Showing posts with label Ufisadi. Show all posts
Showing posts with label Ufisadi. Show all posts

Saturday, March 18, 2017

Comfort Zone - A Poem by Prof Richard Mabala

FROM FACEBOOK

Comfort Zone

By Richard Mabala 

First they came for the big guys
They were all fisadis
But I am not a fisadi so why should I speak out?
Even if no evidence has been given against them
We were told they were fisadis
What greater evidence do you want?
Silently I applauded.
Then they came for the artists
Decadent artists leading immoral lives
Why should I support them?
No evidence again but God had spoken
I said not a word.
Of course they came for the gays
Even wanted to publicly declare their names
Even more disgusting than the artists
I don't care whether they do it in private or not
They deserve it.
No need to speak out
They also came for the activists
Those arrogant unelected nobodies
Pushing their own agendas as if they were the people's choice
They had to be silenced
So silent I remained.
Then they came for an Asian
These Asians, don't we know them
They are just exploiting us
How can he claim to be a citizen like me?
A proud Tanzanian
So what if he was a councillor in my own party
Why should I speak for these exploiters?
And anyway I support that other team
Too patriotic to support him or his team.
So no need to speak out
Even if there seems be a vendetta against him
For daring to threaten the son of God
Silence is golden
Then they came for the opposition.
Why should they go on politicking even after the election.
Throw them in jail
And keep them there to show our leaders brook no opposition
Opposition disrupts their good intentions.
Troublemakers.
They deserve to stay in jail
I said nothing
The same is true of those people
Who used unbecoming language
On Facebook
They should have known better
They were warned
But still the persisted.
Why should I speak in their favour
Then they came for the lawyers
Especially those dumb oppositionist lawyers
Wanting to take over their association
And become activist
Activist? Really?
We know those lawyers are just after money
And power
Corrupt.
Surely they can defend themselves anyway.
Say nothing.
Then they came for their own party members
Ha ha ha. You see their foolishness
Fraternising with the enemy when politics is no longer about adversaries
But enemies.
They couldn't even see which way the wind is blowing
And bow before it
They were flattened
And I will never say a word
Even if they belonged to my party
Unlike them, I am loyal
Always loyal.
But hang on
What are those boots outside my door?
What have I done?
HELP! Will someone speak out for me?
I have done nothing.
Why the silence?
Am I the only one left?

Thursday, January 03, 2013

Maandamano dhidi ya Bomba la Gesi: Kilio cha Uwajibikaji

Maandamano dhidi ya Bomba la Gesi

Picha Hisani ya: Mtwara Kumekucha Blog by Baraka Mfunguo

'Dar inachangia asilimia 80 ya mapato. Kitovu cha Uchumi. Dar inachangia 90% ya ufisadi. Uti wa mgongo wa ufisadi nchini'


Na Mh. Zitto Kabwe
Malumbano kati ya wananchi wa Mtwara na Serikali kuhusu matumizi bora ya utajiri wa nchi yameendelea kwa takribani wiki moja sasa. Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Nishati na Madini kuwaita Watanzania wa Mtwara Wahaini, wapuuzi na watu hatari, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naye aliingia kwenye mjadala huo kwa kuonya watu wanaowaunga mkono watu wa Mtwara na kuwaita watu wanaotafuta umaarufu wa kisiasa na wanaotaka kugawa nchi. Siku moja baada ya hotuba ya Rais, Waziri wa Nishati na Madini alifanya mkutano na waandishi wa habari kueleza suala lile lile ambalo bosi wake alilielezea usiku wa kuamkia mwaka mpya 2013. Hii ni dalili ya Serikali kuweweseka.

Katika kauli ya Serikali, ambayo haikuwa na jipya zaidi ya wimbo ule ule wa ‘kugawa nchi’ ‘umaarufu wa kisiasa’ nk, Serikali ilitaka kuonyesha umma kuwa watu wa Mtwara hawana shukurani. Kwamba miaka yote toka Uhuru watu wa Mtwara wamekuwa wakilishwa na Pamba, Kahawa, Chai, Tumbaku, Sukari, Kidatu nk. Kwamba watu wa Mtwara na Lindi hawakuchangia hata kidogo kwenye hazina ya Taifa. Hivyo wao kupigia kelele gesi yao ni uchoyo na roho mbaya na kukosa shukurani. Kauli ya Serikali ni kauli ya chombo kinachoendelea kukosa ‘legitimacy’ ya kuongoza taifa. Ni kauli ya kukata tamaa. Ni kauli hatari sana dhidi ya Watanzania waliojitolea damu kulinda uhuru wa nchi yetu.

Moja, Serikali katika kauli yake haitaji kabisa kwamba toka Uhuru watu wa Mtwara na Lindi wamekuwa wachangiaji wakubwa sana katika uchumi wa Taifa kupitia zao la Korosho. Takwimu za Uzalishaji wa Korosho zinaonyesha kwamba kuanzia mwaka 1965 mpaka 2011 Korosho imeliingizia Taifa fedha kigeni jumla ya dola za Kimarekani 4.58 bilioni ( Cashewnuts Sub-sector study 2003, Hali ya Uchumi 2012, Cashewnuts Tanzania Report 2010). Katika Mwaka wa Uchumi unaoishia Novemba 2012, Korosho imeliingizia Taifa jumla ya dola za Kimarekani 151 milioni. Katika mwaka 2011 zao hili liliingiza dola 130 milioni wakati Pamba iliingiza dola 53 milioni tu. Licha ya Zao la Korosho kuingiza fedha hizi za kigeni (sawa ni shilingi trilioni 7.2) kwa nchi mikoa ya Lindi na Mtwara ipo miaka 50 nyuma kimaendeleo kulinganisha na mikoa mingine ya Tanzania. Serikali inataka kufuta historia ya mchango wa zao la Korosho kwenye uchumi wa nchi yetu kwa sababu ya uroho wa gesi asilia. Kwa nini kauli rasmi ya Serikali haijataja Korosho kabisa? Kauli hii ilipitishwa na ngazi zote za Serikali? Mawaziri wa Serikali wanaotoka mikoa ya Lindi na Mtwara walikubali kauli kama hii itoke dhidi ya wananchi wao wanaoteseka na zao la Korosho miaka nenda miaka rudi?

Pili, Serikali imesahau kabisa mchango wa watu wa Lindi na Mtwara katika ulinzi wa Taifa letu. Moja ya sababu ya mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa nyuma kimaendeleo ni juhudi za ukombozi wa kusini mwa Afrika. Kambi ya wapigania uhuru wa Msumbiji ilikuwa Nachingwea. Kambi ya Frelimo iliwekwa kwenye Shamba la Mkonge kilometa 17 tu kutoka mjini Nachingwea ambapo ilikuwa makao makuu ya ukombozi wa Msumbiji. Rais Samora Machel, Rais Joaqim Chissano na Rais Guebuza waliendesha mapambano kutoka kusini mwa Tanzania. Makaburu wa Afrika Kusini na Wareno walikuwa wanashambulia nchi yetu na mikoa hii miwili ya Lindi na Mtwara ikawa ‘buffer zone’. Wakati Dar es Salaam inaendelea kwa kila aina ya maendeleo, mikoa ya Lindi na Mtwara ilikuwa inalinda ili wanaoishi Dar es Salaam na mikoa mingine waishi wa amani na starehe. Serikali inapimaje mchango huu wa mikoa hii? Tunaipima kwa fedha? Uroho wa gesi asilia kuzalisha umeme wa kufurahisha walalaheri asilimia 14 nchini ndio inaifanya Serikali kusahau kabisa ‘sacrifice’ ya watu wa Mtwara katika kulinda uhuru wa Taifa letu?

