Showing posts with label Tabora. Show all posts
Showing posts with label Tabora. Show all posts

Friday, September 29, 2017

Tamasha la Tigo Fiesta Lafana Mkoani Tabora

br />
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza kuhusu usalama wa watu na mali zao ulivyoimalishwa  kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati wa tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana.




Benpol akiwapagawisha wakazi wa Mkoa wa Tabora katika Tamasha la Tigo Fiesta katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora



Msanii wa bongo fleva Mr Blue akitumbuiza kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati wa tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana.



Chege akitumbuiza kaaika jukwaa la Tigo Fiesta



Darasa akitumbuiza kaaika jukwad la Tigo fiesta mapema usiku wa kuamkia leo mkoani  Tabora.



Omg Dimpoz akiburudisha wakaz wa Tabora waliojitokeza kwa wingi katika viwanja via 

Jux akitummbuiza wakazi wa Tabora.

Jux katika jukwaa la Tigo Fiesta  katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora 

Maua Sama akiimba kwa hisia 





Maelfu ya wakazi wa Tabora wakiwa katika Tamasha la Tigo Fiesta mapema usiku wa kuamkia jana.

Thursday, December 25, 2014

Ajali Yaua Watu Wawili Nzega Chanza Mwendo Kasi na Mvua

 
Gari ndogo ya binafsi ikiwa nyang'a nyang'a na kusababisha watu wawili kupoteza maisha.

Tukio hilo limetokea  karibu na Ziba,ambapo tunaelezwa kuwa gari ndogo imechakazwa vibaya na inadaiwa kuwa inaelekea Burundi.
Taarifa za awali zinasema chanzo cha ajali hiyo ni pamoja na speed ya gari dogo lakini mvua ilikuwa kubwa kiasi cha barabara kujaa maji na kusababisha gari ndogo kugongana na lori la miziogo.
 Ajali iliyohusisha magari mawili imesababisha waliokuwa kwenye gari dogo kupoteza maisha maeneo ya Nzega mkoani Tabora
Taswira ya Lori la mizigo lililogongana na gari ndogo ya abiria.
 

Saturday, April 26, 2014

Mazishi ya Shangazi Greene ni Leo Mjini Tabora

The funeral of my aunt. Mrs. Greene Kapepela Chale, is being held in Tabora, Tanzania today. Rest in peace Aunt Greene (1933-2014)

Mazishi ya Shangazi yangu, Mrs. Greene Kapepela Chale, yanafanyika leo mjini Tabora. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.


Mrs, Greene Kapepela Chale (nee Che-Mponda)  1933-2014

Thursday, April 24, 2014

Tanzia - Mrs. Greene Kapepela Chale (1933 - 2014) Shangazi Yangu

Wadau, ninasikitika kutangaza kifo cha shangazi yangu, Mrs. Greene Kapepela Chale, ni dada wa baba yangu mzazi tumbo moja. Amefariki saa 8 usiku wa kuamkia leo, huko Kitete Hospital, Tabora. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen. 

Misiba imefululiza. alipoteza wajukuu watatu katika miezi chache na wiki iliyopita alifariki Shangazi Mrs. Rozina Che-Mponda Hauli, mke wa baba mdogo,  ghafla.  Dada yangu anasema  kuwa shangazi alilia sana huzuni zilimzidi na inaeleke alipata stroke (kiharusi).

***************************************
I would like to thank all of those who offered prayers for my Aunt, Mrs. Greene Kapepela Chale (maiden name Che-Mponda). I am deeply saddened to announce that she passed away this morning at 2:00am, Tanzanian time at Kitete Hospital in Tabora, Tanzania. May she rest in peace. We are grief stricken.

Aunt Greene you were such fun despite the tragedies that plagued your life. You now join Uncle Selwin, your children, James, John & Happiness, and your many grandchildren and great grandchildren who died before you, in Heaven. No one should endure the grief you endured, but you stayed strong until you could take it no more. We will always remember you my dear Shangazi Greene.

Rest in Peace. 



Shangazi (mwenye Kilemba), Dada Eliza (katikati), na wifi Mrs, Mburuma (kushoto)

Mimi na Shangazi Greene mwaka 2010 nilipoenda Tanzania

Mrs. Greene Kapepela Chale (1932 - 2014)

Thursday, July 04, 2013

Dar to Kigoma on Central Line takes Three Days

By Mdau A.L.




On 7th June at 10:31PM the adventure began, it hardly took an hour of motion, before we all lost control to the natural taste of sleep, due to trip preparation and tiresome 3 hrs of wait for the journey to begin nobody in my family of 4 could resist any longer.

When I worked up, an awkward voice of random collisions  and shaking of train compartment was growing stronger and stronger, I consulted my clock just to learn that it was 4:00AM on the next day. outside no sign of any building could be seen, just bushes and forests. The Train would remain silent for some 2 to 3 minutes before it begin another fruitless attempt to continue with the journey which would be stopped by loud sounds of collision at the compartment joints and skidding on the rails. 

This continues  with an increasing interval between attempts, until everybody was up at around 6AM.  We latter realized that we were still a long way before reaching Moro town. Later on, some random news was heard.. Engine has failed so another engine from Moro would be on duty soon. After a while we left the venue sluggishly. 

We reached Moro town at 1:00PM, in a very slow but chancy motion, full of shaking and chaotic collisions.  From Moro The same story continued the Engine was even weaker, as a results we reached Dom at 11:00PM and left the station of our capital just after the Mid night. This time a better engine was put on duty and we managed to arrive at Tabora Station at 9:00Am next day.

 The Final journey to Kigoma was unthinkable, a 16 hours trip. We left Tabora at 1:00PM and arrived Kigoma Station at 6:00AM the next day, while Uvinza-Kazuramimba only, took 6 hours due to similar reasons: engine powerlessness. While in Tabora, a hard a rare opportunity to chat with one of the senior TRL staff, who cautious hinted about the disaster of locomotives(engines). In short TRL is on its way to mutually if its ICU status is not updated soon.

On my way back, it took me only 10hour to Kahama plus 12 hours to Dar on the next day, as I have to spend a night in Kahama due to longer queue which requires more than a week to book a ticket on the famous Adventure Connection bus nonstop from kigoma. This is Kigoma, the home events and hopes, thanks to leka dutigite singers for their incredible union on reviving the  community hope.

Wednesday, March 06, 2013

Sifa Za Mikoa ya Tanzania

Nimepokea kwa email:



HIZI NDIO SIFA ZA KILA MKOA TANZANIA:

1. DAR - Utapeli

2. ARUSHA - Ustaarabu

3. MBEYA - Matukio

4. MWANZA - Fujo

5. TANGA - Mapenzi

6. MOROGORO - Starehe

7. DODOMA - Bahati

8. IRINGA - Elimu bora

9. RUVUMA - Pombe

10. RUKWA - Uchawi

11. TABORA - Mikosi

12. SHINYANGA - Njaa

13. SINGIDA - Upole

14. KAGERA - Misifa

15. LINDI - Waoga

16. KIGOMA - Ubishi

17. PWANI - Uvivu

18. MTWARA - Hasara

19. KILIMANJARO - Ubahili

20. MARA - Hasira

21. MANYARA - Utajiri

22. GEITA - Presha

23. SIMIYU - Maradhi

24. NJOMBE - Haraka

24. KATAVI - Aibu

25. Visiwani kote- uchezaji wa karata na bao

Haya mwenzangu watokea mkoa gani?

WaHadzabe wakicheza Ngoma

Monday, January 07, 2013

Ziara ya Rais Kikwete Igunga




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na kutoa ushauri kwa kundi la vijana 10 ambao baada ya kumaliza chuo kikuu wamejikusanya na kuunda kikundi cha ujasiriamali mjini Igunga wakijishugulisha na Kilimo
 
Wananchi wakivuta katika sehemu itayojengwa darala la kisasa la Mbutu la Igunga ambao ujenzi wake umezinduliwa leo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, hatua ambayo itatatua kabisa tatizo la miundombinu.

Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akijiunga na bendi ya Msondo Ngoma kutumbuiza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa daraja la Mbutu la Igung

 
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia mashine ya kuchimbia mashimo ya nguzo za daraja na baadaye anakata utepe kuzindua ujenzi daraja la Mbutu la Igunga
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua mradi wa Chujio la maji safi kwa mji wa Igunga sehemu za Bulenya ambapo wakazi asilimia 70 wa mji huo watapata maji safi

PICHA NA IKULU

Saturday, September 17, 2011

Kuna Nini Igunga? Chadema Wakamata Mkuu wa Wilaya Igunga!

Mkuu wa Wilaya ya Igunga Fatma Kimario Akishikiliwa na WanaCHADEMA

 9/15/11

Kutoka  Gazeti la Mwananchi

Na Boniface Meena na Daniel Mjema, Igunga

VURUGU zimezuka jana katika Kata ya Isakamaliwa, wilayani Igunga zikiwahusisha viongozi wa Chadema na Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatma Kimario.Katika sakata hilo, wanachama wa Chadema walimkamata Mkuu huyo wa Wilaya kwa tuhuma za kuendesha mkutano wa ndani na watendaji wa serikali za vijiji, wakati akijua kuwa kulikuwa na mkutano wa kampeni za chama hicho karibu na eneo hilo.

Msafara wa Chadema ulifika katika eneo la kampeni saa 8.00 mchana na kabla mkutano haujaanza, Meneja Kampeni wa chama hicho, Sylivester Kasulumbai, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mkuu wa wilaya ya igunga alikuwa akifanya kikao cha ndani katika eneo hilo kinyume na taratibu, hivyo wanakwenda kumshughulikia.

Kasulumbai ambaye ni Mbunge wa Maswa Mashariki akiwa na Mbunge wa Viti Maalum, Susan Kiwanga, baadhi ya wananchi na vijana wao, walifika katika ofisi ya Mtendaji wa Kata kulikokuwa kunafanyika mkutano huo na kuanza kuhoji aliko Mkuu huyo wa Wilaya.

Mmoja wa wananchi alimnyooshea kidole mama ambaye alikuwa amekaa mbele na kusema; “..yule ndiye Mkuu wa Wilaya”.Kundi hilo la vijana na viongozi wa Chadema, waliingia katika ukumbi huo na kumtoa nje mama huyo huku wakimtaka aeleze kwa nini anafanya vikao vya ndani katika Kata hiyo wakati anajua kuwa chama hicho kilikuwa na mkutano katika eneo hilo.

Kitendo hicho kilizua purukushani na kutokuelewana kati ya waliokuwa kwenye mkutano wa ndani na viongozi wa Chadema, jambo lililovuta umati mkubwa wa watu.

Maelezo ya DC
Baadhi ya vijana wa Chadema walikuwa wamewashikilia watu waliokuwa wakishiriki mkutano huo huku mama huyo akitolewa nje na kuketishwa kwenye kiti alitakiwa atoe maelezo kuhusu mkutano wake.

Baada ya kukaa kwenye kiti huku akionekana kuchanganyikiwa, alisema yeye ni Mkuu wa Wilaya ya Igunga, jina lake ni Fatma Kimario na kwamba, hakuwa na taarifa za mkutano wa kampeni za Chadema.

“Sina ratiba, iko katika ofisi za halmashauri, hivyo sikujua kama kuna mkutano hapa, hata hivyo watu walikuwepo niliwaruhusu waende mkutanoni na mimi nilikuwa naondoka sasa hivi,” alisema na kuongeza:

“Nilichokuwa nafanya ni mkutano wa viongozi wa serikali kwa ajili ya kuangalia hali ya mifugo inayoibwa sana, elimu kwa wote hasa watoto na ujenzi wa nyumba bora na masuala ya amani”.

Kimario aliwasihi wafuasi wa Chadema kusoma karatasi ya ajenda ili wafahamu kilichokuwa kikijadiliwa kwenye kikao hicho.

Karatasi aliyokuwa akiizungumzia Mkuu huyo wa Wilaya ilikuwa na ajenda tano za kikao hicho ambazo ni; Uhamishaji wa mifugo; Kuwa na choo chenye ubora na nyumba bora; Elimu;  Mipaka ya shule na ajenda ya mwisho ilikuwa Uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Igunga.

Hata hivyo mbunge Kiwanga alimtaka mkuu huyo wa wilaya aeleze tangu lini kikao cha viongozi wa serikali kikahudhuriwa na wazee maarufu na mabalozi wa nyumba kumi, swali ambalo lilionekana kumchanganya mkuu huyo wa wilaya kwa kutoa majibu tata.

Mkutano wa Chadema

Wakati hayo yakiendelea, mkutano wa kampeni ulikuwa nao ukiendelea, hivyo viongozi hao wa Chadema walimtaka DC huyo afike kwenye mkutano huo ili aweze kuonana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa.

Kimario alikubali, lakini akataka dereva wake atangulize gari na kwamba yeye angefuata. “Nitakwenda kwani napaswa kuwepo pale kama msimamizi wa usalama, sijahudhuria mkutano wowote hivyo nitakwenda,” alisema.

Akizungumzia tukio hilo kwenye mkutano wa kampeni, Dk Slaa alisema wakuu wa wilaya na mikoa kufanya mikutano wakati wa kampeni ni kinyume cha sheria, hivyo Kimario alienda kuanzisha vurugu.

“Hapaswi kufanya mkutano wowote hapa hasa akijua kuwa sisi tuna mkutano wa kampeni na yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama wa Wilaya,” alisema Dk Slaa na kuongeza:

“DC anafanya nini huku wakati hiki ni kipindi cha uchaguzi au ndiyo wanapanga mikakati ya uchakachuaji halafu wanadai sisi ndiyo tunaofanya vurugu?”

Mkutano wa kwanza na wa pili wa Chadema, hakukuwa na ulinzi wa polisi kama ilivyokuwa kwenye mikutano mingine.

Askari wamwagwa
Wakati gari la waandishi wa habari likirejea mjini Igunga, lilipisha na magari mawili ya polisi yakiwa yamejaa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), ambayo yalikuwa katika mwendo kasi yakielekea eneo la tukio.

Magari hayo yalifuatiwa kwa nyuma na gari aina ya Toyota Landcruiser ambalo lilikuwa na vioo vyeusi yote yakiwa yamewasha taa kuashiria hali ya hatari.

Hata hivyo polisi wilayani Igunga kupitia kwa Mkuu wake (OCD), Issa Maguha, waliliambia Mwananchi kuwa hawakuwa na taarifa ya tukio hilo na kwamba magari hayo yalikuwa katika doria za kawaida.


CCM yawaangukia wananchi

Katika hatua nyingine CCM kimewaangukia wananchi wa Igunga kikiwataka kuacha jazba na hasira kwani madhara ya kuchagua mbunge kwa chuki yataligharimu jimbo hilo kwa miaka minne ijayo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu wa NEC ya CCM Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba wakati akihutubia mkutano wa kampeni katika kijiji cha Usongo kata ya Nyandekwa kinachoaminika kuwa ngome ya Chadema.

Habari zilizopatikana kijijini hapo kabla ya kuanza kwa mkutano huo zilidokeza kuwa Chadema walitangulia kufanya mkutano wa kampeni kijijini hapo na kumwaga ‘sumu’ ili wananchi waichukie na wasiichague CCM.

Akihutubia mkutano huo, Nchemba alirudia mara kadhaa kusema, “shusheni jazba” na “punguzeni hasira” ambayo ilitafsiriwa na wengi kuwa ni kujaribu kung’oa mizizi ya Chadema.

Katibu huyo alisema Chadema kimekuwa kikipandikiza chuki kwa wananchi kwamba Serikali ya CCM haijafanya lolote katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru. Alisisitiza kuwa huo ni uongo wa karne unaopaswa kupuuzwa.

“Kuwa na vuguvugu la kifikra inaruhusiwa na pia kuwa na mtizamo tofauti inaruhusiwa lakini si katika kipindi hiki ambacho wananchi wa Igunga wanahitaji mgombea wa CCM kuliko kipindi kingine chochote,” alisema.

Nchemba aliendelea kusema: ”kwenye uchaguzi mdogo nawaombeni mshushe jazba.…hata kama ulikuwa tayari na mlengo fulani, basi badilika kwa manufaa ya wana Igunga…, tusishabikie vyama bali tujadili hoja”.

Katibu huyo ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Mashariki, aliwasihi wananchi wa kijiji hicho na Jimbo la Igunga kuacha kushabikia mambo ya maendeleo kama wanavyoshabikia timu za soka hata ambazo hawazijui.

Kwa upande wake, mgombea Ubunge wa CCM, Dk Dalaly Kafumu aliahidi kusimamia mradi wa kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria hadi Igunga kupitia majimbo ya Kahama na Nzega.

Dk Kafumu aliahidi kutumia utaalamu wake wa madini kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wanatengewa maeneo yenye madini katika jimbo hilo na kutatua tatizo na kero ya muda mrefu ya daraja la Mbutu.

Wednesday, September 30, 2009

Kituo cha Reli ya Kati - Tabora

Wadau, mliosoma Tabora, mnakumbuka hii kituo cha Reli? Bado iko vilevile haijabadilika! Mnakumbuka usafiri wa CENTRAL LINE?
Picha kutoka: http://www.5cense.com/EA/Tanz_cent.htm

Monday, October 06, 2008

Habari za Kuudhi! Vifo Vya Toto Disko Tabora

Kutoka Lukwangule Blog:


HABARI za kuudhi zinaendelea kumiminika kuhusiana na mkasa mzito wa kupoteza watoto 19 kwa mpigo wakati wa disko mjini Tabora kwenye sikuku ya Idd.

Baadhi ya watoto walionusurika kifo katika ukumbi wa Bubbles Night Club siku ya Idd mosi ambako wenzao 19 walipoteza maisha, wamesema wanaamini ulevi wa baadhi yao ulisababisha janga hilo.

Watoto hao walisema pia kwamba tathmini yao inaonyesha kwamba waliokuwamo ndani ya ukumbi siku hiyo walikuwa kati ya 1,000 hadi hata 1,500.

Uwezo wa ukumbi huo ambao ulijengwa kwa ajili ya mikutano ni kuhudumia watu wazima 150. Mmoja wa watoto hao akizungumza kwenye maziko ya rafiki yake ambaye walikuwa naye disko siku hiyo, Said Sudy (12) alisema siku hiyo ya tukio, mabaunsa wa ukumbi huo walikuwa wakimlazimisha kila mtoto aliyekuwa anaingia ukumbini kununua pombe aina ya Simba Gin.

Polisi inaendelea kuwatafuta mabaunsa hao ambao walikimbia baada ya tukio hilo .

Kwa habari zaidi ingia saiti ya HabariLeo:

http://www.habarileo.co.tz/

Thursday, October 02, 2008

Maafa mjini Tabora! - Part 2

Okay, ni hivi....hao watoto walikufa kwa kukosa hewa (Suffocation). Wanasema kuwa kuna joto sana mjini Tabora sasa na ule ukumbi ulikuwa umejaa kupita kiasi.

