Showing posts with label Kigoma. Show all posts
Showing posts with label Kigoma. Show all posts

Sunday, June 01, 2014

Mwili wa Mama Yake Mbunge wa Kigoma Zitto Kabwe Wasafirisha Kwenda Kigoma

Zitto kabwe akiwa na Prof  Ibrahimu Lipumba wakati wa kuuaga Mwili wa mama yake kipenzi Bi Shida Salumu aliyefariki leo kabla ya kusafirishwa kwenda Kigoma kwa mazishi
Ndege Ikiandaliwa Ili kuweza Kuingiza Mwili wa Marehemu Mama yake Zitto Kabwe
Waheshimiwa Wabunge na Baadhi ya Viongozi wakibeba Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mama Yake Zitto Kabwe Bi Shida Salum  kuingiza kwenye ndege Tayari kwa safari ya kwenda Kigoma Kwenye mazishi
Prof Ibrahimu Lipumba akijadili jambo na Mwezie baada ya kupakia mwili wa marehemu kwenye ndege kuelekea kigoma Kwenye maziko


Rais wa TASWA Juma Pinto akiwa VIP ya Terminal 1 JKN Airport alipokutana na Cardinal Pengo wakati wa kuaga mwili wa Mama yake Zitto Kabwe
KWA HISANI YA: Dj Sek Blog P.O.BOX Dar es salaam IT DEPARTMENT

Saturday, December 21, 2013

Hotuba ya Mh. Zitto Kabwe Leo Huko Kigoma

 
Mh. Zitto Kabwe - File Photo


HOTUBA YA MH ZITTO Z. KABWE - KIGOMA – 21 DESEMBA 2013

Leo nina furaha kubwa sana kwani baada ya safari ndefu na yenye changamoto nimerudi nyumbani kuwasalimu wananchi wenzangu! Na hii si salamu za kawaida bali nawasalimu kwa salaam za demokrasia, uadilifu, uzalendo na uwajibikaji. Nawasalimu si kama mbunge bali kama mwana wenu wa Kigoma! Na popote niendapo najivunia kujitambulisha kama Mtanzania; kama mwenyeji wa mkoa wa Kigoma na zao la Ujiji.
 
Tuna mengi ya kujivunia kama taifa lakini Ujiji na watu wake mna nafasi ya pekee katika historia. Watu wa Ujiji mlipokea harakati za kudai uhuru wa nchi yetu mapema kabisa mapambano ya uhuru yalipoanza. Watu wa Ujiji mlikuwa wa kwanza kabisa kupokea mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Na Jimbo la Kigoma Mjini ilikuwa miongoni mwa majimbo ya mwanzo kabisa kutoa mbunge wa CHADEMA mwaka 1995. Kabla ya hapo mlitoa madiwani wengi mwaka 1994. Wakati Watanzania wengine wakiwa wanajiuliza mara mbili mbili kuhusu kujiunga na vyama vipya vilivyoanzishwa, watu wa Ujiji, watu wa Kigoma hamkusita kupokea mabadiliko. Wengi wamepoteza maisha yao, wengine kazi zao na wengine hata ndoa zao katika kupata mbegu ya mabadiliko katika nchi yetu. Nawataka msichoke. Wekeni nguvu mpya katika kusimika mabadiliko kwani bado kazi ya kuimarisha demokrasia katika nchi yetu haijaisha na inahitaji uvumilivu, kusameheana na kuaminiana.
 
Na nchi yetu Tanzania ni nchi inayoonyesha uwezo mkubwa katika kupendana, kuaminiana, kuvumiliana na hata kusameheana. Na haya si maneno tu ambayo ninayazungumza kama mwanasiasa. Hii ni hali halisi na maisha niliyoyaishi kwa mifano nilipokuwa ninakua na kusoma katika shule ya Msingi Kigoma na baadaye Shule ya Sekondari Kigoma. Malezi yangu yalikuwa yanaongozwa na jamii nzima ya Kigoma. Nimekuwa nikiwaeleza rafiki zangu niliokutana nao kwenye masomo na kwenye siasa kwamba nimeanza kuvaa viatu kwa mara ya kwanza nikiwa darasa la tatu. Viatu hivyo viliitwa 'asante Salim' vilivyokuwa vinatengenezwa na Kampuni ya Bora Shoes. Vililinunuliwa na mama Coretha Furugunya ambaye tulikuwa tunakaa mtaa mmoja wa Kisangani Mwanga. Mama Coretha hakuninunulia viatu kwa sababu alikuwa ana uwezo mkubwa, la hasha! Alifurahishwa na matokeo yangu ya mitihani ya darasa la pili kwenda la tatu. Ninaamini kitendo cha mama huyu ni ushahidi wa uungwana, upendo na hata uwajibikaji ambao tunao sisi watanzania. Uwajibikaji kwani alichukua jukumu kunilea ingawa hakuwa mzazi wangu, lakini aliona kuwa kama mwanajamii ana nafasi kubwa katika kuwaendeleza watoto wote. Jamii hii ya watu wa Kigoma ilinifunza kuwa nikijitahidi na kukazana kwa bidii kwenye masomo na majukumu, nitafanikiwa. Siwezi kusahau somo hili katika maisha yangu na ni somo hili ndilo limenifanya nijitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu kuwatumikia kwa uadilifu na mafanikio ya hali ya juu sana.
 
Nikiwa nimejaa matumaini haya kuhusu wananchi wenzangu, leo nataka niwakumbushe kwa nini kama jamii tulichagua kufuata njia ya demokrasia. Demokrasia ina maana pale ambapo inatumika kuleta mabadiliko chanya kwenye maisha ya wananchi. Maisha yanayotakiwa ni yale yanayomwezesha mwananchi kupata huduma zake stahili kama Elimu, Afya, Maji na miundombinu. Demokrasia haina maana pale wananchi wanakufa njaa kwa kukosa ajira na kukuza umasikini. Demokrasia inahusu maendeleo. Tumejitahidi kwa upande wetu kuondoa mkoa wa Kigoma kutoka mikoa isiyo na miundombinu kabisa ya maendeleo mpaka kuwa mkoa unaotumika kama mfano kwa miradi mingi ya Maendeleo ikiwemo Daraja la Malagarasi, Uwanja wa ndege wa Gombe-Mahale, barabara za lami na upanuzi wa Bandari, ujenzi wa bandari ndogo mpya na ujenzi wa kituo cha Usafirishaji Mwandiga. Asije mtu akasema yeye ndio kafanya haya. Haya ni matunda ya nyinyi watu wa Kigoma kupokea demokrasia na bila woga kuchagua viongozi wenu bila kujali vyama bali kwa kuangalia uwezo. Haya ni matunda ya viongozi wenu kupaza sauti yenu kwenye baraza la Taifa, Bunge. Haya ni matunda ya uvumilivu wenu na uamuzi wenu wa kutaka maendeleo. Juhudi hizi lazima ziendelezwe kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa nafasi ya mkoa wa Kigoma katika uchumi wa Tanzania inaonekana dhahiri na hivyo kuchochea maendeleo ya nchi yetu kwa kuwa kituo cha biashara katika nchi za maziwa makuu.
 
Lakini tukumbuke pia kuwa Demokrasia ni Uwajibikaji. Katika kipindi cha utumishi wangu kwenu,kutokana na malezi niliyoyapata kutoka kwenu,nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa Serikali inawajibika kwa Wananchi. Nakumbuka wakati napambana kuhusu sheria mbovu ya madini kuna watu hapa nyumbani walisema 'sasa huyu kawa mbunge wa Taifa' lakini watu wengi zaidi wakasema tumemtuma Dodoma kusemea Watanzania wote na sio Kigoma tu. Tuliweza ndani ya miaka mitano kufanya mabadiliko makubwa sana kwenye sera ya Madini na sheria ya madini ambapo baadhi ya mambo ambayo yalikuwa hayafikiriki sasa yametungiwa sheria ikiwemo Serikali kuwa na hisa kwenye migodi, Tanzanite kumilikiwa na Watanzania sio chini ya asilimia 50 na kuzuia kabisa wageni kuchimba vito vya thamani. Uwajibikaji ulipelekea kumshinikiza Rais kufanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri kwa kuwafukuza mawaziri wanane mwaka jana. Hii ilitokana sio tu na hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu bali pia ushiriki mkubwa wa wananchi kupitia simu na mitandao ya kijamii ambapo wabunge walishinikizwa kuweka saini kwenye karatasi za kumtoa Waziri Mkuu. Toka wakati huo kumekuwa na utaratibu sasa ambapo wabunge hawaoni taabu kutaka uwajibikaji waziwazi ili kuzuia ubadhirifu wa fedha za Umma. Ni hivi jana tumeshuhudia mawaziri wanne wamejiuzulu na kufukuzwa kazi kutokana na kashfa ya operesheni Tokomeza ujangili iliyoibuliwa na ripoti ya kamati ya bunge. Mabadiliko haya ni hatua muhimu katika kuimarisha demokrasia yetu.
Pamoja na matunda haya mengi mazuri lakini bado kuna changamoto katika juhudi zetu.
 
Changamoto kubwa tuliyonayo wananchi ni kukosekana kwa imani katika demokrasia yetu.
Kutoaminiana. Ni dhahiri kuwa kutoaminiana katika nchi yetu kumekuwa kwa kiasi kikubwa. Taarifa za kitafiti zinaonyesha kuwa katika kila Watanzania kumi, wanane hawaaminiani. Ni changamoto kubwa sana. Wananchi wameacha kutuamini wanasiasa na wanasiasa wameacha kuaminiana wenyewe kwa wenyewe. Hivi sasa uongo umegeuzwa kuwa ukweli na ukweli umekuwa ni uongo. Hivi sasa ukitaka kuwa mwanasiasa maarufu inabidi ujue kudanganya na ukitaka kuitwa mwanasiasa msaliti inabidi uwe msema kweli. Kukosekana kwa uaminifu na kuaminiana imekuwa ni kansa katika siasa zetu. Itachukua muda mrefu sana kujenga demokrasia imara katika nchi yetu kama hatutapata jibu la changamoto hii ya kutoaminiana na kugeuza uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa uongo. Hivi sasa ukweli umekuwa unatengenezwa badala ya kutafutwa. Ni majanga! Juzi bungeni Mwanasheria Mkuu wa Serikali alielekeza shutuma kwangu kwamba sikushirikiana na kamati maalum iliyoundwa na Bunge kufuatilia mabilioni ya uswisi na kwamba chini ya kiapo nilisema sina majina ya watu wenye akaunti huko Uswisi. Huu ulikuwa ni uongo. Ni uongo kwa sababu niliitika wito wa kamati hata nilipokuwa katika mafunzo ya mgambo huko Tanga na nilikutana nao mara nne. Ni uongo kwa sababu niliwapa wajumbe wa Kamati Maalaum maelezo na taarifa nyingi sana kuhusu utoroshwaji wa fedha nje ya nchi na umiliki wa mali nje ya nchi kinyumecha sheria. Ni uongo kwa sababu mimi kutotaja majina haya haina maana sina majina, bali ni kwamba ninaheshimu utaratibu na nimeachia vyombo husika vikamilishe uchunguzi. Kwani mimi kama mtu binafsi nikianza kuchukua majukumu ya taasisi ninaweza kutia dosari harakati hizi muhimu na hata kupelekea mchakato mzima kuvurugika. Sitaingia mtego huu! Lakini hatua hii ya Mwanasheria Mkuu imenipelekea kujiuliza maswali mengi kwa mfano uongo kama huu ulifanywa kwa malengo gani? Na ninajikuta hata mimi ninaingia katika hali ninayoilalamikia ya KUTOAMINIANA. 
 
Lakini mtambue pia kuwa kutoaminiana kunaleta kutovumiliana. Hivi sasa kuwa na mawazo tofauti katika vyama vya siasa au hata asasi za kijamii ni uhaini. Lakini bila kuenzi tofauti za mawazo hatuwezi kujenga vyama imara wala Taifa imara. Demokrasia imara ni zao la tofauti za mawazo na uhuru wa mawazo. Kama hatuwezi kujenga vyama vinavyorutubisha uhuru wa mawazo na tofauti za mawazo, tutajenga Taifa lenye watu wenye kuogopa na waliojaa woga. Wanachama wanapoogopa uongozi ni udikteta, lakini uongozi unapoogopa wanachama ni demokrasia. Bila demokrasia ya uwazi na kuvumiliana tutakuwa Taifa la kidikteta. Lazima vyama vya siasa, viongozwe kwa namna ile ile ambayo Taifa litaongozwa.
 
Demokrasia bila kuaminiana, demokrasia bila kuvumiliana sio demokrasia ya kweli.
Juzi nilipoingia Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya matukio kadhaa yanayoendelea ndani ya chama chetu nilikaa pamoja na mbunge Tundu Lissu. Wabunge wengine walidhani tutarushiana ngumi na badala yake ikawa ni vicheko na mazungumzo. Hii ni kwa sababu sina chuki na mtu yeyote yule. Mmenifunza kutojenga chuki na watu na badala yake kuchukua kila tukio kama changamoto ya maisha. Siasa ni kupambanisha mawazo tofauti na hatimaye kutafuta suluhu ya pamoja. Na siasa ina misingi yake ambayo sisi wanasiasa huwa tunasahau kwa maksudi. Msingi wa siasa ni kuwa inapaswa kuleta unafuu wa maisha ya wananchi na sio malumbano tu ya kurushiana maneno na kuzushiana ili kujijengea umaarufu wa kisiasa. Siasa si kuwekeana chuki na kuonyeshana ubabe.
Na hapo ni muhimu muelewa wanaKigoma mnapoambiwa kuwa eti ninapofuatilia mabilioni ya Uswisi ninatafuta umaarufu, ni uongo! Mnaposikia eti kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki na kujitafutia umaarufu, ni uongo! Kinachonisukuma kufanya vyote hivi ni ninyi. Ninasukuwa kila ninapowaona watoto bado wanatembea bila viatu;kila ninapoona akina mama wanapoteza maisha yao katika uzazi;kila ninapoona vijana ambao hawana uhakika wa kupata hata mlo moja kwa siku kwa kukosa kazi; ninapoona wazee wa Kigoma kukosa hata shilingi mia moja kununua chai asubuhi. Ninawaona si wanaKigoma bali mamilioni ya watanzania wakiishi katika hali hii. Alafu nalinganisha na taarifa tunazozipata kuhusu ufujaji na utoroshwaji wa pesa zetu. Hebu sasa linganisheni na ukweli kuwa ripoti ya kimataifa iliyotolewa hivi karibuni imeonyesha kuwa mwaka 2010 pekee, jumla ya dola za kimarekani milioni 1315 (bilioni 1.3), yaani shilingi trilioni  2,113,930,000,000 (sh trilioni 2.1) zilitoroshwa kutoka nchini Tanzania. Mwaka 2011 kiasi cha dola za kimarekani milioni 817 yani shilingi za kitanzania zipatazo trilioni 1,315,370,000,000 (trilioni 1.3) zilitoroshwa. Ripoti hiyo inaeleza kuwa jumla ya fedha za Watanzania zilizotoroshwa nje ya nchi katika miaka kumi iliyopita zilifikia dola za kimarekani milioni 4526 (bilioni 4.5) sawa na shilingi za kitanzania trilioni 7,286,860,000,000 (trilioni 7.3).  Nimewatajia hapa namba chungu nzima na matrilioni na mabilioni hayaleti maana. Lakini hii ina maana kwamba kiasi cha pesa zilizotoroshwa katika miaka 10 pesa - robo yake tuingeweza kujenga barabara ya lami ya kiwango cha juu kabisa kutoka Kigoma mpaka Dar-es-salaam! Pesa hizi zingeweza kuajiri na kuwalipa vizuri walimu, madaktari na wafanyakazi wengine ili kuhakikisha tunapata huduma bora na kutengeneza ajira bora kwa vijana wetu. Pesa hizi zingeweza kununua madawa muhimu na kuokoa maisha ya maelfu ya akina mama tunaowapoteza kila mwaka wakati wa uzazi. Pesa hizi zingeweza kuwanunulia watanzania wote si watoto tu angalau pea 10 ya viatu. Sasa nikitafakari haya siwezi kuchapa usingizi mnono na kufumbia macho utoroshwaji wa fedha au matumizi mabaya ya fedha za umma kwa njia ya sisi wabunge kujilipia posho! Hapana! Nafsi yangu hainiruhusu kukaa kimya kwa kuogopa kuitwa mbinafsi au msaliti!
 
Lakini naomba niwasihi kuwa katika nyakati kama hizi za changamoto za kisiasa jambo la msingi kuliko yote ni kutulia maana hakuna linalotokea bila sababu. Licha ya kwamba kuna watu wengi wanapaza sauti zao katika mambo haya lakini pia kuna wengi zaidi ambao wapo kimya lakini wana mawazo yao, ndani na nje ya chama chetu;ndani na nje ya Serikali na ndani nanje ya nchi yetu. Ndio maana lazima kuibadili nchi yetu ili kuweza kuhakikisha kila raia anakuwa na fursa ya kutoa mawazo na fikra zake zinakuwa huru.
 
Maisha ni mabadiliko; mabadiliko hayana ukomo; mabadiliko hayazuiliki kwa sababu bila mabadiliko hakuna ukuaji, bila mabadiliko hakuna maendeleo. Mabadiliko ni kiu kikubwa cha Tanzania kwa sababu mabadiliko huleta matumaini. Na kiu hii ni kubwa zaidi kwetu sisi vijana wa kizazi hiki kipya. Siasa za kizazi kipya cha viongozi ni siasa za majawabu ya kero za wananchi. Siasa za mabadiliko ni siasa za kujenga na kuimarisha; ni siasa za kuaminiana na kuheshimiana hata pale mnapopingana kimawazo. Ninataka tujenge siasa mpya Tanzania;siasa za mabadiliko; siasa zinazojenga matumaini ya kweli;siasa zinazowajali na kuwajengea uwezo wananchi wa Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

Thursday, July 04, 2013

Dar to Kigoma on Central Line takes Three Days

By Mdau A.L.




On 7th June at 10:31PM the adventure began, it hardly took an hour of motion, before we all lost control to the natural taste of sleep, due to trip preparation and tiresome 3 hrs of wait for the journey to begin nobody in my family of 4 could resist any longer.

When I worked up, an awkward voice of random collisions  and shaking of train compartment was growing stronger and stronger, I consulted my clock just to learn that it was 4:00AM on the next day. outside no sign of any building could be seen, just bushes and forests. The Train would remain silent for some 2 to 3 minutes before it begin another fruitless attempt to continue with the journey which would be stopped by loud sounds of collision at the compartment joints and skidding on the rails. 

This continues  with an increasing interval between attempts, until everybody was up at around 6AM.  We latter realized that we were still a long way before reaching Moro town. Later on, some random news was heard.. Engine has failed so another engine from Moro would be on duty soon. After a while we left the venue sluggishly. 

We reached Moro town at 1:00PM, in a very slow but chancy motion, full of shaking and chaotic collisions.  From Moro The same story continued the Engine was even weaker, as a results we reached Dom at 11:00PM and left the station of our capital just after the Mid night. This time a better engine was put on duty and we managed to arrive at Tabora Station at 9:00Am next day.

 The Final journey to Kigoma was unthinkable, a 16 hours trip. We left Tabora at 1:00PM and arrived Kigoma Station at 6:00AM the next day, while Uvinza-Kazuramimba only, took 6 hours due to similar reasons: engine powerlessness. While in Tabora, a hard a rare opportunity to chat with one of the senior TRL staff, who cautious hinted about the disaster of locomotives(engines). In short TRL is on its way to mutually if its ICU status is not updated soon.

On my way back, it took me only 10hour to Kahama plus 12 hours to Dar on the next day, as I have to spend a night in Kahama due to longer queue which requires more than a week to book a ticket on the famous Adventure Connection bus nonstop from kigoma. This is Kigoma, the home events and hopes, thanks to leka dutigite singers for their incredible union on reviving the  community hope.

Wednesday, May 23, 2012

Central Line Kigoma

Central Line (Reli ya Kati) inafufuka. Lakini jamani ni mabehwa yale yale ya tangu nasoma Tabora Girls 1980's! Duh! Sikuamini macho yangu nilipoona picha. Nikajiona kama nimeweka begi kwenye rack, na nakaa kwenye kiti kurudi shule! Duh!  Lakini cha muhimu kuliko behewa ya kisasa ni kufika salama. Next time nikienda Bongo nitasafiri na Central Line nijikumbushe enzi za udenti!  Asante Kaka Maggid.

**********************************************

Kutoka Mjengwa Blog

Kaka Maggid ndani ya Behewa.

Kaka Maggid Mjengwa jana kwenye behewa la Central Line Kigoma

Behewa la First Class Central Line ilipoanza kazi 1914.

... Usafri wa treni utakuwa wa uhakika zaidi kuliko ilivyo sasa. Kwamba wengi tutachagua kusafiri kwa treni kwa vile ni nafuu zaidi na salama zaidi. Na ni usafiri rafiki kwa mazingira.


Siku hiyo inakuja kwa vile tunachoshindwa sasa ni kuwepo kwa wachache ' wanaohujumu' kwa makusudi usafiri wetu wa njia ya reli.

Mapato yanayopatikana yanapotea. Kuna abiria wanaosafiri bila nauli zao kuingia kwenye Shirika bali kwenye mifuko ya wanaojiita wajanja. Kuna mizigo pia inayosafirishwa bila mapato yake kuingia kwenye Shirika, bali, kwenye mifuko ya wanaojiita wajanja. Hali hiyo ni kwa reli ya kati na reli ya Uhuru pia, kwa maana ya Tazara.

Na hao wanaojiita wajanja wengine ni viongozi tuliowapa dhamana za kusimamia mashirika yetu ya umma.

Siku hiyo inakuja tutakapokuwa na mfumo utakaohakikisha mwisho wa wanaojiita wajanja.

Hivyo basi, siku hiyo inakuja tutakapoona fahari kusafiri kwa njia ya reli yanayooendeshwa na mashirika yetu ya umma chini ya uongozi wa wazalendo wa nchi hii watakaokuwa tayari hata kutoa fedha za mifukoni mwao kuhakikisha treni zinatembea kwenye reli zetu.

Naam, siku hiyo inakuja....

Na hili ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa,
Kigoma.
0788 111 765

Saturday, November 20, 2010

Majambazi Wateka Basi Kibondo (Kigoma)

MAJAMBAZI WATEKA BASI KIBONDO KATIBU UVCCM AUAWA


Habari zimeletwa kwa email na:
Frederick M. Katulanda

Basi la Kampuni ya China ya Golden Intercity Express lenye namba za usajili T 457 ARC lilikuwa limebeba abiria 51 lilitekwa na Majambazi leo katika eneo la Mkugwa wilayani Kibondo.

Inasemekana majambazi hao walipiga sana Risasi, akielezea Mkasa huo kwa njia ya simu kutoka eneo la tukio, mmoja wa Wasafiri aliyekuwa ndani ya Basi hilo kutoka Kigoma kwenda Mwanza, Sophia Nasibu alieleza kwamba tukio hilo lilitokea majira ya saa tatu asubuhi ambapo alishuhudia Majambazi yakipiga risasi ovyo kwenye Basi hilo na hivyo Dereva kulazimika kusimama porini hapo.

Katika kufyatua risasi inasemekana wameweza kumuua Willy Muga katibu wa UVCCM mkoani Mara. Aidha Sophia ameeleza kuwa majambazi hao yalikuwa yakipiga kelele kuwaamrisha Askari wawili wanaosindikiza Basi letu wasalimishe Bunduki zao, na baada ya muda mrefu huku yakitupiga risasi kutoboa toboa basi ndipo Askari hao wanaosindikiza Basi waliogopa na kuamua kusalimisha Bunduki zote mbili walizokuwa nazo, walizitupa mlangoni na Majambazi yakazichukua.

Majambazi hayo baada ya kuchukua Bunduki za Askari hao yalipoanza kuwapora Abiria fedha walizokuwa nazo huku wakiwachapa viboko baadhi ya waliokuwa wakorofi na ambao walionekana kukaidi. Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma, George Mayunga alipoulizwa kuhusu tukio hilo alisema kwamba amepata taarifa lakini bado anasubiri taarifa rasmi kutoka kwa Kamanda wa Polisi wilayani Kibondo (OCD) Innocent ili aweze kuandaa taarifa rasmi.-

Monday, July 14, 2008

Mh. Zitto Kabwe hajambo sasa.

Picha kwa hisani ya http://bongopicha.blogspot.com/

Wadau, kuna habari njema. Mh. Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini - Chadema) hajambo sasa na ametoka hospitalini siku ya Alhamisi wiki iliyopita.
*************************************************
Zitto atoka hospitali

Thursday, July 10, 2008

Mbunge Machachari nchini Zitto Zuberi Kabwe (Kulia) akiwa na ndugu yake mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya taifa ya Muhimbili leo jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa siku mbili.Mh Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na ugonjwa wa homa ya matumbo.


Tuesday, October 16, 2007

Sinema kuhusu M.V. Liemba



Kuna sinema aina ya Documentary, itatoka hivi karibuni kuhusu ile meli maarufu ya ziwa Tanganyika, M.V. Liemba. Hiyo meli bado ni imara na inaendelea kufanya kazi japo ina miaka karibu 100!
Kwa habari zaidi na kuona clip nenda: http://www.liemba.org/