PORT-AU-PRINCE, Haiti (AP) - Officials say a fire swept through a Haitian children's home run by a Pennsylvania-based religious nonprofit group, killing 15 children. A child-care worker at the home told The Associated Press that the fire began around 9 p.m. Thursday and firefighters took about 90 minutes to arrive. She said the orphanage had been using candles for light due to problems with its generator. Late Friday afternoon, police raided another home also run by the Church of Bible Understanding and took away several dozen children in a bus over protests from employees. The Associated Press has reported on a long-standing series of problems at children's homes run by the group.
Imeelezwa ili kuwawezesha watoto yatima ambao walizaliwa wakiwa na Virusi vya UKIMWI ambao wanapatikana katika Kituo cha Matumaini kilichopo Manispaa ya Dodoma, Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja na kuwasaidia watoto hao ambao wanaishi katika kituo hicho ili kuwawezesha kuishi mazingira bora pamoja na kupata huduma za bora za afya.
Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Kituo cha Matumaini, Sister Maria Rosaria Gargiulo, alisema kituo hicho chenye watoto 151 wakati kimeanzishwa kilikuwa kikipokea msaada kutoka Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na TACAIDS lakini kwa sasa msaada umesimama na hivyo kuwafanya kwa sasa kuishi katika mazingira magumu.
Sister Maria alisema kuwa hali ya maisha kwa watoto hao ni ngumu na hivyo kuwataka Watanzania kuwakumbuka watoto hao ambao walizaliwa wakiwa na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ili waweze kupata huduma bora ambazo zitawawezesha kuishi katika mazingira bora, kupata elimu na kupata dawa ambazo zitaimarisha afya zao.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu (kushoto) na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni wakiongozwa na Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo mara baada ya kuwasili katika kituo hicho kilichopo katika manispaa ya Dodoma karibu na Hoteli ya Mtakatifu Gasper.(Imeandaliwa na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
“Hapa wanakuja tu watu wa hapa Dodoma mara nyingi siku za Jumamosi na Jumapili ila tofauti na hivyo hatuna msaada mwingine, watoto hawa wanahitaji faraja kutoka kwa watu wengine inapendeza kuona watu wanakuja kuwaona na kuwasaidia nao wanafurahi,
“Ukiangalia hali ya kimaisha inazidi kupanda tunafanya jitihada kujisimamia sisi wenyewe lakini tunashindwa bado tunahitaji msaada sisi tumejitoa kuwasaidia hawa watoto hata hatulipwi lakini tunahitaji sana msaada wa Watanzania,” alisema Sister Maria.
Nae Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999 na Mtalaam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), Hoyce Temu ambaye alifika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa msaada ambapo alituma ujumbe kwa Watanzania wengine ambao wamekuwa hawana utaratibu wa kutoa misaada kwa wahitaji na kuwataka kubadilika.
Bi. Temu alisema kuwa mazingira ambayo wanaishi watoto hao ni magumu na hawana wazazi kutokana na wazazi wao kuwa wamefariki hivyo kuwataka Watanzania kujitoa kwa pamoja na kuwasaidia watoto hao kwa chochote ambacho kinaweza kuwasaidia kuimarisha maisha yao ili waishi mazingira bora.
“Jamani kama watu wanasema tunapoishi kuna shida basi hakuna, shida zipo huku, ukiangalia kuna watoto wengine wana wiki moja na hawana wazazi wametupwa wanahitaji kupata misaada ya Watanzania,
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akimsikiliza kwa makini mmoja wa watoto wanaoishi kituoni hapo aliyewahi kumuona mara ya kwanza alipofika kituoni hapo.
“Nitoe rai kwa Watanzania wenzangu kama una pesa au nguo au chochote ambacho kinaweza kuwasaidia tutoe kwa watoto hawa mazingira yao ni magumu sana, hawana makosa hawa hata mbele za Mungu naomba tuwasaidie,” alisema Bi. Temu.
Kwa yoyote atakayeguswa na angependa kufika kituoni hapo kusaidia anaweza kupiga simu kwa Msimamizi wa Kituo cha Matumaini, Sister Maria Rosaria Gargiulo +255754272707
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu (kulia) na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni wakiwa wamewabeba watoto yatima wanaoishi kituoni hapo.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akifurahia jambo mara tu baada ya kuwasili katika kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma kinacholea watoto yatima ambao 98% wanaishi na Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akiwa kwenye wodi ya watoto wachanga ambao ni yatima wanaoishi waliozaliwa na maambuki ya Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni pamoja na Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo (kulia) walipotembelea wodi ya watoto wachanga waliozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akifurahi na watoto wachanga ambao ni yatima waliozaliwa na maaumbikizi ya Virusi vya Ukimwi waliolazwa katika wodi ya watoto kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma.
