Showing posts with label Rambirambi. Show all posts
Showing posts with label Rambirambi. Show all posts

Thursday, April 02, 2015

Unaweza Kutoa RambiRambi Kwa Familia ya Che-Mponda Kupitia GoFundME


 Mnaweza kutoa Rambirambi kwenye GoFundMe.  Hii ni linki.

You can contribute towards Dr. Aleck Che-Mponda's funeral expenses on GoFundMe.  The link is below.

https://funds.gofundme.com/dashboard/drchempondafund


The late Dr. Aleck H. Che-Mponda 1935-2015

Tuesday, August 19, 2014

Rais Kikwete Atoa Rambirambi Kwa Familia ya Jaji Makame



Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwafariji wafiwa walipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame Masaki jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Agosti, 2014.

 Mama Salma Kikwete akiweha saini katika kitabu cha maombolezo alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Mheshimiwa Lewis Makame Masaki jijini Dar es salaam aliyefariki  katika Hospitali ya AMI Trauma Centre Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Agosti, 2014.

PICHA NA IKULU

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 Rais  wa Jamhuri  ya  Muungano wa Tanzania,  MheshimiwaDkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za  RambirambiMwenyekiti  wa  Tume ya  Taifa  ya  Uchaguzi,  National  Electoral Commission  (NEC)  kufuatia taarifa  za  kifo  cha  aliyekuwaMwenyekiti wa Kwanza wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu, MheshimiwaLewis  Makame  kilichotokea  katika  Hospitali  ya  AMI  TraumaCentre Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Agosti, 2014.

 “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifocha  Jaji  Mstaafu  wa  Mahakama  ya  Rufaa  Tanzania  naMwenyekiti  wa  Kwanza  wa  Tume ya  Taifa  ya  Uchaguzi(NEC)  chini  ya  Mfumo  wa  Vyama  Vingi  vya  Siasa,Mheshimiwa  Lewis  Makame  ambaye  amelitumikia  Taifaletu  katika  Utumishi  wa  Umma  kwa  uaminifu,  uadilifu,bidii  na  umahiri  mkubwa”,  amesema  kwa  masikitiko  RaisKikwete katika Salamu zake.

  Katika utumishi wake, Marehemu Jaji Lewis Makame, enzi zauhai wake, alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kabla yakuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa na baadaye Mwenyekiti wa NECambayo  aliiongoza  kwa  miaka  17  mfululizo  hadi  alipostaafumwaka 2011.  Uongozi wake ulichangia sana kuimarisha amani,utulivu, umoja na mshikamano wa kitaifa katika mazingira mapyaya demokrasia ya vyama vingi vya siasa hapa nchini.“Ni  kwa  kutambua  kipaji  kikubwa  cha  uongozialichokuwa  nacho  Marehemu  Jaji  Lewis  Makame,  Taifa.

Thursday, May 15, 2014

Tanzia - Private Brian Salvatory Rweyemamu (JWTZ)




 
Private Brian Salvatory Rweyemamu JWTZ (19? - 2014)

Bwana Salvatory Rweyemamu wa Kinondoni Dar es Salaam, anasikitika kutangaza kifo cha mtoto wake mpendwa Private Brian Salvarory Rweyemamu aliyefariki alfajiri ya kuamkia leo tarehe 15 Mei, 2014 katika hospitali ya Jeshi Lugalo alipolkuwa akitibiwa.

Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa Bwana Salvatory Rweyemamu Kinondoni jirani na Vijana (Mango Garden).

Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki walioko Dar es Salaam, Kagera, Malawi, Afrika Kusini, Uingereza na Canada.

*************************************** 
Asante Kaka Michuzi kwa Taarifa.
Poleni sana familia ya Rweyemamu. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

Wednesday, July 24, 2013

Pesa Ina Majina Mengi



PESA INA MAJINA MENGI. Ona;

Kwenye ibada inaitwa Sadaka au Zaka,

Msibani inaitwa Rambirambi,

Shuleni inaitwa Ada au Karo,

Kwenye Vyombo Vya Usafiri inaitwa Nauli,

Ukinunulia Haki inaitwa Rushwa,

Kumdhaminia Mtu Mahakamani inaitwa Dhamana,

Pesa ya uchumba inaitwa POSA,

Pesa ya itolewayo mtu akabidhiwe mke inaitwa MAHARI.

Je PESA inayohongwa kwa mpenzi inaitwaje?

 Jibu tafadhali.

Thursday, September 06, 2012

Rais Kikwete Atuma Salamu za Rambirambi Kwa Kifo cha Lt. Col. Adam Makwaia

Lt. Colonel  (ret.) Adam  Hussein Makwaia

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha Luteni Kanali (mst) Adam Hussein Mwandu Makwaia, aliyekuwa Mpambe wa Rais wa kwanza wa Tanzania, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Rais Ali Hassan Mwinyi.

Katika salamu zake, Rais Kikwete amemwambia Jenerali Mwamunyange: “Nimepokea kwa majonzi na masikitiko taarifa za kifo cha Luteni Kanali Makwaia ambaye nimejulishwa kuwa alipoteza maisha Jumanne, Septemba 4, mwaka huu, 2012, katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo mjini Dar es Salaam.”

“Katika miaka yote ya utumishi wa Jeshi na utumishi wa umma, Luteni Kanali Makwaia alikuwa mwadilifu na mwaminifu kwa nchi yake, alikuwa na weledi wa kiwango cha juu katika taaluma yake ya kijeshi na alikuwa mtiifu kwa viongozi wake. Nakutumia wewe Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi salamu zangu za rambirambi kufuatia kifo hiki,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:

“Aidha, kupitia kwako natuma salamu za pole nyingi kwa familia ya marehemu Makwaia ambao wamempoteza baba na mhimili wa familia. Pia, kupitia kwako, natuma salamu za rambirambi kwa maofisa na wapiganaji wote wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao wamempoteza ofisa na mpiganaji mwenzao.”

Luteni Kanali (mst) Makwaia alijiunga na Jeshi Machi 24, mwaka 1974, na alilitumikia kwa miaka 23 na miezi tisa kabla ya kustaafu. Alikuwa Msaidizi wa Mpambe wa Rais kati ya mwaka 1978 na 1981 na kuwa Mpambe wa Rais kwa miaka sita hadi 1987. Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 62.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Septemba, 2012
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ndugu jamaa na marafiki wa Hayati Luteni Kanali (mst) Adam Hussein Mwandu Makwaia leo Septemba 6, 2012 Keko, jijini Dar es salaam.


Hayati Luteni Kanali (mst) Adam Hussein Mwandu Makwaia, akiwa kazini kama  Mpambe wa Rais wa kwanza wa Tanzania, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na baadaye  Rais wa pili wa Tanzania Alhaj  Ali Hassan Mwinyi.


Monday, April 09, 2012

Mama Bishanga na Ohio Wamlilia Kanumba

MAMA BISHANGA NA OHIO WAMLILIA KANUMBA

Nimeguswa na kuumizwa sana na msiba  wa ghafla wa msanii wenzangu wa tasnia ya filamu,  Steve Kanumba, ndugu yetu, kijana wetu, rafiki yetu na mtanzania mwenzetu alietuachia pengo lisilozibika. Itatuchukua muda mrefu sana kusahau msiba huu wa taifa zima kutoka na umahiri wake, juhudi zake na kazi nzuri alizozifanya kwa kipindi kifupi cha uhai wake. 

Nachukua nafasi hii pia kuwapa pole wazazi wake, mimi kama mzazi niko nanyi katika kipindi hiki kigumu sana, nimekuwa nawakumbuka sana katika sala tangu jana nilipopata habari hizi. Poleni sana.

STEVE TULIKUPENDA, TUNAKUPENDA NA TUTAENDELEA KUKUPENDA, MUNGU AKUPOEE KWA AMANI NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE KATIKA JINA LA YESU KRISTO BWANA NA MWOKOZI WETU, AMEN

MRS CHRISTINA INNOECENT MAROLEN
MAMA BISHANGA
OHIO/ USA

Sunday, September 11, 2011

Rambirambi Kwa Waliopata Ajali ya Meli Zanzibar Kutoka Montreal- Canada

Ndugu zetu Watanzania,

Kwa niaba ya Watanzania na wananchi wote wa Afrika Mashariki waishio hapa Montreal- Canada, tumezipokea kwa majonzi na mshtuko mkubwa taarifa za ajali ya kuzama kwa meli ya MV Spicer jana usiku, tarehe 10/9/2011 iliyosabababisha vifo vingi vya Watanzania wenzetu kutoka Zanzibar.

Kwa niaba ya Uongozi wa Montreal Tanzanians Association (http://www.montrealtanzanians.com/), tunapenda kutoa salamu zetu za rambirambi kwa wananchi wote wa Zanzibar na Pemba na Tanzania kwa ujumla waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki zao wapendwa katika kindi hiki kigumu cha maombolezo.

Na pia tungependa kuwapa pole wote waliokoka kwenye ajali hiyo ya kusikitisha na tunawaombea kwa M/Mungu awapuguzie maumivu na awape nguvu na faraja.

Mwisho kabisa, Montreal Tanzania Association (MTA) ingependa kutoa shukrani na pongezi za dhati kwa wote walioshiriki katika harakati za kuokoa maisha ya wahanga wa ajali hii na pia katika shughuli za kuopoa maiti.

Tunamuomba Mwenyezimungu aziweke mahali pema peponi nafsi za wote waliopoteza maisha yao kwenye ajali hii. Ameen.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

Uongozi,

http://www.montrealtanzanians.com/ (MTA)