Showing posts with label Tarime. Show all posts
Showing posts with label Tarime. Show all posts

Wednesday, May 25, 2011

Habari ya Maiti Kutupwa Tarime Sasa Habari ya Kimataifa!


Hii habari imetoka kwenye gazeti la Toronto Star. Makao Makuu ya Barrick iko Toronto. Barrick wanasema hawana habari na maiti kutupwa!!!! Je, Barrick wanawasaidia wananchi wa Tarime? Wamewajengea barabara, zahanati, shule? Wametoa scholarships ili vijana wasome sekondari, Chuo Kikuu? Au kazi kuiba dhahabu yetu? Watu wamepoteza maisha shauri ya vimawe vyenye chembe chembe za dhahabu! Mzungu kwa dhahabu, almasi, Tanzanite! Yaani! Je, Barrick watawasaidia wafiwa, mfano huyo mjane mwenye mimba?
**************************************************************

Kutoka TORONTO STAR:
TARIME, TANZANIA—It was on the side of a dirt road in northern Tanzania that relatives found a coffin containing the body of Emmanuel Magige on Tuesday morning.

The 27-year-old man was one of seven people killed and more than 12 injured on May 16 when villagers at African Barrick’s mine in northern Tanzania clashed with security forces.

Late Monday night, police stormed a mortuary in the small northern town of Tarime and removed bodies belonging to four of the dead in a bid to prevent a memorial planned at the mine for Tuesday, witnesses said.

After finding the bodies of the victims forcibly returned to their villages, families instead held small burial services at their homes in the afternoon.

“It was inhuman. They did this like animals,” said Magige’s 20-year-old wife, Mary.

African Barrick is a subsidiary of Barrick Gold Corp., which is headquartered in Toronto.

African Barrick said on Tuesday that it had no knowledge of the incident.

Barrick, which employs its own security guards as well as government police in order to guard the gold mine, has said that in the May 16 incident more than 800 “intruders” invaded the mine, where locals often come to scavenge for rocks containing gold.

Relatives of the deceased had wanted to hold a memorial service Tuesday at the mine, but say they were informed by police Monday that they would not be allowed to go ahead with the ceremony.

Families of the deceased and their supporters went to the mortuary in Tarime to guard the bodies of their loved ones because they had received information that police might try to steal the bodies.

Six trucks filled with police arrived at the mortuary at 10 p.m., according to relatives who were on the scene.

“The security officers came and asked us what we were doing there,” said Gasaya Matiku, whose 19-year-old nephew, Chacha Ngoka Chacha, was killed at the mine. “They surrounded people and started beating them. Then they took the bodies and put them on a truck.”

Witnesses said eight people were arrested by police and beaten with sticks and the butts of guns before they were taken away.

The arrested include an opposition member of the Tanzanian Parliament, a lawyer from an environmental non-government organization and a relative of one of the dead.

They were charged with criminal trespassing, unlawful assembly and obstructing a medical practitioner in the execution of duty.

Police said the accused had interfered with families’ plans to bury the victims’ bodies.

“They were just people from the opposition party who had nothing to do, so they decided to play a joke for their own benefit, trying to convince the families not to take the bodies and bury them,” said the regional police commander, Paul Ntobi.

Families of the deceased said they were angry at the treatment of their loved ones’ bodies.

“In our culture, this is a taboo. To do such a thing means that those who did it to you despised you,” said Magige Gati, Emmanuel’s father.

“I’m furious. If I could manage to get a gun, I would fight the government personally. The same police force that killed my son stole his body and dumped it.”

The government’s handling of the episode has been beyond callous, according to the families.

Gati said that when he visited the district commissioner to seek help, the official instead told him: “It was very unfortunate that they managed to kill only a few. The law is different in Tarime than in the rest of Tanzania. ”

Mary, the wife of Emmanuel Magige, said her husband got most of the family‘s income from digging for gold-laced stones at the mine.

Eight months’ pregnant with the couple’s first child, now that her husband has been killed, she doesn‘t know how she will survive.

“I will struggle,” she said.

Mauji Tarime - Maiti Zadhalilishwa!

Yaani sikutegemea kusikia habari za ajabu kama hizi kutoka Tanzania. Kwanza watu wameuawa, pili bado tunaibiwa urithi wetu na mzungu! Sasa maiti wanadhalilishwa! Yaani tunakwenda wapi jamani?

Habari Kutoka WAVUTI.Com

Umekuwepo mkanganyiko mkubwa baina ya wafiwa, Serikali na wanaharakati, kufuatia mauaji ya watu kadhaa waliouawa na Askari Polisi kwa kupigwa risasi wakituhumiwa kutaka kupora Mgodi wa dhahabu wa African Barrick North uliopo katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, Tanzania.

Mkanganyiko huo wa ama maiti wazikwe au la ili kupisha uchunguzi, umesababisha mtafaruku ambao umewaacha maiti hao wakiwa wametelekezwa mitaani, vile vile, baadhi ya wanaharakati na viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, wamekamatwa kuhusiana na tukio hili.

Washitakiwa walikana kosa na kurejeshwa rumande kwa 'sababu za kiusalama' kufuatia ombi la Mwendesha mashtaka alkiiomba mahakama kutokutoa dhamana kwa watuhumiwa kwa madai kuwa dhamana hiyo ingeweza kuhatarisha amani na kuchochea ndugu wa marehemu kutoendelea na taratibu za mazishi.

Polisi pia iliwashikilia kwa muda na kuwahoji Mbunge Ester Matiku (Viti Maalumu-CHADEMA), John Heche na waandishi wa habari wanne Mabere Makubi (Channel TEN), Anthony Mayunga (Mwananchi), Berdina Nyakeke (The Citizen) na Anna Mroso (Nipashe) kuhusiana na tuhuma hizo za uchochezi.

Polisi yatoa sababu ya kuchukua maiti

Imearifiwa kuwa miili ya marehemu iliwekwa katika majeneza bila kuvikwa nguo zozote wala sanda na kupelekwa nyumbani kwa wahusika lakini wanakijiji walikataa kupokea maiti hao wakitaka polisi kuirejesha miili hiyo hospitalini ili ichukuliwe upya na kuzikwa kwa heshima na mila za Wakurya. Ndipo ilipotelekezwa barabarani, “Mimi nimefiwa na mtoto wangu Emmanuel Magige, jana tuliambiwa asubuhi ndio tutachukua miili ya watu wetu tukazike sasa tumeamka tunaambiwa eti polisi walichukua marehemu wamekwenda kuwatupa porini na sisi tuko hapa Tarime...” - mzee Magige Ghati, baba wa mmoja wa marehemu.

Baada ya waandishi wa habari kusikia taarifa hiyo, walikwenda ili kushuhudia na ndipo walipokamatwa.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Tarime/Rorya, Costantine Massawe, alisema kuwa walichukua miili ya maiti baada ya wafiwa kuwaomba msaada wa kuwapelekea miili hiyo katika vijiji vyao.

Alisema, baada ya baadhi ya wafiwa kuchukua miili hiyo juzi na kuisafirisha kwao, wafuasi wa CHADEMA waliwafuata hadi Nyakunguru na walipofika huko, waliishawishi familia ya Magige kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka Polisi kwa nia ya wanahabari waliofuatana nao kuupiga picha ili kuonesha taswira kuwa Polisi imetelekeza miili hiyo ili kupotosha jamii na kujenga chuki kwa Jeshi hilo na wananchi wa Tarime

source: WAVUTI.COM

Tuesday, May 24, 2011

Mauaji Tarime: Tamko la Barrick Gold Mine

Nadhani kuna watu ambao watakubaliana na mimi! Mwalimu angekuwa hai angeshafukuzulia mbali hao wazungu! (Persona Non-Grata) Wanaiba urithi wetu halafu wanatuua! Wamezidi! Wezi wakubwa halafu wauaji! Hivi waTanzania tunapata nini kutoka kuwepo kwao pale?

Hii TAMKO/STATEMENT inatoka kwenye website yao. Ukitaka kwenda huko BOFYA HAPA:

Recent Police Action at North Mara

May 19, 2011 — The recent violent confrontation and loss of life at African Barrick Gold’s (ABG) North Mara mine is deeply concerning to Barrick and ABG. African Barrick Gold is working with the Tanzanian government and police to address this situation.

While ABG is still determining all the facts associated with this complex situation, the following is based on information released by ABG and the Tanzanian Police to date:

On May 16, a large group of intruders, many of them armed with machetes, stones and mining implements, stormed the ore stockpile at North Mara, with the intent of stealing ore. Initial reports put this number at 800, but following further reviews, the number is likely to have been more than 1,500. Given the extremely large number of aggressive intruders and the escalating threat of violence, ABG contacted the Tanzanian police for protection. Faced with over a thousand armed intruders, the mine’s main duty was to ensure the safety of its employees.

The Tanzanian police report that upon arriving at the scene, they tried to contain the situation. Police fired warning shots into the air and used tear gas to try to stop the attackers from advancing; however, the organized mob of armed intruders refused to turn back. A violent confrontation ensued as the intruders engaged in a sustained attack on police. A number of intruders were injured in the confrontation, seven fatally. The police have also reported that a number of their officers were injured in the confrontation.

Situations like this are deeply troubling to Barrick, ABG and to the people who live and work around the mine. The vast majority of people living near North Mara share the same desire for security and safety as we do. Both police and company investigations are now underway into the fatal shootings, which involved Tanzanian police. ABG security was not involved in these fatal incidents and, generally, does not deal with incursions of this magnitude and level of organization.

The North Mara mine operates under particularly challenging and complex circumstances, primarily associated with the law and order environment. The mine is located in a very remote, underdeveloped part of the country in close proximity to the Kenyan border, with limited law enforcement capacity, resulting in break-downs in law and order. Organized crime is also present in the region. The operation regularly faces illegal intruders, who may be armed and aggressive. These actions put hundreds of lives at risk, including ABG employees.

ABG is actively engaging with the Tanzanian government to address the severe law and order issues and lack of police resources around North Mara and in the wider community. ABG continues to make improvements to physical security at the site and engage with local community leaders. Its objective is to engage proactively with the community in long-term solutions to these challenges, to improve relations and resolve legacy issues, and to increase community investment expenditures aimed at improving quality of life in the area.

Barrick and ABG remain committed to the long-term future of North Mara and to the stability and security of the communities surrounding this operation.

Shairi - Tuacheni Jamani - Mauaji Tarime!

TUACHENI JAMANI!

Tuacheni jamani!
Polisi tuacheni
Serikali tuacheni
Yenu kazi tayari
Iliyobaki ni yetu!

Sisi ndio wafiwa Tarime
Walioporwa uhai wa ndugu
Uhai wa vijana wabichi

Tuacheni sisi
Sisi ndio wafiwa
Kazi yenu tayari
Ile ya kuua
Kazi yetu yaja:
Kulia, kulaani,
kuomboleza na kuzika.

Tuacheni tulie
Hata kulia mwazuia?
Tuacheni tunune
Hata kununa mwazima?
Tuacheni tuzike
Hata kuzika mkwara mwaweka?

Serikali na polisi
Msingeua tusingelia
Msingeua tusingenuna
Msingeua tusingezika
Tuacheni, tuacheni.

Lenu mmemaliza
Kuua mkilinda nyang'au
Mkilinda mporaji
Mnyakuzi wa mali ya Tarime
Mali ya Tanzania
Tuacheni
Kutuchefua acheni.

Mwizi mkubwa mwalinda
Mwenye mali mwaua
Kwa ujira gani mwatenda
Unyama usio mithili
Mijitu yachota utajiri
Kwao yajenga mbingu
Ninyi: Kwenu
Hapa kwenu, miayo yatanda
Zaidiyo mwaua wanenu
Wezi wa nje kulinda. Tuacheni!

Mmemaliza kezi yenu
Kuua, kulinda nyang'au
Sasa amri mwatoa:
Lia hivi, nuna hivi...Ebo!
Na udikiteta una mipaka.

Tuache tunune kwa ngeli yetu
Tuache tujute kwa mazoea yetu
Tuache!

Tuache tulie machozi yetu
Yatiririke mashavuni mwetu
Yaloanishe vifua vyetu
Yaondoe hasira zetu

Tuache tukunje wafu wetu
Tubebe kwa njia zetu
Tusindikize kwa ngeli zetu
Tuzike mashambani kwetu
Tuache!

Acha Tarime wazike
Wazike kwa mila zao
Kwa uzito wa uchungu wao
Kwa kina cha chuki yao
Kwa wingi wa hasira zao.
Tuacheni jamani!

Hata baada ya kuua
Wakilinda wezi
Wanataka tulie roborobo
Tunune nusunusu
Tuchukie roborobo
Tukasirike nusunusu
Tulaani roborobo
Tushutumu nusunusu
Tuzike juujuu
Au nasi tuuawe moja kwa moja.
Tuacheni jamani.

Tarime zikeni.
Tundu Lissu zika
Marando Nyaucho zika
Zikeni vijana wenu
Kwa ngeli yenu
Kwa ngeli ya wakazi
Wanavyotaka
Wanavyojisikia

Tuacheni jamani
Polisi kaa mbali
Serikali jitengeni
Kazi mliyojipa tayari
Ilobaki ni ya walioumia
Waliopoteza
Tuacheni jamani!

Imetungwa na Ndimara Tegambwage

Friday, September 26, 2008

Mchungaji Christopher Mtikila alazwa baada ya kupigwa Mawe Tarime


Nimesikitika sana kusikia kuwa Mchungungaji Christopher Mtikila, kapigwa huko Tarime leo. Sisi waTanzania si tulikuwa tunajivunia ni watu wa amani? Sioni sababu ya mtu yeyote hata awe mwanasiasa kutoka chama gani kupigwa.
*******************************************************************

Kutoka Lukwangule Blog (Beda Msimbe):


Mtikila apigwa mawe Tarime

MCHUNGAJI Christopher Mtikila amelazwa katika Zahanati ya Tarime mjini hapa baada ya kupigwa jiwe la kichwani wakati akihutubia kumnadi mgombea wake.

Kwa mujibu wa maelezo ya daktari anayemtibu Mchungaji Mtikila, Philemon Hungiro, kiongozi huyo ameumizwa vibaya na jiwe hilo kisogoni kiasi cha kushonwa nyuzi tatu.

Mtikila alisema alipigwa jiwe hilo na mtu asiyemfahamu wakati akimnadi mgombea ubunge kupitia chama chake cha DP, Denson Makanya, kwenye Uwanja wa Shule ya Sabasaba mjini Tarime.

Jiwe hilo alipigwa majira ya saa 11 jioni leo wakati akitoa ufafanuzi wa taarifa zake kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe.

Wakati akiishambulia Chadema kuhusika na kupanga mauaji hayo, ndipo mtu huyo alipochoropoka kutoka nyuma na kumpiga jiwe la kisogoni.

Hata hivyo, Mchungaji Mtikila alidai kipigo alichokipata ni matokeo ya ahadi ya Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa, kwamba damu itamwagika na kwamba kiongozi huyo akifika Tarime atapigwa mawe.

Awali akihutubia mamia ya wananchi waliofurika katika uwanja huo wa mkutano, Mchungaji aliwataka wananchi kumchagua mbunge anayemnadi kwani yeye hana ufisadi wala mipango ya mauaji.


*****************************************************

Kutoka ippmedia.com

Tarime ni soo!

2008-09-26 16:35:51
Na Mwandishi Wetu, Tarime

Wakati siku za kuelekea uchaguzi mdogo wa kumsaka mbunge wa Jimbo la Tarime zikizidi kukaribia, hali ya kisiasa mjini hapa imeanza kuwa tete baada ya wafuasi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kuendelea kufanyiana visa mfululizo, vikiwemo vile vya kumwagiana pilipili na kuwatwangana mawe mikutanoni.

Uchaguzi huo mdogo, unatarajiwa kufanyika Oktoba 12, ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Chacha Wangwe, aliyefariki mjini Dodoma Julai 28 mwaka huu baada ya kupata ajali ya gari.

Jana, muendelezo wa visa vya baadhi ya wafuasi wa vyama hivyo vya CCM, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na DP ulifikia pabaya baada ya Mwenyekiti wa UDP, mchungaji Christopher Mtikila kupigwa jiwe la kichwa wakati akiwa kwenye mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya Sabasaba.

Mtikila alijeruhiwa vibaya na kukukimbiziwa hospitali mjini hapa ambako inadaiwa alishonwa nyuzi saba.

Kutokana na vibweka vinavyoendelea katika kampeni za kuelekea siku ya uchaguzi huo, , viongozi mbalimbali wa vyama vilivyosimamisha wagombea wamekuwa wakitoa kauli tofauti kuhusiana na yanayojiri.

Dk. Sengondo Mvungi (NCCR-Mageuzi)
Yeye aliripotiwa kuwa kiongozi wa kwanza kufanyiwa vurugu wakati wa kampeni jimboni humo.

Mvungi alikumbana na kadhia ya kutimuliwa kwa mawe wakati akimnadi mgombea wa chama chake cha NCCR.

Baada ya hapo, Dk. Mvungi ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alilaani tukio hilo na kueleza kuwa ni la hatari, kwani hakuna chama chenye hakimiliki ya jimbo hilo.

Pius Msekwa (CCM)
Makamu huyu Mwenyekiti wa CCM, naye alionja ya joto ya jiwe ya kufanyiwa vituko vya kampeni hizo wakati alipokuwa akimnadi mgombea wa chama chake, Bw. Ryoba Kangoba.

Msekwa alifanyiwa fujo na kuzomewa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa vyama pinzani.

Aidha, wafuasi wawili wa chama chake wameripotiwa kuumizwa baada ya mmoja kupigwa jiwe na mwingine kumwagiwa pilipili.

Kutokana na hali hiyo, bosi huyo namba mbili wa CCM akailalamikia hali hiyo na kuripotiwa akitishia kulifikisha suala hilo kwa Rais Jakaya Kikwete ili hatimaye zifanyike taratibu za kudhibiti hali ya namna hiyo ambayo ni ya hatari.

Christopher Mtikila (DP)
Baada ya kasheshe la jana la kupigwa mawe kwenye uwanja wa Sabasaba, amekaririwa akilalamikia hali hiyo aliyodai kuwa imetokana na njama za wapinzani wake.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mtikila amekaririwa leo asubuhi akisema: ``Nilitoa taarifa mapema kwa Msimamizi wa Uchaguzi na OCD.. niliwaeleza juu ya agizo la mimi kupigwa mawe...``

Freeman Mbowe (CHADEMA):Mbowe na chama chake cha CHADEMA wamekuwa nao wakilalama kuonewa na askari polisi walio katika operesheni kali ya kulinda amani katika jimbo hili.

Aidha, kwa nyakati tofauti, yeye, Katibu Mkuu wake Dk. Wilbroad Slaa na Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho, Halima Mdee, wamekuwa wakitoa madai ya kuonewa kwa kunyimwa viwanja vya kufanyia kampeni za mgombea ubunge wa chama chao, Bw. Charles Mwera.
Prof. Ibrahim Lipumba (CUF)

Baada ya kutosimamisha mgombea jimboni humo ili kuwapa fursa wenzao wa upinzani jimboni humo, Prof. Lipumba na chama chake wamekuwa katika wakati mgumu wa kuamua wamuunge mkono mgombea yupi baada ya wenzao kuwasaliti kwa kusimamisha mgombea zaidi ya mmoja, kinyume cha makubaliano.

Mkanganyiko huo unadaiwa kutokea baada ya vyama vinavyoungana nacho katika umoja wao wa vyama vikiwemo vya CHADEMA, TLP na NCCR-Mageuzi kushindwa kumsimamaisha mgombea mmoja, hasa baada ya NCCR na CHADEMA kusimamisha wagombea wawili tofauti.

Hata hivyo, ingawa CUF Tarime wameamua kumuunga mkono Bw. Charles Mwera wa CHADEMA, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Wilfred Lwakatare, amekaririwa asubuhi ya leo akisema kuwa wamemtuma jimboni humo kiongozi wao Mustafa Wandwi ili kuangalia ni mgombea yupi anayeelekea kukubalika zaidi ili hatimaye wamuunge mkono.

Wakati huohuo, Jeshi la Polisi jimboni humo limesema liko makini katika kudhibiti vitendo vyote vinavyoashiria kuvunja amani.

Akizungumza na Alasiri juzi, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Liberatus Barlow, amesema FFU na polisi wengine kibao waliomwagwa jimboni humo wamejipanga vilivyo katika kuhakikisha kuwa uvunjifu wa amani unadhibitiwa ipasavyo.

Wakati huohuo, katika kuthibitisha kuwa Polisi wako makini, tayari wameshawanasa watu wanne wanaotuhumiwa kumvurumishia mawe Mchungahji Mtikila jana na kuwawezesha kuburuzwa kortini.

Walionaswa na polisi katika tukio hilo la jana na ambao leo wamepandishwa kizimbani ili kujibu mashtaka.

Kamanda Barlow amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mussa Peter, Mwita Chacha, Hafidh Stanslaus na Mwita Kilongo.

Amesema watuhumumiwa hao, mmoja alikamatwa wakati wa tukio la kupigwa kwa Bw. Mtikila na wengine watatu walikamatwa jana katika msako wa Polisi uliofuatia kujiri kwa tukio hilo la kupigwa kwa Mtikila.

SOURCE: Alasiri

Monday, August 04, 2008

Vigogo Wahaha! - Kifo cha Wangwe

Naona hata mwandishi wa hii stori kahofia maisha yake, wameandika 'mwandishi wetu' . Sasa kilichobaki ni kuita Scotland Yard wachunguze.

*******************************************************

Kutoka ippmedia.com

Kifo cha Wangwe: Vigogo BP juu!

2008-08-04

Na Mwandishi Wetu, Jijini

Mazingira tata ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, Mhe. Chacha Wangwe (CHADEMA), yamewafanya baadhi ya vigogo kuingiwa na hofu kubwa ya maisha yao na sasa wengine wamedai kuwa wana data ambazo hata kuzianika hadharani wanaogopa kwa sababu za kiusalama.

``Uchunguzi umethibitisha wazi kuwa Wangwe hakuuawa kwa risasi... lakini pamoja na ukweli huo, bado baadhi ya vigogo katika siasa, hasa wale wa upinzani, wamekuwa na hofu kutokana na mazingira tata ya ajali yenyewe na kile kilichomtokea (Wangwe) hadi kufa,`` kimesema chanzo chetu kimoja kilicho jirani na vigogo maarufu wa upinzani nchini.

``Hivi sasa kuna data nyingi zilizopatikana na kuibua maswali mengi kuhusiana na kile kilichotokea. Kijana aliyekuwa na Wangwe wakati wa ajali ndiye anayeelekezewa kidole zaidi kutokana na maelezo yake kila alipohojiwa... hili limeongeza hofu zaidi kwa vigogo hao, wakiamini kuwa wao wako hatarini na taifa pia liko hatarini,`` kimeongeza chanzo hicho.

Taarifa hizo za kuwepo kwa hofu miongoni mwa baadhi ya vigogo zimetiwa nguvu na yale yaliyosemwa jana Wenyeviti wa Umoja wa Vyama vinne vya upinzani nchini jana na kunukuliwa na vyombo vya habari leo asubuhi, kuhusiana na shaka iliyopo katika ajali iliyomuua Mheshimiwa Wangwe.

Wakizungumza hiyo jana, wenyeviti wa vyama hivyo vya CUF, CHADEMA, TLP na NCCR, wamesema wanazo taarifa zinazoibua maswali mengi kuhusiana na kifo cha Wangwe, hasa juu ya kijana anayedaiwa kuwa naye ndani ya gari, Bw. Deus Mallya.

Wakasema maelezo ya kijana huyo juu ya tukio hilo, namna Wangwe alivyopata majeraha yaliyomuua na ziada ya taarifa walizopata toka kwa watu wanaomfahamu kijana huyo (Mallya), ni baadhi ya mambo yanayowafanya wawe na hofu kuwa kuna ujasusi umefanyika.

Wakasema viongozi hao ambao ni Prof. Ibrahim Lipumba wa CUF, Augustino Mrema (TLP) na James Mbatia (CHADEMA), kuwa kwa taarifa walizo nazo, wanaamini vilevile kuwa upo mtandao hatari unaotishia usalama wa taifa.

Akizungumzia hofu hiyo, Prof. Lipumba akasema waliyemuona Mallya kabla ya tukio, wanasema alikuwa ni mtaalam wa kompyuta, alikuwa na vitambulisho vingi na vingine vimeandikwa kiarabu na pia, wanahisi kuwa amepata mafunzo ya kijasusi nchini Libya.

``Imekuwaje akawa karibu na marehemu kwa muda mfupi?`` Akahoji Profesa Lipumba wakati wakizungumza na waandishi wa habari. Akautaja utata mmojawapo juu ya kifo cha Wangwe kuwa ni kuonekana kuwa kichwa cha marehemu kimepondeka na hakuna maelezo dhahiri ya suala hilo. ``...mle ndani ya gari hakuna hakukuwa na vyuma wala mabati yaliyopondeka.

Kweli hakufa kwa kupigwa risasi... lakini ile ajali ilitokeaje mpaka lochwa kikapondeka?`` akasema Prof. Lipumba. Aidha, Mbatia naye akasema.

Aidha, Mbatia naye akasema kutokana na utata mwingi juu ya kifo hicho ikiwa ni pamoja na maelezo ya kujikanyaga ya kijana Mallya, wao wameamua kumuona IGP Said Mwema ili wampe taarifa za siri kuhusiana na ukweli wa kifo hicho, kwa maslahi ya taifa.

``Inaonekana kuna mtandao unaohatarisha usalama wa nchi.... kijana huyo (Mallya) ana mafunzo ya Kimafia,`` akasema Mbatia.

SOURCE: Alasiri