Showing posts with label Madakatari. Show all posts
Showing posts with label Madakatari. Show all posts

Friday, July 06, 2012

Chuo Kipya cha Zanzibar School of Health


Chuo cha Zanzibar School of Health kinamilikiwa na Zanzibar School of Health Company Limited.

Tuna wingi wa Shukrani kwa vile Chuo cha Zanzibar School of Health kinatowa mafunzo ya Afya kutokana na ruhusa kutoka Wizara ya Afya Zanzibar.Wanafunzi wanaosoma hapo ni 45 kwa Fani ya Psychology na 88 kwa Fani ya Uuguzi.

Chuo kimeajiri Walimu wenye Sifa kusomesha Fani husika na pia kimeajiri Wafanyakazi wa ngazi mbali mbali ili kuleta ufanisi wa Chuo. Tunayo azma ya kuanzisha na kuendeleza mtandao wa Elimu ya Masafa
ikiwemo ushauri wa Afya wa Masafa yaani Tele Medicine kupitia mitandao ya kimataifa na ya kitaifa. Chuo kinafanya taratibu ya kuwawezesha wanafunzi kupata mazoezi ya vitendo nje na ndani ya Zanzibar. Kuna
azma pia ya kuanzisha Continuing Medical Education kupitia mtandao,semina ,na kongamano za kiwengo cha kimataifa.

Chuo kimepeleka Ombi Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), na kupata Form maalum kwa ajili ya usajili kwa ngazi ya NACTE baada ya kupata Usajili Rasmi kwa Ngazi ya Baraza la Wauguzi la Zanzibar kwa Fani ya Uuguzi na baada ya kupata barua ya kutokuwa na pingamizi kutoka Wizara ya Afya za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuundesha Masomo ya Psychologia Nasaha yaani Counseling Psychology ya Tumaini University College Iringa. Chuo kimejisali na Taasisi ya kodi TRA ,ZRB Taassisi ya Usajili wa Kampuni ya Zanzibar na kupata Zanzibar Government Certificate of Incorporation.

Chuo kimepitisha Mtaala wake wa Diploma ya Nursing chini ya ukaguzi na masahihisho ya Zanzibar Council of Nurse Midwives na kupata School Registration Certificate number PNS/01 ya tarehe 29.09.2011 .

Chuo kitashukuru ikiwa Wawakilishi wetu watapata Nafasi kutembelea Chuo hich ili waweze kutupatia Ushauri wao wa Busara.

Baada ya kukamilisha hesabu za Budget ,Chuo kimewaslisha Form za Maombi kwa Usajili wa NACTE. Pia Chuo kina azma ya kuanzisha Fani zifuatatazo:

1. Diploma in Speech and Language Therapy

2. Diploma in Clinical Pharmacy

3. Diploma in Physiotherapy

4. Diploma in Clinical Medicine

5. Diploma in Medical Laboratory Technology

6. Doctor of Medicine Degree

Chuo kimeunda Board ya Taaluma na kimewaalika wajumbe kutoka Wizara ya Afya kueomo kwenye Board hio. Chuo kinachangia maendeleo ya Taifa kwa kutowa ajira kwa wataalam 10 wa Tanzania kufanya kazi Chuoni hapo . Aidha Chuo kimewasilisha Maombi Wizara ya Ardhi kwa kupatiwa Eneo la Kujenga Teaching Hospital yenye Vitanda 200 ,Maabara ya kisasa, na Taasisi ya Elimu ya Afya ambazo itakuwa na kiwango cha Kimataifa.

Vile vile Cho kimewasiliana na na Baraza la Mitihani yaani NECTA kwa madhumuni ya kuanzisha Shule ya Sekondari maalum na kituo cha kufanya Mitihani ya Kitaifa na Kimataifa.Sasa Chuo kinaandikisha Wanafunzi hao ili waweze kufanya Mitihani ya Kimataifa .

Uongozi wa Chuo unashukuru Wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa kuwaunga mkono kwa kuleta vijana wao kusoma Chuoni hapo na unaahidi Umma wa Nchi hii Elimu bora yenye Ufanisi wa Hali ya Juu.

Chuo kingependa pia kuendelea kupata Ushirikiano ili kiweze kutimiza ahadi zake za kuendeleza Nchi yetu na kutumikia Umma.

Ahsante

AMUR

Monday, July 02, 2012

Madaktari Muhimbili Warejea Kazini

Muhimbili National Hospital, Dar es Salaam, Tanzania

MADAKTARI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI WAREJEA KAZINI

JULAI 2, 2012


Huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili zimerejea katika hali ya kawaida baada ya Madaktari kurejea kazini Jumatatu ya leo Julai 2, 2012.

Tathimini iliyofanyika kuanzia asubuhi saa mbili hadi saa 11 jioni inaonyesha kuwa katika Idara ya Tiba, Madaktari Bingwa 19 kati ya 21 wamefika kazini ambapo watatu wako likizo. Aidha Registrars wote 12 walikuja kazini. Kliniki zote za tiba zimefanyika kama kawaida.

Katika Idara ya watoto, yenye Madakatari Bingwa 16, kati yao 14 walikuja kazini wengine wawili wako likizo na Registrar watatu kati ya sita walikuja kazini ambapo watatu wako likizo

Upande wa OPD yenye Registrars saba, sita kati yao walikuja kazini na mmoja yuko likizo. Aidha Madaktari Bingwa wote walikuja kazini.

Idara ya Magonjwa ya Afya ya Akili yenye Madakatri Bingwa 10, tisa walikuja kazini na mmoja wao yuko masomoni.

Upande wa Emergency Medicine, Registrars wote 10 walikuja kazini.

Kuhusu huduma za upasuaji, wagonjwa wote waliolazwa wodini wameonwa, na baadhi ya kliniki za huduma ya upasuaji zilifanyika. Hata hivyo, upasuaji haukufanyika kwani hakukuwa na orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa upasuaji..

KWA UJUMLA, MADAKTARI WAMEREJEA KAZINI.

Imetolewa na;

Aminiel Buberwa Aligaesha
Afisa Uhusiano Mwandamizi
Julai 1, 2012

Friday, June 22, 2012

Kusitishwa Mgomo wa Madaktari na Mahakama

TAARIFA KUTOKA IKULU
***********************
Mahakama Kuu ya Tanzania imetoa Amri ya kusitisha Mgomo wa Madaktari


Kufuatia Tangazo la Chama cha Madaktari nchini (MAT) la kuanza mgomo siku ya Jumamosi tarehe 23 Juni, 2012, Mahakama Kuu ya Tanzania,Kitengo cha kazi,Dar es Salaam imetoa amri ya kusitisha mgomo huo mpaka hapo pande zote mbili yaani Serikali na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

• Amri hiyo ya Mahakama imetolewa kufuatia maombi namba 73 ya 2012 yaliyowasilishwa chini ya hati ya dharura na Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT).Sababu za msingi amabazo zimepelekea Mahakama kuu kutoa amri hiyo upande mmoja ni pamoja na;

• Iwapo mgomo huo utatokea utakuwa na kuwa amri hii isipotolewa madhara yake ni makubwa isiyoweza kufidiwa kwa namna yoyote ile kama vile kupoteza maisha n.k

• Wajibu maombi,ambao ni MAT, inaundwa na Madaktari ambao wapo katika Sekta ambayo inatoa huduma mahsusi (essential service sector), Aidha Chama cha Madaktari Tanzania kimetangaza mgomo bila kufuatia taratibu zilizoanishwa katika Kifungu cha 76(1 na 2) cha Sheria ya Kazi (Employment and Labour Relations Act No 6 ya 2004.

Masharti hayo ni

• Kuzuia wafanyakazi walio katika Sekta Muhimu kugoma na kama wakigoma,

• Kuwepona makubalianao ya pamoja ya kutoa huduma za msingi wakati mgomo ukiendelea.

Kwa misingi hii,Mahakama Kuu ya Tanzania, kwa Chama cha Madktari Nchini na wanachama wake kusitisha na kutoshiriki katika mgonmo huo.

Saturday, April 28, 2012

Mtaalam wa Upasuaji wa Moyo MBongo

 Tanzania inahitaji wataalam wa kila aina katika sekta ya afya, hasa wapasuaji.  Dr. Godwin Godfrey (32) anasomea upasuaji wa moyo wa watoto (Peadiatric Cardiac Surgeon) nchini Israel. Akirudi Tanzania, atakuwa mtaalam peke yake.  Inadaiwa watoto zaidi ya nusu milioni wana subiri huduma yake.

Nauliza, hivi mtaalam kama huyo atalipwa mshahara anaostahili?  Je, ataishia kuwa 'frustrated' na kukimilia nchi nyingine ambayo watamheshimu?

Mungu ambariki, na tuombe aweze kurudi Tanzania kuhudumia watoto wetu.

Asante Da Subi kwa kunistua kuhusu habari hii:

****************************************************
 
Picture
Dr. Godwin Godfrey

Article cross-posted from NationalPost.com, written by Peter Goodspeed
Friday, Apr. 27, 2012

It’s the numbers that fascinate Dr. Godwin Godfrey, a 32-year-old Tanzanian who is finishing a five-year training course in Israel to become a pediatric cardiac surgeon.

When he graduates next summer, he will become the first and only pediatric heart surgeon in all of Tanzania – a country of 43 million people.

Tanzania’s Ministry of Health already has a waiting list of nearly 500,000 patients who desperately need his services.

The government, which sends most of its patients who need heart surgery overseas to countries like India, can only afford to care for about 100 people a year.

“You can see the chances of making it are slim,” says the surgeon. “A child on the waiting list with a serious heart condition may wait maybe three or four years and die of complications like heart failure.

“Sometimes it can be very depressing being a doctor in a poor country like Tanzania,” he says. “Too many times you see children dying in front of your eyes. You know that you are supposed to do something, like give them medicine, but you don’t have it.”

When he first started his training as a pediatric surgeon in Israel’s Wolfson Medical Centre under a program sponsored by the Save A Child’s Heart charity, Dr. Godfrey said he experienced something akin to “culture shock.”

“I always used to see a lot of death,” he says. “In our department in Tanzania [in the Bugando Medical Center in the city of Mwanza — an 850-bed hospital that serves 15 million people] you could have five or seven children die every day. When I got to Israel to train I realized we weren’t seeing any children die — even in a month.

“This was really an eye-opener. Whatever we were doing; it was wrong,” he says. “It opened my eyes. There is so much that we don’t know. There is so much equipment that we don’t have. There is so much medication that we don’t have.”

‘I always used to see a lot of death’

The son of a surgeon, Dr. Godfrey, who was born in a small town on the slopes of Mount Kilimanjaro, has been familiar most of his life with the difficulties of practicing medicine in a developing country.

After graduating at the top of his class in high school in Tanzania, he won a scholarship to study medicine at Makerere University in neighbouring Uganda. When he returned home to serve his internship, he deliberately selected the Bugando Medical Centre in Mwanza, Tanzania.

“Most of our doctors are actually located in Dar es Salaam, the capital,” he says. “That’s the biggest city and all the government offices are there. But with me being interested in surgery, I thought if I went to work in one of the big hospitals I wouldn’t get the hands-on experience that I wanted.”

In Mwanza, he was overwhelmed with work and because of a shortage of surgeons and specialists found himself doing everything from pediatric cases to orthopedic, ophthalmology and neuro-surgery.

When he started a residency in the Mwanza hospital, he shifted to cardiac surgery, but found himself stymied by a lack of equipment and expertise.

‘Being in Africa, in this hospital, we didn’t have the equipment to conduct open-heart surgery’

“Being in Africa, in this hospital, we didn’t have the equipment to conduct open-heart surgery,” he says. “So we have had to start building our unit from scratch.”

When Dr. Godfrey investigated the possibility of getting some expert training in cardiac surgery, he discovered the only place he could do so in Africa was in South Africa, Egypt, Morocco or Tunisia. But when he tried to apply, he was told those countries weren’t interested in training foreign doctors.

Then in 2006 a visiting German doctor, working for a Christian charity, suggested Dr. Godfrey should apply to study in Israel under a humanitarian project sponsored by the Save A Child’s Heart organization.

Over the last 15 years, cardiac surgeons operating out of the Wolfson Medical Centre in Holon, Israel, have treated more than 2,800 children with congenital heart diseases and adolescents with heart valve diseases.

Patients are now flown into Israel from all over the world for about 225 emergency operations each year, with 43% of the cases coming from Africa and 47% from neighbouring Arab states.

Save a Child’s Heart offered Dr. Godfrey a full five-year scholarship to study pediatric cardiac surgery and has methodically begun to help him train a complete surgery team to work with him in Tanzania.

“Heart surgery is teamwork,” says Dr. Godfrey, who was in Toronto this week to tour Sick Children’s Hospital. “It’s not just the work of a surgeon. You need a cardiologist, an anesthesiologist, an intensive care unit internist, people to operate the heart pumps and ventilators.”

‘We had to stop her heart, go in and close this hole and then start the heart functioning again’

Last summer, a team of 13 doctors from Save a Child’s Heart travelled to Tanzania to stage a cardiac clinic in Dr. Godfrey’s hospital and operated on 13 seriously ill children, including the first ever open-heart operation on a child in Tanzania.

Four year-old Laurencia Simon, the daughter of farmers who live in a mud hut without electricity or running water three hours drive from Mwanza, underwent the historic surgery.

“She had a hole in her heart,” Dr. Godfrey explains. “We had to stop her heart, go in and close this hole and then start the heart functioning again.”

“In places like Canada, you can do this operation any day,” he says “You don’t let patients with the condition become six months old or even a year, without the operation. But in Tanzania, this little girl was four years old and she could have died while being on a waiting list.”

Now, she is healthy and back in school.

In a very small way, things are about to change in Tanzania.

• Email: pgoodspeed@nationalpost.com

Source: http://www.wavuti.com/4/post/2012/04/nearly-500000-children-waiting-for-tanzanias-only-surgeon-dr-g-godfrey.html?utm_source=feedburner&utm_medium=twitter&utm_campaign=Feed%3A+wavuti+%28Wavuti+%29#ixzz1tKF774au

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Maazimio ya Kikao Kati ya Waziri Mkuu na Madaktati Leo CPL

Asante Da Subi kwa Kuleta Taarifa Hii:


Tamko la Kamati: MAAZIMIO YA KIKAO CHA WAZIRI MKUU; MADAKTARI

09/02/20120 Comments Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa Madaktari, Dkt. Stephen Ulimboka baada ya kuzungumza na madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam, Februari 9, 2012. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)
TAARIFA KWA UMMA NA MADAKTARI WOTE NCHINI JUU YA MAAMUZI YALIYOFIKIWA LEO FEBRUARY 9, 2012 KUFUATIA MKUTANO KATI YETU NA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA KATIKA UKUMBI WA CPL, HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari nchini inapenda kuwajulisha madaktari wote pamoja na kada nyingine zote za afya nchini juu ya kile ambacho kimejiri katika siku ya leo ya tarehe 09.02.2012 ikiwa ni matokeo ya kikao wanataaluma wa kada za afya na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na baadaye kufuatiwa na kikao kati ya madaktari na kada nyingine za afya.

Ifahamike kuwa kama Kamati tulipata mwaliko wa kushiriki katika Mkutano huo ambapo ilitarajiwa kuwa Mhe, Waziri mkuu atafika kwa nia ya kutoa mrejesho wa madai ya madaktari yaliyowasilishwa mezani kwake mnamo tarehe 23.01.2012. Madai yetu yalikuwa manane na Mh Wazizri mkuu aliweza kutoa maelezo ya dai moja baada ya lingine.

Miongoni mwa madai ambayo mpaka sasa yamepatiwa majibu ya kuridhisha ni pamoja na;

Kuwawajibisha watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wakiwemo Katibu Mkuu Mama Blandina Nyoni , na Mganga Mkuu wa Serikali Dr. Deo Mtasiwa. Aidha Mh waziri mkuu alisema kuwa ameshalifikisha kwa Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania suala zima la kuwawajibisha watendaji wa wakuu wa kisiasa wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambao ni Waziri Mh Hadji Mponda na Naibu Waziri Mhe. Lucy Nkya.

Kama sehemu ya maridhiano, Mh Waziri Mkuu pia aliahidi mbele ya mkutano kuwa hakutawepo na unyanyasaji au vitisho vya aina yoyote ile kwa wale wote walioshiriki katika kushinikiza Serikali kutatua kero hizo. Aidha kama sehemu ya maridhiano, Mh waziri Mkuu pia alifuta zuio la madaktari kutokufanya mikutano. Lakini pia, Mh waziri Mkuu alisema kuwa Serikali haina kusudio la kumfukuza kazi mtumishi yeyote wa afya yule kazi aliyeshiriki katika mchakato huu wa kuishikiniza Serikali kutafuta ufumbuzi madai ya madaktari nchini.

Aidha, Mh waziri Mkuu amesema “Interns” wote waliokuwa wamehamishwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamesharudishwa bila masharti katika hospitali hiyo ili kuendelea na program kama kawaida. Hili pia linaambatana na kulipwa na kupewa stahiki zao zote.

Pia suala la madaktari na familia zao kuwa na Kadi ya Bima ya Afya ya kijani( Green Card) limekubaliwa na kwa sasa tusubiri utekelezaji.

Pia ilikubaliwa kuwa madaktari watapata fursa ya kukopeshwa magari kama watumishi wengine wa umma.

Mbali na madai hayo, pia Mh. Waziri Mkuu alitoa ufafanuzi juu ya madai yanayuhusu maslahi ya watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na Mishahara na Posho na stahiki mbalimbali. Lakini hata, Mh waziri Mkuu hakutoa majibu ya moja kwa moja ya kiwango gani kitakachoweza kulipwa na Serikali kama mishahara, posho na stahiki mbalimbali kwa minajili kwamba bado zinafanyiwa kazi na kamati ya wataalamu aliyoiunda ili waweze kumshauri. Aidha, Mh waziri Mkuu alisema kuwa kwa wakati huu inaweza kupandisha “on call allowances” za kada mbalimbali za afya kutoka shilingi 3,000 – 10,000/= na kufikia kati ya shilingi 5,000 hadi 25,000. Madaktari bado wanaona ongezeko hili halilingani na ukubwa wa kazi ifanywayo pindi mtumishi wa afya anapokuwa “on call” na hivyo basi kuendelea kupendekeza kuwa “on call” allowance iwe ni 10% ya mshahara wa mtumishi husika.

Pia Mhe, Waziri Mkuu hakuweza kueleza kinagaubaga mkakati kazi wa uboreshaji wa huduma za afya wapatayo wananchi wa Tanzania.

Baada ya tamko hilo la Serikali kumalizika, Mh Waziri Mkuu na ujumbe wake waliondoka, na Mkutano huo ukaendelea kwa Kamati kufanya Mkutano na madaktari wote, lengo ikiwa kujadili tamko hilo na kutoa maazimio.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, madaktari walikubaliana kwamba; kwa kuwa Serikali imeanza kuonyesha nia ya kutatua tatizo hili kwa kutekeleza baadhi ya maazimio yetu, wajumbe kwa niaba ya madaktari wote nchi nzima tulikubaliana na kuazimia yafuatayo;

Kurudi kazini mara moja kuanzia kesho tarehe 10.02.2012 bila masharti yeyote.

Kamati ya jumuiya ya madaktari kama sehemu ya MAT kuendelea kukaa mezani ya majadiliano na Serikali ili kuanza kupitia madai hasa yale yanayohusu maslahi.

Kukutana tena tarehe 03.03.2012 ili kupata mrejesho wa kiwango cha utekelezaji wa madai hayo kwa mujibu wa vikao vya majadiliano na makubaliano na hatimae kuchukua hatua zaidi.

Kujadili utekelezaji juu ya Kuwawajibisha Waziri na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi na Jamii.

Mwisho kabisa Madaktari wote kwa ujumla wake walilaani na kukemea kitendo cha Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwahoji wanaharakati wa haki za kibinaadamu na mashirika ya kijamii wakiwemo Dr. Hellen Kijo-Bisimba na Mama Ananilea Nkya na wanaharakati wengine wote waliokumbwa na kamata kamata hiyo na hivyo basi tunalitaka jeshi hilo kuwaachilia huru mara moja bila masharti yeyoye.

Pamoja Tunaweza

Imetolewa na Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari Tanzania

Dr, Ulimboka Stephen
Mwenyekiti.

Tuesday, August 12, 2008

Rudini Kazini - Mgomo wa Madaktari Bongo


Kwa kweli inasikitisha kuona madaktari wanagoma. Ninaelewa kuwa wanadai maslahi bora zaidi na ni kwali wanastahili kupewa. Lakini wagonjwa wanaowategemea wanaumia na wengine wanapotozea maisha.

Nakumbuka miaka ya 90 mwanzo nikiwa mwandishi wa habari Daily News ilitokea mgomo wa madaktari, manesi na wafanyakazi wengine wa afya. Nilipewa 'assignment' ya kwenda Muhimbili kuona hali ilivyo.
Kwa kweli hali ya wagonjwa ilikuwa mbaya nilitoka huko nalia. Niliona maiti za wagonjwa waliokufa kwenye vitanda walivyofia. Wodi fulani kulikuwa na nesi mmoja tu, anahangaika na wagonjwa wote. Nilimhurumia. Wenye pesa waliondoa wagonjwa wao na kuwapelka private.

Hivi hakuna njia nyingine ya watu wenye kazi nyeti kama madaktari kudai maslahi yao?

*************************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Serikali Yawashukia Madaktari
2008-08-12
Na Mary Edward, PST Dodoma

Serikali imewaagiza madaktari wote waliogoma, kurudi kazini mara moja kama kanuni, taratibu na maadili ya kazi yao inavyowataka la sivyo hatua kali zitachukuliwa kwa watakaokaidi. Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda alitoa agizo hilo kwa niaba ya Waziri wake, Profesa David Mwakyusa mjini hapa jana.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dk. Kigoda alisema, wasipofanya hivyo, hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka agizo hilo. Alisema serikali inashughulikia suala la posho, mishahara na malimbikizo kwa viwango vipya kwa watumishi wote wa umma nchini, na malipo hayo yatakapokamilika, kila mtu atapata stahili yake.
Aidha, Dk. Kigoda alitumia fursa hiyo, kuwapa pole wagonjwa na wananchi kwa ujumla, kutokana na usumbufu uliojitokeza. ``Napenda kuwahakikishia wananchi kwamba, huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, zinaendelea kutolewa na madaktari waliopo, ili kuhakikisha kwamba kila mgonjwa anayestahili kupata tiba, anapata matitabu,`` alisisitiza.
Akitoa maelezo ya suala hilo, Dk. Kigoda alisema, madaktari hao wamechukua hatua hiyo kwa ajili ya kudai mishahara mipya pamoja na malimbikizo ya mishahara, baada ya kuwasilisha madai yao kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambaye aliwaeleza kimaandishi kuwa, suala hilo ni la kiserikali, hivyo litashughulikiwa na wizara. ``Aliiarifu wizara na kuomba Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, akutane na viongozi wao, kwa kuzingatia umuhimu na unyeti wake, Katibu Mkuu alikutana nao Agosti 7 mwaka huu,`` alisema.
Alisema katika kikao hicho, Katibu Mkuu alitumia nafasi hiyo kuwaeleza kuhusu hali halisi kwamba, serikali inashughulikia malimbikizo ya watumishi wote na itakapokuwa tayari watalipwa. Kuhusu mishahara mipya, Dk. Kigoda alisema, Katibu Mkuu aliagiza wataalamu wa fedha wa wizara na wa hospitali wafanye mahesabu, ili kutambua kiasi kinachohitajika ili kiwasilishwe Wizara ya Fedha na Uchumi, kabla ya Agosti 11 ambayo ndiyo siku ya mwisho kwa waajiri wote, kuwasilisha madai hayo ya malimbikizo ya miashahara.
``Hali hii inatokana na ukweli kwamba, wanalipwa fedha zao kwa utaratibu wa posho na si kwa kupitia Pay Roll za serikali,`` alisema.
Aliongeza ``napenda kusisitiza kwamba, ufafanuzi uliotolewa na juhudi zilizoainishwa na Katibu Mkuu wa viongozi wao, ulikuwa unatosha kuthibitisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kuwa, posho yao inazingatia viwango vipya na stahili yao ya malimbikizo ipo pale pale na itashughulikiwa pamoja na watumishi wengine wote wa serikali.``
Aidha, alisema katika muda wote huo wa majadiliano, viongozi hao hawakuonyesha nia wala dhamira ya kupanga wala kutaka kugoma kama ambavyo wamefanya sasa. ``Kitendo hiki kinakiuka kanuni za kiutumishi, taratibu na sheria zinazohusu migomo katika kazi na maadili ya taaluma ya udaktari,`` alisema.
Lakini wakati naibu Waziri wa Afya akitoa agizo hilo, madaktari hao wasaidizi kwa upande wao, wamekubali kusitisha mgomo huo baada ya serikali kuwaahidi kushughulikia madai yao ndani ya siku saba, anaripoti Lucy Lyatuu. Hayo yalisemwa na Rais wa madaktari hao, Bw. Magesa Paulo, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.
Alisema jana walikaa katika kikao kilichomjumuisha Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Mkuu wa Taasisi ya Mifupa (MOI), wawakilishi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambao kwa pamoja walikuwa wakizungumzia madai yao.
Alisema baada ya mazungumzo, walikubaliana kuwalipa madai yao ya mshahara mpya wa serikali wa Julai na Agosti pamoja na malimbikizo yao inayoanzia Januari hadi Juni. Aliongeza kuwa, ndani ya kikao hicho, wawakilishi kutoka serikalini wamewaahidi pia kuwaletea kiwango kamili cha madai yao ifikapo Jumatatu.
Hata hivyo, alisema endapo ahadi hizo zisipotekelezwa katika siku hizo saba, watachukua hatua nyingine ambayo hakuitaja ni ya aina gani. Aidha, alisema anaishangaa serikali kutokuwa na uhakika wa ahadi za kuwalipa licha ya kwamba wamekuwa wakiwaandikia barua kila mara. Kuhusu udaktari kuwa wito na kwamba hawapaswi kugoma ili kutowaathiri wagonjwa, alisema madai ya msingi kwa madaktari ni ya msingi na kwamba hamna wito kama hupati mahitaji ya msingi.
``Bila kula na kushiba nguvu ya kushughulika utaipata wapi,`` alihoji Bw. Magesa. Aliongeza kuwa, kwa kuzingatia misingi hiyo, madaktari watano wasaidizi tayari wameambukizwa virusi vya Ukimwi kutokana na kuwachoma sindano wagonjwa walioathirika.
Alisema kutokana na misingi ya kiubinadamu kupata mahitaji yake, ni hivyohivyo na wao kupewa haki zao ili waweze kutimiza wajibu wao. Alisema asilimia 70 ya huduma za madaktari hospitalini hapo haswa wodini, hutegemea madaktari hao na kwamba kugoma kwao kumeathiri wagonjwa.
Madaktari hao walikuwa wakidai malipo ya mshahara mpya kama ilivyoagizwa katika waraka wa serikali, malimbikizo yanayoanzia Januari hadi Juni pamoja na mapumzikoya siku 28. Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam, Bw. Abbas Kandoro jana alitembelea Hospitalini hapo kwa lengo la kufuatilia hali ya mgomo. Alisema serikali inaanda utaratibu wa kufuatilia madai yao kwani yatajumuishwa pamoja na watumishi wote wa serikali.