Showing posts with label Slades Club. Show all posts
Showing posts with label Slades Club. Show all posts

Wednesday, August 06, 2008

Wazee Vijana

Jana jioni nilitembelea klabu fulani hapa Boston, inaitwa Slades. Siku za Jumanne wanakuwa na kama Karaoke, lakini unaimba na bendi laivu.

Nilishangaa kuona idadi ya wazee pale klabuni waliopanda jukwaani! Kweli hapa Marekani Uzee ni akili yako tu.
Kaka Jay C. anaijiona yeye ndiye marehemu James Brown Sasa. Lazima niseme anaimba kama James Brown anacheza kama yeye na cheki hiyo 'process' ya nywele kama James Brown! Kama wanatengeza sinema juu ya maisha ya James Brown huyu anafaa kuwa James Brown!

Hao vijana walikuwa wanapiga Saxophone kali!

Huyu walimwita Mpwa wa James Brown, aliimba "I Feel Good"

Huyo Babu mwenye miaka 80+ alimba wimbo kutoka miaka ya 1940's "It Don't Mean a Thing if it Ain't Got that Swing!"

Huyu Babu aliimba wimbo 'Ain't No stoppin us now!'

Bluuzi inanoga

Wazee wakicheza bluuzi huko Ron Murphy anaimba Daddy's Home