
Saturday, April 17, 2010
Ndoa ya Makaratasi Yamponza Mcheza Sinema

Bi Romero anatoka Mexico. Alilmlipa Kent Ross afunge ndoa naye. Hawajawahi kukaa pamoja, Baada ya ndoa hiyo ya makaratasi, Bi Romero aliaanza na uhusiano na dume mwingine, Markus Klinko. Walivyoaachana na Klinko ndo kaenda kusema huko uhamiaji kuwa Bi Romero alifunga ndoa ya makaratasi na Ross. Jamani, ni wivu, uchungu au shetani iliyompeleka kwa polisi wa uhamiaji.
Bi Romero na Ross wako hatarini kufungwa miaka mitano!
***********************************************************************
LOS ANGELES (AP) - Mexican-born actress Fernanda Romero has had bit parts in such movies as the horror film "Drag Me to Hell," but federal prosecutors say her biggest act was pretending to be a bride.
The 28-year-old actress and husband were arrested Friday at their separate Los Angeles homes and charged with marriage fraud, the U.S. attorney's office said. They contend Romero paid Kent Ross, 28, to marry her in 2005 so that she could become a U.S. resident.
Authorities said the two never lived together and Romero, whose full name is Maria Fernanda Romero Martinez, submitted phony documents with her residency application.
An investigation began after Romero's ex-boyfriend, fashion photographer Markus Klinko, told immigration authorities her marriage was a sham. The couple started dating after Romero and Ross were married.
If convicted, Romero and Ross could be sentenced to up to five years in federal prison.
Romero has had roles in several small films and is moderately well known in Mexico, where she appeared in the TV Azteca soap "Eternamente Tuya." She has also appeared on the Spanish-language channels Univision and Telemundo in the shows "Control" and "La Ley del Silencio," respectively.
According to her website, she has appeared in television and print ads for several U.S. companies, as well as a music video. She moved to Los Angeles when she was 18 to study fashion design, according to her site.
Messages to her publicist were not returned Friday.
A phone message left for Ross' attorney, Mike Shannon, also was not returned.
Romero and Ross were both released after initial court appearances Friday. However, a judge restricted Romero's travel to certain Southern California counties and said she could not leave the country.
Special Assistant U.S. Attorney James M. Left, said immigration officials began investigating in 2007 after Klinko mentioned the marriage during a lawsuit he filed in New York.
Left says a marriage ceremony was performed on June 12, 2005, but the couple never lived together.
He said immigration marriage fraud cases may be brought in either criminal or immigration courts. The case against Romero was pursued because of "the overwhelming amount of evidence" and repeated misstatements by the actress, Left said.
"Immigration benefit fraud is a serious crime," said Miguel Unzueta, an Immigration and Customs Enforcement special agent in charge in Los Angeles. "Not only does it potentially rob deserving immigrants of benefits they rightfully deserve, it also undermines the integrity of our nation's legal immigration system."
Friday, April 16, 2010
Mume Mzuri!

A guy woke up in the morning with a terrible hangover. Next to the bed was a couple of aspirins, a glass of water, and a note from his wife ? ?Honey, there's a hot breakfast waiting for you in the kitchen. Love, your wife?. He looks around the room and sees that it is in perfect order, spotlessly clean. So is the rest of the house.
He stumbles into the bathroom and notices a huge black eye. After shaving, he goes to the kitchen, and sees that the hall mirror is broken too.
His son is in the kitchen and as he's eating his huge breakfast the guy asks the son what all this is about.
Well, last night you came home drunk off your ass, stumbled into the mirror and hit your head on the doorknob. Mom helped you to bed, and as she's trying to get your pants off you kicked her away and said get off me lady, I'm married?.
If you really enjoyed this story please forward to friend. Or reply and let us know. You might make someone's day!
He stumbles into the bathroom and notices a huge black eye. After shaving, he goes to the kitchen, and sees that the hall mirror is broken too.
His son is in the kitchen and as he's eating his huge breakfast the guy asks the son what all this is about.
Well, last night you came home drunk off your ass, stumbled into the mirror and hit your head on the doorknob. Mom helped you to bed, and as she's trying to get your pants off you kicked her away and said get off me lady, I'm married?.
If you really enjoyed this story please forward to friend. Or reply and let us know. You might make someone's day!
Tuesday, January 05, 2010
Mume Anapokimbia Mke Mjini Na Kuanza Maskani Mapya Kijijini!
SEMA DA FLORA WINGIA! SEMA!!!!!
************************************
Na Flora Wingia
Heri ya Mwaka Mpya 2010 mpenzi msomaji wangu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuvusha mwaka huu. Naamini sote tumejipanga vema katika kufanikisha malengo mapya kwa mwaka mpya.
Wakati wengine wamepania kuboresha maisha ya familia zao, wengine wameamua kumeguka na kuanza maisha mapya kwingineko. Je, unajua ni kwanini? Hebu sikia kituko hiki cha kufunga mwaka 2009.
Ukiona mwanaume anaukimbia mji wake na kwenda kutafuta maskani mapya, ujue maji yamemfika shingoni. Katika hali ya kawaida ya maisha, mwanaume ndiye anayemkaribisha mwanamke nyumbani kwake na wakati mwingine huishia kumuoa.
Ukiona mwanamke anayemtunza mwanaume nyumbani kwake, huwa inaelezwa kuwa ‘mwanaume huyo kaolewa’. Lakini si unajua tena kupenda wakati mwingine mtu huwa zuzu au wengine huita zezeta. Hata akikemewa na wenzake yeye hujifanya hamnazo na kujikausha kwani anajua nini anachofaidi pale.
Pengine yeye ni kula kulala. Kila kitu anagharimia mke kuanzia chakula, mavazi na kadhalika. Mwanaume anayempata mwanamke wa aina hiyo, kwanini ajivunge?
Tukiachana na hayo, yupo mwanaume anayeoa mwanamke iwe ni kwa gharama kubwa au za kawaida, lakini baadaye mke huyo anamnyanyasa kiasi cha kumfanya auhame mji huo na kutamani mji mwingine. Hebu sikia kituko hiki cha funga mwaka.
Yuko baba mmoja nilikutanishwa naye hivi majuzi ambaye amelikimbia jiji la Dar es Salaam na kuhamia kijijini mkoa wa Pwani kutokana na manyanyaso anayopata toka kwa mkewe.
Baba huyu mwenye watoto wawili na mwanamama huyo, ameapa kumwachia mkewe kila kitu hapa jijini, na kisha yeye kuhamia kijijini kuanza maisha mapya mwaka huu mpya.
Baba huyu amenifurahisha sana. Wenzake wanahama vijijini kuja mijini lakini yeye anaamua kurejea maisha ya kijijini kutokana na suluba toka kwa mkewe.
Baba huyu anasema; “Heri kuishi peke yangu eneo la kijijini kuliko kuishi na mwanamke mwenye kero kama mke wangu. Nilimpenda mwenyewe, lakini sikujua kama angenifanyia yale niliyobainisha kwake.
“Mwanamke hataki kufanya kazi yoyote, yeye ni kwenda saluni, kukaa na kujipodoa tu. Nina mifugo, ng’ombe wawili wa maziwa, nguruwe na kuku wa kienyeji. Kutokana na mama huyo kutoonyesha nia ya kujishughulisha, nimeweka wafanyakazi wa kuhudumia mifugo hiyo.
“Akiamua hutoa nguruwe na kuuza na ninapomuuliza anakuja juu na kudai eti ni kwa matumizi ya nyumbani. Hata hivyo, kila siku lazima niache hela ya chakula mezani. Nikirudi nyumbani lazima aninuse eti kama nanukia marashi ya wanawake.
Wakati mwingine tunapopumzika hataki nimguse…hugeukia ukutani. Vituko hivi na vingine vinaninyima raha vibaya sana. Hadi najiuliza ni mwanamke gani huyu?Au anaye mwingine ampendaye?
“Nilimchangua mwenyewe, nikamuoa mwenyewe, lakini sasa nimefikia mwisho sina budi kumtosa. Sitamfukuza, lakini nitamwachia kila kitu, nyumba, mifugo na vitu vyote vilivyo mzunguka. Watoto nitapeleka shule za bweni. Ila mimi nakwenda kuanza maisha mapya”, anasema baba huyu.
Nilipomuuliza kama uamuzi huo amewajulisha wazee alisema; “Nilishaitisha kikao cha pande zote mbili kulalamika vituko vya mke huyu. Napo nilieleza msimamo wangu wa kutengana naye na kumwachia kila kitu. Ingawa hakukubaliana na hilo lakini niliungwa mkono na wajumbe wengi kwamba kwa kuwa hataki kujirekebisha, hakuna jinsi.
Mpenzi msomaji, kwa maelezo ya baba huyu, tayari ameshapata eneo katika kijiji kimoja mkoani Pwani ambako atajenga makao yake mapya na atajikita kwenye Kilimo Kwanza kwani anazo ekari 15 za ardhi. Hataki wala mwanamke wake huyu ajue huko kujiepusha na bughudha zake.
Ama kweli ‘mwenye bahati habahatishi. Mwanamke anapata mume mchakarikaji, lakini yeye anabweteka. Wapo wanaotafuta bahati ya aina hiyo bila mafanikio.
Nijuavyo mimi, mwanaume ni nguzo ya nyumba. Anapoondoka iwe ni kwa mfarakano au kwa kifo, hakika maisha katika nyumba husika huyumba na wakati mwingine hubomoka kabisa.
Mama yule anaonyesha jeuri ile kwa kuwa anamuona mumewe karibu, lakini atakapotokomea kijijini alikopania, mwanamama yule ambaye amekuwa mbwete, hataki kujishughulisha na miradi ya pale nyumbani, atajikuta naye pia akihangaika kama hayawani.
Ninachokiona kwa mwanamke huyu ni majuto mjukuu. Anachoshindwa kufahamu ni kwamba mwanaume wake huyo aliyepania kumponyoka ni hazina kwa maisha yake. Ni vema ajitambue kwamba pamoja na uvivu wake lakini bwana yule alimvumilia. Maandiko ya dini yameweka bayana kwamba ‘mwanamke mvivu na asile’.
Inapofikia hatua hata ile haki yake ya msingi ya ndoa anaikosa, je, baba huyu afanyeje? Ni mfanyabiashara anayekimbizana na kazi zake huku na huko ili aweze kutunza familia yake na pia kusomesha watoto, lakini mkewe hatambui hilo, anamchunguza chunguza eti leo ananukia marashi ya kike au kwanini umechelewa au kwanini umelala nje na kadhalika.
Ebo! Kama unamwekea vigingi kwanini asitafute starehe mahali pengine? Mambo mengine baadhi ya wanawake wanachangia. Mwanaume ni mvumilivu sana hasa inapohusu mambo ya familia yake.
Lakini ukiona mwanaume anasema ‘inatosha’ ujue amefikiria mbali. Amevuta pumzi hadi za mwisho. Kwa maoni yangu kuhusiana na mwanamama huyo ni kwamba kama kweli mumewe amepania kumwachia mji, na hakuwa makini, mali zote zinazomzunguka zitatoweka kama umande.
Inavyoonekana mume huyo amepania kutengana na mwanamama huyu kwa sababu hizo nilizotaja hapo juu huku akionyesha kuwa zipo sababu nyingine zilizojificha ambazo hakutaka kuzitaja hadharani. Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.
Mpenzi msomaji wangu, hayo ndiyo yaliyojiri mwishoni mwa mwaka jana, baba huyu aliyepania kumkimbia mkewe na kuhamia kijijini kisa eti anamnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumnyima haki yake ya unyumba.
Kama hayo ni kweli, basi mwanamama huyo amemkosea sana mumewe na anapaswa kujilaumu kwa uamuzi wowote atakaochukua. Kila mtu anapenda kuishi kwa raha bila bughudha. Maisha yenyewe ni mafupi sana hivyo hayahitaji masharti ya kisanii. Jipe raha na mpe pia raha mwenzako. Maisha Ndivyo Yalivyo.
fwingia@yahoo.com
************************************

Heri ya Mwaka Mpya 2010 mpenzi msomaji wangu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuvusha mwaka huu. Naamini sote tumejipanga vema katika kufanikisha malengo mapya kwa mwaka mpya.
Wakati wengine wamepania kuboresha maisha ya familia zao, wengine wameamua kumeguka na kuanza maisha mapya kwingineko. Je, unajua ni kwanini? Hebu sikia kituko hiki cha kufunga mwaka 2009.
Ukiona mwanaume anaukimbia mji wake na kwenda kutafuta maskani mapya, ujue maji yamemfika shingoni. Katika hali ya kawaida ya maisha, mwanaume ndiye anayemkaribisha mwanamke nyumbani kwake na wakati mwingine huishia kumuoa.
Ukiona mwanamke anayemtunza mwanaume nyumbani kwake, huwa inaelezwa kuwa ‘mwanaume huyo kaolewa’. Lakini si unajua tena kupenda wakati mwingine mtu huwa zuzu au wengine huita zezeta. Hata akikemewa na wenzake yeye hujifanya hamnazo na kujikausha kwani anajua nini anachofaidi pale.
Pengine yeye ni kula kulala. Kila kitu anagharimia mke kuanzia chakula, mavazi na kadhalika. Mwanaume anayempata mwanamke wa aina hiyo, kwanini ajivunge?
Tukiachana na hayo, yupo mwanaume anayeoa mwanamke iwe ni kwa gharama kubwa au za kawaida, lakini baadaye mke huyo anamnyanyasa kiasi cha kumfanya auhame mji huo na kutamani mji mwingine. Hebu sikia kituko hiki cha funga mwaka.
Yuko baba mmoja nilikutanishwa naye hivi majuzi ambaye amelikimbia jiji la Dar es Salaam na kuhamia kijijini mkoa wa Pwani kutokana na manyanyaso anayopata toka kwa mkewe.
Baba huyu mwenye watoto wawili na mwanamama huyo, ameapa kumwachia mkewe kila kitu hapa jijini, na kisha yeye kuhamia kijijini kuanza maisha mapya mwaka huu mpya.
Baba huyu amenifurahisha sana. Wenzake wanahama vijijini kuja mijini lakini yeye anaamua kurejea maisha ya kijijini kutokana na suluba toka kwa mkewe.
Baba huyu anasema; “Heri kuishi peke yangu eneo la kijijini kuliko kuishi na mwanamke mwenye kero kama mke wangu. Nilimpenda mwenyewe, lakini sikujua kama angenifanyia yale niliyobainisha kwake.
“Mwanamke hataki kufanya kazi yoyote, yeye ni kwenda saluni, kukaa na kujipodoa tu. Nina mifugo, ng’ombe wawili wa maziwa, nguruwe na kuku wa kienyeji. Kutokana na mama huyo kutoonyesha nia ya kujishughulisha, nimeweka wafanyakazi wa kuhudumia mifugo hiyo.
“Akiamua hutoa nguruwe na kuuza na ninapomuuliza anakuja juu na kudai eti ni kwa matumizi ya nyumbani. Hata hivyo, kila siku lazima niache hela ya chakula mezani. Nikirudi nyumbani lazima aninuse eti kama nanukia marashi ya wanawake.
Wakati mwingine tunapopumzika hataki nimguse…hugeukia ukutani. Vituko hivi na vingine vinaninyima raha vibaya sana. Hadi najiuliza ni mwanamke gani huyu?Au anaye mwingine ampendaye?
“Nilimchangua mwenyewe, nikamuoa mwenyewe, lakini sasa nimefikia mwisho sina budi kumtosa. Sitamfukuza, lakini nitamwachia kila kitu, nyumba, mifugo na vitu vyote vilivyo mzunguka. Watoto nitapeleka shule za bweni. Ila mimi nakwenda kuanza maisha mapya”, anasema baba huyu.
Nilipomuuliza kama uamuzi huo amewajulisha wazee alisema; “Nilishaitisha kikao cha pande zote mbili kulalamika vituko vya mke huyu. Napo nilieleza msimamo wangu wa kutengana naye na kumwachia kila kitu. Ingawa hakukubaliana na hilo lakini niliungwa mkono na wajumbe wengi kwamba kwa kuwa hataki kujirekebisha, hakuna jinsi.
Mpenzi msomaji, kwa maelezo ya baba huyu, tayari ameshapata eneo katika kijiji kimoja mkoani Pwani ambako atajenga makao yake mapya na atajikita kwenye Kilimo Kwanza kwani anazo ekari 15 za ardhi. Hataki wala mwanamke wake huyu ajue huko kujiepusha na bughudha zake.
Ama kweli ‘mwenye bahati habahatishi. Mwanamke anapata mume mchakarikaji, lakini yeye anabweteka. Wapo wanaotafuta bahati ya aina hiyo bila mafanikio.
Nijuavyo mimi, mwanaume ni nguzo ya nyumba. Anapoondoka iwe ni kwa mfarakano au kwa kifo, hakika maisha katika nyumba husika huyumba na wakati mwingine hubomoka kabisa.
Mama yule anaonyesha jeuri ile kwa kuwa anamuona mumewe karibu, lakini atakapotokomea kijijini alikopania, mwanamama yule ambaye amekuwa mbwete, hataki kujishughulisha na miradi ya pale nyumbani, atajikuta naye pia akihangaika kama hayawani.
Ninachokiona kwa mwanamke huyu ni majuto mjukuu. Anachoshindwa kufahamu ni kwamba mwanaume wake huyo aliyepania kumponyoka ni hazina kwa maisha yake. Ni vema ajitambue kwamba pamoja na uvivu wake lakini bwana yule alimvumilia. Maandiko ya dini yameweka bayana kwamba ‘mwanamke mvivu na asile’.
Inapofikia hatua hata ile haki yake ya msingi ya ndoa anaikosa, je, baba huyu afanyeje? Ni mfanyabiashara anayekimbizana na kazi zake huku na huko ili aweze kutunza familia yake na pia kusomesha watoto, lakini mkewe hatambui hilo, anamchunguza chunguza eti leo ananukia marashi ya kike au kwanini umechelewa au kwanini umelala nje na kadhalika.
Ebo! Kama unamwekea vigingi kwanini asitafute starehe mahali pengine? Mambo mengine baadhi ya wanawake wanachangia. Mwanaume ni mvumilivu sana hasa inapohusu mambo ya familia yake.
Lakini ukiona mwanaume anasema ‘inatosha’ ujue amefikiria mbali. Amevuta pumzi hadi za mwisho. Kwa maoni yangu kuhusiana na mwanamama huyo ni kwamba kama kweli mumewe amepania kumwachia mji, na hakuwa makini, mali zote zinazomzunguka zitatoweka kama umande.
Inavyoonekana mume huyo amepania kutengana na mwanamama huyu kwa sababu hizo nilizotaja hapo juu huku akionyesha kuwa zipo sababu nyingine zilizojificha ambazo hakutaka kuzitaja hadharani. Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.
Mpenzi msomaji wangu, hayo ndiyo yaliyojiri mwishoni mwa mwaka jana, baba huyu aliyepania kumkimbia mkewe na kuhamia kijijini kisa eti anamnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumnyima haki yake ya unyumba.
Kama hayo ni kweli, basi mwanamama huyo amemkosea sana mumewe na anapaswa kujilaumu kwa uamuzi wowote atakaochukua. Kila mtu anapenda kuishi kwa raha bila bughudha. Maisha yenyewe ni mafupi sana hivyo hayahitaji masharti ya kisanii. Jipe raha na mpe pia raha mwenzako. Maisha Ndivyo Yalivyo.
fwingia@yahoo.com
Wednesday, September 09, 2009
Kumuiba Mke au Mume wa Mwenzako ni Ufisadi!

Kutoka ippmedia.com
Kwa tafsiri yangu nyepesi nyepesi, ufisadi ni wizi, udanganyifu, ulaghai, ubadhirifu, umaaluni, ufedhuli, ubaradhuli na mengineyo yanayofanana na hayo. Vitendo vyote hivyo siyo tu vinafanywa na baadhi ya watu dhidi ya serikali na taasisi za umma, bali pia dhidi ya mke au mume wa mwenzako. Unabisha? Subiri nikutoholee.
Naam, mpenzi msomaji, nimeanza kuchombeza hivyo ujiandae kwa vionjo vinavyodhihirisha kirusi cha ufisadi kinavyozitafuna pia familia zetu. Kirusi hiki, ama kinabomoa nyumba zetu au kuzitia nyufa, na zaidi kinazisambaratisha kwa baba na mama, kila mmoja kufikia hatua ya kutafuta sehemu ya kujishikiza nje ya ndoa.
Kwanini hali hii inatokea? Je, ni umasikini ndani ya familia? Au ni utajiri umewakolea kiasi cha kupagawa na hivyo kutafuta maisha mbadala pembezoni? Au ni kitu gani hasa! Majibu yote haya msomaji wangu utayapata ndani ya mtiririko wa makala hii.
Hivi majuzi yupo fundi ujenzi wangu alinisimulia kisa kimoja ambacho kilinivuta kimawazo nikaona nikimwage hapa, ili pengine kirekebishe wenye mwelekeo huo. Hakifurahishi, lakini kina mafundisho muhimu ya kimaisha.
Katika simulizi yake, fundi huyu anasema kwamba yupo baba mmoja wa makamo mwenye mke na watoto wake wanne, wawili ni wasichana. Wawili wako sekondari, wengine vyuo.
Familia hii ina mji kule Mbagala wenye nyumba ya kisasa yenye eneo lenye nafasi.
Jirani na nyumba yao wakaamua kuanzisha baa na duka. Hapo huja wateja kununua na kuondoka na wengine huketi na kupata vinywaji, nyama choma.
Wazee hawa(baba na mama) wa mji huu, nao mara kwa mara huwa sehemu ya wanywaji. Pale hupata fursa ya kukutana na wezee wenzao kubadilishana mawazo. Ni wakamata maji wazuri na yakiwakolea hawasiti kuzua mitafaruku.
Unajua tena, wagidaji pombe ikiwakolea adabu na heshima huchepuka, hivyo kutoa fursa kwa ibilisi kulaghai. Simile hutoweka kwa wengine na kuanza kuongea ovyo.
Unaweza kudhani wanapofanya hivyo wanatania kumbe ni kweli toka kwenye nafsi zao zilizolegezwa na kilevi. Mfano mtu anamwambia mke wa rafiki yake eti ‘nakutamani sana’, na maneno haya anayasema mbele ya mumewe.
Je, mume mtu ataelewa kuwa ni utani? Ipo mitafaruku iliyoibuka kutokana na utani wa aina hii. Na pengine aliyetamka maneno hayo hakuwa anatania bali alimaanisha hivyo kupitia ibilisi wake wa pombe.
Kwa maelezo ya fundi huyu, wazee wa familia ninayozungumzia mara nyingi wamekuwa wakizozana wakiwa wanakunywa kwenye baa yao hiyo na zaidi ni wivu. Hofu yao ni kwamba huenda kila mmoja anao wateja anaowahusudu wanapokuja kunywa mahali hapo.
Baba anamshuku mume kuwa anao kinamama anaoonekana kutaniana nao au kuongea nao sana na huenda mmojawao ni mpenziwe wa pembeni. Na baba vivyo hivyo huhisi kuwa mama ana wazee anaochekacheka nao sana au vijana na huenda wapo anaowahusudu. Ili mradi kila mmoja anamtilia shaka mwenzake.
Chanzo cha mzozo wote huu ni uwepo wa baa hiyo karibu na nyumbani. Pengine isingekuwepo na kila mmoja angevinjari kivyake na migongano ya aina hiyo isingeonekana.
Kwa mtizamo, mama ndiye anayeonekana chakaramu zaidi na mshekumsheku anapoona wanaume, tofauti na mumewe ambaye ni mpole, mkimya ila mpepesaji mzuri wa macho anapoona kinamama au wasichana wanapitapita mbele yake wakija kupata huduma kwenye baa hiyo.
Upole na ukimya wa baba huyo, ulimzidishia mkewe jeuri kwamba hawezi kufurukuta. Hata ndugu za mume hufikiria mara mbili mbili kwenda kumtembelea ndugu yao(mume) kutokana na ukali wa mke.
Ilitokea mama huyu akamgundua mumewe akimkazia macho mwanamama mmoja. Hali hiyo ambayo ilikuwa ikijirudia mara kadhaa, ilimfanya mke ampige marufuku mwanamke yule kutokanyaga kwenye baa yao.
Hisia kuhusu mahusiana ya baba huyo na mwanamke huyo zilipelekea mkewe kumbonda mara nyingi kila wanapokolewa pombe na kutafutiana vijisababu vya kukosana. Na kila zikizuka vurumai, baba huchukua kibegi chake na kutokomea. Inaelezwa kuwa huenda kulala gesti.
Lakini kumbe halali gesti huenda kujichimbia nyumbani kwa mwanamke yule yule anayesababisha mipasuko ndani ya nyumba yao. Na mwanamke huyo baada ya kufukuzwa kwenye baa ile akaapa kutomwacha mzee huyo hadi kieleweke.
Misukosuko ambayo mume huyo alikuwa akipata kwa mkewe ilikuwa kama kichocheo cha kuzidi kumpenda mwandani huyo wa pembezoni.
Fumba na kufumbua mwandani huyo akapata mimba na kukaa sawa mtoto akazaliwa. Mtoto dume.
Taarifa zilipomfikia mama mwenye nyumba inaelezwa hadi sasa ameshikwa na bumbuwazi, na mume naye ndiyo amekuwa mbogo haoni wala hasikii.
Tena humpasulia wazi kwamba nakwenda au nimetoka kwa mke mwenzio. Naye mwandani huyo kila anakopita anatangaza ushindi kwa kumuopoa mume wa mwanamke mwenzake. Ufisadi mkubwa huu. Inauma lakini maji yakimwagika si hayazoleki?
Mpenzi msomaji, huo ndio ufisadi niliogusia tafsiri zake nyepesi nyepesi mwanzoni mwa makala haya. Ukali wakati mwingine huleta kilio. Kumbe pengine hekima ingetumika hata mpasuko uliojitokeza ndani ya familia hii usingekuweko. Hii ni kutokana na ukweli kwamba hekima ni bora kuliko kutumia nguvu. Na kwamba afadhali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima kuliko kusikiliza kelele za mfalme katika kikao cha wapumbavu.
Ufisadi mwingine unaozibomoa nyumba zetu ni huu unaofanyika kupitia simu za kiganjani. Mtu anamdoea mke au mume wa mwenzake na kisha anatumia ujumbe wa simu kumchanganya.
Wenye mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa zao wameshaonja joto la kasheshe zinazotokana na ufisadi huu. Na wenye kiherehere zaidi ni wale washikaji wa nje ya ndoa. Hao huwa wakali kuliko wenye nyumba zao. Kisa wanawaonea wivu na wanaponogewa hudiriki kubomoa nyumba zilizojengwa kwa gharama kubwa.
Anachofanya yule dowezi ni kutafuta simu ya mke wa mshikaji wake na kumtumia maneno ya kashfa kumdhihirishia kuwa mumewe anamdhibiti. Tabia hii wanayo sana wanawake.
Mwingine hupagawa na kuamua ku-forward ujumbe aliotumiwa na mume wa mwanamke mwenzake ili kumringishia kuwa hayuko peke yake na kwamba mumewe anaye kila anapomhitaji. Huu ni ufedhuli, ubedui, umaaluni, ufirauni wa hali ya juu.
Nyumba nyingi zimejikuta katika mpasuko mkubwa kutokana na mahusiano nje ya ndoa. Nyumba inachipuka ndani ya nyumba(nyumba ndogo hizi). Hata mtu akiona mwenzake akapatwa na balaa fulani, badala ya kujifunza na kuepuka, naye hujitosa kama vile shamba la majaribio. Matokeo yake naye anatumbukia.
Kwa ujumla mipasuko ndani ya familia zetu tunaisababisha sisi wenyewe. Kama baba na mama wako imara, hawatamani vya nje, hata Mungu hubariki nyumba hiyo na kuwa imara. Zipo nyumba chache za aina hii. Nyingi ni zile zinazoiga eti kama yule kafanya vile kwanini na mimi nisifanye hivyo. Kumbuka kuiga tembo ku… utapasuka msamba. Au siyo? Maisha Ndivyo yalivyo.
Niishie hapa msomaji wangu niruhusu nawe uchangie maoni, au nipe kisa ukijuacho tukijadili kwa pamoja.
Niandikie:
flora.wingia@guardian.co.tz
Wasalaam.
Kwa tafsiri yangu nyepesi nyepesi, ufisadi ni wizi, udanganyifu, ulaghai, ubadhirifu, umaaluni, ufedhuli, ubaradhuli na mengineyo yanayofanana na hayo. Vitendo vyote hivyo siyo tu vinafanywa na baadhi ya watu dhidi ya serikali na taasisi za umma, bali pia dhidi ya mke au mume wa mwenzako. Unabisha? Subiri nikutoholee.
Naam, mpenzi msomaji, nimeanza kuchombeza hivyo ujiandae kwa vionjo vinavyodhihirisha kirusi cha ufisadi kinavyozitafuna pia familia zetu. Kirusi hiki, ama kinabomoa nyumba zetu au kuzitia nyufa, na zaidi kinazisambaratisha kwa baba na mama, kila mmoja kufikia hatua ya kutafuta sehemu ya kujishikiza nje ya ndoa.
Kwanini hali hii inatokea? Je, ni umasikini ndani ya familia? Au ni utajiri umewakolea kiasi cha kupagawa na hivyo kutafuta maisha mbadala pembezoni? Au ni kitu gani hasa! Majibu yote haya msomaji wangu utayapata ndani ya mtiririko wa makala hii.
Hivi majuzi yupo fundi ujenzi wangu alinisimulia kisa kimoja ambacho kilinivuta kimawazo nikaona nikimwage hapa, ili pengine kirekebishe wenye mwelekeo huo. Hakifurahishi, lakini kina mafundisho muhimu ya kimaisha.
Katika simulizi yake, fundi huyu anasema kwamba yupo baba mmoja wa makamo mwenye mke na watoto wake wanne, wawili ni wasichana. Wawili wako sekondari, wengine vyuo.
Familia hii ina mji kule Mbagala wenye nyumba ya kisasa yenye eneo lenye nafasi.
Jirani na nyumba yao wakaamua kuanzisha baa na duka. Hapo huja wateja kununua na kuondoka na wengine huketi na kupata vinywaji, nyama choma.
Wazee hawa(baba na mama) wa mji huu, nao mara kwa mara huwa sehemu ya wanywaji. Pale hupata fursa ya kukutana na wezee wenzao kubadilishana mawazo. Ni wakamata maji wazuri na yakiwakolea hawasiti kuzua mitafaruku.
Unajua tena, wagidaji pombe ikiwakolea adabu na heshima huchepuka, hivyo kutoa fursa kwa ibilisi kulaghai. Simile hutoweka kwa wengine na kuanza kuongea ovyo.
Unaweza kudhani wanapofanya hivyo wanatania kumbe ni kweli toka kwenye nafsi zao zilizolegezwa na kilevi. Mfano mtu anamwambia mke wa rafiki yake eti ‘nakutamani sana’, na maneno haya anayasema mbele ya mumewe.
Je, mume mtu ataelewa kuwa ni utani? Ipo mitafaruku iliyoibuka kutokana na utani wa aina hii. Na pengine aliyetamka maneno hayo hakuwa anatania bali alimaanisha hivyo kupitia ibilisi wake wa pombe.
Kwa maelezo ya fundi huyu, wazee wa familia ninayozungumzia mara nyingi wamekuwa wakizozana wakiwa wanakunywa kwenye baa yao hiyo na zaidi ni wivu. Hofu yao ni kwamba huenda kila mmoja anao wateja anaowahusudu wanapokuja kunywa mahali hapo.
Baba anamshuku mume kuwa anao kinamama anaoonekana kutaniana nao au kuongea nao sana na huenda mmojawao ni mpenziwe wa pembeni. Na baba vivyo hivyo huhisi kuwa mama ana wazee anaochekacheka nao sana au vijana na huenda wapo anaowahusudu. Ili mradi kila mmoja anamtilia shaka mwenzake.
Chanzo cha mzozo wote huu ni uwepo wa baa hiyo karibu na nyumbani. Pengine isingekuwepo na kila mmoja angevinjari kivyake na migongano ya aina hiyo isingeonekana.
Kwa mtizamo, mama ndiye anayeonekana chakaramu zaidi na mshekumsheku anapoona wanaume, tofauti na mumewe ambaye ni mpole, mkimya ila mpepesaji mzuri wa macho anapoona kinamama au wasichana wanapitapita mbele yake wakija kupata huduma kwenye baa hiyo.
Upole na ukimya wa baba huyo, ulimzidishia mkewe jeuri kwamba hawezi kufurukuta. Hata ndugu za mume hufikiria mara mbili mbili kwenda kumtembelea ndugu yao(mume) kutokana na ukali wa mke.
Ilitokea mama huyu akamgundua mumewe akimkazia macho mwanamama mmoja. Hali hiyo ambayo ilikuwa ikijirudia mara kadhaa, ilimfanya mke ampige marufuku mwanamke yule kutokanyaga kwenye baa yao.
Hisia kuhusu mahusiana ya baba huyo na mwanamke huyo zilipelekea mkewe kumbonda mara nyingi kila wanapokolewa pombe na kutafutiana vijisababu vya kukosana. Na kila zikizuka vurumai, baba huchukua kibegi chake na kutokomea. Inaelezwa kuwa huenda kulala gesti.
Lakini kumbe halali gesti huenda kujichimbia nyumbani kwa mwanamke yule yule anayesababisha mipasuko ndani ya nyumba yao. Na mwanamke huyo baada ya kufukuzwa kwenye baa ile akaapa kutomwacha mzee huyo hadi kieleweke.
Misukosuko ambayo mume huyo alikuwa akipata kwa mkewe ilikuwa kama kichocheo cha kuzidi kumpenda mwandani huyo wa pembezoni.
Fumba na kufumbua mwandani huyo akapata mimba na kukaa sawa mtoto akazaliwa. Mtoto dume.
Taarifa zilipomfikia mama mwenye nyumba inaelezwa hadi sasa ameshikwa na bumbuwazi, na mume naye ndiyo amekuwa mbogo haoni wala hasikii.
Tena humpasulia wazi kwamba nakwenda au nimetoka kwa mke mwenzio. Naye mwandani huyo kila anakopita anatangaza ushindi kwa kumuopoa mume wa mwanamke mwenzake. Ufisadi mkubwa huu. Inauma lakini maji yakimwagika si hayazoleki?
Mpenzi msomaji, huo ndio ufisadi niliogusia tafsiri zake nyepesi nyepesi mwanzoni mwa makala haya. Ukali wakati mwingine huleta kilio. Kumbe pengine hekima ingetumika hata mpasuko uliojitokeza ndani ya familia hii usingekuweko. Hii ni kutokana na ukweli kwamba hekima ni bora kuliko kutumia nguvu. Na kwamba afadhali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima kuliko kusikiliza kelele za mfalme katika kikao cha wapumbavu.
Ufisadi mwingine unaozibomoa nyumba zetu ni huu unaofanyika kupitia simu za kiganjani. Mtu anamdoea mke au mume wa mwenzake na kisha anatumia ujumbe wa simu kumchanganya.
Wenye mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa zao wameshaonja joto la kasheshe zinazotokana na ufisadi huu. Na wenye kiherehere zaidi ni wale washikaji wa nje ya ndoa. Hao huwa wakali kuliko wenye nyumba zao. Kisa wanawaonea wivu na wanaponogewa hudiriki kubomoa nyumba zilizojengwa kwa gharama kubwa.
Anachofanya yule dowezi ni kutafuta simu ya mke wa mshikaji wake na kumtumia maneno ya kashfa kumdhihirishia kuwa mumewe anamdhibiti. Tabia hii wanayo sana wanawake.
Mwingine hupagawa na kuamua ku-forward ujumbe aliotumiwa na mume wa mwanamke mwenzake ili kumringishia kuwa hayuko peke yake na kwamba mumewe anaye kila anapomhitaji. Huu ni ufedhuli, ubedui, umaaluni, ufirauni wa hali ya juu.
Nyumba nyingi zimejikuta katika mpasuko mkubwa kutokana na mahusiano nje ya ndoa. Nyumba inachipuka ndani ya nyumba(nyumba ndogo hizi). Hata mtu akiona mwenzake akapatwa na balaa fulani, badala ya kujifunza na kuepuka, naye hujitosa kama vile shamba la majaribio. Matokeo yake naye anatumbukia.
Kwa ujumla mipasuko ndani ya familia zetu tunaisababisha sisi wenyewe. Kama baba na mama wako imara, hawatamani vya nje, hata Mungu hubariki nyumba hiyo na kuwa imara. Zipo nyumba chache za aina hii. Nyingi ni zile zinazoiga eti kama yule kafanya vile kwanini na mimi nisifanye hivyo. Kumbuka kuiga tembo ku… utapasuka msamba. Au siyo? Maisha Ndivyo yalivyo.
Niishie hapa msomaji wangu niruhusu nawe uchangie maoni, au nipe kisa ukijuacho tukijadili kwa pamoja.
Niandikie:
flora.wingia@guardian.co.tz
Wasalaam.
Tuesday, July 01, 2008
Kuolewa siku hizi ni fasheni au kuondoa nuksi?
Mwandishi wa habari, Flora Wingia, anauliza na kuchambua swali nzito. Inafurahisha kweli kweli.
**********************************************
Kutoka ippmedia.com
Eti wanaoolewa siku hizi ni fasheni ya kuondoa nuksi?
2008-06-29
Na Anti Flora Wingia
Mpenzi msomaji, lipo jambo moja limenivutia kukumegea leo kuhusu ndoa za siku hizi. Huko tulikotoka kuolewa au kuoa lilikuwa ni tukio la baraka. Lakini siku hizi hali ikoje? Liko tukio moja nililosimuliwa kutoka huko Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo dada mmoja aliolewa siku ya Jumamosi, lakini siku mbili baadaye, yaani Jumanne akamwacha yule bwana na kutokomea kwa mwanaume mwingine. Kisa ni nini?
Msimulizi wa tukio hili anasema kuwa dada huyo japokuwa alikuwa na mchumba huyo waliyefunga naye ndoa, lakini hakuwa anampenda kwa dhati bali alikuwepo mwingine wa ubani, tena mume wa mtu aliyemzibua kimapenzi.
Kwa maelezo ya bibie eti mchumba yule hakumpenda ila alitaka afunge naye ndoa ili kuondoa nuksi na iwe kwenye kumbukumbu kwamba hata yeye aliwahi kuoewa kwa ndoa takatifu.
Mashuhuda wa harusi wa bibie huyo wanasema ndoa ilikuwa ya gharama kubwa na iliyofana lakini walishangazwa na taarifa kuwa ndoa imesambaratika na bibie kaenda kwa mshikaji wake ambaye ni mume wa mtu.
Inasemekana ndugu wa bwana harusi wamecharuka na kuapa kumrudisha bibi harusi kwa mumewe kwa gharama zozote zile. Na kwamba shugadadi huyo anayemzingua shemeji yao naye atakiona cha mtema kuni.
Hata hivyo, habari zingine zinadai kuwa bibie katu hatamrejea mumewe kwa kile alichodai, kwanza alitaka tu aolewe ndoa kuondoa nuksi na pili aliyemuoa hamridhishi kimapenzi.
Mpenzi msomaji, hayo ndiyo mambo na hakika maisha ndivyo yalivyo. Eti siku hizi kuolewa ni fasheni ya kuondoa nuksi. Wiki hii nilipata wasaa kusikiliza kipindi cha Longa mwanamume kwenye kituo cha televisheni cha ITV kikihusu baadhi ya kinamama kuwaachia watumishi wa nyumbani kufanya kazi ambazo zingepaswa kufanywa na wao.
Mfano, kumpokea baba arudipo kazini, kumwandalia baba chakula, kumwekea maji bafuni na hata kutandika kitanda. Eti kazi hizi zote alipaswa kuzifanya mama ili kumwepushia baba vishawishi vya kummezea mate housigeli. Nilipogusia jambo hili katika kikao Fulani na marafiki zangu juzi, mmoja akasema; ``Kinamama wengine wako katika nyumba zao tu kuweka rekodi kuwa wameolewa, lakini mapenzi hakuna``.
Mwingine akamdakia; ``wewe hujui ukiona hivyo ujue vituko vya mumewe vimemfika kooni. Pengine anapewa taarifa zake (mume) kuhusu nyendo zake za kihuni huko nje, au mume yule hamjali tena kama mwanzoni walipooana na kadhalika``.
Mwingine akapigilia msumari kwa kusema; ``katika nyumba nyingine ukiona mama hajali kumhudumia mumewe nyumbani, basi ujue anaye mshikaji nje ya ndoa anayemzingua hivyo mume si chochote. Bibie niliyemzungumzia mwanzoni mwa makala hii yeye hakutaka aone vurugu za ndoa ndio sababu akaamua kujiengua mapema na kwenda kumuegemea shugadadi wake.
Lakini swali ni je, haya ndiyo maisha tunayotaka? Hizi fasheni za maisha eti kuondoa nuksi zinatoka wapi? Je, huku ni kuondoa nuksi au ni kuharibiana kimaisha? Kwa ujumla yule mama anayempiga chenga mumewe ndani na kuchepuka kwa bwana wa pembeni, sidhani ana amani yoyote rohoni mwake.
Hali kadhalika yule bibie aliyemtosa mumewe wa ndoa muda mfupi na kukimbilia kwa mume wa mtu, bado atapata vikwazo na vishawishi vya kusaka mabwana wengine. Kama hukutosheka na mmoja ndio utatosheka na wanaume wengine lukuki?
Upo msemo mmoja wa mtaani usemao ``Nimezunguka bucha zote lakini nyama ni ile ile``. Hii ikimaanisha kuwa kile baadhi ya kinamama wanachokimbia kwenye nyumba zao ndio hicho hicho watakikuta kule waendako. Mpenzi msomaji, kinachotakiwa ni watu kuheshimu nyumba zao.
Mke au mume ulimtupia jicho mwenyewe, ukampenda sasa wamtilia shaka ya nini? Si maji uliyavulia nguo, sasa kwa nini uogope kuyaoga? Hakika Maisha Ndivyo Yalivyo. Kuolewa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu siyo fasheni wala kuondoa nuksi kama baadhi yetu wanavyodai. Hata mababu zetu walifurahia sana ndoa na zilidumu tofauti na sasa ambapo tukio hilo linapewa uzito mdogo.
Siyo siri kuwa baadhi ya watu wanaoa au kuolewa lakini wanajenga au wanaendeleza mahusiano ya nje ya ndoa. Raha gani wanapata huko, wahusika wanajua. Faida gani wanapa ndio pamoja na maambukizi ya magonjwa hatari kama Ukimwi. Habari ndiyo hiyo.
Mpenzi msomaji, kwa leo naomba niishie hapa tukutane tena wiki ijayo. Ukiwa na maoni, ushauri usiache kunikandamizia kupitia email ifuatayo;
fwingia@yahoo.com. Wasalaam.
SOURCE: Nipashe
**********************************************

Eti wanaoolewa siku hizi ni fasheni ya kuondoa nuksi?
2008-06-29
Na Anti Flora Wingia
Mpenzi msomaji, lipo jambo moja limenivutia kukumegea leo kuhusu ndoa za siku hizi. Huko tulikotoka kuolewa au kuoa lilikuwa ni tukio la baraka. Lakini siku hizi hali ikoje? Liko tukio moja nililosimuliwa kutoka huko Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo dada mmoja aliolewa siku ya Jumamosi, lakini siku mbili baadaye, yaani Jumanne akamwacha yule bwana na kutokomea kwa mwanaume mwingine. Kisa ni nini?
Msimulizi wa tukio hili anasema kuwa dada huyo japokuwa alikuwa na mchumba huyo waliyefunga naye ndoa, lakini hakuwa anampenda kwa dhati bali alikuwepo mwingine wa ubani, tena mume wa mtu aliyemzibua kimapenzi.
Kwa maelezo ya bibie eti mchumba yule hakumpenda ila alitaka afunge naye ndoa ili kuondoa nuksi na iwe kwenye kumbukumbu kwamba hata yeye aliwahi kuoewa kwa ndoa takatifu.
Mashuhuda wa harusi wa bibie huyo wanasema ndoa ilikuwa ya gharama kubwa na iliyofana lakini walishangazwa na taarifa kuwa ndoa imesambaratika na bibie kaenda kwa mshikaji wake ambaye ni mume wa mtu.
Inasemekana ndugu wa bwana harusi wamecharuka na kuapa kumrudisha bibi harusi kwa mumewe kwa gharama zozote zile. Na kwamba shugadadi huyo anayemzingua shemeji yao naye atakiona cha mtema kuni.
Hata hivyo, habari zingine zinadai kuwa bibie katu hatamrejea mumewe kwa kile alichodai, kwanza alitaka tu aolewe ndoa kuondoa nuksi na pili aliyemuoa hamridhishi kimapenzi.
Mpenzi msomaji, hayo ndiyo mambo na hakika maisha ndivyo yalivyo. Eti siku hizi kuolewa ni fasheni ya kuondoa nuksi. Wiki hii nilipata wasaa kusikiliza kipindi cha Longa mwanamume kwenye kituo cha televisheni cha ITV kikihusu baadhi ya kinamama kuwaachia watumishi wa nyumbani kufanya kazi ambazo zingepaswa kufanywa na wao.
Mfano, kumpokea baba arudipo kazini, kumwandalia baba chakula, kumwekea maji bafuni na hata kutandika kitanda. Eti kazi hizi zote alipaswa kuzifanya mama ili kumwepushia baba vishawishi vya kummezea mate housigeli. Nilipogusia jambo hili katika kikao Fulani na marafiki zangu juzi, mmoja akasema; ``Kinamama wengine wako katika nyumba zao tu kuweka rekodi kuwa wameolewa, lakini mapenzi hakuna``.
Mwingine akamdakia; ``wewe hujui ukiona hivyo ujue vituko vya mumewe vimemfika kooni. Pengine anapewa taarifa zake (mume) kuhusu nyendo zake za kihuni huko nje, au mume yule hamjali tena kama mwanzoni walipooana na kadhalika``.
Mwingine akapigilia msumari kwa kusema; ``katika nyumba nyingine ukiona mama hajali kumhudumia mumewe nyumbani, basi ujue anaye mshikaji nje ya ndoa anayemzingua hivyo mume si chochote. Bibie niliyemzungumzia mwanzoni mwa makala hii yeye hakutaka aone vurugu za ndoa ndio sababu akaamua kujiengua mapema na kwenda kumuegemea shugadadi wake.
Lakini swali ni je, haya ndiyo maisha tunayotaka? Hizi fasheni za maisha eti kuondoa nuksi zinatoka wapi? Je, huku ni kuondoa nuksi au ni kuharibiana kimaisha? Kwa ujumla yule mama anayempiga chenga mumewe ndani na kuchepuka kwa bwana wa pembeni, sidhani ana amani yoyote rohoni mwake.
Hali kadhalika yule bibie aliyemtosa mumewe wa ndoa muda mfupi na kukimbilia kwa mume wa mtu, bado atapata vikwazo na vishawishi vya kusaka mabwana wengine. Kama hukutosheka na mmoja ndio utatosheka na wanaume wengine lukuki?
Upo msemo mmoja wa mtaani usemao ``Nimezunguka bucha zote lakini nyama ni ile ile``. Hii ikimaanisha kuwa kile baadhi ya kinamama wanachokimbia kwenye nyumba zao ndio hicho hicho watakikuta kule waendako. Mpenzi msomaji, kinachotakiwa ni watu kuheshimu nyumba zao.
Mke au mume ulimtupia jicho mwenyewe, ukampenda sasa wamtilia shaka ya nini? Si maji uliyavulia nguo, sasa kwa nini uogope kuyaoga? Hakika Maisha Ndivyo Yalivyo. Kuolewa ni baraka toka kwa Mwenyezi Mungu siyo fasheni wala kuondoa nuksi kama baadhi yetu wanavyodai. Hata mababu zetu walifurahia sana ndoa na zilidumu tofauti na sasa ambapo tukio hilo linapewa uzito mdogo.
Siyo siri kuwa baadhi ya watu wanaoa au kuolewa lakini wanajenga au wanaendeleza mahusiano ya nje ya ndoa. Raha gani wanapata huko, wahusika wanajua. Faida gani wanapa ndio pamoja na maambukizi ya magonjwa hatari kama Ukimwi. Habari ndiyo hiyo.
Mpenzi msomaji, kwa leo naomba niishie hapa tukutane tena wiki ijayo. Ukiwa na maoni, ushauri usiache kunikandamizia kupitia email ifuatayo;
fwingia@yahoo.com. Wasalaam.
SOURCE: Nipashe
Thursday, September 13, 2007
Ujumbe kutoka Kaka Lazurus Mbilinyi 'Mawaidha kuhusu Ndoa'
Wapendwa wasomaji nimepata ujumbe huo kutoka kwa Kaka Lazarus Mbilinyi ambaye aliandika somo la NDOA NA UNYUMBA ambayo umeisoma kwenye blog hii:
http://swahilitime.blogspot.com/search/label/Mbilinyi
**************************************************************************
http://swahilitime.blogspot.com/search/label/Mbilinyi
**************************************************************************
Dada Chemi,
Mimi ndo Lazarus Mbilinyi niliyeandaa hilo somo la ndoa na nyumba na kwa bahati mbaya nilikuwa sijui kama linaweza kusomwa na mtu yoyote kwani katika kuliandaa niliandaa katika mazingira ya Tanzania na hasa vijijini na sehemu ambazo mwanamume anafanya kazi (ameajiriwa) na mwanamke ni mama wa nyumbani (anayejishughulisha na kazi zingine) na pia limeegemea zaidi katika familia za kikristo.
Naamini maoni ninayopata kutokana na hilo somo basi nitayafanyia kazi na kama inawezekana siku nyingine nitoe kitabu cha Ndoa na nyumbaHata hivyo nashukuru sana kwa kueneza ujumbe kwa watu wote ili wajue ndoa ni nini hilo nashukuru.
Kwa sasa nipo Canada kwa ajili ya shule niemfika hapa tarehe 1 Sept 2007 na naamini tutazidi kuwasiliana na pia nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu.
Asante sana kwa kazi njema ya kuelimisha jamii:
--
Lazarus P. Mbilinyi
Mimi ndo Lazarus Mbilinyi niliyeandaa hilo somo la ndoa na nyumba na kwa bahati mbaya nilikuwa sijui kama linaweza kusomwa na mtu yoyote kwani katika kuliandaa niliandaa katika mazingira ya Tanzania na hasa vijijini na sehemu ambazo mwanamume anafanya kazi (ameajiriwa) na mwanamke ni mama wa nyumbani (anayejishughulisha na kazi zingine) na pia limeegemea zaidi katika familia za kikristo.
Naamini maoni ninayopata kutokana na hilo somo basi nitayafanyia kazi na kama inawezekana siku nyingine nitoe kitabu cha Ndoa na nyumbaHata hivyo nashukuru sana kwa kueneza ujumbe kwa watu wote ili wajue ndoa ni nini hilo nashukuru.
Kwa sasa nipo Canada kwa ajili ya shule niemfika hapa tarehe 1 Sept 2007 na naamini tutazidi kuwasiliana na pia nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu.
Asante sana kwa kazi njema ya kuelimisha jamii:
--
Lazarus P. Mbilinyi
Thursday, September 06, 2007
Mawaidha kuhusu Ndoa - Sehemu ya Pili

SIFA ZA MWANAMKE (SIFA NJEMA)
1. Awe mwema - Mith 12:4, 31:10 -30
2. Mwenye hekima - Mith 14:1 16:5,24
3. Mwenye adabu - Mith 19:14, 11:16a
4. Mwenye busara - Mith 19:14
5. Awe mkarimu - Mith 22:9
6. Msafi (mwili na nyumba)
7. Mpole - Mith 15:1
8. Mwenye huruma
9. Mdadisi
10. Mvumilivu
11. Mcheshi (kiasi)Yampasa mke aanze siku kwa kauli nzuri hata kama anaumwa:-
- Amusalimie mume
- Amwage mumewe akimtakia kazi njema baada ya kumuandalia
(a) Maji ya kuoga
(b) Kifungua kinywa
(c) Nguo za kuvaa siku hiyo
Mume atokapo kazini:-
(a) Mkaribishe kwa tabasamu, mkaribishe kwa furaha.
(b) Mpigipige mgongoni
(c) Vaa nguo nzuri (mwanaume hupenda anachoona) macho huvutiwa kwa kuona
(d) Waeleze watoto wako unavyompenda baba yao ( watoto nao watawapenda wote)
(e) Kila mmoja wenu ajue kile anachopenda ua anachotaka
ILI KUMHESHIMU MUME
KAWAIDA MWANAMKE
9. SIFA ZA MWANAUME
1. Mpole
2. Asiwe mwepesi wa hasira
3. Mcheshi
4. Anayeshaurika
5. Anayewajali watu wa nyumbani mwake (mahitaji)
6. Aliye na shukurani na kusifu (kwa lolote jema alilolitenda mkewe)
7. Anayeaga aondokapo kwenda matembezini au kazini au popote.
10. WAJIBU WA WA MUME KWA MKEWE
1. KUPENDA - kwa kiwango cha Kristo kwa kanisa Efe 5:25 matatizo mengi hutokea kwa sababu watu hawajui maana na jinsi ya kupenda kupenda ni matendo (action) siyo kujisikia au kuhisi ni kufanya vitu vizuri kama vile kutoa, kutabasamu, kusamehe nk Yohana 3:16
2. KIONGOZI (KICHWA) MTAWALA - Mume ni kichwa cha mke Efe 5:23 Naye atakutawala Mwanz 3:16c Amri hii hairekebiki kwa kelele za UWT kudai usawa ila utekelezapo maagizo ya Kristo amri amri ya kutawaliwa inakufa
3. MLINZI WA MKEWE - Kama chombo kisicho na nguvu, 1pet 3:7, Naye ni mwokozi wa mwili Efes 5:23 Mke hujiona salama awapo na mumewe Isay 4:1 Hivyo mume mlinde mkeo na maadui wa ndani na nje kama vile baba na mama, mashemeji/mawifi na marafik
4. KUTUNZA FAMILIA. Kuhakiki familia inapata chakula cha kutosha, malazi, mavazi na elimu kwa watoto Mwanzo 3: 17
5. KUMPAMBA MKEWE - mume sharti ampambe mkewe apendeze ili aweze kuvutia (amununulie vipodozi, nguo nk)
KAWAIDA MWANAUME:
12. WAJIBU WA MKE KWA MUMEWE KUTII - Kumtii mume kama kumtii kristo Bwana Yesu efe 5:22 watu huchanganya sana neon kutii na kuheshimu. Kutii kunakosemwa hapa ni kuwa endapo wawili mume na mke mmeshindwa kufikia uamuzi wa pamoja, basi,basi mke atatii uamuzi wa mumewe kama vile wamekubaliana awali
KULEA WATOTO (FAMILIA)
(a) Kuhakikisha afya ya mumeo na watoto
(b) Kuhakikisha kuwa chakula kinaliwa kwa wakati na kizuri
(c) Kuhakikisha usafi wa malazi, mavazi na miili yao
(d) Kufundisha watoto maneno ya Mungu
(e) Kuchunguza nyendo na tabia za watoto na mumeo na kuchukua tahadhari mapema.
KUMSHAURI MUMEO
Mke mwenye busara ni mshauri mwema kwa mumewe. Hatatoa ushauri wa kuleta maangamizi. Ushauri unafaa lakini ushauri mwingine upimwe kabla ya kufanyia kazi. Ona mashauri mabaya ya wanawake kwa waume zao
(f) Hawa kwa Adamu - Mwanza 3:17 (kula tunda)
(g) Sara kwa Ibrahimu - Mwanzo 16: 1-3 kulala na mjakazi (tabu ya mashariki ya kati)
(h) Yezebeli kwa mfalme Ahabu - 1Falm 21:22/2Falm 9:10
(i) Zereshi kwa Hamani mumewe kwa habari ya Mordekai Esta 5:14, 7:9-10
(j) Mkewe Ayubu kwa ayubu mumewe - Ayubu aliukataa ushauri wa mkewe. Ayubu 2:9
13. ADUI WA NDOA NI:-UTAJIRI - Tajiri hupendwa na wasichana na pia huwa na tamaa ya kutafuta fedha kiasi cha kukosa muda na mkewe
UMASKINI - kazi ya kutafuta lishe ni ya baba, hivyo hushughulika sana na kujikuta amekuwa baba zaidi kuliko kuwa mume
MADARAKA - madaraka ya ofisini huyaleta hadi nyumbanini chukuzo kwa mume/mke. Maafisa hawana muda na wake zao kwa sababu ya makongamano/semina/ziara mbalimbali.
- Hivyo wake zao wengi hutumia madereva kukidhi haja zao za kimwili
- Mke ambaye ni ofisa humwachia house girl kazi za kupika, kufagia chumbani, kupeleka maji bafuni na hata kutandika kitanda, hivyo kusababisha mke kupinduliwa na house girl.
MAMBO YANAYOWAKERA WAKE ZETU
1. Awe mwema - Mith 12:4, 31:10 -30
2. Mwenye hekima - Mith 14:1 16:5,24
3. Mwenye adabu - Mith 19:14, 11:16a
4. Mwenye busara - Mith 19:14
5. Awe mkarimu - Mith 22:9
6. Msafi (mwili na nyumba)
7. Mpole - Mith 15:1
8. Mwenye huruma
9. Mdadisi
10. Mvumilivu
11. Mcheshi (kiasi)Yampasa mke aanze siku kwa kauli nzuri hata kama anaumwa:-
- Amusalimie mume
- Amwage mumewe akimtakia kazi njema baada ya kumuandalia
(a) Maji ya kuoga
(b) Kifungua kinywa
(c) Nguo za kuvaa siku hiyo
Mume atokapo kazini:-
(a) Mkaribishe kwa tabasamu, mkaribishe kwa furaha.
(b) Mpigipige mgongoni
(c) Vaa nguo nzuri (mwanaume hupenda anachoona) macho huvutiwa kwa kuona
(d) Waeleze watoto wako unavyompenda baba yao ( watoto nao watawapenda wote)
(e) Kila mmoja wenu ajue kile anachopenda ua anachotaka
ILI KUMHESHIMU MUME
- Muombee kila siku - Yeye alivyo hekima, busara, ulinzi, baraka, ujuzi, kuelewa, kiroho, mafanikio, kushinda majaribu nk - angalia na tarajia majibu ya maombi - Mshukuru Mungu kwa kazi anayofanya kwa familia yako - Mshukuru Mungu kwa ajili ya Mume wako- ombea mtazamo wako.
- Kumbuka Mungu amemuweka mume wako kuwa kiongozi wa nyumba yako pamoja na wewe.
- Angalia sifa za mumeo na uzikubali na ongeza mara kwa mara
- Mwambie mumeo ni namna gani unamfurahia na kumpenda
- Usitoe sifa zake mbaya mbele za watu au kubisha
- Mtie moyo na kuwa msaaada wakati wa jambo gumuJihadhari na jinsi unavyomuuliza maswali
- Changamkia pale anapoonesha upendo
- Fikiria mambo mazuri juu ya mumeo
- Thamini vitu anavyovipenda na asivyovipenda Mith 12:4
KAWAIDA MWANAMKE
- Usitegemee starehe nyingi kama zile ulizokuwa unapata kwa wazazi wako au ndugu zako
- Utakuwa na juhudi katika kujenga nyumba ya mume wako uliye naye. Mith 14: 1 Kila mwanamke aliye na heshima.......................
- Hutakuwa mgomvi na mchokozi wala kumpiga mumeo kwa mwiko Mith 21:19
- Utampa mume wako haki yake 1Kor 7:3-5
- Thamani ya mumeo ni zaidi ya wanaume wote. Ez 16:32
- Umtii mumeo kwa Roho ya upole na unyenyekevu 1Pet 3:1-4
- Usimuruhusu mtu yeyote atambue kwamba unao wakati mgumu ( siri za ndani zisitoke nje) 1pet 5:9
- Utahaakikisha macho yako yanamwangalia mumeo wakati amevaa kabla ya kutoka kwenda kazini au kutembea
- Utajitoa na kumtii mumeo kwa moyo wote na kumruhusu kuwa kichwa cha nyumba Kol 3:18, 1pet 3:6, Ef 5: 33
- Utahakikisha mumeo ni bora kuliko watu wengine Fil 2:3, Wimb 5: 9-16
- Mwanaume ni dereva wa gari la ndoa na mwanamke anaweza akashauri na kupednekeza njia ya kupita na siyo kunyang'anya usukani
9. SIFA ZA MWANAUME
1. Mpole
2. Asiwe mwepesi wa hasira
3. Mcheshi
4. Anayeshaurika
5. Anayewajali watu wa nyumbani mwake (mahitaji)
6. Aliye na shukurani na kusifu (kwa lolote jema alilolitenda mkewe)
7. Anayeaga aondokapo kwenda matembezini au kazini au popote.
10. WAJIBU WA WA MUME KWA MKEWE
1. KUPENDA - kwa kiwango cha Kristo kwa kanisa Efe 5:25 matatizo mengi hutokea kwa sababu watu hawajui maana na jinsi ya kupenda kupenda ni matendo (action) siyo kujisikia au kuhisi ni kufanya vitu vizuri kama vile kutoa, kutabasamu, kusamehe nk Yohana 3:16
2. KIONGOZI (KICHWA) MTAWALA - Mume ni kichwa cha mke Efe 5:23 Naye atakutawala Mwanz 3:16c Amri hii hairekebiki kwa kelele za UWT kudai usawa ila utekelezapo maagizo ya Kristo amri amri ya kutawaliwa inakufa
3. MLINZI WA MKEWE - Kama chombo kisicho na nguvu, 1pet 3:7, Naye ni mwokozi wa mwili Efes 5:23 Mke hujiona salama awapo na mumewe Isay 4:1 Hivyo mume mlinde mkeo na maadui wa ndani na nje kama vile baba na mama, mashemeji/mawifi na marafik
4. KUTUNZA FAMILIA. Kuhakiki familia inapata chakula cha kutosha, malazi, mavazi na elimu kwa watoto Mwanzo 3: 17
5. KUMPAMBA MKEWE - mume sharti ampambe mkewe apendeze ili aweze kuvutia (amununulie vipodozi, nguo nk)
KAWAIDA MWANAUME:
- Utamheshimu mke wako kama mrithi pamoja na wewe katika neema ya uzima katika Kristo Yesu. 1Pet 3:7
- Mke wako ni mtu wa kwanza kwako siyo ndugu zako wala rafiki zako Mwanzo 2: 24 Mtaambatana na kuwa mwili mmoja
- Mara kwa mara utamwambia mke wako alivyo wa muhimu na thamani kwako Fil 2:3 , Mith 31: 10,11
- Utaendelea kumpenda kwa upendo ule wa kwanza wa wakati unampata. Wimb 5: m10 - 16
- Utakuwa kiongozi wa kusimamia nidhamu ya nyumba yako ukisaidiwa na mke wako. Efes 6:4
- Utakumbuka kutekeleza au kutimiza vile vitu vidogo ambavyo ulimwahidi mke wako kwamba utafanya Math 5: 37
- Macho yako yataelekea kwa mke wako tu na sivinginevyo. Mith 5: 15-20, Ayub 31:1, Yer 5:8
- Utafanya juhudi kusikiliza yale yaliyosemwa na mke wako. Mwanz 21:12
- Utambusu kila siku asubuhi kwa upendo. Wimb 8:1
- Hutakuwa mchungu likija swala la fedha. Est 5:3
12. WAJIBU WA MKE KWA MUMEWE KUTII - Kumtii mume kama kumtii kristo Bwana Yesu efe 5:22 watu huchanganya sana neon kutii na kuheshimu. Kutii kunakosemwa hapa ni kuwa endapo wawili mume na mke mmeshindwa kufikia uamuzi wa pamoja, basi,basi mke atatii uamuzi wa mumewe kama vile wamekubaliana awali
KULEA WATOTO (FAMILIA)
(a) Kuhakikisha afya ya mumeo na watoto
(b) Kuhakikisha kuwa chakula kinaliwa kwa wakati na kizuri
(c) Kuhakikisha usafi wa malazi, mavazi na miili yao
(d) Kufundisha watoto maneno ya Mungu
(e) Kuchunguza nyendo na tabia za watoto na mumeo na kuchukua tahadhari mapema.
KUMSHAURI MUMEO
Mke mwenye busara ni mshauri mwema kwa mumewe. Hatatoa ushauri wa kuleta maangamizi. Ushauri unafaa lakini ushauri mwingine upimwe kabla ya kufanyia kazi. Ona mashauri mabaya ya wanawake kwa waume zao
(f) Hawa kwa Adamu - Mwanza 3:17 (kula tunda)
(g) Sara kwa Ibrahimu - Mwanzo 16: 1-3 kulala na mjakazi (tabu ya mashariki ya kati)
(h) Yezebeli kwa mfalme Ahabu - 1Falm 21:22/2Falm 9:10
(i) Zereshi kwa Hamani mumewe kwa habari ya Mordekai Esta 5:14, 7:9-10
(j) Mkewe Ayubu kwa ayubu mumewe - Ayubu aliukataa ushauri wa mkewe. Ayubu 2:9
13. ADUI WA NDOA NI:-UTAJIRI - Tajiri hupendwa na wasichana na pia huwa na tamaa ya kutafuta fedha kiasi cha kukosa muda na mkewe
UMASKINI - kazi ya kutafuta lishe ni ya baba, hivyo hushughulika sana na kujikuta amekuwa baba zaidi kuliko kuwa mume
MADARAKA - madaraka ya ofisini huyaleta hadi nyumbanini chukuzo kwa mume/mke. Maafisa hawana muda na wake zao kwa sababu ya makongamano/semina/ziara mbalimbali.
- Hivyo wake zao wengi hutumia madereva kukidhi haja zao za kimwili
- Mke ambaye ni ofisa humwachia house girl kazi za kupika, kufagia chumbani, kupeleka maji bafuni na hata kutandika kitanda, hivyo kusababisha mke kupinduliwa na house girl.
MAMBO YANAYOWAKERA WAKE ZETU
- Wababa wenye madaraka kuyapeleka madaraka nyumbani
- Wake kuwajibika na mambo ya nyumbani kwa vile wana mishahara minono
- Wababa kutotenga muda wa kutosha kukaa na wake zao ili kuongea yanayowahusu
- Mume kumwachia mke kulea watoto hasa wakati wa usiku
- Mume kutomtia moyo mke wakati wa ujauzito
- Mume kumchanganya mama na watoto wa kike wanapokosa
- Mume kutokuwa na maandalizi mazuri wakati wa kukutana kimwili na mkeo
- Mume kujijari mwenyeweMume kusaidia ndugu zake bila mke wake kujua
- Mume kubagua watoto
- Mume kuwa na upendo na ukaribu au kucheka na binti waishio nao huku yupo mke wake
- Mume kutomshirikisha mkewe katika huduma yake ya ili aweze kumwombeaKutoonesha shukrani wala kutokuwa na msamaha
- Mume kutomtazama mkeo usoni mkiwa chumban
- iMume kuongea kiutani na wanawake wengine mkeo akiwa hayupo.
Subscribe to:
Posts (Atom)