Showing posts with label Peter Owino. Show all posts
Showing posts with label Peter Owino. Show all posts

Friday, August 21, 2009

Update - Hali ya Peter Owino

NDUGU JAMAA NA MARAFIKI,

FAMILIA YA OWINO INATANGULIZA SHUKRANI TELE KWENU NYOTE MLIOTOA HUDUMA YA AWALI/HARAKA KWA KAKA YETU PETER MARA ALIPOFIKISHWA HOSPITALI YA BUGANDO KWA MATIBABU MARA BAADA YA KUVAMIWA NA MAJAMBAZI AKIWA SAFARINI KWENDA SHIRATI KUPITIA BARABARA KUU YA KATI.

KHERI PIA KWA MADAKTARI WOTE WA BUGANDO KWA TIBA NZURI NA MAKINI.

SHUKRANI PIA KWA MARAFIKI NA WATANZANIA WOTE WALIOPATA FURSA KUMJULIA KHALI NA KUTUMA SALAAM ZA TIBA NJEMA NA MAOMBI YA UNAFUU WA HARAKA. MUNGU AWABARIKI.

AIDHA TUNAWASHUKURU MLIOHUZUNIKA ZAIDI NA KUTAKA KUANDAA MICHANGO YA ZIADA ILI KUSAIDIA KTK HUDUMA YA TIBA KWA PETER. NAOMBA NIWAHAKIKISHIE KUWA TUNATHAMINI ARI YA UPENDO HUO LAKINI FAMILIA IMEWEZA NA INAENDELEA KUMUDU HUDUMA ZOTE ZA TIBA VIZURI KWA SASA. PETER AMETOKA HOSPITALI NA ANAPONA HARAKA NYUMBANI.

FAMILIA HAIJAANDAA UTARATIBU WOWOTE WA MICHANGO NA TAFADHALI MASHAURI KAMA HAYA LAZIMA YAWE NA IDHINI YA FAMILIA.

KWA UPENDO NAWASHUKURU NYOTE, MUNGU AWABARIKI.
Maina Ang'iela Owino

k.n.y FAMILA YA OWINO

Friday, August 14, 2009

Mchango wa Kumsaidia - Peter Owino

MCHANGO WA KUMSAIDIA MWENZETU

PETER OWINO


Reading uingereza tunapenda kutoa Taharifa kwamba, Daftarin la kumchangia Peter Owino Aliyevamiwa na majambazi mwanza juzi tarehe, 11/07/09 limefunguliwa Bongo Flavour Reading.

Yeye mwenyewe Bado anaendelea na matibabu katika hospitali ya Rufaa ya bugando (mwanza) na mipango ya kunsafirisha kwenda Hospitali ya taifa muhimbili inafanyika.

Yeyote anakaribiswa kutoa chochote kwa kwenda bongo falaour au kulipia kwa njia ya benki.

Kwa taharifa zaidi Piga simu

01189585878

07900040288

07760200372

07806792348

Kutoa ni moyo usambe ni utajiri

Wednesday, August 12, 2009

Peter Owino na Familia Wavamiwa na Majambazi Nzega

Kutoka Michuzi Blog:

HABARI ZA HUZUNI ZINAWAKILISHA KUWA NDUGU YETU PETER ANG'IELA OWINO ALIYEKUWA ANASAFIRI BARABARA KUU YA KATI AMEVAMIWA NA MAJAMBAZI MAENEO YA NZEGA AKIWA NA MKE NA WATOTO WAWILI WA MIAKA MIWILI NA MWINGINE MIEZI TISA NA WOTE KUKATWA NA MAPANGA VIBAYA NA YEYE YUKO MAHTUTI HOSPITALI YA BUGANDO, MWANZA.

NDUGU OWINO ANAISHI UINGEREZA NA AMEWASILI JUZI AKIWA LIKIZO FUPI KUELEKEA NYUMBANI SHIRATI, RORYA.

MAJAMBAZI HAO WAMEWANYANG'ANYA KILA KITU WALICHOKUA NACHO HADI LISHE ZA WATOTO HAO WADOGO WALIOJERUHIWA PIA. POLISI NZEGA WAMETHIBITISHA KUTOKEA KWA TUKIO HILO LA HUZUNI, NA HABARI ZAIDI ZINAFUATA.

PETER OWINO NI MMOJA WA WATU WALIOTOA MAPOKEZI NA HIFADHI KWA WATANZANIA WENGI WALIOKWENDA KUSOMA UINGEREZA TOKA MIAKA YA 1990
TUMWOMBEE NAFUU YA HARAKA.