Tuesday, August 16, 2011

Unakumbuka SUPA-GHEE?





Wadau, hapo zamani za kale kulikuwa na mafuta ya kupikia Tanzania maarufu yanaitwa SUPA GHEE. Yalikuwa mazuri sana, lakini miaka ya sabini hasa baada ya Vita Vya Kagera, quality ilishuka vibaya mno. Hata hivyo ilikuwa mali kweli kupata SUPA GHEE! Watu walikuwa wanapanga foleni ndefu za makilomita (siyo utani) kuipata. Nyumba zilikuwa zinavunjwa na SUPA GHEE inaibiwa. Supa Ghee ni moja ya bidhaa ambayo wenye uwezo walikuwa wanaunua na mwisho yalikuwa yanuzwa magendo! Mama Mwenye nyumba anatoa kijiko kimoja kwa ajili ya kukaangia mboga halafu yaliyobaki yanafichwa chumbani! Tumetoka mbali wadau. (Picha ya SUPA GHEE kwa hisani ya mdau S.K.)

Monday, August 15, 2011

Huko Asia Weusi ni Mboga!

ONYO - Nimepata kwa email. Kama huna roho ngumu usiangalie hizi picha! Kama sikosei ni Thaliand hapo. Cheki wanavyomkata huyo marehemu kama nyama kwenye bucha! Nadhani tumejua ndugu zetu walioenda huko na wakapotea waliishia wapi sasa! DUH!


































































Email Text:
THAI & CHINESE PEOPLE EATING A BLACK MAN. I have never seen anything like this before! The Asian appetite for "exotic" taste sometimes scare me - from stories of cat eating to dogs, to lizard, snakes to all sorts of crazy fish, then human embryos and now to fully grown humans! The photo of the person you are about to watch could have been somebody's fiance, husband or Dad! This looks too real to be true.
How I wish all black leaders watch these photos and give guidelines of who they allow to migrate into their countries. The time has come for black (Africans, American, West Indies etc) to rise and unite together against attrocities committed by foreigners on them either on their soil or abroad. Time to pray to God is now!

Madiwani Wafuturu Ikulu na Rais

Picha za Mh. Rais Kikwete na Mama Salma na madiwani wa Dar katika futari Jumamosi jioni Ikulu. Zimeletwa na Kaka Michuzi.












Saturday, August 13, 2011

Bibi Arusi Ashikwa na Uchungu Kanisani!

Makubwa. Habari kutoka Muheza, Tanga zinasema Bibi Arusi, Mariam Shabani, kashikwa na uchungu kanisani, na kupelekwa hospitalini na shela yake na kuzaa huko! Pole zake. Mama na mwana wako salama. Wanasema alikuwa na mimba ya mieza saba.

*****************************************************************
Kutoka Gazeti la Mwananchi:


Bibi harusi ashikwa uchungu, ajifungua kanisani Muheza
Thursday, 11 August 2011 21:16

Mwandishi Wetu, Muheza

BIBI harusi aliyefahamika kwa jina la Mariam Shabani, ameshikwa na uchungu wa kujifungua kanisani wakati akifungishwa ndoa na mchumba wake, aliyefahamika kwa jina la Deo Massawe.Tukio hilo lilitokea juzi Kanisa Katoliki lililopo maeneo ya Majengo Shimoni, wilayani Muheza, huku umati wa watu ukiwa umejaa ndani ya kanisa hilo ukiisubiri kufungwa kwa ndoa hiyo.

Mwandishi wa habari hizi alishuhudia tukio hilo ndani ya kanisa hilo, wakati Padri Martin Kihiyo, akiendelea na misa ya kufungisha ndoa hiyo, ghafla bibi harusi akiwa amevaa vazi rasmi la harusi, alianza kupiga kelele akidai anasikia uchungu wa kujifungua.

Hata hivyo, baada ya bibi harusi huyo kupiga kelele, Padri Kihiyo alisitisha misa hiyo na Mariamu kuchukuliwa haraka na kuwekwa kwenye gari huku akiwa hajiwezi hadi Hospitali Teule Muheza.Pia, Mariamu anafahamika kwa jina la Sada Shabani, baada ya kufikishwa hospitali alipelekwa chumba cha kujifungulia huku akiwa na vazi lake la harusi.

Baada ya kuhudumiwa Mariamu, alijifungua mtoto wa kike na kulazwa wodi ya Azimio wanakolazwa wazazi.
Mmoja wa muuguzi hospitalini hapo aliyeomba asitajwe, alisema bibi harusi huyo alijifungua njiti akiwa na miezi saba.Kwa upande mwingine, kwenye ukumbi ambao ulikuwa umeandaliwa kwa sherehe ya harusi hiyo, watu walikuwa wamekaa ndani wakisubiri maharusi bila kufahamu kilichokuwa kikiendelea.

Hata hivyo, kutokana na hali hiyo bwana harusi alilazimika kufunga ndoa na msichana mwingine wa pembeni kwa niaba ya bibi harusi, ili kuhalalisha sherehe hiyo huku bibi harusi mwenyewe akiwa hospitali analea.

Inasemekana Mariamu alianza kusikia uchungu akiwa saluni na aliwaeleza baadhi ya watu, lakini walimjibu kuwa huo ni woga wa harusi.Katika hatua nyingine, mbuzi wa ndafu aliyekuwa ameandaliwa alianguka chini kwenye mchanga.

Baadhi ya Wakristo walisikitishwa na tabia ya viongozi wa dini kuendelea kuwafungisha ndoa watu ambao wake zao wana mimba kwamba, ni aibu.

Thursday, August 11, 2011

MBunge Adai Naibu Spika Mhe. Job Ndugai Ameshindwa Kuendesha vikao vya Bunge




Nimepata kwa email:

(Pichani: Mh. John Mynika Mb. Ubungo)


Leo tarehe 11 Agosti 2011 katika kikao cha 48 cha Mkutano wa Nne wa Bunge la Kumi nilitaka kuomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2007 ) kifungu cha 68 (7) kuhusu maswali na majibu ya Waziri Mkuu na nikarejea pia kanuni ya 133 (1).

Hata hivyo, kabla hata ya kutoa maelezo kamili ya kuomba muongozo wa Spika nilizuiwa na Naibu Spika Mheshimiwa Job Ndugai (Mb) bila hata ya kusikilizwa muongozo ambao nilitaka kuomba kinyume na kanuni ya 5 (1) inayotaka Spika kuongoza Bunge kwa kuzingatia kanuni na pale ambapo kanuni hazijatoa muongozo Spika anapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia katiba, sheria nyingine za nchi, kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali na desturi za kibunge.

Naomba kutoa taarifa kwa umma kwamba sijaridhika na uamuzi uliofanywa na Naibu Spika Mheshimiwa Job Ndugai hivyo nawajulisha kwamba ninakusudia kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni za Bunge kifungu 5 (4) na 7 (3) mara baada ya kupata nakala ya kumbukumbu rasmi ya Bunge (Hansard) ya kikao husika.

Mara baada ya kunukuu kanuni husika nilipoanza tu kuzungumza kwamba katika kipindi cha Maswali na Majibu kwa Waziri Mkuu, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amekuwa akitoa majibu yenye upotoshaji yasiyokuwa ya kweli; baada ya kauli hiyo kabla hata ya kumaliza maelezo niweze kuomba muongozo kwa Spika; Naibu Spika alinikatisha na kuninyima fursa ya kuomba muongozo kinyume na kifungu 68 (7) na 5 (1).

Naomba umma uelewe kwamba nilikuwa naelewa kwa kina mahitaji ya kanuni za bunge kifungu cha 133 na vipengele vyake kuanzia cha kwanza mpaka cha sita; ndio maana katika kuanza kuomba muongozo nikasoma kifungu cha 133(1).

Napenda umma ufahamu kwamba muongozo ambao nilitaka kuomba kwa Spika ni kwamba kumekuwa na kawaida ya Waziri Mkuu wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kutoa maelezo yasiyokuwa ya kweli yenye upotoshaji ambayo ni kinyume cha katiba ya nchi, sheria mbalimbali pamoja na kanuni ikiwemo kanuni za bunge hivyo nilitaka Spika atoe muongozo wenye kumpa nafasi nyingine Waziri Mkuu kutoa ufafanuzi wa kweli kuhusu masuala husika ili kuepusha uwezekano wa wabunge kupoteza imani na Waziri Mkuu kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu cha 133.

Katika maelezo yangu ya kuomba muongozo huo nilikusudia kutaja mifano miwili mikubwa ya majibu ya Waziri Mkuu kwenye maswali ya papo kwa papo yasiyokuwa ya kweli yenye upotoshaji kuhusu kashfa ya Meremeta na kuhusu mgogoro katika Manispaa ya Arusha.

Ikumbukwe kwamba tarehe 14 Aprili 2011 wakati wa kikao cha saba cha mkutano wa tatu wa Bunge la Tanzania wakati wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, nilimuuliza Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwa “Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye vile vile ni Mwenyekiti wa CCM amenukuliwa akizungumzia kuhusu haja ya Chama kinachotawala kujivua gamba. Kati ya mambo aliyoyazungumza ni pamoja na kuondokana na watuhumiwa wa ufisadi. Mheshimiwa Mkuu uliwahi kulieleza Bunge hili tukufu kwamba usingetaka kabisa kuzungumzia masuala ya Meremeta kwa sababu ni siri za Jeshi. Baada ya kauli hii ya Rais na dhamira hii ya kujivua gamba kuhusiana na masuala ya ufisadi. Je, uko tayari Mheshimiwa Waziri Mkuu kutaja wahusika wa Kampuni ya Meremeta na kuelekeza Serikali kuchukua hatua zinazostahili kuhusiana na tuhuma hizo? . Waziri Mkuu katika majibu yake Mheshimiwa Mizengo Pinda hakuitumia nafasi hiyo kurekebisha kauli zake zisizokuwa za kweli zenye upotoshaji alizozitoa kwa nyakati mbalimbali katika Bunge la Tisa kuhusu kashfa ya Meremeta.

Ikumbukwe pia kwamba tarehe 10 Februari 2011 katika kikao cha tatu cha mkutano wa pili wa Bunge la kumi Waziri Mkuu Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa papo ya Mheshimiwa Freeman Mbowe (Mb) kuhusu matukio yaliyojitokeza Arusha wakati na baada ya uchaguzi batili wa Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha. Tarehe 11 Agosti 2011 katika kipindi cha Maswali ya papo kwa papo ya Waziri Mkuu kuliulizwa maswali kuhusu maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA ya tarehe 6 na 7 Agosti 2011 kwa kurejea pia mazungumzo baina ya Waziri Mkuu na viongozi wa taifa CHADEMA kuhusu muafaka batili juu ya mgogoro katika Halmashauri ya Jiji la Arusha na uamuzi wa kuwafukuza uanachama madiwani watano kutokana na kukiuka maagizo ya kamati kuu. Badala ya Waziri Mkuu kuitumia nafasi hiyo kutoa majibu yenye kulenga kutoa ufafanuzi wa kurekebisha upotoshaji uliofanyika awali Waziri Mkuu Mizengo Pinda akatoa majibu mengine yasiyokuwa ya kweli kuhusu mazungumzo yake na viongozi wa CHADEMA pamoja na uamuzi wa chama wa kuwafukuza uanachama madiwani waliokiuka maamuzi ya kamati kuu ya chama.

Majibu ya Waziri Mkuu kuhusu ufisadi wa Meremeta, matukio katika halmashauri ya Jiji la Arusha na masuala mengine ya kitaifa katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo yenye uhusiano na utekelezaji wa majukumu ya Waziri Mkuu yaliyoanishwa katika ibara ya 52 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yana mwelekeo wa kuvunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma, sheria nyingine za nchi yetu pamoja na misingi muhimu ya utawala bora kama ambavyo nitafafanua katika hatua zinazofuata. Naomba umma upuuze upotoshaji uliofanywa na Naibu Spika Job Ndugai kuhusu muongozo nilioomba mpaka pale maamuzi yatakapofanywa na Kamati ya Kanuni za Bunge kwa mujibu wa kifungu 5(5) na Bunge kujulishwa.

Wenu katika utumishi wa umma,

John Mnyika (Mb)

Bungeni-Dodoma

11/08/2011

Tuesday, August 09, 2011

WaTanzania Wanaoishi USA Waandaa Maandamano kumpinga “Baba Ridhiwani”!

Kweli hali inazidi kuwa ngumu Tanzania miaka 50 baada ya Uhuru. Lakini Je, Rais Kikwete peke yake ni wakulaumiwa? Hebu watizime ile 50 year plan ya Mwalimu. Haikutekelezwa!

Vijana wa siku hizi hawakulelewa kama sisi. Tulikuwa hatuna TV, wala internet. Unasikiliza redio na ukipata BBC, VOA, Deutshe Welle, unaona mali! Enzi za Mwalimu ilikuwa ukisema kitu kibaya dhidi yake au kutaka kupinga, unapigwa, unatiwa ndani! Mbu walikuwa tele! Lakini tulikuwa na amani. Hali Tanzania inatisha sasa. Vijana hawajui yaliyopita na tulitoka wapi. Lakini hata mimi naona wananchi wa chini wamesahaulika. Ujamaa ulikufa na Ubepari umerudi kwa nguvu. UTabaka unazidi Tanzania na ndo chanzo cha chuki.

Sasa kuna habari ya kupinga Ziara ya Rais Kikwete kuja Marekani. Itasaidia kuboresha hali ya wananchi Tanzania?

**********************************************************

Kutoka:
http://mgonjahjr.blogspot.com/2011/08/tanzania-yaelekea-kusiko-shwari.html

TANZANIA YAELEKEA KUSIKO SHWARI

Wa Tanzania wanaoishi USA waandaa maandamano kumpinga “Baba Ridhiwani”, Hii ni sehemu ya maandalizi hayo kama yalivyoandikwa na ELIAKIM MALLYA.
Kutokana na kuchoka na hali ngumu inayoendelea hapa Tanzania, ndugu zatu wanaoishi USA wameandaa maandamano ambayo yatakuwa ya amani kupinga utawala mbovu wa “Baba Ridhiwani” hasa baada ya kushindwa kuwachukulia hatua masfidi hapa nchi.

Tunaandaa maandamano ya amani jijini Washington DC Rais Kikwete “Baba Ridhiwani” atakapowasili kwenye kikao cha DICOTA 2011. Tayari watu 150 wamekubali kushiriki kwenye maandamano hayo. Tunataka watu wengi zaidi kujitokeza. Hii ni kumshinikiza huyu fisadi papa na mzururaji kushugulikia matatizo yanayowakabili wananchi wa kawaida. Maandamano yetu yatahitimishwa na kupokelewa na viongozikutoka United States Department. Tayari tumetuma maombi kupinga misaada marekani inayopa Tanzania, kwani hayasaidii Jamii bali Kikwete na genge lake la majambazi

Wote mnakaribishwa karibishwa. Maandamano ya Amani yanaruhusiwa marekani ilimradi mtu hajavunja sheria nchini. Ukiwa na makaratasi yako, njoo tulikomboe taifa letu. Ukombozi wa TANZANIA upo mikononi mwetu. Mabango yanachapishwa tarehe 24, Tunaomba mawazo tofauti kuhusu ujumbe tutakaobeba kwenye mabango yetu. Tumechoka na Kikwete, dawa nikuanza maandamano. Tupo tayari kufa sasa. Tunisia iliokolewa na watu tu kama sisi, tukifa bahati mbaya vizazi vijavyo vitafaidi. Tafadhali sambaza ujumbe. Tutatoa tamko rasmi ya maandalizi tarehe 20 mwenzi huu Ukitaka kushiriki tuma barua pepe EliakimMallya@yahoo.com

Raia wa kawaida anayo haki ya kumfanya Kikwete Anyimwe VISA. Kwa Kupinga Ujio wa Kikwete, au yeye kunyimwa VISA tumeni emails nyingi iwezekanavyo kwenda East African Affairs Bureau. Email Adress wiegertjr@state.gov

UPDATE
Habari njema ni kwamba, kuna familia moja ya kitajiri ambayo ina interest kubwa Tanzania na wanashngaa kuona taifa letu linavyodidimia. Kwa maana hiyo, wamejitolea kulipia mabango, pamoja na mabasi sita.

1. Basi 2 yataanzia NY (Ni ya watu wa Boston, NY, Long-Island, etc...)
2. Yanayotokea Ohio (Ohio, Maryland, Pensylvania, Michigan etc..)
3. MaBasi ya mwisho yatatokea Atlanta Georgia (Texas, Virginia, Florida, Alabama,Kansas, etc..)

Kwa hiyo kaeni mkao wa Kula, mwisho wa mwezi huu, tunawapa ratiba kamili ya maandamano, yatakayoanzia sehemu ambayo tutawapa kuendelea kwenye Ukumbo wa DICOTA, Ubalozini na hatimaye kumalizika kwnye hoteli atakayofikia FISADI Kikwete. Tutakesha hotelini, chakula kitakuwepo na huduma zote muhimu pia zitakuwepo. Tuko pamoja hadi kieleweki. Wanaotaka kushiriki tumeni barua pepe, kwenda
eliakimmallya@yahoo.com. Mimi ni mwana CCM toka UVCCM lakini naapa ya Kwamba nimechoka na JK. Tunamsubiri Marekani, hata kama ni miaka miwili tunamsubiri, wadhamani wapo

Tamko Rasmi la Waziri wa Nishati na Madini Bungeni Kuhusu Upatakanaji wa Mafuta Nchini



TAREHE 9 AGOSTI 2011, DODOMA

Mheshimiwa Spika,
Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kulishukuru Bunge lako tukufu kwa kunipa fursa hii ya kutoa taarifa kuhusu hali ya biashara ya mafuta ya petroli hapa nchini.

Kama tunavyofahamu, mafuta ya petroli ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu kwani viwanda, vyombo vya usafiri, na huduma nyinginezo nyingi hutegemea mafuta na bidhaa zake. Bei ya mafuta inapopanda, bei zingine nyingi hupanda kwa mfano bei za usafiri zinapanda, bei za vyakula zinapanda, bei za bidhaa za viwandani zinapanda; nakadhalika.

Mheshimiwa Spika, tarehe 22 Juni 2011 Serikali, kupitia kwa Waziri wa Fedha wakati akihitimisha Hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12, alitoa maagizo kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kuchukua hatua mbalimbali zitakazochangia kupunguza bei za mafuta. Hatua ambazo ziliagizwa kuchukuliwa ni pamoja na:
Ukokotoaji wa thamani ya shilingi kwa kuioanisha na Dola ya Marekani (yaani Exchange rate);
Kuondoa au kupunguza wigo wa asilimia 7.5 ambayo makampuni yaliruhusiwa kuwekwa ili kufidia baadhi ya gharama;
kupitia upya misingi ya ukokotoaji wa viwango vya tozo mbalimbali za taasisi za Umma kwa lengo la kubakia na tozo stahili na kwa viwango stahili bila kuathiri majukumu ya udhibiti ma usimamizi yanayofanywa na Taasisi hizo;
kupunguza tozo za kampuni za mafuta ikiwa ni pamoja na gharama za kibenki (yaani Financiang Charges); na
Upotevu wa mafuta yanayosafirishwa kwenye meli na gharama ya ukaguzi (yaani inspection fee).

HATUA ZILIZOCHUKULIWA NA SERIKALI

Serikali kupitia EWURA ilianza mara moja mchakato wa kurekebisha Kanuni ya ukokotoaji wa bei za mafuta hapa nchini kwa lengo la kuleta unafuu wa bei kwa mlaji. Hatua ya kwanza ilikuwa kuandaa hoja (discussion paper) ambayo ilitoa mapendekezo ya maeneo mbalimbali yanayofaa kurekebishwa ili kupata maoni ya wadau wa sekta ya mafuta. Mapendekezo hayo yalizingatia maagizo ya Serikali pamoja wa ushauri mbalimbali wa wadau katika sekta ya mafuta hapa nchini.

USHIRIKISHAJI WADAU
Mchakato wa kupata maoni ya wadau (taftishi) ulianza tarehe 4 Julai 2011 na kukamilika tarehe 26 Julai 2011. Kwa kawaida, mchakato huo ungechukua siku 81 lakini kutokana na unyeti wa suala hili, Mamlaka ililazimika kuufupisha hadi siku 23.

Mkutano wadau uliitishwa tarehe 22 Julai 2011 ili kupitia rasimu ya kanuni pamoja na jedwali la uchambuzi wa maoni ya wadau lililoandaliwa na EWURA. Wadau walioshirikishwa katika taftishi hiyo ni pamoja na makampuni ya mafuta, Baraza la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na EWURA (Consumer Consultative Council), Baraza la Ushauri la Serikali, Taasisi za Umma kama vile TRA, TBS, WMA, TPDC, TPA, SUMATRA, na TIPER. Maoni mbalimbali ya wadau yalipokelewa na kuchambuliwa na EWURA ikiwa ni pamoja na kupata maoni ya wataalam kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Uchumi, Shirika la Maendeleo ya Mfuta Tanzania (TPDC), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, EWURA na Makampuni ya Mafuta.

Tarehe 23 Julai 2011, EWURA iliitisha kikao cha wawakilishi wa wadau wakubwa ambao ni pamoja na CCC, TPDC, TPA, Wizara ya Nishati na Madini, Mwanasheria Mkuu na baadhi ya makampuni ya mafuta kupitia mapendekezo yaliyokuwepo na kutoa maoni ya mwisho kabla ya kuwasilishwa kwenye Bodi kwa maamuzi.

MAAMUZI YA EWURA
Tarehe 26 Julai 2011, Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA ilikaa na kupitia mapendekezo ya marekebisho ya vipengele mbalimbali vya kanuni ya kukokotoa bei ya mafuta. Maamuzi hayo ya Bodi yamepelekea punguzo la bei za mafuta kwa viwango vifuatavyo: Petroli TZS 202.37; Dizeli TZS 173.49; na Mafuta ya Taa TZS 181.37. Mabadiliko haya ya bei ni sawa na punguzo la asilimia 9.17; 8.31; na 8.70 kwa mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa sawia. Kanuni hii ya kukokotoa bei za mafuta imeanza kutekelezwa kuanzia tarehe 03 Agosti 2011.

Tarehe 3 na 4 Agosti 2011 makampuni ya mafuta yaliwasilisha kutoridhishwa na maamuzi yaliyofanywa na EWURA hususan kuhusu kupunguzwa kwa wigo wa asilimia 7.5; margins za makampuni ya mafuta, na gharama za kuchelewesha meli bandarini (demmurage charges).

Kufuatia vikao hivyo vya Serikali, makampuni pamoja na EWURA siku ya Ijumaa tarehe 5 Agosti 2011, Mamlaka ya EWURA ilifanya marekebisho mengine katika vipengele vifuatavyo:
Gharama za ucheleweshaji meli bandarini (demmurage charges) ziliongezwa kutoka wastani wa TZS 1.85 kwa lita hadi TZS 8.76 kwa lita.
Viwango vya faida kwa kampuni za mafuta (OMCs margins) ziliongezwa kutoka TZS 108.69 kwa lita hadi TZS 110.57.

HALI YA UPATIKANAJI NA USAMBAZAJI MAFUTA BAADA YA KUANZA KUTUMIKA KWA KANUNI MPYA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini imeendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bishara ya mafuta hapa nchini. Ufuatiliaji uliofanywa kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta umedhihirisha kuwa kuna mafuta ya kutosha hapa nchini na pia kuna meli kadhaa ambazo zipo nje ya gati zikisubiri kupakua mafuta. Aidha, makampuni ya mafuta yameuza mafuta kwa wingi siku ya Ijumaa tarehe 5 Agosti 2011.

Hadi Ijumaa tarehe 05.08.2011, kiasi cha mafuta yaliyokuwepo katika maghala ya baadhi ya makampuni ya mafuta yaliyokaguliwa ni lita milioni 191.813 ambayo inakidhi matumizi ya nchi kwa kati ya siku 8 hadi 67 kulingana na aina ya mafuta kama inavyoonekana kwenye jedwali Na. 1 hapa chini:

Jedwali 1: Mafuta yaliyoko Nchini tarehe 05 Agosti 2011

Maelezo Mafuta ya Petroli Mafuta ya Dizeli Mafuta ya Taa Mafuta ya Ndege Mafuta Mazito
Akiba iliyopo(lita) 41,934,139 92,650,300 41,227,870 4,384,297 10,805,070
Wastani wa Matumizi kwa siku 875,000 3,100,000 615,240 560,500 1,087,695
Makadirio ya siku za kutumika 48 30 67 8 TAMKO LA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUHUSU UPATIKANAJI WA MAFUTA NCHINI

TAREHE 9 AGOSTI 2011, DODOMA

Mheshimiwa Spika,
Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kulishukuru Bunge lako tukufu kwa kunipa fursa hii ya kutoa taarifa kuhusu hali ya biashara ya mafuta ya petroli hapa nchini.

Kama tunavyofahamu, mafuta ya petroli ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu kwani viwanda, vyombo vya usafiri, na huduma nyinginezo nyingi hutegemea mafuta na bidhaa zake. Bei ya mafuta inapopanda, bei zingine nyingi hupanda kwa mfano bei za usafiri zinapanda, bei za vyakula zinapanda, bei za bidhaa za viwandani zinapanda; nakadhalika.

Mheshimiwa Spika, tarehe 22 Juni 2011 Serikali, kupitia kwa Waziri wa Fedha wakati akihitimisha Hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12, alitoa maagizo kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kuchukua hatua mbalimbali zitakazochangia kupunguza bei za mafuta. Hatua ambazo ziliagizwa kuchukuliwa ni pamoja na:
Ukokotoaji wa thamani ya shilingi kwa kuioanisha na Dola ya Marekani (yaani Exchange rate);
Kuondoa au kupunguza wigo wa asilimia 7.5 ambayo makampuni yaliruhusiwa kuwekwa ili kufidia baadhi ya gharama;
kupitia upya misingi ya ukokotoaji wa viwango vya tozo mbalimbali za taasisi za Umma kwa lengo la kubakia na tozo stahili na kwa viwango stahili bila kuathiri majukumu ya udhibiti ma usimamizi yanayofanywa na Taasisi hizo;
kupunguza tozo za kampuni za mafuta ikiwa ni pamoja na gharama za kibenki (yaani Financiang Charges); na
Upotevu wa mafuta yanayosafirishwa kwenye meli na gharama ya ukaguzi (yaani inspection fee).

HATUA ZILIZOCHUKULIWA NA SERIKALI

Serikali kupitia EWURA ilianza mara moja mchakato wa kurekebisha Kanuni ya ukokotoaji wa bei za mafuta hapa nchini kwa lengo la kuleta unafuu wa bei kwa mlaji. Hatua ya kwanza ilikuwa kuandaa hoja (discussion paper) ambayo ilitoa mapendekezo ya maeneo mbalimbali yanayofaa kurekebishwa ili kupata maoni ya wadau wa sekta ya mafuta. Mapendekezo hayo yalizingatia maagizo ya Serikali pamoja wa ushauri mbalimbali wa wadau katika sekta ya mafuta hapa nchini.

USHIRIKISHAJI WADAU
Mchakato wa kupata maoni ya wadau (taftishi) ulianza tarehe 4 Julai 2011 na kukamilika tarehe 26 Julai 2011. Kwa kawaida, mchakato huo ungechukua siku 81 lakini kutokana na unyeti wa suala hili, Mamlaka ililazimika kuufupisha hadi siku 23.

Mkutano wadau uliitishwa tarehe 22 Julai 2011 ili kupitia rasimu ya kanuni pamoja na jedwali la uchambuzi wa maoni ya wadau lililoandaliwa na EWURA. Wadau walioshirikishwa katika taftishi hiyo ni pamoja na makampuni ya mafuta, Baraza la Watumiaji wa Huduma zinazodhibitiwa na EWURA (Consumer Consultative Council), Baraza la Ushauri la Serikali, Taasisi za Umma kama vile TRA, TBS, WMA, TPDC, TPA, SUMATRA, na TIPER. Maoni mbalimbali ya wadau yalipokelewa na kuchambuliwa na EWURA ikiwa ni pamoja na kupata maoni ya wataalam kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Uchumi, Shirika la Maendeleo ya Mfuta Tanzania (TPDC), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, EWURA na Makampuni ya Mafuta.

Tarehe 23 Julai 2011, EWURA iliitisha kikao cha wawakilishi wa wadau wakubwa ambao ni pamoja na CCC, TPDC, TPA, Wizara ya Nishati na Madini, Mwanasheria Mkuu na baadhi ya makampuni ya mafuta kupitia mapendekezo yaliyokuwepo na kutoa maoni ya mwisho kabla ya kuwasilishwa kwenye Bodi kwa maamuzi.

MAAMUZI YA EWURA
Tarehe 26 Julai 2011, Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA ilikaa na kupitia mapendekezo ya marekebisho ya vipengele mbalimbali vya kanuni ya kukokotoa bei ya mafuta. Maamuzi hayo ya Bodi yamepelekea punguzo la bei za mafuta kwa viwango vifuatavyo: Petroli TZS 202.37; Dizeli TZS 173.49; na Mafuta ya Taa TZS 181.37. Mabadiliko haya ya bei ni sawa na punguzo la asilimia 9.17; 8.31; na 8.70 kwa mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa sawia. Kanuni hii ya kukokotoa bei za mafuta imeanza kutekelezwa kuanzia tarehe 03 Agosti 2011.

Tarehe 3 na 4 Agosti 2011 makampuni ya mafuta yaliwasilisha kutoridhishwa na maamuzi yaliyofanywa na EWURA hususan kuhusu kupunguzwa kwa wigo wa asilimia 7.5; margins za makampuni ya mafuta, na gharama za kuchelewesha meli bandarini (demmurage charges).

Kufuatia vikao hivyo vya Serikali, makampuni pamoja na EWURA siku ya Ijumaa tarehe 5 Agosti 2011, Mamlaka ya EWURA ilifanya marekebisho mengine katika vipengele vifuatavyo:
Gharama za ucheleweshaji meli bandarini (demmurage charges) ziliongezwa kutoka wastani wa TZS 1.85 kwa lita hadi TZS 8.76 kwa lita.
Viwango vya faida kwa kampuni za mafuta (OMCs margins) ziliongezwa kutoka TZS 108.69 kwa lita hadi TZS 110.57.

HALI YA UPATIKANAJI NA USAMBAZAJI MAFUTA BAADA YA KUANZA KUTUMIKA KWA KANUNI MPYA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini imeendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bishara ya mafuta hapa nchini. Ufuatiliaji uliofanywa kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta umedhihirisha kuwa kuna mafuta ya kutosha hapa nchini na pia kuna meli kadhaa ambazo zipo nje ya gati zikisubiri kupakua mafuta. Aidha, makampuni ya mafuta yameuza mafuta kwa wingi siku ya Ijumaa tarehe 5 Agosti 2011.

Hadi Ijumaa tarehe 05.08.2011, kiasi cha mafuta yaliyokuwepo katika maghala ya baadhi ya makampuni ya mafuta yaliyokaguliwa ni lita milioni 191.813 ambayo inakidhi matumizi ya nchi kwa kati ya siku 8 hadi 67 kulingana na aina ya mafuta kama inavyoonekana kwenye jedwali Na. 1 hapa chini:

Jedwali 1: Mafuta yaliyoko Nchini tarehe 05 Agosti 2011
10


MAUZO YA MAFUTA KWENYE MAGHALA (JUMLA)
Takwimu zilizowasilishwa EWURA na mkandarasi anayeweka vinasaba katika mafuta yauzwayo hapa nchini (GFI) na kuhakikiwa na wakaguzi wa EWURA zinaonesha kuwa kwa siku ya Ijumaa tarehe 5 Agosti 2011 mauzo ya mafuta kutoka kwenye maghala (depots) yalikuwa ni malori 329 kwa aina mbalimbali za mafuta, kwa ajili ya soko la ndani.

Tarehe 3 Agosti walipakia malori 40 wakati tarehe 4 Agosti 2011 yalipakiwa malori 185. Kwa kawaida, wastani wa mauzo kwa siku ni takriban malori 250 hadi 300. Takwimu hizi zinadhihirisha kuwa kuanzia tarehe 5 Agosti 2011, mauzo ya mafuta yameongezeka na kufikia kiwango cha kawaida.

Katika hali ya kawaida, makampuni mengi ya mafuta hayafanyi kazi katika siku za mapumziko. Kwa hiyo, siku ya Jumamosi tarehe 6 Agosti 2011, jumla ya malori 115 yalipakia mafuta.

MAUZO YA MAFUTA KWENYE VITUO (REJAREJA)
Ukaguzi uliofanywa na EWURA kwenye vituo vya mafuta jijini Dar es Salaam na baadhi ya mikoa unaonesha kuwa vituo vingi vilianza kuuza mafuta kama kawaida. Ukaguzi huo pia umehusisha kupata takwimu za mafuta yaliyopo kwenye vituo ili kuhakikisha kuwa hakuna kituo kinachohodhi mafuta na kuacha kuuza. Kuna baadhi ya vituo vilikuwa vikisubiri kupata mafuta kwa vile walikuwa wameishiwa, hasa kwa sababu makampuni ya mafuta hayakuuza mafuta kwa kiwango cha kawaida siku ya tarehe 3 na 4 Agosti 2011.

Makampuni mengi yaliendelea kupakia malori ya mafuta mpaka usiku 5 Agosti 2011 hivyo ilitarajiwa kwamba kungekuwa na usambazaji mwingi zaidi kwenye vituo kuanzia Jumamosi tarehe 6 Agosti 2011.

VIWANGO VYA BEI
Ukaguzi uliofanywa na EWURA unaonesha kuwa bei za mafuta kwenye vituo vinavyouza mafuta zimezingatia bei kikomo zilizotolewa na Mamlaka ya EWURA tarehe 3 Agosti 2011. Ukaguzi huo umefanyika katika miji ya Arusha, Moshi, Dar es Salaam na Dodoma. Aidha, hakuna taarifa zilizopokewa na EWURA kutoka mji wowote kuhusu kukiukwa kwa bei kikomo iliyopo sasa.

HATUA ZINAZOCHUKULIWA NA SERIKALI

Mheshimiwa Spika, bidhaa za mafuta ya petroli inatoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi katika nchi zote duniani. Upatikanaji wa uhakika wa mafuta na kwa bei stahili vitafanya uchumi wa nchi yetu kukua kwa kasi zaidi na kuwa endelevu.

Serikali inachukua hatua zifuatazo ili kuhakikisha kuwa mafuta ya kutosha yanapatikana sehemu zote nchini.

Serikali kupitia EWURA inafuatilia mwenendo wa usambazaji wa mafuta kutoka katika maghala ya makampuni ya mafuta kwenda kwenye vituo vya mafuta;

Serikali kupitia EWURA itachukua hatua za kisheria kwa kampuni zilizokiuka masharti ya leseni na kusababisha uhaba wa mafuta kwenye vituo vya kuuza mafuta nchini;
Leo Serikali kupitia EWURA imeipa leseni COPEC kampuni tanzu ya Serikali kupitia TPDC kuanza kufanya biashara ya mafuta mara moja; na

Serikali kwa kupitia EWURA imekamilisha taratibu za uagizaji wa mafuta kwa pamoja ili kuhakikisha kuwa mafuta yanapatika na kwa gharama nafuu zaidi wakati wote.

Mheshimiwa Spika, kufuatia hali iliyojitokeza, EWURA imetoa Compliance Order kwa makampuni manne ambayo ni BP, Engen, Oilcom na Camel Oil, ambapo wanatakiwa watekeleze hatua zifuatazo:
Mara moja wanatakiwa kuanza kutoa huduma katika maghala yao ikiwa ni pamoja na kuanza kuuza mafuta katika vituo vya rejareja ikiwemo vituo vilivyo chini ya miliki zao;
Waache mara moja kitendo chochote kitakachosababisha upungufu wa makusudi wa mafuta ya petroli katika soko la Tanzania; na katika kipindi cha masaa 24 wajieleze kwa nini wasichukuliwe hatua za kisheria dhidi yao kwa kukiuka matakwa ya Sheria ya Mafuta pamoja na Sheria ya EWURA.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuisha kwa muda uliotolewa na EWURA, adhabu stahiki zitatolewa kwa wahusika ikiwa ni pamoja na kusitisha ama kufuta leseni.

Mheshimiwa Spika, katika hali ya kawaida na kwa mujibu wa Sheria, mtu asiporidhika na maamuzi ya EWURA anapaswa kukata rufani katika Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal). Hatua hii haijafuatwa hadi sasa na Serikali ingeshauri kwamba masuala kama haya ni vema yakafuata taratibu za kisheria.

Mheshimiwa Spika; naomba kuwasilisha.

Blog Mpya ya Katuni



Njia za mitaani (Vichochoro) zimegeuzwa kuwa vyoo vya wapita nijia, Je, huu nao ni ujanja?? MUUNGWANA NI VITENDO


Kwa KATUNI, VIELELEZO na MICHORO aina zote mnakaribishwa Blog maridhawa ya katuni:
http://www.artsfede.blogspot.com/

Maoni na ushauri vinakaribishwa pia.

--
FeDe; Freelance Artist
P.O.Box 79267,
Dar-es-Salaam, Tanzania.
Mob; +255 783 006545
Blog; www.artsfede.blogspot.com

Father Kidevu ana Blogu Mpya

UNAKARIBISHWA FATHER KIDEVU BLOG www.mrokim.blogspot.com KUPATA HABARI KATIKA PICHA.

FATHER KIDEVU BLOG www.mrokim.blogspot.com , for local and International news in picture.

--

Mroki Mroki

Director MD Digital Company
General Secretary PPAT
Professional Photojournalist & BLOGGER
P.O.BOX 110097,
Mob: +255 755 373999 /+255 717 002303,
Email: mrokim@gmail.com.
Blog: www.mrokim.blogspot.com
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Thursday, August 04, 2011

A Little Black Girl

Nimepata kwa email:

A stranger was seated next to a little black girl on the airplane when the stranger turned to her and said, "Let's talk. I've heard that flights go quicker if you strike up a conversation with your fellow passenger."
The little girl, who had just opened her coloring book, closed it slowly and said to the stranger, "What would you like to talk about?"
"Oh, I don't know," said the stranger. "Since you are an Afro American, do you think that So-called President Barak Obama is qualified for the job?" and he smiles.
"OK", she said. 'That could be an interesting topic. But let me ask you a question first. A horse, a cow, and a deer all eat the same stuff - grass -. Yet a deer excretes little pellets, while a cow turns out a flat patty, and a horse produces clumps of dried grass. Why do you suppose that is?"
The stranger, visibly surprised by the little girl's intelligence, thinks about it and says, "Hmmm, I have no idea."
To which the little girl replies, "Do you really feel qualified to discuss President Barack Obama...when you don't know s--t?"


Rais Obama Asherekea 50th Birthday!


Leo Rais Barack Obama wa Marekani anasherekea miaka hamsini tangu kuzaliwa kwake (nusu karne). Alizaliwa Hawaii, USA siku ya Agosti 4, 1961.


Tuesday, August 02, 2011

Marudio - Miaka Baada ya tukio kaniomba Msamaha!

(Pichani Ukaguzi wa Gwaride Mlale JKT Songea - Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

Naona, kuna 'Anonymous' fulani kagusia hii swala ya yalionipata nikiwa jeshini JKT. Watu wengi wamenitumia e-mail kuulizia details. Nimeamua kuibandika tena. Ni posti ya kutoka April 2006. Lakini mjue enzi za JKT, wasichana wengi walinyanyaswa kijinsia, mimi nilikuwa na bahati maana nafahamu wasichana waliokuwa gang raped. Dada fulani, alimkubali afande, alivyomaliza kaita wenzake kwa kusema, "Njooni, Mboga hii hapa!" Yule dada hakuweza kutembea vizuri kama wmezi baada ya hapo!

*****************************************************************************

Nilipokuwa Jeshi ya Kujenga Taifa (JKT) karibu nibakwe na afande Fulani (jina nahifadhi). Lazima niseme kuwa katika kipindi hicho wanaume wengi waliona makambi ya JKT kama ‘buffet’ ya wasichana. Si maafande wa jeshi tu, bali hata viongozi wa serikali walikuwa wanapitia makambi ya JKT kula tani yao!

Mimi nilikuwa Masange JKT, Tabora. Wakati huo huyo jamaa alikuwa ni Kepiteni wa JKT. Nadhani alidhania kwa vile yeye ni kepiteni basi alikuwa na haki ya kutembea na yeyote aliyemtaka. Kwangu aligonga ukuta! Bila shaka alikuwa hajawahi ‘kunyimwa’ mpaka siku hiyo alipokutana na mimi.

Miaka baada ya tukio nikiwa nafanya kazi Daily News mara nyingi nilikuwa napishana naye Posta Mpya. Basi ananisemesha, na mimi namnunia halafu napita zangu kimya bila kumjibu kwa hasira. Siku moja kanisimamisha kaniambia, "Chemi, naomba msamaha, nisemahe tafadhali, kweli nilikukosea!” Aliongeza kuwa miaka mingi imepita hivyo sina sababu ya kuwa na hasira naye! Na mimi nilimjibu, “Mshenzi sana wewe!” nikaenda zangu.

Ikapita kama mwaka mwiingine. Jamaa anaendelea kunisalimia kila nikimpita njiani na mimi kwa uchungu bado nikashindwa kusema kitu. Basi nikafikiria alichoniambia Posta Mpya. Lakini niliona kama jambo hilo linamsumbua. Na nikasema kama Bwana Yesu aliweza kusamehe watu kwa madhambi yao kwa nini mimi nisimsamehe. Basi baada ya hapo ikiwa nikimwona na akinisalimia naitika na naendelea zangu na nikaona kidogo hata yeye alikuwa na raha.

Lakini bado najiuliza kama kitendo chake kilimsumbua miaka na miaka kama ilivyonisumbua mimi.Unauliza ilikuaje mpaka nikajikuta kwenye situation ya kubakwa. Au mnasema nilitaka mwenyewe. Ngoja niwaelezee ilivyokuwa.

Nilikuwa mhudumu Officer’s Mess, mpishi na msafishaji. Huyo jamaa alikuwa ni mgeni kutoka Makao Makuu ya JKT Dar es Salaam. Kwa kweli sikutaka kufanya kazi pale Mess lakini tulichaguliwa special na Matron, mimi kwa vile niijua kupika vyakula mbalimbali hasa za kizungu. Lakini uzuri wa hiyo kazi ni kuwa uanambulia mabaki ya vyakula (leftovers), na mara nyingine kulikuwa hakuna.

Basi huyo Afande alikaa kambini wiki kadhaa. Katika kumhudumia tukawa tunaongea na mimi nikawa namheshimu kama kaka vile. Wala sikusikia mapenzi yoyote kwake. Basi jioni fulani, kanialika chumbani kwake kunywa soda na biskuti na kwa Maongezi zaidi. Sasa kama ulienda jeshi unajua njaa kali unayokuwa nayo. Nikaenda, kanikaribisha vizuri, nilipewa soda na tukawa tunaongea. Basi nikaona mwenzangu anabadilika ghafla! Mara ananikumbatia kwa nguvu, na kunibusu na mengine. Nikajaribu kuaga lakini jamaa hakuniachia. Baada ya ku-plead naye aniachie, kaniachia. Kaomba msamaha na kaniomba niendelee kukaa nimalize hizo soda alizoninulia.

Kama mjinga nikamwamini, nikakaa nakunywa hizo soda. Tukaendelea na Maongezi, kukaa kidogo huyo kanirukia, najaribu kusimama huyo, kanivuta na kuniangusha kitandani! Mimi saa hizo nikawa naogopa kabisa nia yake!Kaniambia eti, “ukipiga makelele najua nitasema nini! Nyamaza! Huna sababu ya kunikatalia!” LOH! Kanizaba kibao! Nikamwuliza kwa nini anaifanyia hivyo, na mimi nilikuwa namwona kama kaka yangu!Hapo sasa ikaniingia. Nabakwa! Loh!

Nilimpiga mangumi na mateke lakini jamaa alikuwa na nguvu huyo kachana chupi yangu! Baada ya hapo, jamaa kashika miguu yangu huko anafoka kwa sauti kama vile anatoa amri “panua miguu! PANUA MIGUU!” Huko katoa ume wake uliyosimama kwenye suruali! Basi kuona sipanui jamaa kaongeza makofi na kafanikiwa kupanua miguu yangu! Kuona kafanikiwa kupanua huyo kajaribu kupenya. Ilipogusa kwangu nilipiga kelele cha kufa! Nikasema, “Nakuufaaaa!”

Heh! Ghafla jamaa kaniachia kaniambia niende. Alisema, “Nimeigusa na ume wangu, unatosha!” Nenda zako! Na ukimwambia mtu najua nitasema nini!”Loh nilikimbia bwenini na giza lile la Masange huko nalia. Wenzangu wananiuliza vipi, nikashindwa niseme nini! Kwanza niliona haya! Fikiria, niliona haya (shame)!Kesho yake nikaenda dispensary na kujiandikisha mgonjwa. Sikwenda kazini Officer's Mess bali nililala bwenini.

Siku iliyofuatia huyo Afande mshenzi kapita bwenini kwetu kaulizia hali yangu, na mimi huko natetemeka kwa woga nikashindwa niseme nini. Alininunulia Orange squash na biskuti na kuzileta bwenini. Sitasahau alivyonitazama! Ilikuwa kama vile anapanga jinsi gani atanipata. Baada ya hapo alimwopoa msichana mwingine na huyo alimkubali kabisa. Akawa analala kabisa huko Officer’s Mess. Hakuna anayemsumbua wakijua ni bibi wa Afisa. Basi, siku za yule jamaa kukaa kambini zikaisha, na yule binti alienda naye Tabora mjini kwa siku kadhaa. Halafu jamaa karudi zake DSM. Yule binti karudi zake kambini! Kumbe alienda bila pass. Alidhania kwa vile yuko na mkubwa hana haja ya pass. Na yule Afande ndo kaondoka kimoja! Maafande waliobakia wacha wamtese huyo binti alivyorudi kambini! Walimtesa kwa Extra drill na mengine mpaka ikabidi Military Police waombe wakuu wamsamehe la sivyo atakufa. Raha yake iliishia kwa suluba! Sijui yule binti alidhania jamaa atamwoa! Kwa nini alimkubali yule mshenzi.

Anyway, kila mtu na vyake. Alivyotoka kwenye suluba tulimwuguza! Siku haizkupita na mimi nilitolewa kazi Officer’s Mess na kupelekwa kwenye kikosi cha Ujenzi na lazima nisema hapo nilifurahi sana. Basi miaka ilipita. Mimi nilikuwa mwandishi wa habari Daily News, tena nilijenga jina. Sasa nikawa napishana na yule jamaa huko kapandishwa cheo na yuko JWTZ. Jamaa anajaribu kunisalimia na mimi napita zangu kimya, namnunia kabisa.

Nilimwona mshenzi, mnyama, na kila kitu kibaya ndo ilikuwa yeye! Angefanikiwa kuingiza na kunimwagia uchafu wake ningejiona mchafu mpaka leo! Miaka kama 20 imepita sasa na bado nina uchungu naye.Jamani nyie wanaume nawaambia kubaka kinaathari zake kwa wanawake. Unataka raha ya dakika na unamwachia mwenzio na uchungu wa maisha! Wengine mpaka wanakuwa wagonjwa wa akili.

Kwa nini nimeamua kuzungumzia kubakwa kwangu hapa, ni kwa sababu naona wasichana wengi wanabakwa, halafu wanaamua kunyamaza kimya. Kisa wakienda polisi na hospitali wanahofia kuambiwa ni Malaya au walitaka wenyewe! Hata mwamanke mwenzako anaweza kukufokea kuwa ulitaka mwenyewe. Tanzania, wanaume walikuwa na usemi wao kuhusu wanawake na ngono. Walisema eti ukimwomba mwanamke halafu akijibu ndiyo, manake ndiyo atafanya. Akisema labda, manake atafanya, akisema hapana, manake hapana. Lakini jamani tendo si inakuwa tamu kama wote mmekubali? Na kama angefanikiwa kuingiza si angeniumiza sana!

Wengine wanasema ningemshitaki. Je, ningemshitaki ingekuaje? Kwanza jeshini mimi ningepewa Extra Drill mpaka niumie au kufungwa jela ya jeshi iliyojaa maji na mbu kusudi niteswe. Kumbuka ilikuwa Tanzania na yule alikuwa ni Kepiteni wakati huo na mimi nilikuwa Private. Hakuna ambaye angekuwa tayari kunisikia zaidi ya wenzangu maPrivate, na yeye alijua hivyo. SHENZI TAIPU!