kushindwa kutekeleza wajibu wa kuboresha maisha yao na maisha ya wale wanaowategemea. Sheria zilizopitwa na wakati ambazo zinakoleza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa kike zinahitaji taifa kupata viongozi imara na hasa Wabunge wenye ujasiri wa kuisimamia serikali ili iwajibike kubadilishe sheria hizo. Sheria hizo mbaya ni pamoja na ile ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo inaruhusu mtoto wa chini ya miaka 18 kuolewa na hivyo kumkosesha haki yake ya kupata elimu na kuhatarisha maisha yake endapo atapata ujauzito.

Mheshimiwa Balozi,

Mimi ujasiri nilionao kwa kiwango kikubwa umechangiwa na taaluma yangu ya uandishi wa habari na uanaharakati wa masuala ya jinsia, demokrasia, maendeleo na haki za binadamu.

Kunichagua mimi kama mwanamke jasiri mwaka huu 2010, ni motisha kwa wanahabari na wahaharakati; wanawake na wanaume ambao wamekuwa wakijishughulisha kwa namna mbali mbali kuleta mabadiliko katika mila mbaya, mifumo, imani na sera gandamizi ambazo zinabagua na kuwatupa pembezoni wanawake na wasichana.

Kwa hiyo, naipokea tuzo hii kwa niaba ya wanawake wote wa Tanzania na wanaume na wanawake wa umri mbali mbali ambao nimekuwa ninashirikiana nao katika vyombo vya habari, kwenye harakati na Chama cha Wanahabari Wanawake nchini (TAMWA) ambacho tangu kilipoanzishwa miaka 21 iliyopita kimekuwa kikipaza sauti kutetea haki na fursa za wanawake, wasichana na watoto. Tuzo hii niliyoipata leo, sote tuichukulie kama changamoto, mwanzo mpya na kitu cha pekee cha kututia moyo katika kuendeleza jitihada za kutetea usawa, fursa na haki kwa wanawake, wanawake wasichana na watoto wa Tanzania.

Mheshimiwa Balozi,

Kuna msemo wa Kiswahili usemao â€Å“Sema Usiogope Sema”. Naichukulia hii tuzo ya ujasiri niliyopewa leo kama ishara kwamba Marekani inatambua kwamba mapambano katika ngazi ya familia, kitaifa, kikanda na kimataifa kwa ajili ya kuimarisha usawa wa jinsia, haki za binadamu na uhusiano mzuri baina ya mataifa ni muhimili muhimu katika kujenga amani duniani.

Sisi wanaharakati wa Tanzania tunashikamana na wanaharakati wengine duniani kote katika mapambano ya kubadilisha dunia ili iwe mahali pazuri pa kuishi watu wote wanaume na wanawake, maskini na matajiri wa rika zote.

Mhusiano usio sawa katika ngazi ya kimataifa unaguza na kuleta amthari mbaya katika mahusiano ya kikanda, kitaifa na hata ngazi ya familia. Mahusiano kama hayo huchangia moja kwa moja kuwepo na mahusiano yasiyo na uwiano sawa baina ya wanaume na wanawake. Mahusiano yasiyo na usawa huchangia kwa kiasi kikubwa vitendo vya kikatili na ukiukwaji wa haki za binadamu siyo tu dhidi ya wanawake na wasichana, bali pia dhidi ya makundi mengine yaliyoko pembezoni. Hali hii iko dhahiri katika Bara letu la Afrika ambalo limekuwa likishuhudia uporaji wa ardhi ya wanyonye, wimbi la rushwa na ufisadi unaohusisha baadhi ya viongozi na wafanya biasharawakubwa.

Ni imani yangu kuwa tuzo hii ya MWANAMKE JASIRI itaendelea kuimarika na kuwa kichocheo kwa wanaharakati wote ili wasichoke na mapambano, hata yatachukue muda mrefu kiasi gani maana dunia iliyo bora na salama kwa wanawake na watoto ndiyo itatengeneza dunia bora, salama na yenye neema na furaha tele kwa watu wote.

Nawashukuru wote kwa kunisikiliza,

Nakushukuru Mheshimiwa balozi na wananchi wa Marekani kwa wazo hili zuri la kutoa tuzo ya mwanamke jasiri.

Ananilea Nkya

Executive Director (TAMWA)

02/03/2010
*****************************************************
Nami nasema HONGERA Dada Nkya! Kweli umetoka mbali na unfanya kazi nzuri mno TAMWA! - Chemi

Tuesday, September 22, 2009

Wananchi Msidanganywe na Mafisadi - TAMWA

Kutoka http://www.ippmedia.com/

Tamwa Yawaasa Wananchi Wasidanganywe na Mafisadi
Na Mwandishi wetu

22nd September 2009

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa) kimewataka wananchi kuwachunguza kwa makini wagombea uongozi katika vitongoji, vijiji na mitaa ili kuepuka kuwachagua wala rushwa na mafisadi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Ananilea Nkya, alisema wagombea hao wasichaguliwe kwa kuwa ni adui wakubwa wa maendeleo.

"Wananchi wanapaswa kuwachunguza kwa makini watu wote watakaogombea uongozi katika vitongoji, vijiji na mitaa ili kuepuka kuwachagua wala rushwa na mafisadi ambao ni adui mkubwa wa maendeleo ya wananchi," alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jijini jana.

Alisema umuhimu wa wananchi kuwachunguza wagombea unatokana na ukweli kuwa matatizo mengi kwenye vitongoji, vijiji na mitaa yanatokana na baadhi ya wananchi kutotambua kwamba kura yao ndicho kitu muhimu wanachoweza kutumia kuwanyima uongozi wala rushwa na mafisadi.

Alisema ili uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika nchi nzima tarehe 25 mwezi ujao uweze kuweka madarakani watu ambao si wala rushwa na mafisadi ni muhimu wananchi wote watambue kuwa kipindi cha uchaguzi siyo lele mama, bali ni kipindi cha kutafakari kwa makini na kufunga mkanda ili kuepuka vishawishi vya watu wanaonunua uongozi kujinufaisha.

Alisema kutokana na baadhi ya wananchi kutokuwa makini wakati wa uchaguzi, katika miaka ya hivi karibuni uongozi wa umma umegeuzwa kuwa ni mradi wa wanaopata uongozi kujitajirisha badala ya kutumikia umma, hali ambayo inachangia kushamiri kwa kero za wananchi na umaskini miongoni mwa wanawake na wanaume wengi nchini.

"Wagombea wala rushwa na mafisadi huwa wanatumia mbinu kuwadanganya wapiga kura ili kushinda uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuwatisha wananchi, kuwahonga vyakula, vinywaji, mavazi, simu, fedha au kuwapa ahadi za uongo.

"Wala rushwa na mafisadi wakishapata uongozi katika mitaa na vijiji, huzitumia ofisi hizo kwa manufaa yao binafsi zaidi hasa kujitajirisha kwa kuuza na kukodisha mali za mitaa na kuwatoza wananchi fedha wanapokuwa wanahitaji huduma ya kiongozi kwa ajili ya kutatua matatizo yao," alisema.

Alisema baadhi ya viongozi wala rushwa huwatoza wananchi fedha kati ya sh. 1,000 na sh. 5,000 bila kuwapatia risiti wanapohitaji kupata barua ya kuwatambulisha kama wakazi wa eneo husika au kama wanahitaji huduma ya kiongozi kutatuliwa matatizo binafsi yanayowakumba. Alisema Tamwa inaona kuwa viongozi wengine wala rushwa na mafisadi wamekuwa ndio chanzo cha serikali kulalamikiwa na wananchi kutokana na kuua miradi ambayo inaanzishwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Kwa mfano, alisema mwaka 1998 serikali ilijenga visima vya maji safi katika mitaa ya jiji la Dar es Saam ili kupeleka huduma hiyo karibu na wananchi, lakini katika baadhi ya mitaa viongozi waliochaguliwa na wananchi wamegeuza visima hivyo kuwa ni miradi yao binafsi ya kujipatia fedha na katika vingine katika mitaa kadhaa vimekufa kabisa kutokana na ubinafsi wa viongozi.

CHANZO: NIPASHE

Tuesday, September 08, 2009

Wasichana Wanaopata Mimba Kuruhusiwa Kuendelea na Shule?

Wadau, nimefurahi sana kusikia kuwa huenda hivi karibuni wasichana wanaopata mimba wakiwa wanafunzi wataruhusiwa kuendelea na masomo yao baada ya kujifungua. Nakumbuka kuona wanafunzi wenzangu wengi kusimamishwa shule shauri ya ujauzito. Inasikitisha maana hali yao ya maisha inakuwa chini shauri ya kukosa masomo. Wengine walikufa kwa athari za kutoa hizo mimba.

Nilipouliza kwa nini wasichana hawaruhusiwi kuendelea na masomo, watu walisem, nani atalea hao watoto? Pia walisema eti itafanya wasichana wasitake kufanya ngono. Mbona wanafanya? Na je, kwa nini huyo aliyempa mimba kama ni mwanafunzi hasimamishwi masomo? Kazi kuonea wanawake!


Kama TAMWA watafanikiwa kupitisha hiyo sheria mbona watakuwa mashujaa!

************************************************************************
Kutoka ippmedia.com

8th September 2009

Tanzania Media Women`s Association (Tamwa) executive director Ananilea Nkya
Girls becoming pregnant while in school might soon be officially allowed to continue with their studies after giving birth.The remote dream will come true if the government endorses a provision in a draft of the new education policy recommending as much.

Allowing the girls to return to school will be an historic move after decade-long appeals from civil society organisations and the donor community to the government to revisit guidelines instructing schools to expel all girls medically proven to be pregnant.

The decision to produce guidelines stipulating procedures to be followed to reduce the incidence of schoolgirl pregnancies and readmitting schoolgirls put in the family way follows recommendations by a team selected by the government in 2007.

The team was detailed to collect views from education sector stakeholders on how best to address the problem of schoolgirl pregnancies.

It came up with findings showing that over 90 per cent of respondents from eight education zones wanted the girls back in school after delivery, while only two per cent stood against the idea.

Amnesty International estimates that some 14,000 schoolgirls were expelled from school in Tanzania between 2003 and 2006.

Winifrida Rutahindurwa, Gender issues coordinator at the Education and Vocational Training ministry, said when contacted for comment that only those schoolgirls becoming pregnant after the new guidelines are put into use would be allowed to return to school if the new policy is approved.

It is understood that the new guidelines will not come into effect before the draft of the new Education and Training Policy is assented to by the Education and Vocational Training minister later this year.

The policy will have to be sent to the Cabinet for approval in two months time before the final draft is relayed to the Parliamentary Social Services Committee for review, after which the Attorney General will prepare a bill from the national policy on education to amend the 1978 National Education Act.

But an education analyst who preferred anonymity said the bill is likely to face strong opposition from a section of Members of Parliament if it bears even a single clause allowing girls who conceive while attending school to continue with studies after delivery.

He said some legislators had shown strong support in previous debates in the House that such girls be expelled from school because they were seen to have misbehaved and thus deserved severe punishment.

“I know some MPs who will do anything and everything in their power to make sure the bill doesn’t sail through because of the feeling that such a move would fuel teenage pregnancies. But the truth is that these girls deserve to go back to school,” said the analyst, a long-serving educationist.

Speaking in a later telephone interview from Kilimanjaro Region, where she is on a mission to find out why Kilimanjaro had no cases involving schoolgirls dropping out of school due to pregnancy, Ms Rutahindurwa said readmitting such girls into school “is definitely not the best or only solution to the problem”.

Society had a role to play to make sure that girls remained in school and in sound health, she said, adding that poverty played a key role in sustaining the problem.

“Most schoolgirls become pregnant because of poverty, but culture also has a role to play in this because there are regions where girls are taught how to engage in sex at a very early age,” noted Ms Rutahindurwa.

According to the Basic Statistics of Tanzania (Best), an annual booklet that provides data on education in the country, Mtwara Region, where initiation ceremonies are common, had the highest dropout rate due to early pregnancies in 2007. More than 435 girls left school after becoming pregnant.

“Girls must be treated equally with their male counterparts. They must be given another chance to continue with education six months after giving birth, as medically recommended. I see this problem affecting poor people the most because it is they who can’t afford taking their children to private schools after expulsion. Our challenge right now is not only to return the girls to school but cut the cases altogether,” observed Ms Rutahindurwa.

According to the draft policy, the participation of girls in education at primary and secondary levels is lower than that of boys because of early pregnancies and changes ought to be made to make guarantee gender equality at all levels of education.

“The government will continue building more boarding girls’ secondary schools and extending the available ones… It will also come up with guidelines to enable female students who become pregnant to continue with their studies after giving birth,” part of the new policy reads.

It adds that the government would also come up with ways to punish all men involved behind schoolgirl pregnancies, but many observers believe that this is much easier said than done.

Tanzania Media Women’s Association (Tamwa) executive director Ananilea Nkya told this newspaper last year that there were no men who were known to have been prosecuted for impregnating schoolgirls. She suggested that the government and society were taking a stance too lenient to help out the victims, meaning the girls being put in the family way so prematurely.

SOURCE: THE GUARDIAN

Thursday, November 08, 2007

Msanii Ernest Mtaya anaoa kwa staili aina yake!





Ninamfahamu msanii na mchoraji, Ernest Mtaya tangu ni kijana mdogo. Alikuwa anatusaidia TAMWA katika mambo ya uchoraji katika magazeti na vitabu yetu. Sasa ni mwalimu maarufu wa uchoraji. Amewahi kupata zawadi ya uchoraji kutoka Mfuko wa Utamaduni Tanzania.

Pia alishiriki katika sinema ya Maangamizi the Ancient One. Picha zake nyingi zilitumika kwenye hiyo sinema, iliyowakilisha Tanzania katika mashindano ya Oscars Hollywood mwaka 2001.

Ernest na Juddy HONGERA! Nawatakieni maisha mema ya ndoa.

Dada Chemi

***********************************************************************************
Ndugu zangu na marafiki zangu,Natumaini wote ni wazima na kama wapo ambao wanaugua au wanauguliwa naombaMUNGU awasaidie katika matatizo hayo. Mie ni Ernest Mtaya (pichani) na maelezo yangu zaidi yanapatikana katika http://www.ernest.4mg.com/

Madhumuni ya barua hii ni kuwafahamisha natarajia kuoa tarehe 17 Novemba 2007 saa 10 kamili katika kanisa linalojulikana kama st.Peter's church liliopo Oysterbay karibu na shule ya Mbuyuni hapa Dar Es Salaam. Baada ya hapo kutakuwa na msafara wa BAJAJI sita kuelekea eneo la sherehe ambalo ni kijiji cha Makumbusho tena nje chini mwembe.

Sherehe hii itakuwa na vionjo vya kitamaduni zaidi ya "uzungu" katika msafara wa Bajaji tutakapofika eneo la Victoria tutabadilisha usafiri na kupanda GUTA lililotengenezwa kiustadi kabisa na kuitambua Bajaji nitakayokuwa na mtarajiwa wangu itakuwa imepambwakwa makuti.
Sherehe itashereheshwa na msanii maarufu wa jukwqaa Mrisho Mpoto kwa wasiomfahamu ni yule muimbaji wa wimbo wa SALAMU KWA MJOMBA pia kutakuwa na msanii maalufu wa Afro Reggae Jhiko Manyika ambaye amerudi juzi tu kutoka ziara yake ya kimuziki ya Ulaya.
Mtumbuizaji mwingine ambaye atakuwa msimamizi wa mtarajiwa wangu ni muimbaji na mtunzi maarufu anayeitwa Karola Kinasha ambaye mbali na shughuli ya usimamizi kama Matron pia atatumbuiza kwa nyimbo zake tamu na sauti nzuri. keki , shampeni na jukwaa utamaduni wetu wa Afrika utapewa hadhi.

Cha muhimu ndugu na marafiki ni hii sherehe ya watoto ambayo nimefikiri niifanye ili watoto kwa mara ya kwanza washiriki katika sherehe ya Arusi la kwa nia ya kuwaaunganisha na kusaidiana na kutambua matatizo ya watoto wengine wenye shida zaidi yao.

Hivyo basi siku ya pili ya sherehe yaani 18 Novemba 2007 kwa niaba ya mchumba wangu JUDDY nimeandaa sherehe ya watoto ambapo nimeawaarika watoto wa mataifa mbalimbali nia kubwa ikiwa ni kuwaaunganisha watoto wote bila kujali misingi ya rangi, dini na utabaka waaina yoyote, pia kuwafanya watambue matatizo ya watoto wengine ili wakue wakijua kuna watoto wenzao wenye shida zaidi yao na wawe na moyo wakuwasaidia kupitia wazazi wao, pia kuwafanya wafurahi kwa kucheza ,kuimba na chochote chema ili mradi wafurahi.

Hapa tutafanya utafiti wa kugundua vipaji vya watoto na kuwasiliana na wazazi ili kuona mwelekeo wa kuweza kuwasaidiakatika siku za mbele ambapo Mungu akinijalia nategemea kuanzisha taasisi itakayohusika na shughuli za watoto.

Nimewaalika watoto yatima wa Kurasini ili waweze kufurahi na wenzao na kama kuna yoyote atayeweza kusaidia kwa chochote kile hasa kwa walengwa wakuu ambao ni hawa watoto yatima anakaribishwa kusaidia anaweza kupiga simu hii 0713-23 31 74 .

Michango itapokelewa hata baada ya sherehe kwani baad ya sherehe mimi na Juddy tutaelekea Zanzibar kwa mapumziko ingawa tutatumia mapumziko yetu kutembelea vituo vya watoto wenye shida na nyumba za kutunzia wazee.

Tayari kwa niaba ya Juddy nawashukuru Duka la vifaa vya elimu lilopo Upanga la KALL KWIK Bookshop kwa zawadi zao ambazo zitatolewa kwa watoto wote wataohudhuria sherehe hii.
Pia wale walioahidi kusaidia nitawaandika mara nitakapopokea zawadi zao. nawashukuru pia wazazi ambao tayari wamechangia sherehe hii na napenda kuwaahidi michango yao itasaidia kuwaalika watoto yatima na itatumika kwa madhumuni yaliyotajwa kwenye kadi tu.
Nashukuru kwa kuniamini na naahidi sitawaangusha tufanye huu ni mwanzo tu.

Ahsante na MUNGU awabariki wote na kuwajalia imani na huruma.

Ernest kwa niaba ya Juddy

Saturday, October 13, 2007

Mwandishi wa Habari Nellie Kidela amefariki dunia.

Leo nimepata habari kuwa mwandishi wa habari na mtangazaji wa siku nyingi wa Radio Tanzania Dar es Salaam, Nellie Kidela, amefariki dunia.

Dada Nelly ni moja wa waanzilishi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, TAMWA. Mkutano wa kwanza kabisa ulifanyika nyumbani kwake.

Taarifa niliyonayo ni kuwa Dada Nellie alifariki siku ya Jumatatu tarehe nane Oktoba na alizikwa, jumatano tarehe 10 Oktoba katika makaburi ya Kinondoni. Alikuwa ameugua ugonjwa wa kansa siku nyingi. Na miaka ya nyuma aliwahi kupata matibabu hapa Boston.

Dada Nellie alikuwa mama yake mzazi na Nuru Mkeremi wa hapa Boston, Massachusetts.

Mungu ailaze roho take mahali pema mbinguni. AMEN.

Thursday, August 09, 2007

Viongozi wa TAMWA

Hapa niko na Dada yangu mpendwa, Bi Evodia Ndonde, ambaye aliwahi kufanya kazi Tanzania Film Company. Sasa ana kampuni yake ya video production. Naye ni mwanachama wa TAMWA miaka mingi.
Mwandishi wa Habari wa The Guardian, Lucas Lukumbo alipita kusalimia wana TAMWA. Kulia ni mwenyekiti wa TAMWA, Bi Ananilea Nkya.

Hapa niko na Dada Edda Sanga ambaye amestaafu kutoka Radio Tanzania hivi karibuni. Dada Edda aliwahi kuwa Mwenyekiti wa TAMWA.

TAMWA wanapokea interna kutoka nchi mbalimbali kila mwaka. Huyo dada yuko TAMWA kwa kipindi cha mwaka moja, anatoka Norway. Pia kulikuwa na akina dada kutoka Zambia, Ethiopia na Canada.
Hapa nipo na Dada Fatma Alloo, aliyekuwa Mwenyekiti wa TAMWA miaka mingi. Alitufundisha mengi kuhusu uongozi katika zile siku za mwanzo wa TAMWA.
Mwenyekiti wa TAMWA kwa sasa, Bi Ananilea Nkya, Mimi, Dada Evodia Ndonde na Edda Sanga. Dada Ndonde ana kampuni ya video production, na mimi niliwahi kuwa Publicity Secratary wa TAMWA na kwenye Executive Board.

Tuesday, April 03, 2007

TAMWA

Bila shaka mmesikia majina kama Fatma Alloo, Leila Sheikh, Edda Sanga, Maria Shaba, Pili Mtambalike, Wema Kalokola (marehemu), na Ananilea Nkya. Hao ni kati ya waanzalishi wa chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Tanzania, TAMWA. Na mimi ni mmoja wa waanzalishi wa TAMWA (Tanzania Media Women's Association).

Tulitoka mbali maana mwanzoni tulipata pingamizi nyingi kutoka kwa wanawake na wanaume. Tulitukanwa na kuitwa majina ya ajabu kama, 'frustrated women, na malesbo'. Hivi sasa wanaume wakisikia jina la TAMWA wanatetemeka. TAMWA imefanya mengi kutetea haki za akina mama nchini Tanzania na inaendelea kwa nguvu! Tulianzisha kwa ajili ya kusaidia akina mama waliokuwa waandishi wa habari lakini ilikuwa mpaka kutetetea haki za akina mama Tanzania.

TAMWA Oyee!

Hii picha ilipigwa mwaka 1992. Tulikuwa kwenye safari Zanzibar na wageni wetu kutoka vyama vya akina mama mbalimbali barani Afrika. Mimi niko kushoto kabisa na miwani! Pia wamo Edda Sanga (3rd from left, Maria Shaba 5th from left, Halima Shariff 2nd from right). Wengine ni wageni kutoka nje.
Ndo baada ya hii safari iliyofana ilitokea kasheshe kubwa kutokana na picha fulani aliyopiga Muhidini Michuzi, na kuwekwa kwenye front page ya gazeti ya Daily News mpaka ilibidi viongozi wa TAMWA warudi Zanzibar kuomba radhi. Picha eneyewe ilipigwa kwenye shughuli ya mpendwa somo na kungwi mkuu wa Tanzania, Bi Kidude.
Kwa habari zaidi kuhusu TAMWA someni: