Showing posts with label Bi Hindu. Show all posts
Showing posts with label Bi Hindu. Show all posts

Monday, November 12, 2007

Bi Hindu akiigiza kama Mama mwenye Nyumba

Scene kutoka Bongoland II

Josiah Kibira ameandika maoni yake kuhusu mcheza sinema maarufu wa Tanzania, Bi Hindu. Katika sinema ya Bongoland II, Bi Hindu anaigiza kama mama mwenye nyumba.
Kwa habari zaidi soma:

Tuesday, August 14, 2007

Mjue Msanii Mkongwe wa Bongo - Bi Hindu



Bi Chuma Suleiman aka. Bi Hindu, ni msanii maarufu huko Tanzania. Bi Hindu ameigiza katika film na michezo kwenye TV Bongo nyingi sana. Pia ameigiza katika michezo mingi ya redio. Kwa siku hukosi kumwona kwenye television huko Bongo.
Bi Hindu anapenda sana mambo ya usanii na aliniambia alianza miaka mingi sana iliyopita hata kabla ya Uhuru wa Tanganyika. Bi Hindu alisomewa lines zake za kuongea na kuzishika mara moja.
Nilibahatika kukutana naye kwenye siku ya kwanza ya film shoot ya Bongoland II huko Magomeni Dar es Salaam. Katika sinema ya Bongoland II Bi Hindu anaigiza kama mama mwenye nyumba (landlord) wa Juma, wakati anakaa kwenye nyumba ya uswahilini.

Thursday, July 26, 2007

Utengenezaji wa Sinema ya Bongoland II mjini Dar es Salaam

Msaidizi wa Josiah Kibira, Chris Audet kutoka Minnesota, akipanga mambo ya shoot. Hapa ni Manzese.

Mama Thecla Mjata anayecheza kama Mama yaka Juma, na Mzee Olotu anayecheza kama Uncle, akitoka kwa hasira ndani ya nyumba. Hapo ni eneo la Tenki Bovu.

Cameraman Sam Fischer, wakiandaa kufanya scene barabarani na Thecla Mjatta na Mzee Olotu.

Hapa ni Manzese. Tulipiga sinema kwenye maeneo hayo. Utatuona tunkimbia maeneo la uchochoroni, hapo ni sehemu moja tulipokimbia. Huyo baba ni Baba Saidi, mjumbe wa eneo hilo la Manzese. Pia alikuwa anakaanga samaki safi sana waliotoka freshi Ferry.


Josiah Kibira akimwelezea actor kuhusu scene ya 'chooni'.

Bongo Child Superstar Liz Michael Kimemeta alicheza kama mtoto muuza chapati. Liz alitueleza kuhusu ndoto yake ya kuja kuacti kwenye sinema za Hollywood. Kwa kweli mtoto ana kipaji. Nilimowna akihosti kipindi cha watoto kwenye TV Bongo.


Hapa wanashoot scene ya 'chooni' hapo Magomeni Mikumi.

Hapa wako Tanki Bovu nyumabni kwa wazee wangu.


Hapa Peter Omari anayecheza kama mhusika mkuu, Juma, akifanya scene na landlady wake anachezwa na mcheza sinema maarufu wa Bongo, Bi Hindu.