
Tuesday, June 03, 2008
Obama atakuwa Mgombea wa Democrats!!!!

Saturday, May 24, 2008
Obama Hatarini?!

Ukiwa mgombea rais mweusi uko hatarini kuuliwa. Kwa kujua hivyo, Secret Service walitoa ulinzi kwa mgombea rais wa chama cha Democrats mapema. Obama amekuwa akilindwa kwa mieza 18 sasa.
Nchi hii kuna wabaguzi hasa. Yaani white supremacists wanaoamini kwamba mtu mweusi si bindamu na hasthili kuwa na chochote. Huwezi kuamini kuwa mwaka 2008 bado wapo. Sehemu zingine hapa Marekani huwezi kwenda na kuwa na uhakika wa kutoka na maisha yako ukiwa mweusi.
Ajabu, mpinzani wa Obama, Senator Hillary Clinton, amesema kuwa si ajabu watu kugombania nafasi ya mgombea hadi mwezi June, na kusema habari ya kuuliwa kwa Senator Robert F. Kennedy mwaka 1968. Sasa watu wameshutuka! Wametafsiri kuwa Clinton aikuwa na maana kuwa wakimwua Obama, yeye yupo kushika nafasi ya mgombea rais. DUH!
Kwa kweli watu wamemkasirikia Hillary kwa maneno yake.
Kwa habari zaidi someni:
http://blogs.abcnews.com/politicalpunch/2008/05/assassination-d.html
http://afp.google.com/article/ALeqM5jbMPoA_wjG3rgLbbsD-mT30oWfZA
http://ap.google.com/article/ALeqM5g-qGLDs-gAnZiUXD2NU51ry3j3dwD90RJVIO0
Thursday, May 08, 2008
Wazungu Wananitaka Mimi - Hilary Clinton

Na bado, sehemu kama Indiana kuwa watu ambao walisema kuwa hawawezi kumpigia mtu mweusi kura. Basi tu, kwa vile ni mweusi. History ya ubaguzi Marekani ni mbaya sana na ingawa siku hizi hali si mbaya kama ulivyokuwa bado upo!
Watu watauliza, "Unataka N-iga awe raisi wenu?" Na bado! Pia Hao masekreti service wamlinde maana wapo wale wazungu wabaguzi wenye siasa kali wanaotaka kumtungua, kisa mweusi!
****************************************************************
May 8, 2008
Clinton touts support from 'white Americans'
Posted: 12:03 PM ET
"I have a much broader base to build a winning coalition on," Clinton said in an interview with USA TODAY.
Clinton cited an Associated Press poll "that found how Senator Obama's support among working, hard-working Americans, white Americans, is weakening again, and how whites in both states who had not completed college were supporting me."
"There's a pattern emerging here," she said.
Exit polls from Tuesday's primaries in Indiana and North Carolina show Clinton won about 60 percent of the white vote in both states. That percentage is down from the Ohio primary on March 4, in which Clinton won upwards of 65 percent of the white vote. Meanwhile, Clinton garnered 63 percent of the white vote in Pennsylvania on April 22.
Speaking with the paper, Clinton rejected the notion her comments were racially divisive in any way.
"These are the people you have to win if you're a Democrat in sufficient numbers to actually win the election," she said. "Everybody knows that."
Obama spokesman Bill Burton called Clinton's statements "not true and frankly disappointing."
From: CNN Ticker Producer Alexander Mooney
Wednesday, March 05, 2008
Senator Hillary Clinton Afufuliwa! - Uchaguzi 2008

Jana Senator Clinton alishinda states za Ohio na Texas ambazo zina wajumbe wengi watakao piga kura katika mkutano mkuu wa Democrats mwezi Agosti. Hao ndo wanampitisha mgombea. Pamoja na ushindi wake Obama bado ana kura nyingi.
Kwa kweli sijafurahi hizi wiki mbili zilizopita kuona jinsi Mama Clinton alivyochafua jina la Obama. Mara aseme hawezi kuwa na uhakika kuwa si mwislamu. Na alifanya hivyo maksudi kwa vile alijua waMarekani ni waoga na waislamu baada ya mashambulizi ya 9/11. Halafu walifufua ile picha aliyopiga Kenya amevaa nguo za kiSomali mwaka 2006. Na kuna maovu mengine ambayo kampeni yake ilifanya.
Naomba mjue kuwa ubaguzi bado upo hapa Marekani. Hasa katika hizi states za Kaskazini. Sijui kama mlisikia yaliyotokea jana huko Ohio kwenye maeneo ya weusi. Weusi walijitokeza kwa wingi kupiga kura lakini walishindwa. Mfano, sehemu moja walikuwa na kura 50 na watu 300 walijitokeza. Hivyo watu wengi walishindwa kupiga kura. Ilibidi watu wa Obama wamwombe jaji aamuru shemu za kupiga kura zikae wazi kwa saa moja zaidi ili watu wapate nafasi ya kupiga kura. Matatizo kama hayo yalitokea hapa Massachusetts kwenye maeno ya weusi wakati Gavana wetu, Deval Patrick, alivyogombania.
Pia huko Ohio kulikuwa na matatizo kibao, hitilafu za mashine, matishio ya mabomu na mengine.
Halafu washenzi kama Rush Limbaugh, waliomba marepublicans wampigie Senator Clinton kusudi Obama asishinde. Alisema Clinton akishinda basi atazidi kumpaka matope Obama. Siasa bwana!
Leo, Hillary anadokeza kuwa kama atachuguliwa kuwa mgombea wa Democrats atamchagua Obama kuwa running mate, yaani makamu wake. Sijui kama mimi ningekuwa Obama ningekubali maana huyo Mama Clinton ameonyesha ana ukatili ndani yake. Yuko tayari kufanya chochote ili ashinde.
Pia Bush akiondoka January 2009, ataacha nchi na hali mbaya sana ya kiuchumi na kila kitu. Ambaye atashinda atakuwa na kazi kubwa mbele yake. Mungu ambariki atakayeshinda.
Tuesday, February 26, 2008
Kampeni ya Hillary wazua Mambo - Eti Obama ni Msomali!








Leo nimesikitika sana, tena mno, kusikia baadhi ya wazungu wakisema kuwa kumbe ni kweli Obama ni mwislamu. Oh kumbe yuko Al-Qaeda! Oh, kumbe kaelekea zaidi kwenye Uislamu. Kwenye WCVB TV Channel 5 hapa Boston, mtangazaji alisema kuwa kwenye hiyo picha Obama kavaa nguo za Middle East!
Kisa, kampeni ya Hillary wanazungusha picha kwenye neti ya Obama akiwa amevaa nguo za wazee wa kiSomali. Picha ilipigwa alipotembea huko Kenya mwaka 2006. Hivi Obama si MJaLuo?
Nimebandika picha za waheshimwa wakiwemo Hillary wakiwa wamevaa hijab na nguo zinge zi kiutamduni.
Kwa waongea kimombo:
Hey you ignoramuses out there, Mr. Obama's father is from the Luo tribe ofKenya! He is not a Somali. He was just visiting a group of people who live in Kenya and they showed him their respect!
Plus it is a sign of disrespect no to don the attire of the people you are visiting in some foreign lands. Take a look at the photos above!
Kwa habari zaidi someni:
http://youdecide08.foxnews.com/2008/02/25/photo-showing-obama-in-somali-garb-circulated-by-clinton-campaign-source/
http://www.news.com.au/couriermail/story/0,20797,23277403-952,00.html?from=public_rss
http://www.bayoubuzz.com/News/US/Politics/President_Race_2008/Hillary_Clinton_Over_Hill_With_Obama_Somali_Photo__5883.asp
http://bigheaddc.com/2008/02/25/drudge-falsely-accuses-clinton-of-obama-photo-ties/
Wednesday, February 06, 2008
Uchaguzi wa wagombea Rais Marekani - Hakuna mshindi kamili
Hivi kwa Dems, bado tunaye Obama na Clinton. Kwa Republicans bado wapo Huckabee, Romney na McCain.
Kwa habari zaidi soma:
http://www.cnn.com/2008/POLITICS/02/06/super.main/index.html
Tuesday, February 05, 2008
Leo ni Super Tuesday! - Nani atagombea Uraisi wa Marekani!





Wednesday, January 09, 2008
Hillary Clinton ashinda New Hampshire!

Tuesday, January 08, 2008
Inaelekea Obama kashindwa New Hampshire
Hillary ana 39% na Obama 36% za kura. Kwa upande wa Republicans Senator John McCain ameshinda.
Bado uchaguzi katika jimbo 48 zingine za Marekani.
Saturday, December 01, 2007
Ajisalimisha

Friday, November 30, 2007
Ofisi ya Hillary Clinton imetekwa nyara New Hampshire
Watu wawili wametekwa katika ofisi ya mgombea rais wa chama ca Democrats wa Marekani, Senator Hillary Clinton. Ofisi enyewe ni ya kampeni yake na iko Rochester, New Hampshire.
Sakata umeanza saa 7 mchana huu na hivyo navyoandika bado inaendelea. Mama moja aliyekuwa ndani ya hiyo ofisi na mtoto wake wa miezi sita aliachiwa huru pamoja na mtoto.
Jamaa aliyeteka nyara ofisi amejifunga mkanda ambayo anasema ina bomu! Ofisi sasa imezungukwa na polisi, SWAT (FFU) na Secret Service. Kama jamaa hajisalimishi msishangae mkisikia kuwa jamaa katunguliwa kwa kupigwa risasi kichwani na FFU.
Pia polisi wameamuru ofisi za wagombea rais wengine maDeomcrats, Barack Obama na John Edwards zifungwe kwa usalama wa raia na wafanyakazi.
Marekani bwana!
http://www.cnn.com/2007/POLITICS/11/30/clinton.office/index.html