Showing posts with label Daudi Balali. Show all posts
Showing posts with label Daudi Balali. Show all posts

Monday, July 14, 2014

Mwache Mzee Balali Apumzike Kwa Amani!

Jamani, nimeshangaa tangu wiki iliyopita  kuna mzozo kuwa Marehemu Daudi Balali aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu yu au la.  Mzee Balali amefariki! Ni marehemu!  Rest in Peace Mzee Daudi Balali (1942-2008)!

Kama hamwamini basi tumeni maombi ya death certificate huko alipokufa, Maryland, USA. Kama cheti haitoshi basi mlipe hela kwenda mahakamani kuomba kaburi lake lifukuliwe na mfanye testi kwenye mabaki mtakayokuta. Inaweza kuwagharamia dola $65,000!

Kuna mtu ana Twitter akaunti ya Utani! Kuna watu wameapa eti ni Marehemu Mzee Balali anayeandika!
Kaburi la Mzee Balali huko Silver Spring, Maryland, USA
Kutoka Gazeti la Mwananchi:

Mkazi wa Kijiji la Luganga, Wilaya ya Mufindi, Iringa, alikozaliwa Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali analazimika kutumia saa 32 kufika katika kaburi la kiongozi huyo lililopo eneo la Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

Ndugu wa Ballali wanaweza kutaka kwenda kuona kaburi la ndugu yao, kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawakuwahi kupata fursa ya kumzika Gavana huyo ambaye alikuwa kiongozi wa juu kabisa wa taasisi kubwa inayosimamia masuala ya fedha na uchumi wa nchi.

Mwandishi wa gazeti hili alisafiri kwa saa 24 kutoka Dar es Salaam hadi Washington, Marekani ambako alithibitisha pasi na shaka kwamba Ballali alizikwa Mei 21, 2008 katika makaburi ya Gate of Heaven, baada ya kufariki dunia akiwa nyumbani kwake Maryland, Mei 16, mwaka huo.

Safari hiyo ya siku kumi, ilianza Alhamisi Juni 26, 2014 hadi Jumapili, Julai 6. Mwandishi wa habari hizi aliligundua kaburi hilo baada ya kwenda makaburi ya Gate of Heaven kwa siku tatu mfululizo.

Siku ya kwanza, mwenyeji wa mwandishi ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa alimfikisha katika makaburi hayo, lakini kaburi la Ballali halikuonekana na hata mwandishi alipokwenda siku ya pili peke yake, kaburi hilo pia halikuonekana kwa kutokana na ukubwa wa eneo hilo.

Siku ya tatu, Mwandishi wa Mwananchi alilazimika kuomba msaada wa Ofisi ya Makaburi ya Gate of Heaven, ambayo ilimsadia kuonyesha eneo lilipo kaburi hilo, hivyo kuwezesha kupata picha zake.

Kaburi lake liko katika msitari wa mwisho kabisa na Ukanda wa Kijani wa miti iliyozunguka makaburi ya Gate of Heaven, likiwa limeandikwa jina la kiongozi huyo, pamoja na maneno ya Kiingereza yanayosomeka “When the heart weep for what it has lost, the soul rejoices for what it has found”.

Maana ya maneno hayo ni kwamba “wakati moyo ukiomboleza kwa kile kilichopotea, roho hufurahi kwa kile kilichopatikana”. Kaburi hili limezungukwa na makaburi mengine kadhaa ambayo si ya Watanzania, kwani kwa haraka kutokana na mazingira yalivyokuwa, Mwandishi wa Mwananchi hakuweza kuona kaburi jingine lenye majina yenye asili au kuwa na mwelekeo wa asili ya Tanzania.

Uthibitisho huu ni tofauti na hekaya za miaka nenda rudi zilizogubika kifo cha kiongozi huyo, ambaye tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani Agosti 2007, hakuwahi kurejea na badala yake zilisikika taarifa za kuugua kwake, kifo chake na baadaye mazishi yake yaliyokuwa ya siri kubwa yakiwahusisha ndugu wa karibu pekee.

Kutokana na mazingira hayo, kumekuwapo na uvumi kwamba Ballali hakufa na pengine amefichwa kusikojulikana, madai yanayochagizwa na mtu aliyejitokeza katika mitandao wa kijamii ya Twitter na facebook, akidai kwamba yeye ni Ballali na kwamba hajafa, huku akisisitiza kuwa wakati ukiwadia ukweli utafahamika.

Mtu huyo asiyefahamika hadi sasa alianza kujitokeza Twitter, Oktoba Mosi, 2012 pale aliposema “Nitakutana na Rais Kikwete (Jakaya) na ujumbe wake wiki hii hapa Marekani”. Mtu huyo alidai kwamba alikuja nchini Tanzania na kukaa karibu na Hoteli ya Hyatt Kempinski Kilimanjaro na baadaye kuondoka ghafla kwa kile alichokiita sababu za kiusalama.

Novemba 13 mwaka huo alituma ujumbe akisema:“In Dar es Salaam, Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kempinski Kilimanjaro Hotel. Feels good to be close to my former office, BoT,” akimaanisha kwamba niko Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, najisikia vizuri kuwa karibu na ofisi yangu ya zamani BoT.

Mtu huyo ambaye sasa tunaweza kuthibitisha kuwa ni feki amekuwa akiendelea kutuma ujumbe akijitambulisha kwa jina hilo la Ballali.

Ballali alifariki dunia kama ilivyotagazwa, lakini ilikuwaje akaenda safarini Washington, ugonjwa wake na hata kifo chake kilikuwaje? Je ndugu zake wanasemaje, safari ya kwenda Marekani ilikuwaje? Fuatilia mfululizo wa habari hii itakapoendelea kesho.



Source: Mwananchi

*********

 

Monday, September 22, 2008

Skandali nyingine Bank of Tanzania (BoT)






Kutoka kwa Mzee wa Sumo (Mpoki Bukuku) Blog:

" Hii ni kutoana nishaji jamani na ukiukwaji haki za wanawake yaani wengine wameamua kutoa wigi la urembo kujikinga na fedheha! Sijui wengine walikuwa na swaum? " - Mpoki Bukuku akizungumzia picha alizopiga.

TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.

Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.

Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.

Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.

Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.

Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.

Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002. Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.

Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.

Tuesday, May 27, 2008

Serikali Inajikanganya - Kifo cha Dk. Ballali

Misa ya Kumwombea Mzee Ballali huko Washington D.C. (picha kutoka Michuzi Blog)

Wadau, lazima niseme kuwa bado kuna maswali mengi kuhusu kifo cha Mzee Ballali.

************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Serikali inajikanganya kifo cha Ballali - Slaa

2008-05-27

Na Simon Mhina

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amesema hoja za Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Benard Membe kwamba serikali haihusiki na kifo cha Dk. Daudi Ballali, hazijaisaidia serikali, badala yake zimezidi kuleta mkanganyiko.

Alisema yeye pamoja na wapinzani wengine, walijenga hoja kwamba ni kwa nini wanaihusisha serikali na kifo hicho, tofauti na Bw. Membe ambaye amekanusha bila kujibu hoja zao na wala hakutoa maelezo ya msingi.
Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alisema waziri huyo amezidisha kiwango cha wasiwasi walichonacho watanzania, pale aliposhindwa kutoa maelezo kwamba Dk. Ballali alikuwa amelazwa hospitali gani na ugonjwa gani.

Alisema hoja ya Bw. Membe kwamba wanaotoa tuhuma dhidi ya serikali wanafanya hivyo kwa hisia, haina msingi na inadhihirisha jinsi waziri huyo anavyobabaika. ``Yaani ugonjwa wa mtu mkubwa mwenye tuhuma nzito kama Ballali, umefichwa, kifo chake kimefichwa, mazishi yake yamefichwa, hata Maiti yake haikuonekana, halafu anasema tuhuma zetu ni hisia? Huu ni upotoshaji mkubwa na kuzidi kujikanganya,`` alisema.

Mbunge huyo alisema kitu ambacho kingeweza kuinasua serikali katika tuhuma hizo, ni Bw. Membe kutaja sehemu aliyokuwa amelezwa Dk. Ballali. ``Tangu lini hospitali ikawa ni sehemu ya siri, kwa nini hawataki kusema?`` Alihoji.

Alisema madai aliyotoa waziri huyo kwamba mwenye vielelezo toka kwa daktari vinavyoonyesha kwamba Dk. Ballali alikufa kwa sumu avitoe, au yanaonyesha kwamba kweli kifo cha Gavana huyo wa zamani wa BoT kilipangwa. ``Mtanzania wa kawaida atawezaje kumpata daktari aliyemtibu Ballali wakati hata hospitali alipokuwa amelazwa panafichwa?

Kumbe wameficha kwa makusudi ili Watanzania washindwe kupata vielelezo?`` Alihoji na kuongeza: ``Serikali haihitaji vielelezo, bali ndiyo iliyofanya njama za kuhakikisha hakuna kielelezo chochote ambacho kinahusiana na kifo hicho kinachoweza kupatikana.``

Alisema kama kweli serikali inasisitiza kwamba haihusiki, itaje hospitali ambayo Dk. Ballali alikuwa akitibiwa na ugonjwa uliomsibu. ``Bw. Membe anasema mwenye vielelezo apeleke? Kazi yake kama waziri wa Mambo ya Nje ni ipi hasa?
Yeye ndiye alitakiwa azungumze na Balozi wetu kule Marekani ili aeleze habari za ugonjwa na baadaye kifo chake, kama mtu mkubwa kama Ballali anaweza kufikwa na kifo nchi za nje bila watu kujua, sembuse mtu wa kawaida?`` Alihoji.

Dk. Slaa alisema ili serikali ijisafishe, ni vizuri ikasema ni kwa nini hata hapa mjini, matanga ya marehemu huyo yalikuwa ya siri na majirani walikatazwa kuingia huku waandishi wa habari wakifukuzwa.

``Tunataka iundwe tume huru ya kuchunguza kifo hicho, kwa vile hadi sasa serikali haijatoa maelezo yanayojitosheleza. Tunataka tume kwa vile pesa za EPA bado ziko mikononi mwa mafisadi, ambao huenda ni marafiki wakubwa wa serikali,`` alisema.

Friday, May 23, 2008

Balali Aliagwa Jumanne!

Kutoka Ippmedia.com

Balali Aagwa

2008-05-23 22

Na Mwandishi Dar, Mashirika

Aliyekuwa Gavana wa Tanzania, Dokta Daud Balali aliyefariki Ijumaa iliyopita huko nchini Marekani, hatimaye ameagwa rasmi na ndugu na wapendwa wake, kabla ya mwili wake kupelekwa kwenye makazi yake mapya atakapopata pumziko la milele.

Taarifa za mtandao zilizothibitishwa na baadhi ya jamaa wa gavana huyo waishio Marekani zinadai kwamba, familia ya yake iliyo huko majuu na watu wa karibu, waliaga mwili wake Jumanne wiki hii. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Jumanne ndiyo ilikuwa fursa pekee ya watu maalum waliopewa kibali kuona mwili wa Dk. Balali.

Imedaiwa kuwa leo, hakutakuwa na uwezekano wowote wa waombolezaji kuonyeshwa mwili wa marehemu. Kwa mujibu wa taarifa hizo, misa ya kumuombea marehemu ilitarajia kufanyika leo kuanzia saa 4:00 asubuhi (kwa saa za huko) katika kanisa la St. Stephen Martyr lilililo Pennsylvania Ave, NW Washingiton DC.

Ilielezwa kuwa mazishi yatafanyika katika makaburi ya ``Lango la Mbinguni\'\' yaliyopo eneo la Silver Spring, mjini Washington leo mchana. (kwa saa za kule). Taarifa zaidi zinadai kuwa shughuli hiyo nzima ni marufuku kwa wazamiaji ambao hawajaalikwa na kwamba ni maalum kwa ndugu, jamaa, na marafiki wa karibu.

Habari za mtandao zinasema bado haijajulikana kwa uhakika kama mwili wa marehemu utazikwa ardhini kama ilivyo desturi ya Kiafrika au utateketezwa kwa moto kwani makaburi hayo yanatoa huduma hiyo pia.

Kama ulikuwa ni wosia wake kuteketezwa, basi kwa kanuni za Kanisa Katoliki shughuli hiyo, itafanyika mara tu baada ya ibada. Kwa kanuni za Kanisa Katoliki mwili uliolazwa kwa njia ya kuteketezwa kwa moto mabaki yake (majivu) hawapewi familia, kusambazwa au kugawanywa katika mafungu madogo madogo na badala yake ni lazima viwekwe ardhini au kwenye sehemu maalum inayotumika kwa maziko ya namna hiyo.

Dk. Ballali ambaye amefariki akiwa amezungukwa na wingu kubwa la kashfa dhidi yake na dhidi ya taasisi aliyoingoza inasemakana aliacha wosia uliotaka atakapofariki basi azikwe Marekani.

