Saturday, October 19, 2013

Mwanangu Ameingia Siasa za Marekani.


Elechi Kadete




 Wadau, nafurahi kuwatangazia kuwa mwananagu, Elechi Kadete, ameamua kufuata nyayo za Babu yake, Dr. Aleck Che-Mponda, na kuingia katika dunia ya siasa. Anagombea kiti katika Baraza la Maashule (School Committee) katika mji wa Cambridge, Massachusetts. Akifanikiwa baadaye itakuwa rahisi kugombea nafasi katika City Council na kwenye ngazi za State. Kutokana na katiba ya Marekani hataweza kugombea Urais kwa vile hakuzaliwa Marekani. Alizaliwa Tanzania. Lakini ataweza kugombea nafasi zingine kama Congress, Senator na Gavana.

Baba mzazi wa Elechi, ni marehemu Prof. Henry Kadete aliyekuwa kuwa Mkuu wa Idara ya Uhandisi Umeme Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Alifariki mwaka 1995.  Kwao Prof. Kadete ni Tabora.

Kwa kweli naona watu Cambridge wanamchangamkia,  Tunaomba maombi na dua zenu Ashinde!

Kwa habari zaidi za kampeni ya Elechi:

-->
Email:ekfocusedonfuture@gmail.com
Facebook: The committee to Eelect Elechi Kadete
Twitter: Kadete_1
Telephone Number: (617)504-1679
Website: http://vote.cambridgecivic.com/kadete.htm


http://www.cambridgeday.com/2013/10/04/elechi-kadete-announces-candidacy-for-school-committee/

 Wadau, kampeni ni ghali, mabango, literature, simu, huduma kwa ajili ya wasaidizi zina gharama.

Ukitaka kutuma mchango tuma:

The Committee to Elect to Elechi Kadete
10 Laurel St. #4
Cambridge, MA 02139

Uchaguzi ni Jumanne, Novemba 5, 2013. 

No comments: