Showing posts with label ZIFF. Show all posts
Showing posts with label ZIFF. Show all posts

Sunday, June 15, 2014

Balozi Sefu Iddi abariki tamasha la 17 la ZIFF 2014 visiwani Zanzibar

DSC_0157

Makamu wa Rais wa Pili wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi akisalimiana na baadhi ya wageni alipowasili kwenye ufunguzi wa Tamasha la 17 la ZIFF Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF Mh. Mahmoud Thabit Kombo.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).

DSC_0159

Mgeni rasmi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi akisalimiana na Mgeni maalum mwalikwa mwigizaji wa filamu ya MANDELA "Long Walk to Freedom" Terry Pheto ambayo ilifungua tamasha hilo la 17 la ZIFF usiku wa kuamkia leo visiwani Zanzibar.

DSC_0158

Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Mh. Mahmoud Thabit Kombo akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Wananchi Group ambao ni wadhamini wa ZIFF kupitia ZUKU, Bw. Mohammed Jeneby wakati wa tamasha hilo.

DSC_0164

Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na mabalozi kwenye ufunguzi wa tamasha la 17 la ZIFF.

DSC_0174

DSC_0234

Pichani juu na chini ni kikundi cha burudani cha TANURI kutoka Egypt wakitoa burudani kwenye tamasha la 17 la ZIFF.

DSC_0300

DSC_0289

DSC_0386

Mkurugenzi Mkuu wa ZIFF, Profesa Martin Mhando akimkaribisha mgeni Mgeni maalum mwalikwa mwigizaji wa filamu ya MANDELA "Long Walk to Freedom" Terry Pheto kwenye jukwaa.

DSC_0391

Mgeni maalum mwalikwa mwigizaji wa filamu ya MANDELA "Long Walk to Freedom" Terry Pheto akielekea jukwaani wakati wa ufunguzi wa tamasha la 17 la ZIFF 2014.

DSC_0391

DSC_0395

Picha juu na chini Mgeni maalum mwalikwa mwigizaji wa filamu ya MANDELA "Long Walk to Freedom" Terry Pheto, akizungumzia changamoto mbalimbali na mafanikio aliyoyapata baada ya kushiriki kwenye filamu hiyo.

DSC_0409

DSC_0414

Mmoja wa wageni waalikwa akimpongeza mgeni maalum mwalikwa mwigizaji wa filamu ya MANDELA "Long Walk to Freedom" Terry Pheto kwa kazi nzuri aliyofanya kupitia filamu yake.

DSC_0217

Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Mh. Mahmoud Thabit Kombo akimkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Pili wa Rais Balozi Sefu Iddi jukwaani kuzindua rasmi tamasha hilo.

DSC_0213

Mgeni rasmi Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi akisoma hotuba wakati akizindua rasmi wa Tamasha la 17 la filamu la nchi za Majahazi (ZIFF) linaloendelea kwenye viunga vya Ngome Kongwe visiwani Zanzibar.

DSC_0344

Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Mh. Mahmoud Thabit Kombo (kushoto) akimtambulisha mwakilishi wa Com-Net Zanzibar Bw. Mohammed (kulia) kwa Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi.

DSC_0348

Mwakilishi wa Com-Net Zanzibar Bw. Mohammed akikambidhi zawadi ya kifurushi cha Internet ya mwaka mzima mgeni rasmi Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi .

DSC_0351

Mgeni rasmi Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sefu Ali Iddi akimshukuru mwakilishi wa Com-net mmoja wa wadhamini wa tamasha hilo kwa zawadi hiyo.

DSC_0332

Mkurugenzi Wananchi Group ambao ni wadhamini wa ZIFF kupitia ZUKU, Bw. Mohammed Jeneby akizungumzia udhamini wao wa miaka 10 kwenye tamasha hilo ambapo kwa sasa lina mwaka wa tatu.

DSC_0490

Meza kuu ikifuatilia filamu ya "Long Walk to Freedom" inayozungumzia maisha ya MANDELA wakati wa ukombozi wa mtu mweusi kutoka kwa makaburu.

DSC_0375

Mwigizaji Terry Pheto akifurahia jambo wakati wa kutazama filamu yake.

DSC_0342

Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na mabalozi kwenye ufunguzi wa tamasha la 17 la ZIFF.

DSC_0370

Picha juu na chini wakazi wa Zanzibar na wageni mbalimbali kutoka nje ya Tanzania wakitazama filamu ya "Long Walk to Freedom kwenye ukumbi wa Ngome Kongwe linakoendelea tamasha la 17 la ZIFF.

DSC_0317

DSC_0316

DSC_0431

Mwigizaji Terry Pheto akipozi na mmoja wa ushers waliokuwa wakikaribisha wageni kwenye tamasha hilo.

DSC_0574

Mdau Lucy (wa pili kushoto) katika pozi na picha yake kwenye viunga vya Ngome Kongwe wakitoa huduma ya vinywaji.

Thursday, June 05, 2014

Lupita Nyong'o atakuwa ZIFF

*Geneviveve Nnaji na John Dumelo nao ndani

*Habib Koite, Didier Awadi kuburudisha

*Filamu ya Mandela kufungua pazia

DSC_0021

Mkurugenzi Mkuu wa ZIFF, Profesa Martin Mhando (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuzindua rasmi Tamasha la Filamu la nchi za Majahazi la 17 maarufu kama Zanzibar International Film Festival (ZIFF). Kulia Msaidizi wa Kitengo cha habari ZIFF, Lara Prieston, Kushoto ni Meneja wa Tamasha la ZIFF, Daniel Nyalusi (Dean), Afisa Mawasiliano wa ZIFF, Hassan Musa "Has T" (wa pili kushoto) na Music Coordinator wa ZIFF, Edward Lusala (katikati). Picha na Zainul Mzige wa modewjiblog

Na Andrew Chale

DUNIA inatarajia kushuhudia tukio kubwa na la kihistoria ndani ya viunga vya Ngome Kongwe ndani Mji Mkongwe wa Stone Town, Unguja, kwa watu wa mataifa yote watakapoungana na kushuhudia ‘Hatma ya Pamoja’ (A common Destiny) Juni 14 hadi 22, 2014, katika Tamasha la Kimataifa la filamu la Zanzibar (ZIFF).

Tamasha hilo maarufu kama filamu la nchi za Majahazi ZIFF, kwa mwaka huu linatarajiwa kufanyika kwa mara ya 17, tokea kuanzishwa kwake.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es Salaam, kwenye halfa maalum ya uzinduzi wa tamasha hilo la 17, kwa wandishi wa habari iliyofanyika Goethe Institut kituo cha utamaduni, Mkurugenzi Mkuu wa tamasha hilo, Profesa Martin Mhando, alisema tamasha hilo msimu wa mwaka huu linatarajiwa kuwa moto kwani linakuja na mambo mbalimbali yenye kuleta mabadiliko ya hali ya juu.

Ni kutokana na mabadiliko hayo, Profesa Mhando anasema tasnia ya filamu kwa Tanzania inahitaji kubadilika ikiwemo wasanii wenyewe kujituma na hata kuingia darasani ili kufanya kazi zenye uhakika.

Akimaanisha kila msanii wa filamu aweze kufikia malengo yake, hana budi kujifunza na kushirikisha wale waliotangulia katika tasnia hiyo.

Anazungumziaje kaulimbiu ya ‘A Common Destiny’

Prof. Mhando amesema kauli mbiu ya mwaka huu yenye kusema Hatma ya pamoja yenye maana ya ‘A common Destiny’, ina lengo la kuwakutanisha watu wa mataifa mbalimbali kuwa kitu kimoja na kufurahia kwa pamoja ikiwemo kubadilishana mawazo kwa pamoja kwa tasnia ya filamu, muziki, kwa mlengo ya kujenga.

“Tukiwa na haja moja, kuishi kwa amani na kuleta mapinduzi ya kiuchumi, kifikira na maendeleo kwa amani, ZIFF kwa kutumia dira hiyo hasa kupitia filamu zetu za ndani zenye mchanganyiko wa utamaduni na asili yetu.

“Wazanzibari na hata wageni watakaoshuhudia filamu hizi wataweza kuchukua utamaduni huo na kuupeleka nje kwa furaha kubwa katika kufikia hatma ya pamoja” amesema Prof. Mhando.

DSC_0082

Music Coordinator wa ZIFF, Edward Lusala akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na wasanii watakaotoa burudani kwenye tamasha hilo.

Lupita-Nyong-o-729-620x349

Lupita Nyong’o, Genevieve ndani ya nyumba

Tukio kubwa ambalo kwa sasa Tanzania hasa kwenye viunga vya Zanzibar na nchi nyingine duniani katika tamasha hilo la 17, ni ujio wa msanii wa Kenya na Mexico, Lupita Nyong’o, atakayeudhuria utoaji wa tuzo hizo za ZIFF mwaka huu.

Lupita ambaye ametwaa tuzo za Oscar na nyingine nyingi na kupelekea kutikisa Hollywood kwa sasa ni miongoni mwa mastaa watakaokuwa kwenye tamasha hilo huku akitarajiwa kuambatana na wazazi wake wote wawili pamoja na wadogo zake.

Prof. Mhando amesema tayari wazazi wote wawili wa Lupita akiwemo Dorothy na Peter Anyang’ Nyong’o, watakuwapo kwa siku zote 10 kwenye tamasha hilo huku Lupita mwenyewe akiahidi kuangalia uwezekano wa kuhudhuria japo katika utoaji wa tuzo kama ratiba za shughuli zake hazita mbana.

Prof. Mhando alisema Lupita ni zao la ZIFF na ndiyo iliyomfungulia mwanya wa kujulikana na baadaye alienda kusoma zaidi masuala hayo ya filamu, ambapo alishiriki ZIFF 2007 kama Volunteer.

Mara nyingi staa huyo amekua akihudhuria matamasha na halfa mbalimbali za utoaji wa tuzo na zawadi zingine huku akiwa ameambatana na wazazi wake wote wawili.

Lupita mbali na tuzo hiyo ya Oscar, kupitia filamu ya ‘12 Years a Slave’ pia filamu hiyo imempatia tuzo mbalimbali zikiwemo: tuzo ya Steve McQueen kama mwigizaji mwenye mvuto, mwigizaji bora wa kike aliyeshirikishwa, ‘Academy Award’, ‘Screen Actors’ Guild Award’, ‘NAACP Image Award’, ‘Independent Spirit Award’, ‘Broadcast Film Critics Association Award’, na nyingine nyingi.

Genevieve-Nnaji-Cover

Genevieve Nnaji.

Mbali na Lupita, katika kuongeza utamu wa tamasha hilo, mastaa wengine nguli wa Afrika kwa mwaka huu wanaotarajiwa kuwapo katika ushuhudiaji wa utoaji wa tuzo hizo ni pamoja na muigizaji na mwanamitindo nyota wa Nigeria, Genevieve Nnaji.

Wengine ni Amr Waked (Misri), Faouzi Bensaidi (Morocco), Nadia Buari, Richard Mote Damijo ‘RMD’, John Dumelo, Desmond Eliot na Florence Masebe.

DSC_0067

Afisa Habari wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Fizza Moloo akizungumzia kuhusiana na Filamu iliyopewa jina la "Women with Altitude" iliyoandaliwa na WFP ambapo ndani yake imeshirikisha wanawake wa kitanzania watatu waliofanikiwa kufika kilele cha Mlima Kilimanjaro wakiwa wameambatana na wenzao nane kutoka Nepal na kuzungumzia changamoto mbalimbali wakati wa kupata elimu na maisha kwa ujumla itakayoonyeshwa kwenye tamasha hilo tarehe 17/6/2014 saa 19:15 jioni ukumbi wa Old Fort visiwani Zanzibar.

Filamu ya Mandela kufungua pazia

Jumla ya filamu 79, kutoka mataifa mbalimbali zinatarajiwa kuonyeshwa huku filamu iliyoingia kwenye tuzo za Oscar, ya Mandela: ‘A Long Walk to Freedom’ ndiyo itakayofungua pazia kwenye tamasha hilo, Juni 14.

“Katika filamu hizo 79 za kimataifa zitaoneshwa ZIFF, nyingi zikiwa zinatoka katika nchi za Kiafrika na filamu ya Mandela imepata bahati ya kuwa ya ufunguzi”, amesema Profesa Mhando.

Pia Profesa Mhando amesema kuwa zitakuwepo filamu zinatoka katika nchi 35 zikiwemo filamu fupi 38, filamu ndefu za kuburudisha 24 na makala 17.

DSC_0137

Meneja wa Tamasha la ZIFF, Daniel Nyalusi "Dean" akionyesha kitabu chenye ratiba nzima ya tamasha hilo litakalorindima visiwani Zanzibar kuanzia Juni 14 hadi 22 mwaka huu.

Burudani zitakazopamba

Kwa upande wake, Edward Lusala anayeshughulikia muziki kwenye tamasha hilo la 17, anasema kuwa, wamejiandaa kutoa burudani ya aina yake ambayo itaacha historia kwa mwaka huu.

Lusala amesema jumla ya makundi 18 yanatarajiwa kutumbuiza. Huku kwa wasanii gwiji wakiwemo pia Didier Awadi kutoka nchi ya Senegal na Habib Koite (Mali) wanatarajiwa kuja kuishika Zanzibar na viunga vyake.

“Wasanii Koite na Didier ni miongoni mwa wasanii wakubwa sana na wenye heshima kubwa hasa kwa muziki wao kwani wanapiga kimataifa hasa katika matamasha makubwa na wamekuwa wakipiga miziki ya kipekee. Hivyo watu wote watafurahia” amefafanua Lusala.

Ameongeza kuwa, wasanii wengine ni pamoja na Farid Kubanda ‘Fid Q’, Ambwene Yesaya ‘ Ay’, Sauti Soul, Mzungu Kichaa, Ras Inncent Nganyagwa, Grace Matata na wengine wengi ambao watatoka Tanzania.

Na kuongeza kuwa kwa sasa AY yupo nchini Malawi akijifua na moja bendi maarufu ya muziki wa Live ambapo anatajiwa kukaa jukwaani kwa zaidi ya lisaa limoja na nusu huku akiimbaLIVE.

Pia vikundi vya muziki nguli toka Tanzania, Egypt, Kenya, Uganda, Malawi na Afrika ya Kusini vitatumbuiza kila siku katika tamasha hilo.

Aidha, Lusala amesema kuwa, kwa mwaka huu wanatarajia kufanya ‘surprise’ kwa kumleta msanii mkubwa ambaye bado wapo kwenye mazungumzo na msanii huyo kutoka Afrika kusini.

Kwa upande wake Meneja wa tamasha hilo, Daniel Nyalusi amewataja wadhamini wa tamasha hilo ni pamoja mdhamini mkuu ZUKU Pay tv, huku wengine ni Ethiopian Airlines, Tanzania Media Fund TMF, ComNet, Cello, Air Uganda, Gina Din, FASTJET and United Petroleum. Wengine ni shirika la Rosa Luzemburg Foundation, Arterial Networking, Steps International, Azam marine, Prime Time Promotions, Goethe Institut na wengine wengi.

ZIFF moja kati ya matamasha ya filamu makubwa duniani hukutanisha wadau katika tasnia ya filamu. Wakiwemo waigizaji wa siku nyingi na maarufu, waongozaji, waigizaji wachanga na wanafunzi kutoka ulimwenguni kote

DSC_0119

Meneja wa Biashara wa shirika la ndege la Fastjet, Jean Uku akizungumzia udhamini wao kwenye tamasha hilo ambapo wametoa tiketi za safari ya washiriki kutoka Afrika Kusini watakaoshiriki kwenye tamasha hilo.

DSC_0084

Msanii wa Hip Hop, Harry Kaale kutoka kundi la One "The Incredible" akielezea namna watakavyotoa burudani na elimu kwa vijana kwenye tamasha hilo.

DSC_0105

Msanii Mzungu Kichaa akiwashukuru ZIFF kwa kutoa nafasi kwa wazalendo kuonyesha vipaji vyao kwenye tamasha la ZIFF.

DSC_0108

DJ maarufu Kahlil Jacobs-Fantauzzi kutoka Puerto rico akisisitiza kutoa burudani ya aina yake kwenye tamasha hilo.

Tuesday, March 30, 2010

Tuzo ya Ousmane Sembene katika ZIFF 2010 - Mshindi kupata kitita cha Dola elfu 5

Tuzo ya Ousmane Sembene katika ZIFF 2010,Mshindi kupata kitita cha Dola $5,000

Shirika la GTZ likishirikiana na Tamasha la nchi za Jahazi (ZIFF) kwa mara ya tatu tena mwaka huu 2010 watatoa tuzo ya Filamu ya Ousmane Sembene, tuzo hii italenga hasa katika filamu fupi ambazo hazijazidi dakika 20 na ambazo zitakua zimezungumzia au kugusia masuala yanayoikabili jamii ya kitanzania hasa katika mambo ya Ukimwi, Jinsia, Elimu na umasikini.Mshindi atajinyakulia kitita cha dola za kimarekani 5,000 taslimu papo hapo kwaajili ya kumsaidia katika kutengeneza filamu nyingine ama kuboresha kazi zake.Wale wote watakaotaka kushiriki katika tuzo hii wawasilishe filamu zao kabla ya tarehe 30/04/2010 kwa kujaza fomu za kawaida zinazopatikana katika tovuti yetu www.ziff.or.tz

Daniel Nyalusi
Events and Film Program Coordinator
Zanzibar International Film Festival

Tuesday, July 07, 2009

Washindi ZIFF 2009

VERONA Award – Seasons of A Life (Malawi)

SIGNIS Jury Award - Commendation
(1)Mah Saah Sah (Cameroon) Dir: Daniel Kamwa
(2)Go With Peace Jamil (Denmark/Afghanistan) Dir:Omar Sharwagi
- East Africa Region Talent – Suwi (Zambia)-Dir: Cathrine Kaseketi Musola
-Signis Award – Izulu Lami (South Africa) – Dir: Madoda Ncayiyana

SEMBENE OUSMANE Award–Keiskamma-A Story of love (South Africa)
Dir:Miki Redelinghuys

ZIFF Chairman Award – Seasons of a Life (Malawi) – Dir: Dir:Charles Shemu Joyah

ZIFF Life Time Achievement Award – Hamid Vuai

UNICEF Award – Mother Unknown (Sudan) –Dir: Taghreed Alsanhouri

ZIFF Jury Award - Special Juror’s choice – African Tales (Tanzania) Producer:Imruh Bakari
- East African Talent – From a Whisper (Kenya) – Dir: Wanui
- Short/Animation – Warahutseho (Cameroon) Dir: Auguste Bernad Koueho
- Documentary - Bilal (India) – Dir: Sourav Sarangi
- Silver Dhow Award – Mon Histoire…Papy (DRC) Dir: Tunda Wa Munga
- Golden Dhow Award – Jerusalema (South Africa) Dir: Ralph Ziman

Mnaweza kupata habari zaidi ya ZIFF hapa: http://www.ziff.or.tz/

Thursday, July 02, 2009

Danny Glover Awasilli ZIFF

Danny Glover akiongea na Martin Mhando

Kutoka LUKWANGULE BLOG:

Danny Glovver Atua Uwanja wa Zenj

Muigizaji maarufu wa Hollywood na ambaye pia ni balozi wa Shirika la Umoja wa mataifa la Kuhudumia watoto(UNICEF) danny glover amewasili mjini Zanzibar leo majira ya alasiri na kusema ziara yake nchini itasaidia kujenga mahusiano zaidi kati ya Wamarekani weusi na ndugu zao wa Afrika.

Muigizaji huyo alisema hayo akiwa uwanja wa ndege wa zanzibar wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema pamoja na kuwa balozi wa uNICEF na kupeleka salamu za UNICEF maeneo anayotembelea pia ana shirika lisilo la kiserikali ambalo hushughulikia mahusiano na nchi za Kiafrika hasa kudumisha utamaduni ulipo wa miaka mingi kati ya wamarekani weusi na ndugu zao waliopo bara la Afrika.

Amesema katika kuimarisha uhusiano huo anajikita zaidi katika mawasiliano na kunyambua tamadunia mbzo anaona ndio ufunguao wa mahusiano kati ya Afrika na bara la Amerika.
Glovver ambaye atakuwa nchini kwa siku tano anatarajiwa pia kushiriki katika masuala mbalimbali ya tamasha kuwa na mahojiano na vyombo vya habari na kufanya shughuli za UNICEF ikiwa ni pamoja na kumuona Rais wa Zanzibar, Abeid Aman karume.
Pia akiwa hapa atashiriki katika kongamano la watoto na amani linaloandaliwa na GNRC na na kuzungumza na watengeneza sinema .

Pichani kama nilivyomnyaka akiwa na Mkurugenzi wa tamasha la filamu za zanzibar Dk martin wakikumbushana enzi hizo za nairobi, kenya mara tu baada ya kumaliza mazungumzo na waandishi wa habari ndani ya VIP ya zanzibar.

Monday, June 08, 2009

12th Zanzibar International Film Festival Newsletter


This year ZIFF theme is "Enduring Links; Media, People and Environment" stressing the importance of forging coalition to create mass environment awareness.

Media can play a great role to promote sustainable utilization of resource and environmental protection. No matter what level of development we want to achieve, Festival Launch must compromising to environment.

The festival will be launched in Dar Es Salaam, where a press conference will be held and all major components of ZIFF 2009 will be highlighted.

The residents of Dar Es Salaam and Bagamoyo will have opportunity to see best African films produced by Africans, among them, will be film like Jerusalema, which already has won about 7 awards and Seasons of Life, a film from Malawi which now is being considered to be among the best film ever produced in Africa. It is a film that makes anyone who sees it want to see it again. It is has dared to reveal occurrences in many African families that kept as secret.

Workshops

ZIFF is investing a lot of effort to promote film industry; this year several workshops to enhance film industry will be conducted; children film production, script writing, acting for camera, wild films, advanced film production, development and mobile cinema. ZIFF will host the East
African Film Makers/Producers Forum. Participants will share/exchange news and experience.

Tourism Conference

Tourism is a recognized global industry with a considerable impact on local development. It generates foreign exchange, creates employment, and promotes rural enterprises. ZIFF will invite 3 international tourism stakeholders from Europe, Asia and America to meet and network with local tourism stakeholders. The international guests will be able to meet with over 50 Tanzanian local companies/ tourism stakeholders including; Hoteliers, Airlines, Tour operators, Tourist boards. To establish links and create the international tourism.Local and central Governments will highlight their tourism potential to an international audience.

Visual Arts and Exhibition

An old saying that "Violence is the tool of ignorant" was manifested in Kenya, where people took weapons and started hunting their neighbors whose tribes where different from theirs. Burning Kenya exhibition will show how a human turned into savage animals and butchered their neighbors in a day light. Homes, schools, churches, fields were burnt.

Children Photo Exhibition

Featuring photos taken in Zanzibar by children will be exhibited, the rolling story telling and Jua Kali will be exhibited.

Women and Village Panorama

ZIFF will collaborate with TAMWA to run programs in villages, TAMWA will conduct workshops on gender issues and ZIFF will screen film on the subject of the workshops. Women panorama will arrange for dhow race in Matemwe to launch the opening of women panorama. Village panorama will run workshops on water rain harvest and conduct demonstration.

Children Panorama

Children and Youth Panorama highlights important issues concerning children and youths in Zanzibar, it works towards improving the quality of life for Zanzibarʼs most vulnerable children and youths by providing assistance through educational, health and community development programs. The panorama aims at improving the academic, social and cultural achievements of children and youths, meeting their diverse needs.

Young Journalism

Young journalism program initiated by UNICEF and ZIFF conducted workshop in Zanzibar, young people were given skills on HIV/AIDS, taught ABCs of journalism, like news gathering, story writing, and ethical reporting on sensitive issues. The workshop involved training both theoretical and practical aspects of journalism.

Children Film Panorama

The program is supported by Danish Film Institute and is sponsored by Queen of Denmark. DFI will run the film programs for young audiences and master class program for the profession film industry. The key objectives of the collaboration with the DFI are to equip local film producers with necessary knowledge to make and produce quality films for children.

Music and Performing Arts

Household name in the music industry in TanHousehold name in the music industry in Tanzania many of them with several music awards, will team up with foreign artists at Mambo Club Hall where audience will get opportunity to be entertained by music flavorszania many of them with several music awards, will team up with foreign artists at Mambo Club Hall where audience will get opportunity to be entertained by music flavors.

http://www.ziff.or.tz/

Monday, May 18, 2009

Mambo ya ZIFF Mwaka Huu!

Zanzibar International Film Festival/Tamasha la Nchi za Jahazi kwa muda mrefu sasa limekua likitoa nafasi za mafunzo ya muda mfupi (Training Workshops) kwa wadau wa filamu nchini na pia kutoa nafasi kwa soko la filamu la Africa mashariki kwa ulimwengu.

Ikiwa sasa tuko katika Tamasha la 12 la nchi za majahazi, ZIFF imeendelea kunadi na kukuza soko hili la filamu, ZIFF inatambua mahitaji ya kiwanda kizima cha filamu ili kikue na kufikia malengo tuyatakayo. Lakini kumekuwa na mwamko mdogo sana kwa wadau ama washiriki wa fani hii, ukiangalia kiwanda hichi hakina watu wenye ujuzi upasao (Professionalism) na ndio maana kimekua kikizalisha ilimradi kazi tena zisizo na ubora.

Mwaka huu tena ZIFF inatoa nafasi ya mafunzo ya muda mfupi kwa wadau na washiriki wa soko/kiwanda cha filamu. Tunaomba watu wajitokeze kutuma maombi yao ili kuweza kushiriki. Pia tunaomba wadau/washiriki wasisite kuuliza maswali pale wapohisi hawajaelewa au panawatatiza.

Naambatanisha Tangazo la Warsha za Mafunzo ya muda mfupi ili kuwajulisha wadau/washiriki nini kinaendelea katika ZIFF 2009 na pia kuwaomba washiriki.

Nashukuru kwa vyombo vya habari kwa kuwa mstari wa mble kuzungumzia soko na kiwanda cha filamu kwa upana lakini tukumbuke bila elimu kiwanda hichi kitakufa.


WORKSHOP/CONFERENCE/FORUMS AT ZIFF 2009 \

27th June – 3rd July, 2009 - Film Production for Children Workshop by DFI15 Participants (10 From Mainland, 5 Zanzibar), Application Deadline 25th May, 2009For Film Makers/Producers Only.

28th June – 5th July, 09 - Screenwriting Workshop by Maisha Film Lab9 Participants: Application Deadline 21st May, 2009For Script Writers Only.

2nd July, 2009 - Acting for Camera by Ntare Mwine and Danny Glover (USA)20 Participants (15 from Tanzania Mainland/East Africa, 5 from ZanzibarFor Actors Only.Application Deadline 25th May, 2009.

2nd- 3rd July 09 - Tourism Conference by ZIFFFor All Tour Operators in Tanzania (Zanzibar and Mainland)Apply now for this special opportunity.
Deadline for Application 1st June, 2009

3rd July, 2009 - African Film Makers/Producers Forum by ZIFF/TAIPAFor East African Film Makers/Producers
Application Deadline 1st June, 2009

3rd July, 2009 - Wild Life filming by South African WildlifeFor all Wildlife Film Makers/Producers Application Deadline 1st June, 2009

4th July, 2009 – Development Film Workshop by GTZFor All Film Makers/Producers/Media Houses.25 Participants (15 from Mainland, 10 from Zanzibar and East Africa)Application Deadline 1st May, 2009

Wako katika Filamu,

Daniel NyalusiEvents Coordinator/Film Programs
Zanzibar International Film Festival 2009

Wednesday, July 23, 2008

Wabongo wachemsha tamasha la filamu la ZIFF?

Maoni ya Kaka Beda Msimbe Lukwangule Entertainment Blog:

Wabongo wachemsha tamasha la filamu la ZIFF?

There is something very seriously wrong with Tanzania artist and this can been seen katika tamasha la filamu la kimataifa linaloishi ndani ya nchi hii ZIFF ambalo hufanyika Zanzibar kila mwaka. What is wrong jamani!!!!!

Nikiandika katika busati la filamu Habari leo Jumapili nilishawahi kusema jamani tutumbukize filamu huku kwani ipo nafasi ya kwenda maeneo mengine, kukosolewa na pia kuna sababu... lakini Roma haikujengwa kwa siku moja, lazima tusonge mbele.. kwa kujionyesha hadharani.. lakini wapi kw amara nyingine tena tamasha la 11 lina upungufu mkubwa wa local component.

Watu wanatoka all the way from Europe,America and Far East to look for nafasi just to shoo his or her film but Watanzania wanaozalisha filamu kwa fujo kwa sasa wamepeleka filamu hizi zifuatazo na moja nadhani ni ya Da Chemi huko Marekani, Bongoland II ambayo katika entry imeelezwa director wake ni Josiah Kibisa.

ZIFF hufanyika Zanzibar kila mwaka na ni tamasha kubwa kama hutaki filamu yako iingie katika mashindano lakini angalau uonyeshe basi kwa watu:Nini majidai kama hatuwezi hata kufanya kweli kwenye tamasha lenye heshima Afrika Mashariki na Kati?

CEO wa ZIFF mtanzania mwenzetu, manake nasikia wakati ule (zamani) watani zetu wakiingiza filamu kama nyuki tulikuwa tunasema ohh Foreigners hawatutakii mema, sasa huyu mswahili wa Tanga mwenye utaalamu wa filamu ambaye ameishi ughaibuni na anafundisha ughaibuni ametoa wito sana toka mwaka jana akililia filamu za nyumbani lakini mwe wamesema waluguru chilanga komo, yaani unayashangilia maji halafu unakuwa kama huna akili nzuri jamaa wanakucheka, tuache hayo kwani tulikuwa tunazungumzia filamu zilizoingia ZIFF kutoka hapa nyumbani nazo ni hizi zifuatazo:Bongoland ll,Mwanahiti l (oloibon na Layoni)na ll Zawadi ya Fisadi;The Trip ya James Gayo; Sasa na Jando.

Can you imagine?

Watu sijui niwasemeje, labda sijui woga? Haya hatukupeleka hizo sineema zetu je tutaenda kuhudhuria kujifunza manake nasikia kuna manguli wa filamu kutoka Amerika ya Kusini, Amerika kaskazini, Nigeria na Asia ya mbali wanakuja kutufunza mambo ya ABC za utengenezaji sinema, tutakwenda?

Mimi yangu macho.CEO wa ZIFF Dr Martiun mhando amesema kwamba hakuwa na chaguo la kutosha kwani hata zile zilizoletwa hizo zitakazoonyeshwa ni nafuu zaidi na yeye anasema I wonder, kweli hata mimi namuunga mkono I wonder.Hatuwezi kukua kisanii kama tusipokubali kuwa tunamapungufu na lazima tuwasikilize watu watusaidie.

Monday, July 21, 2008

Kwa nini sinema za Tanzania zilifanya vibaya ZIFF

Nimeona watu wanaulizia kwa nini sinema ya Bongoland II haikupata zawadi ZIFF, wala hata mention. Sina jibu. Sikuwepo huko ZIFF.

Ila nimeona hii story kwenye gazeti ya Daily News (TZ) leo iliyoandikwa na kaka Michuzi.

Naona Dr. Martin Mhando anasema kuwa ingawa Bongoland II, ilikuwa sinema pekee ya kiTanzania kwenye mashindano ya 'Feature' ina hadithi mbili, ya familia ya Juma na hadithi ya yeye kurudi Bongo. Alisema ni sinema nzuri kwa ujumla.

Haya, niwaulize wadau walioona sinema ya Bongoland II, mliionaje?

**************************************************************************
ZIFF wants more focus to develop film industry

MUHIDIN ISSA MICHUZI in Zanzibar
Daily News; Tuesday,July 22, 2008

The Zanzibar International Film Festival (ZIFF) believes that developing a funding structure to link up with creative capacity and a local distribution structure is the answer if Tanzania's infant film industry is to grow.

The Chief Executive Officer of ZIFF, Dr Martin Mhando, said this in an exclusive interview with the 'Daily News' here yesterday, adding that one of the key problems with African cinema depended entirely on distribution.

"ZIFF has undertaken research looking into distribution hence the Tanzania Film Chain Study Report that was presented at ZIFF 2008", he said, adding: "We hope we can have time to again discuss it at length with our filmmakers with the view of looking into how to link distribution to production", said Dr Mhando at the climax of the 11th edition of ZIFF on Saturday.

On the poor participation of Tanzanian films at the annual festival, the ZIFF CEO expressed deep concern, saying something should be done to reverse the situation as it makes them feel bad about it.

He said the ZIFF plans to begin serious discussions with local filmmakers so that production efforts on the ground were supported. He, however, pointed out that there a need to encourage local filmmakers to see the use of festivals in marketing or at least promoting their films.

"Festivals generally do not need to chase after filmmakers -- the opposite is the case. However ZIFF needs filmmakers just as filmmakers need ZIFF", he quipped. The ZIFF CEO emphasised that to learn how to distribute films internally was paramount to putting the industry on its feet.

Dr Mhando said until Tanzania reached the point that audiences who clamour for the local product are satisfied one can not say the country has an industry. "Therefore let us deal with what distribution structures exist in the country, know who our audiences are and how to reach them and then start making films for those audiences and their distribution structures" he stressed.

On Bongoland II, which was Tanzania's lone nominated entry in the ZIFF 2008, Dr Mhando said it is a good film but had its setbacks on its story board. He said while the juries did not discuss film by film but one of the things that have been said about Bongoland II is that it went well until it began the story of the family's intrigue.

"The family intrigue needed to be brought in earlier and better fused into the script for the film to work. "Currently it looks like there are two stories - about the young man's problems of resettlement and then the family's", he concluded.

Orodha ya Washindi wa ZIFF

Dr. Martin Mhando, afisa mtendaji mkuu wa ZIFF akiongea kwenye hafla ya kufunga rasmi tamasha la 11 la ZIFF ngome kongwe, Zanzibar (picha kutoka Michuzi Blog)
Watoto wakitazama filamu kwenye ZIFF
Baadhi ya watazamaji kwenye ZIFF

1. THE GOLDEN DHOW -Awarded to a film that exemplifies excellence in film language and one highlighting Dhow culture.Ezra (2007, Dir: Newton I Aduaka, Nigeria/France)


2. THE SILVER DHOW- Awarded to a film that is a runner up to the Golden Dhow awardee.India Untouched (2007, Dir: Stalin K. India)


3. SHORT/ ANIMATION -Awarded to the best short film in the festival reflecting mastery of the short film structure and aesthetics.Subira (2007, Dir: Ravneet Chadha, Kenya/)


4. EAST AFRICA -Awarded to the best film by an East African filmmaker that shows the greatest commercial aptitude and potential marketabilityAfrican Lens (2008, Dir: Shravan Vidyarthi, India/Kenya)


5. SPECIAL JUROR'S CHOICE -Laya Project (2006, Dir: Harold Monfils, India)SEMBENE OUSMANE PRIZEAwarded to a film that takes a particular look at topics of development coperation.INTO THE LIGHT by Peter Glen, 2007, USA


6. SIGNIS JURY AWARD -Awarded to a film that is deemed to to exemplify universal and spiritual values that enhance human dignity, justice and tolerance.TARTINA CITY by Issa Serge Coelo - (Chad)


