Showing posts with label Peter Mizengo Pinda. Show all posts
Showing posts with label Peter Mizengo Pinda. Show all posts

Saturday, November 05, 2016

Mh. Pinda Atembelea Makao Makuu ya CCM, Lumumba

 Wazuri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alipotembelea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, jana.  Kushoto ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka.
 Wazuri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alipotembelea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam
Wazuri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alipotembelea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka, na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Pindi Chana. (Picha zote na Bashir Nkoromo).

Tuesday, October 16, 2012

Waziri Mkuu Pinda Kuunguruma London!


Waziri Mkuu, Mh. Peter Mizengo Pinda

WAZIRI MKUU PINDA KUUNGURUMA LONDON.


*Ni siku chache baada ya uadilifu wake kumuokoa kupigiwa kura ya Imani Bungeni.

*Kuainisha mafanikio ya serikali kuhusu Uraia Pacha na Ardhi kwa wanadiaspora.

Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Peter Kayanda Mizengo Pinda (Mtoto wa Mkulima) leo Alasiri ya Jumanne tarehe 16 Oktoba, 2012 anatarajiwa kuunguruma Jijini London katika mkutano wake na Watanzania waishio hapa Uingereza.

Mheshimiwa Pinda ambaye yuko katika ziara fupi ya kibinafsi hapa London amerudia utaratibu wa kupenda kusemezana na Watanzania hata anapokuwa kwenye itifaki ya ziara fupi na ya binafsi, tabia ambayo imekuwa ikisifiwa na watanzania waishio nje ya nchi.

Aidha mkutano huu ni wa kwanza kwa Mheshimiwa Pinda hapa London tangu jaribio liloongozwa na wabunge wa Upinzani na wachache wa CCM kutaka kumng’oa madarakani liliposhindwa vibaya kwa kupata saini 70 tu kati ya 357 kupinga Ufisadi uliokithiri miongoni mwa watumishi vigogo ndani ya Serikali. Mkutano huu wa Waziri Mkuu unakuja katika kipindi ambacho Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania (CHADEMA) kimebadili ghafla mtazamo wake kwa watanzania nje ya nchi na kuanza kufungua utitiri wa matawi, kumwaga Ruzuku na kufanya ziara ya mara kwa mara kwenye matawi yao ili kuwapika makada wake kwa ajili ya uchaguzi wa 2015. Waziri kivuli wa Mambo ya Nje (CDM) Mhe. Dibogo Wenje ndiyo kwanza amemaliza ziara yake hapa London akiwa ameacha ahadi lukuki kwa wafuasi wao akiwataka wajiandae kushika majimbo ya Ubunge na nyadhifa mbalimbali serikalini kunako baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Awali, tofauti na CCM, CHADEMA walipinga sana uhusishwaji wa watanzania nje ya nchi katika miradi ya kisiasa na maendeleo ya kitaifa.

Katika hoja za msingi, Waziri Mkuu Pinda anategemewa kuainisha bayana msimamo wa serikali na hatua madhubuti ambazo imezichukua kutafsiri kwa vitendo Sera na Ahadi ya Chama cha Mapinduzi ya kujumuisha suala la Uraia Pacha katika marekebisho mapya ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa ikizingatiwa kuwa uwakilishi wake wa awali ulipokelewa kwa hofu miongoni mwa wabunge, baadhi ya wananchi, wanahabari na wafinyanzi wa Sera katika chelezo mbalimbali za kijamii.

Mashauri mengine yanayotarajiwa katika mkutano huu ni pamoja na maombi ya awali ya CCM UK ya kutaka Serikali iandae utaratibu maalum wa kuwasaidia watanzania waishiao nje ya nchi kupata na kuwekeza katika hazina ya ardhi nchini Tanzania kuliko ugumu uliopo sasa hivi. Aidha Serikali kuhamasisha sekta binafsi za kifedha na mitaji ya jamii kuwafikia watanzania ughaibuni ili kuhamisha teknolojia, ubunifu na uwezo wa kuwekeza katika maeneo kama Kilimo Kwanza na Ujasiria mali wa mizania ya kati.

Pamoja na mahudhurio kutarajiwa kuwa makubwa lakini watanzania wengi wanasemezana kuwa na imani na CCM lakini wanahisi Serikali na mamlaka zake bado hazija chukua hatua madhubuti kupunguza ufisadi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kitaifa.

Na Clement Mbawala

Tanzania Now: Freelance Observers Slough. St.Marys Road. SL3

Thursday, October 22, 2009

Wanavijiji Wafukuzwa Morogoro

Premier Mizengo Pinda (C), flanked by Morogoro regional commissioner, Colonel (rtd) Issa Machibya (L), Kilombero district commissioner, Evarist Ndikilo and Kilombero Plantations Limited manager, Carter

Huko Zimbabwe, Mugabe anafukuzwa wazungu kusudi wananchi wa kiafrika wapate ardhi ya kulimia. Sisi Tanzania, tunafukuza waafrika kusudi wazungu wapate ardhi ya kulimia. Ukoloni Mamboleo?
**********************************************************

Kutoka ippmedia.com

Prime Minister Mizengo Pinda has ordered villagers who invaded the Mngeta Rice Farm (MRF) in Kilombero district, Morogoro region to leave immediately to make way for massive agricultural investments.

The premier issued the order over the weekend on the second day of his official tour of Morogoro region to inspect agricultural activities including farms and research centres.

Addressing Mngeta villagers, the Prime Minister said about 2,000 residents of Mngeta and Lukolongo villages have illegally taken over 300 hectares out of 5,000 hectares in the potential area for paddy farming.

He directed Morogoro regional authorities to ensure that villagers who have illegally invaded the area are immediately relocated to other areas.

“But this should be done in a proper manner. I would not prefer the use of force during the process of relocation,” the Premier cautioned, stressing that farmers should continue cultivating around the MRF as out-growers and contract farmers.

He said the move would enable the farmers acquire farming skills and access to rice farming infrastructures.

MRF is co-owned by Rufiji Basin Development Authority (RUBADA) and a UK based investor, Agrica.

The two have formed a new company known as Kilombero Plantations Limited (KPL) to help boost modern agriculture in the region.

The farm was established in 1986 under Korea Tanzania Agricultural Company (KOTACO). KPL started to operate the farm in 2008 and succeeded to cultivate more that 2,000 hectares of rice with an investment of 22bn/-.

Pinda arrived in Morogoro last Saturday and started his tour by visiting Kilombero district where he received information on development of the ‘Kilimo Kwanza’ initiative from the District Commissioner, Eng. Evarist Ndikilo. He also visited the Katrin Agricultural Research Centre.

He also visited Chita-Melela valley which is used for rice cultivation.

The Prime Minister also advised farmers to establish a Savings and Credit Cooperative Society (Saccos) that would provide them with funds to improve their agriculture, and promised to give them 10m/- once they manage to contribute among themselves a total of 10m/-.

Pinda yesterday visited Sagamaganga village to see a demonstration farm for livestock keeping where he promised a 3m/- donation as a contribution for purchases of animal feeds and vaccination.

CHANZO: THE GUARDIAN

Friday, March 13, 2009

Waziri Mkuu Pinda Achachamaa!

Mheshimiwa Pinda anavyochemka ananikumbusha alivyokuwa anachemka Marehemu Edward Moringe Sokoine. Nadhani watu hawakutegemea kuwa angekuwa mchapakazi hivyo! Sema, Usiopgope, Sema!

***********************************************************************
Kumbe kuna mambo pale kwenye kituo cha mabasi Ubungo!

Ubungo bus terminal pact dubious - PM

2009-03-13
By Guardian Reporter

Prime Minister Mizengo Pinda said yesterday that the contract under which Dar es Salaam`s Ubungo Bus Terminal is operating is dubious.

Speaking during a stop-over at the upcountry terminal on his second day of a tour of the city, Pinda said the contract has made the nation incur huge losses in gate collections from bus operators and other users.

He cited a clause in the contract which states that the fee to be paid by the private firms running the terminal will be only 1.5m/- per day.

Pinda said in many similar standard contracts, a fair deal would have been a certain percentage from the total amount collected each day.

Asked to explain the anomaly, city officials accompanying the PM remained mum. The Bus Terminal Manager, Fadhili Izombe, also couldn’t utter a word.

The PM, whose tour ends today, ordered the Dar es Salaam City Council to review the contract as soon as possible.

Smart Holding Company has been running the terminal`s operations since 2004. However, its contract ends in October.

SOURCE: Guardian

Pia soma: http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2009/03/13/133296.html
*************************************************

Na bado! Hatimaye kuna mtu kasema ukweli kuhusu hao wazungu wanaojazana huko Bongo eti ni maExpats! Kumbe huko kwao hawawezi kupata kazi!

WAZIRI MKUU PINDA OYEEEEEE!

Kutoka Ippmedia.com

Pinda: Stop pandering to unqualified expatriates

2009-03-13
By Patrick Kisembo

The government has expressed grave concern over some employers` tendency to deny locals rightful jobs by recruiting unqualified expatriates.

The reservation was sounded by Prime Minister Mizengo Pinda on Wednesday night in Dar es Salaam during an occasion to award the 2008 Employer of the Year Award hosted by the Association of Tanzania Employers (ATE).
The Standard Chartered Bank Limited was awarded as the 2008 Employer of the Year.

He was particularly unhappy with the growing tendency whereby some employers prefer foreigners who in his opinion ``are lazy,`` but some are getting monthly salaries five times the amount paid to locals.

The Premier said: ``Some of these so-called experts are fakes. But they are being paid five times what a local Tanzanian worker earns in this country. Let`s do what we can to stop this.``

Pinda dismissed claims that locals are poor in their command of the English language, charging that some expatriates ``likewise speak broken English,`` but end up fetching huge salaries.

``We should stop this. Let`s address this problem in order to do justice to local employees,`` he insisted.

Pinda said he was aware of employers giving jobs to foreigners and denying locally trained Tanzanians the chance simply because ``they are not fluent in the English language.``

```Locals are not admitted to jobs. Even when employed they are not given decent jobs. They end up serving in low positions.This is a big problem which should be worked on,`` said the Premier.

He also stressed the importance of using existing local academic institutions to get experts and quality workers who can be sold in regional and international labour markets.

``We have enough educational institutions which produce good people who can perform. We have universities, technical colleges.

We need to use these in getting experts and quality workers for quality production,`` he said.

ATE Chairperson Cornelius Kariwa said that employers of the year were expected to promote skilled labour, as a principal factor in productivity improvement.

He, however said ATE has established that there is a huge untapped potential for improving worker productivity and profitability in several member enterprises if workers are well supervised, coached, motivated and remunerated.

Alexio Musindo, who represented the International Labour Organization Director for Tanzania, Kenya and Somalia at the event, applauded ATE for its efforts to promote efficiency and effectiveness of employers in their role of promoting economic growth and reducing poverty.

``However this is a demonstration of your commitment to promotion of harmonious workplaces and of decent working conditions for your workers,`` he said.

According to the National Employment Promotion
Service Act of 1999, Section 25, no employer is allowed to recruit a foreigner in a position in which only citizens may be employed.

The law also stipulates that any employer who employs any foreigner in contravention of the law commits an offence and is liable on conviction, to a fine of not less than one million shillings or to imprisonment for a term of not less than six months, or to both a fine and imprisonment.

SOURCE: Guardian

Saturday, January 24, 2009

Serikali Yafuta Leseni za Waganga wa Kienyeji

Wadau, nasema WAZIRI PINDA NI SHUJAA!!!!

*******************************************************************
Waziri Mkuu Pionda afuta leseni za waganga wa kienyeji

SERIKALI imetangaza kufuta leseni zote za waganga wa jadi kuanzia jana (Ijumaa Jan. 23, 2009) ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe nchini.

Amri hiyo ilitangazwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika mkutano wa hadhara mjini Shinyanga jana mwishoni mwa ziara yake ya mikoa ya Kanda ya Ziwa kuhamasisha mapambano ya Serikali dhidi ya mauaji hayo.

Waziri Mkuu alisema kuwa aliwasiliana na Mwanasheria Mkuu kuhusu uamuzi wa kuchukua hatua hiyo ya kufuta leseni hizo na Mwanasheria Mkuu akasema jambo hilo linawezekana.

"Kuanzia leo leseni zote za waganga wa jadi futa… Mtu yeyote akiendelea na kazi hiyo mfuatilieni," aliwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakuu wa Halmashauri zote za Jiji, Miji na Wilaya nchini.

Waganga wa jadi wamekuwa wakituhumiwa kuwa ndiyo chimbuko la mauaji hayo kwa vile wao ndiyo hupiga ramli za kuelekeza hivyo.

Katika mikutano na viongozi wa mikoa ya Kagera, Mwanza, Mara, Tabora na Shinyanga, wachangiaji wengi waliitaka serikali kufuta leseni hizo. Hata baadhi ya waganga wa jadi waliochangia walikiri.

Waganga wa jadi husajiliwa na kupewa leseni za kufanya kazi zao na Halmashari kwa utaratibu wa kiutawala. Ipo sheria ya mwaka 2002 kuhusu Tiba Asilia na Tiba Mbadala (Traditional and Alterntive Medicine Act), lakini Kanuni za utekelezaji wake zilikuwa hazijatengenezwa.

Waziri Mkuu alisema mganga wa jadi ambaye anaweza kuruhusiwa baadaye ni yule ambaye dawa zake za mitishamba au za asili zitakuwa zimethibitishwa na Kitengo cha Uchunguzi wa Tiba Asili cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuwa kweli zinatibu. Mgonjwa naye atatakiwa awe na cheti kutoka hospitali kitakachothitisha maradhi yake na kuwa tiba yake hopitali imeshindikana.

"Waganga hawa ni waongo wakubwa…Siyo lazima kuwa nao. Wangekuwa waganga wa kweli magonjwa mengi yangepungua nchini, lakini magonjwa yapo na sasa wanapiga ramli na kuwa kichocheo cha mauaji.

Mkoa wa Shinyanga unasemekana unaongoza kwa idadi ya waganga wa jadi waliosajiliwa na wako 1,104 na 94 ambao hawakusajiliwa. Wilaya ya Kahama peke yake ina 763.

Waziri Mkuu aliuambia umati uliofurika kwenye uwanja wa Chuo cha Biahshara cha Shinyanga (Shycom) huku akishangiliwa kuwa mapambano dhidi ya mauaji ya Abino ni vita na ndiyo maana anataka ulinzi wa jadi wa Sungusungu urejeshwe kusaidiana na vyombo vya dola kukabiliana na hali hiyo.

Aliwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa kufnya kazi zao kwa ufanisi zaidi na "kujipanga upya na kuteremka hadi ngazi ya chini" kusimamia mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe.

"Inapotokea kuwa Albino au Kikongwe anauawa katika eneo fulani, mimi nitamshukia Mkuu wa Mkoa na kumuuliza kwa nini aliacha hali itokee hivyo. Mkuu wa Mkoa naye atamshukia Mkuu wa Wilaya na vivyo hivyo," alisema.

Aliongeza: "Tukijumuika wote kwa pamoja tutashinda vita hii kama tulivyoshinda vita dhidi ya nduli Idi Amin wa Uganda".

Waziri Mkuu pia alisema atamwomba Jaji Mkuu kuwa zile kesi za mauaji ya Albino ambazo ziko tayari zinapangiwa majaji maalum ili zikamilike na hatima yake ijulikane haraka.


Tangu Juni mwaka 2007 mpaka Novemba mwaka 2008 jumla ya Albino 34 wameuawa nchini kwa imani za ushirikina kuwa eti viungo vyao vinasaidia kupata utajiri. Idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (19) Mara (4) Kigoma (3) Shinyanga (4), Kagera (3) na Mbeya (1). Mwaka huu tayari wameuawa watatu.

Jumla ya vikongwe waliouawa nao kwa kushukiwa wachawi ni 2583 ambapo idadi yao kimkoa kwenye mabano ni Mwanza (696), Shinaynga (522), Tabora (508), Iringa (256), Mbeya (192) Kagera (186), Singida (120) na Rukwa (103).

Ziara ya Waziri Mkuu Pinda katika mikoa ya Kanda ya Ziwa inamalizika leo kwa majumuisho yatakayowahusisha viongozi wa mikoa hiyo. Alianzia Kagera na badaye kutembelea mikoa ya Mwanza, Tabora na Shinyanga. Mkoa wa Mara ulijumuishwa kwa viongozi wake kuhudhuria mkutano wa viongozi Mwanza.
(mwisho)
Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021,
DAR ES SALAAM

*************************************************************
Pinda ataka jino kwa jino
Na Victor Kinambile, Tabora

KATIKA hali ya isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana aliwaambia wananchi kuwa wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) pamoja vikongwe ni hawana budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri mahakama kuwahukumu, watakuwa wanakosea.

Waziri Pinda, ambaye ameanza ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuhamasisha vita dhidi ya mauaji ya vikongwe na albino, aliutaka Umoja wa Vijana wa CCM kuongoza vita hiyo, akisema lina jeshi zuri.

Mauaji ya albino yamekuwa ni tatizo kubwa nchini na hasa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Pamoja na serikali kutangaza hatua kadhaa za kupambana na wauaji hao, bado matukio ya kuuawa kwa watu hao wenye ulemavu wa ngozi yamekuwa yakiendelea kuripotiwa, lakini Waziri Pinda ameenda mbali zaidi katika kukabiliana na tatizo hilo alipotaka wauaji hao wauawe badala ya kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Kauli ya Pinda, ambayo inaweka maswali katika suala la utawala bora, imekuja wakati ambao wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi na kuua vikongwe kutokana na imani za uchawi.

Akihutubia wakati wa kufungua mkutano wa 16 wa Shirikisho la Vyama vya Kuweka na Kukopa (SCCULT) kwenye ukumbi wa Chuo cha Utumishi Umma mkoani hapa, Waziri Pinda alisema iwapo wananchi wataendelea kuwahurumia wauaji hao ambao wanatafuta viungo vya albino wakitegemea mahakama itatenda haki huku nao wakiongeza kasi ya mauaji kwa Watanzania, watakuwa wanakosea.

Hivyo alisema kwamba kuanzia sasa mtu yeyote atakayemuona mtu amemkata shingo au mkono mweziwe basi naye auawe papo hapo hii itakuwa ndiyo dawa kwani vingozi wote tumechoka na mauji hayo.

"Mkimuona mtu akamkata mwingine shingo naye muueni kwani sasa viongozi wote tumechoka... no more, I can't tolerate anymore (imetosha, siwezi kuvumilia tena)," alisema Pinda huku akiwaacha watu midomo wazi.

Aliviomba vyama vya siasa kushirikiana na wananchi kuhakikisha suala hili la mauji linakwisha kwani wauji "tunaishi nao na ni rahisi kulimaliza iwapo tutakuwa kitu kimoja katika kuondoa kashifa hii ambayo imekuwa mbaya kwa nchi yetu".

Aliuagiza Umoja wa Vijana wa CCM kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa kabisa, akisema kuwa ni jeshi zuri ambalo likiamua kutokomeza kabisa mauaji ya vikongwe na ndugu zetu maalbino inawezekana.

"Umoja wa vijana mna jeshi zuri ambalo naamini mkiamua mnaweza kutokomeza mauaji ya wazee wetu pmoja na ndugu zetu maalbno na kazi hiyo nawaagiza muanze leo msisubri auawe mwingine tena," alisema waziri mkuu.

Baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya watu wanaoonekana kuwa ni wa "serikali" waliwafuata baadhi ya waandishi wa habari, akisihi suala hilo lisiripotiwe magazetini kwa madai kuwa kauli hiyo ya Waziri Pinda inaweza kusababisha matatizo.

Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia amekuwa mstari wa mbele kupiga vita mauaji hayo, alitofautiana na Waziri Pinda katika moja ya hotuba zake aliposema kuwa adhabu ya kuua haitofautishi muuaji wa albino na muuaji mwingine na kwamba watakaopatikana na hatia ya kuua albino, atakabiliana na adhabu ya kifo kama ilivyo kwa muuaji mwingine.

Waziri Pinda alionekana kukerwa na mauaji ya albino wakati alipopata taarifa kwamba kuna mama mwingine aliuawa usiku wa kuamkia juzi.

"Nimeambiwa kuwa juzi wilayani Sengerema kuna mama mmoja ambaye ni mlemavu wa ngozi amekatwa mkono na wauaji wakaondoka na mkono huo na tayari mama huyo amekufa," alisema Pinda na kusisitiza kushughulikia wauaji hao.

Akitoa takwimu za mauaji ya vikongwe na malbino alisema mwaka 2003 waliuwawa vikongwe 517, mwaka 2004 waliuawa vikongwe 444, mwaka 2005 (494), 2006 (vikongwe 386), mwaka 2007 (vikongwe 526) na albino sita na mwaka 2008 (vikongwe 526 na albino 28).

Alisema tayari mwaka huu wameuawa albino watatu hivyo kufanya albino na vikongwe waliouawa kufikia kuwa jumla 2,900.

Waziri mkuu ameanza ziara ya siku nne kutembelea mikoa ya Shinyanga, Tabora na Mwanza ili kuhamasisha wananchi watokomeze vitendo vya mauaji ya vikongwe na watu weye ulemavu wa ngozi.

Friday, November 21, 2008

Waziri Mkuu Pinda

Waziri Mizengo Pinda akiwa ndani ya vazi la jadi huku akishika silaha za jadi katika ziara yake ya "kuhimiza maendeleo" mkoani Dodoma hivi karibuni (Picha: Prime Minister's Office).

Asante Faustine's Baraza Blog:

Wednesday, March 19, 2008

Picha Rasmi za Mh. Waziri Mkuu Pinda



Hizi picha mbili ni picha rasmi (Official Portraits) za Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda. Zimetolewa rasmi na ofisi yake.

Monday, February 11, 2008

Mh. Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda

Mh. Rais Jakaya Kikwete na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda
Mh. Rais Kikwete akisalimiana na baba mzazi wa Mh. Pinda, Mzee Xavery Kayanza Pinda, na mama mzazi, Bi Albetina Kasanga.Mke wa Waziri Mkuu, Mh. Pinda, (kushoto) Tunu Rehani Pinda akiongea na mbunge wa Viti Maalum Martha Mlata mara baada ya sherehe za kumwapisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda zilizofanyika ikulu ndogo ya Chamwino Dodoma.

(picha asante Michuzi blog)

Sijui ni furaha gani wazazi wa Mh. Pinda walionayo kumwaona mwanao anakuwa Waziri Mkuu. Mungu awabariki.

Na nasema hivi, jumatatu ya wiki iliyopita, Mh. Pinda alijua atakuwa Waziri Mkuu? Kweli huwezi kujua mipango ya Mungu.

Na wameumbua skandali ya Richmond, je wataumbua skandali ya machimbo ya madini?

Friday, February 08, 2008

Waziri Mkuu Mpya ni Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda!


Maelezo mafupi ya Mh. Pinda Bungeni leo:


WAZIRI MKUU MTEULE MH. PINDA AMESEMA YEYE NI MTOTO WA KWANZA KWENYE FAMILIA YAO NA ANA SHAHADA YA SHERIA YA CHUO KIKUU NA KWAMBA AMEFANYA KAZI KAMA MSAIDIZI WA RAIS IKULU TOKA ENZI ZA MWALIMU KWA MIAKA 7, KWA ALHAJI MWINYI MIAKA 10 YOTE NA MIAKA KAMA MITANO KWA MH. MKAPA KABLA YA KWENDA JIMBONI KWAKE MPANDA KUOMBA KURA KUWA MBNGE MWAKA 2005.