Saturday, June 11, 2016

Tukumbuke Askari Wetu Waliopigana kwa Niaba ya Mkoloni



Askari Monument in Dar es Salaam, Tanzania
 Leo nimekumbuka ule wimbo tuliokuwa tunaimba jeshini, JKT, inaenda hivi..... Askari Eh, Vitani yee mama......   

Wadau, mnajua ile sanamu pale City Center Dar. Inaitwa Askari Monument.  Ni kumbukumbu ya Askari waafrika waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.  Waafrika walichukuliwa na Mkoloni kuwa Askari katika Majeshi yao, Walifanya kazi ngumu ya kupigana huko wazungu walikaa kwenye viti vyao wanapunga hewa!  Kwa maana hiyo Akari wa nchi fulani, walikuwa wanaua Askari wa nchi nyingine, Kama mchezo vile!  (Gameborad) Askari wengine walipelekwa Ulaya na hawakurudi kwa familia zao, wala familia zao hawajui waliishia wapi!

Nimekusanya picha ya Askari waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, wakati huo Tanzania, inaiitwa Deustche Oost Afrika (German East Africa).

Na Mjerumani alikuwa ni msehenzi mkatiki kwa Waafrika..  Waafrika huko vijijini waliuawa wengi sana na Mjerumani eti wazaa au wagonjwa.

Kwa habari zaidi za Vita Kuu ya Kwanza na Dunia na Tanzania (German East Africa) BOFYA HAPA:

Askari Akiaaga Familia Yake kabla ya kwenda Vitani

Askari kwenye Gwaride Dar es Salaam

Askari kwenye Mafunzo 1918










Askari Monument Mwaka 1945

No comments: