Saturday, June 11, 2016

Kongamano Kubwa Lililotarajiwa Kufanyika Mjini Mwanza Laahirishwa

Lile Kongamano Kubwa la Wajasiriamali lililotarajiwa kufanyika hii leo June 11,2016 katika Uwanja mkongwe wa Nyamagana Jijini Mwanza, limeahirishwa hadi Julai 16,2016.
Kongamano hilo limeahirishwa kutokana na baadhi ya washiriki kuwa katika mfungo wa Mwezi Mtukufu na hivyo kuona si busara kufanyika.

Kongamano hilo linatarajiwa kuwa la Kihistoria kuwahi kufanyika mkoani Mwanza kwa kuwakutanisha Vijana Wajasirimali pamoja na Wawekezaji mkoani Mwanza wapatao 500. 

BMG inakutakia maandalizi mema kwa ajili ya kushiriki katika Kongamano hilo ambalo halitakuwa na kiingilio ambapo Kauli Mbiu yake inasema "Vijana Ndiyo Mhimiri wa Upaishaji wa Pato la Taifa, Usisubiri Kesho Fursa ni Sasa".

Pichani ni Kamati ya Maandalizi ya Kongamano Kubwa la Wajasiriamali linalofanyika hii leo June 11,2016 katika Uwanja mkongwe wa Nyamagana Jijini Mwanza, ilipokutana na Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa (wa pili kushoto), wakati ikiwa ni katika maandalizi ya kuelekea katika Kongamano hilo.

No comments: