Thursday, March 13, 2008

Mjue Prof. Joseph Mbele

Prof. Joseph Mbele

Mbali na kuwa na utajiri wa asili wa aina yake,Tanzania ni nchi ambayo inajivunia kuwa na wasomi maarufu ambao wametapakaa kote ulimwenguni wakifundisha katika mashule na vyuo mbalimbali au kuongoza vitengo nyeti katika idara za kimataifa na zenye uzito wa ki-dunia nzima.

Miongoni mwa wasomi hao ni Prof. Joseph Mbele (pichani), Mtanzania anayefundisha katika Chuo cha St. Olaf kilichopo Northfield jimboni Minnesotta, nchini Marekani.

Miongoni mwa wasomi na wafuatiliaji wa mambo mbalimbali ya kitaaluma jina la Prof. Mbele sio geni hata kidogo. Yeye ni mtunzi wa kitabu maarufu sana kiitwacho ''Africans and Americans:Embracing The Cultural Differences''.

Kitabu hicho ndicho kinachotumika zaidi hivi leo mashuleni na katika taasisi mbalimbali(zikiwemo balozi mbalimbali) wanapokuwa wanawaandaa watu wao kuja kusoma, kutembea tu, kufanya kazi au tafiti mbalimbali barani Afrika.

Mengine mengi zaidi ya msomi huyu nenda http://www.bongocelebrity.com/

No comments: