Showing posts with label Mbagala. Show all posts
Showing posts with label Mbagala. Show all posts

Friday, February 25, 2011

Precision Air Team Visits Chamanzi Orphanage Mbagala

Precision Air Network Planning and Strategy Director - Patrick Ndekana (r) together with Network Planning Staff handover material support to Mama Winifreda- Director of the Chamanzi Orphanage in Mbagala - Dar es salaam over the weekend. The team used their monthly birthday allocation money to buy the donated materials.
Picha na Taarifa zimeletwa na Helen Dallali wa Precision Air

Friday, May 08, 2009

Wamelipua Mabomu Yaliobaki!

Haya, jeshi la wananchi wanasema kuwa mabaki ya mabomu yamelipuliwa. Huko watu wanaumwa POST TRAUMATIC STRESS DISORDER! Hivi watu wamepata ushauri kweli (counselling). Yaliyotokea ni mazito na watu wataathirika kwa mingi. Naona Red Cross wanajitahidi kusaidia huko.

************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Bombs defused safely

2009-05-08

By Felister Peter and Correspondent Zuwena Shame


There was palpable panic among residents of Dar es Salaam`s Mbagala suburb yesterday as the time for detonation of 75 bombs drew near.

The reason: many relived memories of last week`s accidental bomb explosions that have claimed more than 20 lives and left over 4,000 families homeless.

However, a special team of Tanzania People`s Defence Forces (TPDF) field engineers defused the bombs without incident.

Military and other authorities monitoring the detonation exercise spoke of a generally smooth execution of the operation, whose conclusion now suggests that people inhabiting surrounding areas can live without fear of similar destructive blasts in the future.

Despite official assurances by political leaders and the army that yesterday`s explosions would cause no harm to people or their property, scores of families fled the area set aside for the detonation exercise hours earlier.

Defence and National Service minister Hussein Mwinyi announced on Wednesday that bombs which did not go off during last week`s tragic incident but had lost ``stability`` would be detonated yesterday afternoon.

He called on residents of areas near the military camp where the accident occurred, which was also earmarked for yesterday`s event, to keep at least 500 meters away.

But that distance sounded too close for comfort for the devastated residents, most of whom appeared completely unable to withstand any further explosions.

Long queues were seen yesterday as people vacated the area since early morning, many using public transport to go to distant destinations like Kongowe, Yombo Vituka, Kibada as well as Ikwiriri in Coast Region.

Mbagala Kuu and Maendeleo primary schools remained closed for the rest of the afternoon, with parents and guardians taking their children away from the vicinity.

They did not want the children to experience more deafening blasts and the risk of death or injuries.

The accidental explosions at the military stockroom at Mbagala on Wednesday last week left 25 people dead and caused massive destruction to property, with at least 4,631 houses destroyed or seriously damaged.

Hours before yesterday`s detonations, armed police and military officers were seen patrolling the area to make sure that everything was set for the smooth implementation of the exercise.

An ongoing exercise to verify the extent of the destruction and the assistance needed by surviving victims of the earlier explosions was suspended, as most members of families in need of help had long moved to safer ground.

The entire area was all but deserted, with shops, restaurants and other businesses at the local market remained closed. Calls for patience had done little to calm nerves.

Hemedi Seukwa, whose house was reduced to rubble in last week’s tragic incident, said his wife and three children had left for Mtoni Kijichi - some 2 km away - hours earlier and were unlikely to return before nightfall.

``My wife told me that she would not return before Sunday, and then only upon being assured of normalcy. I am taking care of what few earthly belongings we are left with, or thieves will disappear with everything.

And I too must leave this danger zone now,``explained a panicky Seukwa, as he gathered his belongings ready for departure.

Moments later, the firing started. The subsequent two hours of scheduled deafening explosions, from around 5pm, brought most routine activities in the area to a standstill.

The bomb explosions brought a totally new experience to the majority of the people, residents of a country that has known decades of uninterrupted peace and tranquility.

Speaking to journalists shortly after the detonations, Dar es Salaam Regional Commissioner William Lukuvi said the exercise was a resounding success.

``It was very professionally and successfully executed. There was neither loss of life or limb nor damage to property,`` he noted.

He added that the bombs destroyed were those which remained in the ill-fated armoury and not the ones collected from residential areas after last week`s blasts.

But The Guardian witnessed two people, Mbagala woman Matilda Saidi and Balili Secondary School student Rosemary Daniel, faint shortly after the first explosions. They were immediately whisked away by Red Cross staff for first aid.

Meanwhile, Lukuvi told journalists that a woman injured in last week`s blasts died yesterday, bringing the number of people killed in the tragic incident to 26.

He said Temeke municipal hospital had reported receiving 18 more people hurt in the first blasts, ten of whom were attended to and discharged and the rest were admitted.

SOURCE: Guardian

Wednesday, May 06, 2009

Maafa Mbagala



(Picha kwa Hisani ya Global Publishers. Kwa Picha zaidi Bofya Hapa)

Idadi rasmi ya waliokufa kwa ajali ya mabomu Mbagala ni 23. Lakini watu wanadai waliokufa huenda ikafika zaidi ya mia! Serikali inasema itawalipa fidia watu waliopoteza mali katika ajali huo.

Nina swali. Je, serikali na jeshi wanachukua hatua gani kuhakikisha jambo kama hilo halitokee tena?

Na samahani, lakini watu Bongo wanahitaji kuelimishwa. Mnaona hiyo picha ambayo watu wameshika kipande cha kombora? Si ingelipuka watu zaidi wangekufa. Watu wakimbie siyo wakimbilie! Hizo silaha siyo toy. Na si ajabu kuna watu wameweka vitu wasivyovijua majumbani mwao, tutasikia oh, sijui alitaka kutengeza nini, alivyoigonga ikalipuka.

**************************************************************************
Kutoka Ippmedia.com

Ni vilio tu!

2009-05-05

Na Emmanuel Lengwa na Moshi Lusonzo

Wakati hadi sasa taarifa rasmi juu ya idadi kamili ya watu waliopoteza maisha katika mlipuko wa mabomu uliotokea wiki iliyopita Jijini Dar es Salaam ni 23, baadhi ya wananchi wa maeneo ya Mbagala, wanadai kuwa idadi ya waliokufa ni kubwa zaidi na kwamba miili yao huenda imekwama kwenye tope la mto Kizinga.

Kadhalika madiwani wa kata za Mbagala na Mbagala Kuu wameonyesha wasiwasi wao wakidai kuwa, wana hofu kwamba watu kadhaa wakiwemo watoto ambao walitoweka tangu siku ya tukio hilo la mlipuko, wakawa wamefia kwenye mto huo.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova amesema hadi sasa jumla ya watoto 19 wakazi wa Mbagala, tangu siku ulipotokea mlipuko huo, hawajulikani waliko.

Kufuatia hofu hiyo, jana Baraza la Madiwani la Manispaa ya Temeke liliitisha kikao cha dharura kujadili hali hiyo.

Katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, ambapo ndipo lilipotokea tukio hilo, Bw. Anderson Charles alisema kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo watoto wengi waliozama ndani ya mto Kizinga na kuwa miili yao imekwama kwenye tope la mto huo.

Akasema kasi ya uokoaji inayoendelea kufanywa na wananchi kwa kushirikiana na Polisi ni ndogo, hivyo akaomba Jeshi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ, kufanya operesheni maalum kusaka miili ya watoto hao na kuiopoa mtoni.

Hoja ya Bw. Charles iliungwa mkono na Diwani wa Kata ya Mbagala, Bw. Peter Osoro aliyesema kuwa baada ya milipuko, watoto wengi walikimbia na kuingia mtoni, wakiwa na nia ya kuvuka mto Kizinga kwenda ng\'ambo maeneo ya Yombo.

Kwa mujibu wa diwani huyo, watoto wengi walizama mtoni katika maeneo ya Kingugi na Bugudadi mahali ambapo wengi wao walitaka kuvuka wakidhani maji ya mto ni machache, lakini wakajikuta wakizama kwenye tope na kupoteza maisha.

Aidha Bw. Osoro akasema kuwa hadi sasa kuna familia nyingi zinahaha kutafuta ndugu, jamaa pamoja na watoto wao, na hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kupeleka kikosi cha JWTZ kufanya operesheni maalum.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Bw. Steven Kongwa aliwahakikishia madiwani hao ambao wengi wao walikuwa wakibubujikwa machozi kuwa, juhudi kubwa za kuwasaidia wahanga wa tukio hilo zinaendelea na hivyo akawataka waheshimiwa madiwani wasiwe na huzuni sana.

Kwa upande wake, Meya wa Manispaa ya Temeke, Bw. Jerome Bwanausi, ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya maafa hayo, alisema kamati yake iko imara na wahanga wote wanapewa misaada.

Akasema mazishi ya maiti zote za ajali hiyo yamegharimiwa na kamati ya maafa ya mkoa wa Dares Salaam ambayo iko chini ya Mkuu wa Mkoa, Bw. William Lukuvi.

Madiwani hao walimpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kutembelea majeruhi na wahanga wa tukio hilo.

Aidha waliwashukuru watu wote waliotoa misaada ya hali na mali kusaidia wahanga wa tukio hilo.

Katika hatua nyingine, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema kuwa watoto 19 ambao hawajulikani waliko wanahisiwa kuwa wamekimbilia maeneo mbalimbali na wengine wamehifadhiwa majumbani na wasamaria wema.

Ametoa wito kwa watu wanaowahifadhi watoto wasio wao majumbani au wale wanaojua walipo, watoe taarifa ili juhudi za kuwakutanisha na wazazi wao ziweze kufanyika.

``Kuna watoto wamekimbilia maeneo ya mbali, wapo waliofika hadi Arusha, lakini pia kuna wengine wamehifadhiwa na wasamaria wema, nawaomba wote wajitokeze kutoa taarifa zao ili tuwakutanishe na wazazi wao,`` akasema Kamanda Kova.

Ameonya kuwa miongoni mwa watoto hao wamo watoto wa kike na wanafunzi, hivyo kutotoa taarifa zao inaweza kuleta hisia mbaya baadaye na ikawa shida.

SOURCE: Alasiri

Kwa habari zaidi someni:

http://thecitizen.co.tz/newe.php?id=12244

http://www.thisday.co.tz/News/5685.html

http://www.upi.com/Top_News/2009/04/30/Tanzania-munitions-dump-explodes/UPI-26051241071540/

Monday, May 04, 2009

SERIKALI KULIPA FIDIA WALIOATHIRIKA NA MABOMU YA MBAGALA - PINDA

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali imekubali kubeba mzigo wa kulipa fidia fidia kwa wakazi wa Mbagala jijini Dar es Salaam ambao wamehabiriwa nyumba na mali zao kutokana na mlipuko wa mabomu uliotokea wiki iliyopita.

Akizungumza na wakazi wa Mbagala Kuu, wilayani Temeke alipokwenda kuwapa pole jana jioni (Jumamosi, Mei 2, 2009), Waziri Mkuu aliwataka wanakamati waliopangiwa kufanya kazi ya tathmini ya mali zilizoharibika zikiwemo majumba, mali, misikiti na makanisa na kuikamilisha mapema iwezekenavyo.

Alisema kamati iliyoteuliwa ifanye kazi ya kukagua mali na kufanya tathmini ili Seriklai ione namna na kutoa kufidia ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete ambalo lilitolewa Mei Mosi, 2009.

“Serikali imeshaanza kugharimia gharama za mazishi kwa watu waliokufa katika ajali hii, na itaangalia jinsi ya kuwapa pole wale waliofiwa ili kupunguza makali ya maisha na kuwasaidia waliopata ulemavu kwa matibabu na vifaa,“ alisema Waziri Mkuu.

Alisema kazi iliyo mbele ni kubwa lakini Srikali itajitahidi kuendelea kuwahudumia hadi warejee katika hali zao za awali.

Aliwashukuru watu waliojitolea kwa nafasi mbalimbali ikiwemo wale waliojitosa katima mto Mzinga ili kuopoa maiti za watu waliokufa wakati wakijitahidi kujiokoa kutoka kwenye ajali hiyo.

Waziri Mkuu pia alielezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. William Lukuvi juhudi za kuwakimu wahanga ikiwa ni pamoja na kuwapatia magodoro, vyandarua, mablanketi, vyakula na maji ya kunywa.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,
DAR ES SALAAM..

JUMAPILI, MEI 3, 2009.

Friday, May 01, 2009

Athari za Mabomu Dar

Picha kutoka Global Publishers

Je, walioathirika watapata fidia gani?

***********************************************
Mabomu Dar: Inatisha!

2009-05-01

Na Waandishi Wetu,Jijini

Hali imekuwa ya kutisha kufuatia taarifa zaidi za athari ya janga la kulipukiwa mabomu na makombora ya kivita pale karibu na Kambi ya Jeshi la Wananchi Mbagala baada ya vifo vya watu kuongezeka maradufu.

Hadi sasa, kuna taarifa kuwa waliokufa kutokana na tukio hilo lililozua hofu kubwa Jijini juzi baada ya milipuko kutokea kwenye ghala la silaha pale Mbagala, wameshafikia zaidi ya watu 13.

Taarifa zinadai kuwa idadi hiyo imetokana na kubainika kuwa kuna raia wengine wamefariki na pia askari sita wa JWTZ wanahofiwa kufa kwa kukatwa vipande vipande na mabomu hayo, hivyo idadi ya wafu kuongezeka toka ile ya jana iliyokuwa chini ya watu 10.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, ndiye aliyebainisha hayo wakati akizungumza na Alasiri leo asubuhi.

Aidha, inadaiwa kuwa majumba ya raia zaidi ya 300, Kanisa la Pentekoste, Misikiti miwili ya Mbagala Kuu na Mbagala kwa Mwanakote yamefumuliwa kwa baadhi ya makombora hayo na kusababisha hasara kubwa.

Pia, taarifa zaidi toka kwenye eneo la tukio zinadai kuwa baadhi ya makaburi ya pale Mbagala kwa Mwanakote, nayo yamefumuliwa vibaya, hasa yale yaliyokuwa yameshajengewa.

Pia kambi hiyo hivi sasa imesalia kama gofu, baada ya majengo karibu yote kambini hapo kusambaratishwa kwa mabomu na makombora.

Kuhusiana na raia aliyeongezeka katika wafu, Kamanda Kova amemuelezea kuwa ni mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa chini ya miaka 12 ambaye mwili wake uliokotwa katika Mto Kizinga.

Naye Brigedia Jenerali Meela wa JWTZ, amekaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa wanajeshi wao sita wanahofiwa kufariki dunia katika mlipuko huo na kwamba hadi sasa bado hawajaonekana tangu baada ya tukio hilo.

Hata hivyo, kuna taarifa kuwa vipande vya miili ya baadhi ya askari vimeshaonekana na kuhisiwa kuwa ni pamoja na hao sita.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi amesema Serikali imeamua kugharimia gharama zote za mazishi ya watu waliopoteza maisha katika tukio hilo.

Akasema leo wanawazika watu wanne, ambao ni wakazi wa Mbagala, kazi ambayo itafanyika leo huko huko Mbagala.

Akasema ndugu wa marehemu hao wameambiwa kusema bajeti ya mazishi ya wapendwa wao ili Serikali itoe fedha hizo.

Akadai kuwa jamaa za watu wanne wanaozikwa leo wameomba shilingi milioni moja kwa kila marehemu mmoja na Serikali imekubali kuwapatia.

``Hadi hivi sasa tunavyoongea ndugu wa marehemu hao wapo ofisini kwa Meya kupewa fedha hizo za kugharimia mazishi,`` akasema Bw. Lukuvi.

Akasema wapo watu wawili ambao walizikwa jana na familia zao tayari zimesema kuwa zimetumia sh. Milioni 2.5 kila moja na Serikali itazirejesha.

``Wenzetu waliozikwa jana walikuwa ni waislamu, kwa imani yao wasingeweza kusubiri hadi fedha zitolewe ndio wazike, hata hivyo wameshasema gharama walizotumia kwa mazishi kuwa ni Mil. 2.5 kila familia na Serikali itazirejesha,`` akasema Bw. Lukuvi.

Aidha akasema ipo miili ya watu wawili ambayo inatarajiwa kusafirishwa kwenda mikoani, mmoja ukisafirishwa kwenda Singida na nyingine mwingine Musoma mkoani Mara.

Akasema jamaa wa marehemu hao pia wameambiwa watamke bajeti ya mazishi na kufika katika Ofisi ya Meya Adam Kimbisa, ili kupewa fedha za mazishi.

Akasema kwa taarifa alizonazo maiti hizo za kwenda mikoani zitasafirshwa kesho ambapo Serikali imeahidi kuwa bega kwa bega na jamaa wa marehemu hao.
Tukio hilo lilitokea juzi na jana, Rais Jakaya Kikwete aliwatembea wahanga katika pale Mbagala na pia katika Hospitali ya Temeke.

SOURCE: Alasiri

Thursday, April 30, 2009

Statement from U.S. Embassy on Bomb Explosions in Dar

From: DAR CA-ACS (Dar Es Salaam ) drsacs@state.gov
Subject: From US Embassy on explosions in Dar es Salaam (28 April 2009)
Date: Wednesday, April 29, 2009, 5:30 AM

Before noon today (28 April 2009), bombs stored at a munitions storagefacility in Mbagala, Dar es Salaam, accidently exploded. We have beentold that the situation is not yet contained and there could be furtherexplosions.We have been told that the authorities are evacuating the downtown area.The British High Commission, located downtown, has closed. The UnitedStates Government Center for Disease Control offices downtown are alsoclosing. The Embassy compound in Msasani remains open.

We have varying reports as to what extent flight operations at the airport may beaffected.American citizens are advised to avoid downtown and the area aroundMbagala. Americans should follow news reports closely. We will updateas we get more information.Updated information on travel and security in Tanzania may be obtained from the Department of State by calling 1-888-407-4747 toll free in theUnited States and Canada, or for callers outside the United States andCanada, a regular toll line at 1-202-501-4444. For further informationplease consult the Country Specific Information for Tanzania, the East Africa Travel Alert, and the Worldwide Caution Travel Alert, which areavailable on the Bureau of Consular Affairs Internet website athttp://travel.state.gov <http://travel.state.gov/> .

The Consular Section of the U.S. Embassy in Tanzania can be contacted bytelephone [255](22) 266-8001 x 4122 and fax [255](22) 266-8238. You may also contact the U.S. Embassy in Tanzania via email atdrsacs@state.gov.After hours American Citizen emergencies should call [255](22) 266-8001.

Wednesday, April 29, 2009

Ghala La Silaha Lalipuka Mbagala, Dar es Salaam

BBC wanasema watu kadhaa wamekufa!

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/8024656.stm


Kutoka MICHUZI BLOG:

BREKING NYUZZZZZZ: GHALA LA SILAHA LALIPUKA MBAGALA, DAR
GHALA LA SILAHA LA JESHI LIMELIPUKA NA KUSHIKA MOTO KWENYE KAMBI YA JESHI ILIYOKO MBAGALA KIZUIANI NA KUSABABISHA MILIPUKO MIKUBWA YA MABOMU NA KULETA KIZAAZAA JIJI ZIMA.

GLOBU YA JAMII ILIYO KATIKA ENEO LA TUKIO IMESHUHUDIA ASKARI WA JESHI LA ULINZIM POLISI NA ZIMAMOTO WAKIWA WAMEJAZANA NJIA PANDA KUELEKEA KAMBINI HUKO AMBAKO MOSHI MZITO NA MILIPUKO IMEKUWA IKISIKIKA TOKA ASUBUHI.

KUNA HABARI KWAMBA BAADHI YA MABOMU YANARUKA MAZIMA MAZIMA NA KUTUA KILOMETA KADHAA TOKA MBAGALA NA KULIPUKA. KATIKATI YA JIJI TAYARI WATU WAMETANGAZIWA WASHUKE MAGHOROFANI.

HABARI ZINASEMA KWAMBA MOTO HUO WA AINA YAKE UNAWEZA KUZIMIKA KWA UTAALAMU WA HALI YA JUU ILA USALAMA DHIDI YA MLIPUKO WA MABOMU NI MDOGO. WAKAZI WENGI WA MBAGALA WAMESHAONOLEWA SEHEMU HIYO WAKATI JUHUDI ZA KUTHIBITI MOTO NA MILIPUKO IKENDELEA.

GLOBU YA JAMII INAENDELEA KUWA ENEO LA TUKIO NA INAAHIDI PICHA NA HABARI KEDEKEDE BAADAYE KIDOOOOO....