7.Special Commendations-Behind this Convent By 2007, Gilbert Ndahayo (Rwanda)African Lens 2008, by Shravan Vidyarthi (Kenya)East African TalentSubira (2007, Dir: Ravneet Chadha, Kenya)


8. VERONA JURY AWARD -Awarded to a film deemed the best African feature film in competition.Behind this Convent 2007, By Gilbert Ndahayo (Rwanda)


9.FIPRESCI JURY PRIZE- Awarded to a feature film from the Dhow Countries that combines cultural astuteness and commercial potential.EZRA directed by Newton I. Adauka, Nigeria/France, 2007


10. THE ZIFF CHAIRMAN'S AWARD -The award is given to a film that reveals an acute reflection on contemporary issues in a balanced manner in these times of polarised perspectives.In The Name of God , Shoaib Mansour, Pakistan, 2007


11.THE AIR TANZANIA AWARD FOR THE BEST EAST AFRICAN FILM- African Lens (2008, Dir: Shravan Vidyarthi)


12. THE UNICEF AWARD -For the Best film that encapsulates issues of children and WomenThe Kadogo Brothers, 2007, Ivory Coast, By Joseph Muganga

Saturday, July 19, 2008

Washindi wa Tamasha la Filamu Zenj Watajwa

Asante Kaka Beda Msimbe (Lukwengule Entertainment) kwa update:


Hotuba tu ya jaji wa ZIFF kuhusu Tamasha:


Good evening ladies and gentlemen:

As the ZIFF festival enters its eleventh year and is now a key festival in African cinema, we – my colleagues Rachel Dwyer, Flavio Florencio and I - are honoured to have been invited to serve on the ZIFF jury.

Since its inception in 1998, ZIFF has strived to reflect the cultures and traditions of the Swahili culture of East Africa, and to celebrate and explore the Dhow culture emanating from the Indian Ocean Basin. And to recognize, appreciate and most importantly, enjoy African film.

Eleven years on and we’ve been privileged to select four films out of a staggering 41 features and documentaries in competition for the coveted prizes of the Golden Dhow, the Silver Dhow, Best Short film and Best East African film.The films in competition have resonated with this year’s theme of ‘Cultural Crossroads’ and have adhered to the proud tradition, established by the founding ZIFF Jury of 1998 to ‘explore and learn from Dhow culture and its importance in global experience.’

In keeping with the history of the iconic Dhow as ‘a symbol of communication, migration and interaction’, many of the films have explored the contestations that arise from migration.Issues that continue to bedevil Africans on the continent and the diaspora, such as indigenous land-rights, identity, genocide and ethnic cleansing, the exploitation of child soldiers and blood diamonds, have been explored from many angles and in different ways.

While films from the Indian Ocean basin have turned the spotlight on the thorny issues of untouchability and religious fundamentalism.

We were delighted with the number of East African productions and the inclusion of Bongowood films such as Bongoland 2, Mwanaihti and The Trip, all from Tanzania.Films from Tanzania, Kenya, Zimbabwe, South Africa, Rwanda, Nigeria, Ivory Coast, Senegal, the Congo, the Sudan, Liberia, Zambia, Egypt, Uganda, Ghana, Chad and Morocco, speak to the growth of the African cinematic canon.

The canon has not only expanded, but African filmmakers are clearly seizing the opportunity to tell their stories, from their perspectives, in ways that are nuanced, textured, beautiful to look at, and most importantly: cinematically exciting and entertaining.

In conclusion, and before announcing the final winners, the ZIFF Jury 2008 would like to make special mention of three films, which left a lasting impression on us:

Awaiting for Men, from Senegal, director Katy Ndiaye, for its sensitive and transgressive portrayal of women.

We are Watching You from Egypt, directors Sherief Elkatsha & Leila Menjou, for its powerful portrayal of three brave women and their determination to keep their government’s feet to the fire in the pursuit of democracy.

The Iron bone from Morocco, director Hisham Lasri for its beautiful cinematography and contemporary exploration of youthful (if misguided) urban camaraderie.And now, without further delay, the winners are:

Golden Dhow for Best Feature: Ezra (2007, Dir: Newton I Aduaka, Nigeria)

Silver Dhow for Best Documentary: India Untouched (2007, Dir: Stalin K, India)

Best Short/Animation film: Subira (2007, Dir Ravneet Chadha, Kenya)

Best East African film: African Lens (2008, Dir: Shravan Vidyarthi,Kenya)

Special Juror’s Choice: Laya Project (2006, Dir: Harold Monfils, India)for the most relevant to the themeof the Dhow countries

Gail SmithChairperson ZIFF Jury 2008


In the picture Ms Gail Smith reading her speech

Saturday, July 12, 2008

Bongoland II Review - Beda Msimbe

Nimeona hii review ya sinema, Bongoland II huko Lukwengule Entertainment. Imeandikwa na mwandishi wa habari maarufu Beda Msimbe. Aliiona leo kwenye Tamasha la filamu huko Zanzibar.

*********************************************************

Bongoland ll full uzushi full kupendeza

Ndio kwanza natoka kuangalia filamu iliyotengenezwa na watanzania ya Bongolandll katika ukumbi wa sinema wa wazi ndani ya Ngome Kongwe. Nyumba ilikuwa imeshiba, nataka kusema kwamba sinema hii ilipata mapokezimakubwa kwani ilishangiliwa na vile vijembe viliandaliwa kama vinavyostahili,maeneo ya manzese yalionyesha utofauti mkubwa wa maisha ndani ya Bongo ukilinganisha na mahali kazi zinapofanyika, dauni tauni.

Naam kama kuna wakati nilijisikia raha ni pale ambapo nilimuona dada Chemi akiwana waigizaji wazoefu sana nchini kama mama Mjata wakifanya vitu vyenye uhakika.Nilimaliza kuona filamu iliyojaa utata mkubwa wa maisha Bongoland ll nikiwa najisikia kuwapa Hi watanzania ambao wameonyesha tofauti kubwa ya maisha, akili,uwezo na kupozi maswali ambayo yanamgusa mtazamaji.

Ama hakika kazi ya Mtanzania huyu Josiah Kibira anayeishi huko Ughaibuni, Marekani ina maana kubwa na changamoto kwa waandazi wengine wa filamu nchini.Picha ya Bongoland 11 ambayo ni mwendelezo wa picha nyingine iliyoandaliwa naMtanzania huyo Bongoland ni ukakasi wa mapenzi, machungu, uzushi nauwongo,uzembe na kutojali maisha.

Ni filamu iliyoonyeshwa nchini kwa Mara ya kwanza ikiwa pia miongoni mwa filamuza kitanzania chache zilizofikishwa ZIFF kwa ajili ya kushindanishwa. Ikiwa inatumia dakika 109 inazungumzia umaskini kwa namna nyingi.

Umaskini uliomo ndani ya filamu hii ni wa mawazo, akili na swali kama kweli sisi ni mafukara linatawala kila mahali.hivi kama watu hawataki kazi watakuwaje mafukara?

Juma baada ya kurejea nchini akajikuta anatapeliwa, anadanganywa na pia anapata habari nyignine si nzuri, anapambana na bosi wake ambaye ana vibanda na vijumba basi mambo juu ya mambo.Naam ilikuwa filamu ya kuona kwani inasema wazi na ghasia zote sisi tu maskini wa mawazo.

Wednesday, July 02, 2008

Bongoland II - Zanzibar

Kwa wale wote mlioko Bongo!!

Tunafurahi kuwatangazia kuwa sinema ya Bongoland II itaonyeshwa katika Tamasha la filamu la Zanzibar (Zanzibar International Film Festival) Sinema ya Bongoland II itaonyeshwa rasmi Jumamosi, July 12 saa moja na dakika 15 jioni.

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa tamasha, Bwana Martin Mhando, alisema "ratiba hii imezingatia umuhimu wa kuwapatia watanzania wengi fursa ya kuiona sinema hii, ndo maana ikapangiwa jumamosi". Itaonyeshwa kwanza katika sinema zote zitakazoonyeshwa usiku huo.Kama mnavyokumbuka, Bongoland II ilishutiwa katika jiji la Dar mwaka jana mwezi wa saba.

Wasanii wote katika sinema hii ni wakazi wa Bongo. Hii ni sifa kubwa maana sinema hii itachuana na sinema nyingine nyingi kutoka mataifa mbali mbali ulimwenguni.

Mwezi ujao Bongoland II itaonyeshwa Chicago katika Gene Siskel Film Center katika Black Harvest Film Festival. Soma zaidi hapa. TUTAONANA ZENJ!! - link it to in their own words.

Monday, June 23, 2008

Bongoland II itakuwa kwenye DVD hivi Karibuni


BONGOLAND II DVD - An Update

We have been busy getting ready to release BONGOLAND II on DVD. We are getting closer and closer...the date that we have planned to release the DVD is July 15th. More details to come.We are also proud to announce that Bongoland II was officially selected for the Zanzibar International Film Festival and the Black Harvest International Festival this is in Chicago.

Both of these film festivals will take place in the month of July. We are confident that there will be more festivals to come where you can possibly watch Bongoland II.

Please watch the blog to see how you can pre-order your new DVD.

In the meantime, we are working on two new projects. A documentary about the relationships between Africans and African Americans and a love story drama by a cast of mainly actors from Kenya. It is a Kenyan story by all measures.

Thursday, February 28, 2008

Zanzibar International Film Festival 2008





Zanzibar, February 2008 –The Zanzibar International Film Festival has released its programme for the 11th Edition of ZIFF the Festival of the Dhow Countries, to take place between 11th to 20th July this year.


ZIFF will this year welcome top names to the festival proving the status that the festival enjoys in world festival circles., as director Newton Aduaka from Nigeria winner of Etalon Yenenga at FESPACO 2007 confirmed his attendance. Efforts are underway to bring multiple award winner Danny Glover and Charles Burnett with their film Namibia: Struggle for Liberation which is expected to open the festival.

Tanzanian acting circles have applauded plans to bring Ramsey Nouah, the king of Nollywood melodramatic film production who will also conduct acting workshops and show his films at ZIFF! “ZIFF will not have enough space to hold the crowds, should he confirm coming to Zanzibar!”, said a film enthusiast, “Many women have vowed to travel to Zanzibar should the suave actor confirm coming to ZIFF in July”

This year shall carry the theme Cultural Crossroad though which Zanzibar becomes again the crucible of cultural intersections and mutual respect.“Preparations are underway to deliver to our patrons a sumptuous program of films and other cultural offerings befitting the long wait for ZIFF”, said the ZIFF CEO, Dr. Martin Mhando.

Amongst the standout events for the year is the return of the Zanzibar Fensi! This veritable Zanzibari cultural activity has not taken place for over 8 years and this year will see the return of Fensi in its carnival form!

Dr Mhando also announced that Nollywood, the third world largest film feature production industry, will be fêted in Zanzibar during the festival. The impact that Nollywood has had on Africa cinema will also be debated under the Soko Filam program.60 films will be in competitions judged by four International Juries, and currently 4 world Premieres Films have been confirmed.

Amongst the premieres is Tanzanian Josiah Kibira’s Bongoland II which will have its African premiere at the festival.

The ZIFF management again reminded filmmakers that the deadline for entering films into ZIFF 2008 is 31st March.

Entry forms for films and musical groups are available on the ZIFF website http://www.ziff.or.tz/

Thursday, May 03, 2007

Zanzibar International Film Festival - ZIFF






The Zanzibar International Film Festival (Festival of the Dhow Countries) ZIFF will be held June 29th, to July 8th, 2007 in Zanzibar, Tanzania.
ZIFF ni tamasha inayofanyika kila mwaka huko Zanzibar. Wanaonyesha sinema na pia vikundi mbalimbali vya kisanii na muzuki kutoka nchi mbalimbali zinashiriki katika maonyesho kadhaa. Lasiki hasa ni maonyesho ya sinema zinatoka nchi za mwambao ya bahari ya hindi. Huu ni mwaka wake wa kumi. Mwaka huu wataizindua Dar katika hoteli ya Holiday Inn.