Showing posts with label Nursing Home. Show all posts
Showing posts with label Nursing Home. Show all posts

Saturday, September 10, 2016

Mkuu wa Mkoa Mwanza Akabidhi Vyakyula Kwa Niaba ya Rais Magufuli Kwenye Kituo cha Bukumbi

To kmwantepele Dotto Mwaibale Mzee Ahmad Michuzi Cathbert Kajuna and 232 more... Message body
Katika kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj siku ya Jumatatu Septemba 12, 2016, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, ametoa msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi laki saba na elfu themanini (780,000), kwa ajili ya Kituo cha kulelea Wazee na Walemavu wasiojiweza cha Bukumbi Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Akikabidhi msaada huo jana, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, aliuhimiza uongozi wa kituo hicho kusimamia vyema ugawaji wa vyakula hivyo li kuwafikia walengwa, ikizingatiwa kwamba kumekuwa kukiibuka malalamiko kutoka kwa wazee wanaoishi katika kituo hicho kwamba misaada ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali imekuwa haiwafikii yote.

Hata hivyo Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.

Wazee wanaoishi kituoni hapo waliishukuru serikali kwa msaada huo ambapo walisema wanaendelea kumuombea Rais Magufuli na Serikali yake ili iendelee kuboresha kituo hicho ikiweo kuwekewa uzio ili kuondokana na hofu ya kiusalama waliyonayo kwani wakati mwingine wamekuwa wakiibiwa mali zao ikiwemo kuku ambazo wamekuwa wakizifuga.

Vyakula vilitolewa na Mhe.Rais Magufuli ni, mchele gunia sita (kila gunia kilo 50), mafuta ya kupikia madumu manne (kila dumu lita 20) pamoja na mbuzi wawili.
Baadhi ya wazee wanaoishi kwenye Kituo cha Bukumbi, wakifurahia mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza baada ya Rais Magufuli kuwapatia msaada wa vyakula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj, itakayofanyika kesho kutwa jumatatu.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (mwenye kofia), akimsikiliza mmoja wa wazee katika Kituo cha Wazee Bukumbi.
Mmoja wa akina mama kwenye Kituo cha Bukumbi akiishukuru Serikali kwa msaada wa chakula ilioutoa kituoni hapo
Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe.Juma Sweda (kulia), akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa chakula uliotolewa na Mhe.Rais Magufuli katika Kituo cha Wazee Bukumbi wilayani humo. Alisema Serikali inawajali Wazee wanaoishi katika kituo hicho na kwamba ina upendo kwao ndiyo maana inaendelea kuwahudumia.
Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhiri mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.
Vyakula vilivyotolewa na Mhe.Rais Magufuli kwa ajili ya Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Huyu mbuzi, tehe tehe tehe!!
Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo wa BMG

Thursday, February 23, 2012

Bibi Arusi Ana Miaka 100, Bwana Arusi Ana Miaka 87! Kweli Kabisa!

Duh! Naona Cougar wa miaka 100 kaolewa leo na kijana  mwenye miaka 87 huko Kentucky.  Wanaarusi wanaishi katika nyumba ya wazee na walikutana huko.   Ni kweli mapenzi yakinoga unajisikia kijana.  Bibi Dana Jackson (100) anasema kuwa anajiona kama ana miaka 50 tu! Nawatakia maisha mema ya ndoa! 

Congratulations Mr. & Mrs. Strauss!

***************************************************

(Dana Jackson & Bill Strauss)
Woman Weds on Her 100th Birthday


By Bridal Guide

On February 6th, Dana Jackson celebrated a century of life with about 100 of her nearest and dearest at the Rosewood Health Care Center in Kentucky. An ice cream cake in her honor was frosted with the special message, "Congratulations, you are never too old." But this wasn't your average birthday party, not even for a centenarian: Jackson decided to mark the momentous occasion by marrying boyfriend Bill Stauss, 87.

Stauss never imagined that he would ever wed again, since his previous marriage lasted 55 years. However, Jackson was the exception: "I found one that's just as nice as can be. Treats me good. Like a human being should be treated. It's rare to find a girl like that."

"I feel 50," Jackson told BG Daily News. "I don't feel 100."

This was Jackson's third trip down the aisle, but the first time she wore an engagement ring and traditional gown. Her first wedding took place when she was only 15 years old. She marveled at how much has changed since then: "Gettin' married wasn't a big thing back when I was young. It wasn't no big thing...it was just simple, you know? Just simple...we wore clothes and maybe a bouquet cut out of the yard. It's not what you got, it's what you make out of a marriage," she said.

Jackson's message is timeless, and in the AARP video below, her happiness is infectious, just as with any other bride. But marrying at 100 does have its challenges: The couple sipped grape juice in lieu of cocktails and Stauss had trouble seeing his wife walk down the aisle. The moment didn't disappoint-the husband thought his wife looked "beautiful" when he finally got a closer look.

Kuona Video ya Arusi BOFYA HAPA:

Monday, January 05, 2009

Mtu Mzee Kuliko Wote duniani sasa ni Mmarekani Mweusi

Mwezi November mwaka jana, mtu mzee kuliko wote, Bibi Edna Parker, alifariki huko Indiana, USA akiwa na miaka 115!

Leo wataalam wametangaza kuwa Bibi Gertude Baines (pichani), mwenye miaka 114 ni mtu mzee kuliko wote duniani. Bibi Baines, ni mtoto wa watumwa. Alizaliwa mwaka 1894 huko Atlanta, Georgia.

Kwa sasa anakaa Los Angeles,California kwenye nyumba ya wazee.

Ni baraka kuweza kuishi muda wote huo tena katika karne tatu! 1800's, 1900's, 2000's. Ila wakati mwingine nafikiria kuna wakati utakuwa mpweke hasa ukifikiria watu wote uliokuwa unawafahamu wamekwisha kufa.

Hivi huko Afrika hakuna watu wenye umri mkubwa hivyo? Maana naona hao wataalam wanachunguza nchi zilizoendelea na hata siku moja sijasikia walienda Afrika kuchunguza.

Namtakia Bibi Baines, maisha marefu zaidi. Mungu amlinde.

Na kitu kingine, hapa Marekani kuna usemi "Black Don't Crack!" yaani ngozi nyeusi haivunjiki. Wana maana kuwa watu weusi hawazeeki kama wazungu ambao ngozi yao inasinyaa vibaya.

Wadau, kama mnafahamu watu wenye umri mkubwa zaidi ya miaka 100 hebu tutoe ripoti kwa hao wanaojiita watalaam wa umri waingie kwenye record books.

Najua watu wanatania, au kuna mzee fulani asubuhi tunamtoa na kumanika juani. Je, ana miaka mingapi?

GOD BLESS YOU MS. BAINES!

************************************************************************

LOS ANGELES, California (CNN) -- Gertrude Baines, ma 114-year-old California resident, will likely be crowned the world's oldest woman, according to the organization that keeps track of such honors.

Gertrude Baines told CNN two years ago that she has taken good care of herself, "the way (God) wanted me to."

The previous oldest woman was Maria de Jesus, who died this week in Portugal at age 115, Guinness World Records said.

Baines -- born to former slaves in a small town south of Atlanta, Georgia, in 1894 -- now lives in a Los Angeles nursing home.

Baines appeared cheerful and talkative when the Los Angeles Times interviewed her in November as she cast her vote for Barack Obama for president, whom she said she supported because "he's for the colored people."

"I'm glad we're getting a colored man in there," she said.

Baines apparently prefers using the older term for her race. She was well into her 70s when "African-American" became the common reference in the United States. Watch Baines speak to CNN
She told the Times she spends most of her time "doing nothing but eating and sleeping."
When CNN interviewed Baines two years ago, she was asked to explain why she thought she has lived so long.

"God. Ask him. I took good care of myself, the way he wanted me to," Baines said.
Her only child, a daughter, died of typhoid fever at age 18.

Much of her long life was lived in Ohio, where she worked as a "house mom" at a state university. She eventually divorced and traveled to Los Angeles, where she retired.
Baines will not officially be given the title until after Guinness World Records completes an investigation, the organization said.

"Maria was crowned the world's Oldest Living Woman by Guinness World Records on 28 December upon the death of Edna Parker," the group said.
Parker -- an American -- was 115 years, 220 days old when she died November 26, 2008, in an Indiana nursing home, it said.

********************************************

KAMA MNA HABARI ZA WAZEE WENYE UMRI MKUBWA TAFADHALI WASILIANA NA GUINESS BOOK OF RECORDS:

http://www.guinnessworldrecords.com/member/how_to_become_a_record_breaker.aspx