Sunday, February 08, 2009

Anguilla Katika Picha

Nilipiga picha hii nikiwa kwenye ferry. Anguilla haina milima mirefu! Kutoka angani inaonekana fleti kama imepigwa pasi.
Barabara ya kuelekea kwenye hoteli ya fahari (5Star) Cap Juluca. Kwa mbali unaweza kuona kisiwa cha St. Maarten

Ukihitaji maji unaletewa. Ukitaka tanki nzima ni dola $500! Watu wengi wanakinga maji ya mvua.

Mbuzi wa Anguilla ( Waingereza waliabika mwaka 1969 walipovamia Anguilla na kukutana wa wafuga mbuzi badala ya wapiganaji)

Mzungu akijipika juani! Wazungu huko wameungua na jua, wengine wekenduuu! Kwa nini wanataka kuwa weusi halafu wanadharau watu weusi?
Anguilla Health Authority

Huyo Rasta Man anamtungia huyo Bi Kizee wimbo hapohapo. Huyo Bi Kizee anaitwa Nancy na ilikuwa party ya kusherekea Birthday yake....ana miaka 75. Rum punch zilikuwa zimenikolea lakini wimbo ulisema kitu kama, Nancy is so beautiful but she got ugly man.

Usikojoe hadharani!

Boti inajengwa kwa ajili ya mashindano ya mashua. Kushindana mashua ni mchezo mkuu wa Anguilla.
Barabara za Anguilla ni nzuri hazina mashimo. Kwa vile ni kisiwa kadogo, hakuna barabara enye njia zaidi ya mbili. Niliamua kuingia kwenye maji, lakini yalikuwa baridiii! Mchanga kwenye beach zao ni mweupe halafu laini kama unga!
Hapa ni Blowing Point Beach
Ferry iliyonipeleka uwanja wa ndege St. Maarten. Ukitaka kwenda Anguilla inabidi uende kwenye kisiwa jirani cha St. Maarten ambayo iko chini ya waHolanzi na waFaransa. Anguilla ni koloni ya Uingereza.

Ndege wa Taifa wa Anguilla ni Turtle Dove
Jogoo akitamba Anguilla

Watoto wa shule huko wanachukuliwa na School Bus, huduma ya school bus inalipiwa na serikali

Nyumba asili ya Anguilla. Nilibishana na watu huko kuhusu hizo nyumba, walisema eti nyumba asili (huts) za waafrika ni ndogo zaidi. Nikwaambia nyumba zao asili ni ndogo kweli!

Nyumba ya James Ronald Webster ambaye anaitwa mkombozi wa Anguilla. Bwana Webster aliongoza mapinduzi huko mwaka 1967. Mwaka 1969 waingereza walipavamia na walipokelewa kwa shangwe na wenyeji.

1 comment:

Anonymous said...

Asante kwa kutelemisha Da Chemi. Mimi ndo leo nimejifunza kuhusu hiyo nchi hata sikujua kama upo. Naijua Jamaica na Barbados.