Sunday, March 02, 2014

Afrika Inawakilishwa Katika Oscars ya Mwaka Huu!

Wadau, tunangojea kwa hamu kuona kama Lupita Nyong'o kutoka Kenya na Barkhad Abdi mwenye asili ya Somalia watashinda katika tuzo za Oscars leo jioni.

Kwa mara ya kwanza Nchi mbili za Afrika zinawakilishwa katika Tuzo za Juu za Oscars.

Lupita Nyong'o  yuko katika Best Supporting Actress (yaani mwigizaji bora wa kike katika sinema si mwigizaji mkuu).  Na Barkhad Abdi anagombea Best Supporting Actor (yaani mwigizaji bora wa kiume - si mwigizaji mkuu).

Jamani, jamani sijui waafrika tukoje, huyo Barkad kasemwa na waSomali wenzake, eti ana sura mbaya na mengine! Khaa! 

Na nisimsahahau Chiwetel  Ejiofor ambaye ni Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.  Yeye anagombea Mwigizaji bora wa kiume. (Best Actor).

Kushoto ni Lupita Nyong'o na Kulia ni Barkhad Abdi

Mara nyingi nchi ya Afrika inayopata sifa katika Osars ni Afrika Kusini.  Waigizaji wao wazungu kama Charlize Theron wanatambulika sana.  Charlize alikuwa Msouth Afrika wa kwanza kupata Oscar.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

1 comment:

Anonymous said...

Congratulations LUPITA!