Showing posts with label Maji. Show all posts
Showing posts with label Maji. Show all posts

Friday, July 28, 2017

Tigo Imechangia Kisima kwa wakaazi wa Mji Mpya mkoani Morogoro



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akikata utepe kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Meneja wa huduma za jamii Tigo, Halima Okash, Ofisa Mkuu wa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jérôme Albou,  na  Diwani wa mji mpya Wence Kalogelezi

Mkazi wa Mji mpya akiwa kabeba ndoo ya maji mara baada ya uzinduzi wa kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.




Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akihutubia wakazi wa Mji mpya mara baada ya  kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo akiwa katika picha ya pamoja  na Wakazi wa Mji Mpya Mkoani Morogoro mara baada ya uzinduzi w kisima hicho.

 kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.


·        Uchangiaji huu ni ishara ya shukurani kwa wakaazi hao kwa kuzima moto katika kituo cha data cha Tigo.

Tarehe 27 Julai 2017 – Tigo Tanzania imechangia kisima chenye thamani ya TZS milioni 17 kwa hosipitali ya Mji Mpya na maeneo yanayoizunguka katika mkoa wa Morogoro kama mkono wa shukurani kwa wakaazi kwa kuhatarisha maisha yao wakati wakipambana na moto ambao ulilipuka katika kituo cha data cha kampuni katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Tigo, uchimbaji wa kisima hicho pia ulikuwa sambamba na nia ya kampuni hiyo kusaidia ustawi wa jamii ambako Tigo inaendesha  shughuli zake.
Akizungumza katika sherehe za makabidhiano zilizofanyika katika hospitali ya mji mpya katika manispaa ya mji wa Morogoro Afisa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jerome Albou alielezea matarajio yake kwamba kisima hicho kitawafikisha mbali sana katika kuondoa suala la upungufu wa maji katika hospitali na pia kutoa maji safi na salama ya uhakika kwa jamii inayokizunguka.
“Tunawashukuru sana watu wa Mji Mpya kwa kuonesha kujali na kujitoa wakati wa kupambana na moto ambao karibu uteketeze kabisa kituo cha Data mapema mwaka huu. Kweli Tigo ina deni kwa wanajamii, serikali ya mtaa na viongozi wa ulinzi na usalama wa manispaa kwa kuitika  kwa wakati kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu mkubwa unasababishwa wakati wa moto,” alisema Albou.   
“Kwa hiyo msaada huu, unakuja kutimiza ahadi walioiweka Tigo kwa wakazi wa Mji mwema wa kuwapatia maji safi na salama kama namna ya kutambua juhudi zao katika kulinda mali za kituo hicho cha data.”
Albou alibainisha kwamba uchangiaji huo unakamilisha idadi ya vijiji 20 ambavyo vimenufaika kutokana na jitihada za Tigo za kutoa maji safi na salama nchi nzima, ikiwa inawasaidia zaidi ya watu 187,000.
Mwaka huu, Tigo ina mpango wa kuchimba visima zaidi katika maeneo yanayohitaji ambayo zaidi ya watu 350,000 wanatarajiwa kunufaika katika jitihada zetu za kusaidia juhudi za serikali za kuondoa upungufu wa maji safi na salama nchini.
Makabidhiano yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Stephen Kebwa ambaye aliishukuru Tigo kwa kufikiria kutoa msaada huo. Alisema kwamba kisima hicho kitasaidia utoaji wa huduma bora za kiafya katika hospitali ya Mji Mwema na kusaidia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Aliwaomba wasamaria wema wengine kujitokeza na kuunga mkono juhudi za kuondoa upungufu wa maji katika mkoa huo.
Tunapenda kuishukuru Tigo kwa kutusaidia katika juhudi zetu za kutoa huduma za kiafya za uhakika katika eneo hili kwa kutatua tatizo lililokuwepo la upungufu wa maji. Tunaamini kwamba upatikanaji wa maji safi na salama karibu na wakaazi pia itaongeza uzalishaji wa kiuchumi hasa kwa wasichana na wanawake ambao hawatakuwa wanapoteza muda mwingi wa kutafuta maji safi na salama sehemu zingine. Hii itawapatia wasichana fursa ya kuhudhuria masomo kwa uhuru na kuipa jamii fursa ya kuhudhuria kwa ufanisi katika shughuli zao za maendeleo ya Taifa,  Alisema Dr Kebwe. 

Thursday, January 05, 2017

Aloanisha Kitanda katika Mapenzi

Kumbe staili zingine za ngono ni balaa!!!! 


Friday, August 19, 2016

Benki ya Dunia Kuendelea Kusaidia Sekta ya Maji Nchini

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akifungua  kikao cha pamoja na ujumbe wa Benki ya dunia, Wizara ya Maji ,Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es Salaam (Dawasco ) na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka jijini Dar es Salaam (Dawasa) namna ya kutatua changamoto za usambaza Maji kwenye Jiji la Dar es Salaam yakiwamo Mivujo na Miundombinu chavu , kilichofanyika Jijini Dar es salaam.

Dar es Salaam.
KATIKA kuhakikisha sekta ya Maji inakua kwa kasi na inatosheleza mahitaji ya sasa ya huduma ya maji, Benki ya Dunia imejitolea kulisaidia Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (DAWASCO), ili kusaidia katika upatikanaji wa huduma ya Majisafi na Majitaka katika maeneo mbalimbali ya wakazi wa jiji la Dar es salaam pamoja na Miji ya Kibaha na Bagamoyo mkoani Pwani.

Hayo yamezungumzwa na Mwakilishi wa Benki ya Dunia nchini, Bi. Bella Bird, ambaye alikuwa ameambatana na wajumbe wake katika kikao cha pamoja na Waziri wa Maji, Mhandisi Gerson Lwenge, pamoja na Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es Salaam (DAWASCO). 

Kikao ambacho kililenga uboreshaji na upatikanaji wa huduma ya Maji katika maeneo kadhaa ya jijini Dar es Salaam hasa maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo.

Aidha, Mwakilishi huyo wa Benki ya Dunia, ameridhishwa na juhudi za makusudi zinazofanywa na Dawasco katika kuwapatia wananchi huduma ya Majisafi, pamoja na kupambana na kiwango cha Maji kinachopotea bila sababu ya msingi. 

Ameeleza kuwa Benki ya dunia imetenga fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Majisafi na Majitaka ili kuimarisha uendeshaji wa utoaji wa huduma ya Maji kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kutekeleza kikamilifu kampeni ya “Mama Tua Ndoo Kichwani” ili kuwapunguzia akina mama wengi tatizo la Maji, kwani ndio wanaoonekana kuwa wahanga wakuu wa tatizo hilo.

Nimeridhishwa na utendaji wenu wa kazi, jinsi ambavyo mmejipanga katika kufanya kazi, hasa juhudi zenu mnazoziweka katika kupambana na upotevu wa Maji na kuwapatia wananchi huduma ya Maji alisema Bi. Bird

Naye, Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian Luhemeja ameishukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano mzuri waliouonesha, na kwamba kiasi cha fedha kilichotengwa na Benki ya Dunia kitatumika katika kuboresha na kutatua changamoto mbalimbali zinazolikabili shirika katika utoaji wa huduma ya Maji.

Changamoto ni nyingi katika utoaji wa huduma ya Maji, naamini kuwa kiasi cha fedha kilichotengwa kitasaidia kuondoa changamoto hizo alisema Mhandisi Luhemeja.

Benki ya dunia imekuwa ikifadhili miradi mingi ya maendeleo hapa nchini ikiwamo miradi mbalimbali katika sekta ya Maji, Nishati na Madini, Kilimo na Mifugo, pamoja na Uchumi na Biashara.


Thursday, October 16, 2014

Mbinu Mpya ya Majambazi

Nimepata kwa Email:

Kuna watu 3 au 4 wanapita majumbani wakidai wanatoka kampuni ya maji wamekuja kuweka bomba ya mvua ili kuokoa upotevu wa maji au watadai wanatoka Eskom au sehemu kama hizo wanabadilisha balbu bure. Wameonekana sehemu nyingi. USIWARUHUSU kuingia ndani ni wezi majambazi wa kutumia bunduki. Wataarifu wote kwenye kitabu chako cha simu kwani unaweza kuokoa maisha yao. Hakikisha milango na madirisha umefunga na usiwaruhusu watoto kuwafungulia wageni wasiowajua

Wednesday, September 11, 2013

Ziwa Lagunduliwa chini ya Jangwa Nchini Kenya!

Walikuwa wanatafuta mafuta, badala yake wakagundua maji! Kuna maji kibao chini ya janwa la Kenya. Wataalamu wanasema kuwa hayo maji yanaweza kutosheleza mahitaji ya nchi ya Kenya kwa miaka 70! Hiyo sehemu ambapo wamegundua maji ina ukame ile mbaya! Je, wakifanikiwa kuweka mabomba hayo maji yatatumika vizuri?  Na kumbuka wamegundua maji chini ya Sudan lakini bado hawajachimba kwa sababu ya vita.

 ********************************************************
 Kutoka Christian Science Monitor
 
Delaware-sized lake discovered beneath Kenya desert

Scientists say the aquifer may have enough water to fill the parched area's needs indefinitely.

Scientists using technology for discovering oil have found a vast underground water reservoir in one of Kenya’s driest regions that could supply the country's needs for nearly 70 years, potentially turning arid zones into lush farmlands
The new reserves are located in a basin in the extreme northwest that has a surface area the size of Delaware, and is estimated to hold billions of gallons, nearly nine times Kenya’s current reserves.
Almost half of Kenya’s 41 million people have no access to clean water, and farmers in arid areas struggle to raise crops without adequate irrigation.

Scientists say it is possible that, along with water run-off from surrounding hills and plains that replenish the aquifer, the newly discovered resources could fulfill the country's water demands indefinitely.

Tapping the new reserves in the basin, located in Kenya's northern Turkana region, may allow for vast new zones of farmland in landscapes where today even the hardiest plants struggle to survive.
“The news about these water reserves comes at a time when reliable water supplies are highly needed,” Judi Wakhungu, cabinet secretary at the Kenyan environment, water, and natural resources ministry, said in a statement.
“This newly found wealth of water opens a door to a more prosperous future for the people of Turkana and the nation as a whole," Ms. Wakhungu added. “We must now work to further explore these resources responsibly and safeguard them for future generations."

THE HITCH
If there is one hitch, the basin is in a remote area in the extreme northwest. It lies close to Kenya's borders with South Sudan, Ethiopia, and Uganda in an area sparsely populated and prone to conflict over existing scarce resources.
The land that lies above the reservoir is among the most hostile in Kenya. There are few roads or electricity supplies, and the Turkana, Samburu, and Pokot tribes that live there are regularly at war with each other.
The border area between Kenya, South Sudan, and Ethiopia, known as the Ilemi Triangle, has never been officially delineated.
Constructing, fueling, and maintaining boreholes, and building pipelines to bring the water supplies to remote communities, can pose significant difficulties.
WHO FOUND IT?
The discovery was made by researchers from a Texas-based company, Radar Technologies, with assistance from the Kenyan government and Unesco. The team layered satellite, radar and geological maps on top of each other and then used seismic techniques developed to find oil, to identify the reservoir.
“It is important to say that these are early estimates, and these resources must be managed well in order that they benefit the people of Kenya,” says Mohamed Djelid, Unesco’s East Africa director. “But if all goes well, we can say that this really is a game changer.”

Kenya’s government will now carry out further drilling in areas surrounding the sites where the new water supplies were first drawn to the surface, to gather more data on their full extent.
In the past there have been similar announcements of massive new water finds beneath Africa’s driest areas. In 2007, scientists said that they had identified an underground “megalake” in Sudan’s war-torn Darfur region that was 10 times the size of the Kenyan discovery, but its bounty has yet to be tapped.
“Knowing there’s water there, and then getting it to the surface, are two different things,” says Brian McSorley, a water expert at Oxfam in Nairobi. He added that, "There will need to be decent follow up studies and then proper investment to ensure that these newly-discovered resources benefit the poorest people.”

The aquifers lie as deep as 1,000 feet, which poses significant technological and cost challenges compared to shallower reserves, Mr. McSorley says but notes that, “Having said all that, the figures are encouraging and I think this needs to be cautiously welcomed.”

Thursday, February 16, 2012

Matatizo ya Kijiji cha Nanja Wilaya ya Monduli

Nafanya kazi katika Asasi inayotoa elimu ya UKIMWI na Afya ya Uzazi kwa jamii iliyopo Arusha. Mwishoni mwa mwezi huu tulifanya survey ya UKIMWI katika vijiji vya Nanja na Makuyuni vilivyopo wilaya ya Monduli kwa ajili ya mradi tunaotaka kuanza hivi karibuni.

Kilichonisukuma kuandika katika jukwaa hili ni matatizo tuliyoyakuta katika kijiji cha Nanja

HAWANA MAJI

Yaani hakuna kisima wala bomba la maji hivyo hutegemea maji ya mvua ambayo watu wachache ndio wanamatenki ya kuvunia maji hayo. Katika kipindi ambacho si cha mvua hununua maji ndoo ya lita kumi kwa tsh 300 hadi 500.

HAWANA KITUO CHA AFYA

Hakuna kituo cha afya/Zahanati wala clinic ya kutibu wanakijiji. Ikitokea kuna mgonjwa mpaka wampeleke Monduli,Makuyuni au Mto wa mbu ili waweze kupata matibabu. Kwa upande wa kinamama wajawazito wengi wao huzalishwa na wakunga wa jadii hivyo kuna uwezekano mkubwa wa vifo vya mama a mtoto.

Ombi langu kwa wanabidii kama kuna mtu aliyewahi kufanya utafiti au ana uzoefu wa maeneo haya ya Nanja aieleze jamii kuhusu sehemu hii kwakua watanzania wenzetu wanateseka.

Nawakilisha

Malima P. Macha
PM - CHAWAKUA

Wednesday, August 17, 2011

Baraza la Mawaziri Laihenyesha Ewura

Chanzo Habari Leo
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=20352


MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Haruna Masebu,amehenyeshwa kwa kuhojiwa kwa undani na Baraza la Mawaziri kuhusu kuyumbisha bei ya mafuta.

Baraza hilo lilitaka kujua kwa nini mamlaka hiyo imekuwa ikiyumbisha nchi na wananchi kuhusu bei za mafuta.

Kwa zaidi ya saa moja, Masebu na wasaidizi wake waliwekwa kiti moto kuhusu bei zilizotangazwa na Ewura mwishoni mwa wiki, ambazo zimepanda kwa asilimia sita kutoka zile zilizotangazwa awali.

Habari za kuaminika kutoka kwenye mkutano wa Baraza la Mawaziri uliofanyika jana kwenye Ukumbi wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, mjini Dodoma zinasema kuwa waziri mmoja baada ya mwingine walimhoji Masebu na wasaidizi wake kuhusu mwenendo usioridhisha wa bei za mafuta nchini.

Habari zinasema kuwa Masebu ambaye aliingia kwenye ukumbi huo akionesha kujiamini, alianza kupoteza mwelekeo kwa kadri maswali yalivyokuwa yakimiminika kutoka kwa mawaziri.

Hatimaye siyo yeye mwenyewe ama yoyote kati ya wasaidizi wake ambaye alikuwa na majibu ya kutosheleza ama hata ya kuwashawishi mawaziri kuhusu hatua hizo za Ewura na kwa kadri kikao hicho kilivyoendelea, Masebu na wenzake walionekana kukosa hoja.

Habari zinasema kuwa Masebu na wasaidizi wake walitakiwa kujielezea mbele ya Baraza la Mawaziri ili kuliwezesha Baraza hilo, chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kujiridhisha na mwenendo mzima wa bei mafuta.

Baraza hilo lilitaka ufafanuzi kuhusu bei za petroli, mafuta ya taa na dizeli; nishati ambazo ukosefu wake nusura uiingize nchi katika zahama kubwa wiki iliyopita.

Moja ya maswali ya awali kutoka kwa Baraza la Mawaziri ilikuwa ni kwa nini Masebu na Ewura walitangaza kupanda tena kwa bei za mafuta siku chache baada ya kuzishusha kwa asilimia 9.17 kwa petroli, asilimia 8.31 kwa dizeli na asilimia 8.70 kwa bei ya mafuta ya taa.

Hatua hiyo ya Ewura kupunguza bei ya mafuta ilikuwa inatekeleza uamuzi na maagizo ya Serikali yaliyotangazwa na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo Juni 22, mwaka huu, bungeni wakati alipowasilisha Bajeti ya Serikali.

Katika bajeti hiyo, Mkullo alisema kuwa Serikali iliamua kuondoa kodi na tozo kadhaa kwenye bei ya mafuta yanayoingizwa nchini kwa nia ya kupunguza bei ya bidhaa hizo ili kumpungumzia makali ya maisha mwananchi.

Hatua hiyo ya Mkullo, pamoja na ile ya Ewura kupunguza bei za mafuta ziliungwa mkono na Bunge na wananchi kwa kiwango kikubwa ambao walikiri kuwa hatua hiyo ilithibitisha jinsi gani Serikali yao inavyowajali.

Hatua ya Ewura kupunguza bei ya mafuta ilipingwa na kampuni karibu zote kubwa za kuingiza mafuta nchini ambazo zilianzisha mgomo kupinga hatua hiyo hasa BP, Engen, Oilcom na Camel Oil.

Baada ya siku moja ya mgomo huo, kampuni zingine nchini zilianza tena kuuza mafuta, lakini kampuni hizo nne zilikataa kufungua vituo vyao kuuza mafuta.

Agosti 9, mwaka huu, Ewura ilitoa amri ya Kimahakama (Compliance Order), kwa kampuni hizo nne kuanza mara moja kutoa huduma katika maghala yao na katika vituo vya rejareja vikiwemo vile vilivyoko chini ya miliki zao.

