Showing posts with label Gongo la Mboto. Show all posts
Showing posts with label Gongo la Mboto. Show all posts

Thursday, December 13, 2012

Rais Kikwete Akabidhi Nyumba Mpya 35 za Walioathirika na Mlipuko ya Mabomu Gongo la Mboto



Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiakata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012


Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga nyumba mpya 35 kwa ajili ya waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.





 Baadhi ya nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekqana leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete


PICHA NA IKULU

Saturday, February 19, 2011

Picha na Video za Maafa ya Mabomu Dar

Hivi jamani, jeshi inafanya nini kuondoa hayo mabomu yaliyoanguka uraiani? Kuna mengine ambayo hakulipuka, si wananchi wako hatarini? Kuna uwezekano mkubwa kuwa watoto wataende kuyachezea halafu yakalipuka na kuwaua.

************************************************************
Picha kwa hisani ya Bongo5.com na email:

Kombora iliyoanguka kwenye shamba la mchicha

Kombora lililowekewa uzio wa usalama na jeshi la polisi
Wananchi bado wakiwa katika hali ya mshtuko siku baada ya mlipuko wa Mabomu katika kambi ya jeshi Gongo la mboto
Nyumba iliyoathirika na mabomu yaliyolipuka

Picha Kutoka Pugu Secondary School

Mnaweza kuona picha na video zaidi kwa KUBOFYA HAPA:

International Report on Tanzania Explosions

The AP put this story out, but very few media in the USA picked it up,or were very brief in their reporting.

***********************************************************************
2/17/11
DAR ES SALAAM, Tanzania (AP) - Thousands of people crowded a stadium for safety Thursday after a military ammunition depot exploded and showered the city with a series of blasts, killing at least 25 and prompting a stampede getaway.
In the mayhem of residents fleeing the blasts, more than 150 children lost track of their parents, and officials appealed for mothers and fathers to report to the stadium to reunite with their offspring.
"People were just running, so some children were lost in the mobs of people. Now at the centers we are trying to get them connected with their relatives," Red Cross worker Julius Kejo said.
President Jakaya Kikwete promised an investigation into the explosions Wednesday night and Thursday morning, the second fatal military ammo dump explosion in Tanzania's commercial capital in less than two years. An accident at a Dar es Salaam military base in 2009 killed more than a dozen people.
Several houses and a school were leveled during the latest blasts, which sent huge orange bursts into the night sky. Debris showered parts of the city 10 miles (15 kilometers) from the Gongola Mboto military base where the depot was located.
On the base, 23 weapons storage facilities, five vehicles, two soldier dormitories and the general store were destroyed, said Lt. Col. Kapambala Mgawe.
When the explosions hit, thousands of people living in nearby neighborhoods fled. Families scattered, separating parents from their children.
Hidan Ricco, the head of Tanzania's Red Cross disaster management team, said there were about 200 unaccompanied children at the stadium, some of whom are only months old. A city official appealed for parents to find their children.
"We can't figure out how these children ended up here," Ricco said. "We don't know where are their mothers."
The blasts closed the city's international airport, near the Gongola Mboto military base, though it opened later Thursday. Some 4,000 residents were evacuated to the national stadium in Dar es Salaam, which lies along the Indian Ocean in East Africa.
Selina Chacha, 30, was looking for two her boys - ages 8 and 10 - at the stadium.
"I'm so sad that my children are still missing. I have been running up and down looking for my them but they are nowhere to be found," Chacha said, whose house was only 1 mile (2 kilometers) from the blasts.
Stella Philip, 23, was at home cooking when the explosions began around 9 p.m. Her daughter Habiba Saleh, 8, who was playing outside at the time, is missing.
"I have not seen such deafening blasts in my life," she said. "After the blasts everyone ran for his life."
The president visited the site of the blasts and tried to assure a still-jittery public that no more explosions would happen.
Felician Luchagula, a 32-year-old health-related development worker, said he heard blasts beginning at around 9 p.m. Wednesday. They continued for several hours.
"People are getting scared of what may happen to them. People are scared that if they live near a military base it might happen again," he said.
---
Straziuso reported from Nairobi. Associated Press writers Malkhadir M. Muhumed in Nairobi, Kenya and Carley Petesch in Johannesburg contributed to this report.

Friday, February 18, 2011

Blast Kills 25 in Tanzania

Nimeona hii kwenye internet. Lakini inaelekea idadi yawaliokufa ni kubwa zaidi.

***********************************
World Briefs (02/18/11)
From wire reports

Blasts kill 25 in Tanzania
DAR ES SALAAM, Tanzania -- Thousands of people crowded a stadium for safety Thursday after a military ammunition depot exploded and showered the city with a series of blasts, killing at least 25 and prompting a stampede getaway.

In the mayhem of residents fleeing the blasts, more than 150 children lost track of their parents, and officials appealed for mothers and fathers to report to the stadium to reunite with their offspring.

The blasts closed the city's international airport, near the Gongola Mboto military base, though it opened later Thursday. Some 4,000 residents were evacuated to the national stadium in Dar es Salaam, which lies along the Indian Ocean in East Africa

Read more: http://www.post-gazette.com/pg/11049/1126263-82.stm#ixzz1EKmIos00


*************************************************************
Kutoka CNN.Com
(CNN) -- A series of explosions at a military base in Tanzania killed 20 people and displaced 4,000 residents, Prime Minister Mizengo Pinda said Thursday.

In a statement delivered as he adjourned the parliament, Pinda said the blasts occurred Wednesday night at an ammunition bunker at the Gongola Mboto army base in Tanzania's commercial capital, Dar es Salaam. It destroyed 23 munitions depots as well as a nearby school and two houses, and forced 4,000 people to seek shelter at the national stadium.

"The death toll might rise when we ascertain the full extent of the damage caused by the explosions," Pinda said.

Earlier, another official said at least 184 people were injured in the explosions that lit up the night sky in Dar es Salaam and spread debris throughout surrounding areas.
Nyancheghe Nanai, assistant director of disaster management, was unable to say what caused the explosions but added that she "does not think" they were related to terrorism.

Two years ago, explosions at another arms depot in Dar es Salaam left 29 dead from rocket and artillery discharges, Nanai said. Those blasts were not caused by terrorism, she said.

The explosions in the densely populated city rattled neighborhoods and forced the closure of the main international airport, which is near the army base.

Hali Ilivyokuwa Dar Wakati wa Milupuko


Nimepokea picha na habari hizi kwa email:

Wanaoonekana kwenye picha ni watu wakiwa kwenye malori, wengine juu ya Carrier za mabasi aina ya DCM na wengine wakitembea kwa miguu wakiyahama makazi yako kufuatia tangazo la kuwataka wananchi waondoke maeneo hayo.

Kwa sasa simu hazipatikani, ambulance na magari ya msalaba mwekundu ndiyo yanayotoa msaada kwa walio na dharura.

Kwa anaefahamu mtaa wa Kongo DSM au Makoroboi Mwanza, idadi ya wanaotembea kwa miguu ndiyo hali ninayoiona sasa hivi hapa eneo la Tazara hadi Airport.

Tunaomba polisi wa usalama barabarani wasaidie magari yapite kwani kuzuia yanayotoka mjini au yaendayo barabara za kando ya Nyerere Rd, ni kuwanyima haki ambao wanahitaji kwenda kuokolewa.

Inabidi wahusika wajiuzulu mara moja. Its terrible!!!

Naona mabig shot wanapita na mamisafara yao yasiyo na tija kwa wananchi wakienda na kutokea huko Gongo la Mbotto.

Thursday, February 17, 2011

Makombora Dar

Makombora
Thursday, 17 February 2011
Na Waandishi Wetu (Gazeti la Mwananchi)

JIJI la Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo limetaharuki kufuatia milipiko mikubwa ya mabomu iliyotokea ghala la kutunzia silaha la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Gongolamboto, huku kukiwa na taarifa za watu kufa na zaidi ya 100 kujeruhiwa. Timu ya waandishi wa Mwananchi waliotembelea eneo la tukio usiku wa jana, walishuhudua nyumba kadhaa zikiteketea kwa moto baada ya kuangukiwa na mabomu.

Kadhalika waandishi hao wa Mwananchi walishuhudia nyumba moja ambayo ukuta wake ulibomoka baada ya kuangukiwa na bomu na ukuta huo kuangukia kundi la zaidi ya watu 12, watu watano wanadaiwa kufa.

Mmoja wa walionusurika kwenye tukio la kuangukiwa na ukuta, Juma Nganyanga, alisema kuna uwezekano ya maiti wengine kuwa chini ya ukuta huo.

Nganyanga alisema aliona kundi la watu wakiwa wamekimbilia kupumzika kwenye baraza la nyumba hiyo baada ya kukimbia nyumba zao, wakati wakiwa katika maombi ya kuomba Mungu awaepueshe na janga hilo, ghafla aliona vumbi likitimka kwenye nyumba hiyo.

Mwenye nyumba hiyo, Farida Magwa, ambaye alikuwa akibubujikwa na machozi alisema akiwa barabarani na familia yake, aliambiwa kuwa nyumba yake imepigwa bomu na kuna watu wameuawa.

Magwa alisema baadaye waliweza kutoa maiti za watu watano, wakiwamo watoto wawili, lakini kuna uwezekano wa wengine bado wapo wamefunikwa na kifusi cha ukuta huo.

Katika tukio jingine, Mwananchi ilishuhudia maiti ya mwanamke ikiwa kwenye nyumba ambayo imeteketea baada ya kupigwa na bomu eneo la Mzambarauni na maiti nyingine ikipandishwa kwenye gari eneo la gereza la Ukonga.

Pia, Mwananchi lilishuhudia jengo la hosteli ya Kanisa Katoliki Ukonga likiwa linateketea kwa moto baada ya kuangukiwa na bomu, huku wakazi wa hosteli hiyo wakiwa wamekimbia.

Moto huo ambao ulikuwa ukiendelea kuwaka hapakuwapo na jitihada zozote za kuweza kuuzima, kwani watu wote walikuwa wamekimbia.

Mlinzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Tanzania (KKKT) lililopo jirani na hosteli hiyo, alisema alishuhudia mabomu mawili yakitua eneo hilo, moja likitua kwenye nyumba ya hosteli hiyo na lingine pembeni karibu na gereza la Ukonga.

Milipuko hiyo ilianza majira ya saa 2.00 usiku na kuendelea mfululizo hadi saa 6.00 usiku, huku watu wakitaharuki na baadhi ya wanandungu na familia kupotezana.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadiq, alithibitisha kutokea kwa kifo cha mtu huyo ambaye hata hivyo jina lake lilikuwa halijafahamika.

Katika Hospitali ya Amana, Ofisa Mwandamizi wa Wagonjwa wa Nje, Mussa Wambura, alisema watu wawili walifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini hapo na kwamba, hadi saa 7:00 usiku walikuwa wamepokea majeruhi 88, wengine hali zao zikiwa mbaya.

Waandishi wa Mwananchi walishuhudia magodoro yakiwa yametandikwa nje ambako wagonjwa walikuwa wamelazwa na wahudumu wa afya kutoka hospitali za TMJ na Hindu Mandal walipelekwa Amana kuongeza nguvu.

Pia, Sadiq alithibitisha kujeruhiwa kwa watu 43 na kwamba, serikali ya mkoa ilikuwa imetenga hospitali mbili za Ilala (Amana) na Temeke kwa ajili ya kupokea majeruhi na kuwatibu.

Awali, taarifa za zisizo rasmi zilizolifikia Mwananchi zilidai kuwa, mabomu yaliyolipuka ni ya masafa marefu.

Taarifa hizo zilithibitshwa na Sadiq ambaye aliwanukuu JWTZ wakisema, mabomu yaliyolipuka yanaweza kwenda umbali wa kilomita 11 kutoka eneo la tukio, Gongolamboto.

Alisema kwa mujibu wa taarifa hizo, wananchi walipaswa kuondoka eneo hilo na kuelekea katikati ya Jiji la Dar es Salaam na kwamba, wangekuwa salama baada ya kufika eneo la Tazara wakati kwa wale walioelekea Kisarawe alipaswa kwenda hadi eneo la Pugu Kajiungeni.

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, alinukuliwa akiwataka wakazi wa Gongolamboto na maeneo ya jirani kuhama makazi yao kutokana na milipuko hiyo.

Kadhalika Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alinukuliwa akiwataka wakazi wa maeneo hayo kuondoka kuepusha athari zinazotokana na milipuko hiyo.

Wananchi wakimbia makazi
Habari zaidi zilisema mamia ya wananchi waliyakimbia makazi yao, wengi wakielekea katikati ya Jiji la Dar es Salaam, lakini baadaye matangazo yaliyotolewa na vyombo vya usalama yaliwataka kwenda Uwanja wa Taifa kwa ajili ya kupata hifadhi ya muda.

Kwa mujibu wa mashuhuda, watu walikuwa wakikimbia ovyo huku wakipanda magari yaliyokuwa yakielekea katikati ya jiji, kusalimisha maisha yao.

Baadhi ya wananchi waliolazimika kuyakimbia makazi yao, walikuwa wakipiga simu chumba cha habari wakilalamikia kupotezana na ndugu zao.

Mamia ya watu kutoka Gongolamboto, Karakata, Tabata, Segerea, Ukonga, Kitunda, Banana na maeneo mengine jirani, walionekana wakipanda daladala, wengine wakining'inia nyuma ya magari hayo yaliyokuwa yakielekea katikati ya jiji, huku mamia kwa mamia ya watu walikuwa wakitembea kwa miguu kuokoa maisha yao.

Kadhalika pikipiki, bajaj na magari ya kama pick-up pia yalitumika kuwahamisha watu kutoka eneo la tukio kwenda kutafuta sehemu ya hifadhi ya muda.

Uwanja wa ndege wafungwa
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, ulifungwa kwa muda na ndege zote hazikuruhusiwi kuruka wala kutua hadi hapo itakapoarifiwa baadaye.

Waandishi wa Mwananchi walishuhudia abiria wengi wa kigeni wakiwa kwenye uwanja wa huo wakisubiri kujua hatma ya safari zao, baada ya ndege walizokuwa wakizisubiri kuamriwa kutua viwanja vya Kia na Zanzibar hadi hapo watakapopewa maelekezo mengine.

Barabara ya Pugu katika njiapanda inayoingia kambi ya jeshi, ilifungwa na magari yote yaliyokuwa yakielekea katikati ya jiji na yale yaliyokuwa yakielekea Kisarawe yalizuiwa.

Mkazi mmoja wa Kigamboni aliyepiga simu ofisi za gazeti hili jana usiku wakati milipuko ya mabomu hayo ikiendelea, alisema wakazi wengi wa Kigamboni walikuwa nje ya nyumba zao, huku wakishuhudia makombora yaliruka juu kuelekea baharini hali ambayo iliwafanya wakazi hao kukumbwa na wasiwasi mkubwa.

"Hivi ninapokupigia wewe, makombora yanapita juu na kila mtu na familia yake wako nje kwa hofu...unasikia muungurumo huu kombora jingine linapita hapa juu kuelekea baharini," alisikika mwananchi huyo.

Kauli ya Dk Mwinyi
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk Hussein Mwinyi, alisema milipuko hiyo ilitokea ghala namba tano na kwamba, kilichokuwa kikifanyika ni kuzuia usienee sehemu nyingine.

Dk Mwinyi alisema kambi ya Gongo la Mboto wanaishi wanajeshi na familia zao, lakini maghala ya mabomu yako mbali na kuongeza kuwa, kutokana na milipuko hiyo kuwa mikubwa hawezi kuzungumzia athari.

“Ile ni kambi ya jeshi, watu wanakaa mbali na maghala lakini kwa sababu tukio lenyewe ni kubwa sasa hivi hatuwezi kusema lolote,” alisema Dk Mwinyi.
Wakati mabomu hayo yakiendelea kulipuka mwananchi mmoja alipiga simu chumba cha habari cha Mwannchi, akisema Waziri Mwinyi yalipolipuka mabomu ya Mbagala, aliahidi kujiuzulu iwapo ingebainika kulifanyika uzembe.

Hata hivyo, Dk Mwinyi alipoulizwa usiku wa kuamkia leo kuhusu utekelezaji wa ahadi yake hiyo na majibu ya tume zinazoundwa, alisema kilichokuwa kinafanyika usiku ni kuokoa maisha ya watu, masuala mengine yatazungumzwa baadaye.

“Sasa hivi kuna jambo linaathiri watu, kwanza tuwaokoe halafu haya mengine tutazungumza,” alisema Dk Mwinyi.
Milipuko ya kwanza ilitokea barabarani mwaka 1972 wakati mabomu hayo yalipokuwa yanahamishwa kutoka Kambi ya Kunduchi kwenda Gongolamboto.

Kwenye kambi hiyo ni mara ya pili kutokea kwa milipuko ya mabomu, milipuko ya kwanza ilitokea mwaka 2008 na kusababisha maafa kwa wananchi wanaozunguka kambi hiyo, wanajeshi na familia zao.
Kila mwaka wataalam wa mabomu jeshini ambao hujulikana kama Ammo tech, wanaofanya kazi chini ya Chief Logistic and Equipment (CLE) hukagua mabomu ambayo muda wake umemalizika ili yaweze kupelekwa Kimbiji kuteketezwa.

Mbagala
Hali ilikuwa tete maeneo ya Mbagala na kusababisha watu wakiwa na watoto kukimbia ovyo, huku wengine wakijikusanya pembeni mwa barabara.
Wakazi wa Mbagala ambao walikumbwa na milipuko kama hiyo Aprili 2009, walionekana kuchukua tahadhari mapema baada kuanza kusikia milipuko kwa kuondoka ndani ya nyumba zao.

Mwananchi ilishuhudia wananchi hao wakiwa wamekusanyika pembeni mwa barabara ya Mbagala Rangi tatu-Mbande, hasa eneo la Muhimbili wanakopelekwa wagonjwa wa akili baada ya kupata nafuu, ambako kuna nafasi kubwa.
Maeneo ya Chamazi, Mbande, Charambe na Mbagala Rangi tatu, nyumba zilikuwa zikitikisika kutokana na milipuko hiyo, huku angani kukiwa kumetanda miale ya moto.

Mwandishi wa gazeti hili, Midraji Ibrahim, alisema kwenye nyumba yake iliyopo Chamazi, mikanda ya dari (ceiling board) ilidondoka kutokana na kishindo cha milipuko ya mabomu hayo.
Mlipuko wa 2008

Mwaka 2008 kulitokea mlipuko ghala la silaha kwenye kambi hiyo ya jeshi la Gongo la Mboto katika tukio ambalo vyombo vya usalama vilidai kuwa ulitokana na silaha hizo kupata joto kali.

Imeandaliwa na Julius Magodi, Neville Meena, Midraji Ibrahim na Andrew Msechu (Mwananchi)

Wednesday, February 16, 2011

Picha za Maafa ya Mabomu Dar

Pichani baadhi ya Majeruhi wakiwasili Muhimbili. Picha kwa hisani ya Kaka Michuzi

Picha zaidi ziko Michuzi Blog. BOFYA HAPA

Taarifa ya Polisi Kuhusu Mabomu Dar


Mabomu Dar!

Habari nilizopata nikuwa Julius Nyerere International Airport imefungwa!

Watu watano wamekufa na 4o wameumia. Wanasema idadi itaongezeka.

Kuna bomu ilielekea Ubungo/Magomeni/Kigogo.

Wananchi wameelekezwa waende Uwanja wa Taifa kulala leo. Barabara ya kwenda uwanja wa ndege, Nyerere Road (Pugu Road) Imejaa watu.

Simu hazipatani. Najribu kuwapigia watu pamoja na wazazi wangu Tenki Bovu Dar siwapati.

JWTZ na Mabomu

Hivi Jeshi la Wananchi Tanzania inashindwa kuhifadhi mabomu? Mwaka juzi mabomu yao yalilipuka Mbagala. Leo tunasikia yamelikpuka kambi la Gongo la Mboto. Hao wanaotunza mabomu wanafundishwa kuytatunza kweli? Au ni sabotage? AuTutasikia imekuaje miezi kadhaa baada ya Tume kuundwa na kutoa ripoti yake.

Mwaka 1984, nilipokuwa Masange JKT Tabora, kambi ilipewa ruhusa na Makao Makuu kutumia baruti (Dynamite) kutishia simba waliokuwa wanatusumbua. Hao simba wala watu waliua watu kadhaa katika kijiji cha jirani.

Haya, walipewa ruhusa na walikuwa walizitegesha. Aliyekuwa msimamizi alikuwa ni Luteni Usu. Sasa akatokea kuruta/private mwenye ujuzi na dynamite. Alikuwa mhandisi uraiani. Aliwaonya kuwa walikata utambi mfupi mno. Luteni usu alisema kuwa anajua anachofanya, na huyo 'msomi' anayamaze. Kuona wanakaribia kuwasha yule Kuruta alikimbia, waliwasha na walaiokuwepo walilipuliwa! Hakuna aliyakufa lakini jamaa moja alikatika mkono, Lusteni Usu alipofuka na wengine walipata majeraha kadhaa.