Showing posts with label Miss Utalii. Show all posts
Showing posts with label Miss Utalii. Show all posts

Friday, June 29, 2012

Miss Utalii Blog



Tunawatambulisha Kwenu Blog maalum ya Miss Utalii Tanzania/Miss tourism Organisation.


Miss Utalii Tanzania, tofauti na mashndano mengine ya urembo, ni zaidi ya shindano la urembo, kwani linalenga katika kutangaza na kuhamasisha Utalii,Utamaduni, Mianya ya Uwekezaji,Elimu,Afya ya Jamii,Utalii wa ndani,Utalii wa kitamaduni,Utalii wa Michezo na Utalii wa Mikitano Kitaifa na kimataifa. Shindano hili pia linahamasisha vita dhidi ya Umasikini,Iharibifu wa mazingira,uwindaji haramu,Uvuvi Haramu,Ujinga,Maradhi, Tamaduni kongwe na Potofu. Miss Utalii Tanzania pamoja na uchanga wake, tangu kuanzishwa kwake mwaka 2005, ni shindano lenye mafanikio makubwa kuliko shindano jingine lolote nchini kitaifa na kimataifa kwani pamoja na kuipa heshima Tanzania ya kuwa wenyeji wa shindano la Dunia la Miss Tourism World 2006, shindano hili ndilo lililo andika historia ya Tanzania kutwaa taji la kwanza la Dunia kabla na baada ya uhuru, pale tulipo twaa taji la Miss Tourism World 2006, pia shindano hili ndilo pekee nchini linashikilia rekodi ya kutwaa mataji ya dunia katika kila shindano tulilo shiriki,tumetwaa mataji 6 ya dunia tangu 2005. Kutokana na mafanikio haya , Tumepewa heshima ya kuaandaa shindano la Dunia la Miss Umoja wa Mataifa mwaka 2013 hapa Tanzania. Ni shindano pekee nchini ambalo washiriki wake hawavai mavazi ya kuogelea, bali mavazi ya heshima yasiyo mdhalilisha mvaaji wala mtazamaji na yaliyo buniwa na kushonwa kwa malighafi za tanzania tu.

Link yetu ni : http://www.misstourismorganisation.blogspot.com/

Facebook Page: https://www.facebook.com/MissUtaliiTanzania

E-Mail: missutaliitanzania@gmail.com

Asanteni sana.
Miss Tourism Organisation Tanzania.

Saturday, August 30, 2008

Mgombea Miss Utalii aanguka Ziarani

Nimeona hizi picha kwa Michuzi Jr. (Jiachie Blog). Huyo mshiriki wa Miss Utalii alikuwa kwenye ziara. Ghafla alianguka. Wanasema kuwa harufu ya dawa wanazotumia kiwandani zilimwangusha. Inawezekana. Ila navyofahamu hizi pageant za urembo, mara nyingi mtu akianguka hivyo ni shauri ya njaa. Hao wagombea wanakula kidogo sana au hawali kabisa kusudi wakonde au wabakie wembamba. Wakati mwingine wanapata dehydration (ukosefu wa maji mwilini) na utapiamlo. Inatokea sana kwenye pageant za Marekani. Lakini kwa Bongo huenda ana malaria. Pole sana Sara Salum.
Mshiriki wa miss utalii 2008 Sara Salum kutoka Dodoma akipewa sapoti ya kutembea na baadhi ya wasimamizi wa walimbwende hao waliofika kushuhudia kazi za uchapaji ndani ya kiwanda cha Image Printer,kilichopo Nyerere road jijini dar. Moja ya washiriki wa miss Utalii Tanzania 2008, Sara Salum 25, Dodoma alidondoka katika ziara ya kutembelea kiwanda cha Image Printer leo mchana baada ya kuzidiwa na kemikali zinazotumika katika masuala ya uchapaji kiwandani hapo. (Picha kutoka Michuzi Jr. Blog)