Showing posts with label Barrick Gold Mine. Show all posts
Showing posts with label Barrick Gold Mine. Show all posts

Thursday, May 10, 2012

Bilionea wa Barrick anapoitumia Tanzania Kujitakasa!

Asante Kaka Johnson kwa kuandika habari hizi.  Nimesoma na roho imeniuma kweli. Yaani ni yale mambo aliyokuwa anasema Mwalimu Nyerere. Tunanyonywa na makupe. Unaedelea! Lini tutakata mirija yao na rasilimali zetu zifaidi wananchi wa Tanzania.

************************************************************

Bilionea wa Barrick anapoitumia Tanzania kujitakasa...!


Na Johnson Mbwambo

Toleo la 238

9 May 2012

WIKI iliyopita Rais Jakaya Kikwete alilifanyia mabadiliko kidogo baraza lake la mawaziri. Wasomaji wangu wengi walinitumia ujumbe wa e-mailna sms wakinishauri, safari hii, niandike kuhusu mabadiliko hayo ya Kikwete, na kueleza iwapo yataleta unafuu wowote kwa Watanzania.

Jibu langu kwao ni kwamba hakuna kipya cha kuandika ambacho hakijaandikwa, hakuna kipya cha kumshauri Rais Kikwete ambacho hajashauriwa na wabunge, wasomi, wachumi na wachambuzi wa masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii wa hapa nchini.

Binafsi, niandike kumwambia nini kipya Rais Kikwete? Kwamba baraza lake ni kubwa mno sawa na timu tano za soka, na kwamba linateketeza bure tu fedha za walipakodi?

Niandike kumwambia kwamba hapakuwa na haja yoyote kuwa na manaibu mawaziri katika baadhi ya wizara kama vile Wizara Habari, Vijana na Michezo?

Niandike kumwambia kuwa naibu waziri katika wizara kama hiyo hana kazi nyingi za kila siku, na kwamba muda mwingi ataishia kusoma tu magazeti ofisini na kusubiri mialiko ya kuzindua albamu za bongo fleva au kuhudhuria mashindano ya walibwende?

Niandike nini kipya kuhusu mabadiliko hayo madogo ya baraza la mawaziri la Rais Kikwete? Kwamba hawa wapya aliowateua ndo watamaliza ufisadi uliokithiri katika serikali yake? Kwamba impunityimefikia mwisho kwa sababu ya hawa mawaziri wapya aliowateua?

Hapana ndugu zangu. Sina jipya la kumwambia Rais Kikwete. Nilishasema katika safu hii, toleo Na. 237, kwamba “ya Kikwete tumeshayaona, tusibiri ya rais ajaye”.

Niliandika hivyo nikimaanisha kwamba katika miaka mitatu na ushee aliyobakisha Ikulu, hakuna jipya kubwa la kimaendeleo tunaloweza kutarajia kutoka katika serikali yake. Na bado naendelea kuamini hivyo.

Kwa hiyo, ndugu zangu, sitaandika kuhusu mabadiliko hayo ya baraza la mawaziri; bali ninaandika kuhusu tukio jingine linalotuhusu la wiki iliyopita lililotokea huko Toronto, Canada.

Nazungumzia tukio la mkutano mkuu wa mwaka wa wanahisa wa kampuni inayoongoza duniani kwa uchimbaji dhahabu – Barrick. Kampuni hii ndio ambayo pia imetwaa karibu migodi yetu yote mikubwa ya dhahabu nchini.

Mkutano huo uliofanyika Jumatano ya wiki iliyopita ulikuwa wa aina yake kwa sababu, nje ya ukumbi wa mkutano, kulikuwa na mamia ya wanaharakati kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaopinga uwekezaji wa kinyonyaji na usio wa kibinadamu wa Barrick.

Mkusanyiko huo mkubwa ulioratibiwa na Occupy Toronto Movement, nje ya ukumbi wa mkutano, ulikuwa na wanaharakati wenye hasira juu ya uwekezaji huo wa kinyonyaji na usio wa kibinadamu wa Barrick sehemu mbalimbali duniani.

Ni kutokana na hali hiyo ilikuwa ni vigumu wanahisa ndani ya mkutano huo kutolijadili suala la kuendelea kuchukiwa kwa Barrick sehemu nyingi duniani inakomiliki migodi ya dhahabu. Baadhi ya wanahisa (akiwemo wa Chile) walichachamaa kweli kweli mkutanoni na kuitaka Barrick ijirekebishe.

Lakini kulikuwa na mtu mmoja ambaye hakuamiani kirahisi kile kilichokuwa kikitokea nje ya ukumbi huo wa mkutano, na huyo si mwingine bali ni mmiliki na mwanzilishi wa kampuni hilo kubwa la dhahabu duniani, Peter Munk (84).

Peter Munk alikuwa akitetemeka kwa hasira, dhahiri akishindwa kuamini kuwa kampuni yake ilikuwa inachukiwa kiasi hicho; licha ya misaada mingi ya ‘huruma’ ambayo imetoa katika nchi ilikowekeza.

Kwa mujibu wa gazeti la Toronto Metro la Canada, Munk alilazimika kutoka na gari lake kupitia mlango wa nyuma ili kuwakwepa wanaharakati hao, lakini alipoona wingi wao kwa mbali, alimlazimisha dereva wake aendeshe hadi kwa wanaharakati hao ili “awapashe” kuhusu ‘huruma’ ya Barrick kwenye nchi zao.

Kwa sababu ya kuhofia usalama wake, dereva alimkatalia na kumpeleka moja kwa moja nyumbani kwake. Hata hivyo, alipofika nyumbani kitu cha kwanza alichokifanya bilionea huyo ni kupiga simu ofisi kwake na kuelekeza atayarishiwe haraka orodha ya misaada ya kijamii ambayo Barrick imetoa katika nchi ambako ina migodi.

Kesho yake mkutanoni, Bilionea Munk aliisoma orodha hiyo kujaribu kuwashawishi wanahisa waamini kuwa Barrick ni kampuni yenye ‘huruma’ kweli kweli.

Miongoni mwa nchi masikini duniani ambazo bilionea Munk alizitaja kuwa Barrick inatoa ‘misaada ya hiari ya huruma’ ni Tanzania, Papua New Guinea, Peru na Chile.

“Ningependa nitoke nje nipambane na waandamanaji hawa na kuwaambia ukweli,” alifoka Munk mkutanoni na kuongeza:“Sizungumzii tu kodi tunazolipa katika nchi hizo, sizungumzii tu ajira tulizotengeneza; bali nazungumzia ukweli kuwa kama si sisi, basi, ajira na fursa kwenye maeneo hayo zingekuwa ziro”.

Sidiriki, kwenye safu hii, kuzizungumzia Chile, Papua New Guinea au Peru, lakini kwa hapa kwetu Tanzania, nina hakika kilichosemwa na Munk si ukweli wote kuhusu uwekezaji wa Barrick.

Hiyo inayoitwa na Bilionea Munk kuwa ni ‘misaada ya hiari’ inayothibitisha ‘huruma’ ya Barrick, si chochote wala lolote ikilinganishwa na mapesa wanayoyapata kutoka katika mauzo ya dhahabu za migodi yetu.

‘Misaada ya hisani’ anayoizungumzia Bilionea Munk, ni kama ule wa dola 350,000 zilizotolewa na Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania kwa ajili ya ukarabati wa Sungusungu Hospital kule North Mara. Hapa tunazungumzia ukarabati tu, na si ujenzi wa hospitali.

Hivi kweli ukarabati wa hospitali na zahanati na ujenzi wa madarasa na uchimbaji visima hapa na pale, ndio stahili yetu kwa mamilioni ya dola ambayo Barrick hujipatia kila mwaka kutoka katika dhahabu ya nchi masikini kama yetu?

Katika mkutano huo mkuu wa Barrick huko Toronto, Canada, Bilionea Munk alitamba kuwa mapato ya Barrick kote dunia yaliongezeka kwa asilimia 18 hadi kufikia dola bilioni 3.6.

Lakini hapo hapo ripoti ya African Barrick Gold (ABG) inaonyesha kuwa bajeti iliyopangwa kwa Tanzania kwa ajili ya hiyo inayoitwa ‘misaada ya huruma ya hiari’, ni dola milioni 10 tu! Hivi dola bilioni 3.63 na ‘msaada wa hiari’ wa dola milioni 10 ni wapi kwa wapi?

Hata kama katika nchi zote 10 ambako Barrick ina migodi mikubwa ingetenga dola milioni 50 tu, bado kisingekuwa kiwango cha kuridhisha kiasi cha Munk kukitumia kutamba mkutanoni.

Vyovyote vile; ukweli unabakia uleule, nao ni kwamba Barrick itaendelea kuchukiwa katika nchi masikini kama Tanzania kwa sababu uwekezaji wake umeendelea kuwa wa kinyonyaji na usio na ubinadamu.

Na ninapozungumzia uwekezaji usio wa kibinadamu, nawakumbuka Mama Otaigo wa kijiji cha Weigita na kijana Paul wa kijiji cha Nkerege (nikitaja wachache) kule North Mara ambao miili yao imeharibika vibaya kwa sababu ya kutumia maji ya Mto Tigithe yaliyokuwa na sumu inayotoka kwenye mgodi wa Barrick. Mpaka leo waathirika hao wa unyama huo wa mwaka 2009 hawajalipwa fidia na kampuni hiyo tunayoambiwa na mwasisi wake kuwa ni yenye ‘huruma’ nyingi.

Lakini pia ninapozungumzia uwekezaji huo wa Barrick usio wa kibinadamu, nawakumbuka wale wakazi wa Geita ambao sasa wanaishi kwenye mahema katika kambi iliyopachikwa jina la Dafurbaada ya kuwa wametimuliwa kwenye makazi yao ya asili kumpisha mwekezaji mwenye “huruma” ya kupindukia – Barrick. Katika hili rejea makala ya Raia Mwema ya toleo Na.237 yenye kichwa cha habari: Utajiri wa dhahabu wageuka laana Geita.

Ndugu zangu, Bilionea Munk anaweza kuwa amefanikiwa kuwaghilibu wanahisa wenzake kwenye mkutano huo wa Toronto, Canada, kwamba eti Barrick ni kampuni yenye “huuma” , na kwamba imetoa misaada mingi ya kijamii katika nchi ambako ina migodi; lakini ukweli unabakia pale pale, nao ni kwamba Barrick ni kampuni ya kishetani.

Na nijuavyo, kama CCM hakitaondolewa madarakani kwenye uchaguzi wa 2015, Tanzania tutaendelea kunyonywa na Barrick hadi dhahabu katika migodi hiyo zitakapoisha kabisa na wao kuondoka na kutuachia mashimo matupu! Si inasemwa wajinga ndio waliwao?

Tafakari.

Chanzo: Gazeti la RaiaMwema

Saturday, February 04, 2012

Saturday, December 10, 2011

Barrick Gold Mines Wakwepa Kulipa Kodi!


IMEBAINIKA kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama imepoteza mapato zaidi ya sh milioni 300 kutokana na kampuni 30 zinazofanya kazi migodi ya Kampuni ya African Barrick Gold Mines LTD kukwepa kulipa
ushuru wa huduma za jamii.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Biashara wa Wilaya ya Kahama, Boniphace Bulali, alipokuwa akitoa
ufafanuzi juu ya msako mkali wa kuzisaka kampuni hizo katika migodi hiyo unaofanywa
na wakala wa kukusanya madeni ya halmashauri hiyo, Mustered Seed International LTD.

Bulali alisema kampuni hizo zimekwepa kulipa ushuru unaopaswa kulipwa wa huduma za jamii kwa kipindi cha miaka mitatu, hali ambayo imezorotesha mapato ya halmashauri na kushindwa kufikia baadhi ya malengo yake katika kuleta maendeleo stahiki kwa wakati wilayani humo.

Alisema katika msako huo tayari baadhi ya kampuni zimekiri kushindwa kulipa fedha hizo kwa madai
jukumu hilo hufanywa na makao makuu ya ofisi zao zilizopo Dar es Salaam kinyume cha utaratibu
wa sheria ndogo za halmashauri zinazoeleza kulipa ushuru huo kwenye eneo wanalofanyia kazi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mustered Seed International LTD ambayo ni wakala wa kukusanya madeni hayo, Zacharia Soko, alisema kuna kampuni 15 zinazofanya kazi katika mgodi wa
Buzwagi pekee ambazo hazijapata kulipa ushuru huo kwenye halmashauri hiyo tangu zianze
kuwajibika katika mgodi huo.

Soko alisema pia kuna kampuni 15 katika Mgodi wa Bulyanhulu ulio kilometa 74 kutoka Kahama
mjini ambazo nazo zimebainika hazijalipa ushuru huo na tayari katika msako huo baadhi ya mali zake
zikiwamo magari yanashikiliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kahama.

Chanzo: Tanzaniadaima

Wednesday, May 25, 2011

Habari ya Maiti Kutupwa Tarime Sasa Habari ya Kimataifa!


Hii habari imetoka kwenye gazeti la Toronto Star. Makao Makuu ya Barrick iko Toronto. Barrick wanasema hawana habari na maiti kutupwa!!!! Je, Barrick wanawasaidia wananchi wa Tarime? Wamewajengea barabara, zahanati, shule? Wametoa scholarships ili vijana wasome sekondari, Chuo Kikuu? Au kazi kuiba dhahabu yetu? Watu wamepoteza maisha shauri ya vimawe vyenye chembe chembe za dhahabu! Mzungu kwa dhahabu, almasi, Tanzanite! Yaani! Je, Barrick watawasaidia wafiwa, mfano huyo mjane mwenye mimba?
**************************************************************

Kutoka TORONTO STAR:
TARIME, TANZANIA—It was on the side of a dirt road in northern Tanzania that relatives found a coffin containing the body of Emmanuel Magige on Tuesday morning.

The 27-year-old man was one of seven people killed and more than 12 injured on May 16 when villagers at African Barrick’s mine in northern Tanzania clashed with security forces.

Late Monday night, police stormed a mortuary in the small northern town of Tarime and removed bodies belonging to four of the dead in a bid to prevent a memorial planned at the mine for Tuesday, witnesses said.

After finding the bodies of the victims forcibly returned to their villages, families instead held small burial services at their homes in the afternoon.

“It was inhuman. They did this like animals,” said Magige’s 20-year-old wife, Mary.

African Barrick is a subsidiary of Barrick Gold Corp., which is headquartered in Toronto.

African Barrick said on Tuesday that it had no knowledge of the incident.

Barrick, which employs its own security guards as well as government police in order to guard the gold mine, has said that in the May 16 incident more than 800 “intruders” invaded the mine, where locals often come to scavenge for rocks containing gold.

Relatives of the deceased had wanted to hold a memorial service Tuesday at the mine, but say they were informed by police Monday that they would not be allowed to go ahead with the ceremony.

Families of the deceased and their supporters went to the mortuary in Tarime to guard the bodies of their loved ones because they had received information that police might try to steal the bodies.

Six trucks filled with police arrived at the mortuary at 10 p.m., according to relatives who were on the scene.

“The security officers came and asked us what we were doing there,” said Gasaya Matiku, whose 19-year-old nephew, Chacha Ngoka Chacha, was killed at the mine. “They surrounded people and started beating them. Then they took the bodies and put them on a truck.”

Witnesses said eight people were arrested by police and beaten with sticks and the butts of guns before they were taken away.

The arrested include an opposition member of the Tanzanian Parliament, a lawyer from an environmental non-government organization and a relative of one of the dead.

They were charged with criminal trespassing, unlawful assembly and obstructing a medical practitioner in the execution of duty.

Police said the accused had interfered with families’ plans to bury the victims’ bodies.

“They were just people from the opposition party who had nothing to do, so they decided to play a joke for their own benefit, trying to convince the families not to take the bodies and bury them,” said the regional police commander, Paul Ntobi.

Families of the deceased said they were angry at the treatment of their loved ones’ bodies.

“In our culture, this is a taboo. To do such a thing means that those who did it to you despised you,” said Magige Gati, Emmanuel’s father.

“I’m furious. If I could manage to get a gun, I would fight the government personally. The same police force that killed my son stole his body and dumped it.”

The government’s handling of the episode has been beyond callous, according to the families.

Gati said that when he visited the district commissioner to seek help, the official instead told him: “It was very unfortunate that they managed to kill only a few. The law is different in Tarime than in the rest of Tanzania. ”

Mary, the wife of Emmanuel Magige, said her husband got most of the family‘s income from digging for gold-laced stones at the mine.

Eight months’ pregnant with the couple’s first child, now that her husband has been killed, she doesn‘t know how she will survive.

“I will struggle,” she said.

Mauji Tarime - Maiti Zadhalilishwa!

Yaani sikutegemea kusikia habari za ajabu kama hizi kutoka Tanzania. Kwanza watu wameuawa, pili bado tunaibiwa urithi wetu na mzungu! Sasa maiti wanadhalilishwa! Yaani tunakwenda wapi jamani?

Habari Kutoka WAVUTI.Com

Umekuwepo mkanganyiko mkubwa baina ya wafiwa, Serikali na wanaharakati, kufuatia mauaji ya watu kadhaa waliouawa na Askari Polisi kwa kupigwa risasi wakituhumiwa kutaka kupora Mgodi wa dhahabu wa African Barrick North uliopo katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, Tanzania.

Mkanganyiko huo wa ama maiti wazikwe au la ili kupisha uchunguzi, umesababisha mtafaruku ambao umewaacha maiti hao wakiwa wametelekezwa mitaani, vile vile, baadhi ya wanaharakati na viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, wamekamatwa kuhusiana na tukio hili.

Washitakiwa walikana kosa na kurejeshwa rumande kwa 'sababu za kiusalama' kufuatia ombi la Mwendesha mashtaka alkiiomba mahakama kutokutoa dhamana kwa watuhumiwa kwa madai kuwa dhamana hiyo ingeweza kuhatarisha amani na kuchochea ndugu wa marehemu kutoendelea na taratibu za mazishi.

Polisi pia iliwashikilia kwa muda na kuwahoji Mbunge Ester Matiku (Viti Maalumu-CHADEMA), John Heche na waandishi wa habari wanne Mabere Makubi (Channel TEN), Anthony Mayunga (Mwananchi), Berdina Nyakeke (The Citizen) na Anna Mroso (Nipashe) kuhusiana na tuhuma hizo za uchochezi.

Polisi yatoa sababu ya kuchukua maiti

Imearifiwa kuwa miili ya marehemu iliwekwa katika majeneza bila kuvikwa nguo zozote wala sanda na kupelekwa nyumbani kwa wahusika lakini wanakijiji walikataa kupokea maiti hao wakitaka polisi kuirejesha miili hiyo hospitalini ili ichukuliwe upya na kuzikwa kwa heshima na mila za Wakurya. Ndipo ilipotelekezwa barabarani, “Mimi nimefiwa na mtoto wangu Emmanuel Magige, jana tuliambiwa asubuhi ndio tutachukua miili ya watu wetu tukazike sasa tumeamka tunaambiwa eti polisi walichukua marehemu wamekwenda kuwatupa porini na sisi tuko hapa Tarime...” - mzee Magige Ghati, baba wa mmoja wa marehemu.

Baada ya waandishi wa habari kusikia taarifa hiyo, walikwenda ili kushuhudia na ndipo walipokamatwa.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Tarime/Rorya, Costantine Massawe, alisema kuwa walichukua miili ya maiti baada ya wafiwa kuwaomba msaada wa kuwapelekea miili hiyo katika vijiji vyao.

Alisema, baada ya baadhi ya wafiwa kuchukua miili hiyo juzi na kuisafirisha kwao, wafuasi wa CHADEMA waliwafuata hadi Nyakunguru na walipofika huko, waliishawishi familia ya Magige kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka Polisi kwa nia ya wanahabari waliofuatana nao kuupiga picha ili kuonesha taswira kuwa Polisi imetelekeza miili hiyo ili kupotosha jamii na kujenga chuki kwa Jeshi hilo na wananchi wa Tarime

source: WAVUTI.COM

Tuesday, May 24, 2011

Mauaji Tarime: Tamko la Barrick Gold Mine

Nadhani kuna watu ambao watakubaliana na mimi! Mwalimu angekuwa hai angeshafukuzulia mbali hao wazungu! (Persona Non-Grata) Wanaiba urithi wetu halafu wanatuua! Wamezidi! Wezi wakubwa halafu wauaji! Hivi waTanzania tunapata nini kutoka kuwepo kwao pale?

Hii TAMKO/STATEMENT inatoka kwenye website yao. Ukitaka kwenda huko BOFYA HAPA:

Recent Police Action at North Mara

May 19, 2011 — The recent violent confrontation and loss of life at African Barrick Gold’s (ABG) North Mara mine is deeply concerning to Barrick and ABG. African Barrick Gold is working with the Tanzanian government and police to address this situation.

While ABG is still determining all the facts associated with this complex situation, the following is based on information released by ABG and the Tanzanian Police to date:

On May 16, a large group of intruders, many of them armed with machetes, stones and mining implements, stormed the ore stockpile at North Mara, with the intent of stealing ore. Initial reports put this number at 800, but following further reviews, the number is likely to have been more than 1,500. Given the extremely large number of aggressive intruders and the escalating threat of violence, ABG contacted the Tanzanian police for protection. Faced with over a thousand armed intruders, the mine’s main duty was to ensure the safety of its employees.

The Tanzanian police report that upon arriving at the scene, they tried to contain the situation. Police fired warning shots into the air and used tear gas to try to stop the attackers from advancing; however, the organized mob of armed intruders refused to turn back. A violent confrontation ensued as the intruders engaged in a sustained attack on police. A number of intruders were injured in the confrontation, seven fatally. The police have also reported that a number of their officers were injured in the confrontation.

Situations like this are deeply troubling to Barrick, ABG and to the people who live and work around the mine. The vast majority of people living near North Mara share the same desire for security and safety as we do. Both police and company investigations are now underway into the fatal shootings, which involved Tanzanian police. ABG security was not involved in these fatal incidents and, generally, does not deal with incursions of this magnitude and level of organization.

The North Mara mine operates under particularly challenging and complex circumstances, primarily associated with the law and order environment. The mine is located in a very remote, underdeveloped part of the country in close proximity to the Kenyan border, with limited law enforcement capacity, resulting in break-downs in law and order. Organized crime is also present in the region. The operation regularly faces illegal intruders, who may be armed and aggressive. These actions put hundreds of lives at risk, including ABG employees.

ABG is actively engaging with the Tanzanian government to address the severe law and order issues and lack of police resources around North Mara and in the wider community. ABG continues to make improvements to physical security at the site and engage with local community leaders. Its objective is to engage proactively with the community in long-term solutions to these challenges, to improve relations and resolve legacy issues, and to increase community investment expenditures aimed at improving quality of life in the area.

Barrick and ABG remain committed to the long-term future of North Mara and to the stability and security of the communities surrounding this operation.