Showing posts with label Peter Kupaza. Show all posts
Showing posts with label Peter Kupaza. Show all posts

Monday, January 07, 2008

Amwua na Kumpika Mpenzi wake


Kuna nini ndani ya maji ya Texas inayofanya watu wanaoiinya kufanya vituko?

Leo kuna habari kuwa huko Tyler, Texas, jamaa fulani tena mmarekani mweusi, kamwua mpenzi wake, Jana Shearaer (21). Baada ya kumwua kamkatakata vipande, kachemsha vipande hivyo, na kuweka mezani pamoja na uma na kisu tayari kwa kula.

Polisi wanasema walivyofika nyumbani kwa, Christopher Lee McCuin (25), walikuta sufuria ya supu inachemka jikoni, juu ilikuwa inaelea sikio la bindamu. Mezani kulikuwa na kipande cha nyama ya binadamu iliyopikwa na uma ilikuwa ndani tayari kwa kula! DUH! Mauji na vituko vilivyofuata alifanya nyumbani kwa mama yake.

Christopher alimwita mama yake kuja kushuhudia alivyofanya, ndo mama yake alikimbia kwenda kuita polisi.

Polisi hawajui kama alimla sehemu au la. Itabidi kinyesi chake kipimwe.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema mbinguni. Amen.

Kwa vile hayo mauji yalitokea Texas, huyo Christopher atahukumiwa adhabu ya kifo.

Kwa habari zaidi someni:




Thursday, September 20, 2007

Mwivano Kupaza alivyouliwa na Ndugu yake Wisconsin


Marehemu Mwivano Kupaza

Polisi reconstruction ya uso wa marehemu


Muaji Peter Kupaza


Jana niliangalia Documentary kwenye Discovery Channel kuhusu jinsi wataalam wa forensics walivyo gundua kuwa vipande vya maiti yaliotupwa kwanye mto huko Wisconsin yalikuwa ya marehemu Mwivano Mwambashi Kupaza.

Nadhani baadhi yenu mnakumbuka pilipilika za wakati ule miaka ya 1999/2000. Kwa wasiojua nitawasimulia kwa kifupi mambo yalivyokuwa.

Mama moja mzungu na watoto wake walienda kufanya picnic kando ya mto. Walikuta vipande vya maiti vimetupwa ndani ya mifuko ya takataka. Waliita polisi. Polisi walishangaa mambo waliokuta. Maiti ilikuwa imechunwa ngozi, maiti imekatwa katwa viapnde kitaalamu hasa, lakini wali kuta kipande chenye nywele na kujua kuwa ni maiti ya mwanamke mwenye asili ya Afrika.

Polisi walichunguza database zao za watu ambao wamepotea. Hawakupata kitu waligonga ukuta.

Waliomba msaada wa wataalam wa forensics kusudi wajue huyo mwanamke alikuaje. Hata fuvu (skull) yake ilikuwa imebomolewa lakini waliweza kuijenga kwa kutumia kompyuta. Baada ya hapo walipeleka kwa mtaalamu wa kujenga uso (facial reconstruction) ndo ikapatikana ile picha ya juu enye picha nne.

Polisi huko Wisconsin walisambaza hiyo picha sehemu nyingi na katika vyomboa ya habari. Ndo mke wa Peter Kupaza na waTanzania wengine walipiga simu polisi na kusema kuwa hiyo picha inafanana na Mwivano Kupaza. Pia mke wa Peter alimwambia kuwa huko Tanzania mume wake aliwahi kufanya kazi kama bucha na alimsimulia sana jinsi ya kuchinja mnyama na kumchuna ngozi. Hapo sasa Peter kawa suspect namba moja. Polisi waliwahoji sana waTanzania huko Wisconsin wakati huo.

Polisi walimfuata Peter nyumbani kwake. Kwanza Peter alidai hamjui Mwivano. Baadaye alisema kuwa alirudi Tanzania na jamaa anaitwa Shadrack lakini hajui jina lake la pili eti. Polisi wa Wisconsin walipiga simu Tanzania na kuambiwa kuwa Mwivano bado yuko Marekani.

Sasa ingawa Peter walimshuku walishindwa kumkamata kwa sababu walikuwa bado hawana uhakika kuwa hiyo maiti ni ya Mwivano. Wakati huo Peter alikuwa anafanya kazi kama 'Employment and job-training counselor for the Wisconsin Department of Labor and Human Relations'. Alivyondoka Tanzania alikuwa mwalimu.

Polisi walijua wasipokuwa wajanja kesi itaishia hewani. Walichukua mbwa wa kunusa nusa (sniffer dog) na aligundua damu chini ya mabao bafuni. Walifanya DNA Test na kugundua kuwa damu ni ya Mwivano. Lakini hiyo haikutosha kumkamata Peter. Kilichohakikisha kuwa maiti ni ya Mwivano ni kuwa Peter alimpeleka kliniki kutoa mimba! Hiyo mimba ilikuwa ni ya Peter. Kumbe Peter alimgeuza ndugu yake mke mdogo. Mwivano alivyosign ile fomu ya kutoa mimba aliacha fingerprint. Ndo fingerprint hiyo waliomechisha na fingerprint kwenye maiti. Na mimi nasema roho ya kile kichanga kilichouliwa pale kliniki ndo kilimponza Peter Kupaza!

Peter alikamatwa na kesi ilipelekwa mahakamani. Huko mahakami Peter alidai kuwa Mwivano aliuliwa na mwanaume wa kizungu. Peter amefungwa maisha gerezani. Lakini jamaa alivyo mshenzi alijaribu kukata rufaa. Lakini hataachiwa. Huyo Peter Kupaza ataoza gerezani na kwa sasa ni moja wa wake wa Big Bubba huko.

Mungu amlaze roho ya Mwivano Kupaza mahali pema mbinguni. Amen.

* Kwa wasiofahamu mke wa Peter Kupaza, Shari Goss, anaigiza katika sinema ya TUSAMEHE!


KWA HABARI ZAIDI ZA MAUAJI YA MWIVANO KUPAZA SOMA:

Killing Cousins


Rebuilding victim's face key to arrest in killing

http://www2.jsonline.com/news/state/feb00/body03020200a.asp?format=print

Appeal ya Peter Kupaza 2006 (Mshenzi anataka aachiwe huru)

http://caselaw.lp.findlaw.com/scripts/getcase.pl?court=wi&vol=wisctapp2%5C2006%5C2005ap000101&invol=1

WISCONSIN VS. PETER KUPAZA