Wewe acheka afurahi kumuona Aunty....Jiji jiji jiji.....jamani acheka....Ni maneno ya Mlimbwende Hoyce Temu akicheza na mmoja wa watoto hao katika wodi hiyo.
Meneja Mwendeshaji wa mtandao wa Habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige akimbeleza mmoja wa watoto waliozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wanaolelewa katika kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma.
Eweee Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, tunakuomba wajaalie Malaika wako hawa afya njema, maisha marefu, wape uponyaji viumbe hawa wasiokuwa na hatia, Amen!
Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo akimsimulia Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu historia ya mtoto Richard aliyeshikwa mikono na mlimbwende huyo.
Mmoja wa Masista wanaohudumia watoto hao Sista Mary Shayo akifurahi jambo wodini mbele ya kamera ya Modewjiblog.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akicheza kwaya ya wimbo maalum aliokuwa akiimbiwa na bendi ya kijiji cha Matumaini kabla ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali.
Hoyce Temu akigawa zawadi kwa watoto wanaolelewa kwenye kijiji cha Matumaini mkoani Dodoma.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi 'Pampers' kwa mmoja wafanyakazi wanaohudumia (jina lake halikuweza kupatikana) watoto kituoni hapo.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi mfuko wa sukari.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi makopo ya maziwa. (Picha zaidi ingia hapa)
Aida Nakawala (25) mkazi wa kijiji cha Chiwanda, Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, ambaye alijifungua watoto wanne kwa mkupuo (Quadruplets) usiku wa kuamkia Mwaka mpya wa 2014 katika Hospitali ya Wazazi ya META jijini Mbeya.
Misaada toka kwa Bi Gladness Sariah wa Uingereza, Dar es salaam kwaNorah SilverBoutique
Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu akiwakilisha msaada toka kwa familia ya mama Masawe wa DSM kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha NURU kilichopo Uyole, mkoani Mbeya.
----------------------- Kituo cha Mtandao wa kijamii cha Mbeya Yetu (www.mbeyayetu.blogspot.com) kimepokea Misaada mbalimbali kutoka kwa wasamaria wema kwa ajili ya Kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Nuru kilichopo Uyole Jijini Mbeya na Aida Nakawala (25) mkazi wa kijiji cha Chiwanda, Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, ambaye alijifungua watoto wanne kwa mkupuo (Quadruplets) usiku wa kuamkia Mwaka mpya wa 2014 katika Hospitali ya Wazazi ya META jijini Mbeya.
Msaada wa kwanza ulipokelewa hivi karibuni wenye thamani ya shilingi Laki Moja kutoka Familia ya Masawe wa Dar es salaam kwa ajili ya kituo cha Nuru ambapo Mbeya yetu iliuwasilisha kama ulivyo.
Mbali na msaada huo pia Mtandao huu ukishirikiana na mtandao wa kijamii wenye makao yake makuu Jijini Dar es salaam wa www.issamichuzi.blogspot.com ulipokea kutoka kwa Msamaria mwema wa Uingereza, Bi Gladness Sariah, ambaye alitoa maboksi mawili yenye nguo na vitu kadhaa vya watoto.
Aidha katika kuonesha wengi wameguswa na tukio la Mwanamke huyo kujifungua watoto wanne ambao wanaendelea vizuri, pia Msamaria mwema mwingine aliyejulikana kwa jina la Dada Norah SilverBoutique toka Dar es salaam naye ametoa Maziwa Lactogen makopo 24 pamoja na nguo ambavyo vimewasili salama katika ofisi ya Mbeya Yetu.
Shukrani kwa Wazee wa Kazi, Serengeti Freight Forwarders ya huko Uingereza na ofisi za Michuzi Media Group (MMG) kuwezesha kufika kwa mizigo hii Mbeya.
Kutokana na kupokelewa kwa mizigo hiyo ambapo kituo cha Nuru kilikabidhiwa Katoni Mbili za Sukari, Sabuni na Biskuti pia Tunatarajia kuanza safari ya kwenda huko Chiwanda Wilaya ya Momba Kilomita zaidi ya 260 toka Mbeya mjini kufikisha misaada ya Mama wa mapacha wanne.
Hivyo ni wito wetu kwenu kuendelea kutuombea na kutuunga mkono katika safari hiyo ili tuweze kuifikisha salama mizigo hiyo ikiwa ni pamoja na kuangalia maendeleo ya Watoto hao ambapo watakuwa wameshatimiza mwezi mmoja na siku 24.
Tunawashukuru sana tena sana wote mliojitolea na Mungu awabariki sana.
Precision Air Network Planning and Strategy Director - Patrick Ndekana (r) together with Network Planning Staff handover material support to Mama Winifreda- Director of the Chamanzi Orphanage in Mbagala - Dar es salaam over the weekend. The team used their monthly birthday allocation money to buy the donated materials.
Mnakumbuka ile kesi iliyotokea mwezi Oktoba ya wafaransa kujaribu kutorosha watoto zaidi ya 100 kutoka Chad. Walidai kuwa ni yatima kutoka Sudan, kumbe walikuwa wametekwa kutoka majumbani mwao hapo Chad, wengine walikuwa na familia zao.
Hao wafaransa walihukumiwa kukaa gerezani Chad miaka minane na kufanyishwa kazi ngumu. Sasa serikali ya Chad imewarudisha Ufaransa kwa ombi la serikali la huko.
N'DJAMENA, Chad - Six French aid workers sentenced to eight years' forced labor in Chad for trying to kidnap 103 children left for France on Friday, boarding a plane in handcuffs as security officers looked on.
The members of Zoe's Ark were transported to an airstrip in a prison van before taking off. On Thursday, France asked Chad to hand over the six, who were convicted and sentenced Wednesday. Repatriation requests are allowed under a 1976 judicial accord between the two countries.
France does not have forced labor for convicts and there are hopes that if the six are returned, the French justice system will commute or reduce their sentences. A Zoe's Ark spokesman said he was reserving reaction until the aid workers actually land back in France.
"Since Wednesday night, they were supposedly coming home at any moment," Christophe Letien told The Associated Press by phone. "It changes from one minute to the next." "I will react once they are aboard the plane, or even after they land here."
Without confirming that the aid workers would be returned Friday, the office of President Nicolas Sarkozy said he spoke Thursday night by phone with Chadian President Idriss Deby about preparations for their transfer.
In October, Chadian authorities stopped the aid group's convoy with the children, whom the charity was planning to fly to France. The six insisted they were driven by compassion to help orphans in Darfur, which borders Chad. Later investigations showed most of the children had at least one parent or close adult relative.
The case has embarrassed France and sparked protests in Chad, a former French colony. Aid workers say their already difficult job along Darfur's border has been complicated by the suspicion some Chadians now have toward all foreigners professing to offer help. Days after the Zoe's Ark workers were arrested, the Republic of Congo announced it was suspending all international adoptions because of the events in Chad.
France's role in the region has already come under scrutiny in recent months as the European Union plans to send a military mission to Chad to protect refugees fleeing violence in neighboring Sudan.
The deployment of the approximately 4,300-member force, drawn largely from France, has already been delayed because of the lack of necessary equipment. Last month, a Chadian rebel group declared a "state of war" against French and other foreign armies — an apparent warning to the EU force. ___
Kuna kundi la wazungu wamekamatwa nchini Chad wakijaribu kutorosha watoto zaidi ya mia moja. WaChad wanadai kuwa hao watoto ni raia wa Chad. Hao wazungu wanasema ni yatima kutoka Sudan na walikuwa wanapelekwa Ufaransa kukaa na familia kadhaa kule.
Kuna kundi la ufaransa inaitwa Zoe's Ark, ndo ilikuwa imeleta ndege ya kusafirisha hao watoto.
Sasa hao wazungu wanaweza kufungwa kwenye gereza la Chad kwa miaka 20 na kufanyishwa kazi ngumu. Pia wameshika raia wawili wa Chad.
Baadhi ya hao watoto walidai kuwa walitekwa na hao wazungu. Walipewa pipi na biskuti na walijikuta wanatoroshwa.
Inasemekana familia kadhaa huko Ufaransa walilipa kati ya Euro 2,800 hadi 6,000 kumpata mtoto yatima kutoka Sudan.
I worked for Tanzania's Daily News for 11 years leaving as a Senior Reporter. I love acting, films, short story writing and cooking. I blog in English and Swahili. I am a member of the Screen Actors Guild (SAG) and AFTRA.
You can contact me at chemiche3@yahoo.com.