Wednesday, August 06, 2008

Wazee Vijana

Jana jioni nilitembelea klabu fulani hapa Boston, inaitwa Slades. Siku za Jumanne wanakuwa na kama Karaoke, lakini unaimba na bendi laivu.

Nilishangaa kuona idadi ya wazee pale klabuni waliopanda jukwaani! Kweli hapa Marekani Uzee ni akili yako tu.
Kaka Jay C. anaijiona yeye ndiye marehemu James Brown Sasa. Lazima niseme anaimba kama James Brown anacheza kama yeye na cheki hiyo 'process' ya nywele kama James Brown! Kama wanatengeza sinema juu ya maisha ya James Brown huyu anafaa kuwa James Brown!

Hao vijana walikuwa wanapiga Saxophone kali!

Huyu walimwita Mpwa wa James Brown, aliimba "I Feel Good"

Huyo Babu mwenye miaka 80+ alimba wimbo kutoka miaka ya 1940's "It Don't Mean a Thing if it Ain't Got that Swing!"

Huyu Babu aliimba wimbo 'Ain't No stoppin us now!'

Bluuzi inanoga

Wazee wakicheza bluuzi huko Ron Murphy anaimba Daddy's Home

3 comments:

Anonymous said...

Babu ana mika 80 na bado wamo! Lakini Da Chemi usisahu Bongo tuna Bi Kidude ana miaka 120 na bado anaimba!

Anonymous said...

huo ndio utamu wa maisha da chemi,life is beautifull but is very short,sasa basi hata ukiwa una umri zaidi ya miaka 80.wewe lazima enjoy tu je?utasema nini kwa mungu kwa maisha ya baadae?ukiwa na afya njema na siha nzuri wewe fanya mambo.da chemi kisayansi ni vizuri sana binaadamu kuimba ,kila siku hiyo pia inasaidi mapafu yako pia furaha ya kimaisha na kupunguza stress zako..hebu wewe pia jaribu kila siku asubuhi unapo amka jaribu kuimba mara kwa mara..u will make your day to be happier ..pia kama wewe chemi ni mnene ..punguza unene wako kwa kuimba beti nyingi kwa nusu saa kila siku...thats my advice to you....

Anonymous said...

Sijui kwa nini huko Bongo mtu akifikisha miaka 50 tunamwona kama amekwisha na hana maisha tena. Hebu wacheki hao wazee huko US wanavyo starehe. Hivi kuna Hall za kustarehe wazee hivyo kweli?