Showing posts with label Bank of Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Bank of Tanzania. Show all posts

Thursday, December 29, 2011

Mnada wa Hazina Haukuzaa Matunda!

Kwa wanaoelewa habari ya Bonds, hii habari inatisha. Yaani Benki kuu wameuza bonds chini ya asilimia 5% tu!

*****************************************************************
DAR ES SALAAM (Reuters) - A Tanzanian 10-year Treasury bond auction was hugely undersubscribed on Wednesday, with the central bank selling less than 5 percent of the amount of bonds on offer.

The Bank of Tanzania had offered 20 billion shillings of the fixed-rate Treasury bonds with an 11.44 percent coupon.

It received bids worth just 0.926 billion shillings and accepted all of them, making the auction one of the country's worst bond sales in recent history.

The central bank said the weighted average yield to maturity in the auction was 16.9791 percent.
 
The central bank rejected all bids at a Treasury bond sale on December 15 for the second time in four months as investors sought high yields that the bank was unwilling to pay.

Tuesday, March 24, 2009

Wizi Bank of Tanzania

Yaani wanasingizia sikukuu ya Maulidi!!! Kweli watu wana mambo!

**********************************************

BoT hit by another mysterious cash loss


THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

CONTROVERSY surrounds the mysterious disappearance of a large consignment of local currency notes with a value running into millions of Tanzanian shillings, as it was being airlifted into the country from Germany on a Qatar Airways flight.

Sources within the Bank of Tanzania (BoT) have confirmed the apparent large-scale theft which was discovered on arrival at the Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam early last week.

It has yet to be established exactly at what point the consignment of bank notes got stolen whether it was in Germany, where the notes were manufactured; in Doha, where the flight made a stopover; or at the final JNIA destination in Dar es Salaam.

According to THISDAY findings, the consignment contained crisp new bank notes of 10,000/- denomination. However, the exact number of such notes involved and hence the total value of the package could not be immediately verified.

’’The consignment arrived at the airport in Dar es Salaam on the evening of Monday, March 9. But because the following day was a Maulid holiday, it could not be dealt with until Wednesday, March 11. That’s when it was discovered that the notes were gone,’’ said an informed BoT source.

It is understood that besides the new 10,000/- notes, the consignment also contained a substantial amount of old local currency notes that had long been removed from circulation.

Said the source: ’’The old notes were under audit query...during an earlier auditing exercise, the auditors wanted to know why these notes had not been returned for so many years since being sent to the printers overseas because of various technical problems.’’

But it remains unclear of what use the old notes long out of circulation were expected to be at this moment in time, or whether the government or central bank has received or is expecting any compensation from the company manufacturing the notes.

The discovery of a consignment of defective Tanzanian currency notes with a total value of 3.5bn/- back in 2001, led to serious repercussions including the launch of an official investigation by the then Prevention of Corruption Bureau (PCB).

However, no arrests or prosecutions were ever made.

The notes were printed by the German company Glesecke & Devrient Gmbh, on behalf of the Bank of Tanzania (BoT). They were of 1,000-shilling denomination, amounting to a total value of $3,237,492.

Following this scandal, the government vetoed central bank plans to award another print order to the same German firm, while the defective notes were said to have been quietly withdrawn from circulation.

Wednesday, January 28, 2009

Makubwa Benki Kuu!

(picha ya juu kutoka Michuzi Blog)
Bank of Tanzania Personnel and Administration director Amatus Joachim Liyumba (R) and the bank`s Projects Manager, Deogratius Dawson Kweka,at the Kisutu Resident Magistrate`s Court in Dar es Salaam yesterday.


Watu wawajibike sasa huko Bongo! Hii Kali!

********************************************

Kutoka ippmedia.com

BoT Yatikiswa

2009-01-28 11:00:08
Na Richard Makore

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, jana alipandishwa kizimbani akiwa na mfanyakazi mwenzake wakituhumiwa kwa kosa la kutumia madaraka yao vibaya ya utumishi wa umma na kuisababishia serikali hasara ya Sh. 221,197,299,200.95 kupitia ujenzi wa maghorofa pacha ya benki hiyo.

Sambamba na Liyumba, mwingine aliyesomewa mashitaka hayo na Mwendesha Mashitaka kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), John Lubangila, ni aliyekuwa Meneja wa Mradi wa ujenzi huo, Deogratius Kweka.

Watuhumiwa hao wawili walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana mchana wakiwa katika gari la Takukuru lenye namba za usajili T 319 ATD aina ya Toyota Land Cruiser la rangi ya kijani.

Aidha, kabla ya kusimamishwa kizimbani, watuhumiwa hao waliendelea kukaa ndani ya gari katika viwanja vya mahakama kwa takribani saa tatu, ndipo watolewa na kuingizwa mahakamani.

Baada ya kupanda kizimbani, ghafla watuhumiwa walianza kutokwa na jasho kali hali iliyowasababisha muda wote kujifuta kwa kutumia vitambaa vyao.

Aidha, waliingia kizimbani wakiwa wameshika chupa za maji na kutaka kwenda kusimama nazo wakati wanasomewa mashtaka, lakini askari polisi alitokea na kuyachukua.

Mbali na makosa ya kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya fedha, pia walishitakiwa kwa kutoa maamuzi bila kushirikisha Bodi ya Wakurugenzi wa BoT pamoja na kukiuka sheria ya manunuzi ya serikali na sheria ya uendeshaji wa benki hiyo.

Mwendesha Mashtaka aliiambia mahakama kuwa walitenda makosa hayo kati ya mwaka 2001- 2006.

Watuhumiwa hao walisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi, Khadija Msongo, wa mahakama hiyo.

Hakimu Msongo aliiambia mahakama kuwa dhamana ya watuhumiwa hao ipo wazi na itatakiwa kutolewa thamani ya nusu za fedha zinazodaiwa kupotea.

Nusu ya fedha hizo ni sawa na zaidi ya Sh. bilioni 110 ambapo zikigawanywa kwa watuhumiwa wawili, kila mmoja alitakiwa kutoa fedha Sh. bilioni 55 au mali isiyohamishika inayolingana na kiasi hicho cha fedha.

Mshtakiwa namba moja, Liyumba, alianza kuwasilisha nyaraka za mali mbalimbali ili aweze kupata dhamana, lakini upande wa mashtaka ulioomba mahakama kusitisha zoezi hilo.

Upande wa mashtaka ulidai kuwa unaomba hivyo ili upate muda wa kupitia nyaraka hizo ili kuona kama sio feki na zina thamani ya fedha zinazotakiwa.

Mahakama ilikubaliana na upande wa mashtaka na hivyo kusitisha dhamana hiyo na watuhumiwa kupelekwa rumande hadi Februari, 10 mwaka huu.

Majengo ya BoT yamekuwa ni gumzo kubwa nchini tangu wakati wa utawala wa awamu ya tatu, huku kukwa na taarifa kwamba ghama yake ni ghali kuliko ujenzi katika miji mikubwa ya mataifa ya magahribi. Hadi sasa inakisiwa kwamba ujenzi huo umekwisha kugharimu Sh bilioni 700.

SOURCE: Nipashe

Monday, September 22, 2008

Skandali nyingine Bank of Tanzania (BoT)






Kutoka kwa Mzee wa Sumo (Mpoki Bukuku) Blog:

" Hii ni kutoana nishaji jamani na ukiukwaji haki za wanawake yaani wengine wameamua kutoa wigi la urembo kujikinga na fedheha! Sijui wengine walikuwa na swaum? " - Mpoki Bukuku akizungumzia picha alizopiga.

TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.

Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.

Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.

Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.

Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.

Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.

Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002. Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.

Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.

Monday, August 18, 2008

Taarifa ya Ikulu - EPA

Taarifa ya Ikulu kuhusu EPA


DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail : press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120
DAR ES SALAAM.Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo (Jumatatu, Agosti 18, 2008) amepokea rasmi ripoti ya uchunguzi wa upotevu wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Nje (External Payments Accounts - EPA) katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Rais Kikwete amekabidhiwa ripoti hiyo na Mwenyekiti wa Timu iliyokuwa inafanya uchunguzi huo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson P.M. Mwanyika.Mwanasheria Mkuu huyo alifuatana na wajumbe wengine wa Timu hiyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Saidi Mwema na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Edward Hosea.

Rais amewashukuru na kuwapongeza wajumbe wa Timu hiyo kwa kazi kubwa na ngumu lakini nzuri.Rais, baada ya kuwa ameisoma na kuitafakari ripoti hiyo, ataitolea maamuzi katika siku chache zijazo, na taarifa rasmi ya maamuzi hayo ya Rais itatolewa kwa wananchi.

Timu hiyo iliundwa na Rais Kikwete Januari 9, mwaka huu, 2008 katika tangazo rasmi lililotolewa kwa waandishi wa habari na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo.Wakati anaunda Timu hiyo, Rais aliipa muda wa miezi sita kukamilisha kazi yake, ambayo ilikuwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa fedha zilizolipwa isivyo halali zinarudishwa.

Rais aliunda Timu hiyo baada ya kuwa amepitia Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Mwaka wa Fedha 2005/06 za EPA katika Benki Kuu Tanzania (BOT), uliofanywa na Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young, kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.Kampuni hiyo ya Ernst and Young iliombwa na Serikali kuifanya kazi hiyo.

Iliianza Septemba, 2007 na kumalizika Desemba, mwaka huo huo, 2007. Rais Kikwete alikabidhiwa Taarifa hiyo Januari 7, mwaka huu, 2008 na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Siku ya tatu, baada ya kuwa ameisoma na kuifanyia kazi, Rais aliitolea maamuzi Taarifa hiyo, ikiwa ni pamoja na kuunda Timu ya Mwanyika.

Imetolewa naKurugenzi ya Mawasilia ya Rais,

Ikulu,DAR ES SALAAM.

18 Agosti, 2008

Tuesday, May 27, 2008

Serikali Inajikanganya - Kifo cha Dk. Ballali

Misa ya Kumwombea Mzee Ballali huko Washington D.C. (picha kutoka Michuzi Blog)

Wadau, lazima niseme kuwa bado kuna maswali mengi kuhusu kifo cha Mzee Ballali.

************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Serikali inajikanganya kifo cha Ballali - Slaa

2008-05-27

Na Simon Mhina

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amesema hoja za Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Benard Membe kwamba serikali haihusiki na kifo cha Dk. Daudi Ballali, hazijaisaidia serikali, badala yake zimezidi kuleta mkanganyiko.

Alisema yeye pamoja na wapinzani wengine, walijenga hoja kwamba ni kwa nini wanaihusisha serikali na kifo hicho, tofauti na Bw. Membe ambaye amekanusha bila kujibu hoja zao na wala hakutoa maelezo ya msingi.
Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alisema waziri huyo amezidisha kiwango cha wasiwasi walichonacho watanzania, pale aliposhindwa kutoa maelezo kwamba Dk. Ballali alikuwa amelazwa hospitali gani na ugonjwa gani.

Alisema hoja ya Bw. Membe kwamba wanaotoa tuhuma dhidi ya serikali wanafanya hivyo kwa hisia, haina msingi na inadhihirisha jinsi waziri huyo anavyobabaika. ``Yaani ugonjwa wa mtu mkubwa mwenye tuhuma nzito kama Ballali, umefichwa, kifo chake kimefichwa, mazishi yake yamefichwa, hata Maiti yake haikuonekana, halafu anasema tuhuma zetu ni hisia? Huu ni upotoshaji mkubwa na kuzidi kujikanganya,`` alisema.

Mbunge huyo alisema kitu ambacho kingeweza kuinasua serikali katika tuhuma hizo, ni Bw. Membe kutaja sehemu aliyokuwa amelezwa Dk. Ballali. ``Tangu lini hospitali ikawa ni sehemu ya siri, kwa nini hawataki kusema?`` Alihoji.

Alisema madai aliyotoa waziri huyo kwamba mwenye vielelezo toka kwa daktari vinavyoonyesha kwamba Dk. Ballali alikufa kwa sumu avitoe, au yanaonyesha kwamba kweli kifo cha Gavana huyo wa zamani wa BoT kilipangwa. ``Mtanzania wa kawaida atawezaje kumpata daktari aliyemtibu Ballali wakati hata hospitali alipokuwa amelazwa panafichwa?

Kumbe wameficha kwa makusudi ili Watanzania washindwe kupata vielelezo?`` Alihoji na kuongeza: ``Serikali haihitaji vielelezo, bali ndiyo iliyofanya njama za kuhakikisha hakuna kielelezo chochote ambacho kinahusiana na kifo hicho kinachoweza kupatikana.``

Alisema kama kweli serikali inasisitiza kwamba haihusiki, itaje hospitali ambayo Dk. Ballali alikuwa akitibiwa na ugonjwa uliomsibu. ``Bw. Membe anasema mwenye vielelezo apeleke? Kazi yake kama waziri wa Mambo ya Nje ni ipi hasa?
Yeye ndiye alitakiwa azungumze na Balozi wetu kule Marekani ili aeleze habari za ugonjwa na baadaye kifo chake, kama mtu mkubwa kama Ballali anaweza kufikwa na kifo nchi za nje bila watu kujua, sembuse mtu wa kawaida?`` Alihoji.

Dk. Slaa alisema ili serikali ijisafishe, ni vizuri ikasema ni kwa nini hata hapa mjini, matanga ya marehemu huyo yalikuwa ya siri na majirani walikatazwa kuingia huku waandishi wa habari wakifukuzwa.

``Tunataka iundwe tume huru ya kuchunguza kifo hicho, kwa vile hadi sasa serikali haijatoa maelezo yanayojitosheleza. Tunataka tume kwa vile pesa za EPA bado ziko mikononi mwa mafisadi, ambao huenda ni marafiki wakubwa wa serikali,`` alisema.

Thursday, May 22, 2008

Kifo cha Mzee Ballali kimetangazwa Rasmi Washington D.C.


Daudi Timothy Said Ballali

Viewing: PrivateService: May 23, 2008 @ 10AM
Location: St. Stephen The Martyr

Daudi Timothy Said Ballali
On May 16, 2008 of Washington, D.C.
Husband of Anna Ballali

Mass of Christian Burial will be offered on May 23, 2008 at 10AM at St. Stephen, Washington, D.C.
Interment Gate of Heaven Cemetery


http://www.devolfuneralhome.com/index.asp?sid=6&formid=102&serviceid=960

REST IN ETERNAL PEACE, Mzee Ballali.

Eti Balali Amefariki hapa Boston, MA?

Wadau, tangu juzi nimepigiwa simu na wadau wengi kuniuluiza kama Mzee Balali alikuwa hapa Boston, Massachusetts kwa matibabu. Ukweli sijui na wala sikuwahi kusikia kama yupo hapa. Niliambiwa kuwa alifariki Washingtion D.C. siku ya Ijumaa iliyopita.

Kwa kawaida mtu akifariki hapa kuna kuwa na matangazo kwenye gazeti kama Boston Herald na Boston Globe. Bado sijaona Obituary yake. Kama nikiona nitaiposti hapa.

Sasa nashangaa jana Ippmedia.com walisema kuwa serikali imetangaza kuwa Mzee Balali alifariki Washington D.C., leo wanasema amefariki hapa Boston. Niko confused sasa. Juu ya hayo kuna mtu alisema Mzee Balali yu mzima na anategemea kuwasili Dar es Salaam kesho! Heh!

Mnaonaje hii issue wadau?

***********************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Yes, Ballali is dead - BoT

2008-05-22

By Angel Navuri and Correspondent Njonanje Samwel

The Bank of Tanzania confirmed yesterday that its immediate former governor, Daudi Ballali, is dead. A section of the media broke the surprise sad news yesterday morning, as the nation awaited word on developments relating to a saga on grand corruption allegations involving him.

A statement issued by BoT said the office of central bank Governor Benno Ndulu had learnt with shock on Tuesday night that Ballali died on Friday last week in Boston, the US, where he was understood to have been undergoing treatment.

``We at the Bank join the late Ballali`s family in mourning his death and pray to God that his soul rest in eternal peace,`` read part of the statement. Neither Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe nor his deputy, Seif Ali Iddi, could be reached for comment on the issue yesterday.

However, a man who identified himself as a close Ballali relative said in an interview with this paper that the former governor died last Friday in the US ``after long but undisclosed illness``. At the residence of Ballali's sister at Boko in suburban Dar es Salaam, The Guardian found scores of people assembled to mourn his death.

The woman was identified only as Eliza, while the people at her residence were said to be family members, close relatives, family friends and neighbours. ``It`s true that Ballali is no more. We are gathered here as family members to discuss what to do,`` said an informer, who flatly refused to give his name.

According to a close Ballali relative, family members were having a hard time planning how to break the sad news to the former BoT chief's ailing mother. She is said to have heart problems and is currently cared for at Eliza`s residence.

Ballali was taken to South Africa last year after developing health problems. He was later flown to Boston for further medical attention, where he was subsequently admitted. Last December doctors there released him after his condition improved, instructing him to stay home for three months - until March this year - before returning to the hospital.

But his condition soon reportedly began deteriorating, forcing his doctors to order his re-admission. President Jakaya Kikwete relieved Ballali of his duties after revelations that the former governor had occasioned a loss amounting to billions of shillings through shady dealings with phony companies in 2005. Sooner after, the president named Prof Ndulu as Ballali's successor at the central bank.

Ernst & Young, the international auditing firm contracted by the government to screen the central bank`s accounts, revealed that payments amounting to 133,015,186,220/74 were dubiously made to 22 domestic companies under the External Payments Arrears (EPA) account scheme in 2005. Some 90,359,078,804/- out of this was paid to 13 companies on the strength of fake or forged documents.

Another nine firms were said to have been paid an equivalent of 42,656,107,417/- without any documents to support their claims.

Wednesday, May 21, 2008

Habari zaidi kuhusu Kifo cha Balali

Hayati Dk. Daudi Balali (picha kutoka Michuzi Blog)

Written by KLHN/Tanzania Daima

Wednesday, 21 May 2008

KLH News imeweza kuthibitisha kwa uhakika kuwa misa ya kumuombea Marehemu Balali inatarajiwa kufanyika saa nne asubuhi katika Kanisa la Mt. Stephen Washington DC. Kutoa heshima za mwisho kutafanyika katika kanisa hilo hilo na itakuwa si kwa hadhara nzima.

Mwili wake unatarajiwa kulazwa kaburini kwenye makaburi ya "Gate of Heaven" huko hukoJamaa wa karibu wa Ballali walioko Dar es Salaam na Washington walilithibitishia Tanzania Daima kuhusu kutokea kwa msiba huo.

“Ni kweli amefariki nyumbani kwake Ijumaa usiku. Na sasa hivi tuko katika maandalizi ya kwenda funeral home (taasisi ya kuandaa shughuli zote za mazishi) kwa ajili ya kuanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msiba,” alisema ndugu wa karibu wa Ballali kutoka Washington.

Habari zaidi zinaeleza kwamba, tayari familia ya gavana huyo wa zamani wa BoT imeshaitaarifu serikali kuhusu kutokea kwa msiba huo na kwamba taarifa rasmi kuhusu kifo hicho zitatolewa leo hii.Ndugu mwingine wa karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima majira ya saa 4:00 usiku jana alisema mazishi ya gavana huyo wa zamani wa BoT yanatarajiwa kufanyika Ijumaa hii huko huko Marekani.

Mmoja wa wanasiasa aliye karibu na familia ya Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana alithibitisha pia kupokea taarifa za kifo cha Ballali kutoka kwa mkewe, Anna Muganda. Ndugu mmoja wa Ballali alipoulizwa na Tanzania Daima sababu za kushindwa kutangazwa kwa taarifa za kifo hicho mapema alisema walilazimika kufanya hivyo ili wapate fursa ya kuwasiliana na serikali kwanza na kisha ndugu, jamaa na marafiki wa familia yao kabla ya habari hizo kusambazwa.

Badhi ya jamaa za Ballali waliozungumza na Tanzania Daima walisema kulikuwa na wasiwasi kwamba kifo cha gavana huyo wa zamani wa BoT kikawa kikawa si cha kawaida.“Kuna wasiwasi kwamba huenda alilishwa sumu wakati akiwa nchini mwaka jana na hili limekuwa likizungumzwa sana ndani ya familia,” alisema mmoja wa jamaa za karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana.

Taarifa za kuwapo kwa wasiwasi wa Ballali kulishwa sumu zilipata kusikika mwaka jana na wakati fulani ilielezwa kwamba alipelekwa Marekani kwa matibabu kutokana na sababu hizo.

Habari za kifo hicho cha Ballali ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete Januari mwaka huu zimekuja siku chache tu baada ya serikali kupitia Ofisi ya Rais Ikulu kutoa tamko la kutangaza kwamba ilikuwa haimtafuti gavana huyo wa zamani wa BoT.

Tamko hilo la serikali lilitolewa mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu.Rweyemamu alisema kuwa serikali ina mkono mrefu na iwapo itafikia hatua ya kumtafuta gavana huyo wa zamani wa BoT ili aje atoe maelezo yake kuhusu wizi wa zaidi ya shilingi bilioni 133 uliogundulika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) haitashindwa kamwe kumfikia alipo.

Alisema kutokuwepo nchini kwa Ballai, au kutojulikana alipo, si jambo linaloisumbua serikali kwa sasa kwa sababu hivi sasa yeye ni raia wa kawaida, hivyo anao uhuru wa kuishi popote anapopenda.“Serikali haimtafuti Ballali (kwa sasa), lakini ikiamua kufanya hivyo haitashindwa.

Kwanza ni private citizen (raia huru) siyo mwajiriwa wa serikali tena,” alisema Rweyemamu na kuongeza kuwa, mkono wa serikali ni mrefu hautashindwa kumpata Ballali iwapo itamhitaji. kifafanua zaidi, alisema baada ya kutenguliwa kwa uteuzi wake, serikali iliunda timu ya kuwachunguza watuhumiwa wa EPA, kuhakikisha fedha zilizoibwa zinarudi na kuwachukulia hatua waliohusika, akiwemo Ballali.

Alisema: “Ninachofahamu ni kwamba, timu iliyopewa kazi kuhusu ubadhirifu wa EPA inaendelea na kazi yake na tunaona jinsi fedha zinavyorudishwa.”Mkurugenzi huyo pia alikiri kwamba serikali haifahamu hospitali aliyokuwa akitibiwa Ballali, licha ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo, kukaririwa akisema alimtafuta Ballali bila mafanikio alipokuwa jijini Washington, Marekani.

“Kwa kweli sifahamu hasa Ballali alikuwa akitibiwa katika hospitali gani, lakini najua alikuwa nchini Marekani katika Jimbo la Boston, ila hospitali kwa kweli siijui.“Lakini huyu ni mtu huru hivyo anaweza kuishi popote… huyu ana nyumba yake nchini Marekani… yupo huko anaishi na familia yake,” alisisitiza Rweymamu katika ufafanuzi wake.

Wiki iliyopita, ikiwa ni siku chache tu baada ya taarifa hiyo ya Ikulu, vyombo kadhaa vya habari viliandika habari zilizokuwa zikieleza kuwa makachero kutoka hapa nchini, walikuwa wamekwenda nchini Marekani katika miji ya Boston na Washington kufuatilia nyendo na maisha ya gavana huyo wa zamani.

Kwa mujibu wa habari hizo, ambazo zilikariri taarifa za ndani kutoka serikalini, makachero hao walikuwa wamekwenda huko ili kujua mahali anakoishi ili wakati wa kumhitaji utakapofika iwe rahisi kumpata. Ballali aliondoka nchini, Agosti mwaka jana kwenda Marekani kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa matibabu, na tangu wakati huo taarifa zake zilikuwa ni zenye utata mkubwa.

Mara ya mwisho kwa Ballali kuonekana hadharani ilikuwa ni Julai 12 mwaka jana alipozungumza na wanahabari na akasema alikuwa hatarajii kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu.

Katika mkutano huo, Ballali alisema madai ya ubadhilifu yanayotolewa dhidi yake ni uzushi na uongo mtupu.Huku akionekana kujiamini alisema; “Niko Comfortable, moyo wangu mweupe, ari yangu ya kazi iko juu kwani tuhuma hizo ni uongo na uzushi mtupu na siwezi kujiuzulu kwa tuhuma zisizo na ushahidi.

“Tuhuma zote dhidi yangu ni za uongo mtupu. Kwanza sijui zimetoka wapi, nani mtunzi na kwanini amefanya hivyo. Hilo tunawaachia wanaofanya uchunguzi na naamini siku moja atajulikana na ukweli utajulikana, lakini mimi siwezi kujiuzulu kwa mambo ya uzushi,” alisisitiza.

Kashfa ya BoT kupitia mtandao wa Internet, uliibuliwa mara ya kwanza Bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (CHADEMA).Akichangia maoni ya kambi ya upinzani wakati wa mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani imefarijika baada ya Waziri wa Fedha kukiri kufahamu taarifa aliyoitoa Bungeni kuhusu ubadhirifu mkubwa ndani ya BOT unaomgusa Ballali, pamoja na wafanya biashara wengine wakubwa akiwemo Mbunge wa Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya (CCM), kupitia kampuni anayoimiliki.

Dk. Slaa alisema Dk. Mzindakaya alichukua mkopo kwa shughuli za kampuni yake ya SAAFI wa sh 6.217 bilioni, uliogawanyika kama ifuatavyo. Alisema aliomba ‘Overdraft facility ya 450 millioni zitakazolipwa kwa miaka 5; mkopo wa shs 2.8 bilioni zitakazolipwa katika miaka mitano; na Dola za Marekani 2.528. Jumla yote ni Bilioni 6.217.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, fedha zote zilikopwa Benki ya Standard Charter na Benki Kuu ilitoa (Guarantee) mdhamana wa asilimia 100. Mwaka huu wa 2007 Benki kuu kutokana na Mdhamana huo tayari imelipa kiasi cha sh 8.1 Billion kwa niaba ya Mzindakaya na fedha hizo pamoja na riba zinakisiwa kufikia 9.7 billioni hadi sasa (Hati ref. CIBD-14662 ya tarehe 24 May, 2007, na mkopo kutolewa 2005.

Kutokana na tuhuma hizo, Meghji wakati akifanya majumuisho ya hoja yake, alisema Serikali imeagiza kuanza kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje zinazoikabili Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Alikiri serikali kupata taarifa za kuwapo kwa vitendo vya rushwa na nyingine za matumizi mabaya ya fedha katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Waziri Meghji alisema, tayari alikuwa ameshamwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali, kuanza uchunguzi kuhusu tuhuma hizo.Meghji alisema, serikali ilikuwa ikitarajia kukamilisha kazi hiyo na taarifa kamili ya uchunguzi huo kutangazwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Mbali ya BoT kutuhumiwa kutumia fedha nyingi kuliko inavyostahili katika ujenzi wa majengo yake mapya ya ‘minara miwili pacha’ (Twin Towers), kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.8 sawa na shilingi bilioni 40 kinatuhumiwa kufujwa katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje.

Taarifa zinaonyesha kuwa, wakopeshaji wa kimataifa kutoka nchi 12 waliingia mkataba wa kusimamia akaunti hiyo na kampuni ya Kitanzania ijulikanayo kwa jina la Kagoda Agriculture Ltd kati ya Septemba na Novermba mwaka jana.Uchunguzi wa awali wa wakaguzi wa nje wa mahesabu ya akaunti hiyo unaonyesha kuwapo kwa mazingira yenye utata mkubwa unaozingira makubaliano kati ya wakopeshaji na kampuni hiyo iliyolipwa dola milioni 30.8.

Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA) alihoji kwa nini Serikali ilikalia kimya suala la kashfa ya BoT mara baada ya habari za kashfa kutangazwa kupitia mtandao wa internet tangu Novemba 2006 na kuonya kuwa hali hiyo inaathali kubwa kiuchumi iwapo kashfa kama hizi zinaachwa bila ya ufuatiliaji wa serikali.

Taarifa za awali za uchunguzi huo zinaonyesha kuwa, BoT ilifikia hatua ya kuipa kampuni hiyo fedha zote hizo ikidai kuingia mkataba na wakopeshaji hao katika mazingira ambayo nyaraka zilizopatikana zinaonyesha kuwa na hitilafu nyingi.Miongoni mwa hitilafu zilizobainishwa katika uchunguzi wa awali ni, kukosekana kwa karatasi rasmi zenye majina ya makampuni hayo ya kimataifa.

Dr. Daudi Balali Amefariki!

Habari kutoka ippmedia.com zinasema kuwa aliyekuwa Gavana wa Beni ya Tanzania, Daudi Balali alifariki dunia siku ya Ijumaa iliyopita tarehe 5/16/08 huko Washingtom D.C.. Atazikwa Washington D.C. kesho. Sasa hii siri aliyotake kufichua ni upi? Naona kazi ya wapelelezi umeisha. Wanaweza kurudi Tanzania na kupeleleza mambo mengine.

****************************************************************
Kweli Balali kafariki!

2008-05-21

Na Mwandishi Wetu, Jijini


Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, BOT, Dokta Daud Balali amefariki dunia. Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake nchini na huko Marekani, zimethibitisha kuwa Dk. Balali alifariki dunia Ijumaa iliyopita.

Vyanzo hivyo vimedai kuwa Dk. Balali alifariki baada ya mashine iliyokuwa ikimsaidia kupumua kuondolewa. Aidha, vyanzo hivyo vimedai kuwa kabla ya kifo chake, Dk. Balali aliandaa ujumbe mzito, ambao ndani yake umeanika ukweli wote kuhusiana na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikielekezwa kwake, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusiana na kashfa ya upotevu wa mabilioni ya pesa za nchi kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya nje, EPA.

Alasiri imeambiwa na vyanzo hivyo kuwa Dk. Balali alimkabidhi ujumbe huo wenye siri zote ndugu yake mmoja anayemuamini na kumpa maelekezo ya namna ya kuufikisha kunakohusika na hatimaye Watanzania kujua ukweli wa suala zima.

Hata hivyo, chanzo hicho kimedai kuwa hadi sasa haijafahamika ni ndugu yupi ameachiwa ujumbe huo. Imedaiwa zaidi na chanzo hicho kuwa Dk. Balali aliamua kuandaa ujumbe huo wenye siri zote kwa vile hakutaka achafuliwe peke yake wakati wahusika wa sakata hilo wapo na anawafahamu.

Aidha, imedaiwa alikuwa akisema kuwa hakutaka aondoke na siri nzito kuhusiana na yote aliyokuwa akielekezewa kidole. Dk. Balali alifukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete baada ya uchunguzi uliofanywa na Kampuni ya Kimataifa ya Ernst &Young kubaini upotevu wa Shilingi Bilioni 133 zilikuwa zimechotwa BOT kupitia EPA wakati wa uongozi wake.

Dk. Balali alienguliwa nafasi ya ugavana na Rais wakati akiwa nje ya nchi kwa matibabu na tangu wakati huo, hakuwahi kurejea nchini mpaka umauti ulipomkuta. Habari zinadai kuwa Dk. Balali anatarajiwa kuzikwa keshokutwa huko Jijini Washington DC, Marekani.

SOURCE: Alasiri

Tuesday, May 20, 2008

Daudi Balali Asakwa na Wapelelezi Marekani!


Sijui yataishaje. Wengine wanasema Mzee Daudi Balali (pichani) amefariki, (soma Jamii Forums) wengine wanasema amejificha Boston au Washington D.C. hapa Marekani!

Kuna hii habari iliyotoka jana kwenye African Baraza kuwa Mzee Balali anasakwa na wapepelezi kuhusiana na wizi wa dola $133 milioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

****************************************

Detectives Hunt for Ex-Governor

By ADAM LUSEKELO

Dar-es-Salaam, Tanzania

Posted On: 19/05/2008

A team of local investigators is currently in the United States attempting to trace the whereabouts of former Bank of Tanzania governor Daudi Ballali, as part of the ongoing investigation into the theft of over $133 million from the central bank’s external payment arrears (EPA) account.

Well-placed sources have said at least seven detectives are combing Washington DC and Boston in a bid to locate the ex-governor – a central figure in the investigation, who has surprisingly not been officially questioned by authorities.

But with less than eight weeks to go before the expiry of the six-month deadline given by President Jakaya Kikwete to the EPA investigations team lead by Attorney General Johnson Mwanyika, the focus now seems to be firmly shifting onto Balali.

“There is a team of Tanzanian investigators in the US right now, apparently trying to locate Ballali. It isn’t clear if their orders are to arrest or just question him,” said a source familiar with the investigation.

“The clock is certainly ticking for the EPA probe team to wrap up its work, and there have already been suggestions that the AG (Mwanyika) will ask the president for an extension of about two months to finish the job.” The source added.

A senior government official has confirmed that the US government has offered “full cooperation with Tanzanian authorities in tracking down Ballali.”

The US government revoked Ballali’s visa shortly after he was sacked from his job as governor by President Kikwete back in January, as a direct result of the EPA scandal discovery.

This comes amidst public speculation on Ballali’s health.There are growing suggestions that the condition of the ex-governor, who has been undergoing medical treatment in the US since last year is critical.

Some are sceptical. They claim that Ballali has been deliberately edged out of Tanzania to keep him from disclosing the names of those involved in the scandal.

“Since he went to the US nobody in government is revealing what he is suffering from. I think they are deliberately keeping him out of the country to keep him from naming names.” An informed source has said.

The Mwanyika team, which says it has so far recovered about half of the $133 million embezzled from the EPA account, has also come under strong criticism for failing to make to make any arrests so far.

Critics claim that this simply confirms that there is a cover up to shield big operatives from prosecution.

Mr Ballali is believed to have been one of the key architects in the scandal. Apart from authorising the dubious payments as central bank governor, he is also understood to have gone out of his way to get rid of the bank’s former external auditors Delloit & Touche of South Africa, after they uncovered suspicious payments from the EPA accounts in 2005/06 audit.

Tuesday, January 29, 2008

Skandali ya BOT - Marekani watarudisha pesa zilizowekwa kwenye mabenki yao!

Makubwa! Serikali ya Marekani inasema itarejesha pesa ambazo zilifujwa kutoka Bank of Tanzania (BOT) na kuwekwa katika mabenki Marekani. Na watafanya kweli. Ila inabidi serikali ya Tanzania iombe hizo pesa zirudishwe.

Sasa hivi wana-freeze akaunti za watu bila huruma. Tangu 9/11 wamekuwa wakali hasa!

*****************************************************************************
From Ippmedia.com

US ready to remit all looted funds

2008-01-29

US Ambassador Mark Green has said the United States will cooperate in tracing and remitting back to Tanzania any deposits in American banks which might have been siphoned through the misappropriation of the External Payments Account of the Bank of Tanzania.

Speaking to editors in Dar es Salaam yesterday Green said American laws compelled the tracing down of such funds, even if they had simply passed through an American bank. Green was responding to a question by this reporter about the possibility that some of the billions that had been embezzled at the BoT might be safely banked in Western countries, including the US, and if his government was prepared to facilitate the return of the looted funds to Tanzania.

He however said any such move depended on receiving a substantive request from the concerned state. BoT, under former governor Dr Daudi Ballali, occasioned multi-billion losses to the nation mostly through dubious payments and dealings with phony companies in 2005. President Jakaya Kikwete fired Ballali as BoT governor early this month and his position was taken by Prof. Benno Ndulu. Ballali was in USA undergoing treatment when the president sacked him. He has not returned yet.

Soon after his appointment was rescinded the US government revoked his visa saying his termination from work means he no longer represents the Tanzanian government and is thus not eligible for his current non-immigrant visa status.

Asked whether the US- now that it had cancelled Ballali`s visa-would proceed to extradite Ballali to Tanzania, Green said that the US fully supported President Jakaya Kikwete`s anti-corruption drive and was quite willing to work on any request that would enable the Tanzanian government to achieve that goal. He added that he was quite optimistic that President George Bush, during his upcoming visit to Tanzania, would make clear his stance in regard to corruption.

When the envoy was called upon to state categorically if Ballali was still in the US, and the precise location he was staying, Green said he did not know. He added that American laws did not allow him to make public any private information on a person`s whereabouts or location.

Responding to allegations made to the effect that former BoT governor Daudi Ballali was already an American citizen because he had acquired a Green Card, and that the revocation of his visa was therefore a blunt move, Ambassador Green said: ``What I know is that if somebody applies for a visa, then this person is not a citizen of that country.``