Sasa si uchu wa pesa huo? Mnajaza watu kupita kiasi katika eneo ndogo, unatagemea nini? Wafilisiwe hao washenzi wenye klabu na wafungwe gerezani maisha!


Watoto wamepoteza maisha yao shauri ya uchu wa pesa!

Hivi hakuna standards za kusema, eneo fulani unatosha watu kiasi fulani tu? Mfano chumba kinatosha watu 50 lakini mnaweka watu 300! Kuna wakaguzi huko? Hapa Marekani hiyo ni moja ya kazi ya zimamoto.

Hii ni jambo la kisikitisha sana tena mno na ni aibu kwa nchi yetu.

Poleni wafiwa. Mungu alaze roho za marehemu mahala pema mbinguni. AMEN.

Vyombo vya habari vya kimataifa sasa wanatangaza habari hizi someni:

http://www.bloomberg.com/apps/news?pid=20601116&sid=apHD09_PuR1w&refer=africa

http://www.nation.co.ke/News/-/1056/476772/-/tkwn0r/-/

http://afp.google.com/article/ALeqM5j4Yux0NoN6fz9qovrCN9uTpMSNsA

http://www.cnn.com/2008/WORLD/africa/10/02/disco.deaths.ap/index.html

**************************************************************************
Kutoka gazeti la Daily News:

http://dailynews.habarileo.co.tz/home/?id=7627

RAPHAEL LUCAS in Tabora
Daily News; Thursday,October 02, 2008 @19:01

President Jakaya Kikwete has sent condolences to the families of 19 children who died in a discotheque when celebrating Idd el Fitr, calling for a thorough investigation into the matter -and stern measures taken against all those involved. Six other children are hospitalized, two of them in critical condition, following the incident.

The owner of the club, Mr Shashi Patel, is under police custody as authorities continue with investigations. The Minister for Labour, Employment and Youth Development, Prof Juma Kapuya, said that the president had also given 500,000/- to the families of children who perished in the accident.

Prof. Kapuya said that President Kikwete received with profound shock the children’s death that occurred at around 6:30 pm at Bubbles Night Club within Tabora municipality on Wednesday. According to the Tabora Acting Regional Police Commander, Mr Daudi Siasi, the tragedy struck after the children suffocated within the club’s overheated poorly ventilated dance floor.

Tabora municipality is at the moment very hot with temperatures recorded at over 33 degrees Centigrade. The children who perished were aged between 7 and 15 years. Reports from Tabora say that the Uyui District Medical Officer, Dr Moses Makelele, lost two children in the tragedy. His wife passed away three weeks ago.

The National Social Security Fund (NSSF), owners of the building that houses the club, have also promised to give another 500,000/- to the families of each of the children that died in the tragedy and 100,000/- to the families of the injured children.

Tabora regional authorities have given each family of the deceased children 50,000/- and the go-ahead for them to bury their dead. Mr Siasi identified those who died in the incident as Veronica Manigu (7), Beatrice Makelele (14), Jacob Gerald (12), Salma Hamis (12), Khadija Waziri (13), Rehema Moto (14), Selemani Iddi (11), Mrisho Selemani (10), Abdallah Rehani (14) and Agatha Manigu (12).

Others are Paulina Emmanuel (11), Mohammed Kapaya (15), Ramla Yenga (15), Habiba Shabani (15), Donald Kasera (12), Mwanahamisi Waziri (11), Philipo Haule (11), Ashura Jacob (12) and Yasini Rashidi (11). Those injured are Msimu Rehani (14), Tatu Amani (15), Kulwa Iddi (12), Sakina Alli (10); the latter was discharged but later returned to hospital. Two of the casualties are in critical condition – Jumanne Abdullah (age not immediately established) and Naomi Joseph (13).

Maafa mjini Tabora!

Kitete Hospital Tabora Mortuary
Wazazi ndugu na marafiki wakisubiri kuchukua miili ya wapendwa wao

Wadau, bado sijaelewa watoto wote 19 hao walikufaje. Walilishwa sumu? Kulikuwa na sumu kwenye hewa? Paa iliwaangukia?

Na pia nimesikitika kuona mortuary ya Kitete hospital ni ile ile tangu nasoma Tabora Girls miaka ya 80! Haina refrigeration (ubaridi). Pia mjia wa Tabora umepanuka sana mbona mortuary ndogo?
Mungu alaze roho za marehemu mahala pema mbinguni. Amen. Hii ni hasara kwa taifa letu na ninshukuru kuona kuwa rais ameagiza uchunguzi ufanyike. Hongo isitembee hapo!
******************************************************************


RAIS Jakaya Kikwete amemuagiza Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw. Abed Mwinyimsa kuchunguza na kubaini chanzo cha vifo vya watoto 19 waliokuwa wakishiriki disko toto, tukio lililotokea jana jioni mjini humo.

Pamoja na watoto hao kufa wengine 16 wapo hospitalini Kitete kwa matibabu.
Watoto waliofariki ni Veronica Wanigu(7)Beatrice Makelele(14)Jacob Gerald (12)Salma Hamisi(12)Hadja Waziri(10) Rehema Moto (12)Seleman Idd (11) MrishoSeleman (10)Abdalah Rehan (14’)Agatha Manigu(12) Paulina Emanuel (11) Mohamed Kapaya (15) Ramla Yenga(15)Habiba Shaaban (14).Wengine ni Donald Kasela (12)Mwanahamisi Waziri (11) Ashura Jabal (12) na Yasin Rashid (11).

Waliolazwa hospitali hospitali hadi sasa baada ya wengine kumi kuruhusiwa ni Msimu Rehani (14) Naomi Joseph (13) Tatu Amani (15) Kulwa Idd(12) Sakina Ally (10) na Jumanne Abdallah(11) .

Rais kwa kupitia Waziri Athuman Juma Kapuya amesema kwamba amesikitishwa sana na tukio hilo na kutuma salamu zake za rambirambi kwa mkuu huyo wa Tabora na wafiwa.

Kutokana na agizo hilo serikali mkoani hapa imeunda tume maalumu itakayoshirikish
a wadau mbalimbali ili kubaini chanzo cha tatizo hilo na kuhakikisha halijirudii tena.

Kutokana na msiba huo, Rais Kikwete ametoa ubani wa shilingi laki tano kwa kila marehemu ambapo shirika la hifadhi ya jamii(NSSF) ambalo jengo lake ndilo lina kumbi hizo limetoa shilingi tano kwa kila marehemu na shilingi laki moja kama pole kwamajeruhi, na serikali ya mkoa wa Tabora imetoa shilingi elfu hamsini kwa kila marehemu.

Mitaa mingi ya mji huu imebaki kuwa na watu katika makundi makundi wakijadili tukio hilo na wengine wakilia kwa kupoteza watoto au ndugu zao.

Mkuu wa Mkoa ameagiza kufungwa kwa kumbi zote za disko na dansi mpaka atakavyotangaza vinginevyo.

Naye Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Tabora amesema kwamba wamiliki wa kumbi mbili za disko Bubbles Night Club, Shashikanti Patel na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Projestus ambaye anamiliki Top Five disco sound wanashikiliwa na polisi mjini hapa kufuatia tukio hilo.
Watu hao wanatakiwa kuisaidia polisi katika uchunguzi wake.

Msanifu wa majengo aliyesanifu jengo hilo la NSSF ambako tukio hilo lilitokea John Mlundwa alisema kuwa kumbi hizo zilijaza watoto kinyume na uwezo wake nakuongeza kuwa kumbi hizo zilijengwa kwa matumizi ya mikutano na matumizi ya ofisi na siyo matumizi ya sherhe za watoto kwani watoto wanatakiwa kustarehekatika maeneo ya wazi.

Picha hizi japo hazipendezi kwa namna yoyote ile ni jengo la NSSF Tabora ambalo lilikuwa na kumbi hizo za disko,chumba cha maiti cha hospitali ya kitete ambapo miili ya watoto hao ilikuwa inahifadhiwa na mamia ya wananchi wakiwa katika hospitali.Picha na mdau wa Tabora.
********************************************************

Monday, October 01, 2007

Mapacha wabaka na kuua Tabora!

Hivi wanaume wanakuwa na nyege za ajabu kiasi gani mpaka kumbaka mtoto mdogo asiyejua kitu kuhusu ngono. Kwenye ippmedia.com nimesoma habari ya hao mapacha vichaa waliobaka mtoto wa darasa la kwanza ambaye bila shaka, hakuwa na matiti kifuani na sehemu zake nyeti bado za kitoto.

Kama tunavyojua nyeti za wanaume waliokuwa ni kubwa na kwa mtoto mdogo hazifai kabisa. Na kwa kawaida mwanaume aliyekuwa hawezi kumtamani mtoto mdogo hivyo.

Bila shaka hao mapacha walimchana huyo mtoto uko chini na kuharibu kizazi chake na viungo vingine. Huenda alipata 'internal injuries' pia. Yaani walishindwa kumpata mwanamke wa umri wao? Hakuna malaya huko walipokuwa? Kwa nini aliamua kufanya 'gang rape' kwa huyo mtoto? Yaani hao mapacha wanafanya kupigwa mawe hadharani hadi kufa!

Mungu alaze roho ya huyo mtoto mahali pema mbinguni. AMEN.

Naomba na hao mapacha wafungwe gerezani maisha!

****************************************************************************
From ippmedia.com

Mwanafunzi afa kwa kubakwa na mapacha 2007-10-01

Na Lucas Raphael, PST Tabora

Mwanafunzi wa darasa la kwanza wa Shule ya Msingi Mkoani ya mjini Tabora, amekufa baada ya kubakwa na wavulana mapacha wenye umri wa miaka 17. Kufuatia mauaji hayo, watuhumiwa (majina yanahifadhiwa kwa ajili ya umri mdogo), walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Tabora.

Mapacha hao walipandishwa kizimbani Ijumaa iliyopita kujibu tuhuma za kubaka na kuua mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Bi.Roda Ndimilanga. Mwendesha Mashitaka wa Polisi Bw.Wilibad Kaiza alidai mbele ya Hakimu Bi.Ndimilanga kuwa washitakiwa kwa pamoja walimbaka mtoto huyo na kupelekea kifo chake.

Aliendelea kuileza mahakama hiyo kuwa washitakiwa hao walitenda kosa hilo Agosti 28, mwaka huu, majira ya mchana, katika Mtaa wa Kwihara katika Manispaa ya?Tabora. Kaiza aliendalea kudai kuwa watuhumiwa hao walimsababishia mtoto huyo (jina limehifadhiwa) maumivu makali sehumu za siri na kupelekea kifo chake.

Watuhumiwa hao walifikishwa kwa mara ya pili katika mahakama hiyo, ambapo mara ya kwanza ilikuwa Agosti 30, mwaka huu, kwa tuhuma za kumbaka mtoto huyo. Hata hivyo, watuhumiwa hao walifikishwa mara ya pili mahakamani kwa tuhuma zakubaka na kusababisha kifo cha mtoto huyo.

Washitakiwa hawakutakiwa kujibu chochote hadi watapofikishwa katika mahakama kuu? kwa kuwa kesi hiyo imeangukia katika kesi za mauaji na hivyo kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Oktoba 11 mwaka huu.