Showing posts with label Emmanuel Myamba. Show all posts
Showing posts with label Emmanuel Myamba. Show all posts

Sunday, August 03, 2014

Pastor Myamba Azawadiwa Gari Na Pesa Taslim Shilingi 250M/- Katika Harusi Yake Huko Zanzibar!

Pastor Emmanuel Myamba na Mke wake


Picha na Maelezo Kutoka Swahili World Planet Blog:

Harusi ya Pastor Myamba pengine ndiyo harusi ya star wa Tanzania kuzawadia mali nyingi zaidi ! Myamba amefunga ndoa Zanzibar weekend hii huku akizawadia zawadi kibao za mamilioni likiwemo gari na pesa taslim shilingi milioni 250 za kitanzania. Mastaa mbalimbali wamehudhuria harusi hiyo visiwani Zanzibar. piacha zaidi zinakujia...........



Wednesday, February 20, 2008

Mwigizaji wa Bongo - Emmanuel Myamba

(kutoka kushoto, Emmuel Myamba, Mimi, Steven Kanumba)

Hii picha nilipiaga mwezi wa saba mwaka jana Bongo. Tulikuwa Magomeni, Dar es Salaam kwenye shoot ya filamu Bongoland II siku ya kwanza. Bongo Superstars Steven Kanumba na Emmanuel Myamba walikuja kututembelea kwenye seti. Sikujua kuwa huyo Emmanuel naye ni actor alielekea mpole kweli.

Nimebahatika kuona sinema ya Fake Pastors. Mle Emmanuel anaigiza kama Evangelist wa kanisa. Kwa kweli ana kipaji cha kuigiza yaani kama kuna tuzo ya Best Supporting Actor Bongo, anastahili yeye. Anaigiza vizuri mno mpaka wewe mtazamaji unasema unataka kumwona zaidi na zaidi. Unaamini kabisa kuwa huyo ni Evangelist anayependa kanisa lake, dini yake na waumini wake. Haonekani kama anaigiza hata kidogo. Natabiri ataenda mbali sana katika fani ya uigizaji na si Bongo tu hata nje ya nchi. Sinema ya Fake Pastors ina kasoro zake lakini huyo jamaa ni nyota!

Thursday, July 26, 2007

Mimi na Steven Kanumba


Siku ya kwanza kwenye shoot ya Bongoland II huko Magomeni Mikumi, tulibahatika kutembelewa na maSuperstar wa Bongo. Kulia kwangu ni mcheza sinema maarufu wa Bongo Steven Kanumba. Kushoto ni Emmanuel Myamba ambaye naye ni Bongo Superstar.

Kwa kweli nilifurahi sana kuwaona, hasa Steven maan nilikuwa nimesikia sifa zake na hasa habari ya sinema ya Dar 2 Lagos. Bado sijaiona lakini.
Kwa habari zaidi za Steven Kanumba soma: