Showing posts with label US Airways. Show all posts
Showing posts with label US Airways. Show all posts

Saturday, September 03, 2011

Fesheni 'GawaKundu' Yaleta Matatizo!

Hii fesheni ya kutangaza kuwa unagawa mkundu, umemletea mtu mwingine matatizo hapa Marekani.

Leo kuna habari kuwa mwimbaji Billie Joe Armstrong wa bendi Green Day alifukuzwa kwenye ndege ya Southwest Airlines alipokataa kupandisha suruali yake zilizokuwa fesheni GawaKundu. Alikuwa anasafiri kutoka Oakland, California kwenda Burbank, California. Soma habari kamili kwa kubofya HAPA.

Msemaji wa Southwest anasema kuwa Armstrong aliruhusiwa kupanda ndege nyingine. Nadhani kwa vile mzungu.

Kuna kijana mwingine mweusi ambaye alifungwa mwaka huu kwa vile alijaribu kupanada ndege ya US Airways na fesheni GawaKundu. Deshon Marman ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha New Mexico na pia mcheza football alikamatwa na kushitakiwa kwa makosa kadhaa ya jinai.

Lakini ajabu, kuna mwanaume wa kizungu aliyeruhusiwa kupanda ndege ya US Airways akiwa amevaa chupi ya kike na sidiria tu!

Soma habari ya Marman na Bikini Man kwa kubofya HAPA:


US Airways wamefuta mashitaka dhidi ya Marman, lakini keshateseka na kuaibika, na pia hawajamrudishia nauli ya $500 wala kumwomba msamaha! Wanasema kuwa Crew walikuwa na haki ya kufukuza kwenye ndege. Ukiwa mtu mwenye rangi Marekani ushike adabu ukipanda kwenye ndege asante 9/11! Sasa hao crew ya ndege wanaweza kukufukuza kwenye ndege hata wasipopenda sura yako!

Kwa habari zaidi ya kesi ya kijana Marman tembelea:

http://www.sfexaminer.com/local/peninsula/2011/07/deshon-marman-sue-us-airways-after-saggy-pants-arrest

NOTE: Fesheni GawaKundu si mbayawakati mwingine, nimeshaona matako ya vijana wengi wa kizungu, weusi na waAsia baada ya suruali zao kuanguka wakiwa wanatembea!!! LOL!

Thursday, January 15, 2009

Ndege Imeanguka New York!


Ndege ya US Airways, imeanguka huko New York. Ni US Airways Flight 1549. Kwa bahati imeaguka mtoni Hudson River. Ilikuwa hewani, dakika tatu kabla ya ndege aina ya bata kuingia kwenye injini zote mbili.
Abiria wote 148 wako salama! Ndege ilikuwa inatoka LaGuardia Airport kwenda Charlotte, North Carolina.

Abiria wanasema walibakia kuomba baada ya rubani kutangaza "Brace for Impact"!
Kwa habari zaidi someni: