Showing posts with label Arusi. Show all posts
Showing posts with label Arusi. Show all posts

Sunday, November 30, 2014

Wafunga Ndoa Uchi

Haya jamani, kwa nini mnapoteza kununua nguo za harusi wakati mnaweza kusevu pesa kwa kufunga mkiwa uchi?  Hao wazungu walisema hela ya nguo watatumia kwa ajili ya kulipa mortgage ya nyumba! Ingekuwa safi kama wageni nao wangekuwa uchi.  Kutoka https://www.facebook.com/pages/Ijebu-News-Xtra/121224847988714?fref=photo


Saturday, November 02, 2013

Fesheni Mpya ya Picha za WanaHarusi Bongo

Wadau, naomba maoni yenu kuhusu hii picha. Mimi nasema Tarzan angefurahi sana kuona wanaharisu kwenye miti! Bibi harusi alipandaje na hiyo gauni na heels?

Thursday, July 25, 2013

Vazi la Nusu Uchi Lazuia Ndoa Kufungwa Kanisani St. Peter Dar!

Binafsi sioni shida ya kuvaa nguo ya harusi ya mabega wazi, ndo fesheni sehemu nyingi. Mbona, tunavaa khanga na vitenge na tunakuwa mabega wazi? Lakini kama umeambiwa mapema kuwa nguo hiyo haifai kanisani basi msikilize Padri au tafuta Kanisa lingine!

***************************************
KUTOKA  GAZETI LA HABARI LEO

VAZI LA NUSU UCHI LAZUIA NDOA KUFUNGWA JIJINI DAR....PADRI AGEUKA MBOGO NA KUWATIMUA WAPAMBE


KIVAZI cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa  Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri.

*“Ninatoa dakika 10 kwa aliyeingia na mavazi ambayo hayatakiwi kanisani humu kutoka mara moja akavae vizuri, la sivyo ndoa yao haitafungwa,”* alisema Padri Haule wa Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

Awali vurugu hizo zilizotokea Jumamosi iliyopita, zilianzia nje, wakati Katekista wa Parokia hiyo, Yohane Maboko, alipotangazia wanandoa na ndugu zao waliokuwa mabega wazi au kuvaa nguo fupi, kutafuta nguo za kujifunika au wasiingie kabisa kanisani.

Maharusi walikubali kutekeleza ombi hilo, wakavishwa vitambaa mabegani vya rangi tofauti na gauni jeupe la harusi, wakaruhusiwa kuingia kanisani, tayari kufunga pingu zao za maisha.


Aliyegoma kutoka na nguo yake ya nusu uchi

Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa maharusi hao ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alipotaka kulazimisha kuingia na kivazi chake cha mabega wazi, alizuiwa na Katekista Maboko. Katekista huyo alimfuata mwanamke huyo ili kumrudisha akavae vizuri, lakini aliibua zogo na kulazimisha kuingia na
vazi hilo.

Zogo hilo lilipoendelea, wanandugu waliingilia kati, wakitetea vazi hilo ambapo mmoja wa wanandugu, alimvua miwani Katekista Maboko na kuipiga chini ikavunjika huku yeye na wenzake wakimtolea maneno makali ya kumtaka asimzuie ndugu yao kuingia kanisani.

Wakati ndugu hao wakimdhibiti Katekista Maboko, mwanamke huyo alitumia mwanya huo na kupenya hadi ndani ya Kanisa, ambamo Padri Haule, alikuwa akijiandaa kuanza ibada.

*Baada ya Padri Haule kupata taarifa, alitangaza kuwa ndoa ya maharusi wa msichana huyo, haitafungwa hadi awe ametoka. *

Licha ya Paroko kutangaza hivyo, bado ukaidi uliendelea jambo lililomfanya Katekista Maboko kumfuata tena dada huyo na kumwamuru atoke nje, ambapo aliendelea kupinga na baadaye akatekeleza amri hiyo ya Paroko.

Baada ya hapo shughuli za kufungisha ndoa ziliendelea kwa amani na utulivu hadi mwisho maharusi wakatoka kwenda kuendelea na mambo mengine.

Akizungumza na mwandishi wetu, Katekista Maboko alisema waumini hao walikiuka maadili ambayo Kanisa lina wajibu wa kulinda na kuyasimamia ili  waumini wake wayafuate.

Alisema miwani yake iliyovunjwa ilikuwa na thamani ya Sh 90,000 na baada ya  ibada hiyo, aliyetenda kosa hilo alimwendea na kumwomba radhi na kulipa Sh 50,000 na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki wakati wowote.

Maboko alisema uvaaji wa mavazi yasiyotakiwa kanisani hapo, umekuwa ukipigiwa kelele mara kwa mara, na hata katika mafundisho ya ndoa huambiwa lakini ukaidi unaendelea.

*“Maharusi wakati wa mafundisho ya ndoa tunawaambia kuhusu mavazi yao na hata ya ndugu zao watakaowasindikiza kanisani, kuwa wavae kistaarabu lakini  hawasikii,”* alisema Katekista Maboko.

Makanisa mengi siku hizi yamekuwa yakipiga marufuku uvaaji wa nguo fupi na  zinazoacha mabega wazi kwa wasichana na wanawake, wakati wa ibada za kawaida na za ndoa.

Habari Leo

Hii fesheni inapendwa na vijana wengi

Saturday, September 08, 2012

Wazazi Wangu Washerekea Miaka Hamsini ya Ndoa

Wadau, napenda kuwafahamisha kuwa wazazi wangu, Dr. Aleck na Mrs. Rita Che-Mponda wamesherekea miaka hamsini ya ndoa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam. Ndoa yao ilibarikiwa katka kanisa la Anglikana St. Albans, Dar es Salaam. Walifunga ndoa mwaka 1961, baba akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Howard. Mama alikuwa amemaliza masomo yake ya unesi.

Mungu azidi kuwabariki.

Dr. & Mrs. Aleck Che-Mponda 
Misa ya Kuwabarika St. Albsans




Wazee wakiwa na baadhi ya ndugu


Tuesday, July 10, 2012

Mbunge Frank ndiye wa Kwanza Kufunga Ndoa ya Kishoga!

Mbunge wa Massachusetts, Barney Frank amekuwa mbunge wa kwanza kufunga ndoa ya kishoga Marekani. Frank, mbunge wetu mpendwa wa miaka mingi hakuficha ushoga wake.  Aliwahi kuwa na skandali ya kutembea na malaya wa kiume na pia kutembea ma kijana wa kiume ambaye alikuwa intern Bungeni.
Mbunge wa Massachusetts Barney Frank (kulia) na mke wake Jim Ready

 
Congressman Barney Frank (D-MA) (72) married  longtime partner, Jim Ready (43) this past weekend . The couple got hitched Saturday at the Newton Marriott in a ceremony officiated by Governor Deval Patrick , and attended by Representatives Nancy Pelosi , Dennis Kucinich , and Steny Hoyer , and Senator John Kerry .

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Kwa picha zaidi ya arusi yao BOFYA HAPA:

Wednesday, March 07, 2012

I Refuse to be Part of Your Wedding Committee!

Nimepata kwa email. Naona MKenya kaja juu na hivyo vikao vyao arusi vya kila siku. Nilipokuwa Bongo kwa shangazi nilishangaa sana kuona  hizo invites za kamati zilikuwa tano moja! Haki ya Mungu!

***************************************************

Dear Friend,


I refuse to be part of your wedding committee!

I got your invitation card to the committee. I see you quoted an amount that I am expected to contribute.I must say that I feel honoured that you remember me. It has been years since the last time we spoke. I remember we used to be in the same school, and we recently befriended each other on Facebook.

However, friend, I must say that this came as a surprise to me. You see, I am unable to afford a wife myself. I have been planning to get a lady and head to the A.G chambers. I hear it will cost me very little money.

I see that your wife is trying to keep up with the Kardashians. It is a dream wedding that she wants. If you are able to afford that, my friend, it will be a very good thing to do. But, kindly do not tie me to financial obligations when mine are choking me. The current economic times have put a rope around everyone’s neck. I cannot afford Kshs 10,000/- (180,000/- Tsh) as contribution towards your wedding.

I am willing, more than willing to be a service provider- to oversee pitching of tents, directing guests to the sitting places, showing them the little rooms, collecting gifts.I am willing to attend the committee to pray for your marriage. I am willing to attend your wedding. I am willing to do all this. Friends need friends. But
friends don’t exploit friends.

I saw a facebook group you had created earlier as well- something about a goat eating party in preparation for ruracio (pre-wedding).   You will forgive me, because the first thing I thought was: what a money collecting idea!

I could push myself and bring you a gift on your wedding day. It is a noble thing to do. However, I will not buy you a wife, help you wed her in an expensive ceremony, then stock your house. I often tell people to live within their means. I know you will thank me someday.

If you cannot afford your wife’s dream wedding, and you give it to her still, what happens when she is about to deliver, and she needs a dream delivery at the Aga Khan-Princess Zuhura Pavillion? Will you call us for an emergency ‘my-wife-is-delivering’ committee? When the kid wants to go to school and has to go to Cianda School and Makini School, will you call us in as well? The world has needier people, and more deserving causes!

All I am saying is a wedding, a luxurious one in this case is not for you if you cannot afford three quarter of the money required.

Thursday, February 23, 2012

Bibi Arusi Ana Miaka 100, Bwana Arusi Ana Miaka 87! Kweli Kabisa!

Duh! Naona Cougar wa miaka 100 kaolewa leo na kijana  mwenye miaka 87 huko Kentucky.  Wanaarusi wanaishi katika nyumba ya wazee na walikutana huko.   Ni kweli mapenzi yakinoga unajisikia kijana.  Bibi Dana Jackson (100) anasema kuwa anajiona kama ana miaka 50 tu! Nawatakia maisha mema ya ndoa! 

Congratulations Mr. & Mrs. Strauss!

***************************************************

(Dana Jackson & Bill Strauss)
Woman Weds on Her 100th Birthday


By Bridal Guide

On February 6th, Dana Jackson celebrated a century of life with about 100 of her nearest and dearest at the Rosewood Health Care Center in Kentucky. An ice cream cake in her honor was frosted with the special message, "Congratulations, you are never too old." But this wasn't your average birthday party, not even for a centenarian: Jackson decided to mark the momentous occasion by marrying boyfriend Bill Stauss, 87.

Stauss never imagined that he would ever wed again, since his previous marriage lasted 55 years. However, Jackson was the exception: "I found one that's just as nice as can be. Treats me good. Like a human being should be treated. It's rare to find a girl like that."

"I feel 50," Jackson told BG Daily News. "I don't feel 100."

This was Jackson's third trip down the aisle, but the first time she wore an engagement ring and traditional gown. Her first wedding took place when she was only 15 years old. She marveled at how much has changed since then: "Gettin' married wasn't a big thing back when I was young. It wasn't no big thing...it was just simple, you know? Just simple...we wore clothes and maybe a bouquet cut out of the yard. It's not what you got, it's what you make out of a marriage," she said.

Jackson's message is timeless, and in the AARP video below, her happiness is infectious, just as with any other bride. But marrying at 100 does have its challenges: The couple sipped grape juice in lieu of cocktails and Stauss had trouble seeing his wife walk down the aisle. The moment didn't disappoint-the husband thought his wife looked "beautiful" when he finally got a closer look.

Kuona Video ya Arusi BOFYA HAPA:

Monday, February 06, 2012

Aolewa na Wanaume Wawili huko Katavi!

Sijui ilitoka kwenye gazeti gani. Lakini kwa kweli nimependa ushujaa wa huyo Mama Kaela!

********************************************************
MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME WAWILI


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani hapa, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zililifikia gazeti hili na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Ndugu wa Arcado wao wanalaani kitendo cha ndugu yao kuolewa na mama huyo, wakidai kuwa walishamshauri na kumuahidi kuwa endapo ataachana na mama huyo watamwozesha mwanamke mwingine, lakini yeye Arcado, amedai kuwa yuko tayari kufa, lakini si kuachana na mama huyo, kwani ndiye ubavu wake wa maisha.

“Sasa tumebaki tunamwangalia tu huyu ndugu yetu Arcado, tumemshauri, lakini mkaidi, hatusikilizi. Basi nasi hatuna la kufanya zaidi ya kumwangalia,“ alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Arcado. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Florence Katobasho, alikiri kuwa mwanamke huyo anaishi kinyumba na wanaume wawili na wanaishi kwa amani kwani hajawahi kufikishiwa malalamiko yoyote kuhusu wanandoa hao.

“Ni ukweli usiopingika, kwamba Mama Kaela anaishi na wanaume hao wawili … lakini kwa kuwa sijafikishiwa malalamiko yoyote kuhusu maisha ya wanandoa hao, mimi kama kiongozi hapa sina la kufanya na siwezi kuwafukuza, kwa kweli wanaishi kwa amani, mengine ni yao,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji

SOMA   ZAIDI http://www.fotobaraza.me/profiles/blogs/mwanamke-aolewa-na-wanaume#ixzz1lVfLAlP4

Monday, October 31, 2011

Arusi ya Musau Kabongo na Orrin Kennedy Boston

Wadau, napenda kwajulisha kuwa ya binti tuliyemfanyia Kitchen Party mwezi uliopita ameolewa jana, jumapili 30.10.11 hapa Boston. Binti Musau Kabongo ameolewa na kijana Orrin Kennedy ambaye asili yake ni kisiwa cha Trinidad.  Musau ni mtoto wa Dada Margaret Kabula kutoka Mwanza lakini anakaa Boston sasa. Baba Musau anatoka Congo. Arusi ilifanyika kwenye kanisa la Seventh Day Dorchester, MA na Reception ilifanyika DAV Function Hall Braintree, MA.
Mimi na Wana Arusi Musau na Orrin


Musau na Orrin Kabla ya Kukata Keki

Dada Doreen Kutoka Rhode Island Akisimamia Chakula

Bwana Arusi Akitafuta Garter kwenye mguu wa Bibi Arusi
 
Kama Kawaida Akina Mama waTanzania walipika Chakula Kingi

Orrin na Musau Wakikata Keki

Wageni Wakijipatia Mlo
Mama wa Bibi Arusi, Margaret Kabula (amesimama) na Vicky Mareaelle na mume wake

Mimi, wana arusi na kulia kabisa ni Rafiki yangu na msanii mwenzangu Charles Jackson Aka. Mzee Matumbi

Saturday, August 13, 2011

Bibi Arusi Ashikwa na Uchungu Kanisani!

Makubwa. Habari kutoka Muheza, Tanga zinasema Bibi Arusi, Mariam Shabani, kashikwa na uchungu kanisani, na kupelekwa hospitalini na shela yake na kuzaa huko! Pole zake. Mama na mwana wako salama. Wanasema alikuwa na mimba ya mieza saba.

*****************************************************************
Kutoka Gazeti la Mwananchi:


Bibi harusi ashikwa uchungu, ajifungua kanisani Muheza
Thursday, 11 August 2011 21:16

Mwandishi Wetu, Muheza

BIBI harusi aliyefahamika kwa jina la Mariam Shabani, ameshikwa na uchungu wa kujifungua kanisani wakati akifungishwa ndoa na mchumba wake, aliyefahamika kwa jina la Deo Massawe.Tukio hilo lilitokea juzi Kanisa Katoliki lililopo maeneo ya Majengo Shimoni, wilayani Muheza, huku umati wa watu ukiwa umejaa ndani ya kanisa hilo ukiisubiri kufungwa kwa ndoa hiyo.

Mwandishi wa habari hizi alishuhudia tukio hilo ndani ya kanisa hilo, wakati Padri Martin Kihiyo, akiendelea na misa ya kufungisha ndoa hiyo, ghafla bibi harusi akiwa amevaa vazi rasmi la harusi, alianza kupiga kelele akidai anasikia uchungu wa kujifungua.

Hata hivyo, baada ya bibi harusi huyo kupiga kelele, Padri Kihiyo alisitisha misa hiyo na Mariamu kuchukuliwa haraka na kuwekwa kwenye gari huku akiwa hajiwezi hadi Hospitali Teule Muheza.Pia, Mariamu anafahamika kwa jina la Sada Shabani, baada ya kufikishwa hospitali alipelekwa chumba cha kujifungulia huku akiwa na vazi lake la harusi.

Baada ya kuhudumiwa Mariamu, alijifungua mtoto wa kike na kulazwa wodi ya Azimio wanakolazwa wazazi.
Mmoja wa muuguzi hospitalini hapo aliyeomba asitajwe, alisema bibi harusi huyo alijifungua njiti akiwa na miezi saba.Kwa upande mwingine, kwenye ukumbi ambao ulikuwa umeandaliwa kwa sherehe ya harusi hiyo, watu walikuwa wamekaa ndani wakisubiri maharusi bila kufahamu kilichokuwa kikiendelea.

Hata hivyo, kutokana na hali hiyo bwana harusi alilazimika kufunga ndoa na msichana mwingine wa pembeni kwa niaba ya bibi harusi, ili kuhalalisha sherehe hiyo huku bibi harusi mwenyewe akiwa hospitali analea.

Inasemekana Mariamu alianza kusikia uchungu akiwa saluni na aliwaeleza baadhi ya watu, lakini walimjibu kuwa huo ni woga wa harusi.Katika hatua nyingine, mbuzi wa ndafu aliyekuwa ameandaliwa alianguka chini kwenye mchanga.

Baadhi ya Wakristo walisikitishwa na tabia ya viongozi wa dini kuendelea kuwafungisha ndoa watu ambao wake zao wana mimba kwamba, ni aibu.

Friday, May 06, 2011

Bwana Arusi ana Miaka 100, Bibi Arusi Miaka 90!

Africa ukifika miaka 40, basi wewe mzee! Ukifikisha 70 basi unstahili kutotelewa nje na kuanikwa juani. Huna thamani tena. Mapenzi, ndo usahau kabisa, unabakia kukumbuka katika ndoto zako ujana wako!

Hapa Marekani, wazee Forrest Lunsway (100) na Bi Rose Pollard (90), wamefunga ndoa. Hebu cheki nyuso zao za furaha, mapenzi motomoto! Inasemekana wamevunja rekodi ya umri wa wafunga ndoa. Doh! Wamejuana karibu miaka 28. wote wanakaa kwenye nyumba ya wazee. Nawatakia maisha mema ya ndoa. Kumbe hata ukiwa na miaka bado wamo! Ila Zaeni matunda mema haifia kusemwa hapa.
***************************************************************************



(pichani wanaarusi Forrest (100) na Rose (93))


Kutoka YAHOO.COM

For some people, it's never too late for love.

That's certainly the case for Forrest Lunsway and Rose Pollard, an Orange County, Calif. couple who were married this March 19, Forrest's 100th birthday. With a combined age of 193--Rose is a spring chicken--they're believed to be the world's oldest newlyweds.

A spokesman for the Guinness Book of World Records said they had been informed of the wedding and are set to verify it as a record. For 27 years, Forrest smoked a pack of cigarettes a day, and he still drinks the odd glass of wine or whiskey and 7-Up, he said in a recent interview with the The Daily. He attributes his longevity to never having had a desk job: He spent his youth trapping animals and selling their fur in Kansas before moving to California, where he worked as a pipe welder.

You can watch a video of them here.

Both Forrest and Rose had been married before, but were single when they met back in 1983 at a senior's dance. Though they soon started dating, wedding bells seemed unlikely.

'I told him up front I had no intention of getting married," Rose said. "But then one day he asked me 'how come we never got married? and I said 'because you never asked me.'"

''So he got down on one knee and said, 'Well I'm asking you now, just set the date.' I told him, 'I'll marry you on your 100th birthday.' And I did."

And being on the older side, the couple also has some wisdom to share on how to make a marriage work. Rose, 93, told The Daily: 'Take your time and get to know one another. Get to know if you like all the things that person stands for. ... Be forgiving and patient and say I love you once in a while."

Rose also told The Daily that their advanced age means that she and Forrest don't have many of the anxieties that can be a challenge for other newlyweds. "That's one of the things we can forget about--time. Because time doesn't mean that much."

And it's time well spent together: They both love ballroom dancing, and they want to kayak in Alaska and walk the coast of California.

"We've got many happy years left as I intend to stick around until I'm at least 110," Forrest said. "You've got to use it or lose it."
(The Daily)

Thursday, April 28, 2011

Mama Bishanga Ameremeta!!!

Bwana na Bibi Marolen baada ya kufunga ndoaKwa mila ya waMakua kwa wanawake hulala chini na bibi arusi kupita juu yao mpaka kwenye kiti atapokaa.
Familia ya Hatia, familia ya Mrope, na familia ya Kamota wakipiga picha ya pamoja na wanaarusi



Wadau, Mama Bishanga jina halisi Christina Innocent Hatia amefunga ndoa hivi karibuni huko Dar es Salaam, Tanzania. Bwana harusi ni Mr. Marolen kutoka Afrika Kusini.

Arusi ilifanyika siku ya tarahe 5 Machi, 2011 katika knaisa la St. Peters Oyster Bay. Reception ilifanyika Peacock Hotel.

Nawatakia maisha mema ya ndoa.

Tuesday, September 07, 2010

Dr. Slaa Afunguliwa Mashitaka Mahakama Kuu!

(Pichani Dr. Wilbrod Slaa - CHADEMA)

Jamani, sasa badala ya kuwa kampeni ya siasa, ugombea rais wa Dr. Wilbrod Slaa wa chama cha CHADEMA, unageuka kuwa Soap Opera (Tamthiliya)! Majuzi huko Babati walimwuliza Dr. Slaa ana wake wangapi(BOFYA HAPA kupata maelezo zaidi), leo eti mume halali wa mke wa Dr. Slaa, kaenda mahakamani na kusema kuwa Dk. Slaa kamwibia mke wake! Kusoma habari zaidi za kesi BOFYA HAPA.
Huo mchezo wa kukuchunguza mpaka umevaa chupi gani kama ni mwanasiasa ni mchezo mkuu hapa Marekani. Ukiwa mwanasiasa lazima uwe msafi. Kwa maana hiyo usitembee nje ya ndoa, usiwe na kimada, usizae nje, usifanye ngono na malaya... listi ni ndefu. Bado wanafanya na wakigundulika wengi wanalazimishwa kujiuzulu.

Enzi za Mwalimu ulikuwa husikii kwenye vyombo vya habari kiongozi fulani anatembea na fulani! Sasa ni jambo la kawaida, sijui ndo uhuru wa vyombo vya habari au nchi kukua kisiasa. Wangekuwa wanasema mambo ya watu enzi za Mwalimu mbona yangesemwa mengi. Ungesikia fulani kazaa katika kila mkoa wa Tanzania, fulani ana familia nyingine sehemu fulani, binti fulani katoa mimba ya kiongozi fulani n.k. Sidhani kama kuna kiongozi 'msafi', hata kwa upande wa wanawake! Kiongozi fulani kazaa sehemu fulani, kiongozi huo kapata ugonjwa fulani mahala fulani.....Doh! Tunaelekea wapi?

Mwisho nauliza kwa nini wanamsakama Dk. Slaa sasa? Naona kampeni yake imepamba moto kweli halafu ndo jamaa anataka alipe eti mabilioni!

Friday, June 19, 2009

Arusi Inapovunjika Dakika Za Mwisho




Na Da Flora Wingia


Zipo harusi zingine ukisimuliwa mikasa yake utadhani ni sinema za kuigiza. Pilikapilika nyingi tokea uchumba, maandalizi ya harusi zenyewe lakini katika kuhitimisha ndoa hazifungwi. Kulikoni?

Hivi majuzi nilikuwa sehemu katika kikao fulani cha harusi. Ni eneo linalotizamana na barabara kubwa iendayo Bagamoyo. Kabla ya kikao, ukapita msafara ambao tulidokezwa kuwa ni wa Kitchen Party.

Kitchen Party ni tafrija ndogo inayotangulia send-off kisha baadaye harusi. Tafrija hiyo inalenga kumfunda bibi harusi mtarajiwa kabla ya kuanza maisha ya ndoa na mumewe.

Naam. Mimi nikasema, “hayo ni maandalizi ya harusi bila shaka…siku hizi upo msemo kwamba wanaooa au kuolewa miaka hii wanapeleka matatizo nyumbani”.

Baba mmoja aliyeketi pamoja nami akadakiza; “umesema ukweli, harusi za siku hizi si lolote si chochote, gharama kibao lakini muda si mrefu wanaachana”.

Baba mwingine bila kuchelea akasema, “Ngoja niwasimulie ndoa moja iliyovunjika dakika za mwisho na kuacha wengi midomo wazi. Ilihusu jamaa yangu mmoja.

Katika simulizi yake akasema kuwa yupo kaka mmoja ambaye ni jamaa yake alipania kumuoa mwanamama fulani. Maandalizi yakafanyika kuanzia kitchen Party, na send-off vyote vikafanyika.

“Maandalizi ya harusi yenyewe yaligharimu shilingi milioni 18,” kwa mujibu wa baba huyu. Kila kitu kikawa tayari ikabakia kwenda kanisani ili ndoa ifungwe.

Siku ya harusi, bibi harusi akapelekwa saluni kutengenezwa na kuvalishwa.

Bwana harusi naye akapelekwa kuandaliwa. Wageni waalikwa, ndugu na marafiki wakawahi kanisani.

Alivyoeleza baba yule ni kwamba muda wa kwenda kanisani ulipokaribia, ilitakiwa bwana harusi na mpambe wake waenda kumfuata bibi harusi ili kwa pamoja waweze kwenda kanisani.

Lakini ajabu ni kwamba bwana harusi alijaribu kumsaka aliko mkewe mtarajiwa bila mafanikio. Walipokwenda saluni alikopambiwa aliambiwa kuwa yuko jamaa aliyekuja kumchukua na gari lililokuwa limepambwa vilivyo.

Kule kanisani wageni waalikwa pamoja na mtumishi wa Mungu aliyejiandaa kufungisha ndoa ile wakawa wanasubiri kwa muda mrefu wasijue kilichotokea.

Mwishoni wote wakakata tamaa na kutawanyika kurejea kwenye sherehe za harusi kujua kulikoni.

Kumbe baadaye akabainika kuwa yule jamaa aliyekwenda kumchukua bibie pale saluni alikuwa mpenzi wake wa zamani na hivyo kwa pamoja walitorokea kusikojulikana. Inaonekana bibi alikuwa anampenda aliyemtorosha kuliko yule waliyetaka kufunga ndoa naye.

Swali ni je, kwanini mwanamama huyu hakuwa wazi mapema kwa kueleza bayana kwamba bwana harusi yule mtarajiwa hakumpenda bali alikuwa na mwandani wake mwingine?

Hiyo ingesaidia mambo mengi pamoja na kuzuia gharama za maandalizi, usumbufu wa watu waliochanga fedha zao, wakaenda hata kanisani lakini harusi haikufungwa. Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.

Ndoa zingine ni vurugu tupu. Usione watu wamesimama mbele ya mashekhe au pale madhabahuni huku maneno mazuri yaliyojaa upendo na matumaini yakiwatoka vinywani. Wengine ni usanii mtupu kama siyo unafiki.

Katika nafsi zao bado wanawakumbuka wapenzi wao wa zamani. Pale altareni inakuwa ni kuthibitisha tu kwamba eti nao wameoa au wameolewa kwa kufunga ndoa takatifu. Kumbe wakishatoka pale, mawasiliano na wachuchu wa zamani yanaendelea kama kawaida.

Matokeo yake ndiyo hayo tunashuhudia kuchipuka kwa nyumba ndogo au wengine wakikufuru zaidi huachana na wenzi wao au kutafuta visingizio ili ndoa zivunjikie mbali.

Haya siyo maisha bali ni kuongeza majanga ya kifamilia. Nyumba moja inakushinda sembuse nyumba mbili au tatu? Sijui labda niseme ‘mwenye nguvu mpishe’ lakini madhara yake hayako mbali.

Msomaji wangu nikuachie nawe uchangie mawazo tuweze kusonga mbele kwa pamoja. Kama unacho kisa unadhani tunaweza kujadili kwa pamoja usisite kuniandikia kupitia email hii hapa chini.

fwingia@yahoo.com
Wasalaam

Wednesday, September 10, 2008

Ajali ya Gari Dar - Wapambe wa wanaarusi wafariki!

Jamani mmetoka kusherekea arusi halaffu kitu kama hii kinatokea. Mungu awape nguvu hao wanaarusi maana lazima marehemu ni ndugu au marafiki wa karibu. Nawapa pole maana ni njia mbaya sana ya kuanza maisha ya ndoa. Leo mnasherekea arusi kesho kilio. Jamani!

*******************************************************
Kutoka IPPMEDIA.com
Ajali mbaya Dar!

2008-09-10

Na Moshi Lusonzo, Jijini

Watu wawili wanaotajwa kuwa ni wapambe wa maharusi wamefariki dunia huku wengine kadhaa wakiwemo bwana na bibi harusi kuumia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuvaana na lori la mizigo.

Tukio hilo la kusikitisha, limetokea hivi karibuni, katika eneo la Ubungo ambapo gari lililobeba maharusi na wapambe wao lilipoteza muelekeo na kulivaa lori la mizigo kwa mbele kabla ya kupinduka.

Wakizungumza na Alasiri, baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo akiwemo dereva wa lori la mizigo lililogongwa kwa mbele, Bw. Juma Gwao, 38, wamesema tukio hilo lilijiri mishale ya saa 7:00 usiku.

Wameeleza mashuhuda hao kuwa mara tu baada ya ajali hiyo, bwana na bibi harusi walijeruhiwa na kukimbiziwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, huku wapambe wawili kati ya wale walioambatana nao wakifariki dunia papo hapo.

Akisimulia zaidi ajali hiyo, dereva Gwao ambaye bado amelazwa wodi 17 ya Jengo la Sewahaji pale katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili, MOI, amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari lililobeba maharusi na wapambe wao kushindwa kuumiliki vyema usukani wa gari na kusababisha aajali ya kugongana uso kwa uso.

Akiasema Gwao kuwa wakati ajali hiyo ikitokea, yeye alikuwa akiendesha gari lake lenye namba T 908 aina ya Fuso, akitokea Ubungo kwenda mkoani Shinyanga kwa ajili ya kuchukua shehena za mizigo.

Akasema wakati akiwa ndio kwanza anaianza safari hiyo eneo la Ubungo, ghafla likatokea gari aina ya Canter ambayo ilibeba maharusi pamoja na wapambe wao kibao.

Akasimulia dereva Gwao kuwa pamoja na kujitahidi kukwepa, bado gari hilo lilimfuata aliko na kuigonga gari yake kwa mbele na kisha kupinduka.

``Nadhani dereva mwenzangu alishindwa kuhimili usukani... kwani licha ya kujitahidi kumkwepa, bado alinifuata niliko na kuigonga gari yangu kwa mbele,`` akasema Gwao.

Shuhuda mwingine akasema mara tu baada ya ajali hiyo, wapambe wawili waliokuwa wakiwasindikiza maharusi hao wakapoteza maisha huku wengine kadhaa wakijeruhiwa na kukimbiziwa Muhimbili.

Afisa Uhusiano wa MOI, Bw. Almas Jumaa, amesema ukiacha dereva Gwao, majeruhi wengine wote wa ajali hiyo walipatiwa matibabu na kuruhusiwa kurudi makwao.

Akaeleza vilevile kuwa hadi sasa, majeruhi Gwao ambaye ni pekee aliyelazwa hadi sasa, angali akiendelea vyema na matibabu na tayari ameanza kupata nafuu kubwa, ukilinganisha na hali aliyokuwa nayo wakati akifikishwa hospitalini hapo.

SOURCE: Alasiri

Wednesday, September 03, 2008

Bibi Arusi ni....Khadija Kopa! Anameremeta!




Malkia wa mipasho, Khadija Kopa ameolewa!
Hebu wapashe dada! Ulipendeza sana siku ya arusi.
Picha kutoka Michuzi Blog.

Tuesday, September 02, 2008

Bwana Arusi achinjwa Dar

Jamani, mbona mauaji yanazidi Dar? Wivu kitu kibaya sana. Mola ailaze roho yake mahala pema peponi. Amin.

***************************************************

Kutoka ippmedia.com
Bwana harusi Dar achinjwa!

2008-09-02
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Mwanaume mmoja anayedaiwa kuwa mbioni kufunga ndoa wiki hii ameuawa kinyama baada ya kuchomwa kisu na kisha mwili wake kukutwa kandoni mwa barabara.

Taarifa ambazo Alasiri imezipata toka kwa baadhi ya waliodai kuwa ni mashuhuda wa tukio hilo, zinadai kuwa tukio hilo limejiri mishale ya saa 4:00, usiku wa kuamkia jana na kwamba marehemu ametambuliwa kwa jina la Nassoro Shomari.

Taarifa hizo zinadai kuwa bwanaharusi ni dereva taksi aliyekuwa akifanya shughuli zake katika Kituo cha Sinza Madukani Jijini.

Wanadai mashuhuda hao kuwa mwili wa bwanaharusi huyo mtarajiwa ulikutwa katika eneo la Tandale, kandoni mwa njia ya kuelekea Kijitonyama.

Aidha, taarifa hizo zinadai kuwa mmoja wa wale wanaotuhumiwa kufanya mauaji ya dereva taksi huyo ni mwanamke mmoja aitwaye Aisha, anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa zamani wa marehemu.

Wakieleza zaidi, wanadai wasimuliaji kuwa chanzo cha kuuawa kinyama kwa dereva taksi huyo ni kisa cha kimapenzi, hasa kutokana na ukweli kuwa wiki hii alikuwa afunge pingu za maisha na mwanamke mwingine na kuwatosa wengine aliowahi kuwa nao hapo kabla.

Wanadai wasimuliaji kuwa kabla ya uamuzi wake wa kutangaza ndoa, marehemu aliwahi kuwa na uhusiano na mwanamke mmoja pale Tandale, jirani na njia ya kuelekea Kijitonyama.

Wanadai kutokana na utamu wa penzi lao, marehemu akafikia mahala pa kujifunga mbele ya mwanamke huyo, kwa ahadi kwamba atamuoa.

``Na tena ndiye aliyempangia chumba hapo Tandale... na alikuwa akimhudumia kwa kila kitu kiasi kwamba mwanamke wa wenyewe alijua kuwa yeye ndiye yeye tu... hakuna mwingine zaidi yake,`` akadai mmoja wa wasimuliaji.

Inadaiwa kuwa licha ya kuwa na ahadi ya kumuoa mwanamke huyo, marehemu alikuja kughairi na badala yake akatangaza kufanya mipango ya ndoa na mwanamke mwingine.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa zikiwa zimebaki siku chache kabla ya harusi yake wiki hii, ndipo marehemu alipochepuka kidogo na kwenda nyumbani kwa mpenziwe wa zamani.

``Akiwa huko, haieleweki ni kitu gani hasa kilimkuta... lakini mwili wake ukakutwa kandoni mwa njia ukiwa umechomwa visu,`` akadai mmoja wa watu waliodai kuwa ni mashuhuda.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni hakupatikana ili kuzungumzia tukio hilo la kusikitisha.

Baadhi ya maaskari polisi wameiambia Alasiri kuwa ni kweli kuna tukio la mwanaume kuuawa kwa kuchomwa visu, na ambalo limejiri mishale ya saa 4:00, usiku wa kuamkia jana.

Hata hivyo, wamesema mwanaume huyo ni dereva wa daladala aina ya DCM linalofanya safari kati ya Mbagala na Sinza, likiwa na namba za usajili T 223 AUS.

Wanadai askari hao kuwa juhudi za kumsaka mtuhumiwa Aisha zinaendelea, kwani anadaiwa kutimka baada ya kujiri kwa tukio hilo.

SOURCE: Alasiri

Tuesday, June 17, 2008

Mr. Sulu anaoa!


George Takei na Mchumba wake Brad Altman

Wapenzi wa Star Trek, hatimaye mcheza sinema, George Takei, (71) maarufu kwa kuigiza kama Mr. Sulu anaoa...bibi arusi ni mwanaume mwenzake! Anamwoa mpenzi wake wa siku nyingi Brad Altman (54).

Kama hamkujua Takei alijitokeza mwaka juzi na kusema yeye ni shoga. Tangu leo asubuhi huko California ni ruksa kwa wapenda jinsia moja (wasenge na mashoga) kufunga ndoa. Wanasema yeye alikuwa wa kwanza kuchukua kibali kwenye mji anayokaa, West Hollywood.

Jimbo la California sasa ni la pili nyuma ya Massachusetts nchini Marekeni kuruhusu mashoga kufunga ndoa.
Kwa habari zaidi someni:
http://www.eonline.com/uberblog/b143090_george_takei_licensed_wed.html