Katika amri hiyo, kampuni hizo zilitakiwa kuacha mara moja kusababisha upungufu wa makusudi wa mafuta ya petroli katika soko la Tanzania na kujieleza katika saa 24 kwa nini wasichukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka matakwa ya Sheria ya Mafuta na Utaratibu wa Ewura.

Siku iliyofuata, kampuni tatu zilianza kutoa huduma lakini BP (T) Ltd iliendelea kukaidi amri ya Ewura.

Bodi ya Ewura katika kikao chake cha Agosti 12, ilichukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kutoa onyo kali kwa kampuni za Oilcom, Camel Oil na Engen, na kuisitishia BP leseni ya biashara ya jumla ya mafuta kwa miezi mitatu na kuamuru Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo na mwenyekiti wake wa bodi wafikishwe kortini.

Lakini katika muda wa saa 48 tu, baada ya hatua hiyo ambayo iliungwa mkono na nchi nzima, Ewura ilibadilisha msimamo na mwelekeo wake na kutangaza kupandisha tena bei ya mafuta hayo ya petroli, dizeli na taa kwa asilimia tano.

Hatua hiyo ya Ewura, ilisababisha hasira ya Serikali yenyewe, Bunge, wabunge na wananchi kwa jumla.

“Ulichofanikiwa kufanya Masebu ni kuharibu kabisa mamlaka na madaraka ya Ewura. Hii ni taasisi ambayo ilikuwa imeanza kujijengea heshima kubwa kwa wananchi kwa kuchukua hatua mwafaka, na sasa mmevuruga kabisa heshima hiyo ya Ewura.

“Kwa kuvuruga heshima ya taasisi hiyo mmezitia doa siasa za nchi yetu,” waziri mmoja alimwambia ana kwa ana Masebu katika mkutano huo.

Masebu alijaribu kujitetea kwa kusema kuwa upandishaji huo wa bei ya mafuta uliofanywa na Ewura kwa mujibu wa Sheria na kwa mujibu wa makubaliano ya kuangalia upya bei kila baada ya wiki mbili kwa sababu mafuta huingizwa nchini kutoka Uarabuni kila baada ya wiki mbili.

Lakini Masebu aliambiwa kuwa hakuna mafuta yoyote yaliyoingizwa nchini tangu mvutano ulipoanza kati ya Ewura na kampuni za mafuta baada ya tangazo la kupunguza bei ya mafuta la Agosti Mosi, mwaka huu.

“Mheshimiwa Mwenyekiti ni mafuta yapi yameingia nchini kutoka Uarabuni katika wiki mbili zilizopita kwa sababu katika muda wote kwanza ulikuwepo mgomo wa kampuni za mafuta uliokolezwa zaidi na kampuni zile kubwa nne.

“Katika kipindi hiki, hakuna mafuta yaliyoingia nchini kwa sababu mafuta yalikuwepo kwenye matangi ya maghala na hayakuuzwa. Sasa Mkurugenzi anatuambia mafuta haya mapya yametoka wapi?” Alihoji waziri mmoja na kuongeza;

“Walichofanya Ewura ni kupandisha bei ya mafuta ambayo yalikuwa yamekwishafika nchini kabla ya mzozo kuanza mwanzoni mwa Agosti mwaka huu,” alisema waziri huyo.

Masebu alipojaribu kujitetea kuwa kwa taratibu za Ewura ni lazima bei za mafuta zipitiwe upya kila baada ya wiki mbili, waziri mwingine aliingia kati na kumwuliza:
“Mnapitia tu hata kama hakuna mafuta mapya yaliyoingizwa nchini kama ilivyotokea katika wiki mbili zilizopita? Mnafanya kazi kama mashine bila kutilia maanani hali halisi?” Alihoji.

Waziri mwingine alionya kuwa vitendo vya Ewura katika wiki mbili zilizopita vililenga kuyumbisha nchi na kuipeleka pabaya bila sababu za msingi.

“Inaelekea nyie Ewura mnahangaika zaidi kutetea maslahi ya wafanyabishara kuliko maslahi ya wananchi wetu,” alisema Waziri huyo.

Monday, May 03, 2010

Ukosefu wa Maji Safi Boston


Wadau, nikikukumbuka shida ya maji Bongo, lazima nicheke na vituko vya watu hapa Boston na miji kadhaa iliyoathirika shauri ya bomba kuu la majio kupasuka huko Weston.

Basi leo, huwezi kununua kahawa, wala chai. Sehemu chache walikuwa wanauza na walikuwa wanatumia maji ya chupa kutengeneza. Huko watu wanalia kukosa kahawa ya asubuhi, mimi nilileta kahawa ya unga kutoka nyumbani, nilichemsha maji ya kutoka kwenye bomba la jikoni kwenye microwave. Watu wamenishangaa mno! Walinitizama kama nina kichaa!

Nilienda Shaw's supermarket huko Fenway jana kununua mahitaji machache jana. Nilipoingia pale mbele walikuwa na zile packs za chupa 24 za maji, $3.99. Ilikuwa palate nzima. Nivyotoka zilibaki mbili tu!

Watu wameambiwa wasifue nguo wala kuosha nguo na hayo maji! Hapa kazini walitupiga marufuku kunawa mikono. Walisema ukinawa lazima utumie hand sanitizer.

Jana mzungu fulani kanipigia simu na kuniambia niwapigie watu wote kwenye idara yangu simu kuwaonya kuhusu maji. Nilimwambia kuwa huo bomba ulipasauka zaidi ya masaa 24 iliyopita, hivyo huenda watu wamekunywa. Na bila shaka watakuwa na habari kwa vile iliotangazwa kwenye vyombo voyte vya habari na miji kadhaa iliwapigia simu watu kuwaonya. Pia nilimwambi nilikuwa natoka kwenda kwenye shughuli saa hiyo. Mzungu alianza kulia oh watu wataugua sana usipowapigia simu! Jana ilikuwa jumapili!!!!

Hayo maji yanayotoka kwenye bomba ukitazama yanaonekana masafi kweli kweli. Huko Bongo watu wangesema ni salama. Wengine wangetia kwenye chupa na kuuza!

- Watu wamepigana mangumi madukani wakigombania chupa za maji.

- Poland Springs, Dasani, Everest, na hao wengine wanaotengeneza maji ya chupa wa ruka ruka kwa furaha. Shareholders wao watapata faida kubwa kweli mwaka huu!

- Maduka mengi yamepandisha bei ya maji. Mayor Menino anagomba!

- Watu wanafaya hoarding ya maji! Unakuwa mtu ana minivan imejaa maji! Sasa maduka wanawauzia watu crate mbili tu!

Lakini jamani, lazima niulize. Hivi watu wanashindwa kuchukua sufuria na kuchemsha maji ya kunywa? Huenda wamesahau! Maana siku hizi kila kitu ni take-out, microvae, frozen!

Tuesday, November 10, 2009

Kipindupindu (Cholera) Dar es Salaam

Jamani, ugonjwa wa kipindupindu umeingia tena Dar es Salaam. Kuna shida kubwa mno ya maji jijini. Watu wameongezeka lakini uwezo wa kuleta maji safi ya kutosha haipo. Watu wananunua maji ya kunywa na ya mahitaji ya nyumbani nk. kuoga, kuflashi vyoo. Lakini je, hayo maji wanoletewa ni masafi? Kuna watu wanaopitsiha maji na videbe kwenye mikokoteni, je, ni masafi? Hapo zamani za kale, eheee, uliweza kunywa maji ya bomba mjini Dar es Salaam. Hivi sasa huwezi maana watu wametoboa mabomba na mauchafu yanaingia kwenye maji! Uchafu kutoka kwenye vyoo vya shimo unaingia humo pia! Mungu Atunusuru!

Je, serikali ina mpango gani wa kuleta maji safi ya kutosha kwa wakazi wa Dar es Salaam?

******************************************************************************
Kutoka ippmedia.com

10th November 2009

18 admitted to special camps

At least 18 people in Dar es Salaam suffering from cholera, have been admitted to a special camp set up to control the disease.

Dar es Salaam City’s acting chief medical officer; Dr Hawa Kawawa said yesterday that the patients have been hospitalized in three special camps for people who have contracted cholera.
She said that the affected patients come from Temeke, Ilala and Kinondoni municipalities.
She said that one patient is from Ilala, seven are from Kinondoni and ten are from From Temeke.

“We have decided to introduce these three special camps which deal with cholera in each municipality, where full time medical doctors have been deployed,” said Kawawa.
The camps are located at Tambuka Reli in Temeke, Buguruni in Ilala and Mburahati in Kinondoni.
She said the patients were from Tabata, Tegeta-Kibaoni,Makurumla, Mburahati , Tandale, Magomeni, Tuangoma,
Tandika and Maguruwe.
According to her, medicines were available to treat the patients.
The official further underscored the need for extensive awareness campaign to address the problem, in the country’s metropolitan city.
She said the city council will introduce house-to-house inspections to ensure that surroundings were clean.
“I urge Dar es Salaam dwellers to ensure that their homes are clean all the time. And those whose surroundings would be found to be dirty would face serious consequences,” she stressed.
It was reported recently that at least 59 people have died of the disease in the past two months in the country, with the most affected being the north-eastern coastal region of Tanga.

SOURCE: THE GUARDIAN

Thursday, December 18, 2008

Tatizo la Maji DSM - Maoni ya Mdau

Tanzania sijui ni Shida sijui ni Umaskini sijui ni nini?

Baada ya wiki nzima ya mateso ya kukosa maji leo asubuhi maji yametoka hapa jijini Dar es saam na umeme ukakatika kwa hivyo vimepokezana,na kutoka kwenyewe yaani yale sio maji ni mchanganyiko wa udongo yaani kama maji ya Cocoa vile.Nikisoma baadhi ya maoni ya wabeba mabox hapa kwenye kijiji chetu cha jamii,uwa wanasema wao wanakunywa maji moja kwa moja toka bombani na bila kudhurika,nikasema lo! Wenzetu wanafaidi sana,na wanapunguza gharama za kuchemsha maji ya kunywa kwenye mkaa,maana ukidhubutu kunywa maji ambayo hayajachemshwa hapa bongo ni kujitakia kupelekwa hospitali ya rufaa kwa kipundupindu na hata kuweza kupoteza maisha kabisa.

Je vipi kuhusu mbanano wa ndani ya mabasi, imagine umepanda basi la kivukoni mbagala au Kariakoo-Mbagala,mwanangu iyo harufu ya samaki na mchanganyiko wa jasho la siku nzima kama ni mgeni lazima utazimia tu,najiuliza ni kwa nini Serikali yetu kama wao hawawezi wakaruhusu wawekezaji wakaja kuwekeza kwenye usafiri wa jumuia hapa mjini ili kuepukana na hii adha ya usafiri ambayo inaweza ikakuambukiza magojwa ya ngozi,mafua,TB na magonjwa mengine ya kuambukiza kwa hewa na mgusongamano?.

Pia uwa najiuliza wapanga miji wako wapi,wewe Mtanzania unayeishi Masaki,Mikocheni,Osterbay Mbezi beach n.k,je umewahi fika maeneo kama ya mburahati ndani ndani ukaona wenzako wanavyoishi huko,choo bado ni passport size,mifereji ya kupitisha maji taka hakuna,mvua ikinyesha vyoo vinatapishwa,unaambiwa utakuta watoto wanaogelea juu ya vinyesi vya binadamu maana ya hapo nenda sasa Amani hosp utakutana na watoto kibao wanapoteza maisha kwa kipundupindu, Tena maeneo kama hayo ukipita usithubutu kifungua kifurushi kilichofungwa cheusi cheusi hivi,wewe yaani kwa jina lingine vinaitwa vibomu huko uswahilini,basi utakutana na kinyesi nyumba zima wamejiachia humo,hii inatokea pale choo kimejaa na hakuna mvua kwa muda kuwezeka kukifungua choo kiondoke mtaani.

Yaani unaweza kusema kipindupindu ni ugonjwa wa maskini,maana idadi kubwa ya wagonjwa ni hao ni wakipato cha chini mno,

Vipi kuhusu Uchafu barabarani na barabara mbovu sizizo na mpangilio hapa town,yaani ni balaa tupu,mimi niliwahi kukaa pale Upanga toka nizaliwe hadi leo,unaambiwa hata siku moja sijaona wakiweka barabara ya rami,kipindi cha kiangazi ni vumbi hadi chumbani,kipindi cha mvua ni kukanyaga maji ya mvua nje yaliyochanganyika na maji taka yaliyoziba kwa sababu ya uchakavu wake ,maana nahisi toka wahindi waijenge enzi hizo hadi leo haijaweza kurekebishwa na watu ndo ivyo wanazidi kuongezeka,Sasa hapo Serikali za mitaa zinafanya nini au ziko kwa ajili ya nini.

Achana na hilo,hadi leo tumekosa kabisa wazoa taka wa kuweza kusema taka zinazolewa hakuna,magari ni mabovu yaani sio Gari la takataka ni Gari taka.na wale wanaozoa wenyewe hawana groves,mabuti wala mask za kuzuia harufu ya uchafu,na utakuta wanakaa juu ya uchafu.

Elimu yetu je ikoje,leo hii ukitaka kuomba kazi lazima waandike uwe unajua kiingereza safi cha kuandiaka na kuongea,mimi kajamba nani vyeti ninavyo lakini School bus huko sekondari na primary sijapanda(yaani sijasoma shule ya kizungu)hivyo kiingereza changu si salama sana. Na watu kama mimi hapa bongo tuko wengi kuliko hao waliopanda School bus,sasa hapo hauoni wametutenga?.

Mimi nasema viongozi wetu wanabahati sana,wanatoa ahadi na hawatekelezi vilevile lakini wananchi wao tumetulia tuli kama maji mtungini tukiomba ipo siku tutakuwa kama angalau mazingira kama Ulaya(Lol)

Umewahi kutembelea mbuga za wanyama kama mkiwa group hivi mmetoka Dar mnakwenda huko,labda vyumba mlivyofikia jirani na vyumba vya wazungu watalii,basi mkiongea na kucheka kwa nguvu,wahudumu wanawafuata,nyie mbona mnapiga makelele kuna wageni watawashangaa.mnyamaze au tutawahamisha,lakini huko mnawasikia hao wageni wazungu wakiongea na kupiga makelele kweli,wangine wanaimba na kucheza hadi usiku kweli,tena nyie mlionyamaza sasa hata usingizi mnakosa kuwasubiri hao wageni hadi nao wachoke walale.Sasa sielewi makelele ya wazungu watalii ni mazuri kuliko makelele ya Wa Tz watalii.

Kuna vitu vingi sana vinaumiza Bongo,kama Rushwa,Kodi kubwa zinazomuumiza mTanzania,Mikataba inayonufaisha wachache n.k

Wadau mimi nafikiri hii Blog inasomwa hata na Serikali yetu sasa tunaweza labda kuwapa maoni wafanye nini ili na sisi tuwe na unafuu hapa Nchini kwetu.

Mdau Dar es Salaam

Tatizo la Maji Dar!


Hivi jamani, kwa nini baada ya siku kumi maji bado ni tatizo mjini Dar es Salaam. Na ni miaka mingapi baada ya Uhuru? Ni aibu kwa Dar kuwa na tatizo la maji kama Harare au Monrovia enzi za vita! Aibu kubwa sana.

Wale wataalam wa maji waliosomeshwa na Chuo cha Maji nk. wako wapi? Kuna nini hasa kinachofanya maji yaye ya shida hivyo wakati tumebarikiwa ma maziwa makubwa kama Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa na mito kibao!

Nakumbuka enzi zile sisi tuliokuwa tunaishi Chuo Kikuu cha DSM tulikuwa tunachekwa kwa sababu ya matatizo ya maji. Walikuwa wanashindwa kuyapandisha mlimani eti.

Serikali infanya nini kutatua matatizo ya maji? Wasipofanya kitu tutasikia watu wanaugua kipindupindu na magonjwa mengine ya kuharisha.


*****************************************************

Kutoka ippmedia.com

Dar vendors pray for prolonged water scarcity

2008-12-18
By Correspondent Gadiosa Lamtey

An acute water shortage that had hit Dar es Salaam and its outskirts for the past ten days, had turned into a blessing in disguise for others.

Vendors selling the precious liquid have been making lucrative business, praying for the scarcity to continue a little bit longer.

A vendor, Hamisi Majaliwa, said God had listened to their prayers as they could now afford to celebrate the year end festivals.

``The scarcity guarantees my daily bread. I no longer worry about celebrating Christmas because I have earned quite a sum over the past few days,`` said Majaliwa.

A survey conducted by The Guardian across the country`s commercial hub found out that the scarcity was getting worse, with a 20-litre gallon of tap water selling at between 800/- and 1,000/- respectively.

The high prices have forced some low income earners in the city to resort to drawing water from the drainage system, thus inviting grave health risks.

Margaret Richard, a resident of Ubungo suburb, said she resorted to buying bottled water as it was safe to cook and brush her teeth with.

``I am skeptical with the water sold by street vendors,? said Margaret.

She said the scarcity had made vendors fetch water from any place for the sake of money, while ignoring all the health risks.

``Worse still, their prices are unfair,`` she said. Margaret, however, wondered how the unemployed and housewives afford buying water from street vendors.

``I can`t blame vendors because survival is for the fittest. Everyone must earn their bread. However, I call upon Dawasco to speed up their efforts to restore water supply.

Dar es Salaam is densely populated. No one will survive should it happen that there is a cholera outbreak,`` said Margaret.

Alfa Laizer of Kinondoni said some people had already suffered after consuming salty water drawn from shallow wells.

Laizer said: ``Salty water is only good for washing clothes and house cleaning, but you can`t use it to cook or drink. Some people are already becoming allergic from bathing salty water.``

``We are not comfortable with what is going on, although we are aware what the problem is.

The authorities should find a solution before the situation gets worse, especially for children,`` he said.

A resident of Chang`ombe, Fatuma Kamugisha, said water had become as precious as gold but the digging of boreholes had in a way helped to avert the problem.

When contacted for comments, Dawasco public relations officer Mary Lyimo said their engineers were busy working on a defective transformer.

``Since last Saturday, our engineers have been tirelessly working on the transformer and by tomorrow (yesterday) things will be back to normal,`` she confidently said.

Last week, Dawasco announced that the city would temporarily go without water because of a defective transformer that supplies power to water pumps at Lower Ruvu.

As we went to press, Dawasco public relations officer Mary Lyimo said water supply had been restored in several Dar es Salaam suburbs, except Magomeni, Sinza, Mwenge and Ilala.

She said problems affecting such areas would be sorted out within the shortest possible time
``It will not take long to normalize the city supply. The delay has been caused by low pressure from our pumping machines,`` she said.

SOURCE: Guardian

Tuesday, March 25, 2008

DAWASCO kuwa na viosk Dar

Tuone kama watakuwa na mafanikio. Au tutasikia hajkuna maji ila kwa wanaoweza 'kuongeza kidogo'. System ya maji inahaitaji kukarabatiwa. Si ni ile ile aliyoacha mkoloni iliyojengwa kuhudumia watu milioni moja tu?

****************************************************************

Dawasco to introduce 300 water selling kiosks

2008-03-21

By Our Correspondent

The Dar es Salaam Water and Sewerage Corporation (Dawasco) has announced new plans to use trucks to distribute water at designated selling points in Dar es Salaam. The water utility firm says it will introduce kiosks and start physical distribution of water, apart from installing water pipes.

Dawasco Public Relations Manager Badra Masoud told The Guardian that water kiosks would be placed in areas that face acute water crisis, adding that the services would be offered at affordable price. According to the official, a 10-litre container will be selling at 20/- and a 20-litre one at 30/-.

``The facility will be managed by DAWASCO employees. A respected and trustworthy member of the community will be picked to manage these kiosks,`` said Masoud. On the monitoring of sales, she said the company would directly deal with the appointed sales persons who would be required to submit collected money against meter records.

Masoud said collections from the respective water points would be divided equitably - part of the money would go to the maintenance of the facility and the other for paying the salary of the manager. According to the official, Dawasco has drawn up a two-year plan to put up 300 water-kiosks in Dar es Salaam. She added that all problematic areas would be covered satisfactorily.

Meanwhile, DAWASCO has dismissed as baseless claims that its workers have polluted the water source at Ruvu, saying the security level at the location was too high for that to be done.

``Those were mere rumours. No one is allowed to stay close to the source. Even those who are going for a study tour must be scrutinised thoroughly before they are allowed in. How come that a stranger could find his way in? asked Masoud.

As part of Water Week celebrations, a number of Dar es Salaam residents turned up at Mnazi Mmoja grounds to clear their outstanding debt balances, according to the official.

SOURCE: Guardian

Thursday, March 13, 2008

Kipanya na Maji

Translation:

Mzungu - We have succeeded in reducing unnecessary water usage by 50 percent.

Arab - We recycle waste water for other usage.

Tanzanian - If there is an award we should get it! We hold back our water supply almost 100 percent. WE DON'T EVEN SUPPLY WATER!

Monday, March 10, 2008

Madawa yakutwa kwenye Maji ya Kunywa Marekani



Hii habari mbona inatisha! Madawa ya aina mbalimbali yamekutwa kwenye maji ya kunywa Marekani kwenye miji mbalimbali. Kumbe ingawa maji machafu yanasafishwa (recycling) bado kuna kuwa na madawa mle. Watu wanameza wanajisaidia yanaingia kwenye maji machafu lakini process ya kusafisha haiondoi kila kitu. Aarrgh!

**********************************************

-- A vast array of pharmaceuticals -- including antibiotics, anti-convulsants, mood stabilizers and sex hormones -- have been found in the drinking water supplies of at least 41 million Americans, an Associated Press investigation shows.

Officials in Philadelphia say testing there discovered 56 pharmaceuticals or byproducts in treated drinking water.

To be sure, the concentrations of these pharmaceuticals are tiny, measured in quantities of parts per billion or trillion, far below the levels of a medical dose. Also, utilities insist their water is safe.
But the presence of so many prescription drugs -- and over-the-counter medicines like acetaminophen and ibuprofen -- in so much of our drinking water is heightening worries among scientists of long-term consequences to human health.

In the course of a five-month inquiry, the AP discovered that drugs have been detected in the drinking water supplies of 24 major metropolitan areas -- from Southern California to Northern New Jersey, from Detroit, Michigan, to Louisville, Kentucky.
Kwa story nzima BOFYA HAPA

Tuesday, March 04, 2008

Mji wa Dar es Salaam kukosa Maji siku Tano!


Wadau huko Dar, naomba mtueleze hali ilivyo kule. Poleni sana!
*****************************************************************
TANGAZO.
Dar kukosa maji siku tano

Kutoka Food for Thought Blog

JIJI la Dar es Salaam, litakumbwa na uhaba wa maji kwa muda wa siku tano kuanzia leo.Taarifa ya kukosekana huko kwa maji imetolewa jana kwa vyombo vya habari na Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam na Pwani (DAWASCO) kwa niaba ya Shirika la Majisafi na Majitaka (DAWASA).

Hata hivyo, ukosekanaji wa maji hayo ambao unatokana na kufanyiwa ukarabati mkubwa wa mtambo wa Ruvu Juu utayakumba baadhi ya maeneo ya jiji.Kwa mujibu wa Dawasco, ukarabati huo mkubwa wa mtambo umearifiwa kufanywa na Shirika la Majisafi na Majitaka (Dawasa).
“Dawasa inawataarifu wakazi wa jiji kwamba mtambo wa kuzalisha maji wa Ruvu Juu utafanyiwa ukarabati mkubwa kwa siku tano mfululizo kuanzia Jumatatu Machi 3 hadi Ijumaa Machi 7, 2008 hivyo kusababisha kutopatikana kabisa kwa maji baadhi ya maeneo ya jiji,’ ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa maeneo yaliyotajwa kukumbwa na ukosefu huo wa maji ni ambayo yanapata maji kutoka Ruvu juu.

Maeneo hayo ni Kibaha, mkoani Pwani, Kibamba, Mbezi, Kimara, Changanyikeni, Ubungo, Kibangu, Makuburi, Tabata na Kisukuru. Dawasa imewaomba radhi wateja wake kwa usumbusu utakaotokea wakati wa ukarabati huo.

Friday, December 07, 2007

Vigogo wakatiwa maji

Kama umekaa Dar lazima umekumbwa na tatizo la kukosa maji. Unaweza kusikia eneo fulani umekosa maji kwa karibu wiki! Siku hizi biashara ya kuuza maji, na matenki ya maji umekuwa kubwa kweli kweli. Hiyo ni kwa vile maji ya bomba hayamiki usafi wake, na pia hakuna uhakika kuwa kutakuwa na maji kwenye mabomba.

Sijui wanaweza kufanya nini mjini Dar kupata suluhisho ya kudumu ya tatizo la maji. Ujenzi holela una maana mabomba ya maji yameunganishwa ovyo. Kama mtu una bahasha ya kutosha utapata maji. Wengine wanaofuata sheria za kupata huduma ya maji hawapatiwi. Na wengine hawapati bili kabisa wengine wanapata bili kubwa aajabu.

Jana, DAWASCO, ilikata huduma ya maji kwenye nyumba za baadhi ya mawaziri na manaibu wao kwa vile walikuwa na bili za muda mrefu ambazo hazijalipwa. Nawapongeza kwa hatua hiyo. Natumaini hizo bili zitalipwa sasa. Serikali watunge sheria kuwachukulia hatua kali watu wanaozuia wasoma mita kufanya kazi yao. Kama hutaki mtu asome mita basi usiwe na huduma ya maji!

Tatizo siyo hao vigogo tu, kuna tatizo kubwa zaidi. Maji mengi yanapotea kutoka 'source' (chanzo) mpaka yanafika kwa mteja. Watu wametoboa mabomba makusudi kuiba maji. Mabomba mengine yanavuja. Je, DAWASCO inajua kila sehemu mambomba yametobolewa?Hakuna usimamizi mzuri wa kukagua watu wanaojenga juu ya mabomba makubwa. Mtu anachimba choo na kinatoboa bomba la maji, hajali, uko uchafu unaingia kwenye 'maji safi'!

Lazima serikali iingilie swala ya maji. Swala huu inazidi kuwa sugu miaka inavyozidi kwenda.

Enzi za Ujamaa, Mwalimu aliahidi kila mTanzania atakuwa na maji safi karibu. Bado kabisa!

************************************************************************

Mawaziri wakatiwa maji
2007-12-07

Shirika la Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASCO), jana lilifanya kweli kwa kuwakatia maji baadhi ya Mawaziri na Naibu wao kadhaa wanaoishi maeneo ya Masaki na Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam kutokana na malimbikizo makubwa ya bili zao. hatua hiyo ilikuja baada ya mwanzoni mwa wiki, DAWASCO kueleza bayana azma yake ya kuwakatia maji vigogo hao kwa maelezo kuwa madeni yao ni ya muda mrefu.

Uchunguzi uliofanywa na Nipashe umebaini kuwa, hadi kufikia jana, Mawaziri na Naibu wao kadhaa, tayari walikuwa wamekatiwa huduma hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea vituo mbalimbali vya DAWASCO jijini jana, Meneja Uhusiano wa mamlaka hiyo, Bi. Badra Masoud, alisema huduma ya maji ilikatwa eneo la Masaki asubuhi na zoezi la kukata maji eneo la Mbezi Beach, lilikuwa likielekea kukamilika.

Alisema zoezi hilo pia litaendelea katika maeneo ya Msasani, Mikocheni, Ada Estate, Mikocheni na Mwenge. Alisema baada ya ziara hiyo, amegundua kwamba wananchi wengi wamejitokeza kulipia ankara zao, ili kuepuka usumbufu na adha ya kukatiwa maji. Hata hivyo, Bi. Badra alisema bado kiwango cha ukusanyaji wa madeni hakiridhishi, hivyo hawatasitisha zoezi hilo. Alisema wamebaini kwamba watu ambao hawalipi bili ya maji wengi wao ni wale wenye uwezo na vipato vikubwa, na hatua yao ya kutolipa inatokana na kupuuza wajibu wao.
Bi.
Badra alisema visingizio vya kusema mimi sijapata ankara ya mwezi huu au ule, havitasikilizwa na wala havisaidii. Alisema imekuwa tabia ya wateja wakishakatiwa huduma hiyo, hutoa visingizio kama “Unajua mimi ni mtu wa kusafirisafiri sana au silipi kwa vile sijapatiwa ankra” Bi. Badra alisema suala la kusafiri na kukosa nafasi ya kulipa bili haliingii akilini kwa vile DAWASCO inaendelea kuwapatia huduma. Pia alisema si kweli kwamba kuna mteja ambaye hapelekewi ankara.

Katika kituo cha Kawe, ambacho kinawahudumia watu wa maeneo ya Mbezi, wafanyakazi walimlalamikia Bi. Badra kwamba wanapata adha kubwa, za kutukanwa, kukimbizwa na Mbwa na kutishiwa maisha, wanapokwenda kusoma mita.
Mmoja wa wafanyakazi hao, alimweleza Meneja huyo kwamba kuna siku aliwekwa `rumande` ndani ya chumba cha mkaa cha kigogo mmoja huko Mbezi beach, baada ya kuonekana akisoma mita ya maji.

Mfanyakazi mwingine alisema Sisi wafanyakazi wa Dawasco wanatuona nuksi kiasi cha kufukuzwa na walinzi tunapofika kusoma mita, yote hayo yanatokana na ukweli kwamba watu hawataki kulipa bili. Akihitimisha ziara hiyo katika Kituo cha kinondoni, Bi. Badra aliwataka wateja wa DAWASCO, waelewe kwamba mamlaka hiyo inatumia gharama kubwa kuwapatia huduma ya maji hivyo wajenge moyo wa kulipa, ili kurahizisha kazi ya kuwapatia watu wengi zaidi huduma hiyo muhimu.