Tatu, Serikali inasema lazima bomba lije Dar es Salaam kwa sababu Dar ndio inazalisha asilimia 80 ya Mapato ya Serikali. Kwanza huu ni uwongo. Ni aibu Serikali kujitetea kwa uwongo. Dar es Salaam ni kituo tu cha kukusanyia mapato ya Serikali. Uzalishaji mkubwa wa nchi yetu wenye kuzalisha kodi unafanyika nje ya Dar es Salaam. Walipa kodi wakubwa wengi Ofisi zao Kuu zipo Dar es Salaam lakini uzalishaji wao unafanyika nje ya Dar es Salaam. Serikali itoe orodha ya walipa kodi wakubwa 100 tuone uzalishaji halisi wa mapato hayo unafanyika wapi. Hata hivyo inawezekana kuwa ikawa kweli Dar es Salaam inakusanya asilimia 80 ya mapato ya nchi. Basi na tuseme Dar es Salaam inachangia asilimia 90 ya ufisadi wote nchini. Kashfa zote kubwa za Ufisadi zinafanyika Dar es Salaam na fedha nyingi za ufisadi zinatumika Dar es Salaam.

Mwisho, maandamano ya watu wa Mtwara ni kielelezo tosha kwamba watu wa mikoa ya Lindi na Mtwara wamechoshwa na longolongo za Serikali. Wananchi wa Mtwara na Lindi wanataka Uwajibikaji wa Serikali kuhusu utajiri wa nchi. Mtanzania yeyote mwenye tahadhari ya nchi yetu kutokuwa na laana ya rasilimali ataungana mkono na watu wa Lindi na Mtwara kudai maendeleo. Nilitoa mfano wa Mgodi wa Golden Pride ambao umemaliza dhahabu yote tani 76 katika eneo la Lusu wilayani Nzega. Kampuni ya Resolute ya Australia iliwekeza dola 370 milioni kuanzia mwaka 1998 (mkataba wao ulisainiwa 25th June 1997). Katika kipindi cha uhai wa mgodi, miaka 14, Kampuni hii imeuza dhahabu ya thamani ya dola za kimarekani 3.3 bilioni. Kabla Serikali haijawaita watu Mtwara wahaini, wapuuzi na watu hatari, iwaambie watu Watanzania kodi kiasi gani imekusanywa kutoka mgodi huu katika kipindi cha miaka 14. Mpaka mwaka 2008, kwa mujibu wa Taarifa ya Kamati ya Bomani, kampuni hii ilikuwa imelipa mrahaba wa dola 11 milioni na kodi nyingine dola 16 milioni. Serikali itwambie ilipofika Disemba 2012 kodi kiasi imekusanywa kutoka kampuni hii?

Pia watu wa Mtwara na Lindi wameona historia ya bomba la Songosongo. Hata kodi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa (0.3%) ilikuwa inalipwa Halmashauri ya Manispaa Ilala na kampuni ya Pan Africa Energy. Ilichukua juhudi za mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu kuingilia kati ndio kodi ikaanza kulipwa Kilwa ambapo uzalishaji unafanyika. Watu wa Mtwara ni werevu, wanajua wafanyalo. Wanataka utajiri wa nchi unufaishe nchi kwa kuanzia kule utajiri ulipo. Kuna dhambi gani?

Uwajibikaji katika uvunaji wa Rasilimali ya Gesi ndio chanzo cha maandamano ya watu wa Mtwara. Serikali isikimbilie kulaumu wanasiasa kwamba ndio wamechochea maandamano haya. Haya ni maandamno ya wananchi wakitaka Serikali yao iwajibike kwao. Serikali ithubutu kufanya ubabe wa kujenga bomba la gesi bila ridhaa ya Wananchi wa Lindi na Mtwara. Wananchi wanapohitaji uwajibikaji ni wajibu wa Serikali kuwajibika kwao ni sio kuwaita wahaini, wachochezi, watu hatari, wapuuzi. Watu wa Mtwara wamechangia maendeleo ya Taifa letu kwa jasho na damu. Serikali ina wajibu wa kuwasikiliza, kuwaelimisha na kupata mwafaka. Kauli ya Serikali imewatukana watu wa Mtwara na Lindi. Hawatakubali kudhalilishwa. Hawatakubali historia yao kufutwa. Hawatakubali waendelee kubaki nyuma kimaendeleo. Serikali ifikirie tena.

Tuesday, November 20, 2012

Mabilioni ya Uswisi – Tusigeuzwe Mazezeta

Mabilioni ya Uswisi – Tusigeuzwe Mazezeta

by Mh. Zitto Kabwe


Jumanne tarehe 20 Novemba 2012, baadhi ya vyombo vya habari vimebeba habari zinazohusu matamshi ya Waziri wa Utawala Bora ndugu George Mkuchika kuhusu sakata ya mabilioni ya Uswisi. Waziri amesema kwamba Serikali ya Uswisi inataka majina ya Watanzania walioficha fedha huko ndio waweze kusaidia uchunguzi. Habari kama Hiyo, yenye maudhui na malengo hayo hayo iliandikwa na Gazeti la The Guardian on Sunday la tarehe 18 Novemba 2012.
Nimeona ni vema nitoe kauli yangu rasmi kuhusu suala hili. Lengo ni kuweka rekodi sawa juu ya Azimio la Bunge na kwamba Serikali inapaswa kutekeleza Azimio na sio kutoa kauli tata za kukata tamaa.

Moja, Suala hili japo sio jipya lakini limeandikwa kama ni jambo jipya. Suala la Serikali ya Uswisi kutaka majina lilisemwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati akichangia hoja binafsi niliyowasilisha Bungeni na pia wakati akileta maombi yake ya kuiondoa hoja ambayo yalikataliwa na Bunge. Kama sio sababu mpya ni kwanini imeibuka upya na kwa kasi? Ni wazi Serikali inajihami kwa kuona kuwa itashindwa kutekeleza azimio la Bunge. Watanzania wasikubali propaganda hii ya Serikali. Bunge limeagiza Serikali kufanya uchunguzi kwa kutumia njia za kiserikali au wachunguzi binafsi wa kimataifa. Kwa nini Serikali inaanza kubwabwaja ilhali wala haijaanza kazi hiyo? Serikali inajaribu kuficha nini? Kwa nini baada ya wiki iliyopita Benki Kuu kufanya uchunguzi kwenye Mabenki ya Biashara jijini Dar es Salaam na namna fedha zimekuwa zikipelekwa nje (international transfers), leo Serikali inakuja na kauli za kukakata tamaa? Kunani?

Pili, Watanzania wajue kwamba Taifa la Swiss limejengwa na linajengwa kwa fedha hizi za wizi ambazo watu mbalimbali duniani wanaiba au kukwepa kodi kwenye nchi zao na kuzificha huko. Serikali ya Swiss hata siku moja haiwezi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika suala kama hili. Ndio maana Azimio la Bunge linataka wachunguzi binafsi ambao hawatahitaji ushirikiano wa Serikali ya Swiss. Nawakumbusha kwamba mwaka 1997 mara baada ya Joseph Desire Mobutu kuangushwa na Rais Joseph Kabila kule Kongo - Kinshasa, Serikali ya Swiss iliitaka Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuonyesha ushahidi kuwa hela hizo za Mobutu zilikuwa zimepatikana kwa njia haramu! Waswiss walitaka Kabila awakakikishie kuwa fedha zile zaidi ya dola bilioni nane za Kimarekani Mobutu hakuzipata kihalali ndio waweze kuzirejesha. Zaire ilikadiriwa kuwa na zaidi ya dola za Kimarekani bilioni thelathini katika Mabenki ya nje ya nchi hiyo. Majibu ya aina aina hii ni majibu ‘standard’ ambayo kila nchi inapewa. Hata Marekani ilipokuwa inafuatilia wakwepa kodi wao walijibiwa hivi hivi. Hatimaye Serikali ya Marekani ikaamua kununua taarifa hizo na kuwakamata wakwepaji kodi wao walioficha fedha Uswisi. Hao ndio Waswiss ambao Serikali ya Tanzania inashabikia majibu yao. Bila Aibu Mawaziri wetu wanayanukuu majibu ya Waswiss kama kasuku. Tunasahau historia haraka sana. Tunakuwa kama mazezeta.

Tusiwe Taifa la mazezeta. Mabwege na mazezeta huimba kila wanachoambiwa kuimba. Sasa Serikali ya Tanzania imekuwa msemaji wa Serikali ya Swiss badala ya kuchunguza utoroshaji wa fedha haramu na kisha kutoa taarifa Bungeni. Naitaka Serikali ianze uchunguzi mara moja kama namna ilivyoelekezwa na Bunge. Suala hili sio suala la kisiasa, sasa ni Azimio la Bunge ambalo linahitaji kutekelezwa kikamilifu. Suala hili sio suala la Zitto Kabwe tena, ni suala la Bunge, ni suala la Wananchi. Wananchi hawataki uzezeta wa watu waliopewa dhamana ya kutekeleza Azimio lao. Kama hawawezi wapishe watu wenye uwezo wa kusimamia maslahi ya Watanzania kwa kuchukua hatua stahili za kuchunguza utoroshaji mkubwa wa fedha za kigeni, ukwepaji mkubwa wa kodi na ufisadi uliopelekea Watanzania kuficha mabilioni kwenye mabenki nje ya Tanzania. Hatutakaa kimya mpaka tuone mwisho kamilifu wa suala hili. Utekelezaji wa Azimio la Bunge itakuwa ni salamu tosha mafisadi na watoroshaji wa fedha haramu kwamba hawana pa kujificha na Tanzania sio Taifa la kuchezeachezea. Lazima tushinde vita hii. Anayeona hawezi kutuongoza kuishinda atupishe mapema. Hatupaswi kuwa Taifa la Mazezeta. Watanzania sio mabwege tena, Mwakyembe alipata kusema.


Kabwe Zuberi Zitto, Mb

Kigoma Kaskazini.

Tuesday, May 01, 2012

Management by Crisis at Mzumbe University: The Failure of Core Values [2]

Mzumbe University Mission Statement


Kuna nini Mzumbe University?

Nimepata kwa E-Mail:

*************************************
Comrades,


Last year in January, I wrote an article on "Management by Crisis at Mzumbe University: The Failure of Core Values". The article was centred on the "University Services Marketing" and depicted the deficiencies in the management of staff and the services so envisaged. Today, the 01st May, 2012 I am sending you an article on the same topic. However, this time mine observations have been derived with respect to the Controller and Auditor General (CAG) Audit Report 2010/2011 dated 28th March, 2012 that was tabled and discussed in House of Assembly (Dodoma, April, 2012). Mzumbe University was in the CAG Audit spotlight and where there are three audit queries and/or anomalies, namely:

1. Ghost workers payments = TZS 194.4 million for just four months;


2. Procurements outside Annual Procurement Plan [APP] = TZS 1.9 billion; and


3. Mis-information on number of staff between two departments of the University.

I therefore, as an internal cusotmer, do hereby convey my discussion, analysis and recommendations for your synthesis and reaction. My fundamental aim is to make the University (Mzumbe) the centre of academic excellence that could provide exemplary execution of the good governance principles. It is therefore our noble task in compliance with the core values - transparency, professionalism, integrity, fairness, ethical behaviour and in line with the requisites of corrupt free Tanzania in public services delivery systems.

I submit,

Bakari M Mohamed, BBA [PLM], CPSP [T], MSc (PSCM), Reg. PSP (AU 0005)

1. Lecturer in Procurement and Supply Chain Management
2. Procurement and Supply Chain Auditor
3. Procurement and Supply Chain Specialist, Consultant, Researcher and Trainer in Procurement Contracts Management
4. Doctor of Alternative Medicines [DAM] & Natural Healing Therapist

Department of Procurement and Logistics Management
Mzumbe University
Box 6
Tel (Office): + 255 23 2604381/3/4
Mobile : + 255 713 593347
MZUMBE, Tanzania.

Wednesday, September 09, 2009

Kumuiba Mke au Mume wa Mwenzako ni Ufisadi!

Na Dada Flora Wingia

Kutoka ippmedia.com

Kwa tafsiri yangu nyepesi nyepesi, ufisadi ni wizi, udanganyifu, ulaghai, ubadhirifu, umaaluni, ufedhuli, ubaradhuli na mengineyo yanayofanana na hayo. Vitendo vyote hivyo siyo tu vinafanywa na baadhi ya watu dhidi ya serikali na taasisi za umma, bali pia dhidi ya mke au mume wa mwenzako. Unabisha? Subiri nikutoholee.

Naam, mpenzi msomaji, nimeanza kuchombeza hivyo ujiandae kwa vionjo vinavyodhihirisha kirusi cha ufisadi kinavyozitafuna pia familia zetu. Kirusi hiki, ama kinabomoa nyumba zetu au kuzitia nyufa, na zaidi kinazisambaratisha kwa baba na mama, kila mmoja kufikia hatua ya kutafuta sehemu ya kujishikiza nje ya ndoa.

Kwanini hali hii inatokea? Je, ni umasikini ndani ya familia? Au ni utajiri umewakolea kiasi cha kupagawa na hivyo kutafuta maisha mbadala pembezoni? Au ni kitu gani hasa! Majibu yote haya msomaji wangu utayapata ndani ya mtiririko wa makala hii.

Hivi majuzi yupo fundi ujenzi wangu alinisimulia kisa kimoja ambacho kilinivuta kimawazo nikaona nikimwage hapa, ili pengine kirekebishe wenye mwelekeo huo. Hakifurahishi, lakini kina mafundisho muhimu ya kimaisha.

Katika simulizi yake, fundi huyu anasema kwamba yupo baba mmoja wa makamo mwenye mke na watoto wake wanne, wawili ni wasichana. Wawili wako sekondari, wengine vyuo.

Familia hii ina mji kule Mbagala wenye nyumba ya kisasa yenye eneo lenye nafasi.

Jirani na nyumba yao wakaamua kuanzisha baa na duka. Hapo huja wateja kununua na kuondoka na wengine huketi na kupata vinywaji, nyama choma.

Wazee hawa(baba na mama) wa mji huu, nao mara kwa mara huwa sehemu ya wanywaji. Pale hupata fursa ya kukutana na wezee wenzao kubadilishana mawazo. Ni wakamata maji wazuri na yakiwakolea hawasiti kuzua mitafaruku.

Unajua tena, wagidaji pombe ikiwakolea adabu na heshima huchepuka, hivyo kutoa fursa kwa ibilisi kulaghai. Simile hutoweka kwa wengine na kuanza kuongea ovyo.

Unaweza kudhani wanapofanya hivyo wanatania kumbe ni kweli toka kwenye nafsi zao zilizolegezwa na kilevi. Mfano mtu anamwambia mke wa rafiki yake eti ‘nakutamani sana’, na maneno haya anayasema mbele ya mumewe.

Je, mume mtu ataelewa kuwa ni utani? Ipo mitafaruku iliyoibuka kutokana na utani wa aina hii. Na pengine aliyetamka maneno hayo hakuwa anatania bali alimaanisha hivyo kupitia ibilisi wake wa pombe.

Kwa maelezo ya fundi huyu, wazee wa familia ninayozungumzia mara nyingi wamekuwa wakizozana wakiwa wanakunywa kwenye baa yao hiyo na zaidi ni wivu. Hofu yao ni kwamba huenda kila mmoja anao wateja anaowahusudu wanapokuja kunywa mahali hapo.

Baba anamshuku mume kuwa anao kinamama anaoonekana kutaniana nao au kuongea nao sana na huenda mmojawao ni mpenziwe wa pembeni. Na baba vivyo hivyo huhisi kuwa mama ana wazee anaochekacheka nao sana au vijana na huenda wapo anaowahusudu. Ili mradi kila mmoja anamtilia shaka mwenzake.

Chanzo cha mzozo wote huu ni uwepo wa baa hiyo karibu na nyumbani. Pengine isingekuwepo na kila mmoja angevinjari kivyake na migongano ya aina hiyo isingeonekana.

Kwa mtizamo, mama ndiye anayeonekana chakaramu zaidi na mshekumsheku anapoona wanaume, tofauti na mumewe ambaye ni mpole, mkimya ila mpepesaji mzuri wa macho anapoona kinamama au wasichana wanapitapita mbele yake wakija kupata huduma kwenye baa hiyo.

Upole na ukimya wa baba huyo, ulimzidishia mkewe jeuri kwamba hawezi kufurukuta. Hata ndugu za mume hufikiria mara mbili mbili kwenda kumtembelea ndugu yao(mume) kutokana na ukali wa mke.

Ilitokea mama huyu akamgundua mumewe akimkazia macho mwanamama mmoja. Hali hiyo ambayo ilikuwa ikijirudia mara kadhaa, ilimfanya mke ampige marufuku mwanamke yule kutokanyaga kwenye baa yao.

Hisia kuhusu mahusiana ya baba huyo na mwanamke huyo zilipelekea mkewe kumbonda mara nyingi kila wanapokolewa pombe na kutafutiana vijisababu vya kukosana. Na kila zikizuka vurumai, baba huchukua kibegi chake na kutokomea. Inaelezwa kuwa huenda kulala gesti.

Lakini kumbe halali gesti huenda kujichimbia nyumbani kwa mwanamke yule yule anayesababisha mipasuko ndani ya nyumba yao. Na mwanamke huyo baada ya kufukuzwa kwenye baa ile akaapa kutomwacha mzee huyo hadi kieleweke.

Misukosuko ambayo mume huyo alikuwa akipata kwa mkewe ilikuwa kama kichocheo cha kuzidi kumpenda mwandani huyo wa pembezoni.

Fumba na kufumbua mwandani huyo akapata mimba na kukaa sawa mtoto akazaliwa. Mtoto dume.

Taarifa zilipomfikia mama mwenye nyumba inaelezwa hadi sasa ameshikwa na bumbuwazi, na mume naye ndiyo amekuwa mbogo haoni wala hasikii.

Tena humpasulia wazi kwamba nakwenda au nimetoka kwa mke mwenzio. Naye mwandani huyo kila anakopita anatangaza ushindi kwa kumuopoa mume wa mwanamke mwenzake. Ufisadi mkubwa huu. Inauma lakini maji yakimwagika si hayazoleki?

Mpenzi msomaji, huo ndio ufisadi niliogusia tafsiri zake nyepesi nyepesi mwanzoni mwa makala haya. Ukali wakati mwingine huleta kilio. Kumbe pengine hekima ingetumika hata mpasuko uliojitokeza ndani ya familia hii usingekuweko. Hii ni kutokana na ukweli kwamba hekima ni bora kuliko kutumia nguvu. Na kwamba afadhali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima kuliko kusikiliza kelele za mfalme katika kikao cha wapumbavu.

Ufisadi mwingine unaozibomoa nyumba zetu ni huu unaofanyika kupitia simu za kiganjani. Mtu anamdoea mke au mume wa mwenzake na kisha anatumia ujumbe wa simu kumchanganya.

Wenye mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa zao wameshaonja joto la kasheshe zinazotokana na ufisadi huu. Na wenye kiherehere zaidi ni wale washikaji wa nje ya ndoa. Hao huwa wakali kuliko wenye nyumba zao. Kisa wanawaonea wivu na wanaponogewa hudiriki kubomoa nyumba zilizojengwa kwa gharama kubwa.

Anachofanya yule dowezi ni kutafuta simu ya mke wa mshikaji wake na kumtumia maneno ya kashfa kumdhihirishia kuwa mumewe anamdhibiti. Tabia hii wanayo sana wanawake.

Mwingine hupagawa na kuamua ku-forward ujumbe aliotumiwa na mume wa mwanamke mwenzake ili kumringishia kuwa hayuko peke yake na kwamba mumewe anaye kila anapomhitaji. Huu ni ufedhuli, ubedui, umaaluni, ufirauni wa hali ya juu.

Nyumba nyingi zimejikuta katika mpasuko mkubwa kutokana na mahusiano nje ya ndoa. Nyumba inachipuka ndani ya nyumba(nyumba ndogo hizi). Hata mtu akiona mwenzake akapatwa na balaa fulani, badala ya kujifunza na kuepuka, naye hujitosa kama vile shamba la majaribio. Matokeo yake naye anatumbukia.

Kwa ujumla mipasuko ndani ya familia zetu tunaisababisha sisi wenyewe. Kama baba na mama wako imara, hawatamani vya nje, hata Mungu hubariki nyumba hiyo na kuwa imara. Zipo nyumba chache za aina hii. Nyingi ni zile zinazoiga eti kama yule kafanya vile kwanini na mimi nisifanye hivyo. Kumbuka kuiga tembo ku… utapasuka msamba. Au siyo? Maisha Ndivyo yalivyo.

Niishie hapa msomaji wangu niruhusu nawe uchangie maoni, au nipe kisa ukijuacho tukijadili kwa pamoja.

Niandikie:

flora.wingia@guardian.co.tz

Wasalaam.

Friday, October 17, 2008

Jaji Mkuu Atoboa siri ya Mafisadi

SEMA USIOGOPE SEMA! Yaliyosemwa na Mheshimwa Augustino Ramadhani ni mazito!

************************************************************************
Kutoka ippmedia.Com

Jaji Mkuu apasua bomu

2008-10-17
Na Simon Mhina

Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustino Ramadhani, ametoboa siri ya ufisadi unaokua kila kukicha nchini kwamba unatokana na uchaguzi.

Ameonya kama rushwa kwenye uchaguzi haitadhibitiwa basi ufisadi ambao umekithiri kila eneo utaendelea kuitafuna nchi.

Alisema rushwa na ufisadi katika nchi ni sawa na watoto mapacha, na mama yao ni uchaguzi.

Jaji Mkuu alisema hayo jana wakati akitoa mada katika kongamano la siku mbili la kujadili rushwa katika siasa na ugharimiaji wa shughuli za kisiasa katika vyama.

Katika hutuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Msajili wa Mahakama Kuu, Ferdinand Wambali, Jaji Mkuu alisisitiza kuwa bila kudhibiti rushwa kwenye uchaguzi, uovu huo utaendelea hata katika vyombo vya kutunga sheria na vile vya utoaji haki kama mahakama.

``Ukimpitisha mgombea kwa misingi ya rushwa, ujue kiongozi huyo ndiye utakayekutana naye mbele ya safari katika kukuhudumia. Mtu aliyetokana na rushwa kwake ni vigumu kukemea rushwa hata kama imemzunguka,`` alisema.

Naye Jaji Kiongozi Mstaafu, Amir Manento, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, alisema umefika wakati sasa kumpa nafasi Rais kuteua mawaziri nje ya wabunge kwa kuwa wengi wao wamepata nafasi hizo kwa kutoa rushwa.

Alisema wabunge ambao huingia bungeni kwa njia ya rushwa, wanapoteuliwa kuwa mawaziri hutumia fursa hiyo kurudisha fadhila kwa wale waliowakopesha takrima.

Alionya kwamba hakuna mfadhili yeyote ambaye anaweza kutoa fedha zake bure bila kuwa na lengo ya kupata faida baadaye.

Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema chanzo cha rushwa, ufisadi na aina zote za ubadhirifu wa mali ya umma, ambavyo vimeshamiri nchini vinatokana na viongozi kuingia madarakani kwa njia ya rushwa.

Aidha, alisema bila kukomesha rushwa katika uchaguzi, itakuwa vigumu kukomesha ufisadi nchini, kwa vile viongozi wengi wameogolea katika rushwa hadi kufikia katika ngazi walizo nazo.

Kutokana na sababu hizo, Warioba aliona kwamba ni vigumu kwa viongozi waliochaguliwa kwa rushwa kuweza kupambana na janga hilo.

Kongamano hilo lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kushirikiana na Tasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) lilianza jana jijini Dar es Salaam na linamalizika leo.

Jaji Warioba alisema hivi sasa Tanzania inaelekea kubaya kwani rushwa inaonekana kukubalika kabisa kuwa moja ya kigezo cha kumpima mgombea.

``Hivi sasa hata kama utahubiri sera nzuri kiasi gani, hata kama mgombea anayo sifa kubwa kiasi gani, hawezi kupita bila kutoa rushwa, hizi ni dalili mbaya,``alisema.

Jaji Warioba alisema kutokana na rushwa kushamiri, hivi sasa kampeni za mgombea kuomba kuteuliwa na chama chake zimekuwa nzito kuliko kampeni za ujumla za kiserikali.

Alisema hata baada ya sheria ya takrima kufutwa bado wagombea wamekwa wakibuni mbinu mbalimbali za kugawa rushwa.

Warioba alipinga vikali madai kwamba umasikini wa wananchi ndio unasababisha rushwa kushamiri.

Alisema kwa maoni yake, rushwa inashamirishwa nchini na matajiri pamoja na viongozi ambao tayari wanazo pesa.
Alisema hata hapa nchini, miaka ya nyuma watu walikuwa masikini wa kutupwa, lakini hapakuwa na rushwa katika uchaguzi.

``Kwa hiyo si kweli kwamba umasikini ndio unasababisha rushwa katika uchaguzi, wanaosababisha rushwa na kuwafundisha watu waamini katika rushwa ni viongozi na matajiri,`` alisema.

Jaji warioba alisema kunatokea matatizo makubwa wakati wa upigaji kura, kwani imebainika kwamba baadhi ya wasimamizi, wanapokea rushwa ili `kuvizima` vyama ambavyo hawavipendi.

Alisema japokuwa wagombea huwaamini sana mawakala, lakini sio siri kwamba mawakala hao pia hutumiwa kuwahujumu baada ya kupewa rushwa.

Alionya kuwa kutunga sheria nyingi za kuzuia rushwa hakusaidii kama jamii yenyewe haijaamua kupinga suala hilo.

Vilevile, alisema daftari la kudumu la wapiga kura kimsingi sio mwarobaini wa matatizo ya uchaguzi nchini, kwani linaweza kuchezewa ili kuharibu kumbukumbu sahihi.

Kuhusu mapato ya vyama, Warioba alisema kunahitajika uwazi kwa wale wanaofadhili vyama, ili kuviepusha vyama hivyo visigeuke kuwa vibaraka.

Mathalan, alisema kuna uwezekano mkubwa wa viongozi kugeuka vibaraka wa mafisadi kama waliingia madarakani kwa kufadhiliwa kwa njia za rushwa.

Alionya kuwa si sahihi kutoa ruzuku kwa vyama vyenye wabunge pekee, na kutaka utafutwe taratibu wa kuvipatia vyama vyote ruzuku ili kuweka uwiano.

Vilevile, alisema si sahihi kuvifuta vyama vitakavyokosa kura kabisa, badala yake ameshauri viachwe kwani huenda kuna siku wananchi wakavihitaji.

``Kanu kilikuwa chama kikubwa sana, lakini sasa ni kidogo na vile vidogo sasa vimekuwa vikubwa, hivyo tusifute chama eti kwa vile ni kidogo au hakikubaliki, kuna siku kitakubalika,`` alisema.

Naye Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) akichangia katika kongamano hilo alisema kwamba ufisadi nchini unashamiri kutokana na matajiri na wanasiasa kuendeleza tabia hiyo na wala si umaskini kama wengi wanavyopotosha.

Dk. Emmanuel Makaidi, Mwenyekiti wa National Legue for Democracy (NLD) alisema kwamba serikali ilifuta sheria ya takrima ambayo ilikuwa uchochoro wa kutoa rushwa, lakini inataka kuirudisha kwa njia nyingine ambayo ni mfuko wa jimbo.

Pia alisema daftari la wapigakura linapaswa kuhakikiwa mara kwa mara kuepusha chama kimoja kutumia watendaji kufuta au kuongeza majina kwa manufaa ya chama chao.

SOURCE: Nipashe

Friday, August 15, 2008

Chacha Wangwe aibuka toka Kuzimu

Wadau, niliona hii huko World Press. Kwa kweli maneno ni mazito si mchezo:

*********************************************************************
Kutoka
http://tarishi.wordpress.com/2008/08/

Chacha Wangwe aibuka toka kuzimu

Filed under: habari ndio hiyo — tarishi @ 12:15 pm

JARIDA LA CHACHA ZAKAYO WANGWE MBUNGE WA TARIME CHADEMA

Utangulizi:

Jarida hili la Mheshimiwa Chacha Zakayo Wangwe lina sehemu tatu. Sehemu ya kwanza litaweka bayana na kufafanua sababu za mimi kuchafuliwa kisiasa na baadhai ya viongozi wa ngazi za juu za Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, na sehemu ya pili itaonyesha baadhi ya maswali ya msingi niliyopata kuuliza Bungeni na majibu yake na sehemu ya tatu itakuwa na michango mbalimbali niliyopata kuchangia kwa muda wa miezi miaka miwili na nusu.

Lengo hasa la Jarida hili ni kumwelewesha Mtanzania na hususan MWANADEMOKRASIA juu ya tuhuma zilizoelekezwa kwangu kwa lengo la kunichafua kisiasa huku viongozi wa CHADEMA wakidai kukisafisha chama jambo ambalo si kweli na ni kampeni chafu zilizoandaliwa na baadhi ya viongozi wa Chama na kuwarubuni wajumbe 31 wasiokuwa wanademokrasia na kunipaka matope ya siasa zao zisizo na hata chembe ya Demokrasia.

Nasema hivi nikijua wazi kwamba, CHADEMA kama chama kinaendeshwa kwa katiba na kwa wakati huo huo kikiwa kinaendeshwa kidikteta na kauli za NDIYO MZEE. Ninajua wazi kwamba, viongozi wa sasa wa chama changu wanatofautiana sana na viongozi wa mwanzo wakati CHADEMA ikianzishwa kwani wanatofautiana kiitikadi, kisera na hata kimtazamo. Kwa mfano, mzee Mtei alikuwa akikieneza chama hasa vijijini miaka ya 95 kwa kutumia magari chakavu na alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwashawishi wananchi na wakijua kuwa CHADEMA si chama cha mjini, na hapa ndipo mwanzo wa CHADEMA kuwa Chama Tawala kule Tarime hadi sasa. Ila katika uongozi huu wa kizazi kipya basi kila kitu kinaenda kwa kauli za “Mheshimiwa Mwenyekiti kasema” na matumizi mabaya huku ufisadi ukikitafuna chama kwa matumizi hewa na kwa kigezo kuwa eti wanajilipa madeni ya Kampeni. Nililia sana juu ya matumizi ya helkopta katika kampeni lakini nikaanza kuonekana kuwa mini ni mbaya. Binafsi sikuona sababu za Chama kutumia helkopta ilhali bado wanachama wa vijijini hawakijui chama wala sera zake huku viongozi wa wilaya na mikoa wakishindwa hata kutoa durufu (photocopy) za viepeperushi vya chama kwa kukosa ruzuku. Hii si sawa.

SEHEMU YA KWANZA

Sababu za baadhi ya Viongozi wa CHADEMA kuamua kunichafua kisiasa.

Baadhi ya Kampeni za chini chini dhidi yangu, tarehe 28 na 29 Juni 2008 katika kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Dodoma ambacho kiluhudhuriwa na wajumbe 31 kiliridhia mimi kuondolewa kwenye wadhifa niliokuwa nao ndani ya chama kama Makamu Mwenyekiti kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutuhumiwa kuwa navujisha siri za chama kwa CCM. Binafsi kwangu kama mwanasiasa wa kiwango cha juu ni pigo kubwa sana kisiasa kuchafuliwa na watu 31 tu ndani ya chama. Ninachokiamini hapa ni kwamba, kutokana na msimamo wangu wa siku nyingi hata kabla sijawa makamu mwenyekiti CHADEMA, ndiyo sababu rasmi ya kupigiwa kampeni na baadaye kura za kutokuwa na imani na mimi kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba anaandaliwa Dr. Slaa kushika nafasi hiyo. Hapa ikumbukwe kuwa Mke wa Dr. Slaa ni diwani kupitia CCM hivyo kuna uwezekano wa sera za chama zikavuja kupitia Mama huyu katika njia mbalimbali.

Ofisi ya Katibu Mkuu (Ofisi ya Slaa) ndiyo ya kwanza kunituhumu kuwa nawaingilia majukumu yao katika suala zima la matumizi mabovu ya fedha za ruzuku ya chama. Chama hupata zaidi ya milioni 60 kila mwezi. Ni fedha nyingi sana kukijenga chama kama zikipata mipango mizuri na kuachana na matumizi mabovu kama matumizi ya helkopta kwenye kampeni kama ilivyotokea kwenye chaguzi zetu pamoja na baadhiya viongozi kudai kuwa wanajilipa madeni waliokikopesha chama wakati wa kampeni za 2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za 2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za 2005, Freeman Mboe ambaye hadi sasa ni Mwenyekiti wa chama changu katika ngazi ya Taifa naye kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba kila mwezi hulipwa shilingi milioni 10 ili kufidia fedha anazodai kukikopesha chama ambazo ni zaidi ya milioni 500 katika kampeni hizo hizo na hadi sasa anaendelea kukidai chama mamilioni ya shilingi.

Mimi nilipoonyesha wasiwasi juu ya madeni haya yasiyoisha, ikaundwa tume ya kampeni za kutokuwa na imani na mimi. Binafsi sijui kama viongozi wanaojiita makini kama kina Dr. Slaa na Kabwe Zitto wangeweza kuusimamia ufisadi mkubwa kama huu ndani ya chama huku wakiwa mstari wa mbele kuwafichua mafisadi Serikalini. Au ni kawaida kuwa Mganga hajigangi? CHADEMA kuna ufisadi wa aina nyingi sana kuanzia uchapaji bendera hadi manunuzi ya vifaa vya chama!

Katika ofisi ya Vijana nako kunanuka ufisadi kwani ni vijana wachache sana ambao hupata nafasi ya kwenda nje ilhali mikoani nako kuna vijana wanaohitaji kujifunza. Ofisi hii ina watu maalumu wa kwenda kwenye Semina na Matamasha mbalimbali. Na watu hao hupangwa na John Mnyika.

Pamoja na hayo, Kurugenzi hii inayoendeshwa na John Mnyika imekuwa ikifanya hesabu za “Mbili mara Mbili toa nne”. Nakumbuka matamasha mbalimbali yaliyowahi kuratibiwa na Kurugenzi hii kwa kutumia fedha za chama yamekuwa hayana maslahi yoyote kwa chama ….labda kwake mwenyewe kwani itakumbukwa kwamba Kurugenzi ilizindua mfuko ulioitwa Tumaini jipya Septemba 16, 2007 katika hafla ya wafanyakazi vijana na akaunti ya Tumaini Jipya 01810301 NBC ilifunguliwa. Jumla ya shilingi milioni 6,176,500 zimekusanywa na shilingi milioni 6,064,300 zimetumika kwa shughuli mbalimbali za vijana ikiwemo gharama za hafla yenyewe. Hafla nyingine kama hiyo ilifanyika Arusha.

Hafla hii ilifanyika tarehe 29 Machi, 2008 The New Polygon Triangel Arusha na kuhudhuriwa na washiriki 67 mgeni rasmi akiwa Mhe. Mzee Edwin Mtei. Jumla ya shilingi milioni 2,300,700 zilikusanywa na shilingi milioni 1,885,000. Zimetumika kwa shughuli mbalimbali za vijana ikiwemo gharama za hafla yenyewe. Sasa najiuliza, kulikua na mantiki gani ya kutumia fedha za chama kiasi cha shilingi 6,064,300 na kukusanya shilingi 6,176,500/=? Ni faida ya shilingi ngapi ilipatikana kama ameamua kukiingiza chama katika kufanya biashara ya matamasha?

Jingine, tangu nimekuwa mbunge Chadema na Baadaye Makamu Mwenyekiti sijawahi kuandaliwa safari za kibunge ama za kukiwakilisha chama ilhali kuna watu wasio na uwezo kiakili, kifikra na hata nafasi za uongozi lakini waliandaliwa safari za nje. Chama kimefikia hatua ya kuwakilishwa kimataifa na watu wasio na vigezo kwa ajili ya utawala mbovu! Siandiki haya kwa kuwa nimeondolewa katika uongozi, hapana! Hizi ni harakati zangu za muda mrefu juu ya utawala bora. Tazama, wafuatao wamewahi kusafiri katika mataifa mbalimbali kwa shughuli mbalimbali kukiwakilisha chama. Mhe. Suzan Lymo (Mb. Viti maalumu) Cape Towan, Afrika Kusini kwa Mkutano wa Interparliamentary Union. Susan pia amesafiri kwenda USA kwa High Level meeting ya HIV/AIDs mwezi June, 2008. Mhe. Zitto Kabwe, (Mb) alisafiri kwenda Berlin mara mbili – Mhe. Zitto pia alisafiri kwenda Marekeani kwa wiki 3 kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani pamoja na Wabunge vijana toka dunia nzima ambako walipata nafasi ya kutembelea majimbo mbalimbali ya Marekani. Mhe. Mhonga Said (Mb – Viti maalum) alisafiri kwenda Burundi kwa Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu. Mhe. Dr. Slaa amesafiri kwenda Johannesburg, Windhoek na Manzini Swaziland kwa vikao vya Kamati na Bunge la SADC. Dr. Slaa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya InterParliamentary Cooperation Committee ya Bunge la SADC. Mhe. Maulida Komu (Mb. Viti Maalumu) alisafiri kwenda Nairobi na pia Finland. Mhe. Ndesamburo (Mb) alisafiri kwenda Australia kama Commissioner wa Bunge.

Wafuatao walisafiri kichama; Mhe. Mhonga Said (Mb – Viti Maalum), Maulida Komu (Mb – Viti Maalum), Suzan Kiwanga (Afisa Msaifizi Idara ya Uchaguzi na Kampeni) na John Mnyika Mkurugenzi wa Idara ya Vijana) walisafiri kwenda Norway na Sweden. Anthony Komu (Mkurugenzi wa Fedha na Utawala) alisafiri kwenda Norway kwa mwaliko wa Centre Party, Mhe. Balozi Ngaiza (Mjumbe wa heshma wa kamati kuu wa kuteuliwa na Mwenyekiti), John Mnyika (Mkurugenzi katika Ofisi ya Vijana), John Mrema (Afisa katika Kurugenzi ya Halmashauri na Bunge), walisafiri kwenda Windhoek Namibia kwa Mkutano wa Dua, na Mhe. Kimesera (Katibu Mtendaji wa kuteuliwa na Mwenyekiti), Suzan Lymo (Mb) Viti maalum, na John Mrema walisafiri kwenda Kampala, Uganda kwa Mkutano wa Dua.

Ndugu Regia Mtema (Afisa katika Kurugenzi ya Vijana) alisafiri kwenda Malawi kwa Mkutano wa NIMD. Mama Naomi Kaihula (Mkurugenzi katika Idara ya Wanawake) na Regia Mtema walisafiri kwenda Finland kwa mwaliko wa Shirika la Demo Finland. Johna Mrema, Msafiri Mtemelwa na Happiness Mwaipopo (Sina hakika kama ni Mwanachama) walisafiri kwenda London/Uingereza kwa mwaliko wa Conservative Party/WFD wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mhe. Benson Kigaila (Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo) alienda Zimbabwe katika uchaguzi uliofanyika 27 June, 2008 kupita Ofisi ya Msajili wa Vyama.

Suala la ukabila ni jambo ambalo halihitaji kupingwa kwani asilimia karibu 85 ya viongozi wa CHADEMA wametoka katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha pamoja na kwamba baada ya mimi kulishupalia jambo hili wameanza kubadilisha majina.

Wapo wanachama kama mimi ambao nao wakipewa nafasi za uongozi ndani ya chama hiki watafanya vizuri zaidi ya hawa na wengine ambao ni Jobless! Pengine niweke wazi hapa kuwa, mimi ni kiongozi shupavu nisiye kuwa na hata chembe ya woga katika kuteta na kusimamia haki za mwanachama wa CHADEMA tena nisiyependa siasa za kisanii. Ukweli huu ndio uliowafanya kina Mbowe, Slaa kuwa mstari wa mbele katika kupiga kampeni na baadaye kura ya kutokuwa na Imani na mimi. Binafsi naamini katika chama cha siasa mtu muhimu ni Mwanachama na si Mwenyekiti au Katibu. Hapa mimi siandiki maneneo haya kukufanya udhani kuwa nataka kuwa king’ang’anizi kwenye wadhifa niliovuliwa, la hasha bali napenda upate picha halilisi ya uendeshwaji wa Siasa ya CHADEMA na kisha uweze kugundua uhalisia wa mgogoro ulivyo. Viongozi wa CHADEMA Makao Makuu wamening’oa kutoka katika wadhifa niliokuwa nao kwa sababu zao binafsi na si sababu za chama kama chama, na wanajitahidi kuzunguka mikoani kwa siri kuendelea kunichafua kisiasa kuwa sifai. Kweli sifai kwa wafuja ruzuku ya chama, kweli sifai kwa mafisadi ndani ya chama ila nafaa kukiendesha chama katika ngazi ya taifa katika nafasi yoyote na siku zote. Nafaa kwa sababu nimefukuzwa kwa kusema ukweli hivyo nikageuka mwiba kati kati ya majipu, nikatolewa. Ndiyo, nafaa kwa sababu siko tayari kufanya kazi na watu waliozoea kukaa ofisini kama mafaili! Nafaa kwa sababu mimi ni mpambanaji, kamanda shujaa niliye tayari kuwajibishwa kwa ajili ya kuwatetea WANADEMOKRASIA hususan WANACHADEMA nchi nzima.

Kuliendesha Taifa kama Tanzania hakuhitaji siasa za kisanii, fitina, na chuki. Kinachotakiwa ni nani abadilike alete mabadiliko katika siasa ili aweze kukabidhiwa dola na alete mabadiliko. Wananchi wamechoshwa na siasa zetu ndio maana wanaziita siasa za kisanii. Wanahitaji mabadiliko. CHADEMA maana yake ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo, lakini huku wanakoelekea tayari uongozi wa Mbowe na Slaa wameiondosha Demokrasia kwa kunitoa katika wadhifa wa umakamu Mwenyekiti kwa kupiga kampeni ndogo ya wajumbe 31 tu! Tena huku wakinituhumu kuwa navujisha siri za chama!!. Dhahama kama hii siwezi kuivumilia hata kidogo na ni wazi kuwa hata wanachama wetu hawajafurahishwa na jambo hili. Mimi nilipokuwa kwenye ngazi hiyo ndipo fedha zilipoanza kupelekwa mikoani kwa viwango halali, ndipo ukarabati wa Makao Makuu ulifanyika. Niweke wazi hapa kuwa, jambo lililonifanya niandike jarida hili si kuwashawishi Freeman Mbowe na Slaa kunirudisha kwenye nafasi waliyonitoa kwa matusi, la hasha! Lengo ni kuweka wazi kwa wanachama wajue aina ya uongozi uliopo Makao Makuu ya Chama. Kama ni suala la mimi kurudi katika nafasi hiyo ni mimi mwenyewe nikiamua na kwa kutumia Demokrasia. Ikumbukwe kuwa, Freeman ndiye aliyesema kuwa hataki kufanya kazi na mimi na kutokana na UMANGIMEZA na Kauli za NDIYO MZEE akapata kuungwa mkono na wajumbe 31 tu! Baada tu ya mimi kutangazwa kuwa nimetolewa kwenye wadhifa niliokuwa nao nilipata simu nyingi sana za wanachama na hata baadhi ya watendaji Makao Makuu wakiniambia kuwa kama Mbowe hayuko tayari kufanya kazi na mimi, wao bado wananihitaji katika Uongozi Taifa. Kuna mila ya kichagga kuwa, katika eneo la kazi/biashara, ukimuona anayekusababisha ukose maslahi Fulani unatakiwa kumuondoa kwa gharama yoyote! Na hili ndilo lililojiri kwangu na mwenyekiti wangu.

Aluta Continue…………………..

Wangwe Chacha Zakayo,
Mbunge wa Tarime-CHADEMA


KAULI YANGU KWA MSOMAJI

Awali ya yote, nasikitika sana kwa maamuzi yaliyofikiwa na wajumbe 31 kule Dodoma aidha, kwa hasira, chuki au majungu na kuamua kuniondoa katika wadhifa niliokuwa nao wa Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara wakitumia kivuli cha Katiba ya Chama. Pili nimezidi kuumia zaidi pale nilipotuhumiwa kuwa eti navujisha siri za Chama kwa CCM! Niliwapa siku Arobaini (40) kuwaza kuthibitisha juu ya tuhuma hizo lakini wameshindwa hadi leo! Inamaanisha kuwa walitumia tuhuma hizo ili kunitoa kati yao ili nisiendelee kutetea ahadi za wanachama wa CHADEMA na nisiendelee kupinga ubadhirifu wa fedha za chama. Pengine kutokana na hasira, chuki na majungu hayo hayo wakaamua kuzidi kunichafualia jina katika mkutano uliofanyika Tanga kwa kunisema kuwa mimi ni mhuni. Hapa sintakuwa na huruma wala urafiki na yeyote aliye mstari wa mbele kunichafua kisiasa nitahakikisha nawafungulia mashtaka na waweze kuthibitisha tuhuma hizo. Mpendwa msomaji, pamoja na hayo ni vyema ukumbuke kuwa, uongozi wa CHADEMA Taifa umeshindwa kukieneza chama hadi vijijini. Ni kwa ajili ya majungu haya haya!.

Kimsingi, tusiposhikamana kwa sauti moja, lengo moja na kwa msimamo, ni dhahiri kuwa chama cha mapinduzi kitaendelea kushika Dola hadi Ukamilifu wa Dahari! Chama kisipokuwa madhubuti hakitaweza kushika Dola hakiwezi kuaminika na Wananchi. CHADEMA tufike mahali tugeuke, tujue tuna lengo la kuiongoza Tanzania na si vinginevyo. Badala ya kulewa katika kuwafichua mafisadi. Tumejisahau!.

Naamini kuwa, nguvu za umma ndiyo nguvu inayoweza kuleta mabadiliko ya kweli.

Naamini kuwa, katika chama chochote cha siasa, mwanachama ndiye bora kuliko Kiongozi.

Naamini kuwa msingi bora wa chama hujengwa na watu makini.

Naamini pia baada ya kusoma Jarida hili ukiwa kama mwanachama au Mwanademokrasia utaungana nami katika kupiga vita UFISADI ndani ya CHADEMA.

Tuesday, May 13, 2008

Mafisadi watajwa Bongo

Hivi kweli ni hao tu?

*********************************************************
Kutoka ippmedia.com

Mafisadi: Majina yatua ikulu

2008-05-13

Na Mwandishi wetu, Jijini

Hatimaye ile orodha ya watumishi wa Serikali wanaotuhumiwa kushiriki dili lililoiwezesha kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond kuweza kuingia mkataba wa kifisadi ulioiingiza nchi katika hasara ya mabilioni ya pesa imetua ikulu kwa ajili ya kusubiri hatua za kiutawala kuchukuliwa dhidi yao.

Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda amesema tayari Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo ameshakabidhiwa orodha ya wahusika na na kupewa maelekezo ya kuchukua hatua za kiutawala.

Amesema Bw. Luhanjo anatakiwa kuchunguza na kuwachukulia hatua watumishi wote wa Serikali wanaotuhumiwa na sakata hilo la mkataba `bomu` wa Richmond, lililozua gumzo kubwa nchini.

Akasema Katibu Mkuu Kingozi ataanza kwa kuwachukulia hatua watuhumiwa wote waliotajwa kwenye ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyochunguza mkataba wa Richmond.

Miongoni mwa watuhumiwa waliohusishwa na sakata hilo na kutakiwa kujiuzulu kutokana na kuzembea ama vinginevyo, kutokana na ripoti ya Kamati hiyo ya Bunge ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU, Bw. Edward Hosea na Mkurugenzi wa Nishati na Madini katika Wizara ya Nishati na Madini Bw. Bashir Mlindoko.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya kamati hiyo teule ya Bunge iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake Dk. Harrison Mwakyembe, kigogo mwingine anayepaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ni Katibu Mkuu wa makosa yao au vinginevyo, kadiri sheria zitakavyoruhusu. ``Maelekezo yote amepewa Katibu Mkuu, suala hili sasa linafikia mwisho kwa kuwa anaandaa hatua za kuwachukulia, kama ni Wizara ya Nishati na Madini Bw. Arthur Mwakapugi.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu Pinda, watuhumiwa hao wanaweza kutimuliwa kazini au kupunguziwa madaraka, kutokana na uzito wakuwafukuza kazi au kuwateremsha vyeo, well and good,`` akasema Bw. Pinda. Waziri Mkuu amesema hivi sasa Serikali haikubali kuchafuliwa na hivyo kila anayebainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi anawajibishwa.

SOURCE: Alasiri