Wednesday, February 17, 2010

Wateule wa Oscars 2010 Wala Chakula Pamoja!


Wadau, kila mwaka ni kawaida kwa walioteuliwa kupata tuzo ya Oscars kula chakula cha mchana pamoja. Leo walivigida huko Hollywood. Chakula chenyewe kina kuwa cha fahari kweli. Sherehe ya kujua nani kashinda na kutuza wasanii bora, na watengeneza sinema bora itaka siku ya jumapili, March 7, 2010.

Nangojea kwa hamu kumwona dada Mo'nique akishinda Oscar ya Best Supporting Actress. Mo'nique lazima ashinde maana hiyo kazi aliyofanya kwenye sinema Precious ni kiboko. Pia nina hamu ya kumwona Gabourey Sidibe akitembea kwenye Red Carpet. Akishinda Tuzo ya Mcheza sinema bora wa kike itakuwa maajabu. Nasmea hivyo kwa sababu kwanza ni mweusi, tena kwa hapa Marekani mweusi tii, mnene, na ni mara yake ya kwanza kuigiza katika sinema. Akimshinda Meryl Streep nitasema kweli Hollywood imebadilika.

No comments: