Showing posts with label Ndoa. Show all posts
Showing posts with label Ndoa. Show all posts

Wednesday, October 19, 2016

Mbinu ya Kutafuta Makaratasi ya Kukaa Marekani

Siku hizi ni ruksa Kwa wasenge na mashoga kufunga ndoa. Ona huyo kijana wa Nigeria kamuoa dume wa kizungu anayejiona kama ni mwanamke. Tena hao gays wanasema wanaume wa Africa maana wanasema wamejaliwa vyombo mirefu na migumu.

Saturday, November 07, 2015

Kizee wa Miaka 72 Aolewa na Kijana wa Miaka 22


Wadau, kijana wa miaka 22 kutoka Dominican Republic, amemwoa bi kizee tajiri wa kiMarekani mwenye miaka 72.  Ni mapenzi au.... labda kizee anapenda ngono anayopata kutoka kwa huyo kijana, na huyo kijana anataka hela ya huyo bi kizee na pia atapata makaratasi ya kukaa Marekani.  Haya tuwatakie maisha mema ya ndoa.

Sunday, June 15, 2014

Misukosuko ya Flora Mbasha

Flora Mbasha na Mume Wakewakiwa na furaha kabla ya Skendeli

Kutoka VIJIMAMBO BLOG:

Mpasuko wa ndoa ya wasanii wa nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha na mkewe Florah umewagawa wachungaji wa makanisa mbalimbali nchini baada ya kibao kumgeukia Flora kwamba ndiye anadaiwa kusuka mpango wa kumwangamiza mumewe ili afungwe kwa kosa la ubakaji…..
Wakizungumza na wanahabari wetu kwa nyakati tofauti, wachungaji hao walisema endapo itabainika ni kweli Flora ameshiriki kumsaliti mumewe kwa kutembea na mmoja wa wachungaji maarufu nchini hapatakuwa na haja ya kumwalika kwenye huduma zao kwani hawawezi kuhudumiwa na mwimbaji mzinzi.
Mchungaji Ambonile Mwakipesye na Amani Joseph wa makanisa ya Tanzania Assemblies of God ( TAG) walisema kuwa kama kulikuwa na matatizo kwenye ndoa yao walipaswa kuwaona watumishi wa Mungu na kusuluhisha badala ya kutengenezeana mitego na kuingizana majaribuni kama inavyodaiwa kutokea kwa Mbasha….
Wakati wachungaji hao wakisema hivyo, mchungaji Thomas Methew yeye alisema kuwa ukweli wa jambo hilo wanaujua wanandoa wenyewe kwani mpaka sasa hakuna anayelijua tatizo kubwa mpaka wakafikia hatua ya kutengana.
 
**********************
 Kutoka Jamii Forum
 
SIKU chache baada ya tuhuma za ubakaji na mzozo wa familia ya mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha na mumewe, Emanuel Mbasha, mambo mengine yameibuka.



Mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha

Yaliyoibuka safari hii ni taarifa kwamba, juzikati, Flora alivamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake, Tabata Kimanga jijiini Dar dakika chache baada ya yeye kuingia na gari akitokea mafichoni anakoishi kwa sasa.



Kwa mujibu wa chanzo, siku ya tukio ilikuwa saa 9.15 alasiri ambapo Flora aliingia nyumbani kwake na kufunguliwa geti kubwa kisha kuingiza gari ndani na geti kufungwa tena.

Flora aliingia na gari akitokea hotelini anakoishi kwa sasa. Alikuwa ameshaingia na geti likafungwa. Ghafla, watu wakafika na kugonga geti hilo kwa nguvu huku wakisema watalibomoa geti kama wenyeji hao hawatafungua,” kilisema chanzo.



Mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha akiwa na mumewe, Emanuel Mbasha,

Chanzo kikazidi kudai kwamba, ilibidi Flora apige simu polisi ili wafike kumuokoa yeye na familia yake.

“Polisi wawili walifika haraka sana wakiwa na bunduki na kukuta wale watu wamekimbia maana walimsikia Flora akiongea na polisi kuomba msaada.


“Lakini polisi wenyewe ilibidi watumie nguvu kubwa kugonga geti na kujitambulisha ndipo akatokea Flora na kuchungulia nje kupitia dirisha dogo. Alipowaona polisi akafungua mlango,” kilisema chanzo hicho.

Akihojiwa na polisi hao, Flora alisema watu hao walikimbia na hakuwajua kwa sura wala hawakujitambulisha ni akina nani.


Alizungumza na gazeti hili baada ya tukio, Flora alisema: “Unajua kwa sasa nina hofu sana na nilihisi wale watu walikuwa wakinifuatilia kwa karibu kila sehemu, sasa naogopa kuendelea kuishi hapa, wanaweza kurudi na sijui lengo lao.”


Hata hivyo, baada ya askari hao kuondoka katika eneo hilo, Flora naye aliingia kwenye gari lake akiwa na mdogo wake na kuondoka.

Mume wa Flora, Mbasha naye yupo mafichoni baada ya kudaiwa kumbaka binti wa miaka 17 ndani ya nyumba yao huku utata ukitawala kuhusu ukweli wa tukio hilo ambalo limeigawa jamii.

Saturday, September 08, 2012

Wazazi Wangu Washerekea Miaka Hamsini ya Ndoa

Wadau, napenda kuwafahamisha kuwa wazazi wangu, Dr. Aleck na Mrs. Rita Che-Mponda wamesherekea miaka hamsini ya ndoa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam. Ndoa yao ilibarikiwa katka kanisa la Anglikana St. Albans, Dar es Salaam. Walifunga ndoa mwaka 1961, baba akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Howard. Mama alikuwa amemaliza masomo yake ya unesi.

Mungu azidi kuwabariki.

Dr. & Mrs. Aleck Che-Mponda 
Misa ya Kuwabarika St. Albsans




Wazee wakiwa na baadhi ya ndugu


Monday, July 16, 2012

Dawa ya Kuzuia Maambukizi ya UKIMWI Yapatikana!

Hatimaye kuna dawa ya kuzuia maambukizi ya UKIMWI.  Hii dawa itafiaidi wasiowathirika tayari.  Ina maana kuwa kama mtu anataka kufanya mapenzi na muathirika akimeza hiyo dawa haatambukizwa ugonjwa!  Vita dhidi ya UKIMWI unaendelea lakini, tiba bado haijapatikana. Ila kwa sasa kuna dawa za kurefusha maisha na wenye virusi vya UKIMWI wanaweza kuishi maisha ya kawaida.

**************************************************************
KUTOKA CNN.COM

FDA approves Truvada for prevention of HIV/AIDS


Adults who do not have HIV but are at risk of getting the disease will now be able to take a drug to reduce their chance of getting infected. For the first time, the U.S. Food and Drug Administration approved a drug for this use on Monday.

The drug is Truvada, an antiretroviral medication made by Gilead Sciences, Inc., which was already approved by the FDA in 2004 to help control HIV infection.

Truvada is a combination of two HIV medications - emtricitabine (Emtriva) and tenofovir (Viread) - into one pill that is taken once a day. As a treatment for HIV, it is always used in combination with other HIV drugs.

Recent studies showed pre-exposure prophylaxis or PrEP can reduce transmission of the virus significantly–up to 96% - when uninfected partners of people infected with HIV took Truvada.

Dr. Debra Birnkrant, M.D., director of the Division of Antiviral Products, Center for Drug Evaluation and Research at the FDA stressed Truvada alone should not be used to prevent HIV infection. It should be used in combination with other safe sex practices.

“Practicing safer sex and good health practices must be part of the treatment," Birnkrant said. “We will be putting a box warning to let those using Truvada know that it is part of the therapy with combination of safer sex practices, and that doing this, will reduce the risk of the development of AIDS/HIV.”

Dr. Anthony Fauci, director of the National Institute for Allergy and Infectious Diseases at the National Insitutes of Health, agrees.

“The approval of Truvada to prevent HIV infection in uninfected individuals who are at high risk of sexually acquired HIV infection is a signficant development, providing an important addition to our toolkit of HIV prevention interventions,” Fauci says. “However, it is critical to stress that Truvada as ‘pre-exposure prophylaxis’ should not be considered a stand-alone method, but should be used in conjunction with other proven HIV prevention stratgies such as condom use, risk-reduction counseling, and frequent HIV testing.”


Birnkrant says she hopes the right messages will get out, and that Truvada is used properly. "We have the box warning that a negative HIV test must be reported before Truvada is prescribed," she said.

According to Gilead, Truvada the most-prescribed antiretroviral in the United States. “Today’s decision is the culmination of almost 20 years of research involving investigators, academic and medical institutions, funding agencies and nearly 20,000 trial participants around the world, and Gilead is proud to have been a partner in this effort,” said Norbert Bischofberger, Executive Vice President, Research and Development and Chief Scientific Officer, Gilead Sciences.

Dr. Robert Grant, the lead investigator of the iPrEx trial at the University of California San Francisco who looked at Truvada as a prevention treatment among high-risk men who have sex with men (MSM), says the approval is a major milestone in the 30-year fight against AIDS. “The use of PrEP alongside routine HIV testing gives us a tremendous opportunity to reduce the rate of new HIV infections in this country and around the world.”

At the University of Washington another PrEP study proved very successful in reducing infection rates in couples where one partner is infected and the other is not (called serodiscordant).

“The data clearly demonstrate that Truvada as pre-exposure prophylaxis is effective at reducing the risk of HIV infection acquired through sexual exposure,” said Dr. Connie Celum, Professor of Global Health and Medicine at the University of Washington and lead investigator of the Partners PrEP trial. “It is exciting to consider the potential impact of this new HIV prevention tool, which could contribute to significantly reducing new HIV infections as part of a combination HIV prevention strategy. Although the implementation of PrEP will bring challenges, they can be anticipated and systems developed to address these challenges."

But the AIDS Healthcare Foundation, the nation's largest HIV/AIDS group, blasted the FDA's decision. "The FDA’s approval of Gilead’s Truvada as a form of HIV prevention today, without any requirement for HIV testing is completely reckless and a move that will ultimately set back years of HIV prevention efforts,” said Michael Weinstein, AHF’s President.

“From the beginning, we believe there was a rush to judgment by government officials and others in favor of such approval despite decidedly mixed studies offered in support. And while the FDA recommends a negative HIV test prior to use of Truvada as PrEP and states that use by people with an ‘…unknown or HIV positive status…’ is ‘contraindicated,’ it in no way actually requires HIV-testing in any manner-just strengthening of the ‘Boxed Warning’ on Gilead’s packaging. The FDA’s move today is negligence bordering the equivalence of malpractice which will sadly result in new infections, drug resistance and serious side effects among many, many people."

Tuesday, July 10, 2012

Mbunge Frank ndiye wa Kwanza Kufunga Ndoa ya Kishoga!

Mbunge wa Massachusetts, Barney Frank amekuwa mbunge wa kwanza kufunga ndoa ya kishoga Marekani. Frank, mbunge wetu mpendwa wa miaka mingi hakuficha ushoga wake.  Aliwahi kuwa na skandali ya kutembea na malaya wa kiume na pia kutembea ma kijana wa kiume ambaye alikuwa intern Bungeni.
Mbunge wa Massachusetts Barney Frank (kulia) na mke wake Jim Ready

 
Congressman Barney Frank (D-MA) (72) married  longtime partner, Jim Ready (43) this past weekend . The couple got hitched Saturday at the Newton Marriott in a ceremony officiated by Governor Deval Patrick , and attended by Representatives Nancy Pelosi , Dennis Kucinich , and Steny Hoyer , and Senator John Kerry .

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Kwa picha zaidi ya arusi yao BOFYA HAPA:

Monday, February 06, 2012

Aolewa na Wanaume Wawili huko Katavi!

Sijui ilitoka kwenye gazeti gani. Lakini kwa kweli nimependa ushujaa wa huyo Mama Kaela!

********************************************************
MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME WAWILI


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani hapa, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zililifikia gazeti hili na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Ndugu wa Arcado wao wanalaani kitendo cha ndugu yao kuolewa na mama huyo, wakidai kuwa walishamshauri na kumuahidi kuwa endapo ataachana na mama huyo watamwozesha mwanamke mwingine, lakini yeye Arcado, amedai kuwa yuko tayari kufa, lakini si kuachana na mama huyo, kwani ndiye ubavu wake wa maisha.

“Sasa tumebaki tunamwangalia tu huyu ndugu yetu Arcado, tumemshauri, lakini mkaidi, hatusikilizi. Basi nasi hatuna la kufanya zaidi ya kumwangalia,“ alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Arcado. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Florence Katobasho, alikiri kuwa mwanamke huyo anaishi kinyumba na wanaume wawili na wanaishi kwa amani kwani hajawahi kufikishiwa malalamiko yoyote kuhusu wanandoa hao.

“Ni ukweli usiopingika, kwamba Mama Kaela anaishi na wanaume hao wawili … lakini kwa kuwa sijafikishiwa malalamiko yoyote kuhusu maisha ya wanandoa hao, mimi kama kiongozi hapa sina la kufanya na siwezi kuwafukuza, kwa kweli wanaishi kwa amani, mengine ni yao,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji

SOMA   ZAIDI http://www.fotobaraza.me/profiles/blogs/mwanamke-aolewa-na-wanaume#ixzz1lVfLAlP4

Monday, October 31, 2011

Arusi ya Musau Kabongo na Orrin Kennedy Boston

Wadau, napenda kwajulisha kuwa ya binti tuliyemfanyia Kitchen Party mwezi uliopita ameolewa jana, jumapili 30.10.11 hapa Boston. Binti Musau Kabongo ameolewa na kijana Orrin Kennedy ambaye asili yake ni kisiwa cha Trinidad.  Musau ni mtoto wa Dada Margaret Kabula kutoka Mwanza lakini anakaa Boston sasa. Baba Musau anatoka Congo. Arusi ilifanyika kwenye kanisa la Seventh Day Dorchester, MA na Reception ilifanyika DAV Function Hall Braintree, MA.
Mimi na Wana Arusi Musau na Orrin


Musau na Orrin Kabla ya Kukata Keki

Dada Doreen Kutoka Rhode Island Akisimamia Chakula

Bwana Arusi Akitafuta Garter kwenye mguu wa Bibi Arusi
 
Kama Kawaida Akina Mama waTanzania walipika Chakula Kingi

Orrin na Musau Wakikata Keki

Wageni Wakijipatia Mlo
Mama wa Bibi Arusi, Margaret Kabula (amesimama) na Vicky Mareaelle na mume wake

Mimi, wana arusi na kulia kabisa ni Rafiki yangu na msanii mwenzangu Charles Jackson Aka. Mzee Matumbi

Monday, October 03, 2011

Sinema 'Historia ya Khanga" Cheki Mimi na Kaka Michuzi!

MaStaa wa Bongowood 1991 Michuzi & Chemi


Kabla ya Kanumba na Ray kulikuwa na Chemi na Michuzi!

Wadau, kwenye mwaka 1992 nilishiriki katika sinema ya TAMWA, "The History of Khanga".  Hebu itizame, Utaniona mimi na Kaka Michuzi, "Tunajiandaa kulala"

Mwongozaji alikuwa Dada Fatma Alloo. Pia kuna mahojiano na marehemu Bibi Titi Mohamed.

Sinema sasa iko YOU TUBE kwa hisana ya Dada Fatma na Kaka Michuzi:

http://www.youtube.com/watch?v=jAuhAB0HeeA&feature=player_embedded

Friday, May 06, 2011

Bwana Arusi ana Miaka 100, Bibi Arusi Miaka 90!

Africa ukifika miaka 40, basi wewe mzee! Ukifikisha 70 basi unstahili kutotelewa nje na kuanikwa juani. Huna thamani tena. Mapenzi, ndo usahau kabisa, unabakia kukumbuka katika ndoto zako ujana wako!

Hapa Marekani, wazee Forrest Lunsway (100) na Bi Rose Pollard (90), wamefunga ndoa. Hebu cheki nyuso zao za furaha, mapenzi motomoto! Inasemekana wamevunja rekodi ya umri wa wafunga ndoa. Doh! Wamejuana karibu miaka 28. wote wanakaa kwenye nyumba ya wazee. Nawatakia maisha mema ya ndoa. Kumbe hata ukiwa na miaka bado wamo! Ila Zaeni matunda mema haifia kusemwa hapa.
***************************************************************************



(pichani wanaarusi Forrest (100) na Rose (93))


Kutoka YAHOO.COM

For some people, it's never too late for love.

That's certainly the case for Forrest Lunsway and Rose Pollard, an Orange County, Calif. couple who were married this March 19, Forrest's 100th birthday. With a combined age of 193--Rose is a spring chicken--they're believed to be the world's oldest newlyweds.

A spokesman for the Guinness Book of World Records said they had been informed of the wedding and are set to verify it as a record. For 27 years, Forrest smoked a pack of cigarettes a day, and he still drinks the odd glass of wine or whiskey and 7-Up, he said in a recent interview with the The Daily. He attributes his longevity to never having had a desk job: He spent his youth trapping animals and selling their fur in Kansas before moving to California, where he worked as a pipe welder.

You can watch a video of them here.

Both Forrest and Rose had been married before, but were single when they met back in 1983 at a senior's dance. Though they soon started dating, wedding bells seemed unlikely.

'I told him up front I had no intention of getting married," Rose said. "But then one day he asked me 'how come we never got married? and I said 'because you never asked me.'"

''So he got down on one knee and said, 'Well I'm asking you now, just set the date.' I told him, 'I'll marry you on your 100th birthday.' And I did."

And being on the older side, the couple also has some wisdom to share on how to make a marriage work. Rose, 93, told The Daily: 'Take your time and get to know one another. Get to know if you like all the things that person stands for. ... Be forgiving and patient and say I love you once in a while."

Rose also told The Daily that their advanced age means that she and Forrest don't have many of the anxieties that can be a challenge for other newlyweds. "That's one of the things we can forget about--time. Because time doesn't mean that much."

And it's time well spent together: They both love ballroom dancing, and they want to kayak in Alaska and walk the coast of California.

"We've got many happy years left as I intend to stick around until I'm at least 110," Forrest said. "You've got to use it or lose it."
(The Daily)

Thursday, April 28, 2011

Mama Bishanga Ameremeta!!!

Bwana na Bibi Marolen baada ya kufunga ndoaKwa mila ya waMakua kwa wanawake hulala chini na bibi arusi kupita juu yao mpaka kwenye kiti atapokaa.
Familia ya Hatia, familia ya Mrope, na familia ya Kamota wakipiga picha ya pamoja na wanaarusi



Wadau, Mama Bishanga jina halisi Christina Innocent Hatia amefunga ndoa hivi karibuni huko Dar es Salaam, Tanzania. Bwana harusi ni Mr. Marolen kutoka Afrika Kusini.

Arusi ilifanyika siku ya tarahe 5 Machi, 2011 katika knaisa la St. Peters Oyster Bay. Reception ilifanyika Peacock Hotel.

Nawatakia maisha mema ya ndoa.

Saturday, April 17, 2010

Ndoa ya Makaratasi Yamponza Mcheza Sinema

Mcheza sinema Fernanda Romero anashikiliwa na polisi wa uhamiaji huko California baada ya kugundulika kuwa na ndoa ya makaratasi. Mume wake feki amekamatwa pia.

Bi Romero anatoka Mexico. Alilmlipa Kent Ross afunge ndoa naye. Hawajawahi kukaa pamoja, Baada ya ndoa hiyo ya makaratasi, Bi Romero aliaanza na uhusiano na dume mwingine, Markus Klinko. Walivyoaachana na Klinko ndo kaenda kusema huko uhamiaji kuwa Bi Romero alifunga ndoa ya makaratasi na Ross. Jamani, ni wivu, uchungu au shetani iliyompeleka kwa polisi wa uhamiaji.

Bi Romero na Ross wako hatarini kufungwa miaka mitano!

***********************************************************************

LOS ANGELES (AP) - Mexican-born actress Fernanda Romero has had bit parts in such movies as the horror film "Drag Me to Hell," but federal prosecutors say her biggest act was pretending to be a bride.

The 28-year-old actress and husband were arrested Friday at their separate Los Angeles homes and charged with marriage fraud, the U.S. attorney's office said. They contend Romero paid Kent Ross, 28, to marry her in 2005 so that she could become a U.S. resident.

Authorities said the two never lived together and Romero, whose full name is Maria Fernanda Romero Martinez, submitted phony documents with her residency application.

An investigation began after Romero's ex-boyfriend, fashion photographer Markus Klinko, told immigration authorities her marriage was a sham. The couple started dating after Romero and Ross were married.

If convicted, Romero and Ross could be sentenced to up to five years in federal prison.
Romero has had roles in several small films and is moderately well known in Mexico, where she appeared in the TV Azteca soap "Eternamente Tuya." She has also appeared on the Spanish-language channels Univision and Telemundo in the shows "Control" and "La Ley del Silencio," respectively.

According to her website, she has appeared in television and print ads for several U.S. companies, as well as a music video. She moved to Los Angeles when she was 18 to study fashion design, according to her site.

Messages to her publicist were not returned Friday.

A phone message left for Ross' attorney, Mike Shannon, also was not returned.
Romero and Ross were both released after initial court appearances Friday. However, a judge restricted Romero's travel to certain Southern California counties and said she could not leave the country.

Special Assistant U.S. Attorney James M. Left, said immigration officials began investigating in 2007 after Klinko mentioned the marriage during a lawsuit he filed in New York.
Left says a marriage ceremony was performed on June 12, 2005, but the couple never lived together.

He said immigration marriage fraud cases may be brought in either criminal or immigration courts. The case against Romero was pursued because of "the overwhelming amount of evidence" and repeated misstatements by the actress, Left said.

"Immigration benefit fraud is a serious crime," said Miguel Unzueta, an Immigration and Customs Enforcement special agent in charge in Los Angeles. "Not only does it potentially rob deserving immigrants of benefits they rightfully deserve, it also undermines the integrity of our nation's legal immigration system."

Friday, April 16, 2010

Mume Mzuri!


A guy woke up in the morning with a terrible hangover. Next to the bed was a couple of aspirins, a glass of water, and a note from his wife ? ?Honey, there's a hot breakfast waiting for you in the kitchen. Love, your wife?. He looks around the room and sees that it is in perfect order, spotlessly clean. So is the rest of the house.

He stumbles into the bathroom and notices a huge black eye. After shaving, he goes to the kitchen, and sees that the hall mirror is broken too.

His son is in the kitchen and as he's eating his huge breakfast the guy asks the son what all this is about.

Well, last night you came home drunk off your ass, stumbled into the mirror and hit your head on the doorknob. Mom helped you to bed, and as she's trying to get your pants off you kicked her away and said get off me lady, I'm married?.

If you really enjoyed this story please forward to friend. Or reply and let us know. You might make someone's day!

Tuesday, January 05, 2010

Mume Anapokimbia Mke Mjini Na Kuanza Maskani Mapya Kijijini!

SEMA DA FLORA WINGIA! SEMA!!!!!

************************************
Na Flora Wingia

Heri ya Mwaka Mpya 2010 mpenzi msomaji wangu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuvusha mwaka huu. Naamini sote tumejipanga vema katika kufanikisha malengo mapya kwa mwaka mpya.

Wakati wengine wamepania kuboresha maisha ya familia zao, wengine wameamua kumeguka na kuanza maisha mapya kwingineko. Je, unajua ni kwanini? Hebu sikia kituko hiki cha kufunga mwaka 2009.

Ukiona mwanaume anaukimbia mji wake na kwenda kutafuta maskani mapya, ujue maji yamemfika shingoni. Katika hali ya kawaida ya maisha, mwanaume ndiye anayemkaribisha mwanamke nyumbani kwake na wakati mwingine huishia kumuoa.

Ukiona mwanamke anayemtunza mwanaume nyumbani kwake, huwa inaelezwa kuwa ‘mwanaume huyo kaolewa’. Lakini si unajua tena kupenda wakati mwingine mtu huwa zuzu au wengine huita zezeta. Hata akikemewa na wenzake yeye hujifanya hamnazo na kujikausha kwani anajua nini anachofaidi pale.

Pengine yeye ni kula kulala. Kila kitu anagharimia mke kuanzia chakula, mavazi na kadhalika. Mwanaume anayempata mwanamke wa aina hiyo, kwanini ajivunge?

Tukiachana na hayo, yupo mwanaume anayeoa mwanamke iwe ni kwa gharama kubwa au za kawaida, lakini baadaye mke huyo anamnyanyasa kiasi cha kumfanya auhame mji huo na kutamani mji mwingine. Hebu sikia kituko hiki cha funga mwaka.

Yuko baba mmoja nilikutanishwa naye hivi majuzi ambaye amelikimbia jiji la Dar es Salaam na kuhamia kijijini mkoa wa Pwani kutokana na manyanyaso anayopata toka kwa mkewe.

Baba huyu mwenye watoto wawili na mwanamama huyo, ameapa kumwachia mkewe kila kitu hapa jijini, na kisha yeye kuhamia kijijini kuanza maisha mapya mwaka huu mpya.

Baba huyu amenifurahisha sana. Wenzake wanahama vijijini kuja mijini lakini yeye anaamua kurejea maisha ya kijijini kutokana na suluba toka kwa mkewe.

Baba huyu anasema; “Heri kuishi peke yangu eneo la kijijini kuliko kuishi na mwanamke mwenye kero kama mke wangu. Nilimpenda mwenyewe, lakini sikujua kama angenifanyia yale niliyobainisha kwake.

“Mwanamke hataki kufanya kazi yoyote, yeye ni kwenda saluni, kukaa na kujipodoa tu. Nina mifugo, ng’ombe wawili wa maziwa, nguruwe na kuku wa kienyeji. Kutokana na mama huyo kutoonyesha nia ya kujishughulisha, nimeweka wafanyakazi wa kuhudumia mifugo hiyo.

“Akiamua hutoa nguruwe na kuuza na ninapomuuliza anakuja juu na kudai eti ni kwa matumizi ya nyumbani. Hata hivyo, kila siku lazima niache hela ya chakula mezani. Nikirudi nyumbani lazima aninuse eti kama nanukia marashi ya wanawake.

Wakati mwingine tunapopumzika hataki nimguse…hugeukia ukutani. Vituko hivi na vingine vinaninyima raha vibaya sana. Hadi najiuliza ni mwanamke gani huyu?Au anaye mwingine ampendaye?

“Nilimchangua mwenyewe, nikamuoa mwenyewe, lakini sasa nimefikia mwisho sina budi kumtosa. Sitamfukuza, lakini nitamwachia kila kitu, nyumba, mifugo na vitu vyote vilivyo mzunguka. Watoto nitapeleka shule za bweni. Ila mimi nakwenda kuanza maisha mapya”, anasema baba huyu.

Nilipomuuliza kama uamuzi huo amewajulisha wazee alisema; “Nilishaitisha kikao cha pande zote mbili kulalamika vituko vya mke huyu. Napo nilieleza msimamo wangu wa kutengana naye na kumwachia kila kitu. Ingawa hakukubaliana na hilo lakini niliungwa mkono na wajumbe wengi kwamba kwa kuwa hataki kujirekebisha, hakuna jinsi.

Mpenzi msomaji, kwa maelezo ya baba huyu, tayari ameshapata eneo katika kijiji kimoja mkoani Pwani ambako atajenga makao yake mapya na atajikita kwenye Kilimo Kwanza kwani anazo ekari 15 za ardhi. Hataki wala mwanamke wake huyu ajue huko kujiepusha na bughudha zake.
Ama kweli ‘mwenye bahati habahatishi. Mwanamke anapata mume mchakarikaji, lakini yeye anabweteka. Wapo wanaotafuta bahati ya aina hiyo bila mafanikio.

Nijuavyo mimi, mwanaume ni nguzo ya nyumba. Anapoondoka iwe ni kwa mfarakano au kwa kifo, hakika maisha katika nyumba husika huyumba na wakati mwingine hubomoka kabisa.
Mama yule anaonyesha jeuri ile kwa kuwa anamuona mumewe karibu, lakini atakapotokomea kijijini alikopania, mwanamama yule ambaye amekuwa mbwete, hataki kujishughulisha na miradi ya pale nyumbani, atajikuta naye pia akihangaika kama hayawani.

Ninachokiona kwa mwanamke huyu ni majuto mjukuu. Anachoshindwa kufahamu ni kwamba mwanaume wake huyo aliyepania kumponyoka ni hazina kwa maisha yake. Ni vema ajitambue kwamba pamoja na uvivu wake lakini bwana yule alimvumilia. Maandiko ya dini yameweka bayana kwamba ‘mwanamke mvivu na asile’.

Inapofikia hatua hata ile haki yake ya msingi ya ndoa anaikosa, je, baba huyu afanyeje? Ni mfanyabiashara anayekimbizana na kazi zake huku na huko ili aweze kutunza familia yake na pia kusomesha watoto, lakini mkewe hatambui hilo, anamchunguza chunguza eti leo ananukia marashi ya kike au kwanini umechelewa au kwanini umelala nje na kadhalika.

Ebo! Kama unamwekea vigingi kwanini asitafute starehe mahali pengine? Mambo mengine baadhi ya wanawake wanachangia. Mwanaume ni mvumilivu sana hasa inapohusu mambo ya familia yake.

Lakini ukiona mwanaume anasema ‘inatosha’ ujue amefikiria mbali. Amevuta pumzi hadi za mwisho. Kwa maoni yangu kuhusiana na mwanamama huyo ni kwamba kama kweli mumewe amepania kumwachia mji, na hakuwa makini, mali zote zinazomzunguka zitatoweka kama umande.

Inavyoonekana mume huyo amepania kutengana na mwanamama huyu kwa sababu hizo nilizotaja hapo juu huku akionyesha kuwa zipo sababu nyingine zilizojificha ambazo hakutaka kuzitaja hadharani. Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.

Mpenzi msomaji wangu, hayo ndiyo yaliyojiri mwishoni mwa mwaka jana, baba huyu aliyepania kumkimbia mkewe na kuhamia kijijini kisa eti anamnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumnyima haki yake ya unyumba.

Kama hayo ni kweli, basi mwanamama huyo amemkosea sana mumewe na anapaswa kujilaumu kwa uamuzi wowote atakaochukua. Kila mtu anapenda kuishi kwa raha bila bughudha. Maisha yenyewe ni mafupi sana hivyo hayahitaji masharti ya kisanii. Jipe raha na mpe pia raha mwenzako. Maisha Ndivyo Yalivyo.

fwingia@yahoo.com

Wednesday, September 09, 2009

Kumuiba Mke au Mume wa Mwenzako ni Ufisadi!

Na Dada Flora Wingia

Kutoka ippmedia.com

Kwa tafsiri yangu nyepesi nyepesi, ufisadi ni wizi, udanganyifu, ulaghai, ubadhirifu, umaaluni, ufedhuli, ubaradhuli na mengineyo yanayofanana na hayo. Vitendo vyote hivyo siyo tu vinafanywa na baadhi ya watu dhidi ya serikali na taasisi za umma, bali pia dhidi ya mke au mume wa mwenzako. Unabisha? Subiri nikutoholee.

Naam, mpenzi msomaji, nimeanza kuchombeza hivyo ujiandae kwa vionjo vinavyodhihirisha kirusi cha ufisadi kinavyozitafuna pia familia zetu. Kirusi hiki, ama kinabomoa nyumba zetu au kuzitia nyufa, na zaidi kinazisambaratisha kwa baba na mama, kila mmoja kufikia hatua ya kutafuta sehemu ya kujishikiza nje ya ndoa.

Kwanini hali hii inatokea? Je, ni umasikini ndani ya familia? Au ni utajiri umewakolea kiasi cha kupagawa na hivyo kutafuta maisha mbadala pembezoni? Au ni kitu gani hasa! Majibu yote haya msomaji wangu utayapata ndani ya mtiririko wa makala hii.

Hivi majuzi yupo fundi ujenzi wangu alinisimulia kisa kimoja ambacho kilinivuta kimawazo nikaona nikimwage hapa, ili pengine kirekebishe wenye mwelekeo huo. Hakifurahishi, lakini kina mafundisho muhimu ya kimaisha.

Katika simulizi yake, fundi huyu anasema kwamba yupo baba mmoja wa makamo mwenye mke na watoto wake wanne, wawili ni wasichana. Wawili wako sekondari, wengine vyuo.

Familia hii ina mji kule Mbagala wenye nyumba ya kisasa yenye eneo lenye nafasi.

Jirani na nyumba yao wakaamua kuanzisha baa na duka. Hapo huja wateja kununua na kuondoka na wengine huketi na kupata vinywaji, nyama choma.

Wazee hawa(baba na mama) wa mji huu, nao mara kwa mara huwa sehemu ya wanywaji. Pale hupata fursa ya kukutana na wezee wenzao kubadilishana mawazo. Ni wakamata maji wazuri na yakiwakolea hawasiti kuzua mitafaruku.

Unajua tena, wagidaji pombe ikiwakolea adabu na heshima huchepuka, hivyo kutoa fursa kwa ibilisi kulaghai. Simile hutoweka kwa wengine na kuanza kuongea ovyo.

Unaweza kudhani wanapofanya hivyo wanatania kumbe ni kweli toka kwenye nafsi zao zilizolegezwa na kilevi. Mfano mtu anamwambia mke wa rafiki yake eti ‘nakutamani sana’, na maneno haya anayasema mbele ya mumewe.

Je, mume mtu ataelewa kuwa ni utani? Ipo mitafaruku iliyoibuka kutokana na utani wa aina hii. Na pengine aliyetamka maneno hayo hakuwa anatania bali alimaanisha hivyo kupitia ibilisi wake wa pombe.

Kwa maelezo ya fundi huyu, wazee wa familia ninayozungumzia mara nyingi wamekuwa wakizozana wakiwa wanakunywa kwenye baa yao hiyo na zaidi ni wivu. Hofu yao ni kwamba huenda kila mmoja anao wateja anaowahusudu wanapokuja kunywa mahali hapo.

Baba anamshuku mume kuwa anao kinamama anaoonekana kutaniana nao au kuongea nao sana na huenda mmojawao ni mpenziwe wa pembeni. Na baba vivyo hivyo huhisi kuwa mama ana wazee anaochekacheka nao sana au vijana na huenda wapo anaowahusudu. Ili mradi kila mmoja anamtilia shaka mwenzake.

Chanzo cha mzozo wote huu ni uwepo wa baa hiyo karibu na nyumbani. Pengine isingekuwepo na kila mmoja angevinjari kivyake na migongano ya aina hiyo isingeonekana.

Kwa mtizamo, mama ndiye anayeonekana chakaramu zaidi na mshekumsheku anapoona wanaume, tofauti na mumewe ambaye ni mpole, mkimya ila mpepesaji mzuri wa macho anapoona kinamama au wasichana wanapitapita mbele yake wakija kupata huduma kwenye baa hiyo.

Upole na ukimya wa baba huyo, ulimzidishia mkewe jeuri kwamba hawezi kufurukuta. Hata ndugu za mume hufikiria mara mbili mbili kwenda kumtembelea ndugu yao(mume) kutokana na ukali wa mke.

Ilitokea mama huyu akamgundua mumewe akimkazia macho mwanamama mmoja. Hali hiyo ambayo ilikuwa ikijirudia mara kadhaa, ilimfanya mke ampige marufuku mwanamke yule kutokanyaga kwenye baa yao.

Hisia kuhusu mahusiana ya baba huyo na mwanamke huyo zilipelekea mkewe kumbonda mara nyingi kila wanapokolewa pombe na kutafutiana vijisababu vya kukosana. Na kila zikizuka vurumai, baba huchukua kibegi chake na kutokomea. Inaelezwa kuwa huenda kulala gesti.

Lakini kumbe halali gesti huenda kujichimbia nyumbani kwa mwanamke yule yule anayesababisha mipasuko ndani ya nyumba yao. Na mwanamke huyo baada ya kufukuzwa kwenye baa ile akaapa kutomwacha mzee huyo hadi kieleweke.

Misukosuko ambayo mume huyo alikuwa akipata kwa mkewe ilikuwa kama kichocheo cha kuzidi kumpenda mwandani huyo wa pembezoni.

Fumba na kufumbua mwandani huyo akapata mimba na kukaa sawa mtoto akazaliwa. Mtoto dume.

Taarifa zilipomfikia mama mwenye nyumba inaelezwa hadi sasa ameshikwa na bumbuwazi, na mume naye ndiyo amekuwa mbogo haoni wala hasikii.

Tena humpasulia wazi kwamba nakwenda au nimetoka kwa mke mwenzio. Naye mwandani huyo kila anakopita anatangaza ushindi kwa kumuopoa mume wa mwanamke mwenzake. Ufisadi mkubwa huu. Inauma lakini maji yakimwagika si hayazoleki?

Mpenzi msomaji, huo ndio ufisadi niliogusia tafsiri zake nyepesi nyepesi mwanzoni mwa makala haya. Ukali wakati mwingine huleta kilio. Kumbe pengine hekima ingetumika hata mpasuko uliojitokeza ndani ya familia hii usingekuweko. Hii ni kutokana na ukweli kwamba hekima ni bora kuliko kutumia nguvu. Na kwamba afadhali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima kuliko kusikiliza kelele za mfalme katika kikao cha wapumbavu.

Ufisadi mwingine unaozibomoa nyumba zetu ni huu unaofanyika kupitia simu za kiganjani. Mtu anamdoea mke au mume wa mwenzake na kisha anatumia ujumbe wa simu kumchanganya.

Wenye mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa zao wameshaonja joto la kasheshe zinazotokana na ufisadi huu. Na wenye kiherehere zaidi ni wale washikaji wa nje ya ndoa. Hao huwa wakali kuliko wenye nyumba zao. Kisa wanawaonea wivu na wanaponogewa hudiriki kubomoa nyumba zilizojengwa kwa gharama kubwa.

Anachofanya yule dowezi ni kutafuta simu ya mke wa mshikaji wake na kumtumia maneno ya kashfa kumdhihirishia kuwa mumewe anamdhibiti. Tabia hii wanayo sana wanawake.

Mwingine hupagawa na kuamua ku-forward ujumbe aliotumiwa na mume wa mwanamke mwenzake ili kumringishia kuwa hayuko peke yake na kwamba mumewe anaye kila anapomhitaji. Huu ni ufedhuli, ubedui, umaaluni, ufirauni wa hali ya juu.

Nyumba nyingi zimejikuta katika mpasuko mkubwa kutokana na mahusiano nje ya ndoa. Nyumba inachipuka ndani ya nyumba(nyumba ndogo hizi). Hata mtu akiona mwenzake akapatwa na balaa fulani, badala ya kujifunza na kuepuka, naye hujitosa kama vile shamba la majaribio. Matokeo yake naye anatumbukia.

Kwa ujumla mipasuko ndani ya familia zetu tunaisababisha sisi wenyewe. Kama baba na mama wako imara, hawatamani vya nje, hata Mungu hubariki nyumba hiyo na kuwa imara. Zipo nyumba chache za aina hii. Nyingi ni zile zinazoiga eti kama yule kafanya vile kwanini na mimi nisifanye hivyo. Kumbuka kuiga tembo ku… utapasuka msamba. Au siyo? Maisha Ndivyo yalivyo.

Niishie hapa msomaji wangu niruhusu nawe uchangie maoni, au nipe kisa ukijuacho tukijadili kwa pamoja.

Niandikie:

flora.wingia@guardian.co.tz

Wasalaam.

Tuesday, July 01, 2008

Kuolewa siku hizi ni fasheni au kuondoa nuksi?

Mwandishi wa habari, Flora Wingia, anauliza na kuchambua swali nzito. Inafurahisha kweli kweli.

**********************************************
Kutoka ippmedia.com

Eti wanaoolewa siku hizi ni fasheni ya kuondoa nuksi?

2008-06-29


Na Anti Flora Wingia

Mpenzi msomaji, lipo jambo moja limenivutia kukumegea leo kuhusu ndoa za siku hizi. Huko tulikotoka kuolewa au kuoa lilikuwa ni tukio la baraka. Lakini siku hizi hali ikoje? Liko tukio moja nililosimuliwa kutoka huko Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo dada mmoja aliolewa siku ya Jumamosi, lakini siku mbili baadaye, yaani Jumanne akamwacha yule bwana na kutokomea kwa mwanaume mwingine. Kisa ni nini?

Msimulizi wa tukio hili anasema kuwa dada huyo japokuwa alikuwa na mchumba huyo waliyefunga naye ndoa, lakini hakuwa anampenda kwa dhati bali alikuwepo mwingine wa ubani, tena mume wa mtu aliyemzibua kimapenzi.

Kwa maelezo ya bibie eti mchumba yule hakumpenda ila alitaka afunge naye ndoa ili kuondoa nuksi na iwe kwenye kumbukumbu kwamba hata yeye aliwahi kuoewa kwa ndoa takatifu.

Mashuhuda wa harusi wa bibie huyo wanasema ndoa ilikuwa ya gharama kubwa na iliyofana lakini walishangazwa na taarifa kuwa ndoa imesambaratika na bibie kaenda kwa mshikaji wake ambaye ni mume wa mtu.

Inasemekana ndugu wa bwana harusi wamecharuka na kuapa kumrudisha bibi harusi kwa mumewe kwa gharama zozote zile. Na kwamba shugadadi huyo anayemzingua shemeji yao naye atakiona cha mtema kuni.

Hata hivyo, habari zingine zinadai kuwa bibie katu hatamrejea mumewe kwa kile alichodai, kwanza alitaka tu aolewe ndoa kuondoa nuksi na pili aliyemuoa hamridhishi kimapenzi.

Mpenzi msomaji, hayo ndiyo mambo na hakika maisha ndivyo yalivyo. Eti siku hizi kuolewa ni fasheni ya kuondoa nuksi. Wiki hii nilipata wasaa kusikiliza kipindi cha Longa mwanamume kwenye kituo cha televisheni cha ITV kikihusu baadhi ya kinamama kuwaachia watumishi wa nyumbani kufanya kazi ambazo zingepaswa kufanywa na wao.

Mfano, kumpokea baba arudipo kazini, kumwandalia baba chakula, kumwekea maji bafuni na hata kutandika kitanda. Eti kazi hizi zote alipaswa kuzifanya mama ili kumwepushia baba vishawishi vya kummezea mate housigeli. Nilipogusia jambo hili katika kikao Fulani na marafiki zangu juzi, mmoja akasema; ``Kinamama wengine wako katika nyumba zao tu kuweka rekodi kuwa wameolewa, lakini mapenzi hakuna``.

Mwingine akamdakia; ``wewe hujui ukiona hivyo ujue vituko vya mumewe vimemfika kooni. Pengine anapewa taarifa zake (mume) kuhusu nyendo zake za kihuni huko nje, au mume yule hamjali tena kama mwanzoni walipooana na kadhalika``.

Mwingine akapigilia msumari kwa kusema; ``katika nyumba nyingine ukiona mama hajali kumhudumia mumewe nyumbani, basi ujue anaye mshikaji nje ya ndoa anayemzingua hivyo mume si chochote. Bibie niliyemzungumzia mwanzoni mwa makala hii yeye hakutaka aone vurugu za ndoa ndio sababu akaamua kujiengua mapema na kwenda kumuegemea shugadadi wake.

Lakini swali ni je, haya ndiyo maisha tunayotaka? Hizi fasheni za maisha eti kuondoa nuksi zinatoka wapi? Je, huku ni kuondoa nuksi au ni kuharibiana kimaisha? Kwa ujumla yule mama anayempiga chenga mumewe ndani na kuchepuka kwa bwana wa pembeni, sidhani ana amani yoyote rohoni mwake.

Hali kadhalika yule bibie aliyemtosa mumewe wa ndoa muda mfupi na kukimbilia kwa mume wa mtu, bado atapata vikwazo na vishawishi vya kusaka mabwana wengine. Kama hukutosheka na mmoja ndio utatosheka na wanaume wengine lukuki?

Upo msemo mmoja wa mtaani usemao ``Nimezunguka bucha zote lakini nyama ni ile ile``. Hii ikimaanisha kuwa kile baadhi ya kinamama wanachokimbia kwenye nyumba zao ndio hicho hicho watakikuta kule waendako. Mpenzi msomaji, kinachotakiwa ni watu kuheshimu nyumba zao.

Mke au mume ulimtupia jicho mwenyewe, ukampenda sasa wamtilia shaka ya nini? Si maji uliyavulia nguo, sasa kwa nini uogope kuyaoga? Hakika Maisha Ndivyo Yalivyo. Kuolewa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu siyo fasheni wala kuondoa nuksi kama baadhi yetu wanavyodai. Hata mababu zetu walifurahia sana ndoa na zilidumu tofauti na sasa ambapo tukio hilo linapewa uzito mdogo.

Siyo siri kuwa baadhi ya watu wanaoa au kuolewa lakini wanajenga au wanaendeleza mahusiano ya nje ya ndoa. Raha gani wanapata huko, wahusika wanajua. Faida gani wanapa ndio pamoja na maambukizi ya magonjwa hatari kama Ukimwi. Habari ndiyo hiyo.

Mpenzi msomaji, kwa leo naomba niishie hapa tukutane tena wiki ijayo. Ukiwa na maoni, ushauri usiache kunikandamizia kupitia email ifuatayo;

fwingia@yahoo.com. Wasalaam.

SOURCE: Nipashe

Thursday, September 13, 2007

Ujumbe kutoka Kaka Lazurus Mbilinyi 'Mawaidha kuhusu Ndoa'

Wapendwa wasomaji nimepata ujumbe huo kutoka kwa Kaka Lazarus Mbilinyi ambaye aliandika somo la NDOA NA UNYUMBA ambayo umeisoma kwenye blog hii:

http://swahilitime.blogspot.com/search/label/Mbilinyi

**************************************************************************
Dada Chemi,

Mimi ndo Lazarus Mbilinyi niliyeandaa hilo somo la ndoa na nyumba na kwa bahati mbaya nilikuwa sijui kama linaweza kusomwa na mtu yoyote kwani katika kuliandaa niliandaa katika mazingira ya Tanzania na hasa vijijini na sehemu ambazo mwanamume anafanya kazi (ameajiriwa) na mwanamke ni mama wa nyumbani (anayejishughulisha na kazi zingine) na pia limeegemea zaidi katika familia za kikristo.

Naamini maoni ninayopata kutokana na hilo somo basi nitayafanyia kazi na kama inawezekana siku nyingine nitoe kitabu cha Ndoa na nyumbaHata hivyo nashukuru sana kwa kueneza ujumbe kwa watu wote ili wajue ndoa ni nini hilo nashukuru.

Kwa sasa nipo Canada kwa ajili ya shule niemfika hapa tarehe 1 Sept 2007 na naamini tutazidi kuwasiliana na pia nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu.

Asante sana kwa kazi njema ya kuelimisha jamii:

--
Lazarus P. Mbilinyi

Thursday, September 06, 2007

Mawaidha kuhusu Ndoa - Sehemu ya Pili


SIFA ZA MWANAMKE (SIFA NJEMA)

1. Awe mwema - Mith 12:4, 31:10 -30
2. Mwenye hekima - Mith 14:1 16:5,24
3. Mwenye adabu - Mith 19:14, 11:16a
4. Mwenye busara - Mith 19:14
5. Awe mkarimu - Mith 22:9
6. Msafi (mwili na nyumba)
7. Mpole - Mith 15:1
8. Mwenye huruma
9. Mdadisi
10. Mvumilivu
11. Mcheshi (kiasi)Yampasa mke aanze siku kwa kauli nzuri hata kama anaumwa:-
- Amusalimie mume
- Amwage mumewe akimtakia kazi njema baada ya kumuandalia
(a) Maji ya kuoga
(b) Kifungua kinywa
(c) Nguo za kuvaa siku hiyo

Mume atokapo kazini:-
(a) Mkaribishe kwa tabasamu, mkaribishe kwa furaha.
(b) Mpigipige mgongoni
(c) Vaa nguo nzuri (mwanaume hupenda anachoona) macho huvutiwa kwa kuona
(d) Waeleze watoto wako unavyompenda baba yao ( watoto nao watawapenda wote)
(e) Kila mmoja wenu ajue kile anachopenda ua anachotaka

ILI KUMHESHIMU MUME
  1. Muombee kila siku - Yeye alivyo hekima, busara, ulinzi, baraka, ujuzi, kuelewa, kiroho, mafanikio, kushinda majaribu nk - angalia na tarajia majibu ya maombi - Mshukuru Mungu kwa kazi anayofanya kwa familia yako - Mshukuru Mungu kwa ajili ya Mume wako- ombea mtazamo wako.
  2. Kumbuka Mungu amemuweka mume wako kuwa kiongozi wa nyumba yako pamoja na wewe.
  3. Angalia sifa za mumeo na uzikubali na ongeza mara kwa mara
  4. Mwambie mumeo ni namna gani unamfurahia na kumpenda
  5. Usitoe sifa zake mbaya mbele za watu au kubisha
  6. Mtie moyo na kuwa msaaada wakati wa jambo gumuJihadhari na jinsi unavyomuuliza maswali
  7. Changamkia pale anapoonesha upendo
  8. Fikiria mambo mazuri juu ya mumeo
  9. Thamini vitu anavyovipenda na asivyovipenda Mith 12:4

KAWAIDA MWANAMKE
  1. Usitegemee starehe nyingi kama zile ulizokuwa unapata kwa wazazi wako au ndugu zako
  2. Utakuwa na juhudi katika kujenga nyumba ya mume wako uliye naye. Mith 14: 1 Kila mwanamke aliye na heshima.......................
  3. Hutakuwa mgomvi na mchokozi wala kumpiga mumeo kwa mwiko Mith 21:19
  4. Utampa mume wako haki yake 1Kor 7:3-5
  5. Thamani ya mumeo ni zaidi ya wanaume wote. Ez 16:32
  6. Umtii mumeo kwa Roho ya upole na unyenyekevu 1Pet 3:1-4
  7. Usimuruhusu mtu yeyote atambue kwamba unao wakati mgumu ( siri za ndani zisitoke nje) 1pet 5:9
  8. Utahaakikisha macho yako yanamwangalia mumeo wakati amevaa kabla ya kutoka kwenda kazini au kutembea
  9. Utajitoa na kumtii mumeo kwa moyo wote na kumruhusu kuwa kichwa cha nyumba Kol 3:18, 1pet 3:6, Ef 5: 33
  10. Utahakikisha mumeo ni bora kuliko watu wengine Fil 2:3, Wimb 5: 9-16
  11. Mwanaume ni dereva wa gari la ndoa na mwanamke anaweza akashauri na kupednekeza njia ya kupita na siyo kunyang'anya usukani

9. SIFA ZA MWANAUME
1. Mpole
2. Asiwe mwepesi wa hasira
3. Mcheshi
4. Anayeshaurika
5. Anayewajali watu wa nyumbani mwake (mahitaji)
6. Aliye na shukurani na kusifu (kwa lolote jema alilolitenda mkewe)
7. Anayeaga aondokapo kwenda matembezini au kazini au popote.

10. WAJIBU WA WA MUME KWA MKEWE

1. KUPENDA - kwa kiwango cha Kristo kwa kanisa Efe 5:25 matatizo mengi hutokea kwa sababu watu hawajui maana na jinsi ya kupenda kupenda ni matendo (action) siyo kujisikia au kuhisi ni kufanya vitu vizuri kama vile kutoa, kutabasamu, kusamehe nk Yohana 3:16
2. KIONGOZI (KICHWA) MTAWALA - Mume ni kichwa cha mke Efe 5:23 Naye atakutawala Mwanz 3:16c Amri hii hairekebiki kwa kelele za UWT kudai usawa ila utekelezapo maagizo ya Kristo amri amri ya kutawaliwa inakufa
3. MLINZI WA MKEWE - Kama chombo kisicho na nguvu, 1pet 3:7, Naye ni mwokozi wa mwili Efes 5:23 Mke hujiona salama awapo na mumewe Isay 4:1 Hivyo mume mlinde mkeo na maadui wa ndani na nje kama vile baba na mama, mashemeji/mawifi na marafik
4. KUTUNZA FAMILIA. Kuhakiki familia inapata chakula cha kutosha, malazi, mavazi na elimu kwa watoto Mwanzo 3: 17
5. KUMPAMBA MKEWE - mume sharti ampambe mkewe apendeze ili aweze kuvutia (amununulie vipodozi, nguo nk)

KAWAIDA MWANAUME:

  1. Utamheshimu mke wako kama mrithi pamoja na wewe katika neema ya uzima katika Kristo Yesu. 1Pet 3:7
  2. Mke wako ni mtu wa kwanza kwako siyo ndugu zako wala rafiki zako Mwanzo 2: 24 Mtaambatana na kuwa mwili mmoja
  3. Mara kwa mara utamwambia mke wako alivyo wa muhimu na thamani kwako Fil 2:3 , Mith 31: 10,11
  4. Utaendelea kumpenda kwa upendo ule wa kwanza wa wakati unampata. Wimb 5: m10 - 16
  5. Utakuwa kiongozi wa kusimamia nidhamu ya nyumba yako ukisaidiwa na mke wako. Efes 6:4
  6. Utakumbuka kutekeleza au kutimiza vile vitu vidogo ambavyo ulimwahidi mke wako kwamba utafanya Math 5: 37
  7. Macho yako yataelekea kwa mke wako tu na sivinginevyo. Mith 5: 15-20, Ayub 31:1, Yer 5:8
  8. Utafanya juhudi kusikiliza yale yaliyosemwa na mke wako. Mwanz 21:12
  9. Utambusu kila siku asubuhi kwa upendo. Wimb 8:1
  10. Hutakuwa mchungu likija swala la fedha. Est 5:3

12. WAJIBU WA MKE KWA MUMEWE KUTII - Kumtii mume kama kumtii kristo Bwana Yesu efe 5:22 watu huchanganya sana neon kutii na kuheshimu. Kutii kunakosemwa hapa ni kuwa endapo wawili mume na mke mmeshindwa kufikia uamuzi wa pamoja, basi,basi mke atatii uamuzi wa mumewe kama vile wamekubaliana awali

KULEA WATOTO (FAMILIA)
(a) Kuhakikisha afya ya mumeo na watoto
(b) Kuhakikisha kuwa chakula kinaliwa kwa wakati na kizuri
(c) Kuhakikisha usafi wa malazi, mavazi na miili yao
(d) Kufundisha watoto maneno ya Mungu
(e) Kuchunguza nyendo na tabia za watoto na mumeo na kuchukua tahadhari mapema.

KUMSHAURI MUMEO
Mke mwenye busara ni mshauri mwema kwa mumewe. Hatatoa ushauri wa kuleta maangamizi. Ushauri unafaa lakini ushauri mwingine upimwe kabla ya kufanyia kazi. Ona mashauri mabaya ya wanawake kwa waume zao

(f) Hawa kwa Adamu - Mwanza 3:17 (kula tunda)
(g) Sara kwa Ibrahimu - Mwanzo 16: 1-3 kulala na mjakazi (tabu ya mashariki ya kati)
(h) Yezebeli kwa mfalme Ahabu - 1Falm 21:22/2Falm 9:10
(i) Zereshi kwa Hamani mumewe kwa habari ya Mordekai Esta 5:14, 7:9-10
(j) Mkewe Ayubu kwa ayubu mumewe - Ayubu aliukataa ushauri wa mkewe. Ayubu 2:9

13. ADUI WA NDOA NI:-UTAJIRI - Tajiri hupendwa na wasichana na pia huwa na tamaa ya kutafuta fedha kiasi cha kukosa muda na mkewe

UMASKINI
- kazi ya kutafuta lishe ni ya baba, hivyo hushughulika sana na kujikuta amekuwa baba zaidi kuliko kuwa mume

MADARAKA - madaraka ya ofisini huyaleta hadi nyumbanini chukuzo kwa mume/mke. Maafisa hawana muda na wake zao kwa sababu ya makongamano/semina/ziara mbalimbali.
- Hivyo wake zao wengi hutumia madereva kukidhi haja zao za kimwili
- Mke ambaye ni ofisa humwachia house girl kazi za kupika, kufagia chumbani, kupeleka maji bafuni na hata kutandika kitanda, hivyo kusababisha mke kupinduliwa na house girl.

MAMBO YANAYOWAKERA WAKE ZETU
  1. Wababa wenye madaraka kuyapeleka madaraka nyumbani
  2. Wake kuwajibika na mambo ya nyumbani kwa vile wana mishahara minono
  3. Wababa kutotenga muda wa kutosha kukaa na wake zao ili kuongea yanayowahusu
  4. Mume kumwachia mke kulea watoto hasa wakati wa usiku
  5. Mume kutomtia moyo mke wakati wa ujauzito
  6. Mume kumchanganya mama na watoto wa kike wanapokosa
  7. Mume kutokuwa na maandalizi mazuri wakati wa kukutana kimwili na mkeo
  8. Mume kujijari mwenyeweMume kusaidia ndugu zake bila mke wake kujua
  9. Mume kubagua watoto
  10. Mume kuwa na upendo na ukaribu au kucheka na binti waishio nao huku yupo mke wake
  11. Mume kutomshirikisha mkewe katika huduma yake ya ili aweze kumwombeaKutoonesha shukrani wala kutokuwa na msamaha
  12. Mume kutomtazama mkeo usoni mkiwa chumban
  13. iMume kuongea kiutani na wanawake wengine mkeo akiwa hayupo.