Monday, March 31, 2008

Bongo na Face of Tanzania










Yafuatayo ni maoni ya mdau.


Imeandikwa na Dada Tanzania


Bongo na Face of Tanzania “mimi kisura najitambua”

Je kisura atakayeshinda Tanzania atakubaliwa South Africa au……?

Mambo vipi wadau wenzangu,na Chemi Che Mponda pole na kazi na hongera kwa kupata shavu la kuwa kwenye filamu ya ukweli.Huo ni mwanzo na unajitengenezea profile nzuri ambayo itakusaidia hapo baadae.

Haya wapedwa,wale mlio Tanzania nafikiri wengi wenu mmepata nafasi ya kuangalia mchakato mzima wa kinyang’anyilo cha kumtafuta kisura wa Tanzania unaoendelea hapa home,Mshindi atapata mkataba huko kwa mzee Mandiba South Africa.(mkataba na moja ya kampuni ya mitindo SA)

Kwanza kabla ya kuelezea zaidi napenda kuwapongeza au kumpongeza muandaaji Irene Kiwia kwa ubunifu na kujiamini kwa hali ya juu kufanya kitu kama hicho.

Nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa hayo mashindano katika luninga yetu ya Taifa,toka walipoanza mikoani na hadi hapa Dar es salaam. Kwa kweli walifanya kazi ngumu sana na kwa sasa hawa washiriki wamepatikana na wako kambi na mchujo unaendelea kila wiki.

Swali ni je huyu mshiriki atakubaliwa huko SA, embu waangalieni hao washiriki pita 8020fashions.blogspot.com kwa picha zaidi.Mimi nimewatazama hawa washiriki kwa mtazamo wangu hakuna hata mmoja mwenye kiwango cha uanamitindo.wengi wao ni warefu na ni wazuri sana tu.Tatizo kimtazamo wa kimtindi wanatuchanganya.

Hapa najaribu kusema kuwa,waandaaji hawajajiandaa vya kutosha,kifedha kuweza kuendesha show nzima.kama kimatangazo,kimavazi nk

Kama kule mikoani,waandaji walitangaza mabinti waende kwenye audition, lakini washiriki hawajajitokeza kabisa kama wamejitokeza ni wawili au watatu tu.kusema la ukweli hadi mi nilikuwa nawaonea huruma.kama kule Mwanza. Mwanza ni jiji kubwa tu,cha kushangaza walikosa kabisa washiriki,hadi waliamua kwenda kwenye nyumba za starehe na mitaani kutafuta.washiriki,hii inaonyesha ni jinsi gani hawakutangaza vya kutosha,na kueleza faida ya uanamitindo ni nini,ivyo ilisababisha kutokuwa na msisimko.

Tuache hapo,hao washiriki wengi wao wamelazimishwa,kama akikutwa mrembo barabarani mrefu tu kafikia 174m basi wanamlazimisha akashiriki hata kama hapendi na hata kama anaonekana mrefu tu lakini hana haiba za kiuana mtindo.

Kwangu mimi, Irene na timu yako kama unataka kufanya kitu lazima ukipende na ukifahamu.na ukikipenda utakifanyia kazi na hautataka kukiacha,hao warembo wako wote hakuna hata mmoja anayependa kupiga picha(yaani wanapooza ile mbaya na waoga kwenye picha).iyo pia inafanya uzuri wao ufichike.

Au basi wanafaa nyie hamna vifaa,maana Irene nilikuona kwenye TV wewe ndo unacamera yako ya digital ndogo inamuonekano ya kupiga picha za nyumbani tu. unawapiga picha wewe mwenyewe.kwa iyo hawapigwi picha kiufundi.(professional) ndio maana hawatokei kimtindo.

Embu tuchukulie mfano wa wenzetu kama “America next top model”,wanawashirikisha wanamitindo waliopata mafanikio,kama Tyra mwenyewe,mtu aliyebobea kwenye kupiga picha za uanamitindo,waandishi wa majarida muhimu ya mitindo nk.
Sasa ukiangalia nyie yenu hata hakuna mtu mmoja anayejua mambo ya mitindo na ambaye amewahi kufanya shughuli za mitindo mnayemshirisha.kwenye ushauri na kuwaweka sawa hao wabinti wapate muonekano wa kiuanamitindo.

Ni siku moja tu juma lililopita,mlipotembelea TBL ,kulikuwa na kaka mpiga picha yeye angalau ongea yake kuusiana na picha alizowapiga kwa siku iyo,alionyesha na ufahamu na upigaji picha.je kwa nini msimtumie uyo kuwapiga picha models wenu?.Je pia hamuoni kama mkiwapatia elimu ya kutosha kuhusiana na mitindo pia mtawanufaisha hata watakapoenguliwa wakajiendeleza wenyewe kwa namna moja au nyingine?.

Embu hayo yabaki kama maswali tu,Lakini picha za mitindo mara nyingi zinaongea,yaani unaijaji picha na kuhisi mwanamitindo anataka kusema nini au kufanya nini.lakini karibia picha zote mlizozitoa kwenye vyombo vya habari hazisemi hata kidogo(zimenuna).na toka hao washiriki waingie kambini hawajabadilika kimitindo, wako vile vile.badiliko nililoliona ni yule mmasai kuacha nguo zake za asili na kukimbilia jeans.(na ni kawaida tu,sio kimsingi)

Tukianza na wewe Irene mwenyewe na Nancy Sumari,wote nyie hamkuwahi kufanya shughuli za mitindo bali mliwahi kuwa warembo tu.hali urembo na uanamitindo ni vitu viwili tofauti kabisa.naona jinsi mnavyowafundisha kupose kwenye picha ,sio kabisa ni kikawaida mno.kwenye kutembea je,Nancy siku aliwahi kukiri kwenye kipindi chake alikuwa akimuhoji Richa (Miss TZ),kuwa Richa anatembea vizuri kuliko yeye Nancy. Pia nimewahi kumuona Nancy kwenye fashion shows za hapa home ya Mustafah Hassanali hatembei vzuri kabisa,wanampa tu chance kama mgeni na mtu mashuhuri wa TZ kwa heshima naye aoenyeshe mavazi.

Inakuwaje hawa waandaaji wasiweze kualika wanamitindo mbalimbali kama Happiness Magesa,Hawa n.k wawasaidie kuwashauri washiriki kama kupose kwenye picha,kutembea,kuvaa kutokana na mazingira na halikadhalika kuweka make up(kujiremba)n.k

Inasikitika sana kuona washiriki wote wanapiga picha na nywele kama vile wanaenda sokoni(sorry sio naponda).,wengine wamevaa nguo za ofisini kwa kifupi saa ingine haieleweki kabisa.

Mi naona msipowafundisha hao mabinti kupose kwenye kamera,kutembea,kuwa wasafi,wanaweza hata wasikubaliwe huko SA.Lakini hao visura ni wazuri na wakifundishwa watawakilisha vizuri.

Huo ni mtazamo wangu tuu,cha muhimu waandaaji mmeamua kufanya kitu basi jitoleeni kabisa,sio kubip (msemo wa mtaani),zaidi ya yote hii ni changamoto na watu wengi wameona haya,na mimi nimeamua kuwakilisha mtazamo wangu na jamii.


Asante ni mimi Dada TZ

5 comments:

Anonymous said...

Dada umesema vizuri sana hapo kwenye maoni yako na hasa ulipozungumzia juu ya maandalizi ya hiyo shoo.Mimi ni mpenzi sana na mwanaharakati mwanfunzi wa mambo haya ya sinema na mambo ya tv production.
hapa nyumbanai kuna tatizo kubwa sana nionavyo mimi watu wanavipaji kwa kweli lakini suala zima la kujifunza jinsi ya kuvifanyia kazi kibiasha yaani show buzz kwa kweli bado sana.wengi huishia kutengeneza shoo za ubora wa chini sana na kuishia kunyonywa tuu na wenye vituo vya tv na tena shoo hizo huwezi kuziuza hata kenya tuu hapo kwa majirani na kwa maoni yangu naona ni vizuri wahusika watumie muda kudadisi how to run a show be it soap,series,reality show,gossip show,fashion,mapishi,chat show,variety show ,game show nk kuzitaja hapa ni nyingi sana
sasa ni vema dada Irene (kama ni kweli ulikuwa na upungufu ktk kuproduce hiyo show yako) ukajifunze uzuri wa siku hizi unaweza tumia muda kwenye internet vitabu kama vile The show runner,pia jaribu kutuma maombi ya kujifunza kama intern kwenye hizo production mfano kwa tyra banks production,na production nyingine nyingi. tuu kwa kawaida hawana hiana ukijieleza vizuri wanakupa nafasi la kama hata kwa miezi miwili tuu,pia njia nyingine ya kujifunza tafuata mwenye ujuzi wa show running au show production yaani PRODUCER fanya naye kazi kwa ushrikianao japo ktk production ya season moja tuu ,utakuwa umejifunza mengi sana

Pesa
Ndiyo maana zinaitwa Biashara ya show kuna pesa humo!
je wewe na team yako mtafaidika vipi kwa kuendesha show na kwa kiwango gani?
na pesa hizo zinatoka wapi? na huko zinapotoka kwa nini watoe hizo pesa kwako na production yako?
Pesa hizo hpatikana kwa mtindo gani?
Na ni jinsi gani uta manage pesa pamoja na resources muhimu zinazihitajika ajili ya show season nzima
Haaya yoote yapo vitabuni semina,shortcourses nk huhitaji kusoma degree juu ya hili kam huna muda na financial resources
Pre production
Pia kama ni mgeni na biashara ya ku run show ni vema ukafanya pre production at least two years in advance au hata mwaka na nusu.
Mambo ya whee hours, kana kwamba wewe ni pro husababaisha ile kitu inaitwa catch tweny two na once this kicks in ,in your project dada, you are heading for disaster! For a novice in this kind of business always allow enough time in pre production .you wont regret,guarantee!
The same goes to the pundits
Tena najaribu kujiuliza kama dada Irene ulikuwa na script ya show hasa production script.Dada kama ulikuwa huji hakauna show ndogo wala kubwa zoote zinahitaji a well written blue print! hii ndio muongozo wa every part and side of the project
na haya ninayokuamabia sio tu kwa wa novice wa show running bali hata wenye experience nchi za wenzetu yanawakuta

Talent
hapa nazungumzia siyo tu wahusika wa mbele ya kamera bali woote walipo nyuma ya kamera ni watu muhimu sana na hasa wenye experience .usione aibu dada walipe vizuri au share nao kile kidogo ulichonacho kwa uwazi tengeneza uhusiano mzuri ili ujifunze kutoka kwao utafanikiwa hapa sio suala la aibu kama hujui ujui tuu na hakuna aliyejua kila kitu kutoka amezaliwa, amejifunza kutoka mahali fulani

Debut Season
kwa ushauri wangu usijali sana hela ktk kuandaa season ya kwanza fanya kwa ajili ya experience na daima fanya na watu producers,directors managers wenye experince na wewe ukawa ni executive producer tuu

Basi hata kama haikuwa nzuri dada Irene usikate tamaa chukua hiyo kama ni nafasi au kioo sasa unaweza kuona ni wapi ulipo mess up
kitu kimoja ni lazima ku-acknowlwdge kama ni kweli your show went from the face of tanzania to the face of mess!
hii itakusaidia, kwanza kubali na pili misifa ya unafiki ya sisi watanzania isikudanganye kwa sababu watanzania sisi ni vinara wa misifa na japo issue haikwenda vizuri kwa hali halisi
Nilishawahi kuandika siku za nyuma Irene kwamba i respect you a lot for the fact that u miongoni mwa watanzania vijana majasiri wa kujaribu na harakati za kujenga msingi wa entertaiment industry ya hapa nyumbani
great job
Raceznobar

Anonymous said...

Bado hawajachelewa kama wako serious wanaweza kurekebisha hayo. Ali Remtullah ana rafiki yake ni mpiga picha mahiri wa mamodels, hata picha yako ya zamani ukimpa atakavyocheza nayo utapenda sana, simkumbuki jina lakini nilishawahi kuingia kwenye website yake, ana ofisi na Nairobi au Mombasa kama sikosei jamaa ni mkali.

Halafu hao hao mamodels wenu niliwaona kwenye bongo 5 kama sikosei wakitembea kwenye fasheni show ya Fatma Amour, yaani ni kishekesho kitupu, watu warefu wanatembea huku wameinama, they dont walk upright kifua mbele, unajua catlwalk ni artwalk sio kujitembelea na kupeleka kiuono huku na kule. No hutakiwi kubend shingo yangu kabisa, how you walk show how confident you are! Mtumieni hata huyo Hawa atawasaidia kuwafunda ama sivyo mnatia aibu.

Kuhusu picha afadhali hata mie mama wa miaka 40 niko photogenic! Unajua kuwa photogenic sio maajabu ni lazima mwili wako uongee wazungu wanaita body language. OOps sorry nitaonekana nina chuki bure lakini to tell you the truth gals hizi station zetu za TV zinaonekana mbali sana mpaka west Africa. Rafiki yangu alikuwa anaangalia vipindi vya ITV na C5 akiwa Mali hata Nigeria. So thats how you potray our country to the rest of the world.

Anonymous said...

Hao warembo wa juu wabaya kweli.

Anonymous said...

kweli huu ni ushauri mzuri sana ulieandika nakupa +ve lakini maoni sijasoma niko busy kazini kidogo maana camera zinawenifukuzisha kazi

Anonymous said...

Huyo wa chini mzuri ila wale warefu wabaya!