Friday, July 28, 2017
Thursday, January 05, 2017
Friday, August 19, 2016
Benki ya Dunia Kuendelea Kusaidia Sekta ya Maji Nchini
Thursday, October 16, 2014
Mbinu Mpya ya Majambazi
Kuna watu 3 au 4 wanapita majumbani wakidai wanatoka kampuni ya maji wamekuja kuweka bomba ya mvua ili kuokoa upotevu wa maji au watadai wanatoka Eskom au sehemu kama hizo wanabadilisha balbu bure. Wameonekana sehemu nyingi. USIWARUHUSU kuingia ndani ni wezi majambazi wa kutumia bunduki. Wataarifu wote kwenye kitabu chako cha simu kwani unaweza kuokoa maisha yao. Hakikisha milango na madirisha umefunga na usiwaruhusu watoto kuwafungulia wageni wasiowajua
Wednesday, September 11, 2013
Ziwa Lagunduliwa chini ya Jangwa Nchini Kenya!
********************************************************
Kutoka Christian Science Monitor
Delaware-sized lake discovered beneath Kenya desert
Scientists say the aquifer may have enough water to fill the parched area's needs indefinitely.
The new reserves are located in a basin in the extreme northwest that has a surface area the size of Delaware, and is estimated to hold billions of gallons, nearly nine times Kenya’s current reserves.
Almost half of Kenya’s 41 million people have no access to clean water, and farmers in arid areas struggle to raise crops without adequate irrigation.
Scientists say it is possible that, along with water run-off from surrounding hills and plains that replenish the aquifer, the newly discovered resources could fulfill the country's water demands indefinitely.
Tapping the new reserves in the basin, located in Kenya's northern Turkana region, may allow for vast new zones of farmland in landscapes where today even the hardiest plants struggle to survive.
“The news about these water reserves comes at a time when reliable water supplies are highly needed,” Judi Wakhungu, cabinet secretary at the Kenyan environment, water, and natural resources ministry, said in a statement.
“This newly found wealth of water opens a door to a more prosperous future for the people of Turkana and the nation as a whole," Ms. Wakhungu added. “We must now work to further explore these resources responsibly and safeguard them for future generations."
THE HITCH
If there is one hitch, the basin is in a remote area in the extreme northwest. It lies close to Kenya's borders with South Sudan, Ethiopia, and Uganda in an area sparsely populated and prone to conflict over existing scarce resources.
The land that lies above the reservoir is among the most hostile in Kenya. There are few roads or electricity supplies, and the Turkana, Samburu, and Pokot tribes that live there are regularly at war with each other.
The border area between Kenya, South Sudan, and Ethiopia, known as the Ilemi Triangle, has never been officially delineated.
Constructing, fueling, and maintaining boreholes, and building pipelines to bring the water supplies to remote communities, can pose significant difficulties.
WHO FOUND IT?
The discovery was made by researchers from a Texas-based company, Radar Technologies, with assistance from the Kenyan government and Unesco. The team layered satellite, radar and geological maps on top of each other and then used seismic techniques developed to find oil, to identify the reservoir.
“It is important to say that these are early estimates, and these resources must be managed well in order that they benefit the people of Kenya,” says Mohamed Djelid, Unesco’s East Africa director. “But if all goes well, we can say that this really is a game changer.”
Kenya’s government will now carry out further drilling in areas surrounding the sites where the new water supplies were first drawn to the surface, to gather more data on their full extent.
In the past there have been similar announcements of massive new water finds beneath Africa’s driest areas. In 2007, scientists said that they had identified an underground “megalake” in Sudan’s war-torn Darfur region that was 10 times the size of the Kenyan discovery, but its bounty has yet to be tapped.
“Knowing there’s water there, and then getting it to the surface, are two different things,” says Brian McSorley, a water expert at Oxfam in Nairobi. He added that, "There will need to be decent follow up studies and then proper investment to ensure that these newly-discovered resources benefit the poorest people.”
The aquifers lie as deep as 1,000 feet, which poses significant technological and cost challenges compared to shallower reserves, Mr. McSorley says but notes that, “Having said all that, the figures are encouraging and I think this needs to be cautiously welcomed.”
Thursday, February 16, 2012
Matatizo ya Kijiji cha Nanja Wilaya ya Monduli
Kilichonisukuma kuandika katika jukwaa hili ni matatizo tuliyoyakuta katika kijiji cha Nanja
HAWANA MAJI
Yaani hakuna kisima wala bomba la maji hivyo hutegemea maji ya mvua ambayo watu wachache ndio wanamatenki ya kuvunia maji hayo. Katika kipindi ambacho si cha mvua hununua maji ndoo ya lita kumi kwa tsh 300 hadi 500.
HAWANA KITUO CHA AFYA
Hakuna kituo cha afya/Zahanati wala clinic ya kutibu wanakijiji. Ikitokea kuna mgonjwa mpaka wampeleke Monduli,Makuyuni au Mto wa mbu ili waweze kupata matibabu. Kwa upande wa kinamama wajawazito wengi wao huzalishwa na wakunga wa jadii hivyo kuna uwezekano mkubwa wa vifo vya mama a mtoto.
Ombi langu kwa wanabidii kama kuna mtu aliyewahi kufanya utafiti au ana uzoefu wa maeneo haya ya Nanja aieleze jamii kuhusu sehemu hii kwakua watanzania wenzetu wanateseka.
Nawakilisha
Malima P. Macha
PM - CHAWAKUA
Wednesday, August 17, 2011
Baraza la Mawaziri Laihenyesha Ewura
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=20352
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Haruna Masebu,amehenyeshwa kwa kuhojiwa kwa undani na Baraza la Mawaziri kuhusu kuyumbisha bei ya mafuta.
Baraza hilo lilitaka kujua kwa nini mamlaka hiyo imekuwa ikiyumbisha nchi na wananchi kuhusu bei za mafuta.
Kwa zaidi ya saa moja, Masebu na wasaidizi wake waliwekwa kiti moto kuhusu bei zilizotangazwa na Ewura mwishoni mwa wiki, ambazo zimepanda kwa asilimia sita kutoka zile zilizotangazwa awali.
Habari za kuaminika kutoka kwenye mkutano wa Baraza la Mawaziri uliofanyika jana kwenye Ukumbi wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, mjini Dodoma zinasema kuwa waziri mmoja baada ya mwingine walimhoji Masebu na wasaidizi wake kuhusu mwenendo usioridhisha wa bei za mafuta nchini.
Habari zinasema kuwa Masebu ambaye aliingia kwenye ukumbi huo akionesha kujiamini, alianza kupoteza mwelekeo kwa kadri maswali yalivyokuwa yakimiminika kutoka kwa mawaziri.
Hatimaye siyo yeye mwenyewe ama yoyote kati ya wasaidizi wake ambaye alikuwa na majibu ya kutosheleza ama hata ya kuwashawishi mawaziri kuhusu hatua hizo za Ewura na kwa kadri kikao hicho kilivyoendelea, Masebu na wenzake walionekana kukosa hoja.
Habari zinasema kuwa Masebu na wasaidizi wake walitakiwa kujielezea mbele ya Baraza la Mawaziri ili kuliwezesha Baraza hilo, chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kujiridhisha na mwenendo mzima wa bei mafuta.
Baraza hilo lilitaka ufafanuzi kuhusu bei za petroli, mafuta ya taa na dizeli; nishati ambazo ukosefu wake nusura uiingize nchi katika zahama kubwa wiki iliyopita.
Moja ya maswali ya awali kutoka kwa Baraza la Mawaziri ilikuwa ni kwa nini Masebu na Ewura walitangaza kupanda tena kwa bei za mafuta siku chache baada ya kuzishusha kwa asilimia 9.17 kwa petroli, asilimia 8.31 kwa dizeli na asilimia 8.70 kwa bei ya mafuta ya taa.
Hatua hiyo ya Ewura kupunguza bei ya mafuta ilikuwa inatekeleza uamuzi na maagizo ya Serikali yaliyotangazwa na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo Juni 22, mwaka huu, bungeni wakati alipowasilisha Bajeti ya Serikali.
Katika bajeti hiyo, Mkullo alisema kuwa Serikali iliamua kuondoa kodi na tozo kadhaa kwenye bei ya mafuta yanayoingizwa nchini kwa nia ya kupunguza bei ya bidhaa hizo ili kumpungumzia makali ya maisha mwananchi.
Hatua hiyo ya Mkullo, pamoja na ile ya Ewura kupunguza bei za mafuta ziliungwa mkono na Bunge na wananchi kwa kiwango kikubwa ambao walikiri kuwa hatua hiyo ilithibitisha jinsi gani Serikali yao inavyowajali.
Hatua ya Ewura kupunguza bei ya mafuta ilipingwa na kampuni karibu zote kubwa za kuingiza mafuta nchini ambazo zilianzisha mgomo kupinga hatua hiyo hasa BP, Engen, Oilcom na Camel Oil.
Baada ya siku moja ya mgomo huo, kampuni zingine nchini zilianza tena kuuza mafuta, lakini kampuni hizo nne zilikataa kufungua vituo vyao kuuza mafuta.
Agosti 9, mwaka huu, Ewura ilitoa amri ya Kimahakama (Compliance Order), kwa kampuni hizo nne kuanza mara moja kutoa huduma katika maghala yao na katika vituo vya rejareja vikiwemo vile vilivyoko chini ya miliki zao.
Katika amri hiyo, kampuni hizo zilitakiwa kuacha mara moja kusababisha upungufu wa makusudi wa mafuta ya petroli katika soko la Tanzania na kujieleza katika saa 24 kwa nini wasichukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka matakwa ya Sheria ya Mafuta na Utaratibu wa Ewura.
Siku iliyofuata, kampuni tatu zilianza kutoa huduma lakini BP (T) Ltd iliendelea kukaidi amri ya Ewura.
Bodi ya Ewura katika kikao chake cha Agosti 12, ilichukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kutoa onyo kali kwa kampuni za Oilcom, Camel Oil na Engen, na kuisitishia BP leseni ya biashara ya jumla ya mafuta kwa miezi mitatu na kuamuru Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo na mwenyekiti wake wa bodi wafikishwe kortini.
Lakini katika muda wa saa 48 tu, baada ya hatua hiyo ambayo iliungwa mkono na nchi nzima, Ewura ilibadilisha msimamo na mwelekeo wake na kutangaza kupandisha tena bei ya mafuta hayo ya petroli, dizeli na taa kwa asilimia tano.
Hatua hiyo ya Ewura, ilisababisha hasira ya Serikali yenyewe, Bunge, wabunge na wananchi kwa jumla.
“Ulichofanikiwa kufanya Masebu ni kuharibu kabisa mamlaka na madaraka ya Ewura. Hii ni taasisi ambayo ilikuwa imeanza kujijengea heshima kubwa kwa wananchi kwa kuchukua hatua mwafaka, na sasa mmevuruga kabisa heshima hiyo ya Ewura.
“Kwa kuvuruga heshima ya taasisi hiyo mmezitia doa siasa za nchi yetu,” waziri mmoja alimwambia ana kwa ana Masebu katika mkutano huo.
Masebu alijaribu kujitetea kwa kusema kuwa upandishaji huo wa bei ya mafuta uliofanywa na Ewura kwa mujibu wa Sheria na kwa mujibu wa makubaliano ya kuangalia upya bei kila baada ya wiki mbili kwa sababu mafuta huingizwa nchini kutoka Uarabuni kila baada ya wiki mbili.
Lakini Masebu aliambiwa kuwa hakuna mafuta yoyote yaliyoingizwa nchini tangu mvutano ulipoanza kati ya Ewura na kampuni za mafuta baada ya tangazo la kupunguza bei ya mafuta la Agosti Mosi, mwaka huu.
“Mheshimiwa Mwenyekiti ni mafuta yapi yameingia nchini kutoka Uarabuni katika wiki mbili zilizopita kwa sababu katika muda wote kwanza ulikuwepo mgomo wa kampuni za mafuta uliokolezwa zaidi na kampuni zile kubwa nne.
“Katika kipindi hiki, hakuna mafuta yaliyoingia nchini kwa sababu mafuta yalikuwepo kwenye matangi ya maghala na hayakuuzwa. Sasa Mkurugenzi anatuambia mafuta haya mapya yametoka wapi?” Alihoji waziri mmoja na kuongeza;
“Walichofanya Ewura ni kupandisha bei ya mafuta ambayo yalikuwa yamekwishafika nchini kabla ya mzozo kuanza mwanzoni mwa Agosti mwaka huu,” alisema waziri huyo.
Masebu alipojaribu kujitetea kuwa kwa taratibu za Ewura ni lazima bei za mafuta zipitiwe upya kila baada ya wiki mbili, waziri mwingine aliingia kati na kumwuliza:
“Mnapitia tu hata kama hakuna mafuta mapya yaliyoingizwa nchini kama ilivyotokea katika wiki mbili zilizopita? Mnafanya kazi kama mashine bila kutilia maanani hali halisi?” Alihoji.
Waziri mwingine alionya kuwa vitendo vya Ewura katika wiki mbili zilizopita vililenga kuyumbisha nchi na kuipeleka pabaya bila sababu za msingi.
“Inaelekea nyie Ewura mnahangaika zaidi kutetea maslahi ya wafanyabishara kuliko maslahi ya wananchi wetu,” alisema Waziri huyo.
Monday, May 03, 2010
Ukosefu wa Maji Safi Boston

Wadau, nikikukumbuka shida ya maji Bongo, lazima nicheke na vituko vya watu hapa Boston na miji kadhaa iliyoathirika shauri ya bomba kuu la majio kupasuka huko Weston.
Basi leo, huwezi kununua kahawa, wala chai. Sehemu chache walikuwa wanauza na walikuwa wanatumia maji ya chupa kutengeneza. Huko watu wanalia kukosa kahawa ya asubuhi, mimi nilileta kahawa ya unga kutoka nyumbani, nilichemsha maji ya kutoka kwenye bomba la jikoni kwenye microwave. Watu wamenishangaa mno! Walinitizama kama nina kichaa!
Nilienda Shaw's supermarket huko Fenway jana kununua mahitaji machache jana. Nilipoingia pale mbele walikuwa na zile packs za chupa 24 za maji, $3.99. Ilikuwa palate nzima. Nivyotoka zilibaki mbili tu!
Watu wameambiwa wasifue nguo wala kuosha nguo na hayo maji! Hapa kazini walitupiga marufuku kunawa mikono. Walisema ukinawa lazima utumie hand sanitizer.
Jana mzungu fulani kanipigia simu na kuniambia niwapigie watu wote kwenye idara yangu simu kuwaonya kuhusu maji. Nilimwambia kuwa huo bomba ulipasauka zaidi ya masaa 24 iliyopita, hivyo huenda watu wamekunywa. Na bila shaka watakuwa na habari kwa vile iliotangazwa kwenye vyombo voyte vya habari na miji kadhaa iliwapigia simu watu kuwaonya. Pia nilimwambi nilikuwa natoka kwenda kwenye shughuli saa hiyo. Mzungu alianza kulia oh watu wataugua sana usipowapigia simu! Jana ilikuwa jumapili!!!!
Hayo maji yanayotoka kwenye bomba ukitazama yanaonekana masafi kweli kweli. Huko Bongo watu wangesema ni salama. Wengine wangetia kwenye chupa na kuuza!
- Watu wamepigana mangumi madukani wakigombania chupa za maji.
- Poland Springs, Dasani, Everest, na hao wengine wanaotengeneza maji ya chupa wa ruka ruka kwa furaha. Shareholders wao watapata faida kubwa kweli mwaka huu!
- Maduka mengi yamepandisha bei ya maji. Mayor Menino anagomba!
- Watu wanafaya hoarding ya maji! Unakuwa mtu ana minivan imejaa maji! Sasa maduka wanawauzia watu crate mbili tu!
Lakini jamani, lazima niulize. Hivi watu wanashindwa kuchukua sufuria na kuchemsha maji ya kunywa? Huenda wamesahau! Maana siku hizi kila kitu ni take-out, microvae, frozen!
Tuesday, November 10, 2009
Kipindupindu (Cholera) Dar es Salaam
Je, serikali ina mpango gani wa kuleta maji safi ya kutosha kwa wakazi wa Dar es Salaam?
******************************************************************************
Kutoka ippmedia.com
10th November 2009
18 admitted to special camps
At least 18 people in Dar es Salaam suffering from cholera, have been admitted to a special camp set up to control the disease.
Dar es Salaam City’s acting chief medical officer; Dr Hawa Kawawa said yesterday that the patients have been hospitalized in three special camps for people who have contracted cholera.
She said that the affected patients come from Temeke, Ilala and Kinondoni municipalities.
She said that one patient is from Ilala, seven are from Kinondoni and ten are from From Temeke.
“We have decided to introduce these three special camps which deal with cholera in each municipality, where full time medical doctors have been deployed,” said Kawawa.
The camps are located at Tambuka Reli in Temeke, Buguruni in Ilala and Mburahati in Kinondoni.
She said the patients were from Tabata, Tegeta-Kibaoni,Makurumla, Mburahati , Tandale, Magomeni, Tuangoma,
Tandika and Maguruwe.
According to her, medicines were available to treat the patients.
The official further underscored the need for extensive awareness campaign to address the problem, in the country’s metropolitan city.
She said the city council will introduce house-to-house inspections to ensure that surroundings were clean.
“I urge Dar es Salaam dwellers to ensure that their homes are clean all the time. And those whose surroundings would be found to be dirty would face serious consequences,” she stressed.
It was reported recently that at least 59 people have died of the disease in the past two months in the country, with the most affected being the north-eastern coastal region of Tanga.
SOURCE: THE GUARDIAN
Thursday, December 18, 2008
Tatizo la Maji DSM - Maoni ya Mdau
Baada ya wiki nzima ya mateso ya kukosa maji leo asubuhi maji yametoka hapa jijini Dar es saam na umeme ukakatika kwa hivyo vimepokezana,na kutoka kwenyewe yaani yale sio maji ni mchanganyiko wa udongo yaani kama maji ya Cocoa vile.Nikisoma baadhi ya maoni ya wabeba mabox hapa kwenye kijiji chetu cha jamii,uwa wanasema wao wanakunywa maji moja kwa moja toka bombani na bila kudhurika,nikasema lo! Wenzetu wanafaidi sana,na wanapunguza gharama za kuchemsha maji ya kunywa kwenye mkaa,maana ukidhubutu kunywa maji ambayo hayajachemshwa hapa bongo ni kujitakia kupelekwa hospitali ya rufaa kwa kipundupindu na hata kuweza kupoteza maisha kabisa.
Je vipi kuhusu mbanano wa ndani ya mabasi, imagine umepanda basi la kivukoni mbagala au Kariakoo-Mbagala,mwanangu iyo harufu ya samaki na mchanganyiko wa jasho la siku nzima kama ni mgeni lazima utazimia tu,najiuliza ni kwa nini Serikali yetu kama wao hawawezi wakaruhusu wawekezaji wakaja kuwekeza kwenye usafiri wa jumuia hapa mjini ili kuepukana na hii adha ya usafiri ambayo inaweza ikakuambukiza magojwa ya ngozi,mafua,TB na magonjwa mengine ya kuambukiza kwa hewa na mgusongamano?.
Pia uwa najiuliza wapanga miji wako wapi,wewe Mtanzania unayeishi Masaki,Mikocheni,Osterbay Mbezi beach n.k,je umewahi fika maeneo kama ya mburahati ndani ndani ukaona wenzako wanavyoishi huko,choo bado ni passport size,mifereji ya kupitisha maji taka hakuna,mvua ikinyesha vyoo vinatapishwa,unaambiwa utakuta watoto wanaogelea juu ya vinyesi vya binadamu maana ya hapo nenda sasa Amani hosp utakutana na watoto kibao wanapoteza maisha kwa kipundupindu, Tena maeneo kama hayo ukipita usithubutu kifungua kifurushi kilichofungwa cheusi cheusi hivi,wewe yaani kwa jina lingine vinaitwa vibomu huko uswahilini,basi utakutana na kinyesi nyumba zima wamejiachia humo,hii inatokea pale choo kimejaa na hakuna mvua kwa muda kuwezeka kukifungua choo kiondoke mtaani.
Yaani unaweza kusema kipindupindu ni ugonjwa wa maskini,maana idadi kubwa ya wagonjwa ni hao ni wakipato cha chini mno,
Vipi kuhusu Uchafu barabarani na barabara mbovu sizizo na mpangilio hapa town,yaani ni balaa tupu,mimi niliwahi kukaa pale Upanga toka nizaliwe hadi leo,unaambiwa hata siku moja sijaona wakiweka barabara ya rami,kipindi cha kiangazi ni vumbi hadi chumbani,kipindi cha mvua ni kukanyaga maji ya mvua nje yaliyochanganyika na maji taka yaliyoziba kwa sababu ya uchakavu wake ,maana nahisi toka wahindi waijenge enzi hizo hadi leo haijaweza kurekebishwa na watu ndo ivyo wanazidi kuongezeka,Sasa hapo Serikali za mitaa zinafanya nini au ziko kwa ajili ya nini.
Achana na hilo,hadi leo tumekosa kabisa wazoa taka wa kuweza kusema taka zinazolewa hakuna,magari ni mabovu yaani sio Gari la takataka ni Gari taka.na wale wanaozoa wenyewe hawana groves,mabuti wala mask za kuzuia harufu ya uchafu,na utakuta wanakaa juu ya uchafu.
Elimu yetu je ikoje,leo hii ukitaka kuomba kazi lazima waandike uwe unajua kiingereza safi cha kuandiaka na kuongea,mimi kajamba nani vyeti ninavyo lakini School bus huko sekondari na primary sijapanda(yaani sijasoma shule ya kizungu)hivyo kiingereza changu si salama sana. Na watu kama mimi hapa bongo tuko wengi kuliko hao waliopanda School bus,sasa hapo hauoni wametutenga?.
Mimi nasema viongozi wetu wanabahati sana,wanatoa ahadi na hawatekelezi vilevile lakini wananchi wao tumetulia tuli kama maji mtungini tukiomba ipo siku tutakuwa kama angalau mazingira kama Ulaya(Lol)
Umewahi kutembelea mbuga za wanyama kama mkiwa group hivi mmetoka Dar mnakwenda huko,labda vyumba mlivyofikia jirani na vyumba vya wazungu watalii,basi mkiongea na kucheka kwa nguvu,wahudumu wanawafuata,nyie mbona mnapiga makelele kuna wageni watawashangaa.mnyamaze au tutawahamisha,lakini huko mnawasikia hao wageni wazungu wakiongea na kupiga makelele kweli,wangine wanaimba na kucheza hadi usiku kweli,tena nyie mlionyamaza sasa hata usingizi mnakosa kuwasubiri hao wageni hadi nao wachoke walale.Sasa sielewi makelele ya wazungu watalii ni mazuri kuliko makelele ya Wa Tz watalii.
Kuna vitu vingi sana vinaumiza Bongo,kama Rushwa,Kodi kubwa zinazomuumiza mTanzania,Mikataba inayonufaisha wachache n.k
Wadau mimi nafikiri hii Blog inasomwa hata na Serikali yetu sasa tunaweza labda kuwapa maoni wafanye nini ili na sisi tuwe na unafuu hapa Nchini kwetu.
Mdau Dar es Salaam
Tatizo la Maji Dar!

Wale wataalam wa maji waliosomeshwa na Chuo cha Maji nk. wako wapi? Kuna nini hasa kinachofanya maji yaye ya shida hivyo wakati tumebarikiwa ma maziwa makubwa kama Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa na mito kibao!
Nakumbuka enzi zile sisi tuliokuwa tunaishi Chuo Kikuu cha DSM tulikuwa tunachekwa kwa sababu ya matatizo ya maji. Walikuwa wanashindwa kuyapandisha mlimani eti.
Serikali infanya nini kutatua matatizo ya maji? Wasipofanya kitu tutasikia watu wanaugua kipindupindu na magonjwa mengine ya kuharisha.
*****************************************************
Kutoka ippmedia.com
Dar vendors pray for prolonged water scarcity
2008-12-18
By Correspondent Gadiosa Lamtey
An acute water shortage that had hit Dar es Salaam and its outskirts for the past ten days, had turned into a blessing in disguise for others.
Vendors selling the precious liquid have been making lucrative business, praying for the scarcity to continue a little bit longer.
A vendor, Hamisi Majaliwa, said God had listened to their prayers as they could now afford to celebrate the year end festivals.
``The scarcity guarantees my daily bread. I no longer worry about celebrating Christmas because I have earned quite a sum over the past few days,`` said Majaliwa.
A survey conducted by The Guardian across the country`s commercial hub found out that the scarcity was getting worse, with a 20-litre gallon of tap water selling at between 800/- and 1,000/- respectively.
The high prices have forced some low income earners in the city to resort to drawing water from the drainage system, thus inviting grave health risks.
Margaret Richard, a resident of Ubungo suburb, said she resorted to buying bottled water as it was safe to cook and brush her teeth with.
``I am skeptical with the water sold by street vendors,? said Margaret.
She said the scarcity had made vendors fetch water from any place for the sake of money, while ignoring all the health risks.
``Worse still, their prices are unfair,`` she said. Margaret, however, wondered how the unemployed and housewives afford buying water from street vendors.
``I can`t blame vendors because survival is for the fittest. Everyone must earn their bread. However, I call upon Dawasco to speed up their efforts to restore water supply.
Dar es Salaam is densely populated. No one will survive should it happen that there is a cholera outbreak,`` said Margaret.
Alfa Laizer of Kinondoni said some people had already suffered after consuming salty water drawn from shallow wells.
Laizer said: ``Salty water is only good for washing clothes and house cleaning, but you can`t use it to cook or drink. Some people are already becoming allergic from bathing salty water.``
``We are not comfortable with what is going on, although we are aware what the problem is.
The authorities should find a solution before the situation gets worse, especially for children,`` he said.
A resident of Chang`ombe, Fatuma Kamugisha, said water had become as precious as gold but the digging of boreholes had in a way helped to avert the problem.
When contacted for comments, Dawasco public relations officer Mary Lyimo said their engineers were busy working on a defective transformer.
``Since last Saturday, our engineers have been tirelessly working on the transformer and by tomorrow (yesterday) things will be back to normal,`` she confidently said.
Last week, Dawasco announced that the city would temporarily go without water because of a defective transformer that supplies power to water pumps at Lower Ruvu.
As we went to press, Dawasco public relations officer Mary Lyimo said water supply had been restored in several Dar es Salaam suburbs, except Magomeni, Sinza, Mwenge and Ilala.
She said problems affecting such areas would be sorted out within the shortest possible time
``It will not take long to normalize the city supply. The delay has been caused by low pressure from our pumping machines,`` she said.
SOURCE: Guardian
Tuesday, March 25, 2008
DAWASCO kuwa na viosk Dar
****************************************************************
Dawasco to introduce 300 water selling kiosks
2008-03-21
By Our Correspondent
The Dar es Salaam Water and Sewerage Corporation (Dawasco) has announced new plans to use trucks to distribute water at designated selling points in Dar es Salaam. The water utility firm says it will introduce kiosks and start physical distribution of water, apart from installing water pipes.
Dawasco Public Relations Manager Badra Masoud told The Guardian that water kiosks would be placed in areas that face acute water crisis, adding that the services would be offered at affordable price. According to the official, a 10-litre container will be selling at 20/- and a 20-litre one at 30/-.
``The facility will be managed by DAWASCO employees. A respected and trustworthy member of the community will be picked to manage these kiosks,`` said Masoud. On the monitoring of sales, she said the company would directly deal with the appointed sales persons who would be required to submit collected money against meter records.
Masoud said collections from the respective water points would be divided equitably - part of the money would go to the maintenance of the facility and the other for paying the salary of the manager. According to the official, Dawasco has drawn up a two-year plan to put up 300 water-kiosks in Dar es Salaam. She added that all problematic areas would be covered satisfactorily.
Meanwhile, DAWASCO has dismissed as baseless claims that its workers have polluted the water source at Ruvu, saying the security level at the location was too high for that to be done.
``Those were mere rumours. No one is allowed to stay close to the source. Even those who are going for a study tour must be scrutinised thoroughly before they are allowed in. How come that a stranger could find his way in? asked Masoud.
As part of Water Week celebrations, a number of Dar es Salaam residents turned up at Mnazi Mmoja grounds to clear their outstanding debt balances, according to the official.
SOURCE: Guardian
Thursday, March 13, 2008
Kipanya na Maji
Monday, March 10, 2008
Madawa yakutwa kwenye Maji ya Kunywa Marekani

Officials in Philadelphia say testing there discovered 56 pharmaceuticals or byproducts in treated drinking water.
To be sure, the concentrations of these pharmaceuticals are tiny, measured in quantities of parts per billion or trillion, far below the levels of a medical dose. Also, utilities insist their water is safe.
But the presence of so many prescription drugs -- and over-the-counter medicines like acetaminophen and ibuprofen -- in so much of our drinking water is heightening worries among scientists of long-term consequences to human health.
In the course of a five-month inquiry, the AP discovered that drugs have been detected in the drinking water supplies of 24 major metropolitan areas -- from Southern California to Northern New Jersey, from Detroit, Michigan, to Louisville, Kentucky.
Tuesday, March 04, 2008
Mji wa Dar es Salaam kukosa Maji siku Tano!

TANGAZO.
Dar kukosa maji siku tano
Kutoka Food for Thought Blog
JIJI la Dar es Salaam, litakumbwa na uhaba wa maji kwa muda wa siku tano kuanzia leo.Taarifa ya kukosekana huko kwa maji imetolewa jana kwa vyombo vya habari na Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam na Pwani (DAWASCO) kwa niaba ya Shirika la Majisafi na Majitaka (DAWASA).
Hata hivyo, ukosekanaji wa maji hayo ambao unatokana na kufanyiwa ukarabati mkubwa wa mtambo wa Ruvu Juu utayakumba baadhi ya maeneo ya jiji.Kwa mujibu wa Dawasco, ukarabati huo mkubwa wa mtambo umearifiwa kufanywa na Shirika la Majisafi na Majitaka (Dawasa).
“Dawasa inawataarifu wakazi wa jiji kwamba mtambo wa kuzalisha maji wa Ruvu Juu utafanyiwa ukarabati mkubwa kwa siku tano mfululizo kuanzia Jumatatu Machi 3 hadi Ijumaa Machi 7, 2008 hivyo kusababisha kutopatikana kabisa kwa maji baadhi ya maeneo ya jiji,’ ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa maeneo yaliyotajwa kukumbwa na ukosefu huo wa maji ni ambayo yanapata maji kutoka Ruvu juu.
Maeneo hayo ni Kibaha, mkoani Pwani, Kibamba, Mbezi, Kimara, Changanyikeni, Ubungo, Kibangu, Makuburi, Tabata na Kisukuru. Dawasa imewaomba radhi wateja wake kwa usumbusu utakaotokea wakati wa ukarabati huo.
Friday, December 07, 2007
Vigogo wakatiwa maji

Jana, DAWASCO, ilikata huduma ya maji kwenye nyumba za baadhi ya mawaziri na manaibu wao kwa vile walikuwa na bili za muda mrefu ambazo hazijalipwa. Nawapongeza kwa hatua hiyo. Natumaini hizo bili zitalipwa sasa. Serikali watunge sheria kuwachukulia hatua kali watu wanaozuia wasoma mita kufanya kazi yao. Kama hutaki mtu asome mita basi usiwe na huduma ya maji!
Tatizo siyo hao vigogo tu, kuna tatizo kubwa zaidi. Maji mengi yanapotea kutoka 'source' (chanzo) mpaka yanafika kwa mteja. Watu wametoboa mabomba makusudi kuiba maji. Mabomba mengine yanavuja. Je, DAWASCO inajua kila sehemu mambomba yametobolewa?Hakuna usimamizi mzuri wa kukagua watu wanaojenga juu ya mabomba makubwa. Mtu anachimba choo na kinatoboa bomba la maji, hajali, uko uchafu unaingia kwenye 'maji safi'!
Lazima serikali iingilie swala ya maji. Swala huu inazidi kuwa sugu miaka inavyozidi kwenda.
Enzi za Ujamaa, Mwalimu aliahidi kila mTanzania atakuwa na maji safi karibu. Bado kabisa!
Mawaziri wakatiwa maji
Shirika la Maji safi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASCO), jana lilifanya kweli kwa kuwakatia maji baadhi ya Mawaziri na Naibu wao kadhaa wanaoishi maeneo ya Masaki na Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam kutokana na malimbikizo makubwa ya bili zao. hatua hiyo ilikuja baada ya mwanzoni mwa wiki, DAWASCO kueleza bayana azma yake ya kuwakatia maji vigogo hao kwa maelezo kuwa madeni yao ni ya muda mrefu.