Taarifa zaidi zimedai kuwa ibada ya mazishi inatarajiwa kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiongozwa na Balozi wa Tanzani nchini Marekani Bw. Ombeni Sefue, watumishi wa idara mbalimbali alizowahi kuzitumikia ikiwemo IMF, ndugu zake ambao waliwasili siku chache zilizopita, na baadhi ya Watanzania kadhaa waishio maeneo ya Washington DC.

Balali alizaliwa mwaka 1942 huko Iringa. Baada ya Elimu ya msingi na sekondari alipata shahada ya kwanza katika Uchumi mwaka 1965 toka Chuo Kikuu cha Howard nchini Marekani na kupata shahada ya pili toka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Marekani miaka miwili baadaye.

Alijiunga na Benki Kuu ya Tanzania mwaka 1967 na kupanda ngazi taratibu hadi kufikia cheo cha Ukurugenzi wa Utafiti mwaka 1973. Baada ya hapo ndipo alipoanza kazi katika shirika la Fedha Duniani, IMF hadi mwaka 1997 alipoitwa nyumbani na Rais Mkapa na kuteuliwa kuwa mshauri wa Rais mambo ya Uchumi. Mwaka 1998 aliteuliwa na Rais kuwa Gavana mpya wa Benki Kuu

Ballali ameacha mke na familia.

SOURCE: Alasiri

Thursday, May 22, 2008

Kifo cha Mzee Ballali kimetangazwa Rasmi Washington D.C.


Daudi Timothy Said Ballali

Viewing: PrivateService: May 23, 2008 @ 10AM
Location: St. Stephen The Martyr

Daudi Timothy Said Ballali
On May 16, 2008 of Washington, D.C.
Husband of Anna Ballali

Mass of Christian Burial will be offered on May 23, 2008 at 10AM at St. Stephen, Washington, D.C.
Interment Gate of Heaven Cemetery


http://www.devolfuneralhome.com/index.asp?sid=6&formid=102&serviceid=960

REST IN ETERNAL PEACE, Mzee Ballali.

Eti Balali Amefariki hapa Boston, MA?

Wadau, tangu juzi nimepigiwa simu na wadau wengi kuniuluiza kama Mzee Balali alikuwa hapa Boston, Massachusetts kwa matibabu. Ukweli sijui na wala sikuwahi kusikia kama yupo hapa. Niliambiwa kuwa alifariki Washingtion D.C. siku ya Ijumaa iliyopita.

Kwa kawaida mtu akifariki hapa kuna kuwa na matangazo kwenye gazeti kama Boston Herald na Boston Globe. Bado sijaona Obituary yake. Kama nikiona nitaiposti hapa.

Sasa nashangaa jana Ippmedia.com walisema kuwa serikali imetangaza kuwa Mzee Balali alifariki Washington D.C., leo wanasema amefariki hapa Boston. Niko confused sasa. Juu ya hayo kuna mtu alisema Mzee Balali yu mzima na anategemea kuwasili Dar es Salaam kesho! Heh!

Mnaonaje hii issue wadau?

***********************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Yes, Ballali is dead - BoT

2008-05-22

By Angel Navuri and Correspondent Njonanje Samwel

The Bank of Tanzania confirmed yesterday that its immediate former governor, Daudi Ballali, is dead. A section of the media broke the surprise sad news yesterday morning, as the nation awaited word on developments relating to a saga on grand corruption allegations involving him.

A statement issued by BoT said the office of central bank Governor Benno Ndulu had learnt with shock on Tuesday night that Ballali died on Friday last week in Boston, the US, where he was understood to have been undergoing treatment.

``We at the Bank join the late Ballali`s family in mourning his death and pray to God that his soul rest in eternal peace,`` read part of the statement. Neither Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe nor his deputy, Seif Ali Iddi, could be reached for comment on the issue yesterday.

However, a man who identified himself as a close Ballali relative said in an interview with this paper that the former governor died last Friday in the US ``after long but undisclosed illness``. At the residence of Ballali's sister at Boko in suburban Dar es Salaam, The Guardian found scores of people assembled to mourn his death.

The woman was identified only as Eliza, while the people at her residence were said to be family members, close relatives, family friends and neighbours. ``It`s true that Ballali is no more. We are gathered here as family members to discuss what to do,`` said an informer, who flatly refused to give his name.

According to a close Ballali relative, family members were having a hard time planning how to break the sad news to the former BoT chief's ailing mother. She is said to have heart problems and is currently cared for at Eliza`s residence.

Ballali was taken to South Africa last year after developing health problems. He was later flown to Boston for further medical attention, where he was subsequently admitted. Last December doctors there released him after his condition improved, instructing him to stay home for three months - until March this year - before returning to the hospital.

But his condition soon reportedly began deteriorating, forcing his doctors to order his re-admission. President Jakaya Kikwete relieved Ballali of his duties after revelations that the former governor had occasioned a loss amounting to billions of shillings through shady dealings with phony companies in 2005. Sooner after, the president named Prof Ndulu as Ballali's successor at the central bank.

Ernst & Young, the international auditing firm contracted by the government to screen the central bank`s accounts, revealed that payments amounting to 133,015,186,220/74 were dubiously made to 22 domestic companies under the External Payments Arrears (EPA) account scheme in 2005. Some 90,359,078,804/- out of this was paid to 13 companies on the strength of fake or forged documents.

Another nine firms were said to have been paid an equivalent of 42,656,107,417/- without any documents to support their claims.

Wednesday, May 21, 2008

Habari zaidi kuhusu Kifo cha Balali

Hayati Dk. Daudi Balali (picha kutoka Michuzi Blog)

Written by KLHN/Tanzania Daima

Wednesday, 21 May 2008

KLH News imeweza kuthibitisha kwa uhakika kuwa misa ya kumuombea Marehemu Balali inatarajiwa kufanyika saa nne asubuhi katika Kanisa la Mt. Stephen Washington DC. Kutoa heshima za mwisho kutafanyika katika kanisa hilo hilo na itakuwa si kwa hadhara nzima.

Mwili wake unatarajiwa kulazwa kaburini kwenye makaburi ya "Gate of Heaven" huko hukoJamaa wa karibu wa Ballali walioko Dar es Salaam na Washington walilithibitishia Tanzania Daima kuhusu kutokea kwa msiba huo.

“Ni kweli amefariki nyumbani kwake Ijumaa usiku. Na sasa hivi tuko katika maandalizi ya kwenda funeral home (taasisi ya kuandaa shughuli zote za mazishi) kwa ajili ya kuanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msiba,” alisema ndugu wa karibu wa Ballali kutoka Washington.

Habari zaidi zinaeleza kwamba, tayari familia ya gavana huyo wa zamani wa BoT imeshaitaarifu serikali kuhusu kutokea kwa msiba huo na kwamba taarifa rasmi kuhusu kifo hicho zitatolewa leo hii.Ndugu mwingine wa karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima majira ya saa 4:00 usiku jana alisema mazishi ya gavana huyo wa zamani wa BoT yanatarajiwa kufanyika Ijumaa hii huko huko Marekani.

Mmoja wa wanasiasa aliye karibu na familia ya Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana alithibitisha pia kupokea taarifa za kifo cha Ballali kutoka kwa mkewe, Anna Muganda. Ndugu mmoja wa Ballali alipoulizwa na Tanzania Daima sababu za kushindwa kutangazwa kwa taarifa za kifo hicho mapema alisema walilazimika kufanya hivyo ili wapate fursa ya kuwasiliana na serikali kwanza na kisha ndugu, jamaa na marafiki wa familia yao kabla ya habari hizo kusambazwa.

Badhi ya jamaa za Ballali waliozungumza na Tanzania Daima walisema kulikuwa na wasiwasi kwamba kifo cha gavana huyo wa zamani wa BoT kikawa kikawa si cha kawaida.“Kuna wasiwasi kwamba huenda alilishwa sumu wakati akiwa nchini mwaka jana na hili limekuwa likizungumzwa sana ndani ya familia,” alisema mmoja wa jamaa za karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana.

Taarifa za kuwapo kwa wasiwasi wa Ballali kulishwa sumu zilipata kusikika mwaka jana na wakati fulani ilielezwa kwamba alipelekwa Marekani kwa matibabu kutokana na sababu hizo.

Habari za kifo hicho cha Ballali ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete Januari mwaka huu zimekuja siku chache tu baada ya serikali kupitia Ofisi ya Rais Ikulu kutoa tamko la kutangaza kwamba ilikuwa haimtafuti gavana huyo wa zamani wa BoT.

Tamko hilo la serikali lilitolewa mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu.Rweyemamu alisema kuwa serikali ina mkono mrefu na iwapo itafikia hatua ya kumtafuta gavana huyo wa zamani wa BoT ili aje atoe maelezo yake kuhusu wizi wa zaidi ya shilingi bilioni 133 uliogundulika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) haitashindwa kamwe kumfikia alipo.

Alisema kutokuwepo nchini kwa Ballai, au kutojulikana alipo, si jambo linaloisumbua serikali kwa sasa kwa sababu hivi sasa yeye ni raia wa kawaida, hivyo anao uhuru wa kuishi popote anapopenda.“Serikali haimtafuti Ballali (kwa sasa), lakini ikiamua kufanya hivyo haitashindwa.

Kwanza ni private citizen (raia huru) siyo mwajiriwa wa serikali tena,” alisema Rweyemamu na kuongeza kuwa, mkono wa serikali ni mrefu hautashindwa kumpata Ballali iwapo itamhitaji. kifafanua zaidi, alisema baada ya kutenguliwa kwa uteuzi wake, serikali iliunda timu ya kuwachunguza watuhumiwa wa EPA, kuhakikisha fedha zilizoibwa zinarudi na kuwachukulia hatua waliohusika, akiwemo Ballali.

Alisema: “Ninachofahamu ni kwamba, timu iliyopewa kazi kuhusu ubadhirifu wa EPA inaendelea na kazi yake na tunaona jinsi fedha zinavyorudishwa.”Mkurugenzi huyo pia alikiri kwamba serikali haifahamu hospitali aliyokuwa akitibiwa Ballali, licha ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo, kukaririwa akisema alimtafuta Ballali bila mafanikio alipokuwa jijini Washington, Marekani.

“Kwa kweli sifahamu hasa Ballali alikuwa akitibiwa katika hospitali gani, lakini najua alikuwa nchini Marekani katika Jimbo la Boston, ila hospitali kwa kweli siijui.“Lakini huyu ni mtu huru hivyo anaweza kuishi popote… huyu ana nyumba yake nchini Marekani… yupo huko anaishi na familia yake,” alisisitiza Rweymamu katika ufafanuzi wake.

Wiki iliyopita, ikiwa ni siku chache tu baada ya taarifa hiyo ya Ikulu, vyombo kadhaa vya habari viliandika habari zilizokuwa zikieleza kuwa makachero kutoka hapa nchini, walikuwa wamekwenda nchini Marekani katika miji ya Boston na Washington kufuatilia nyendo na maisha ya gavana huyo wa zamani.

Kwa mujibu wa habari hizo, ambazo zilikariri taarifa za ndani kutoka serikalini, makachero hao walikuwa wamekwenda huko ili kujua mahali anakoishi ili wakati wa kumhitaji utakapofika iwe rahisi kumpata. Ballali aliondoka nchini, Agosti mwaka jana kwenda Marekani kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa matibabu, na tangu wakati huo taarifa zake zilikuwa ni zenye utata mkubwa.

Mara ya mwisho kwa Ballali kuonekana hadharani ilikuwa ni Julai 12 mwaka jana alipozungumza na wanahabari na akasema alikuwa hatarajii kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu.

Katika mkutano huo, Ballali alisema madai ya ubadhilifu yanayotolewa dhidi yake ni uzushi na uongo mtupu.Huku akionekana kujiamini alisema; “Niko Comfortable, moyo wangu mweupe, ari yangu ya kazi iko juu kwani tuhuma hizo ni uongo na uzushi mtupu na siwezi kujiuzulu kwa tuhuma zisizo na ushahidi.

“Tuhuma zote dhidi yangu ni za uongo mtupu. Kwanza sijui zimetoka wapi, nani mtunzi na kwanini amefanya hivyo. Hilo tunawaachia wanaofanya uchunguzi na naamini siku moja atajulikana na ukweli utajulikana, lakini mimi siwezi kujiuzulu kwa mambo ya uzushi,” alisisitiza.

Kashfa ya BoT kupitia mtandao wa Internet, uliibuliwa mara ya kwanza Bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (CHADEMA).Akichangia maoni ya kambi ya upinzani wakati wa mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani imefarijika baada ya Waziri wa Fedha kukiri kufahamu taarifa aliyoitoa Bungeni kuhusu ubadhirifu mkubwa ndani ya BOT unaomgusa Ballali, pamoja na wafanya biashara wengine wakubwa akiwemo Mbunge wa Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya (CCM), kupitia kampuni anayoimiliki.

Dk. Slaa alisema Dk. Mzindakaya alichukua mkopo kwa shughuli za kampuni yake ya SAAFI wa sh 6.217 bilioni, uliogawanyika kama ifuatavyo. Alisema aliomba ‘Overdraft facility ya 450 millioni zitakazolipwa kwa miaka 5; mkopo wa shs 2.8 bilioni zitakazolipwa katika miaka mitano; na Dola za Marekani 2.528. Jumla yote ni Bilioni 6.217.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, fedha zote zilikopwa Benki ya Standard Charter na Benki Kuu ilitoa (Guarantee) mdhamana wa asilimia 100. Mwaka huu wa 2007 Benki kuu kutokana na Mdhamana huo tayari imelipa kiasi cha sh 8.1 Billion kwa niaba ya Mzindakaya na fedha hizo pamoja na riba zinakisiwa kufikia 9.7 billioni hadi sasa (Hati ref. CIBD-14662 ya tarehe 24 May, 2007, na mkopo kutolewa 2005.

Kutokana na tuhuma hizo, Meghji wakati akifanya majumuisho ya hoja yake, alisema Serikali imeagiza kuanza kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje zinazoikabili Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Alikiri serikali kupata taarifa za kuwapo kwa vitendo vya rushwa na nyingine za matumizi mabaya ya fedha katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Waziri Meghji alisema, tayari alikuwa ameshamwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali, kuanza uchunguzi kuhusu tuhuma hizo.Meghji alisema, serikali ilikuwa ikitarajia kukamilisha kazi hiyo na taarifa kamili ya uchunguzi huo kutangazwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Mbali ya BoT kutuhumiwa kutumia fedha nyingi kuliko inavyostahili katika ujenzi wa majengo yake mapya ya ‘minara miwili pacha’ (Twin Towers), kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.8 sawa na shilingi bilioni 40 kinatuhumiwa kufujwa katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje.

Taarifa zinaonyesha kuwa, wakopeshaji wa kimataifa kutoka nchi 12 waliingia mkataba wa kusimamia akaunti hiyo na kampuni ya Kitanzania ijulikanayo kwa jina la Kagoda Agriculture Ltd kati ya Septemba na Novermba mwaka jana.Uchunguzi wa awali wa wakaguzi wa nje wa mahesabu ya akaunti hiyo unaonyesha kuwapo kwa mazingira yenye utata mkubwa unaozingira makubaliano kati ya wakopeshaji na kampuni hiyo iliyolipwa dola milioni 30.8.

Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA) alihoji kwa nini Serikali ilikalia kimya suala la kashfa ya BoT mara baada ya habari za kashfa kutangazwa kupitia mtandao wa internet tangu Novemba 2006 na kuonya kuwa hali hiyo inaathali kubwa kiuchumi iwapo kashfa kama hizi zinaachwa bila ya ufuatiliaji wa serikali.

Taarifa za awali za uchunguzi huo zinaonyesha kuwa, BoT ilifikia hatua ya kuipa kampuni hiyo fedha zote hizo ikidai kuingia mkataba na wakopeshaji hao katika mazingira ambayo nyaraka zilizopatikana zinaonyesha kuwa na hitilafu nyingi.Miongoni mwa hitilafu zilizobainishwa katika uchunguzi wa awali ni, kukosekana kwa karatasi rasmi zenye majina ya makampuni hayo ya kimataifa.

Dr. Daudi Balali Amefariki!

Habari kutoka ippmedia.com zinasema kuwa aliyekuwa Gavana wa Beni ya Tanzania, Daudi Balali alifariki dunia siku ya Ijumaa iliyopita tarehe 5/16/08 huko Washingtom D.C.. Atazikwa Washington D.C. kesho. Sasa hii siri aliyotake kufichua ni upi? Naona kazi ya wapelelezi umeisha. Wanaweza kurudi Tanzania na kupeleleza mambo mengine.

****************************************************************
Kweli Balali kafariki!

2008-05-21

Na Mwandishi Wetu, Jijini


Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, BOT, Dokta Daud Balali amefariki dunia. Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake nchini na huko Marekani, zimethibitisha kuwa Dk. Balali alifariki dunia Ijumaa iliyopita.

Vyanzo hivyo vimedai kuwa Dk. Balali alifariki baada ya mashine iliyokuwa ikimsaidia kupumua kuondolewa. Aidha, vyanzo hivyo vimedai kuwa kabla ya kifo chake, Dk. Balali aliandaa ujumbe mzito, ambao ndani yake umeanika ukweli wote kuhusiana na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikielekezwa kwake, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusiana na kashfa ya upotevu wa mabilioni ya pesa za nchi kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya nje, EPA.

