
Showing posts with label Safarini Dar. Show all posts
Showing posts with label Safarini Dar. Show all posts
Tuesday, July 07, 2015
Wednesday, December 13, 2006
Nilitolewa Ushamba Dar - Text Messaging

Haya nimezungumza habari ya watu wengi kuwa na cell phone Dar. Sasa kuna hiyo kitu 'text messaging'. Naona ndo mawasiliano ya bei rahisi kuliko voice call. Kila mtu anajua kutuma text message, isipokuwa mimi!
Niliazima simu ya mama yangu. Watu walikuwa wananitumia text message. Doh, niliweza kuzisoma, lakini nilishindwa kutuma jibu! Niliona aibu kweli. Dada moja kanipigia na kusema, 'Nilivyona hujajibu niijua hujui kutumia texting!"
Ni kweli nilikuwa najibu watu kwa kuwapigia simu na of course ni ghali. Japo nina cell phone miaka mingi na nimeona hiyo text feature, huwa nasoma message na kuinua phone na kupiga kama inabidi nijibu. Nimeona vijana na watoto wadogo wanajua kutumia lakini haikuniingia kuwa nami nitumie. Na mara nyingi kwenye TV utasikia, send a Text message to halafu wanakupa namba. Lakini hata siku moja sijajaribu! Jamani USHAMBA! Ni kama vile compyuta. Mtu unaona lakini unaogopa kutumia! Ukianza kutumia unasema, Kumbe ni rahisi hivyo!
Sasa nimerudi Boston, na natazama cell phone yangu. Na ndo nimekuwa na-explore jinsi ya kutumia hiyo text message. Nimeanza kupatia. Lakini naomba mnieleza jinsi ya kuweka space kati ya maneno! Kwa sasa naweka period kati ya maneno.
Kumbe ni simple na mawasiliano rahisi. Nimeanza kupenda text messaging. Ushamba wa text messaging umenitoka.
Thursday, December 07, 2006
Dar es Salaam kuna Joto!

Jamani Dar kuna joto! Loh! Unapigwa nayo ukishuka tu kwenye ndege. Siku mbili za mwanzo nilivyokuwa huko niliona joto kweli. Ni kweli kuwa Novemba/Desemba joto unazidi Dar, lakini kwa kweli nilikipata. Kwa siku nilikuwa na kunywa maji mengi kweli, na vinywaji vingine. Jamani nilitoka jasho zile siku za mwanzo.
Halafu mara nyingi umeme ulikatika kwa hiyo feni na Air Conditioning hazifanyi kazi, kwa hiyo unaendelea kuchemka. Unakwenda ofisini mwa mtu halafu unabakia kujipepea na gazeti shauri ya joto. Asubuhi, umeme ulikuwa unakatika saa 12 kamili. Basi unaamka kwa sababu feni chumbani unazimika na joto unaanza kuzidi. Hata hivyo siku zilivyopita nilianza kuzoea joto.
Haya nilivyondoka nilianza kusikia baridi kwenye ndege. Nilitamani ningebaki Bongo nifaidi joto. Na kufika Boston nilikaribishwa na snow (theluji)! Unatoka kwenye joto kuingia kwenye snow.
Basi nimerudi Boston na ka-tan. Nilikuwa navaa sleveless Dar, basi unaona kabisa mikono umekuwa Dark. Sehemu zilizokuwa zimefunikwa zilikuwa light. Wazungu kazini waliniuliza kama nimepata 'sunburn'. Nikawaambia hapana ni tan, na sisi weusi tunapata tan pia. Lakini wacha nifaidi hiyo Vitamin E ya jua, maana kipindi hiki cha winter jua unaliona tu. Mambo ya kukaa nje na mwili kuganda shauri ya baridi hatutaki.
Thursday, November 30, 2006
Kila Mtu ana cell Phone Dar
Jamani, mawasiliano ya simu ni rahisi sana Dar. Cell phone nyingi, makampuni yanashindana kupata wateja, phone cards zinauzwa kila mahala, tena bei si mbaya hata shilingi 500/- unapata! Watu wengi wanazo! Mbona cell phone USA ni ghali sana, tena ukiweka kwenye credit kadi ndo unalaguliwa kabisa! USA wanaweza kujifunza kutoka Bongo!
Lakini jamani barabara mbovu sana Dar, tena sana! MAVUMBI!
Baadaye!
Lakini jamani barabara mbovu sana Dar, tena sana! MAVUMBI!
Baadaye!
Sunday, November 26, 2006
Diary from Dar es Salaam
Haya, ni siku yangu ya tano Dar. Malalamiko yangu makuu ni:
Ukosefu wa umeme
Barabara mbovu
Maji shida
Mbu!
Nimetafunwa na mbu! Na nimetumia mosquito repellent. Labda wamekuwa sugu. Lakini wamekunywa damu ya Boston!
Niko Mbezi kwenye cafe iliyoko barabarani kabisa. Kwa kweli computer zao ni safi sana, kuliko cafe iliyoko karibu na nyumbani. Wale wana computer nzee na slow.
Vumbi na michanga!
Lakini jana nilikuwa kwenye sherehe ya arusi. Jamani kuna catering companies siku hizi! Juzi nilikuwa kwenye Graduation party, ilikuwa kama arusi Ama kweli Tanzania kumekuwa Party Culture!
Ukosefu wa umeme
Barabara mbovu
Maji shida
Mbu!
Nimetafunwa na mbu! Na nimetumia mosquito repellent. Labda wamekuwa sugu. Lakini wamekunywa damu ya Boston!
Niko Mbezi kwenye cafe iliyoko barabarani kabisa. Kwa kweli computer zao ni safi sana, kuliko cafe iliyoko karibu na nyumbani. Wale wana computer nzee na slow.
Vumbi na michanga!
Lakini jana nilikuwa kwenye sherehe ya arusi. Jamani kuna catering companies siku hizi! Juzi nilikuwa kwenye Graduation party, ilikuwa kama arusi Ama kweli Tanzania kumekuwa Party Culture!
Subscribe to:
Posts (Atom)