Alasiri imeambiwa na vyanzo hivyo kuwa Dk. Balali alimkabidhi ujumbe huo wenye siri zote ndugu yake mmoja anayemuamini na kumpa maelekezo ya namna ya kuufikisha kunakohusika na hatimaye Watanzania kujua ukweli wa suala zima.

Hata hivyo, chanzo hicho kimedai kuwa hadi sasa haijafahamika ni ndugu yupi ameachiwa ujumbe huo. Imedaiwa zaidi na chanzo hicho kuwa Dk. Balali aliamua kuandaa ujumbe huo wenye siri zote kwa vile hakutaka achafuliwe peke yake wakati wahusika wa sakata hilo wapo na anawafahamu.

Aidha, imedaiwa alikuwa akisema kuwa hakutaka aondoke na siri nzito kuhusiana na yote aliyokuwa akielekezewa kidole. Dk. Balali alifukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete baada ya uchunguzi uliofanywa na Kampuni ya Kimataifa ya Ernst &Young kubaini upotevu wa Shilingi Bilioni 133 zilikuwa zimechotwa BOT kupitia EPA wakati wa uongozi wake.

Dk. Balali alienguliwa nafasi ya ugavana na Rais wakati akiwa nje ya nchi kwa matibabu na tangu wakati huo, hakuwahi kurejea nchini mpaka umauti ulipomkuta. Habari zinadai kuwa Dk. Balali anatarajiwa kuzikwa keshokutwa huko Jijini Washington DC, Marekani.

SOURCE: Alasiri

Tuesday, May 20, 2008

Daudi Balali Asakwa na Wapelelezi Marekani!


Sijui yataishaje. Wengine wanasema Mzee Daudi Balali (pichani) amefariki, (soma Jamii Forums) wengine wanasema amejificha Boston au Washington D.C. hapa Marekani!

Kuna hii habari iliyotoka jana kwenye African Baraza kuwa Mzee Balali anasakwa na wapepelezi kuhusiana na wizi wa dola $133 milioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

****************************************

Detectives Hunt for Ex-Governor

By ADAM LUSEKELO

Dar-es-Salaam, Tanzania

Posted On: 19/05/2008

A team of local investigators is currently in the United States attempting to trace the whereabouts of former Bank of Tanzania governor Daudi Ballali, as part of the ongoing investigation into the theft of over $133 million from the central bank’s external payment arrears (EPA) account.

Well-placed sources have said at least seven detectives are combing Washington DC and Boston in a bid to locate the ex-governor – a central figure in the investigation, who has surprisingly not been officially questioned by authorities.

But with less than eight weeks to go before the expiry of the six-month deadline given by President Jakaya Kikwete to the EPA investigations team lead by Attorney General Johnson Mwanyika, the focus now seems to be firmly shifting onto Balali.

“There is a team of Tanzanian investigators in the US right now, apparently trying to locate Ballali. It isn’t clear if their orders are to arrest or just question him,” said a source familiar with the investigation.

“The clock is certainly ticking for the EPA probe team to wrap up its work, and there have already been suggestions that the AG (Mwanyika) will ask the president for an extension of about two months to finish the job.” The source added.

A senior government official has confirmed that the US government has offered “full cooperation with Tanzanian authorities in tracking down Ballali.”

The US government revoked Ballali’s visa shortly after he was sacked from his job as governor by President Kikwete back in January, as a direct result of the EPA scandal discovery.

This comes amidst public speculation on Ballali’s health.There are growing suggestions that the condition of the ex-governor, who has been undergoing medical treatment in the US since last year is critical.

Some are sceptical. They claim that Ballali has been deliberately edged out of Tanzania to keep him from disclosing the names of those involved in the scandal.

“Since he went to the US nobody in government is revealing what he is suffering from. I think they are deliberately keeping him out of the country to keep him from naming names.” An informed source has said.

The Mwanyika team, which says it has so far recovered about half of the $133 million embezzled from the EPA account, has also come under strong criticism for failing to make to make any arrests so far.

Critics claim that this simply confirms that there is a cover up to shield big operatives from prosecution.

Mr Ballali is believed to have been one of the key architects in the scandal. Apart from authorising the dubious payments as central bank governor, he is also understood to have gone out of his way to get rid of the bank’s former external auditors Delloit & Touche of South Africa, after they uncovered suspicious payments from the EPA accounts in 2005/06 audit.